Search This Blog

Saturday, July 9, 2011

COUNTDOWN TO KAGAME CASTLE CUP FINAL:VITUKO VYA MECHI ZA WATANI WAJADI


Timu mbili zenye upinzani wa enzi na enzi katika soka la Tanzania Yanga na Simba Jumapili hii july 10 zinakutana katika mchezo wa Fainali ya Kombe la Kagame Castle cup mwaka 2011, mchezo huo utakaofanyika kwenye uwanja Mkuu wa Taifa jijini Dar es Salaam. Blog yako inaaangalia baadhi ya vituko vya kusisimua vilivyowahi kutokea wakati wa matayarisho, wakati au baada ya michezo baina ya timu mbili hizo kumalizika.
- Mwaka 1968 katika matayarisho ya mechi ya Simba (wakati huo Sunderland) na Yanga mchezaji wa Simba Emmnuel Mbele ‘Dubu’ alikuwa amefungiwa kucheza mpira kwa kipindi cha miezi 6 kutokana na utovu wa nidhamu uliotokea katika moja ya michezo ya ligi (wakati huo ligi ya taifa). Mchezo huo ulikuwa umepangwa kufanyika uwanja wa Ilala (Sasa Uwanja wa Karume zilipo ofisi za TFF). Timu zote mbili zilifika uwanjani huku wachezaji wakiwa tayari wamevaa jezi lakini kumbe Suderland hawakuwa tayari kucheza mchezo huo kwa madai kwa sharti kuwa wasingecheza huku mchezaji wao tegemeo, Mbele akiwa amefungiwa. Kutokana na hali hiyo kikaitishwa kikao cha dharura kilichohusisha viongozi wa Chama cha mpira wa Miguu Tanganyika (Tanganyika Football Assocation - TFA) Sunderland na Yanga. Baada ya hoja ya Sunderland kuwekwa mezani huku ikiaminika kuwa Yanga walikuwa wakihofia uwezo wa Mbele, Kwa mshangao Yanga waliwaambia viongozi wa TFA kuwa kama kikwazo cha mchezo ilikuwa ni mchezji mmoja tu basi afuguliwe na mchezo uendelee. TFA ikamfugulia Mbele ili akipige. Mchezo ukachezwa Sunderland wakapata kipigo cha aina yake cha magoli 5-0 yaliyofungwa na Maulid Diluga (2), Salehe Zimbwe (2) na Kitwana Manara.

- Agosti 10, 1974 Uwanja wa Nyamagana Mwanza magwiji wawili Gibson Sembuli (Yanga) na Saad Ally (Simba) waligongana katika harakati za kuwania mpira katika mchezo huo unaoaminika kuwa moja ya michezo iliyokuwa ya kiwango cha juu kabisa katika historia ya timu hizo mbili. Inaaaminika kuwa mahali walipogongana magwiji hao kiliota kichuguu ambacho hadi leo kipo. Bado hakuna uthibitisho wa kisayansi kuwa kichuguu hicho kilitokana na kugongana huko.

- Agosti 10, 1985 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mlinzi wa kati wa Simba Twalib Hilal anaushika mbira uliokuwa ukilekea golini baada ya kupigwa kichwa na Abeid Mziba-aliyejipatia umaarufu mkubwa wa kufuga magoli kwa kichwa kuliko miguu. Inaamuliwa ipigwe adhabu kubwa (penati) kuelekea laqngo mwa mwa Simba. Mpira unawekwa na anakwenda kupiga Juma Mkambi ‘Jenerali’ Simba wanatoka katika eneo la mita kumi na nane ili penati ipigwe lakini ghafla mpigaji anabadilishwa na anakwenda kupiga Hussein Iddi. Kuona hivyo Zamoyoni Mogella (wa Simba) anakimbia na kuupiga nje ili penati isipigwe. Mpira unavunjika na baadaye Yanga wanapewa ushindi wa magoli 2-0 na kuibuka mabingwa mwaka huo.

- Agosti 31, 1991 Katika kile kilichoonesha imani za ushirikina zilizopindukia mipaka, ilinunuliwa mipira mipya ya kuchezea kwenye mchezo huo chini ya uwakilishi wa wazee wawili mmoja kutoka kila upande wa Simba na Yanga na kisha wazee hao wakaiweka mipira hiyo ndani ya mfuko mmoja na kwenda nayo uwanjani wakiilinda kwa zaidi ya saa nne hadi pambano lilipoanza. Simba ilipokea kipigo cha goli 1-0 lililofungwa na Said Sued ‘Scud’.

- Novemba 13, 1991, (Ligi ya Muungano), Mchezo wa marudiano wa ligi hiyo ulifikia mapumziko huku timu hizo zikiwa hazijafungama. Timu zilipoingia katika vyumba vya kubadilishia mavazi, Simba hawakurejea dimbani. Madai ambayo hadi leo hayajawahi kuthibitishwa na mtu au chombo chochote ni kuwa mwamuzi wa mchezo huo – Hafidh Ali alinukuliwa akiwaambia wachezaji wa Simba kuwa wangepokea kipigo cha magoli 3-0 iwapo wangethubutu kurejea uwanjani baada ya mapumziko.

- Septemba 26, 1992 Yanga iliyokuwa tayari imetawazwa mabingwa kwa mwaka wa pili mfululizo iligoma kupeleka timu uwanja wa Taifa kwa madai kuwa mchezo huo haukuwa na umuhimu wowote kwao, hivyo Simba ikapewa ushindi na chama cha mpira wa miguu FAT.




- Julai 2, 1994 Yanga inafungwa goli 4-1 kipigo ambacho kinabakia kuwa kikubwa zaidi cha karibuni katika michezo ya ligi. Magoli ya George Masatu, Atuman China, Madaraka Seleman na Dua Said yalitosha kuikandamiza Yanga huku goli la Yanga likifungwa na Costantine Kimanda. Baada ya mchezo ambao ulichangia kuipa Simba ubingwa baada ya kuukosa kwa miaka mitatu, timu ya Yanga ikisambaratika huku wachezaji waandamizi kama Stephene Nemes, Said Mwamba, Nico Bambaga na Edibily Lunyamila wakiiacha timu hiyo ikipepesuka na hatimaye kusajili wachezaji wengi vijana wakiwemo Willy Mtendamema, Nonda Shaban Maalim Saleh na Sylvatus Ibrahim ‘Polisi’

- Februari 25, 1996 Simba iligoma kupeleka timu uwanja wa Taifa ikiishinikiza FAT kuilipa kwanza fedha kutoka CAF kutokana na faini iliyolipwa na klabu ya Chapungu ya Zimbabwe. Chapungu ilitozwa faini hiyo baada ya kushindwa kusafiri nchini kucheza mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Afrika. Inasadikiwa kuwa Simba haikuwahi kulipwa deni hilo.

