Search This Blog

Saturday, August 20, 2011

MATOKEO YA VODACOM PREMIER LEAGUE.

PREMIER LEAGUE RESULTS




COASTAL UNION 1:1 MTIBWA SUGAR



TOTO AFRICANS 3: 0 VILLA SQUARD



POLISI 0: 0 AFRICAN LYON



AZAM FC 1: 0 MORO UTD






Arsenal 0-2 Liverpool: Kutolewa kwa Frimpong na Mabadiliko ya Liverpool yalibadilisha mchezo.



VIKOSI VYA KWANZA
Bao la kujifunga la Aaron Ramsay na lingine rahisi la Luis Suarez yalitosha kuipa Liverpool ushindi wao wa kwanza wa msimu na ushindi wao wa kwanza dhidi ya Arsenal kwenye uwanja wa Emirates .
Arsene Wenger alilazimika kumchezesha Samir Nasri pamoja na ‘issue’ yake ya kuhamia Man City . Emmanuel Frimpong alichukua nafasi ya Alex Song anayetumikia adhabu na majeraha ya wachezaji wengine yalimaanisha kuwa Arsenal ilimuanzisha Carl Jenkinson kwenye upande wa kulia wa ‘defense’ na kwa mshangao wa wengi akamchezesha Bacary Sagna kwenye nafasi ya beki wa kushoto.
Kenny Dalglish hakumwanzisha Luis Suarez kwa kuwa bado hana ‘match fitness’ kwa hiyo akampanga Dirk Kuyt kwenye upande wa kulia wa ‘midfield’ huku Martin Kelly akicheza nyuma yake .
Kwa ujumla hii ni mechi ambayo ilikosa vitu vingi kiufundi kwa pande zote mbili za Liverpool na Arsenal –Nafasi nyingi za wazi zilitokana na makosa pamoja na mashuti ya mbali na hakukuwa na ufundi wala ujanja wowote kwa timu hizi mbili na Liverpool walipata nafasi ya kuufungua mchezo baada ya mchezaji wa Arsenal Emmanuel Frimpong kuonyeshwa kadi nyekundu kinyume na hapo ilikuwa inaonekana kama sare nyingine ya 0-0 ingetokea.

SARE YA MWANZONI.
Dalglish alikuwa na wepesi wa kuweza kutumia mifumo kati ya 4-4-2 na 4-3-3 kutegemea na ambavyo viungo Jordan Henderson na Dirk Kuyt walivyojipanga kuendana na ‘move’.Dalglish alimpendelea zaidi Kuyt kwa mtindo wake wa uchezaji ambapo hachoki na anakimbia muda wote na hii ikaonekana kama Liverpool wanatumia 4-2-3-1 dhidi ya 4-3-3 ya Arsenal, huku Frimpong akimiliki mpira mara nyingi.

Kwa mchezo dhidi ya Liverpool Frimpong alikuwa mchezaji bora na ndiyo sababu kuu ya Arsenal kufungwa kwa Arsenal , alitolewa kwa kadi nyekundu kwa rafu ya kijinga ambayo hakuwa na sababu ya kuicheza kwa Lucas na akatolewa kwenye dakika ya 70 baada ya kupewa kadi ya njano ya kizembe kwenye dakika ya 7.
Hatari za kiungo mkabaji kuonyeshwa kadi ya njano mapema zimezungumzwa sana na kutolewa kwa Frimpong kuliigharimu Arsenal na ishara za kutolewa kwake zilionekana tangu mapema .
Frimpong alimiliki mpira vizuri sana .

Huku Henderson akikabana na Ramsay kwa muda mrefu kwenye mchezo na Charlie Adam akilazimika kurudi nyuma ili kuwa karibu na Lucas , Frimpong alikuwa na nafasi kubwa sana kwenye eneo la katikati mwa uwanja na alitumia uhuru alioupata kupandisha timu mbele na kuanzisha mashambulizi kuliko kupiga pasi za ‘square’ pembeni mwa uwanja .
Mara nyingi alipiga pasi zilizoelekea mbele na alikaribia hata kufunga kwa shuti la mbali .
PRESSING YA LIVERPOOL’.
‘Pressing’ ya Liverpool iliisaidia Arsenal kwa kiasi Fulani kwa sababu upigaji wao wa pasi kuanzia nyuma mpaka mbele kwa washambuliaji haukutofautiana sana na ule wa kwenye mchezo dhidi ya Newcastle , ulikuwa wa kasi ndogo mno .

Tatizo la majeraha ambayo yamekuwa yakiwakumba wachezaji wa Arsenal halikuwasaidia . Bacary Sagna alikuwa anapata tabu sana kupandisha mipira upande wa kushoto na tatizo hilo pia lilionekana kwa Vermalaen pale ambapo alilazimika kuhamia upande wa kulia baada ya kutoka kwa Laureant Koscielny.Huku Sagna na Vermalaen wakicheza sehemu ambazo si sehemu zao za kawaida , na wachezaji kama Miquel na Jenkinson wakiwa kwenye mechi yao ya kwanza jambo ambalo liliwafanya wacheze kwa woga , pasi za Arsenal kuanzia nyuma zilikuwa mbaya mno kwa kuwa hazikuwa kwenye kasi ya Arsenal iliyozoeleka .
Liverpool wanapaswa kupongezwa kwa aina yao ya ‘pressing’ . Kuyt , Henderson na Stewart Downing waliwatia mabeki na Viungo wa Arsenal presha ya hali ya juu ukizingatia kuwa Charlie Adam kwa kawaida hana kasi na hana ‘movement’ nyingi awapo uwanjani japo kwa mchezo dhidi ya Arsenal alijitahidi sana hasa pale alipokuwa hana mpira , akifanya ‘tackling’ karibu tano ambazo zilifanikiwa na alifanya ‘interceptions’ tatu za uhakika .
Liverpool walimiliki mpira zaidi ya Arsenal pia kitu ambacho si cha kawaida kwa Arsenal ambao humiliki mpira zaidi na Liverpool ambao mpira wao ni wa kasi na moja kwa moja zaidi usiozingatia sana kumiliki mpira kwa muda mrefu.

