Search This Blog

Saturday, July 16, 2011

OFFICIAL: STEWART DOWNING AJIUNGA RASMI NA LIVERPOOL


Winga wa kimataifa wa England Stewart Downing amemalizana na klabu ya Liverpoo na leo ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa majogoo wa jiji kwa £20million.
Downing amesaini mkataba wa miaka 4 na atakuwa akilipwa £80,000 kwa wiki.

EXCLUSIVE INTERVIEW

SHAMTE ALLY: SITAKI KWENDA MORO UNITED


Siku moja baada ya dirisha la usajili kufungwa mshambuliaji wa Yanga Shamte Ally aliyepelekwa kwa mkopo Moro United amesema hataki kucheza kwenye timu hiyo ilipanda daraja msimu huu.
Shamte ambaye alitokea Kagera Sugar kabla ya kujiunga na mabingwa wa Tz amesema haweze kujiunga na Ruvu kwa sababu transfer hiyo imekwenda kinyume na mkataba wake mpya unavyoelekeza.
"Nilisaini mkataba mpya wa miaka na Yanga mwezi uliopita mara baada ya ligi kumalizika, huku ukiwa na kipengele cha probation ya miezi kadhaa, ambayo kama nikishindwa kuperform vizuri uwanjani then nitapelekwa kwa mkopo sehemu nyingine.Sasa nashangaa wakati sijaanza rasmi kuitumikia klabu naambiwa niende Moro kwa mkopo kitu ambacho ni kinyume na mkataba wangu na Yanga.
"Mimi najiamini nipo vizuri sana kimchezo na kama Yanga wangeniambia mapema kama sipo kwenye mipango ya mbele ya timu basi sasa hivi ningekuwa nimeshapata nafasi katika nyingine kubwa kama Yanga ambayo ilikuwa ikinitaka kwa udi na uvumba."-Shamte

Wakati huo huo taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga zinasema baada ya mchezaji huyo kugoma kwenda Moro, timu hiyo imeamua kufuata matakwa ya mkataba wao na Shamte, hivyo mchezaji huyo ataendelea kuitumikia Yanga msimu ujao.

USIMBA NA YANGA WA UWANJA WA TAIFA WATOKEA MALAYSIA

PHOTOS: SUNZU AKISAINI MKATABA NA SIMBA

FELIX SUNZU AKISAINI MKATABA WA WA MIAKA 2 WA KUCHEZA SIMBA

MATHARE UNITED WASAINI MKATABA NA PUMA


Klabu ya Mathare United inayoshiriki katika ligi kuu ya Kenya imefanikiwa kuingia mkataba wa udhamini wa mwaka mmoja na moja ya makampuni makubwa ya vifaa ya michezo PUMA.

Udhamini huo wa Mathare United kutoka kwa PUMA una thamani ya kshs 3million, huku klabu hiyo ikipata jezi rasmi na za mazoezi, na viatu.

USAJILI WA TEGETE SIMBA WASHINDAKANA


Uhamisho wa mshambuliaji Jerryson Tegete kuelekea Simba kwa klabu hiyo ya msimbazi kumtoa beki Kelvin Yondan pamoja na kiasi cha pesa umeshindakana.

Chanzo cha habri kutoka ndani ya pande mbili za uongozi wa watani wa jadi kinasema kuwa kushindakana kwa dili hilo ni kutokana muda, "Ni kweli Simba walipeleka ofa ya kutaka kumsajili Tegete lakini Yanga wameshindwa kutoa maamuzi kutokana na kwamba suala la zima maamuzi ya usajili linapaswa kutolewa maamuzi na kamati ya utendaji ya klabu hiyo ambao imeshindwa kukutana kwa dharura mpaka dirisha la usajili lilipofungwa leo saa 6 usiku."

Friday, July 15, 2011

MBWANA SAMATTA AIFUNGIA TP MAZEMBE BAO LA USHINDI.

MBWANA SAMATTA JEZI NAMBA 29 AKIFUNGA BAO PEKEE KWA KICHWA.



Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta juzi aliikoa timu yake ya Tp Mazembe na kuipa ushindi wa bao moja bila katika mchezo wa ligi . Samatta aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Serge Lofo alifunga bao hilo katika dakika ya 89 ya mchezo huo ambao kwake ulikuwa wa kwanza tangu ajiunge toka Simba Sports Club .
Sammatta aliingia kwenye mchezo huo sambamba na mwenzie waliyejiunga naye toka Simba Patrick Ochan ambaye naye alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza ambapo alichukua nafasi ya Rainford Kalaba aliyeumia dakika 15 baada ya mchezo kuanza . Tp Mazembe pia ilimkaribisha kiungo wake Guy Lusadisu aliyecheza mchezo wake wa kwanza tangu atoke kwenye adhabu ya kifungo cha FIFA baada ya kufanya fujo kwenye michuano ya kombe la Kagame huko Rwanda mwaka jana.


Hii ni mara ya tata kwa Samatta kufunga bao kwenye mchezo wake wa kwanza rasmi ambapo aliifungia Simba mabao mawili dhidi ya African Lyon ambayo ni timu yake ya zamani katika mchezo wake wa kwanza akiwa na Simba kwenye ligi kuu ya Vodacom msimu uliopita , pia aliifungia timu ya taifa ya wakubwa katika mchezo wake wa kwanza akitokea benchi dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya kati na sasa ameifungia klabu yake mpya kwenye mchezo wake wa kwanza wa ligi.

MESHACK ABEL: "SIMBA NIACHENI NIONDOKE NA SITAKI KUCHEZA RUVU SHOOTING"


Masaa machache baada ya uongozi wa klabu ya Simba kutangaza kumpeleka kwa mkopo katika klabu ya Ruvu Shooting, beki Meshack Abel ameongea na blog hii na kufunguka juu sakata hilo la uhamisho wake.

"Kiukweli nimeshangazwa sana na taarifa hizi za mimi kupelekwa kwa mkopo Ruvu Shooting, kwa sababu mimi nilishakataa kwenda huko.Jumatatu iliyopita Uongozi uliniita na kuniambia juu ya suala hili na mimi nikawaambia siwezi kwenda Ruvu, ni bora wanipe barua ya kuniacha ili niende nikatafute timu ninayoitaka mwenyewe lakini uongozi ukaniambia mimi ndio niandike barua ya kuvunja mkataba.Kutokana na sharti hilo nikashindwa coz sikuwa na uwezo wa kulipia gharama za contract termination, hivuo nikawaomba waniache nitafute timu mwenyewe lakini sitaki kuichezea Ruvu Shooting.