- 2002, mchezo ambao ulikuwa umepangwa miezi kadhaa uliahirishwa dakika za mwisho kwa amri ya Waziri wa Kazi Maendeleo ya Vijana na michezo Juma Kapuya kutokana kile ambacho Yanga walidai walikuwa wakinyanyaswa kisaiklojia baada ya kiungo wao wa pembeni kulia Said Maulid ‘SMG’ kutangazwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuwa si raia wa Tanzania. Mchezo huo ulichezwa baadaye na timu hizo kutoka sare ya magoli 2-2.

- Oktoba 24, 2007 Uwanja wa Jamhuri Morogogoro; Pambano linamalizika huku Simba wakiwa washindi goli 1-0 la Ulimboka Mwakingwe. Baada ya hapo mashabiki wa Yanga wanawashmbulia baadhi ya wachezaji na kuwapiga wakati wakielekea kupanda gari lao. Jioni hiyohiyo baadhi ya wchezaji waliopigwa kipa Ivo Mapunda na mlinzi Shadrack Nsajigwa wanaondoka kambini wakidai kuhofia usalama wao. Uongozi wa Yanga unakutana siku chache baadaye na kuamua kuwafungia kutocheza mpira kwa kipindi cha miezi 6.

- Julai 27, 2008 (Kombe la Kagame). Yanga inakataa kupeleka timu uwanjani kuikabili Simba katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu ya Kombe la Kagame ambao ungekuwa mchezo wa kwanza kuzikutanisha timu hizo katika Uwanja Mkuu wa Taifa. Yanga ilidai kuwa haikupeleka timu kwa vile haikutekelezewa ahadi ya kulipwa na TFF shilingi milioni 50 kabla ya mchezo huo kama yalivyokuwa makubaliano ya kuwalipa Yanga na Simba kila moja kiasi hicho cha fedha. Yanga inaadhibiwa na CECAFA kutocheza michezo yake kwa kipindi cha miaka 3 na pia kutozwa faini ya Dola za Marekani 35,000. TFF nayo inaifungia Yanga kutocheza michezo yote ya kimataifa ya kirafiki na mashindano kwa kipindi cha miaka miwili. Hata hivyo adhabu hiyo ilitenguliwa baadaye na Kamati ya Nidhamu ya TFF na badala yake Yanga ikatozwa faini ya Dola za Marekani 20,000 na kutakiwa kuiomba radhi TFF na wadau wa mpira wote nchini.

NGASSA SAFARINI U.S KWA MILLIONI 12


Mchezaji ghali zaidi katika historia ya soka nchini Tanzania Mrisho Khalfan Ngassa anayeitumikia klabu tajiri nchini Bongo Azam FC, anaondoka leo saa 3 usiku kuelekea Obamaland kwa ajili kufanya majaribio na klabu ya Seattle Sounders. Ngassa anatarajiwa kuondoka nchini na ndege ya shirika la Continental Airlines kwa tiketi ya Business class yenye thamani ya $7500. Ngassa akiwa U.S na Seattle katika majaribio atacheza katika mechi kati ya Seattle Sounders dhidi ya Manchester United itakayofanyika Julai 20 mwaka huu.
Now we can see that Ngassa is getting the treatments of a Football superstar.

COUNTDOWN KAGAME CASTLE CUP FINAL: SIMBA vs YANGA.


Pazia la michuano ya 37 ya kombe la Kagame kwa ngazi ya vilabu vya ukanda wa Afrika ya mashariki na kati, linafungwa hapo kesho kwenye uwanja mkuu wa taifa jijini Dar es salaam, kwa mchezo wa fainali utakaowakutanisha mafahari wawili wa soka la Bongo.

Ni Simba na Young Africans, pambano ambalo linajulikana kama Dar es salaam Derby, linalowakutanisha mahasimu wa kandanda wan chi ya Tanzania, kwa miaka dahar sasa.

Hii ni fainali yao ya tatu, kukutana kwenye michuano mikubwa katika ngazi ya vilabu vya ukanda huu wa Cecafa, baada ya kuwa zimlikwishafanya hivyo katika miaka ya 1975 na 1992 pale visiwani Zanzibar kwenye uwanja wa Aman.

Mwaka 1975, fainali hiyo ilizikutanisha timu hizo, na Young Africans ikaibuka mbabe kwa kuibwaga Simba mabao mawili kwa sifuri, katika fainali ya kusisimua ya michuano iliyokuwa ya pili.

Simba, mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo, wakalipa kisasi kwenye uwanja huo huo wa Aman mnamo mwaka 1992, kwa ushindi wa changamoto ya mapigo ya penati, mitano kwa minne, kufuatia sare ya bao moja kwa moja mnamo dakika mia moja na ishirini za mchezo.

Katika ardhi ya Tanzania bara, bado wana wa Jangwani hawajaonja ladha ya kutwaa uchampioni huo, na hii ni mara ya kwanza kwa timu hizo kukipiga kwenye mchezo wa fainali katika ardhi hii ya Tanzania bara, japo mara mbili zimekutana kwenye ardhi ya upande wa pili, wa Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Ni mchezo ambao unazikutanisha timu mbili zilizo na sura nyingi mpya, tofauti na ilivyozoeleka, kwani takriban nusu ya kila kikosi, kina wanandinga wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao wa ligi ya Premier ya Tanzania bara, na mashindano ya kimataifa.

Simba, bingwa wa kihistoria wa michuano hii, inaingia uwanja mkuu wa taifa hapo kesho ikisaka heshima zaidi kwenye michuano hii, kwani itakuwa inasaka ubingwa wake wa saba, baada ya kuwa ilikwishafanya hivyo mara sita.

Ina historia nzuri pale michuano hii inapofanyika kwenye uwanja wa nyumbani, na haijawahi kushindwa katika mchezo wa fainali ya michuano hii kwenye ardhi ya Tanzania bara.





