Search This Blog

Saturday, July 21, 2012

PHOTOS - HIVI NDIVYO SIMBA WALIVYOPAMBANA NA VITA

 Mchezaji wa TP Vita Club ya DRC, akiwatoka Kigi Makasi na Kanu Mbiayavanga wa Simba
wakati wa mchezo wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki ya Kagame Cup, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. Timu hizo zimetoka sare ya bao1-1

Mashabiki wa timu ya Simba wakifuatilia mchezo wa Klabu Bingwa ya Afrika ya Mashariki
na Kati, kati ya timu yao na TP Vita Club ya DRC, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam


Mashabiki wa Simba wakiwa wamesimama kwa dakika 1 kuwakumbuka wahanga wa ajali ya boti iliyotokea Zanzibar wiki hii

Kikosi cha Simba kilichoanza leo

Kikosi cha Vita

Sunzu akijaribu kumtoka beki wa Vita katika mechi ya leo - ambayo pia Sunzu alikosa penati.

EPIQ BONGO STAR SEARCH NDANI YA MBEYA - GREEN CITY - WAWAKUMBUKA WAHANGA YA AJALI YA BOTI ZANZIBAR

Majaji wa Epiq BSS - Madam Ritha, Salama na Master Jay wakisimama kwa dakika 1 kuwakumbuka wahanga wa ajali ya boti iliyotokea Zanzibar.


Umati wa vijana wenye vipaji wakitafuta nafasi ya kufunguka na Epiq Bongo Star Search


Mmoja ya washiriki akichangia damu kabla ya kuingia kwenye chumba cha sindano kwa majaji kuonyesha uwezo wake.

LIVE MATCH CENTRE: SIMBA 1 - 0 VITA - FULL TIME


 FULL TIME: SIMBA 1 - 1 AS VITA

 DK 91:FELIX SUNZU ANAIKOSESHA SIMBA PENALT

DK 91: SIMBA WANAPATA PENALT

DK 90: SIMBA 1 - 1 AS VITA

DK 84: SIMBA 1- 1 VITA

 DK 66: SIMBA 1 (HARUNA MOSHI) - 1 AS VITA

DK 61: AS VITA WANAKOSA BAO

DK 61: SIMBA WANAKOSA BAO

DK 59:AS VITA WANAKOSA BAO

DK 51: SIMBA WANAKOSA BAO

DK 49: AS VITA WANAKOSA BAO

DK 47: SIMBA WANAKOSA BAO

DK 46: SIMBA 0 -1  AS VITA

DK 45: SIMBA 0 - 1  AS  VITA

DK 43:SIMBA 0- 1  AS VITA (penalt)

DK 1: Simba 0 - 0  Vita

SUALA LA KELVIN YONDANI KUCHEZA KAGAME NA UTATA WAKE WA KIKANUNI: IWEJE YEYE ARUHUSIWE KUCHEZA WAKATI KISIGA NA EMMANUEL GABRIEL WALIZUIWA?-



Baada ya jana shirkisho la soka la Tanzania (TFF) kupitia kamati yake Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji, kufikia uamuzi wa kumruhusu Kelvin Yondan kuichezea klabu ya Yanga kwenye mashindano ya Kagame tu, na mustakabali wake wa mbele kuhusu kuendelea kuichezea Yanga utajulikana baadae.


Kutokana na suala hili kumetojitokeza maswali mengi ambayo TFF na CECAFA itabidi watupe majibu wadau wa soka nchini.


Kwanza kabisa mojawapo ya kanuni ya mashindano ya CECAFA - ili mchezaji fulani aweze kuwa halali kuichezea timu fulani kwenye mashindano haya ni lazima awe pia halali kuichezea klabu yake kwenye mashindano ya ligi kuu ya nchini husika inapotoka klabu yake. Kwa maana hiyo kifungu hiki kinamuhukumu Yondani kuruhusiwa kucheza Kagame Cup, kwa kuwa bado hajathibitishwa kuwa na uhalali wa kuitumikia Yanga kwenye ligi kuu ya Tanzania bara.
Emmanuel Gabriel
Ikumbukwe suala kama hili limewahi kutokea huko nyuma - kuna wakati Shabaan Kisiga aliporudi Tanzania akitokea Oman akasajiliwa na Simba lakini hakuwa amepata ITC, na Simba ikaomba kumtumia kwenye Kagame lakini kipengele kama hicho kikambana kuitumikia klabu yake mpya mpaka pale atakapokuwa halali kuichezea timu yake kwenye ligi kuu. Pia suala kama hili limeshawahi kumtokea Emmanuel Gabriel huko nyuma - lakini tena kipengele hiki cha kanuni za CECAFA zikambana akashindwa kuitumikia Simba kwenye Kagame.