Waliomiliki mpira kwa kiasi kikubwa walikuwa mabeki wa pembeni japo kulikuwa hakuna mpango wowote wa kutafuta bao mapema tofauti na ule wa kumtumia Andy Caroll wa kumlisha mipira ya juu kwa kutegemea urefu wake . Mabeki wa kati wa Arsenal wanapswa kupongezwa pia kwa jinsi walivyoweza kummudu Caroll na urefu wake huku ‘combinationa ya Downing na Caroll ikionekana kufanya kazi vyema japo hadi sasa hakuna krosi yoyote ya Dwoning ambayo imekutana na kichwa cha Caroll na kuzalisha bao .
Jose Enrique alikuwa mchezaji bora kwa Liverpool kwenye na Theo Walcott hakuwa na jinsi ya kumzidi ujanja , Enrique ana kasi kuliko Walcott na ana nguvu na’positioning’ yake ni nzuri kiasi cha kutokuwa na tatizo lolote akiwa anamkaba na Walcot kwa upande wake hakuwa na mchango mkubwa kwenye mchezo .Walcott na Arshavin wanahitaji kuingia ndani na kutafuta mabao wakati mpira uko kwenye winga nyingine –Walcott anasema kuwa anapenda kuchezeshwa kati kama mshambuliaji lakini kuna ‘move’ kwenye dakika ya 28 ambapo Walcott alibaki kwenye winga ya kulia wakati kama angekimbia kuingia kati angeweza kupata bao rahisi.

DAKIKA YA 70

Mchezo ulikuwa sare hadi dakika ya 70 ambapo mambo mawili yalitokea . Kwanza Frimpong alitolewa kwa kadi nyekundu na pili Raul Mereles aliingia kuchukua nafasi ya Jordan Henderson na Andy Caroll alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Luis Suarez.
Mambo haya yalitokea kwa kufuatana na ni vigumu kusema ni tukio gani lilikuwa na ‘impact’kwenye mchezo kuliko linguine lakini yote yalikuwa na ‘impact’ kubwa .
Liverpool walifaidika na kuwa na mtu mmoja zaidi uwanjani kwani walimiliki mpira .

Mpaka kufikia dakika ya 70 Arsenal walikuwa wamepiga pasi 322 na Liverpool walikuwa wamepiga 281 –lakini kuanzia dakika ya 71 kwenda mbele hadi mwisho Arsenal walipiga pasi 105 na Liverpool walipiga 141 .Faida ilikuwa upande wa Liverpool.
Hapa ndipo msingi wa ushindi wa Liverpool ulipojengewa na ‘move’ nyingi zilianzia kipindi hiki huku Meireles na Suarez wakitengeneza nyingi zaidi .

Kutoka kwa Frimpong kulimaanisha kuwa Arsenal ililazimika kutumia mfumo wa 4-4-1, hii ilimpa Meireles nafasi kubwa katikati ya wachezaji wa Arsenal na aliweza kupeana pasi na wenzie .
Kuingia kwa Suarez kuliongeza ‘movement’ za kijanja zaidi ya zile zilizokuwepo wakati Caroll akiwa uwanjani . Mabao yote mawili yalianza na pasi za Meireles kwa Caroll . La kwanza ilikuwa bahati mbaya kwa Aron Ramsay kujifunga nala pili lilikuwa ‘move’ nzuri ambayo ilimkuta Suarez akiwa mwenyewe na kumaliza .


Mwisho.
Mchezo haukuwa wa kusisimua kama ilivyotarajiwa na ulipata uhai kwenye dakika 20 za mwisho –nidhamu mbaya iliwagharimu Arsenal , lakini mbinu za Dalglish zilifanya kazi na kufanikiwa .

Alitoka sawa na Arsenal wakiwa 11 v 11 , na akaingiza wachezaji ambao walikuwa wajanja kuyafanyia kazi mashimo yalionekana nyuma baada ya Arsenal kubaki 10. Arsenal bado hawajawa na ushinda uliozoeleka toka kwao .
Walikosa uzoefu kwenye wachezaji wanaocheza nafsi muhimu kama nyuma na pia walikosa ubunifu mbele mara nyingi Robin Van Persie akipiga miayo mwenyewe, hakuna anayejua nini kitawakuta wiki ijayo watakapokutana na Man United .















FIFA YARUHUSU ITC YA KAGO ITOLEWE

Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) limeruhusu Shirikisho la Mpira wa Miguu Jamhuri ya Afrika ya Kati kutoa Hati ya Uhamisho ya Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Gervais Anold Kago aliyejiunga na timu ya Simba kutoka Olympic Real de Bangui ya huko.

FIFA imeruhusu ITC itolewe baada ya kubaini kuwa Simba ilituma maombi ya kuomba hati hiyo ndani ya muda uliopangwa, lakini CAR ilishindwa kufanyia kazi. Hivyo kinachosubiriwa sasa ni CAR kutuma ITC hiyo.

Licha ya FIFA kuagiza hivyo, TFF imeitaka Simba kukata jina moja kati ya sita ya wachezaji wa kigeni ilionao katika orodha yake. Kanuni ya Ligi Kuu ya Vodacom inaruhusu timu kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi watano.

Wachezaji wa kigeni ambao Simba ina mikataba yao ni Derrick Walulya, Emmanuel Okwi, Felix Sunzu, Gervais Kago, Patrick Mafisango na Jerry Santo.

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji wakati ikipitia usajili iliagiza kuwa Walulya ambaye Simba ilisema imemuacha ni mchezaji wake kwa vile bado ina mkataba nayo. Hivyo inachotakiwa kufanya Simba ni kuvunja mkataba wa mchezaji mmoja ili kubaki na watano.

AFRICAN LYON KULIPA WACHEZAJI KWA MAKATO

Timu ya African Lyon imeomba kuwalipa kwa makato ya mlangoni wachezaji wake wawili wanaoidai; Godfrey Komba na Abdul Masenga ambao ilikatiza mikataba yao msimu uliopita. Awali Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji iliiagiza Lyon kuwalipa wachezaji hao kufikia Agosti 17 mwaka huu vinginevyo isingeruhusiwa kushiriki Ligi Kuu ya Vodacom inayoanza leo (Agosti 20 mwaka huu).