Mara ya mwisho kufanya hivyo ilikuwa ni mnamo mwaka 2002 pale kwenye uwanja wa Aman visiwani Zanzibar, ikiondosha St Louis ya Bujumbura Burundi kwa kuilaza bao moja kwa sifuri, hivyo ina kiu ya ubingwa huo kwa kipindi cha miaka nane.

Kwa upande wa mahasimu wao Dar es salaam Young Africans wameshindwa kuupata ubingwa huo tangia walipofanya hivyo mnamo mwaka 1999 kule mjini Kampala nchini Uganda, kwa kuilaza sports club Villa ya Uganda kwa changamoto ya mapigo ya penati, minne kwa mmoja.

Miamba hawa wa bara wamekuwa na historia nzuri ya kutwaa ubingwa huu nje ya ardhi ya Tanzania, kwani kabla ya mwaka huo wa 1999, ilifanya vivyo hivyo kwenye uwanja wa Nkivubo mjini Kampala kwa kuilaza pia Villa mabao mawili kwa moja.

Katika fainali kumi ilizocheza za michuano hiyo, Simba ilipoteza kwenye fainali dhidi ya Young Africans mnamo mwaka 1975 kule visiwani ZANZIBAR, ikapoteza kwa changamoto ya mikwaju ya penati dhidi ya Kampala City Council mitatu kwa miwili mnamo mwaka 1978, kisha ikapoteza mnamo mwaka 1981 kule jijini Nairobi nchini Kenya mbele ya Gor Mahia ikilala bao moja kwa sifuri na dhidi ya Villa mjini Kampala kwa kulala pia bao moja kwa sifuri lililowekwa kimiani na mshambuliaji Vincent Tendwa.

Young Africans imecheza fainali sita za michuano hii, ambapo ilipoteza kwenye fainali tatu, ikiwamo dhidi ya Luo Union ya Kenya mnamo mwaka 1976 kwa kulala mabao mawili kwa moja, kisha mnamo mwaka 1986 dhidi ya El Mereikh kwenye uwanja wa taifa wa zamani jijini Dar es salaam kwa changamoto ya mikwaju ya penati, minne kwa miwili baada ya sare ya mabao mawili kwa mawili kwenye dakika 120.

Kisha ikipoteza dhidi ya hasimu wake Simba kwa changamoto ya mikwaju ya penati mitano kwa minne kwenye uwanja wa Aman visiwani Zanzibar, mnamo mwaka 1992, baada ya sare ya bao moja kwa moja kwenye dakika 120 za mchezo.

EXCLUSIVE: MR.LIVERPOOL ACHUKUA NAFASI YA NDIMBO SIMBA.


Miezi michache baada ya kujiuzulu kwa Cliford Mario Ndimbo kujiuzulu nafasi ya usemaji ndani ya klabu ya Simba, klabu hiyo leo imemteua Ezekiel Kamwaga a.k.a Mr.Liverpool kuwa msemaji rasmi wa timu hiyo.
Ezekiel ambaye ni moja kati wanahabari wakongwe nchini anakuwa ni msemaji wa pili wa klabu hiyo ndani ya uongozi wa Simba chini ya Aden Rage.

EXCLUSIVE: MWINYI KAZIMOTO ASAJILIWA RASMI SIMBA

KAZIMOTO AKIWA RAISI KIKWETE-IKULU


Kiungo wa kimataifa wa Tanzania aliyekuwa anaitumikia klabu ya JKT Ruvu msimu uliopita Mwinyi Kazimoto amekamilisha rasmi taratibu za uhamisho wake wa kujiunga klabu bingwa ya kihistoria ya Cecafa Kagame Castle Cup-Simba Sports Club.

Kukamilika kwa usajili wa mchezaji huyu ambaye amekuwa kwenye rada za Msimbazi kwa takribani miaka miwili kunamaanisha mchezaji kwa sasa ana uhalali wa kuitumikia Simba kuanzia katika mechi ya Fainali ya Kagame Cup dhidi ya Yanga na kuendelea.

Friday, July 8, 2011

HEARTS OF OAK NA ASANTE KOTOKO WAOTA MBAWA


Mashindano yaliyokuwa yawashirikishe timu kongwe za barani la Afrika kutoka nchini Ghana, Hearts of Oak na Asante Kotoko kwa pamoja na 2011 Kagame Castle Cup’s finalists Simba na Yanga hayatakuwepo tena.

Mashindano hayo ambayo yalipewa jina la “Tanzania International Cup” na yalipangwa kufanyika ndani ya siku mbili kupitia usimamizi wa kampuni mbili za Afrika Kusini Lumuli Marketing na Octagon.

Chanzo cha kutofanyika kwa michuano kunasemekana ni waandaji kushindwa kuhimili gharama kubwa za kutumia uwanja wa taifa walizotajiwa na wasimamizi wa uwanja huo.

BREAKING NEWS: YANGA YAMSAJILI IDRISA RAJABU

Klabu Bingwa ya Tanzania Bara Dar Young African wamefanikiwa kumsajili mchezaji wa Sofapaka ya Kenya na timu ya taifa ya Tanzania Idrisa Rajabu.
Idrisa ambaye hucheza upande wa beki wa kushoto alisajiliwa Sofapaka akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro misimu miwili iliyopita, na sasa anarejea Tz kuja kuitumikia Yanga.

SHAY GIVEN KUHAMIA VILLA WIKI IJAYO


Aston Villa wana matumaini kuwa Shay Given atakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Alex McLeish wiki ijayo kwa dili la paundi 3.5 million kutoka Manchester City.
Villa wanataka huduma za kipa huyo kutoka Ireland ambaye amekosa nafasi ndani ya kikosi cha Eastlands ili kumbadili golikipa Brad Friedel aliyehamia Tottenham.
Klabu hizo mbili kwa muda sasa wamekuwa kwenye mazungumzo na chanzo cha habari kutoka Villa zinasema dili hilo kumsajili kipa huyo litakamilika wiki ijayo.
Given alikuwa namba 1 akiwa Newcastle kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 kabla hajaamia City miaka miwili iliyopita.

WAYNE ROONEY AMVALISHA MWANAE JEZI EVERTON.

Mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney leo ame-post picha ya mtoto wake wa kiume KAI akiwa amevaa jezi ya timu aliyokuwa anaichezea zamani ya Everton, huku akihaidi kutoa picha nyingine ya mtoto wake akiwa amevaa jezi mpya ya United, Kesho.

