Search This Blog

Saturday, January 19, 2013

SHABAAN KADO AIDHINISHWA KUICHEZEA COASTAL UNION - PINGAMIZI LA MTIBWA LAPIGWA CHINI

AZAM YAANZA KWA KIPIGO KENYA - YACHAPWA 2-1 NA AFC LEOPARDS

Timu ya soka ya Azam leo imepokea kipigo cha kwanza katika ziara yake huko nchini Kenya. Azam ambayo hivi karibuni walitetea ubingwa wao wa Kombe la Mapinduzi kwa kuifunga Tusker ya Kenya, leo walicheza na AFC Leopards katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi na wakafungwa 2-1 huku wachezaji wao wawili Atudo na Mcha Vialli kukosa penati mbili walizopewa ndani ya dakika 90 za mchezo.

HII NDIO YANGA BWANA - HIVI NDIVYO ILIVYOWATANDIKA WASAUZI TAIFA LEO

 Didier Kavumbagu (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Black Leopards, wakati wa Mchezo huo, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete.
jj
 Kikosi cha Yanga.
 Kikosi cha Black Leopards.
 Mchezaji wa Yanga, Kabange Twite (kushoto) akimiliki mpira huku akidhibitiwa na beki wa Black Leopards, Nkosiabo Xakane, wakati wa mchezo huo.
Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete. (PICHA NA SUFIANI MAFOTO)

TEGETE ANATISHA - APIGA MBILI YANGA IKIWAPIGA WASAUZI 3-2 UWANJA WA TAIFA

EXCLUSIVE: WAPINZANI WA YANGA - BLACK LEOPARDS WAJIFUA UWANJA WA TAIFA TAYARI KULIKABILI JESHI LA MANJI KESHO

Wachezaji wa timu Black Leopards kutoka Afrika ya kusini jioni ya leo hii wakiwa kwenye uwanja wa taifa wakifanya mazoezi tayari kwa kuikabili Yanga kesho katika dimba hili hili.

SIMBA WAPIGWA 3-1 NA TIMU YA JESHI LA OMAN

Mabingwa wa soka Tanzania, Simba walifungwa mabao 3-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya jeshi la Oman..
mechi ilichezwa Ijumaa jioni kwenye uwanja wa Qaboos complex jijini muscat.
Bao la simba lilifungwa katika kipindi cha pili na Haruna Moshi 'boban'.
Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage alikuwa jukwaani pamoja na viongozi wengine wa Simba, Rahma Al Kharusi na Musleh Rawahi pamoja na kocha Talib Hilal wakiishuhudia simba ikizama mbele ya wanajeshi hao ambao kikosi chao kina wachezaji tisa wanaocheza timu ya taifa ya Oman.
Boban na wenzake wakishangilia goli
Washabiki wa Simba wakishangilia goli lilofungwa na Boban
Kaseja, Mwinyi Kazimoto, Mrisho Ngassa, Sunzu wakiwa benchi huku wakizungumza na mfadhili wa safari yao Bi.Rahma na mwenyekiti wao Aden Rage.
Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage akiwa wenyeji wake huko Oman wakiangalia Simba ikisurubiwa na wanajeshi. (
PICHA NA SALEH ALLY WA CHAMPIONI/GLOBAL PUBLISHERS