"Kiukweli Simba wamekuwa hawanitendei haki tangu wanisajili, mpaka sasa nawadai fedha zangu za usajili za mwaka jana, waliniahidi kunilipa kwa kunipa gari lakini mpaka msimu unaisha sikupewa kitu, na wakati tunajiandaa kwa ajili ya mechi ya pili ya Motema Pembe niliumia hivyo nikashindwa kuitumikia klabu, lakini cha ajabu mwisho wa mwezi(May) ulipofika walinikata mshahara wangu eti kwa madai walitumia fedha waliyonikata kunitibia majeraha niliyoumia nje ya Simba.

"Mambo yote haya niliyavumilia lakini sasa imefika mwisho, nahitaji uongozi wa klabu ya Simba waniache niende sehemu ninayoitaka kama walivyowaachia Haruna Shamte na Jabu kuchagua sehemu wanazozitaka."

Meshack ambaye alihamia Simba akitokea Mtibwa Sugar anasema tayari amepeleka maombi rasmi ya kuomba Simba wamuandikie barua ya kumuacha kwa sababu ameshapata timu ya kuichezea nchini Botswana, "Niliongea na katibu na nimweleza kuwa nimepata timu inayotaka kunisajili nchini Botswana inayoshiriki ligi kuu ya nchini humo "Tigers Sports Club, na kama mambo yakienda vizuri Jumapili natarajia kwenda Gabarone kumalizana nao.Naamini bado nina uwezo mkubwa wa kucheza na nitathibitisha uwezo wangu ndani ya msimu mmoja tu."


Premier League yabadilisha sheria ya vikosi dhaifu.

Ligi kuu ya England imeamua kuachana na sheria ya kutoa adhabu kwa timu zitakazopeleka vikosi dhaifu kwenye michezo ya ligi hiyo . Kwa sasa Timu za ligi kuu zitaruhusiwa kuchezesha mchezaji yoyote aliyemo kwenye kikosi cha wachezaji 25 siku ya mechi bila kuogopa kukumbana na adhabu yoyte kama ambavyo imewahi kutokea kwa timu za Wolves na Blackpool ambao walitozwa faini ya paundi 25,000 baada ya kocha Ian Holloway kufanya mabadiliko 10 kwenye kikosi chake cha kwanza.

Mkutano uliowakutanisha wadau ambao ni vilabu 20 vya vya ligi kuu nchini England ulifikia makubaliano kuwa mchezajo yoyote kati ya wachezaji 25 walioko kwenye timu anaweza kuchaguliwa kwenye mechi , sheria hii hata hivyo haiwahusu wachezaji walioko kwenye vikosi vya wachezaji wadogo yaani “reserve” na timu itakumbwa na adhabu ya faini kama itachagua wachezaji toka kwenye vikosi vya reserve kwa ajili ya mechi .
Msemaji wa Premier League Nick Noble amesema kuwa sheria hii inaruhusu vilabu kuchagua idadi yoyote ya wachezaji wa vikosi vya wachezaji walio na umri chini ya miaka 21 hivyo sheria hii itavibana vilabu kutotumia idadi kubwa ya wachezaji toka vikosi vya vijana ili kulinda heshima ya mchezo wa soka na ligi kwa ujumla .


Itakumbukwa kuwa Novemba iliyopita , Blackpool walitoka sare ya mabao 2-2 wakiwa nyumbani dhidi ya Everton na siku nne baadae kocha Ian Holloway alifanya mabadiliko 10 kwenye kikosi chake kilichovaana na Aston Villa na matokeo yake ilikuwa ni fine ya paundi 25,000.

KITABU CHENYE UMRI MKUBWA CHAPIGWA MNADA

Kitabu chenye umri mkubwa kuliko vyote cha sheria za soka ambacho kilikuwa chini ya umiliki wa Sheffield Fc kimepigwa mnada na kuuzwa kwa thamani ya paundi 881,250.
Kitabu hicho ambacho kimeandikwa kwa mkono tangu mwaka 1857 kinadhaniwa kuwa moja ya vitabu vya awali kuliko vyote vya mchezo wa soka na kimeuzwa kama sehemu ya kumbukumbu muhimu za klabu YA Sheffield Fc. Klabu hiyo imekipiga mnada kitabu hicho kama sehemu ya mpango wake wa kuchanga fedha kwa ajili ya kuendesha klabu hiyo.


HIKI NDO KIKOSI CHA KLABU KONGWE KABISA ULIMWENGUNI YA SHEFFIELD FC ILIYOANZISHWA MNAMO MWAKA 1857

Ndani ya kitabu hicho kuna sheria ambazo baadhi ziko hadi leo hii kama vile “in-direct free kick” , kona na matumiz ya sehemu ya juu ya goli maarufu kama mtambaa panya .
Sheria nyingine inaonyesha kuwa mchezaji anaruhusiwa kusukuma kwa kutumia mikono ila sio kumuangusha au kumpiga mchezaji mwenzie mweleka

HIKI NDO KITABU CHENYEWE

NDOLLO AKATWA USAJILI YANGA


Klabu ya Yanga leo imemaliza utata katika usajili wa wachezaji watano wa kigeni baada ya kutangaza majina ya wachezaji watakaoingia katika usajili rasmi wa klabu hiyo.

Majina ya wachezaji hao ni kama ifuatavyo:

1: Kenneth Asamoah

2: Haruna Niyonzima

3: Hamis Kiiza

4: Yew Berko

5: Davis Mwape


Wakati huo huo klabu hiyo ya Yanga imemtoa kwa mkopo mchezaji Idd Mbaga kwa klabu ya African Lyon inayoshiriki katika ligi kuu ya Tanzania.

SAKATA LA USAJILI WA YONDANI NA TEGETE

Wakati dirisha la usajili Tanzania likiwa linafungwa leo saa 6 usiku klabu ya Simba imethibitisha kuwa wamepeleka ofa ya kutoa kiasi cha pesa pamoja na kumtoa beki Kevin Yondan ili waweze kupata saini ya mshambuliaji Jerryson Tegete kutoka Dar Young Africans.

Simba ambao leo hii pia wamefanikiwa kukamilisha usajili wa Felix Sunzu wanamhitaji Tegete aje kuziba pengo lilioachwa na mshambuliaji Mussa Hassan Mgosi anayekaribia kujiunga na DC Motema Pembe.

BREAKING NEWS: SUNZU ASAINI MKATABA WA MIAKA 2 NA SIMBA


Hatimaye klabu ya Simba imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia Felix Sunzu kwa mkataba wa miaka 2.

Taarifa rasmi kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinasema kuwa mshambuliaji huyo ambaye aliwasili Bongo leo asubuhi amelipwa kiasi cha $35,000 kama gharama za usajili(signing fee).