WANYAMA AKARIBIA KUTUA CELTICS


Mdogo wake kiungo wa kimataifa wa Kenya anayecheza soka lake huko Italia kwneye klabu ya Inter Milan McDonald Mariga anayekwenda kwa jina Victor Wanyama Mugabe yuko mbioni kujiunga na klabu kubwa nchini Scotland ya Glasgow Celtics . Wanyama ambaye ambaye ameichezea timu yake ya taifa ya Harambee Stars mara kadhaa na anakaribia kusaini kuichezea Celtics baada ya kushinda rufaa yake ya kibali cha kazi nchini Scotland. Wanyama ambaye ana umri wa miaka 20 alikuwa anaichezea Germinal Beerschot na anaongeza idadi ya Waafrika mashariki wanaocheza soka huko Scotland baada ya Mganda David Obua ambaye anaichezea Hearts baada ya kusajili toka Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.

LIVERPOOL KUWAFUATA ARSENAL NA MAN CITY


Baada ya Manchester City na Arsenal kuuza haki za jina uwanja wao, sasa klabu ya Liverpool nayo iko mbioni kuuhama uwanja wake wa kihistoria wa Anfield . Klabu hiyo kwa sasa iko mbioni kuanza mradi wa kujenga uwanja mwingine lakini ili kufanikisha mradi huo klabu hiyo inatakiwa kutengeneza fedha za ziada ambazo kwa taarifa toka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa italazimika kuuza haki za kuupa jina uwanja wa Anfield YAANI “Naming Rights ” kwa kampuni itakayofika bei na kutoa fedha ambazo zitatumika kujenga uwanja mwingine kama ilivyokuwa kwa uwanja wa Arsenal The Emirates ambao kampuni ya usafiri wa Anga inayomiliki ndege za Emirates ambayo inadhamini uwanja huo kwa kuwa imelipia haki za kutumia jina la Brand yao kama jina la uwanja . Sasa unapoingia kwenye uwanja wa Anfield kaka inavyoonekana hapo kwenye picha inayomuonyesha Fernando Torres na Rafa Benitez kuna bango limeandikwa “THIS IS ANFIELD”, je Bango hili litabailishwa na kuandikwa “THIS ISN’T ANFIELD”??

KUTOKA EASTLANDS MPAKA ETIHAD STADIUM NA £100M


MANCHESTER CITY wametangaza dili lilivunja rekodi kupitia udhamini wa Etihad Airways.
Matajiri wa Premier League wameuza haki za jina la uwanja wao wa Eastlands, ambao sasa utajulikana kama Etihad Stadium. The Abu Dhabi Airline wamekubali kutoa udhamini wa miaka 10 wenye thamani paundi millioni 100, hivyo kuushinda mkataba kati ya Arsenal na Emirates Airline ambao nao una thamani ya £ 100m lakini ukiwa ni kwa kipindi cha miaka 10 kwa ajili ya kuupa jina la "Emirates " uwanja wa Gunners. Manchester City's CEO Garry Cook ameusifu mkataba huo kuwa ndio bora na muhimu katika historia ya soka.
"Tuna furaha kutangaza kuongeza mkataba wetu na Etihad Airways.Partnership yetu haitakuwa kwa jezi pekee lakini pia utahusu uwanja wetu- Etihad Stadium.Sehemu pana inayozunguka uwanja itajulikana kama "Etihad Campus".Kuna vitu vingine kama vile media, biashara na ushirikiano wa jamii na vitu vingine vingi. "Pengine huu unaweza kuwa mkataba mzuri zaidi katika historia ya Soka." Etihad tayari wameshakuwa wadhamini wa jezi za City kwa mkataba wa £ 2.8m per year. Huu ni mfano mwingine wa uwekezaji mkubwa kutoka Abu Dhabi ndani ya klabu hii, baada ya mwaka 2008 Sheikh Mansour kuinunua klabu hii na kutumia zaidi ya £ 1 billioni katika kuijenga upya timu kwa kununua wachezaji, mishahara, kukarabati uwanja na vifaa vya mazoezi. Mpaka sasa Sheikh Mansour ameshatumia pesa nyingi sana katika kununua wachezaji na mpaka mwisho wa msimu huu wa usajili anakadiriwa kutumia kwa jumla zaidi ya £ 400m.

CHRIS SMALLING ASAINI MKATABA MPYA NA UTD


MANCHESTER UNITED wamempa Chris Smalling mkataba mpya wa miaka 5 baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mwaka wake wa kwanza ndani ya kikosi cha Red Devils. The 21-year old defender alihamia United akitokea Fulham last summer kwa deal la paundi million 7. Na akiwa ameonyesha uwezo mkubwa katika kuisadia United kushinda ubingwa wa 19 wa EPL , amezawadia mkataba huu mnono. Boss Sir Alex aliongea kuhusu mkataba huu mpya wa Smalling na kusema: "Nina furaha sana baada ya Chris kusaini mkataba mpya. Smalling amekuwa mchezaji muhimu tangu ajiunge nasi kutoka Fulham mwaka jana, ana umri mdogo lakini ana kipaji kikubwa, ana nguvu, akili na anajua kuusoma mchezo.Ni hazina kubwa kwa klabu hii." Smalling nae alisema: "Naangalia mbele kudumu na kupata mafanikio ndani ya klabu ya Manchester United".

FIESTA MWANZA TULIONA KIPAJI HIKI

OWEN HARGREAVES AJIKUBALI YUKO FITI KWA KLABU YOYOTE INAYOMTAKA BAADA YA KUA HURU AKITOKEA KLABU YA MANCHESTER UNITED.


Thursday, July 7, 2011

Asamoah, Mwape, Canavaro na Berko wakifanya maandalizi ya mwisho ndani ya BM Executive Barbershop & Beauty Centre kabla ya kuwakabili ST GEORGE.

KAMERA YA BLOG HII IMEWANASA WACHEZAJI WA YANGA ( DAVIS MWAPE RAIA WA ZAMBIA,ASAMOAH KENETH RAIA WA GHANA,NADIR HAROUB 'CANAVARO'-TANZANIA PAMOJA NA GOLIKIPA YAW BERKO RAIA WA GHANA WAKIJIPIGA SOAP SOAP KABLA YA MPAMBANO WAO WA NUSU FAINALI YA KAGAME CASTLE CUP DHIDI YA ST GEORGE YA ETHIOPIA.