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liliitaka Lyon ithibitishe kwa maandishi kuwa itakatwa kwenye mapato yake ya mlangoni katika mechi hadi deni la wachezaji hao litakapomalizika. Lyon imetekeleza maagizo hayo, hivyo imeruhusiwa kucheza mechi yake ya leo (Agosti 20 mwaka huu) dhidi ya Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Hivyo Lyon itakatwa katika mechi yake ya leo ili kulipa deni hilo. Kama fedha ilizopata katika mgawo hazitatosha kulipa deni hilo itakatwa sehemu iliyobaki katika mechi inayofuata.

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji katika kikao chake cha Januari 7 mwaka huu chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa kiliiagiza Lyon iwalipe wachezaji hao baada ya kusitisha mikataba yao nje ya taratibu za kimikataba. Masenga na Komba kila mmoja anadai sh. milioni 4.3.

Wachezaji hao wataarifiwa juu ya utaratibu wa malipo yao ambapo TFF ndiyo itakayofanya makato kwa niaba yao.

Friday, August 19, 2011

PREVIEW: ARSENAL VS LIVERPOOL

Siku zote mechi kati ya timu hizi mbili huwa za kusisimua sana . Kumbuka bao la kusawazsiha la Dirk Kuyt kwenye dakika ya 112 mwezi aprili , bao ambalo lilimaliza kabisa matumaini ya Arsenal kwenye mbio za ubingwa kwa msimu uliopita , ukiacha bao hilo la Dirk Kuyt kuna kosa alililofanya Pepe Reina kwenye mchezo wa raundi ya kwanza kosa lililoipa Arsenl pointi moja kwenye mchezo wa kwanza wa Roy Hodgson msimu uliopita .

Hakuna atakayesahau mabao manne ya Andrey Arshavin kwenye sare ya 4-4 kwenye uwanja wa Anfield mwaka 2009, mchezo wa Jumamosi unaweza kutazamwa kama mchezo wa kuwania nafasi ya 4 na timu zote mbili zina mengi ya kufanya ili kuridhisha mashabiki wake .

Liverpool inatarajiwa kuwatumia Dirk Kuyt na Martin Kelly kwenye upande wa kulia wa kiungo na beki,haya yakiwa mabadiliko tofauti na kikosi cha wiki iliyopita ambapo Liverpool ilianza na Jordan Henderson na John Flanagan kwenye upande wa kulia .

Zaidi ya hapo Kenny Dalglish anatarajiwa kuchezesha kikosi kile kile ambacho kwa kutazama kipindi cha kwanza cha mchezo dhidi ya Sunderland kilicheza vizuri sana lakini kikaja kufunikwa kwenye kipindi cha pili .
Liverpool inataraji kutumia mfumo rahisi wa 4-2-3-1 au wa 4-4-1-1 ambao unampa Suarez ‘free role’ kuzunguka uwanja mzima akitafuta nafasi. Kwa upande mwingine wachezaji wapya Stewart Downing na Jose Enrique wanajaribu kujenga’patnership’ kwenye upande wa kushoto na Lucas Leiva na Charlie Adam wanategemea kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwenye sehemu ya katikati mwa uwanja japo Dalglish ana watu wengine ambao anaweza kuwachagua kina Jay Spearing , Raul Meireles Jordan Henderson na Alberto Aquilani ambao wako kikosini.


Jammie Caragher na Daniel Agger wako katika kwenye nafasi zao kama mabeki wa kati wakimpa ulinzi kipa Pepe Reina.
Arsenal wana sababu chache za kuwa na matumaini kuelekea kwenye mchezo wao dhidi ya Liverpool.


Ukiacha kumuuza aliyekuwa nahodha wao Cesc Fabregas kwa Barcelona huku Samir Nasri akiwa anafungasha kilicho chake akielekea Man City Arsenal wanaandamwa na issue ya majeruhi na baadhi ya wachezaji kufungiwa . Wenger anaingia kuwavaa Liverpool huku akiwakosa Abou Diaby , Alex Song , Gervinho, Johan Djorou , Jack Wilshere, Kieran Gibbs na Armand Traore.
Hii inamaanisha kuwa Arsenal watalazimika kumtumia Emmanuel Frimpong kiungo mwenye miaka 19 kuziba pengo la Alex Song anayelazimika kutumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu kwa kumkanyaga Joey Barton.Pamoja na Frimpong Arsenasl watalazimika kumpa mchezaji mpya Carl Jenkinson mechi yake ya kwanza akichukua nafasi ya Kieran Gibbs ambaye ameumia.


Andrey Arshavin na Theo Walcott wataanza kama viungo wanaoshambulia toka pembeni mwa uwanja japo Wenger amesema kuwa anaweza kuwatumia wachezaji wapya Alex Oxlade Chamberlain na Ryo Miyachi .
Riyo Miyachi ni winga toka Japan mwenye miaka 18 ambaye amekuwa akicheza kwa mkopo huko Feyenord Rotterdam na ana uwezo mkubwa huku akitumia sana mbio zake kama silaha yake kuulakini kama ambavyo imezoeleka kwa Arsenal mchezaji huyu ni kipaji ambacho hakijakomaa wala hakina uzoefu wa kutosha , hivyo anaweza kupewa nafasi ya kuingia toka benchi kuwakimbiza kina Martin Kelly na Jose Enrique.
Kwa macho ya haraka miundo ya timu hizi mbili inafana . Ila tofauti zipo ., Kwanza ni upande wa Luis Suarez ambaye kwa hakika lazima ataelekezwa kukaa sana upande wa juu wa uwanja ili kumuepuka Aron Ramsay , katika hali itakayosababisha Liverpool ionekane kama inacheza 4-4-2, huku Ramsay kwa upande wake atalazimika kuingia ndani kwenye ‘midfield’ ili kuipa Arsenal shape ya 4-3-3 wakiwa hawana mpira .


Mawinga wa Liverpool (kuyt na downing) pia watalazimika kushuka sana wakati timu yao ikiwa inalinda kwani Dalglish anapendelea sana kutumia mabeki wanne akiwa analinda . Walcott na Arshavin hawatakimbia sana nyuma kulinda kitu ambacho kinaweza kuwalazimu mabeki wa pembeni wa Liverpool (Enrique na Kelly) wawe macho na waegemee sana kwenye kulinda na si kupanda hali itakayowanyima Liverpool mashambulizi mengi ya pembeni .