Friday, January 18, 2013

KUIONA YANGA IKIPIMA UBAVU NA BLACK LEOPARDS NI SHILINGI 3500 - 30,000

WAKATI mabingwa wa soka wa Afrika Mashariki na Kati, Yanga kesho watacheza mechi ya kwanza ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini, kocha wa Black Leopards ametema cheche na kusema wataibuka na ushindi mkubwa kutokana na uzoefu wao wa mashindano ya Kimataifa.
Mchezo huo umepangwa kuanza saa 10.00 jioni na maandalizi yake yamekwisha kamilika huku waandaaji wakipunguza viingilio ili kuwawezesha mashabiki wengi kufika.
Mratibu wa mechi hiyo, Shafii Dauda wa Prime Time promotion alisema jana kuwa maandalizi yote yamekamilika na wamepunguza kiingilio cha shs 5,000 na shs 7,000 na kuwa cha shs 3,500 ili kuwafanya mashabiki wengi kuona mechi hiyo.
Viingilio vingine ni shs 7,000 kwa viti vya rangi ya machungwa, wakati VIP C ni shs 15,000 , VIP B shs 20,000 na VIP A shs 30,000
Dauda alisema kuwa Black Leopards wamewasili na kutamba kushinda mechi hiyo kutokana na uzoefu waliopata katika mashindano mbali mbali ikiwa pamoja na kombe la Shirikisho.
Kocha wa timu hiyo, Abel Makhubela alisema kuwa wanauzoefu wa siku nyingi na walifanya ziara nchi mbali mbali katika afrika na kuja Tanzania ni moja ya faraja kwao.
“Ziara hii ziara yetu ya kwanza Tanzania, tumefanya ziara nchini Zimbabwe na nchi nyingie, tulipata matokeo mazuri na vile vile tunatarajia kupata matokeo mazuri hapa, nimekuja na wachezaji wangu wote wa kikosa cha kwanza, jumla ya wachezaji ni 23, mashabiki watarajie mchezo mzuri,” alisema Makhubela.
 Alisema kuwa wanaijua Yanga na Simba ni moja ya timu nzuri na maarufu bara la Afrika na hivyo wamejiandaa kwani ni kipimo kizuri cha ligi ya kwao ambayo ipo katikati..


BLACK LEOPARDS YATUA TAYARI KUIPIMA YANGA KESHO TAIFA


 
 Kikosi cha  Wachezaji 28 na viongozi 11 wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini,wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili mchana wa leo kwa ndege ya shirika la Afrika Kusini, kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius kambarage Nyerere.
Kikosi cha  Wachezaji 28 na viongozi 11 wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini,wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waratibu wa shindano hilo,kutoka kampuni ya Prime Time Promotions Ltd,Pichani kushoto ni Shaffih Dauda,Mmoja wa Wakurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Godfrey Kusaga,Mtangazaji wa kipindi cha Sports Extra,Mbwiga Mbwiguke,Mdau Juma pamoja na Stuart
 Nahodha wa timu ya  Black Leopards ya Afrika Kusini akizungumza na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali mara baada ya kuwasili na kikosi chake kizima leo mchana tayari kwa kupambana na timu ya Yanga Sports Club,kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
 Waratibu kutoka Prime Time Promotions Ltd,Shaffih Dauda pamoja na mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni hiyo Godfrey Kusaga wakifanya mawasiliano leo mchana mara timu ya  Black Leopards ya Afrika Kusini ilipowasili kwenye uwanja wa  ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K.Nyerere.
 Shaffih Dauda akiwa ameambatana kocha wa timu ya  Black Leopards ya Afrika Kusini,Abel Makhubele mara baada ya kuwasili leo mchana kwenye uwanja wa  ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K.Nyerere.
 Wachezaji wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini,wakiingia kwenye basi kubwa la timu ya Yanga,wayatarajia kumenyana nayo hapo kesho kwenye uwanja wa Taifa,Jijini dar.
 Kikosi cha  Wachezaji 28 na viongozi 11 wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini,wakiwasili mapema leo mchana kwa ndege ya shirika la Afrika Kusini, kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K. kambarage Nyerere.Picha zote na JIACHIE BLOG.
======  ======= ======= =======
WAKATI mabingwa wa soka wa Afrika Mashariki na Kati, Yanga kesho watacheza mechi ya kwanza ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini, kocha wa Black Leopards ametema cheche na kusema wataibuka na ushindi mkubwa kutokana na uzoefu wao wa mashindano ya Kimataifa.