Asamoah, Mwape and Canavaro at BM Executive Barbershop Mara baada ya kupata huduma za salon na Massage







Yaw Berko na Davis Mwape mara baada ya kupata huduma ya salon VIP BM Executive Barbershop & Beauty Centre - Kinondoni.












Yaw Berko akipata huduma ya Salon Bm Executive Barbershop & beauty Centre - Kinondoni






Davis Mwape akipata huduma ya salon BM Executive Barbershop & Beauty Centre - Kinondoni






Asamoah, Mwape, Canavaro wakiwa BM Executive Barbershop & Beauty Centre mara baada ya kupata huduma za salon wengine ni Choki na Hassan wafanyakazi wa BM





Asamoah, Canavaro na Mwape wakiwa BM Executive Barbershop & Beauty Centre - Kinondoni kwa huduma za Salon wengine ni Ustadhi na Kulwa wafanyakazi wa BM

WASHAMBULIAJI WAKALI AMBAO HAWAJAWAHI KUTOKEA TANZANIA



1970-1976
Tukiangalia kwa makini historia ya soka la Tanzania kuanzia mwaka 1970 hadi 1976 inaelezwa ndiko walipokuwapo washambuliaji wakali walioweza kufanya vema katika timu zao na ile ya Taifa, hao wanaongozwa na Gibson Sembuli, Adam Sabu, Kitwana Manara, Abdallah Kibaden, Jumanne Hassan ‘Masimenti’ na wengine ambao waliweza kutoa changamoto ya soka nchini.

Hawa waliweza kufanya vizuri kutokana na vitu vingi, ikiwemo utayari wao kwa mchezo wa soka. Pia ni kipindi ambacho wachezaji walipatikana kutoka mashuleni na mitaani.

Kwa mfano Sembuli aliweza kufanya vizuri kutokana na uwezo binafsi wa kumiliki mpira, kutekeleza kile alichokuwa anaelezwa na kocha kila wakati awapo uwanjani, mwili uliojengeka vema kimichezo kuweza kuhimili shuruba za mabeki wakorofi.

Sembuli anaelezwa kuwa, alikuwa na uwezo wa kukaa na mpira kwa muda mrefu zaidi na kuleta madhara langoni kwa adui wakati wowote awapo uwanjani.

Lakini yatasemwa yote kuhusu washambuliaji wa wakati ule, kubwa zaidi ni akili yao kuzama katika soka zaidi kuliko jambo jingine lolote. Hiki ni kitu pekee kinachoweza kumfanya mchezaji kuwa katika kiwango chake wakati wote.

Kati ya wote aliokuwa akicheza nao wakati huo, Sembuli anatajwa kuwa mshambuliaji bora wa ‘enzi’ zake akiwaacha kina Manara, Kibaden na Masimenti.




1977-1982
Hiki ndicho kipindi zilipochomoza timu nyingi za maeneo yaliyohamasika kisoka kama Coastal Union, African Sports, Mseto na nyinginezo ambazo zilikuwa na wachezaji mahiri walioweza kutandaza vema kabumbu.

Miongoni mwa wachezaji hao ni Mohamed Salim (Coastal), Thuwen Ally (Simba), Peter Tino (African Sports), Omar Hussein (Mseto-Yanga), George Kulagwa, Rashid Hanzuruni na wengineo.

Ndani ya kipindi hiki timu zilizoweza kutoa wachezaji wengi kwa timu ya taifa ni Simba na Pan African pekee. Ikumbukwe kuwa, Pan ilipata uhai baada ya baadhi ya wachezaji kujiengua kutoka Yanga na kuunda timu hiyo.






1982-1985
Baada ya Tanzania kushiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1980, wachezaji wengi kwa ridhaa yao waliachana na soka, hivyo kutoa nafasi kwa wanasoka wengine kujitokeza katika timu mbalimbali.

Miongoni mwa nyota wapya waliojitokeza ni Innocent Haule, Madaraka Selemani, Makumbi Juma, Richard Lumumba, Juma Mgunda, Zamoyoni Mogela, Gebo Peter, Malota Soma bila ya kumsahau mchezaji aliyekuwa kinda wakati huo Edward Chumila ‘Edo Boy’.

Kizazi hiki kinaelezwa kupokea vema kijiti kutoka kwa kaka zao wa 1977-1982, nguvu ya kampuni na mashirika mbalimbali ya umma iliweza kuwafanya waonekane bora katika soka wakati huo.

Katika kipindi hiki, unaweza kukumbuka jinsi kina Edo Boy walivyoweza kuinusuru Simba isishuke daraja baada ya kuwa katika hali mbaya kufuatia kufanya vibaya kwenye Ligi Daraja la Kwanza—Tanzania Bara.

Hiki ni kipindi ambacho wachezaji hawakuwa na shaka juu ya maisha yao kwani fedha kutoka katika mashirika waliyochezea ziliweza kuwainua kimaisha; pia hakukuwapo na tamaa ya fedha miongoni mwao bila kuwajibika kwanza.

Ni kipindi ambacho, timu kama Majimaji, Pamba, Coastal Union na African Sports ziliweza kuchomoza.




EDIBILY LUNYAMILA AKIWA NA MOHAMED HUSSEIN.


1985-1991
Ndani ya kipindi hiki hakukuwapo na wachezaji wengi sana waliojitokeza, zaidi ya wale waliovuma katika kipindi cha 1982-1985 kuendelea kusakata soka, lakini kwa kiasi kikubwa utawala wa Simba na Yanga katika soka uliweza kupungua kidogo.

Timu za Majimaji, Pamba, African Sports, CDA, Tukuyu Stars, Bandari na nyinginezo ziliweza kufanya vizuri katika ligi na kuonyesha msisimko mpya, lakini nyingi ya timu hizo zikipata msaada mkubwa kutoka kwa mashirika yaliyokuwa yakizimiliki.

1991 – sasa
Hiki ndicho kizazi asilia cha soka; kimeweza kupotea na kutuletea wachezaji wachache ambao mpaka leo wangali wanajaribiwa kuweza kuwa na mshambuliaji wa kuisaidia nchi.

Mwanzoni mwa 1991, wakongwe kama Mogela, Madaraka na Edo Boy waliweza kushirikiana na chipukizi kama Nteze John, Edibily Lunyamila, Thomas Kipese, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Dua Said, Said Sued ‘Scud’, Mao Mkami, Fumo Felician, Kitwana Suleiman, Beya Simba na wengineo kuleta changamoto katika nafasi za ushambuliaji miongoni mwa timu zao, lakini hali haikuwa kama zamani.