Battle za pembeni mwa uwanja zinaweza kuwa muhimu kwenye mchezo huuhasa kwenye winga ya kulia ya Liverpool ambako Dirk Kuyt atapambana na Carl Jenkinson mchezaji ambaye amewahi kucheza mechi nane tu za ligi yoyte kwenye maisha yake ya soka (zote akiichezea Charlton Athletic kwenye ligi daraja la kwanza)Beki huyu aliingia kwenye dakika 20 za mwisho dhidi ya Udinese na japo baadhi ya mashabiki wa Arsenal walifurahishwa na kiwango chake alifanya makosa kadhaa ambayo yalitokana na uzoefu mdogo na Kenny Dalglish hakika atawaelekeza wachezaji wake watumie sana upande wake.
Tomas Rosicky amewahi kucheza kwenye upande wa kushoto wa midfield ya Arsenal kwenye michezo miwili ya mwisho ya timu yake lakini si mchezaji ambaye ana uwezo mkubwa wa kulinda wala hana kawaida ya kurudi nyuma kusaidia wakati timu inashambuliwa na unaweza kusema hivyo hivyo kwa upande wa Andrey Arsharvin hivyo bwana mdogo Jenkisnon atajikuta mwenyewe kwenye upande wa kushoto .


Hapa ndio ile ‘free role’ ya Luis Suarez inapoweza kutumika na kuwa na madhara makubwa kwa Arsenal.Kwa vyovyote atakuwa anakimbilia upande wake wa kulia ili yeye na Kuyt wafanye ‘double team’’ kwa Jenkinson na kuiletea Arsenal matatizo.

Kama hii italazimu Arsenal kumtumia beki wake anayekuwa upande wa kushoto kwenye ‘central defensive patnership’ Thomas Vermalaen kusogea upande wa kushoto kumsaidia Jenkinson atakuwa anaacha shimo kubwa ambalo litakuwa nafasi muhimu kwa Andy Caroll au kiungo yoyote wa kati kama Charlie Adam kuingia na kuleta matatizo.
Arsenal walikuwa hatarini sana kufungwa kwenye hatua za mwisho za mchezo wao dhidi ya Udinese siku ya jumanne .


Pia dhidi ya Newcastle waliwaruhusu viuongo wao wa kati kuingia sana ndani kwenye nusu ya Newcastle huku wakiwa na matarajio kwamba mmoja wao atabaki na kuwa mlinzi wa mabeki .

Idea hii ya ‘total football’ iliwahi kufanya kazi msimu uliopita kwa Jack Wilshere na Alex Song ambapo wachezaji hawa walijenga uelewano mkubwa kati yao, ila kwa Udinese ilionekana kushindikana kidogo hasa kwa sababu Wilshere hakuwepo na Udinese waliweza kuingia kwenye nusu ya Arsenal wakiwa huru sana kwenye eneo la katikati huku wakiiweka defense ya Arsenal katika hali ya 2-vs-2 na 4-vs-4 .

Kwa mara nyingine Luis Suarez ana uwezo mkubwa sana wa kuwaletea madhara Arsenal kwenye hali kama hii akipata nafasi ya kuwakimbia mabeki .
Kitu kingine ambacho Arsenal imekuwa ikikifanya ni kuweka mstari wa ulinzi ambao unalinda kuanzia eneo la juu na hik ni ktu ambacho kinatarajiwa kurejewa kwenye mchezo dhidi ya Liverpool ili kujaribu kuuza makali ya Andy Caroll amnaye watahakikisha kuwa wanahimili mipira ya juu ambayo ndio silaha yake kubwa .


Mstari huu ambao unakabia juu ulipitwa kirahisi sana na na wachezaji wa Udinese Kwadwo Asamoah na Pablo Amero na mara zaidi ya moja kipa Wojciech Szczesny alilazimika kutokea ili kuokoa . Hili ni suala ambalo Liverpool watalitumia kama udhaifu kwa wapinzani wao.
Liverpool pia wana sababu za kuwa na wasiwasi na timu yao .


Wachezaji wapya bado wanahitaji muda zaidi kuzoea mazingira ya timu taratibu nah ii inamanisha kuwa watahitaji zaidi ya mechi mbili ili kuwa na ‘match fitness’ jambo limeonekana kuwa tatizo kubwa . Pia wanahitaji kufanyia kazi uwezo wao wa kuupata mpira pale unapopotea jambo liloonekana kuwa tatizo jumamosi iliyopita walipocheza na Sunderland .

Liverpool walimaliza mpira wakiwa na asilimia 39% ya umiliki wa mpira kwenye mara ya mwisho walipocheza na Arsenal na kwa soka lao ambalo ni la moja kwa moja wanaweza kupata tabu kwenye ‘ball possesion’ .

Kwenye mchezo ambao timu hizi mbili zilitoka sare ya 1-1 mwezi aprili goalkick nyingi alizopiga Pepe Reina alizielekeza kwenye kichwa cha Andy Caroll.
Kama mbinu ya kumtumia Andy Caroll kama Targetman haitatumika ipasavyo Liverpool watakuwa wanapoteza sana mpira kwa timu ya Arsenal ambayo inajua jinsi ya kumiliki mpira kwani ndio silaha yake kubwa .

Kama Liverpool haitamiliki mpira vya kutosha uwezo wa kupiga pasi za mbali wa Charlie Adam na krosi za Stewart Downing hautakuwa na faida yoyote .
Kama Liverpool hawatakuwa na mpango thabiti wa kumiliki mpira na kutengeneza nafsi wataonekana kupoteana kama walivyoonekana kwenye mchezo dhidi ya Sunderland . Arsenal wana mapungufu makubwa sana kwenye safu yao ya ulinzi na Liverpool wana kia sababu na uwezo wa kutumia mapungufu haya kwa faida yao lakini wanapaswa kuutazama mchezo wao dhidi ya Sunderland ili kutimiza hilo .