Sasa linakuja swali iweje kanuni hii ibadilike kwa Kelvin Yondani tu, ama imebadilishwa na kwa bahati mbaya wadau hatuna taarifa?


Kama kuna mwenye jibu au ufafanuzi juu hili naomba atoe hapa kwenye maoni.


Ni mtazamo tu - nawasilisha.

BAADA YA YONDANI - SIMBA WAPIGWA BAO LINGINE - IBRAHIMU JEBA ARUDI AZAM APOKELEWA


Baada ya TFF kutangaza kuwa Yondan ni wa Yanga 100%, Jeba naye karejea Chamazi na kuomba msamaha na kusamehewa na sasa anapiga Jaramba na chama lake la Azam FC... Poleni wazee wa Magazeti na Redio... Nilisema kuwa Jeba atacheza Azam FC na yametimia
· · · 3 hours ago
 
Kwa mujibu wa manager wa timu ya Azam Patrick Kahemele ni kwamba kinda la klabu hiyo lilisajiliwa na Simba mwanzoni mwa mwezi uliopita kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo msimu, amerudi tena Azam baada ya taratibu za kumsajili kutofuatwa na Simba.

MANCHESTER UNITED WAKIWA NCHINI SOUTH AFRIKA

Anderson akiwa amembeba nyoka huku Valencia akiwa anamshangaa

Watoto wa kutoka bara la Amerika wakipiga ngoma

Valencia nae ikafika zamu yake ya kucheza na nyoka



Anderson alionekana mzoefu kuliko wenzie kwenye kucheza na Nyoka

Shinji Kagawa

OFFICIAL: UTAMABULISHO RASMI WA MECKY MEXIM KUWA KOCHA MKUU WA MTIBWA SUGAR



PICHA YA SIKU: MCHAGULIE ROBIN VAN PERSIE TIMU YA KWENDA - UNITED, CITY AU JUVE?


INTERVIEW YA KWANZA YA SHINJI KAGAWA MAN UNITED: ASEMA ANAJIONA MWENYE BAHATI KUICHEZEA UNITED

TIMU YA KITUO CHA TSC MWANZA YAENDELEA KUFANYA VIZURI UJERUMANI - YATOKA SARE NA WAPINZANI WA BAYERN - 1860 MUNICH B

Kikosi cha TSC Mwanza kikijifua kabla ya pambano.
Timu U20 ya TSC Sports Academy, leo imeanza mashindano ya Inselcup, katika kundi B kwa kutoka sare ya magoli 2 kwa 2 na timu ngumu kabisa ya 1860 Munich, amboyo ni moja ya tumu bora 5 katika ligi ya vijana ya Ujerumani.
 
 Magoli ya TSC ya lifungwa na Saidi Hassan katika kipindi cha kwanza, na Tito Jonathani aliongeza bao la kuongoza katika kipindi cha pili.
 


Timu  zikiwa zimejipanga uwanjani kuanza mchezo
Katika mchezo huo 1860 Munich ndio walioanza kufunga katika kipindi cha kwanza, dk ya nne ya mchezo na baadae TSC kusawazisha katika dk ya 11 ya kipindi cha kwanza, kipindi cha pili kilipoanza TSC waliongoza bao, na baadae kusawazishwa na timu ya 1860 Munich dk 7 kabla ya mchezo kumalizika. Mchezo huo ulikuwa mgumu kabisa kwa timu zote kushambuliana zamu kwa zamu. 
Kikosi cha 1860 Munic B kikiwa jukwaani kusubiri mechi yao ianze.
Mechi nyingine ya Kundi B ilikuwa kati ya Maccabi Haifa ya Israel (Mabingwa katika logi ya vijana Israel wametoka suluhu ya 1-1 na TSG 1899 Hoffenheim, ambayo pia inacheza ligi ya vijana ujerumani.
Haya ndio makombe wanayogombania
Katika mechi nyingine za kundi A zilizofanyika katika uwanja huo huo wa Mannheim (Uliopo jimbo la Mannheim) hapa Ujerumani,
Timu wenyeji -SV Waldhof Mannheim 07 walifungwa na H.N.K Hajduk Split ya Croation Magoli 2 - 0
Pia katika kundi hilo timu ya........SPVGG 03 Ilvesheim iko katika daraja la chini kabisa ligi ya vijana Ureumani, walifungwa goli 7-0 na timu ya Karlsruher Sports Club ambayo ipo kwenye moja ya nafasi za juu katika ligi ya vijana Ujerumani.