Baadaye kidogo kikaja kizazi cha kina Maalim Saleh, Nonda Shaaban ‘Papii’, Clement Kahabuka, Bitta John, Victor Bambo na wengineo ambao walionekana kama watu wa kupita wasiokuwa na malengo ya kufika; badala yake wakaendelea kutoa nafasi kwa kina Lunyamila, Madaraka, Nteze, Edo Boy na wengine kuendelea kutamba.

Baadaye kidogo kikaja kizazi cha kina Athuman Machupa, Athuman Macheppe, Emmanuel Gabriel, Abdallah Juma, Monja Liseki, Akida Makunda, Steven Mapunda ‘Garincha’ na baadhi yao kidogo, lakini hawakuweza kufikia uwezo na kasi ya kina Sembuli, Mogela na hata Mohamed Salim.

Ikumbukwe ya kuwa hicho ndicho kipindi ambacho wafanyabishara walijitokeza kwa wingi kudhamini timu mbalimbali ili ziweze kufanya vizuri, bado baadhi ya wachezaji wa wakati huo wangali wanacheza soka hadi leo hii.

MTOTO WA NYOKA NI NYOKA...

Alli Abdallah Kibaden mtoto wa kocha wa siku nyingi nchini Tanzania ambaye kwa sasa anachezea timu ya soka ya watoto ya Convetry City ya England wa tatu kushoto waliosimama.

OKWI AENDA KUFANYIWA VIPIMO KAIZER CHIEFS


Mshambuliaji wa Uganda “Cranes” na Simba ya Tanzania Emmanuel Okwi anakaribia kukamilisha usajili wake kutoka Msimbazi kuelekea katika klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini.

Okwi ambaye bado ana mkataba wa kuichezea klabu yake ya Simba amekuwa kwenye rada za moja ya klabu kubwa kusini mwa afrika, anatarajiwa kufanyiwa vipimo leo na endapo atafaulu atasaini mkataba ambao utaoiingizia akaunti ya Simba donge nono kama ilivyokuwa kwa wachezaji Mbwana Samatta na Patrick Ochan waliouzwa fedha zaidi ya shilingi mil. 300.

JOSEPH OWINO MAISHA NJE YA SOKA


Beki wa kimataifa wa Uganda aliyekuwa anaichezea klabu ya Simba msimu uliopita Joseph Owino ameongea nab log hii kuelezea maisha yake nje ya soka.

Owino ambaye recently alifanyiwa operation ya goti nchini India kwa sasa yupo kwao nchini Uganda akijiendeleza na elimu huku akijishughulisha na biashara katika kuhakikisha hayumbi kimaisha.

“Nashukuru mungu naendelea vizuri na goti langu, na kwa sasa natumia muda wangu kuwa nje ya uwanja kujiendeleza kielimu, nachukua masters ya Business Administration @Makerere University, na vilevile najishughulisha uuzaji wa ujumla wa vifaa vya stationery.-Owino

JOHN O'SHEA ANAFANYIWA VIPIMO @ SUNDERLAND


Baada ya jana Wes Brown kwenda North East kufanyiwa vipimo na kukamilisha deal la kuhamia Sunderland. Leo mchezaji mwingine kutoka Man United, the versatile John O’shea ameelekea Stadium Of Light kufanyiwa vipimo.

Ikiwa O’shea na Brown watafanikiwa kufaulu vipimo na kujiunga na Sunderland, kocha Steve Bruce atakuwa ametimiza usajili wa wachezaji nane ndani ya kipindi hiki cha usajili , huku Darren Gibson nae akiwa njiani kujiunga na Black Cats.

EXCLUSIVE: JERRY TEGETE NJIANI KUELEKEA MSIMBAZI

"CHUKUA JEZI YA UKWELI HII" JERRY TEGETE AKIWA NA ULIMBOKA MWAKINGWE.

Kutothaminiwa na viongozi na kutopata nafasi ndani ya kikosi cha timu yake kumefungua milango ya klabu ya Yanga kwa mshambuliaji Jerryson Tegete.

Habari kutoka chanzo cha habari kilicho karibu na viongozi wa klabu ya Simba na Tegete zinasema kwa zaidi ya 60% mtoto wa meneja wa uwanja wa CCM Kirumba atakuwa mchezaji wa klabu ya Simba muda wowote kutoka sasa.

Tegete ambaye katika michuano inayoendelea ya CECAFA Kagame Cup anaonekana kuporwa na namba na washambuliaji Asamoah, Hamis Kiiza na Davis Mwape hali ambayo imemkosesha amani mshambuliaji huyo.

Wednesday, July 6, 2011

NINI YANGA KURUDIA KUPIGA PENALTY MARA MBILI, PENALTY HII IMERUDIWA MARA SITA KUPIGWA!!!!

TARATIBU NA SHERIA ZA KUPIGA PENATI

PENALTY SHOOT-OUT

"Penalty shoot out" ni mipigo ya mpira kutoka kwenye alama maalum iliyowekwa katika "Penalty Box" ya uwanja wa mpira wa miguu.

Hii ni njia inayotumika katika sheria za mchezo wa soka zinazotumika kuamua ni timu gani isonge mbele kwenda hatua inayofuata katika michuano au kushinda michuano.

Mipigo hii ya penati inasimamiwa na sheria na kanuni ambazo zimewekwa na FIFA.




  • TARATIBU ZA KUPIGA PENATI

    *Timu ya kwanza kupiga mkwaju wa kwanza kuamuliwa kwa kurushwa shilingi na rafa ataamua ni goli lipi litumike kwa kupigia penati.

    *Mikwaju yote ya penati itapigwa katika goli moja ili kuhakikisha wapigaji wa penati na magolikipa wote wanakutana na hali yoyote isiyokuwa ya kawaida (kama ikiwepo).

    *Wachezaji wote isipokuwa mpigaji na magolikipa wanapaswa kubakia katikati ya uwanja.

    *Mipigo yote inatakiwa kupigwa kutokea katika alama ya kupigia penati, huku golini kukiwa na golikipa wa timu tofauti na mpigaji.Kipa anatakiwa kubaki katikati ya milingoti miwili huku akiwa amesimama katika mstari wa goli mpaka pale mpira utakapokuwa umepigwa, ingawa anaweza kurukaruka, kunyoosha mikono, kwenda upande mmoja mpaka mwingine akiwa ndani ya mstari wa goli.