KWANINI UDHAMINI WA LIGI KUU VODACOM VILABU HAVIHUSISHWI ?

Timu za ligi kuu Tanzania Bara mwishoni mwa juma hili zilikabidhiwa vifaa vya michezo kwa ajili ya ushiriki wa ligi hiyo ambayo inataraji kuanza hapo kesho. Mimi ni mmoja wa wadau waliokuwepo katika ghafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na wadau wote kutoka katika timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo.
Mambo ambayo nimeyaona kama sikosei nilimsikia Ndugu George Rwehumbiza akizungumzia vifaa ambavyo vimetolewa kwa timu zote vilikua vina thamani ya shilingi milioni 352 kama sikosei lakini siku iliyofuata ndiyo lile zoezi zima la kukabidhi vifaa lilifanyika.

Nawapongeza sana Vodacom kwa nia yao nzuri ya kuendeleza michezo na katika kipindi chote wamekua mstari wa mbele kuhakikisha soka letu linachezwa with efficiency lakini napata tatizo moja Je? Vodacom wanaingia mkataba na nani? Vilabu au Tff na kama vilabu ni muhimu ,kwa nini viongozi wa vilabu hawapewi fursa japo ya kutoa maoni mbalimbali kuhusiana na mkataba ambao wao ndio stakeholders na ndio wanaitangaza Vodacom kwenye vifua vya jezi zao?

Moja kati ya maswali yanayonisumbua ni kutaka kufahamu vile vifaa vilivyotolewa ni msaada au ni sehemu ya mkataba.

Siku ya ugawaji wa vifaa nilimsikia kiongozi mmoja wa timu ya Moro United akiuliza kwa nini viatu walivyopata Yanga,Simba,Azam,na African Lyon havifanani na viatu walivyopewa timu zingine kama Polisi, Villa,Toto na zilizosalia.

Baada ya mabishano mmoja wa wagavi wa vifaa hivyo alisema kuwa Tff walishavikagua, yote hayo tisa jezi zenyewe ukizitazama zimefanana mno na huenda kuna Baadhi ya mechi timu zikashindwa kuwa na contrast ya rangi.

Ninapozungumzia Mkataba sibahatishi na nazungumzia Vilabu kushirikishwa ni muhimu ili ikikiuka matakwa ya mkataba iweze kushitakiwa.

Ligi ya 2008/2009 tulishuhudia kampuni ya kurusha matangazo ya television GTV ikisitisha mkataba huku timu zikiwa zimeahidiwa sh milioni ishirini na sita (26 Mil shs/=) kutokana na udhamini huo lakini kwa sababu vilabu havikushirikishwa hakuna aliyeweza kulitolea jambo hili ufafanuzi

Kuna vilabu vilishuka Daraja kutoakana na athari iliyojitokeza baada mkataba huo kuvunjika kutoka na bajeti kupelea, sasa nani anayesaini mikataba kwa niaba ya vilabu?

PROFESSOR JAY: MIMI NI MSIMBAZI DAMU


Siku ya Jumatano tarehe 17, August, ilikuwa ni siku nzuri sana kwa mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania Joseph Haule a.k.a Professor Jay, baada ya timu yake ya soka anayoishabikia kuifunga timu pinzani.

Professor Jay ambaye ni mnazi na shabiki mkubwa wa Simba Sports Club, watoto wa Msimbazi, anasema alianza kuipenda Simba tangu alipopata ufahamu wa soka mpaka sasa amekuwa mpenzi mkubwa klabu hiyo ndio maana siku ya Jumatano iliyopita ilikuwa siku ya furaha baada ya Mnyama kumuumiza Yanga 2-0 katika mchezo wa Ngao ya Hisani.

“Mimi shabiki wa kutupwa wa Mnyama kiasi kwamba tukifungwa nakosa sana amani na furaha kwa siku nzima, na kama ilivyo kawaida timu ambayo sina kabisa mapenzi nayo hapa Bongo ni mtani wetu wa Jadi Yeboyebo “Dar Young African”.


“Kwa upande wa nje ya Bongo, kwanza siipendi kabisa Manchester United kwa kuwa mimi ni Liverpool damu, yaani huniambii kitu kuhusu The Reds.Huu ndio muda wetu wa kurudisha heshima yetu iliyopotea kwa kipindi kirefu, kwa sababu timu chini ya King Kenny Daglish imefanya usajili mzuri sana.Watu kama Luis Suarez, Stewart Downing, Charlie Adam na wengineo watatusaidia sana.Man U na timu nyingine wajitaarishe kwa vipigo tu msimu huu na kazi inaanzia kwa Arsenal kesho, na wengine waelekee Qibra mapema tukija tunachinja tu.

Liverpool “we will never walk alone”. – Prof.Jay

DEIN: KUWENI NA HESHIMA KWA WENGER AU ATAONDOKA


Arsene Wenger anaweza kuacha kazi ya ukocha Arsenal ikiwa mashabiki wataendelea kuwakosea adabu yeye na kikosi chake, makamu mwenyekiti wa zamani wa Gunners David Dein amesema.

Akiongea na shirika la habari la Uingereza, alionya kuwa kocha huyo mfaransa yupo njia njiapanda, huku mashabiki wakiendelea kuonyesha hasira zao juu ya Arsenal kukosa ubingwa kwa miaka 6 mfufulizo.

Dein alisema kuondoka Emirates inaweza ikawa chaguo kwa Wenger kwa sababu itafikia kipindi atasema “Imetosha”.

“Hivyo mimi ndivyo ninavyoona na ni vizuri na mashabiki wakawa na mtazamo huo, wanatakiwa atleast kumpa heshima anayostahili kwa mambo mazuri na makubwa aliyoifanyia klabu hii,

“Watu wanazungumza kuisha kwa muda wake kuwepo klabu kuisha?

“Hilo ni jambo la hatari kuzungumza kwa sababu ni rahisi kuwatimua watu kazi halafu nini kinafuata?Watu wanaongea kuhusu kununua wachezaji wapya.Sawa lakini hilo linaweza lisiwe suluhisho,

“Naelewa wasiwasi wa mashabiki , lakini Arsene Wenger amekuwa nasi kwa zaidi ya miaka 15 na kila msimu tumekuwa tukifaulu kucheza ligi ya mabingwa, ingawa mashabiki bado wana hamu ya kushinda kombe.