Mchezo huo umepangwa kuanza saa 10.00 jioni na maandalizi yake yamekwisha kamilika huku waandaaji wakipunguza viingilio ili kuwawezesha mashabiki wengi kufika.
Mratibu wa mechi hiyo, Shafii Dauda wa Prime Time promotion alisema jana kuwa maandalizi yote yamekamilika na wamepunguza kiingilio cha shs 5,000 na shs 7,000 na kuwa cha shs 3,500 ili kuwafanya mashabiki wengi kuona mechi hiyo.
Viingilio vingine ni shs 7,000 kwa viti vya rangi ya machungwa, wakati VIP C ni shs 15,000 , VIP B shs 20,000 na VIP A shs 30,000
Dauda alisema kuwa Black Leopards wamewasili na kutamba kushinda mechi hiyo kutokana na uzoefu waliopata katika mashindano mbali mbali ikiwa pamoja na kombe la Shirikisho.
Kocha wa timu hiyo, Abel Makhubela alisema kuwa wanauzoefu wa siku nyingi na walifanya ziara nchi mbali mbali katika afrika na kuja Tanzania ni moja ya faraja kwao.
“Ziara hii ziara yetu ya kwanza Tanzania, tumefanya ziara nchini Zimbabwe na nchi nyingie, tulipata matokeo mazuri na vile vile tunatarajia kupata matokeo mazuri hapa, nimekuja na wachezaji wangu wote wa kikosa cha kwanza, jumla ya wachezaji ni 23, mashabiki watarajie mchezo mzuri,” alisema Makhubela.
 Alisema kuwa wanaijua Yanga na Simba ni moja ya timu nzuri na maarufu bara la Afrika na hivyo wamejiandaa kwani ni kipimo kizuri cha ligi ya kwao ambayo ipo katikati..

UPANGAJI MATOKEO YA MECHI KWENYE KAMARI UNAZALISHA MABILIONI YA FEDHA KWA MWAKA

Katibu mkuu wa Interpol Ronald K. Noble amesema mapato yanayotokana na upangaji wa matokeo kwenye mechi za soka yanafikia mabilioni ya fedha.
 
Pamoja na vyombo vinavyoongoza soka UEFA na FIFA, Interpol inaongoza mkutano wa siku mbili kuhusu upangaji wa matokeo kwenye soka huko mjini Rome-Italy. 

Noble alisema biashara isiyo halali ya kucheza kamari kwenye soka inayopelekea upangaji matokeo inatengeneza mabilioni ya Euro kwa mwaka, mapato ambayo ni sawa ya na kampuni kubwa duniani ya CocaCola. 

Katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke amesema njia sahihi ya kupambana na suala hili kuanzia kwenye ngazi ya chini kabisa, kwa wanasoka wa wadogo na kuwafundisha maadili mazuri ili wakue nayo na kujiepusha na mchezo huo wa upangaji wa matokeo ambao ameuita ni kirusi kwenye soka.

Mapema wiki hii makamu wa Raisi wa La Liga alisema kwamba anaamini kwenye ligi kuu ya Spain kumekuwepo na mechi nyingi zinazopangwa matokeo, huku akionya kwamba skendo iliyoikumba soka la Italia inakaribia kwenye la liga.

BAADA YA SUAREZ KUKIRI KUJIRUSHA ILI KUPATA PENATI - LIVERPOOL YASEMA ITAMUADHIBU KWA KITENDO CHAKE

BRENDAN RODGERS amembwatukia Luis Suarez baada ya mshambuliaji huyo wa Uruguay kukiri kwamba ajirusha ili kuweza kuipa ushindi timu yake.

Suarez jana alikaririwa na vyombo vya habari akikiri kwamba alijirusha kwenye mechi dhidi ya Stoke msimu huu na kuisadia timu yake kupata penati illiyoipa ushindi Liverpool.

Lakini masaa machache bvaada ya Suarez kukiri dhidi ya vitendo vyake hivyo, kocha Brendan Rodgers amekasirishwa sana, huku akiapa kumuadhibu mshambuliaji huyo.