NIKE KURUDIA YA RONALDO KWENYE UHAMISHO WA SNEIJDER


Sekeseke la usajili wa kiungo Wesley Sneijder kutoka Inter Milan kuelekea Manchester United limechukua sura mpya baada ya taarifa za kampuni kubwa mavazi ya Nike kuingilia kati juu ya kukamilisha kwa usajili huo unaotajwa kuwa wenye thamani ya £35.2million.

Kampuni hiyo kubwa ya kimarekani ambayo ndio mdhamini wa jezi za mabingwa wa England inasemekana wapo tayari kulipa kiasi cha pesa kilichopungua katika matakwa ya mshahara anaotaka Sneijder ili kuhakikisha uhamisho huo unafanikiwa.

Nike waliwahi kufanya kitu cha namna hii wakati mbrazili Ronaldo De Lima alipohama kutoka Barcelona kwenda Inter wakati mahasimu wao wa kibiashara Adidas, ambao wanaidhamini Real Madrid, walihusika kwa kiasi kikubwa katika kurahisha mambo kwenye usajili wa Cristiano Ronaldo na David Beckham kwenda Benebeu.

United wamekuwa wakijaribu kukamilisha dili la usajili wa Sneijder ndani ya wiki hii, huku CEO David Gill akikacha safari ya US ili aweze kupata muda wa kuongea na Inter Officials jijini Milan.

Taarifa zisizo rasmi zinasema kuwa United wapo tayari kulipa £35.2m wanayoitaka Inter lakini mazungumzo yamekwama katika matakwa binafsi ya mchezaji.Kambi ya mchezaji wanataka mshahara wa £200,000 kwa wiki huku Red Devils wakiwa tayari kulipa mshahara wa £170,000 per week.


EXCLUSIVE: CHUJI AJIUNGA RASMI NA VILLA SQUAD



Mchezaji wa zamani wa mabingwa wa Tanzania na CECAFA Kagame Cup Athumani Idd Chuji leo ametangazwa rasmi kuwa mchezaji wa klabu ya Villa Squad ya Dar Es Salaam.


Chuji ambaye baada ya kutoka Yanga alirudi Simba na kuitumikia klabu hiyo katika michuano Kagame iliyomalizika last weekend amejiunga na Villa baada ya kukatwa katika usajili wa Simba,blog hii imepewa taarifa na msemaji wa timu hiyo bwana Idd Godgod.


Wakati huo huo Villa Squad leo wamethibitisha rasmi kuwa watatumia uwanja Chamazi wa Mbagala unaomilikiwa na matajiri wa ligi kuu klabu ya Azam kama uwanja wao wa nyumbani kwenye michezo ya ligi kuu ya vodacom msimu ujao .

JUVENTUS WAINGIA KATIKA VITA YA KUMTWAA TEVEZ


Klabu ya Juventus nayo imeingia rasmi katika vita ya kutaka kumsaini Manchester City star Carlos Tevez baada ya kutuma ofa ya £45million, kwa mujibu kwa Corinthians.


City juzi walikataa ofa ya £35million kutoka kwa wakatoliki wa Brazil kwa ajili ya Carlos Tevez, lakini sasa ofa mpya iliyo mezani imeongezeka kwa £10million.

Ingawa raisi wa Corinthians Andres Sanchez amesisitiza kuwa hatoongeza ofa lakini anaamini kuwa Carlotos ana matamanio ya kurejea South America na kuwa karibu na familia yake, hivyo bado ana imani kuwa Tevez atachagua kujiunga na timu yake ya zamani.

Alisema: "Hakuna kilichobadilika, hajaamua kumuuza wala kuendelea kuwa nae.

"Wamepokea ofa ya £45m kutoka Juventus, lakini Tevez hataki kuendelea kubaki ulaya.

"Naendelea kuamini ofa niliyotuma ni nzuri, lakini inategemea na City wataamuaje.Kama ningekuwa raisi wa klabu anayochezea Tevez, basi nisingekubali kumuuza lakini kauli ya mchezaji ina uzito zaidi.Kama anataka kuondoka then ataondoka tu kwa njia yoyote.Katika soka mikataba imewekwa ili kuvunjwa."


SAMI KHEDIRA AMLIPIZIA OZIL


KIUNGO WA REAL MADRID SAMI KHEDIRA AKIWA NA MCHUMBA LENA GERCKE WAKIWASILI KATIKA MERCEDEZ BENZ FASHION WEEK, IN BERLIN LAST WEEKEND.

SUNZU KUWASILI LEO ASUBUHI SAA 3


Mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia Felix Sunzu anatarajiwa kuwasili nchini kuja kujiunga na Simba asubuhi hii.

Sunzu ambaye ni moja ya wachezaji waliong'ara katika michuano ya CECAFA SENIOR CHALLENGE CUP yaliofanyika mwishoni mwaka jana, ameachwa na timu yake ya Al Hilal ya Sudan baada ya kushindwa kuonyesha uwezo mkubwa na hivyo kupelekea nafasi yake kuchukuliwa na raia mwingine wa kigeni ndani ya timu hiyo.

Thursday, July 14, 2011

FALCAO ASAINI MKATABA MPYA NA PORTO


Mshambuliaji Rademel Falcao amemaliza utata juu ya tetesi zinahusu kuhama Porto baada ya kusaini mkataba wa mpya na mabingwa wa Ureno.

Falcao amesaini mkataba wa wa miaka 4 utakaomuweka Estadio do Dragao mpaka mwaka 2015, mabingwa hao Portugal wameithibitishia soko la hisa la Ureno.


The Colombia international ambaye alikuwa amebakiza mkataba wa miaka 2 katika mkataba wake wa mwanzo, ambao ulikuwa una kipengele cha kumruhusu kuondoka kwa euro millioni 30, lakini mkataba mpya wa Falcao una kipengele cha kumruhusu kuondoka kwa euro million 45, fedha ambayo itakuwa ni kizingiti kikubwa kwa timu zitakazomtaka.
Chelsea ni moja ya timu kubwa zinazohusishwa kwa kiasi kikubwa kutaka kumsaini mcolombia huyo mara baada tu ya kumteua Andre Villas Boas, ambaye aliiongoza Porto kushinda makombe 3 msimu uliopita.

MANCHESTER UNITED TIMU YENYE THAMANI ZADI DUNIANI


Mabingwa wa ligi kuu ya England Manchester United wametajwa na jarida la FORBES kuwa ndio klabu ya michezo yenye thamani kubwa zaidi duniani.

The Red Devils wanatajwa kuwa na thamani paundi billion 1.165 ikiwazidi vilabu tajiri kama Dallas Cowboys na New York Yankees.

Thamani ya United inahusisha timu, uwanja, mapato na mikataba ya udhamini.