    *Kila mpigaji anaweza kupiga mpira mara moja tu, ikiwa mpira aliopiga utazuiwa na golikipa, ukigonga mwamba mpigaji haruhusiwi kuupiga tena (lakini hii ni tofauti ni penati za ndani dk 90).

    *Hakuna mchezaji wa timu ya mpigaji anaruhusiwa kuugusa mpira.

    *Mpira unaweza kumgusa golikipa, milingoti ya pembeni na wa juu kwa idadi yoyote.

    Hali kama hii iliwahi kutokea katika mechi ya fainali za kombe la dunia mwaka 1986-Mexico katika mechi ya Brazil vs France, mechi ambayo iliamuliwa kwa mikwaju ya penati.Wakati wa kupiga penati mchezaji wa Ufaransa Bruno Bellone alipiga mkwaju ambao uligonga mwamba na kurudi uwanjani kisha ukarudi na kuingia golini.Mwamuzi Loan Igna akaamuru kuwa ni goli na nahodha wa Brazil Edinho alipopinga kuwa mpira ulipogonga mwamba na kurudi uwanjani ilitakiwa iamuriwe kuwa tayari France wamekosa akapewa kadi, lakini mwaka 1987 International Football Association Board walithibitisha kuwa kupitia sheria namba 14 inayohusu upigaji wa penalty kuwa maamuzi ya refa yalikuwa sahihi.

    *Ikiwa baada ya mipigo mitano kukamilika na timu zote zikalingana kwa idadi ya magoli, basi zitaanzwa kupigwa penati moja moja kwa kila timu mpaka timu moja itakapofunga na nyingine ikakosa.

    • *Wachezaji 22 pekee waliokuwepo ndani ya mchezo mpaka ulipomalizika ndio wanaruhusiwa kushiriki katika kupiga penati.
    • *Timu inaweza kumbadilisha golikipa ambaye atakuwa ameumia kipindi cha upigaji wa penati, ikiwa timu husika itakuwa haijamaliza idadi ya wachezaji wanaopaswa kubadilishwa.
    • *Ikiwa golikipa atapewa kadi nyekundu, mchezaji mwingine aliyekuwepo ndani uwanja kabla ya mpira kumalizika atachukua jukumu la kukaa golini.
    • *Ikiwa mchezaji mwingine isipokuwa golikipa akiumia au kupewa kadi nyekundu, mikwaju ya penati itaendelea bila kuwepo na mabadiliko yoyote.
    • *Mchezaji yoyote anaweza kuchukua majukumu ya golikipa aliyetolewa kwa kuumia au kwa kadi, na sio lazima mchezaji yuleyule adake mipigo yote anaweza akabadilishwa.
    • *Hakuna mchezaji anayeruhusiwa kupiga penati mara mbili kupigia mpaka pale mzungumko wa wachezaji wote wa timu husika watakapokuwa wamemaliza kupiga mpigo wa kwanza, akiwemo golikipa.
    • *Ikiwa itatokea hali ya ulazima kwa wachezaji kupiga penati kwa mara ya pili (kwa sababu kumekuwa na usawa wa matokeo mara ambapo wachezaji wote halali watakapokuwa wamemaliza mipigo yao ya kwanza) timu hazina ulazima wa kurudia wachezaji wale wale waliowatumia katika penati za 5 za kwanza.
    • *Ikiwa katika mwanzo wa upigaji penati timu moja itakuwa na wachezaji wengi uwanjani tofauti na nyingine, basi timu ambayo imebakiwa na wachezaji wengi uwanjani itabidi ichague mchezaji au wachezaji ambao watakuwa na idadi sawa na wapinzani wao.Mfano, ikiwa timu Team A itakuwa na wachezaji 11 lakini Team B ina wachezaji 10, basi Team A itabidi imchague mchezaji mmoja ambaye hatahusika kabisa na zoezi la upigaji penati hivyo golikipa hawezi kuchaguliwa kuondolewa katika listi ya wachezaji kumi wataohusika na kupiga penati huku akiendelea kudaka.Hatua inahusika ikiwa tu wachezaji/mchezaji alitolewa nje kwa kuumia au kwa kadi ndani ya dakika za kawaida za mchezo na sio ndani ya kipindi cha upigaji penati.

PHOTOS: FABIO COENTRAO NDANI YA REAL MADRID




FABIO COENTRAO AKISAINI MKATABA WA KUICHEZEA REAL MADRID AKIWA NA RAISI WA MADRID- FLORENTINO PEREZ.



DIRISHA LA USAJILI BARANI ULAYA





Kocha msaidizi wa klabu ya Manchester United Rene Meulensteen amesema mchezaji wa Inter Milan Wesley Sneijder ndiye kiungo anayepaswa kusajiliwa na Red Devils msimu huu.

Rene ambaye ni mholanzi anaamini kuwa Sneijder ndio mtu sahihi anayepaswa kuja kuleta uhai katika dimba la uwanja ndani kikosi cha Man United.

"Hakuna Paul Scholes mpya, kama ambavyo hajawahi kutokea Roy Kean mpya, lakini Sneijder atakuwa mtu sahihi na atafiti vizuri ndani kikosi chetu, " Meulensteen aliuambia mtandao wa Voetbal International.

"Siwezi kuona mchezaji mwingine mzuri zaidi kwa timu yetu.Nasema hivi sio kwa sababu mimi mholanzi.Nimefanya kazi hapa kwa muda sasa, naijua timu ndani na nje na nafahamu kuwa usajili wa Wesley utakuwa mzuri sana.

Anaonekana kama mtu sahihi wa kucheza na wachezaji kama Hernandez, Rooney, Park, Ahley Young, Valencia, Nani na Giggs, na kikubwa zaidi Wesley ana uzoefu wa lazima katika kucheza katika level za juu.

Sijui kuhusu mipango yake ya baadae ndani ya Inter, kama ataondoka au kama bei yake ni nafuu, lakini katika suala ya uwezo wa kucheza soka, Nasema Sneijder ndio mtu sahihi kusajiliwa na United kwa sasa."

BERBATOV + CASH FOR BASTIAN SHWEINSTEIGER


Wakati huo huo gazeti la Daily Star linaripoti kuwa kocha mkuu wa Mabingwa wa England Manchester United anajipanga kumtumia mshambuliaji Dimitar Berbatov katika kufanikisha uhamisho wa Bastian Schweinsteiger kutoka Bayern Munich.