“Chini ya uongozi wa Arsene Wenger tumekuwa na vipindi vingi vya furaha na naamini hakuna sababu itakayotufanya tusiwe tena na furaha tuliyowahi kuwa nayo.”

MARIGA KUJIUNGA NA REAL SOCIEDAD


Mchezaji wa kimataifa wa Kenya na klabu ya Inter Milan McDonald Mariga amewasili nchini Hispania kwa ajili ya kufanyiwa vipimo na kujiunga Real Sociedad, na anategemewa kutambulishwa leo Ijumaa baada na atapewa jezi namba 18.

Mchezaji huyo wa zamani wa Parma ameuzwa kwa mkopo na Inter lakini anaweza akasajiliwa moja kwa moja baada ya kuisha kwa muda wa mkopo mnamo June 30 mwakani.

Mariga ambaye atavaa jezi namba 18, atatambulishwa leo Ijumaa mbele ya mashabiki wa wapenzi wa klabu hiyo ya Spain.

Siku inayofuata Mariga atakuwa jijini Nairobi kujiunga na timu ya taifa ambayo itawakaribisha Guinea Bissau katika yenye ulazima wa kushinda ya michuano ya kugombea nafasi ya kushiriki African Cup of Nations

MILLION 72 ZAMPELEKA JOSEPH OWINO CHAMAZI


Beki wa kimataifa wa Uganda Cranes Joseph Owino amejiunga rasmi na Azam Fc kwa ada ya uhamisho wa dola za kimarekani 30,000.

Owino ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia Simba Sports Club kabla ya kupata majeraha ya goti yaliyomweka nje ya uwanja kwa msimu wote uliopita na mwishowe aliachwa na Simba katika usajili wa msimu huu.

Beki huyo ambaye kwa sasa anaendelea vizuri na majeraha yake ya goti baada ya kuachwa na Simba, matajiri wa Vodacom Premier League Azam FC waliamua kumchukua na kumpeleka nchini India kwa ajili ya matibabu yaliyogharimu kiasi cha pesa kinachofikia dola 15,000 na baadae wakamsainisha mkataba wa miaka 3 wenye thamani ya $30,000.

Owino anatarajiwa kujiunga rasmi na Azam na kuanza kuitumikia klabu hiyo mwezi January mwakani wakati wa dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa.

FALCAO AJIUNGA NA ATLETICO MADRID



Atletico Madrid wamefanikiwa kuwasajili wachezaji wawili kutoka Porto Rademel Falcao & Ruben Micael kwa ada ya uhamisho ya Euro million 45.

Porto wametangaza katika soko la hisa la Ureno kwamba wamekubali kumuuza mshambuliaji Rademel Falcao na kiungo Ruben Micael kwenda Atletico Madrid kwa ada ya jumla ya uhamisho ya Euro million 45.

Mabingwa wa Ureno hao waliongeza kuwa usajili wa wachezaji hao umebakiza uchukuaji wa vipimo na na wachezaji kukubaliana mahitaji binafsi na Atletico.

Ruben Micael amenunuliwa kwa 5, na Falcao amejiunga na Atletico kwa dili lenye thamani ya, lakini fedha ya usajili ya Falcao inaweza kuongezeka mpaka kufikia euro million 47 ikiwa mchezaji atafanya vizuri akiwa na timu hiyo kutoka Vicente Calderon.

Thursday, August 18, 2011

ATHUMANI MACHUPPA AFUNGA BAO HUKO SWEDEN.

Vasalunds Juzi ilitoka sare na Karstad United bao 2 - 2 Mohammed Rajab Machuppa alitupia Moja
































BREAKING NEWS : JOSEPH OWINO AJIUNGA NA AZAM FC

BEKI WA SIMBA JOSEPH OWINO HATIMAYE AMEJIUNGA RASMI NA AZAM FC.

HABARI ZAIDI BAADAE....


HARUNA '' MAN OF THE MATCH '' NA HARUNA UMUHIMU WAKE UPO PALE PALE..

Hatimaye tambo zimefikia mwisho na dakika 90 zimeamua nani bora . Simba imeibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya mahasimu wao na kwa asilimia kadhaa walistahili kupata ushindi kwani kwa dakika zote 90 ni wao ndio waliotengeneza nafasi nyingi za wazi na walizitumia .




SAFU YA USHAMBULIAJI YA SIMBA.


Simba waliingia na mfumo wa 4-4-2 ambao ilikuwa unabadilika na kuwa 4-5-1 kuendana na movement ya mpira na wakati mwingine ilikuwa inabadilika na kuwa 4-3-3 .



Wakati ilipokuwa inabadilika na kuwa 4-3-3 Simba ilikuwa inawatumia Felix Sunzu , Emanuel Okwi na Haruna Moshi . Okwi alikuwa anashambulia kutokea kushoto Boban akishambulia kutokea kulia na Sunzu alikuwa katikati akicheza kama ‘target man’.



Safu hii ya ushambuliaji ilikuwa mwiba mchungu kwa Yanga kwani kufikia dakika 10 za mwanzo Simba walikuwa wameshabisha hodi langoni mwa Yanga mara mbili katika ‘move’ za hatari ambazo kama Salum Machaku na Amir Maftah katika nyakati tofauti wangekuwa makini basi Simba wangecheka mapema .



Washambuliaji hawa watatu walikuwa wana-link vizuri sana na viungo wao kina Jerry Santo,Patrick Mafisango na Salum Machaku huku waki-take ‘advantage’ kwa mawasiliano mabovu baina ya mabeki wa Yanga na haikushangaza kuwa kufikia dakika ya 17 Simba walikuwa wanaongoza kwa bao moja .
Kwa upande wa safu ya ulinzi ya Yanga kulikuwa na matatizo makubwa sana . Chacha Marwa na Nadir Haroub hawakuwa na mawasiliano kati yao . Mara nyingi walikuwa wanacheza pasipo kuwa na mpango wa jinsi ya kuwakabili wachezaji wa Simba .