Taarifa hizi ni nzuri kwa familia ya Glazer ambayo ilinunua klabu hii kwa £790m in 2005, ingawa bado wana deni la linalokaribia £500.
Mapato ya matangazo ya United yamechangia sana kwa timu hii ku-top the chart, wakiwa wanapata £80m kwa mkataba wa miaka 4 kwa udhamini wa jezi waliosaini na kampuni ya bima ya Aon pamoja na mkataba mwingine Nike wa miaka 13 wenye thamani ya £300m.

Real Madrid walishika nafasi ya pili kwa vilabu vya soka wakiwa na thamni ya £900m.
Huku habari nzuri kwa wapenzi wa Arsenal ni baada ya timu yao kushika nafasi ya saba wakiwa na thamani ya £740m.

Chelsea walishika nafasi ya 46, na timu nyingine za soka zilizoingia katika top 50 ni Bayern Munich(19), AC Milan(34) na Juventus wakashika nafasi ya 49.

Jambo la kushangaza ni kwamba timu inayoaminika kuwa ni bora ulimwenguni kwa sasa Barcelona wameshika nafasi 26 wakiwa na thamani ya £606million.

LIST YA VILABU 10 VYA MICHEZO VYENYE THAMANI KUBWA
1. Manchester United £1.165billion
2. Dallas Cowboys £1.13bn
3. New York Yankees £1.06bn
4. Washington Redskins £960million
5. Real Madrid £900m
6. New England Patriots £850m
7. Arsenal £740m
8. New York Giants £734m
9. Houstan Texans £727m
10. New York Jets £708m



OFFICIAL: JEROME BOATENG KUJIUNGA NA BAYERN


Klabu ya Bayern Munich imethibitisha rasmi kuwa inakaribia kukamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Ujerumani Jerome Boateng kutoka Man City..
Bayern wamekuwa wakimfuatilia Boateng kwa muda mrefu sasa na leo hatimaye wametangaza kufanikiwa kukubaliana na Man City dau la uhamisho ambalo halijatajwa na kuweza kumsaini Jerome kwa mkataba wa miaka 4.
Boateng, 22, alijiunga na City mwaka jana akitokea Hamburg lakini alishindwa kung'ara ndani ya Eastlands kutokana na kuandamwa na majeruhi.
Uhamisho wa beki huyo unatarajiwa kukamilika


The deal will be completed once Boateng has passed a medical in Bavaria.


VEIRA ASTAAFU SOKA ACHUKUA MAJUKUMU YA NJE UWANJA


Mchezaji wa klabu ya Manchester City mfaransa Patrick Viera ametangaza rasmi kustaafu soka na sasa atachukua majukumu mapya ndani ya klabu hiyo ya Eastlands.
Viera mwenye umri wa miaka 35 aliachwa na City baada ya kuisha kwa msimu uliopita na sasa amekubali kuchukua nafasi ya football development executive na atakuwa akishugulikia maendeleo ya soka la vijana ndani ya klabu hiyo.








OKWI AIKATAA KAIZER CHIEFS ATAKA KUCHEZA ULAYA


Mshambuliaji wa klabu ya Simba S.C Mganda Emmanuel Okwi amekataa kujiunga na klabu kongwe ya Afrika ya Kusini kwa madai kuwa anataka kucheza barani ulaya na yupo mbioni kupata timu in Europe.
Okwi ambaye bado ana mkataba wa kuichezea Simba aliivutiwa Kaizer Chiefs na timu hiyo ya Bondeni ilikuwa tayari kutoa kiasi cha dola 150,000 kwa Simba ili kuweza kumsajili kinda hilo ya timu ya Uganda under 23.
Kufuatia hatua hiyo sasa Okwi amerudi nchini Uganda kujipanga na safari yake ya kwenda kufanya majaribio barani ulaya ndani siku chache zifuatazo.

BLOG YETU IMEIBUKA KIDEDEA !!

Napenda kutumia fursa hii kuwajulisha kwamba BLOG yetu imefanikiwa kupata medali kwenye category yetu ya blog bora ya michezo kwenye tuzo za Tanzania Blogs Awards.
Naomba nitumie nafasi hii kuwashukuru woote mlioipigia kura na hatimaye kufanikiwa kuibuka kidedea, kiukweli sikuwatangazia juu ya hizi tuzo wasomaji wa hii BLOG nikiamini muda wa kuingia kwenye mashindano makubwa kama hayo ulikua bado ukichukulia ya kwamba wakati kinyang'anyiro hicho kinaanza BLOG yetu ndo kwanza ilikua na majuma takribani mawili tu kuanzishwa.. kwahiyo basi sina budi kuwambia tena AHSANTENI SANA kwa wote mliopiga kura. na nawa-promise sitawaangusha kwa nguvu za mwenyezi mungu nitajitahidi kuwapatia MADINI ADIMU YA MICHEZO kutoka kwenye huu MGODI.

Best Sports Blog

http://shaffih.blogspot.com/ 24.14%
http://fullshangwe.blogspot.com/ 22.99%
http://mamapipiro.blogspot.com 22.99%
http://aboodmsuni.blogspot.com/ 12.64%
http://mtotowakitaa.blogspot.com/ 6.9%
http://rockersports.blogspot.com 5.75%
http://sheinrangers.blogspot.com 2.3%
www.sherib.webs.com 2.3%


Best Advertising/Marketing Blog

www.bongostarlink.com/ 37.5%
http://jobstanzania.blogspot.com 18.18%
http://dartalk.com/ 15.91%
http://infotanzania.blogspot.com 7.95%
http://kingkapita.blogspot.com/ 5.68%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 5.11%
http://chickabouttown.com/ 3.98%
http://florasalon.blogspot.com/ 3.98%
www.JigambeBlogs.com 1.14%
http://dallyestate.blogspot.com/ 0.57%


Best Beauty Blog

http://8020fashions.blogspot.com/ 36.05%
http://missjestinageorge.blogspot.com 27.9%
http://thesporahshow.blogspot.com/ 13.3%
http://kilinyepesi.blogspot.com/ 7.73%
http://aidanleonce.blogspot.com/ 6.44%
http://bumimmusese.blogspot.com 2.15%
http://chickabouttown.com/ 2.15%
http://beautytouchdar.blogspot.com 1.72%
http://missiepopular.blogspot.com/ 1.72%
http://jojosssfashions.blogspot.com/ 0.86%


Best Collaboration or Group Blog

http://scholarshipnetwork.ning.com/ 32.99%
http://bongoflavortz.blogspot.com/ 19.8%
http://sherianamavazi.blogspot.com/ 11.68%
http://kilinyepesi.blogspot.com/ 10.66%
www.thehabari.com/ 5.58%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 5.08%
http://mrokim.blogspot.com 5.08%
http://novatzdream@blogspot.com 4.57%
http://bumimmusese.blogspot.com/ 4.06%
http://oswinking.blogspot.com 0.51%