Ferguson ambaye amekuwa akimtamani Schweinsteiger kwa muda mrefu anamuona kiungo huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani kama mtu sahihi wa kwenda kuziba mapengo katika safu ya kiungo mkabaji ndani ya kikosi cha Red Devils.

Hivyo katika kujaribu kuwashawishi Bayern SAF anapanga kumtumia Berbatov ambaye amekuwa akizivutia klabu kadhaa barani ulaya ikiwemo Bayern katika deal hilo ambalo pia litahusisha kiasi cha pesa.

HATIMAYE CHARLIE ADAM KUELEKEA ANFIELD

Klabu za Liverpool na Blackpool zimefikia muafaka katika uhamisho wa Nahodha wa Blakcpool Charlie Adam kuelekea Anfield.

Scotland midfielder mwenye umri wa miaka 25, sasa atasafiri kwenda Merseyside kwa ajili ya kufanyiwa vipimo na kukubaliana na Liverpool kuhusu matakwa yake binafsi.

Liverpool walikuwa wakimfuatilia Adam kwa miezi takribani 6, leo jioni hii wamethibitisha kwamba wamekubaliana na "Seasiders" kuhusu bei ya kumsajili Charlie Adam.




MAN CITY YAKAMILISHA USAJILI WA SAVIC




Manchester City wamekamilisha usajili wa beki Stefan Savic kutoka Partizan Belgrade kwa mkataba wa miaka wa miaka 4.

Beki huyo raia wa Montenegro mwenye umri wa miaka 20 alifanikiwa kupata kibali cha kufanya kazi nchini England na kuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na City ndani ya siku 3, baada ya Gael Clichy aliyetokea Arsenal.

Savic ambaye miezi 12 iliyopita alikuwa akifanya majaribio na Arsenal lakini hakufanikiwa kupata mkataba @ Emirates ameuambia mtandao wa Manchester City kuwa: "Nimekuwa nikiitizama Premier League muda wote na najua ni sehemu nzuri ya kuendeleza kipaji changu katika kuisaidia klabu hii kushinda vitu vikubwa.Tuna uwanja mzuri na nimeona ni jinsi gani mashabiki wa City walivyo na mapenzi na klabu hii."

Montenegro watacheza na England baadae mwaka huu hivyo nategemea kuwa na uchezaji wa kirafiki na waingereza, Nina furaha sana kuwa mchezaji wa Manchester City." - Amelonga Savic.

TWIGA STARS v ZIMBABWE

Harare,
Tanzania 'Twiga Stars' inajitupa uwanjani kesho (Julai 7) kuwakabili wenyeji
Zimbabwe 'Mighty Warriors' katika mechi ya pili ya nusu fainali ya michuano ya
Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayochezwa
Uwanja wa Rufaro, jijini hapa.

Mechi ya Twiga Stars itachezwa saa 9.15 kwa saa za hapa (saa 10.15 kwa saa za
Tanzania), wakati nusu fainali ya kwanza kati ya Afrika Kusini 'Banyana Banyana'
dhidi ya Malawi itaanza saa 6.30 mchana kwa saa za hapa.

Twiga Stars inayoongozwa na nahodha wake Sophia Mwasikili imefanya mazoezi
mepesi leo asubuhi kwenye Uwanja wa Rufaro kujiweka tayari kwa ajili ya pambano
hilo ambalo tayari limekuwa gumzo kwa mashabiki wa hapa.

Akizungumza baada ya mazoezi, Kocha Mkuu wa Twiga, Charles Mkwasa amesema
Zimbabwe ni timu nzuri lakini amekiandaa kikosi chake kwa ajili ya kuibuka na
ushindi ili kiweze kucheza nusu fainali na hatimaye kunyakua kombe hilo.

"Zimbabwe watakuwa na faida ya kucheza mbele ya mashabiki wao. Kwa kawaida
wanamtegemea yule mshambuliaji wao mrefu wa kati (Rufaro Mutyavaviri) huku
wakitumia sana wingi ya kulia. Nimewaandaa wachezaji wangu kwa hilo.

"Kikosi hakitakuwa na mabadiliko ambapo Ettoe Mlenzi aliyekuwa na kadi mbili za
njano atarejea uwanjani. Mabadiliko yatakuwa kwa beki wa kushoto ambapo kwenye
mechi ya Zimbabwe ataanza Fatuma Khatibu," amesema Mkwasa ambaye timu yake
imeingia katika michuano hiyo ikiwa mwalikwa kwa vile si mwanachama wa COSAFA.

Mutyavaviri ndiye anayeongoza katika ufungaji katika michuano hiyo ambapo kwenye
mechi kati ya timu yake na Malawi alifunga mabao matano. Mighty Warriors
ilishinda mabao 8-2 na mshambuliaji huyo amekuwa akifunga katika kila mechi.

Twiga Stars ni miongoni mwa timu ambazo tangu awali zilikuwa zikipewa nafasi ya
kutwaa ubingwa kutokana na kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika
zilizofanyika mwishoni mwa mwaka jana nchini Afrika Kusini. Nyingine ni wenyeji
Mighty Warriors na Banyana Banyana ambazo zote zimefuzu kwa hatua ya nusu
fainali.

Wachezaji watakaonza kwa Twiga Stars katika mechi ya kesho ni Fatuma Omary,
Fatuma Makusanya, Fatuma Khatibu, Sophia Mwasikili, Mwanaidi Tamba, Mwajuma
Abdallah, Mwanahamisi Omary, Ettoe Mlenzi, Fatuma Mustafa, Asha Rashid na
Fadhila Kigalawa.

Twiga Stars imekuwa ikishangiliwa kwa nguvu na Watanzania wanaoishi hapa
wakiongozwa na Balozi Adadi Rajab ambaye ameshuhudia mechi zote za timu hiyo.

Mechi kati ya Twiga Stars na Mighty Warriors itaoneshwa moja kwa moja (live)
kupitia SuperSport 4 na Shirika la Utangazaji la Zimbabwe (ZBC). Fainali na
mechi ya kutafuta mshindi wa tatu (classification) zitachezwa Julai 9 mwaka huu
kwenye Uwanja wa Rufaro.

Timu ambazo zimeaga mashindano baada ya kushindwa kufuzu kwa hatua ya nusu
fainali jana ni Botswana, Zambia, Lesotho na Msumbiji.

Boniface Wambura
TFF Media Officer
Harare