Friday, July 20, 2012

MTAKATIFU TOM WA YANGA: MBINU ZETU NDIO SIRI YA USHINDI WETU

WASIKILIZE ATHUMANI IDD CHUJI NA KELVIN YONDANI WAKIONGELEA USHINDI DHIDI YA APR

EXCLUSIVE INTERVIEW: CANNAVARO TUMEANZA KUELEWA MBINU ZA MWALIMU - TUTATISHA ZAIDI ROBO FAINALI

CHEMSHA BONGO: TAJA JINA LA MCHEZAJI HUYU WA SPAIN

Iker Muniain dreams of how he will look in a Man Utd jersey (@D_DeGea)

THIAGO SILVA: MASHABIKI WA AC MILAN SIKUPENDA KUHAMA SAN CIRO ILINIBIDI.

Pale mchezaji ambaye mashabiki wa klabu fulani wanakuwa wana mapenzi nae makubwa na akahama basi ni kawaida sana kusikia akiitwa mroho wa fedha, na maneno mengi ya kejeli. Lakini baada ya kukamilisha uhamisho wake wa kwenda PSG pamoja na Zlatan Ibrahimovic, Thiago Silva ameamua kuweka wazi kwamba hakutaka kuhama Milan na wala hajaenda PSG kwa sababu ya fedha na utajiri wa klabu hiyo.

Silva alikaririwa na FourFourTwo akisema: "Nilikuwa na furaha kwenye uhamisho huu na nilijisikia huzuni kuondoka Milan kwa sababu nilitokea kuipenda sana klabu ile.

"Watu wananiita mroho wa fedha, ambo ambalo linanikera. Sipati fedha nyingi sana hapa PSG. Hili sio kosa langu. Ningependa kuomba samahani kwa mashabiki wa AC Milankwa kuondoka.

"Uhamisho huu ulikuwa mgumu sana kuutekeleza. Sikutaka kuondoka Milan hata familia yangu pia. Lakini lilikuwa jambo chanya kufanya kwa sababu mkurugenzi wa michezo wa PSG Leonardo na kocha Carlo Ancelotti waliniita."

LIVE MATCH CENTRE - KAGAME CUP: YANGA 2 - 0 APR - FULL TIME


DK 90: Anatoka Niyonzima anaingia Rashidi Gumbo.
DK 81: Yanga 2 - 0 APR
DK 72: Yanga  inafanya mabadiliko anaingia Jeryson Tegete anatoka Said Bahanunzi
DK 70: APR wanalisakama sana lango  Yanga na Yew Berko anafanya kazi ya ziada kuokoa michomo.
DK 67: Said Bahanuzi anafunga bao la pili hapa baada ya bekiwa APR kuteleza na kumpokonya mpira na kufunga bao la pil. Mpaka sasa ametimiza mabao manne kwenye mashindano haya.
DK 59: APR wanafanya mashambulizi makali kwenye lango la Yanga lakini Yew Berko anaokoa, na kwa bahati mbaya napata maumivu tena.
DK 57: Yanga inafanya mabadiliko, anaingia Juma Seif Kijiko anatoka Nizar Khalfan
DK 55: APR wanaonekana kubadilika kwa kipindi hiki cha pili, wanalishambulia goli la Yanga lakini wanashindwa kutumia nafasi.

DK 53: Yew Berko anagongana na mchezaji wa APR na anaonekana kuumia, ingawa baada ya kupatiwa matibabu aninuka na kuendelea kucheza.