Best Design Blog

http://missjestinageorge.blogspot.com 32.11%
http://bongoflavortz.blogspot.com/ 16.32%
http://dartalk.com/ 11.58%
http://laprincessaworld.blogspot.com 11.05%
http://aidanleonce.blogspot.com/ 10%
www.babkubwa.com/ 8.95%
www.thehabari.com/ 6.32%
http://missiepopular.blogspot.com 2.11%
www.mtotosix.co.cc 1.05%
http://fromcoast.blogspot.com/ 0.53%


Best Education Blog

http://makulilo.blogspot.com/ 63.21%
www.wavuti.com 21.24%
http://hapakwetu.blogspot.com/ 10.88%
http://nderumo.blogspot.com/ 2.59%
http://itycoon4idevices.blogspot.com 2.07%


Best Informative - Lifestyle Blog

http://thesporahshow.blogspot.com/ 33.07%
http://mwanasosholojia.blogspot.com/ 18.9%
http://bongoflavortz.blogspot.com/ 18.11%
http://adeladallykavishe.blogspot.com/ 10.24%
http://mtangazaji.blogspot.com/ 8.66%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 5.51%
http://nyombwe.blog.co.uk/ 2.36%
http://nderumo.blogspot.com/ 1.57%
http://bwaya.blogspot.com/ 0.79%
http://fromcoast.blogspot.com/ 0.79%


Best Informative - Entertainments Blog

http://ankomo.blogspot.com 26.36%
http://kilinyepesi.blogspot.com/ 19.38%
http://sherianamavazi.blogspot.com/ 13.18%
www.thehabari.com/ 12.4%
http://miram3.blogspot.com/ 10.08%
http://beautytouchdar.blogspot.com 6.98%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 5.43%
http://chingaone.blogspot.com/ 4.65%
http://nyombwe.blog.co.uk/ 1.55%


Best Informative - Political Blog

http://Issamichuzi.blogspot.com 39.77%
www.chahali.com 26.25%
http://mjengwa.blogspot.com/ 11.97%
http://mikochenireport.blogspot.com 9.27%
www.mohammeddewji.com/blog 2.7%
www.wavuti.com 2.7%
http://www.hakingowi.com/ 2.32%
http://nipe5.blogspot.com/ 1.93%
http://novatzdream.blogspot.com 1.93%
http://ruhuwiko.blogspot.com/ 1.16%


Best Informative - Economy Blog

http://bugangoborder.blogspot.com/ 41.44%
www.mohammeddewji.com/blog 18.23%
http://mwanasosholojia.blogspot.com 11.6%
http://fullshangwe.blogspot.com/ 11.05%
http://hapakwetu.blogspot.com/ 5.52%
http://economyticker.blogspot.com/ 4.97%
http://chesimpilipili.blogspot.com/ 2.76%
http://mrokim.blogspot.com/ 2.76%
http://chingaone.blogspot.com 1.66%


Best Informative – Sports

http://fullshangwe.blogspot.com/ 34.04%
http://mamapipiro.blogspot.com/ 22.34%
http://kinyaiyas.blogspot.com/ 12.77%
http://aboodmsuni21.blogspot.com 11 11.7%
http://allyshams.blogspot.com/ 8.51%
http://www.itsdar.net/ 5.32%
www.sherib.webs.com 4.26%
http://liwazozito.blogspot.com/ 1.06%


Best Entrepreneur Blog

www.mohammeddewji.com/blog 23.5%
http://josephatlukaza.blogspot.com 17.49%
http://mwanasosholojia.blogspot.com 14.75%
http://sherianamavazi.blogspot.com/ 13.66%
http://kilinyepesi.blogspot.com/ 12.57%
http://laprincessaworld.blogspot.com 9.84%
http://allyshams.blogspot.com/ 6.01%
http://Liwazozito.blogspot 1.64%
http://itycoon4id 0.55%
http://www.JigambeBlogs.com 0 0%


Best Entertainments Blog

http://www.bongostarlink.com/ 25.24%
http://bongocelebrity.com 19.05%
http://thesporahshow.blogspot.com/ 15.24%
http://ankomo.blogspot.com 11.9%
http://bongoflavortz.blogspot.com/ 11.9%
http://dartalk.com/ 8.57%
http://isaackin.blogspot.com/ 5.71%
http://mtotowakitaa.blogspot.com/ 1.9%
http://mrokim.blogspot.com 0.48%
http://hotspotmagazinetz.blogspot.com/ 0 0%


Best Fashion Blog

http://8020fashions.blogspot.com/ 42.29%
www.missjestinageorge.blogspot.com 25.37%
http://sherianamavazi.blogspot.com/ 11.44%
http://laprincessaworld.blogspot.com 10.95%
http://florasalon.blogspot.com/ 3.48%
http://bumimmusese.blogspot.com/ 2.49%
http://chickabouttown.com/ 1.49%
http://missiepopular.blogspot.com/ 1%
http://mtangazaji.blogspot.com/ 1%
http://jojosssfashions.blogspot.com/ 0.5%


Best Family Blog

http://bugangoborder.blogspot.com/ 40.64%
http://www.hakingowi.com/ 17.65%
http://mamanamwana.blogspot.com 11.76%
http://miram3.blogspot.com/ 5.88%
http://damija.blogspot.com 5.35%
http://adeladallykavishe.blogspot.com/ 4.81%
http://jipende.com/ 4.28%
http://ruhuwiko.blogspot.com/ 3.74%
http://mtangazaji.blogspot.com 3.21%
http://mrokim.blogspot.com 2.67%


Best Food Blog

http://activechef.blogspot.com/ 51.77%
http://mapishimatamu.blogspot.com/ 28.37%
http://tasteoftanzania.com/ 11.35%
http://mrokim.blogspot.com 5.67%
http://www.bartycake.blogspot.com/ 2.84%


Best Inspiration Blog

http://Issamichuzi.blogspot.com 32.2%
www.chahali.com 20%
http://kmanaseh.blogspot.com 18.64%
http://mjengwa.blogspot.com/ 7.8%
http://thesporahshow.blogspot.com/ 7.12%
http://mwanasosholojia.blogspot.com/ 5.76%
www.wavuti.com 4.41%
www.mohammeddewji.com/blog 3.05%
http://jipende.com/ 0.68%
http://nderumo.blogspot.com/ 0.34%