Rodgers alisema: “Nadhani sio sahihi na haikubaliki. Nimeongea na Luis na suala hili litashughulikiwa na klabu.

“Kujirusha sio kitu ambacho tunaweza kukivumilia, maadili yetu yapo sahihi."

Suarez jana kupitia mahojiano yake na  Fox Sports Argentina alikaririwa akisema: 'Natuhumiwa kuwa najirusha sana kwenye mechi tena hasa kwenye eneo la hatari. Walisema hivyo tulipocheza na Stoke City, kwa siku ile walikuwa sahihi. Nilijirusha ili kupata penati kwa sababu nataka timu yangu ishinde."

SIMBA WAANDALIWA TAFRIJA NZITO NA MDHAMINI WA SAFARI YAO OMAN


Mdhamini wa safari ya Simba Rahma jana aliwaalika Simba nyumbani kwake eneo la Al Kheri jijini Muscat, Oman jana usiku kwa ajili ya chakula cha usiku.
Walikula pamoja na baadaye bendi maalum kutoka Tanzania iliwapigia muziki na wakaserebuka pamoja huku Rahma akimwaga noti kama maji.

Katika hafla hiyo, Rahma alikabidhiwa jezi ya Simba na Musleh Rawah ambaye ni mmoja wa wadau wa Msimbazi na jezi ya timu ya taifa ya Oman na kocha wa makipa wa timu hiyo, Haroun Amur.

PICHA NA SALEH ALLY WA CHAMPIONI/GLOBAL PUBLISHERS

Thursday, January 17, 2013

CHEMSHA BONGO: HUYU NI MCHEZAJI GANI WA LIGI KUU YA ENGLAND


ASAMOAH GYAN: SITOPIGA PENATI TENA - MAMA ALINIKATAZA

Gyan discovered you're not allowed to throw the ball between your legs (Getty) 

Michuano ya 29 ya AFCON  ikiwa imebakiza siku chache kabla ya kuanza, huku timu ya taifa ya Ghana ikiwa ni moja ya timu zinazopewa nafasi kubwa ya kunyakua ubingwa wa michuano hiyo kwa pamoja na timu za Zambia, Ivory Coast na Nigeria.

Ghana itakuwa ikiongozwa na nahodha Asamoah Gyan, lakini kwa hakika itakuwa ngumu kumuona mshambuliaji wa zamani wa Sunderland na Udinese akienda kupiga mpira wa penati ikiwa Black Stars watapata penati.

Sio kwa sababu nyingine yoyote bali binafsi - hayati mama yake mzazi alimwambia asipige. 

 KutokaBBC:
"Nimeamua kutokupiga penati kwenye mechi za timu ya taifa," Gyan alisema.
"[...] Nilisema miezi michache iliyopita kwamba sitopiga penati, kabla mama yangu hajafariki mwezi November 2011 aliniambia nisipige penati tena."
Kwanini hayati mama yake alimwambia maneno hayo ambayo yamelionyesha hakuwa anamuamini mwanae?? Gyan anajibu kwamba penati aliyokosa katika robo fainali ya kombe la dunia 2010 dhidi ya Uruguay, ambayo ingeifanya Black Stars kutinga nusu fainali ya WOZA 2010.

Pia katika michuano ya AFCON 2012, Gyan alikosa penati katika mechi ya nusu fainali dhidi ya Zambia ambayo iliingia fainali na kuifunga Ivory Coast kisha kubeba ubingwa.

Ingawa mshambuliaji huyo mwenye miaka 27 anaweza akalazimika kupiga penati ikiwa timu yake itakwenda katika hatua ya kupigiana penati ili kuamua mshindi.

SEATTLE SOUNDERS WAKUTANA NA MH.RAISI JAKAYA KIKWETE








LOOK ROO'S BACK??: WAYNE ROONEY AIVUSHA MAN UNITED FA CUP VS WEST HAM


Manchester United vs West Ham 1:0 MATCH HIGHLIGHTS by UCL2410