DK 46: Kipindi cha pili kinaanza hapa uwanjani.

DK 45: Mchezo unaenda mapumziko Yanga wakiwa wanaongoza kwa 1 - 0. Kwa kifupi Yanga wamecheza vizuri sana hasa kwenye safu ya ulinzi na kiungo ndani ya dakika 45 za mchezo huu.
 
DK 43: Yanga wanapata goli lakini linakataliwa. APR wanashindwa kuweza kucheza mchezo wao uliozoeleka katika michezo yake iliyopita.

DK: 30 - Yanga 1 - 0 APR

DK 23: Said Bhanuzi anaiandikia Yanga bao la kwanza.

DK 19: Nizar Khalfan anapoteza nafasi nzuri ya kufunga bao hapa.


DK 15:  Mchezo unaonekana kuchezwa kati kati ya kiwanja sana, Yanga wakitawala eneo hilo, matokeo n 0-0.

DK 7: Yanga wanaonekana kutulia na kulishambulia lango la APR kwa dakika hizi za mwanzo mwa mchezo.

DK: 1: Mpira unaanza hapa uwanja wa taifa.

 1.Yaw Berko - 19,
2.Juma Abdul - 14,
3.Oscar Joshua - 4,
4.Nadir Haroub Cannavaro (C) - 23
5.Kelvin Yondani - 5
6.Athuman Idd Chuji - 24
7.Nizar Khalfan - 7
8.Haruna Niyonzima - 8
9.Said Bahanunzi - 11
10.Hamis Kiiza - 20
11.Stephano Mwasika - 3

Subs;
1.Ally Mustapaha 'Barthez' - 1
2.Godfrey Taita - 17
3.Juma Seif Kijiko - 13
4.Idrisa Rashid - 12
5.Rashid Gumbo - 16
6.Shamte Ally - 15
7.Jeryson Tegete - 10

Head Coach: Tom Saintfiet
Assistant Coach: Fred Felix Minziro,
Goalkeeper Coach: Mfaume Athumani
Team Physician: Dr Sufian Juma
Massagist: Jacob Onyango
Kit Manager: Mahmoud Omary (Mpogolo)

OFFICIAL: TFF YATOA UAMUZI DHIDI YA SUALA LA YONDANI - YARIDHIA AICHEZEE YANGA

Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za wachezaji (ambayo katika uamuzi huu itarejewa kama ‘Kamati’) iliyokutana Julai 17 mwaka huu, baada ya kupitia mikataba na nyaraka zote zinazohusiana na mchezaji Kevin Yondani katika kujiridhisha juu ya hadhi yake ya usajili katika mashindano ya Kombe la Kagame kama zilivyowasilishwa mbele yake imefikia uamuzi ufuatao;
1.   Kwa mujibu wa mapitio ya nyaraka zote zilizotajwa hapo juu na kufanyiwa upembuzi yakinifu, Kamati iliridhika pasi na shaka yoyote kuwa suala zima la mchezaji Kevin Yondani ni la kiutendaji, hivyo uamuzi wa Sekretarieti ya TFF kuwasiliana na Klabu ya Simba kwa suala hilo la kiutendaji  kama Sekretarieti  ilivyofanya katika barua yake ya Julai 14 mwaka huu ulikuwa sahihi.
 
2.   Kamati ilibaini kuwa Mkataba wa mchezaji Kevin Yondani na Klabu ya Simba ulimalizika Mei 31 mwaka huu. Hivyo kwa taratibu za usajili mchezaji Kevin Yondani kuanzia Juni 1 mwaka huu alikuwa ni mchezaji huru.
 
3.   Aidha Kamati ilibaini kuwa Mkataba uliowasilishwa na Klabu ya Simba TFF ukiwa na maana ya kuongeza mkataba uliokuwepo TFF baina ya mchezaji Kevin Yondani na Klabu ya Simba uliwasilishwa TFF, Juni 7 mwaka huu ambapo ni kinyume cha utaratibu wa kuongeza mikataba ya wachezaji unaozitaka klabu kuwasilisha mikataba ya kuongeza muda wa mikataba ya wachezaji wao wakati mkataba halisi haujaisha muda wake. Hivyo mkataba huo kwa jicho la kisheria haupo.
 