Best News Blog

http://Issamichuzi.blogspot.com 38.4%
www.chahali.com 24%
http://josephatlukaza.blogspot.com 12.8%
http://ankomo.blogspot.com 7.6%
http://dartalk.com 7.2%
www.wavuti.com 6.4%
http://chingaone.blogspot.com 1.6%
www.mrokim.blogspot.com 1.6%
http://fullshangwe.blogspot.com/ 0.4%


Best Music Blog

http://bongoflavortz.blogspot.com/ 26.06%
http://dartalk.com/ 19.01%
http://ankomo.blogspot.com 14.79%
http://www.babkubwa.com/ 9.15%
http://aidanleonce.blogspot.com/ 8.45%
www.tzhiphop.com 6.34%
http://hassbaby.blogspot.com 4.93%
http://mrokim.blogspot.com 3.52%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 2.82%
http://kingkapita.blogspot.com/ 2.82%
www.mtotosix.co.cc 2.11%


Best Out Of Towner Blog

http://bugangoborder.blogspot.com/ 52.12%
http://mjengwa.blogspot.com 29.7%
http://chingaone.blogspot.com 4.24%
http://mtwarakumekucha.blogspot.com/ 3.64%
http://kalulunga.blogspot.com/ 3.03%
www.musoma-tanzania.blogspot.com 3.03%
http://mitiki.blogspot.com/ 1.82%
http://nderumo.blogspot.com/ 1.21%
http://upolesana.blogspot.com/ 1.21%
http://nyombwe.blog.co.uk/ 0 0%


Best Personal Blog

http://fullshangwe.blogspot.com/ 22.9%
http://chekaupasuke.blogspot.com/ 19.08%
http://mikochenireport.blogspot.com 19.08%
http://simon-kitururu.blogspot.com 13.74%
http://mtangazaji.blogspot.com/ 6.11%
http://nipe5.blogspot.com/ 6.11%
http://kalulunga.blogspot.com 5.34%
http://mtotowakitaa.blogspot.com/ 4.58%
http://gadiola25.blogspot.com/ 2.29%
http://nderumo.blogspot.com/ 0.76%


Best Political Blog

http://Issamichuzi.blogspot.com 26.95%
http://bugangoborder.blogspot.com/ 26.56%
www.chahali.com 26.17%
http://mikochenireport.blogspot.com 7.42%
http://mjengwa.blogspot.com/ 5.86%
www.hakingowi.com/ 2.73%
http://novatzdream.blogspot.com 2.34%
www.thehabari.com/ 1.17%
www.mrokim.blogspot.com 0.39%
http://musoma-tanzania.blogspot.com 0.39%


Best Poetry Or Writing Blog

http://tct-blog.blogspot.com 31.25%
http://fadhilimshairi.blogspot.com/ 23.21%
http://hapakwetu.blogspot.com/ 20.54%
http://miram3.blogspot.com 20.54%
http://upolesana.blogspot.com/ 2.68%
http://saharasoulfood.wordpress.com/about/ 1.79%


Best Photography Blog

http://bongopicha.blogspot.com/ 16.22%
http://harusini.blogspot.com/ 16.22%
http://kilinyepesi.blogspot.com/ 16.22%
http://sherianamavazi.blogspot.com/ 16.22%
http://harusiyetu.blogspot.com 12.61%
http://weddingbellstz.blogspot.com/ 12.61%
http://chickabouttown.com/ 6.31%
http://chesimpilipili.blogspot.com/ 3.6%


Best Religion Blog

http://hosannainc.blogspot.com/ 20.88%
http://nyimbozadini.blogspot.com/ 18.68%
http://zanzibarislamicnews.wordpress.com/ 16.48%
http://christianceleb.blogspot.com/ 15.38%
http://strictlygospel.wordpress.com/ 10.99%
http://mtangazaji.blogspot.com/ 7.69%
http://kabulageorge.blogspot.com/ 5.49%
http://sayuni.blogspot.com/ 4.4%


Best Travel Blog

http://othmanmichuzi.blogspot.com/ 35.29%
http://mjengwa.blogspot.com/ 23.53%
http://ilovetanzania.blogspot.com 11.76%
http://ahmed-kidume.blogspot.com/ 7.06%
http://chickabouttown.com/ 7.06%
http://mrokim.blogspot.com 7.06%
http://mtangazaji.blogspot.com/ 4.71%
http://chesimpilipili.blogspot.com/ 3.53%


Best Wedding Blog

http://harusiyetu.blogspot.com 36.9%
http://harusini.blogspot.com/ 29.76%
http://weddingbellstz.blogspot.com 28.57%
http://mrokim.blogspot.com 4.76%

RENATUS NJOHOLE FOUNDATION COMING SOON!

PJ ,NJOHOLE NA MIMI

KIUNGO WA ZAMANI WA TIMU ZA MILAMBO,SIMBA NA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA RENATUS NJOHOLE AMEINGIA NCHINI HAPO JANA AKITOKEA NCHINI USWISI ANAKOISHI HIVI SASA,NJOHOLE AMEKUJA KUKAMILISHA TARATIBU ZA KUFUNGUA MFUKO WAKE WA KUSAIDIA JAMII ( NJOHOLE FOUNDATION ).



LADY JAY DEE AWAANDALIA PARTY YANGA @ NYUMBANI LOUNGE

DAVIS MWAPE, PIUS KISAMBALE NA NADIR HAROUB CANNAVARO WAKIINGIA NDANI YA NYUMBANI LOUNGE

LADY JAY DEE AKISALIMIANA NA MWENYEKITI WA YANGA LLOYD NCHUNGA.

SHEDRACK NSAJIGWA AKIMTAMBULISHA JAY DEE KWA WACHEZAJI WENZIE.
WACHEZAJI WA YANGA WAKIPATA PICHA NA SHABIKI WAO LADY JAY DEE.

WANACHAMA WAPYA WA YANGA LADY JAY DEE NA MUMEWE GARDNER WAKIHOJIWA NA CLOUDS TV.

MASHUJAA WA "KAMPALA" ALLY MAYAI NA SALVATORY EDWARD NAO WALIKUWEPO.

SHABIKI MKUBWA WA YANGA ACTOR RAY KIGOSI AKISALIMIANA NA JERRY TEGETE NA LUIS SENDEU.

KEKI YA KUWAPONGEZA MABINGWA WAPYA WA KAGAME CASTLE CUP.

MWENYEKITI NCHUNGA AKITOA SHUKRANI KWA JAY DEE NA MUMEWE.

MWENYEKITI WA YANGA AKIWAKABIDHI KADI ZA UANACHAMA "THE HABASH FAMILY"

WANACHAMA WAPYA WA YANGA LADY JAY DEE NA MUMEWE GARDNER WAKIONYESHA KADI ZAO.