Presha iliyokuwa inakuja upande wao ilizidi kuwachanganya na kuwalazimu kucheza rafu ambazo zilikuwa zina madhara kwao na mfano mzuri ni kwenye goli la pili ambapo Haruna Moshi alichezewa vibaya na Nadir Haroub na kusababisha penati iliyokwamishwa wavuni na Felix Sunzu .



Pembeni upande wa kulia alikokuwa Shadrack Nsajigwa kulikuwa na matatizo pia, Fusso hakuwa anapewa msaada wa kutosha na mwenzie aliyekuwa anacheza winga ya kulia Godfrey Taita hali iliyokuwa inasababisha mipira mingi ya hatari kupita upande wa kulia wa ‘defence’ ya Yanga hata goli la kwanza lilitokea huko baada Felix Sunzu kuambaa na mpira na kutoa krosi fupi iliyomalizwa na Haruna Moshi.


UKOSEFU WA HOLDING MIDFIELD KWA YANGA.

Moja ya mambo ambayo yalikuwa yanafanya ‘defense’ ya Yanga iwe ‘under pressure’ ni kukosekana kwa cover muhimu inayotoka kwa ‘Holding midfielder’ , labda ni kukosekana kwa Nurdin Bakari ambaye kwenye safu ya kiungo ya Yanga huwa anafanya kazi mbili kwa wakati mmoja wakati timu ikipanda juu huwa anakuwa kiungo mwendeshaji na timu inapokuwa ikishambuliwa anafanya kazi ya ‘holding midfielder’ na hivyo kuwahakikishia usalama mabeki wake .

Hilo halikuwepo leo na badala yake Yanga waliwapanga Juma Seif Kijiko na Haruna Niyonzima Fabregas .

Fabregas alipangwa kucheza kwenye dimba la chini jambo lililoigharimu sana Yanga kwa kuwa Niyonzima ni aina ya viungo ambao wana madhara wakiwa na mpira lakini timu inapokuwa kwenye presha anakuwa hana msaada.

Madhara yake yalionekana kwani Yanga walilikimbia dimba huku presha ikiwa kubwa mno kwenye safu yao ya Ulinzi na ndio maana Simba walimaliza mchezo kwenye kipindi cha kwanza .

Kulikuwa hakuna haja ya kuwapanga Juma Seif Kijiko na Niyonzima kwa pamoja kulikuwa na haja ya kumchezesha mtu kama Godfrey Bonny ambaye angeleta Balance kwenye midfield ya Yanga .

‘MAN OF THE MATCH PERFOMANCE’-HARUNA NIYONZIMA .

Si kitu cha kawaida kwa mchezaji bora wa mchezo kutoka kwenye timu iliyopoteza mchezo lakini mtu aliyestahili kuwa man of the match kiukweli alikuwa Haruna Niyonzima . Bahati mbaya ni kwamba alikuwa man of the match kwenye timu iliyofungwa .

Fabregas aliipa Yanga uhai kwa mpira wake alioucheza ambao ulikuwa wa kiwango cha juu kupita kiasi , huyu jamaa ana akili kupita maelezo . Alitengeneza movement nyingi ambazo kama isingekuwa mbinu ambazo si sahihi za Yanga pengine zingeleta faida kwa timu yake .

Mara nyingi alijaribu kupiga mashuti na alitawala mno eneo la kiungo kwa bahati mbaya hakuwa anapata msaada toka kwa wenzie .




UWEPO WA VICTOR COSTA KWENYE SAFU YA ULINZI YA SIMBA .


Kama ulipitia kwenye hii blog mapema kabla ya mchezo utakuwa umepitia ‘analysis’ ya vitu mbalimbali vya kutegemea toka kwa timu mbili za Simba na Yanga.




Kwa upande wa Simba moja ya matatizo makubwa ambayo yaliainishwa ni ukosefu wa umakini kwenye eneo la ‘defense’. Tatizo hili linasababishwa na kimo lakini sababu nyingine ya msingi ni mabeki wa kati wa Simba kuwa na aina moja ya uchezaji .




Juma Nyosso na Kevin Yondani wote ni watu wazuri sana wakicheza kwenye nafasi ya beki anayekaba , lakini kati ya watu hawa hakuna yoyote anayekuwa ‘ kamanda’ kwa wenzie .


Tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi na ufumbuzi huo ni Victor Costa Nampoka aka Nyumba . Mashabiki wa Simba wanamkumbuka vizuri beki huyu na ndio maana taarifa za usajili wake zilipokelewa kwa shangwe na hilo lilidhihirika kwenye mchezo wa ngao ya hisani.




Mtu kama Nyosso ni beki mzuri sana lakini uzuri wake huwezi kuuona akicheza na Kevin Yondani au Meshack Abel , kwa sababu wote ni watu wa aina moja yaani ni kama vile jinsi ya mtindo huo huo lakini Victor Costa ameleta kitu tofauti ambacho Simba wamekikosa tangu alipoumia Joseph Owino .




Costa alikuwa anwaelekeza mabeki wenzie jinsi ya kukaba , jinsi ya kusimama , alikuwa anatuliza presha ya mchezo na uzoefu wake ulionekana .

KIPINDI CHA PILI.


Huu ulikuwa mchezo wa vipindi viwili ambapo Simba walicheza na kutawala kipindi cha kwanza lakini Yanga waliamka na kutawala kipindi cha pili japo hawakuweza kurudisha mabao waliyofungwa kipindi cha kwanza .


Sababu kuu ya Simba kushindwa kutawala kipindi cha pili ni kuumia kwa washambuliaji wawili wa Simba waliosumbua sana Yanga mwanzoni.




Haruna Moshi na Emanuel Okwi waliumia na kasi yao kwa kiasi Fulani ilipungua hali iliyosababisha kocha kuwatoa na kuwaingiza Shomari Kapombe na Gervais Kago.




Mabadiliko haya yalimaanisha kuwa Simba ilicheza kwa mfumo wa 4-4-2 flat ambapo ule ujanja wa kubadilisha na utumia 4-3-3 na 4-5-1 haukuwepo tena .