"KATA KEKI TULE" JAY DEE, NSAJIGWA NA LLOYD NCHUNGA WAKIIMBA KUFURAHIA UKATAJI KEKI
GOLIKIPA YEW BERKO AKILISHWA KEKI NA BINTI MACHOZI

IKAFUATIA ZAMU YA JERRYSON TEGETE KULA KEKI

BEKI MPYA WA YANGA GODFREY TAITA AKILISHWA KEKI

MOJA YA WACHEZAJI WALIOKAA YANGA KWA MUDA MREFU FREDY MBUNA NAE AKIPATA KEKI

MUUAJI WA MNYAMA KENNETH ASAMOAH AKILISHWA KEKI NA JA YDEE

KWANINI MATOLA ASIWE NA MAJUKUMU KAMA YA ZIDANE NDANI YA SIMBA?

Mchezo wa soka ni mchezo ambao unachezwa na watu kumi na moja uwanjani ambao wana idara tofauti na majukumu tofauti ya kufanyia kazi, mfano kuna makipa ambao kazi yao ni kuzuia mpira usitinge wavuni.
Kuna mabeki ambao kazi yao ni kuhakikisha kipa hadhuriki na mchezaji wa timu pinzania hapati upenyo wa kuja kukwamisha mpira wavuni , kuna viungo ambao wengine huwa na kazi ya kuwalinda mabeki na wengine wanasaidia idara ya ushambuliaji na kuna washambuliaji ambao kazi yao ni kufunga ,wachezaji hawa kama ulivyoona wana idara tofauti ila kwa pamoja wanaunda timu ambayo ina lengo moja tu nalo ni kupata ushindi iwe ni kwenye mechi ya ligi, kombe na kadhalika .
Wachezaji wanacheza ndani ya uwanja ila kuna wachezaji wengine ambao wako nje ya uwanja ambao wanaanzia kwa kocha mkuu.
Kuna mifumo mbalimbali ambayo makocha wanafanyia kazi, kuna makocha ambao kazi yao ni kufuatilia kila kitu kinachohusu timu na wanasimamia mazoezi wao wenyewe kama vile Arsene Wenger,Fabio Capello na wengineo ambao wanafanya kila kitu mpaka kupanga koni wakati wa mazoezi hadi kuipanga “first eleven” na kuna wengine ambao wanafanya mambo kwa ujumla huku wakisaidiwa na timu ya watu mfano mzuri ni Harry Redknapp, Sir Alex Fergusson, Jose Mourinho na Kenny Dalglish.
Hawa wanasaidiwa na watu kama makocha wa makipa ambao ukienda Old Trafford utamkuta mtu anaitwa Luke Steele ambaye ni kocha wa makipa wote wa Manchester United , pia wanasaidiwa na makocha wa wachezaji kwa nafasi zao kama unakuta kuna kocha wa viungo mfano Tim Sherwood ambaye anawanoa viungo pale White Hart Lane na hata makocha wa mabeki na washambuliaji halafu kuna kocha wa timu ya kwanza yaani “first team coach” kama Joe Jordan wa tottenham, steve Clarke wa Liverpool na Mike Phelan pale Old Trafford .
Wote hawa ndio hapa wanaitwa wachezaji wa nje ya uwanja ila kuna eneo lingine ambalo kuna wachezaji wa nje ya uwanja nalo ni eneo la chumba cha mikutano ambapo kwa lugha ya kigeni “board-room”. Hili ni eneo muhimu sana ambalo pengine ndio kiini kabisa cha mafanikio ya timu . Nchi mbalimbali zina mifumo mbalimbali ya kuwapa watu madaraka ambayo ni kiungo cha uwanjani , benchi la ufundi na chumba cha mikutano ambako kuna wakurugenzi wa timu .



Ukienda Italia na Hispania Sporting directors na ukienda England kuna technical directors . Watu hawa kama ingekuwa uwanjani wangeweza kucheza eneo la namba sita ile ya kizamani ambayo falsafa yake ni kuwa mchezaji wa kila nafasi .
Miezi michache iliyopita Real Madrid ilikuwa na mtu anayeitwa Jorge Valdanao , mtu huyo hakuwa na uhusiano mzuri na kocha wake Jose Mourinho na ilifikia hatua ya kuwa mmojawapo ilibidi aondoke na hapo Valdano alionyeshwa njia kupitia kwa Rais wa timu Florentino Perez ambaye ni mtu wake wa karibu , alimwambia kuwa unaondoka hapa lakini wewe ni mwanangu na nitakupa shavu sehemu nyingine na maisha yanaendelea .
Mlango aliotokea Jorge Valdano akaingia mtu mmoja ambaye si mgeni machoni pa watu , si mgeni machoni pa walimwengu wa mchezo wa soka na zaidi ya yote si mgeni pale Real Madrid, Zinedine Zidane .
Hili lilikuwa pendekezo la Jose Mourinho ambaye kama anavyofahamika hajatazama karibu kwenye hili , hakika macho yake yametazama mbali kuliko watu wengi . Ukirejea nyuma kwenye msimu ambao Inter Millan ililiteka bara la ulaya Mourinho alimuita kwenye benchi mkurugenzi wa mawasiliano na mambo ya kimataifa wa Inter Milan Luis Felipe Madeira Figo . Kwa haraka unaweza usione mchango wa mreno huyu lakini amini usiamni , kubali ukatae Figo alichangia mawazo mengi kuiua Barcelona kwenye mchezo wa nusu fainali kama ilivyokuwa kwa Mourinho, kina Eto’o ,Militto na kina Sneijder. Baada ya hapo Mourinho anataka kurudia hayo kwa kumpa nafasi muhimu ya ‘ukurugenzi wa soka ‘ gwiji wa zamani wa Real na timu ya taifa ya Ufaransa Zinedine Zidane .
Zidane ni mtu ambaye anaheshimika ulimwenguni kote . Unakumbuka wakati kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa Laurent Blanc a.k.a “le president” au rais kwa Kiswahili alipojikuta katikati ya skendo ya ubaguzi wa rangi pamoja na shirikisho la soka la ufaransa , aliyemuokoa machoni pa watu hakuwa Nicolas Sarkozy rais wa ufaransa wala hakuwa rais wa shirikisho la soka la ufaransa bali alikuwa mtu ambaye neno lake kwa wafaransa ni kama sheria inayotungwa bungeni Zinedine Zidane .
Hiyo ndiyo heshima aliyo nayo Zidane , waandishi wa habari hawamuandiki vibaya mtu huyu , kumbuka alipomtwanga kichwa materazzi na kuinyima nchi yake ubingwa wa dunia , hakuna mwandishi aliyemuandika vibaya , wote walimuandika vibaya materazzi kwa kumdhihaki na kumfanya zizzou apandwe na hasira kiasi kile .



Na kubwa kuliko yote ni ukweli kuwa Zidane ni mtu ambaye anachukuliwa kama mfano wa kuigwa na wachezaji wote , ametwaa mataji yote unayoyajua ulimwenguni , Serie A, La liga,ligi ya mabingwa , kombe la dunia , kombe la ulaya, kombe la mabara na ametimiza ndoto ambazo wachezaji wengi nyota wametimiza na hiyo ni changamoto tosha kwa wachezaji wa Real Madrid ambao kwa muda mrefu wamekuwa hawana kitu cha kuwa mshawasha na mzuka wa kupata ushindi kama wenzo Barcelona ambao wanae Zidane wao Pep Guardiola ambaye anajua jinsi ya kuwapa “inspiration” wachezaji wake.
Hapa nchini kwetu wapo kina Zidane ambao wanaweza kuwekwa kwenye maeneo muhimu ya mchezo wa soka katika ngazi ya vilabu na hata timu za taifa .
Klabu ya Simba ina mtu anayekwenda kwa jina la Selemani Matola , wenyewe Msimbazi enzi zake walikuwa wakimuita “veron”. Matola amekuwa Simba kwa muda mrefu na ndiye nahodha wa klabu hiyo ambaye ana historia nzuri inayong’aa . Katika wakati wake ametwaa mataji mengi sana ambayo hakuna nahodha mwingine sio tu Simba hata kwa watani wao Yanga anayeweza kumfikia , Matola ni mtu ambaye Simba inaweza kumfanya kama Madrid walivyomfanya Zidane . Wachezaji wa Simba wanaweza kufaidika kwa Matola kwani anaweza kuwapa vitu vingi sana vya msingi kwani amekuwa hapa walipo na amefanya wanayofanya wao na zaidi .
Super sports United walimwona Matola kwenye mchezo mmoja tu na ulitosha kuwashawishi kuilipa Simba fedha na kumchukua “Veron” kwenda naye ‘sauzi’ ambako kama isingelikuwa umri angecheza mpaka leo hii, na huko si kwamba alikuwa akisugua benchi , Matola alikuwa anaanza mechi karibu zote .
Kwa bahati mbaya hakuwahi kuwa na historia nzuri kwenye timu ya taifa lakini Matola ni gwiji pale Simba na klabu hii inahitaji mchango wake .
Ana mengi ambayo yanaweza kuisaidia klabu hii na kama viongozi wake ni watu makini wanaojua mpira wanaweza kufuata mfano wa Florentino Perez ambaye alimsikiliza Mourinho na kutimiza alichohitaji nacho ni kumpa Zizzou nafasi ya Mkurugenzi wa michezo, vivyo hivyo nafasi kama hii inaweza kumfaa Selemani Matola kwenye klabu ya Simba .

Wednesday, July 13, 2011

KAMA INGEKUA HII IMETOKEA BONGO HUYU JAMAA ANGEFANYWAJE ?

MICHEZO YA AFRIKA (ALL AFRICA GAMES)


Timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twiga Stars) imepangwa kundi B katika Michezo ya Afrika (All Africa Games). Michezo hiyo ya Kumi itafanyika kuanzia Septemba 3-18 mwaka huu jijini Maputo, Msumbiji.

Upangaji makundi kwa ajili ya michezo hiyo kwa upande wa wanawake na wanaume ulifanywa jana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Hicham El Amran.

Rais wa CAF, Issa Hayatou pia alishuhudia upangaji huo wa makundi uliofanyika makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri wakiwemo pia wawakilishi wa timu zilizofuzu kwa ajili ya michezo hiyo.

Twiga Stars imepangwa pamoja na timu za Afrika Kusini, Zimbabwe na Ghana. Kundi A lina wenyeji Msumbiji, Cameroon, Algeria na Guinea. Mabingwa wa mwaka 2007 Nigeria wameshindwa kufuzu kwa ajili ya michuano ya mwaka huu.

Wiki iliyopita Twiga Stars ilikuwa Harare, Zimbabwe kwenye mashindano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA). Ilishika nafasi ya tatu ambapo ilicheza na Zimbabwe na Afrika Kusini. Zimbabwe ‘Mighty Warriors’ ndiyo walioibuka mabingwa wakati Afrika Kusini ‘Banyana Banyana’ ilikuwa makamu bingwa.

Twiga Stars inayofundishwa na Charles Mkwasa akisaidiwa na Nasra Mohamed inatarajia kuingia kambini mwezi mmoja kabla ya kuanza michuano hiyo inayoshirikisha timu nane.

Kwa upande wa wanaume kundi A lina wenyeji Msumbiji, Afrika Kusini, Libya na Madagascar wakati kundi B ni Cameroon, Uganda, Ghana na Senegal.

CORINTHIANS WAGOMA KUONGEZA OFA YA TEVEZ


Manchester City wameambiwa na Corinthians: Ofa yetu kwa Tevez ndio ya mwisho chukueni au iacheni.

Ofa ya wabrazili hao ya paundi million 35 ilikataliwa na Eastlands club jana usiku.

City wanataka kupata angalau paundi million 50 na inaamnika klabu mbili za jiji la Milan zinafuatilia kwa karibu.

Raisi wa Corinthians Andre Sanchez alisema: “Ikiwa uhamisho wa Tevez hautokamilika mpaka kufikia Jumapili basi dili hili halitakuwepo mwaka huu.Tevez amekubali kusaini kwa miaka 4 na kupunguza kiwango cha mshahara kwa sababu anatamani kurudi hapa.

“Kama City wanataka paundi 50m basi atabaki England, Corinthians hatutoongeza ofa hiyo.”

MAN CITY WAMENIDHARAU SANA - ADEBAYOR



Emmanuel Adebayor amekubali kurudi katika mazoezi ya Manchester City Jumatatu, ingawa amehuzunishwa sana na taarifa aliyopewa na klabu hiyo.

Adebayor amekasirika sana na jinsi alivyoondolewa kutoka ziara ya America ya timu hiyo, Manu anahisi kudhalilishwa baada ya kupokea email akiwa mapumzikoni akiambiwa anaweza kufanya mazoezi na reserves tu na kwamba hatakuwa na nafasi katika kikosi cha kwanza.

The straiker , ambaye alikataa kuhudhuria mazoezi wiki hii, anaamini hakutendewa sawa: "Sijui nimewakosea nini.Nilipata email kutoka kwa klabu, nikiwa kwenye mapumziko akiniambia kuwa sitoweza ku-train na kikosi cha kwanza.Hili ni tusi kwangu kwa kuniambia kuwa na-fit kufanya mazoezi na reserves tu.

"Nitarudi mazoezini lakini nimejisikia kutukanwa na kukosewa heshima."