Pia Felix Sunzu na Gervais Kago hawakuweza kutengeneza ‘chemistry’ baina yao kwani wote wawili ni ‘terget men’ yaani watu wa kusimama jambo ambalo lilitengeneza shimo baina yao na viungo na japo kina Mafisango na Jerry Santo walikuwa wanafanya kazi kubwa sana , ‘momentum’ ya mchezo ilibadilishwa na mabadiliko haya .

KUINGIA KWA RASHID GUMBO NA HAMIS KIIZA .


Kutawala mchezo kwenye kipindi cha pili kwa Yanga kuliendana na matukio mengine ambayo ni mabadiliko ya Simba na wakati huo huo mabadiliko ya Yanga kwa kuwatoa Kiggi Makassi na Kenneth Asamoah na kuwaingiza Rashid Gumbo na Hamis Kiiza .




Walipoingia watu hawa Yanga ilikuwa inamiliki sana mpira na hivyo walionekana kuja na uhai hasa Hamis Kiiza ambaye alikuwa anamtoka sana Nassor ‘chollo’ beki wa kulia wa Simba ambaye mara nyingi sana alikuwa anamsahau mshambuliaji huyu toka Uganda.




Kwa bahati mbaya hakukuwa na matokeo yoyote ya utawala wa wachezaji hawa kwenye eneo la kiungo kwa Gumbo na Kiiza kwa upande wa ushambuliaji.

PATNERSHIP YA JERRY TEGETE NA KENETH ASAMOAH.


Safu ya ushambuliaji kwa Yanga ilikuwa chini ya Jerryson Tegete na Keneth Asamoh , huu ni muungano ambao haukufanya kazi kwa kuwa wachezaji hawa wana mitindo ya uchezaji inayofanana hivyo ili kucheza pamoja walilazimika kucheza tofauti na walivyozoea na hivyo hawakuwa ‘comfortable’.




Tegete ni mzuri akiachwa aongoze mstari mwenyewe kama ‘target man’ lakini uwepo wa Asamoah ulimlazimu Tegete kushuka chini ambako hana madhara yoyote .




Tegete ni mchezaji ambaye umahiri wake wote uko kwenye kufunga na maeneo yake uwanjani ni eneo la 6 au kama atatoka mbali basi asikae mbali sana na eneo la yadi 18 . Anapotoka kushuka hadi katikati ya uwanja hawezi kuwa na madhara yoyote .


Mwisho .


Simba walistahili kushinda mchezo huu kwani walitengeneza nafasi za wazi na kati ya hizo walitumia mbili kupata mabao ambayo watani wao hawakuweza kujibu .




Kipindi cha kwanza Simba waliingia na malengo ambayo yalitimia , kwa vyovyote kocha wao aliwaambia kuwa ‘biashara ni mapema’ na ndio kilichotokea kwani kipindi cha kwanza ndio kilichoipa Simba ushindi .




Kwa kawaida Yanga huwa wamezoea kuwa Simba huingia na lengo la kushambulia tangu mwanzo huku wao (yanga) wakiwasoma na kurudi mchezoni taratibu hadi wanafikia kuuteka moja kwa moja lakini hilo halikuonekana leo kwani Simba walitengeneza nafasi za wazi zilizowaacha Yanga wakiwa hawajui linalotokea na hawakurecorver kutoka kwenye huo mshangao .




Kocha wa Yanga hakutumia mbinu sahihi kwa timu yake kwani jinsi alivyoipanga safu yake ya viungo hakukuwa na ‘balance’ .

WADAU MBALI MBALI WALIOHUDHURIA MECHI YA SIMBA NA YANGA..

MHESHIMIWA JUMA ATHUMANI KAPUYA PIA ALIKUWEPO








NAHODHA WA ZAMANI WA SIMBA SELEMANI MATOLA AKIWA NA SAAD KAWEMBA.

















KUSHOTO MSEMAJI WA YANGA LUIS SENDEU,ALEX MGONGOLWA NA MOHAMED BHINDA WAKIWA HAWAAMINI KAMA KWELI YANGA YUPO NYUMA KWA MABAO 2-0.











MWENYEKITI WA YANGA Lloyd Nchunga AKIWA HOI JUKWAA KUU.














HUYU NI SHABIKI MAARUFU WA SIMBA BWANA SAMIR MUCHACHO.




















WADAU IDDY MPITA ( KUSHOTO ) NA OPERATIONS MANAGER WA MULTICHOICE TANZANIA BWANA BARAKA SHELUKINDO.









KATIKATI NI MKURUGENZI WA BIG BON Bw AHMED AKITETA JAMBO NA VIONGOZI WA TFF..









IMANI MADEGA MWENYEKITI WA AMANI WA YANGA NAYE ALIKUWEPO.









HUYU NI MASANJA MKANDAMIZAJI AKIWA AMEKANDAMIZWA NA MNYAMA.....










WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA SIMBA, IBRAHIM MASOUD ' MAESTRO '
SWED NKWABI ( KATIKATI ) WAKIFURAHIA NAMNA TIMU YAO INAVYOTANDAZA KANDANDA.









AISEE HUYU BOBAN NI BALAAA.......SASA HAKUNA NAMNA LAZIMA NIMUITE TU KWENYE TIMU YA TAIFA LA SIVYO SAFARI HII WANANCHI HAWATANIELEWA..

















MUDY SEBENE HOI..........JAMAA ANAIPENDA YANGA KULIKO HATA CHAKULA...































SIMBA YANYAKUA NGAO YA HISANI KWA KUIFUNGA YANGA MABAO 2-0.

JUMA KASEJA AKINYANYUA NGAO YA HISANI.

MAKAMU WA KWANZA WA RAISI WA TFF ATHUMANI NYAMLANI AKIMKABIDHI NGAO YA HISANI JUMA KASEJA.



MENEJA MASOKO WA BENKI YA NMB BWANA IMANI KAJULA AKIMKABIDHI ZAWDI MCHEZAJI BORA MCHEZO WA NGAO YA HISANI,KIUNGO PATRICK MAFISANGO WA SIMBA.









KOCHA WA SIMBA MOSES BASENA AKIWA NA MAKAMU MWENYEKITI GEOFREY NYANGE













PATRICK MAFISANGO AKISALIMIANA NA HARUNA NIYONZIMA.