4.   Hata kama kamati ingeuona mkataba huo katika jicho la sheria, bado mkataba huo una tatizo la kisheria hasa katika tarehe ambazo pande mbili husika ziliingia makubaliano hayo. Ukiuangalia mkataba huo unabainisha kuwa, wakati mchezaji Kevin Yondani aliingia makubaliano Desemba 23 mwaka jana, upande wa pili wa kimkataba ambao ni Klabu ya Simba inaonekana iliingia makubaliano hayo kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wake Geofrey Nyange Kaburu, Desemba 23 mwaka huu. 
 
5.   Kisheria utata huu unaweza kuondolewa na pande husika tu kwa kurekebisha dosari hiyo kwa maridhiano kuweka saini katika mabadiliko hayo ili kuthibitisha mabadiliko hayo. Hivyo katika jicho la kisheria mkataba huo hauwezi kutumika kumzuia mchezaji huyo kwenda katika klabu anayoipenda wakati akiwa huru.
 
Kutokana na maelezo yote hapo juu, Kamati imeridhia hatua iliyochukuliwa na Sekretarieti ya TFF ya kumruhusu mchezaji Kevin Yondani kuichezea timu ya Yanga katika mashindano ya Kombe la Kagame 2012.
 

WADAU WA EPL BIG FOUR FORUM WAKUTANA JIJINI DSM.

Wadau wa Forum Ya Mashabiki wa Soka la Uingereza ijulikanayo kama EPL BIG FOUR FORUM hivi kariubuni walikutana kwa ajili ya kufahamiana.
forum hii inaundwa na wadau mbali mbali kutoka taasisi mbali mbali na Serikali na Binafsi hapa nchini .

 Wadau hawa waliamua kupimana nguvu kwa kukutanisha mashabiki wa SIMBA na Yanga kutoka katika forum hiyo siku ya Jumamosi Tarehe 14-July-12 katika viwanja vya chuo kikuu. Mtanange huo uliishia kwa Watani hao kutoshana nguvu ya Goli 3-3.

 Na baadae wadau hao waliamua kwenda maeneo ya Changanyikeni Upland Center kwa ajili ya kuendelea na Forum Day hiyo ambayo inakua inafanyika kila mwaka.






RONALDO DE LIMA, FIGO, EDGAR DAVIDS, YORKE, TOLDO, ROBERO CARLOS WAUNGANA KUCHEZA MECHI YA HISANI DHIDI YA BENFICA - ANGALIA MTANANGE HAPA


Benfica 5-1 Luis Figo Foundation highlights HD... by vik2003

PICHA YA SIKU: RIO FERDINAND AKIWA AMETOKA KUWINDA NA MZULU SOUTH AFRICA


UNAPENDA KUMSIKILIZA MBWIGA MBWIGUKE - ANGALIA VIDEO ZAKE 5 AKIWA KWENYE TOUR BUS

Hapa tulikuwa safarini kuelekea Mbeya kwenye Serengeti Fiesta Bonanza 2012. Tukiwa kwenye tour bus yetu Mbwiga akawa anatupa tupa raha kwa story zake.

BAADA YA KUIFUNGA YANGA 2-0: KOCHA WA ATLETICO ASEMA URA PEKEE NDIO INAYOMTISHA KWENYE KAGAME

Baada ya jana kukuletea mahojiano mafupi na kocha wa APR, leo hii nakuletea interview yangu niliyofanya na kocha wa klabu ya Atletico ya Burundi ambayo leo hii imeifunga Wau Salaam goli 5-0.
 
 Atletico - Kaze Cedric
 
Swali: Nini malengo yako katika mashindano haya?
Jibu: Malengo ni kuonyesha ushindani na tukifanikiwa tufike hatua ya fainali na kubeba kombe, na naamini hilo ndio lengo kuu la kila timu kwenye mashindano.
 
Swali: Baada ya mechi ulizoziona, unazungumziaje viwango vya timu nyingine?
Jibu: Viwango vya timu zote zina ufanano hazizidiani sana.
 
Swali: Timu gani unakuumiza kichwa na kwanini?
Jibu: Nafiki ni ile ya Uganda (URA) kwa sababu ina wachezaji wazuri pia wanaonekana wamezoeana sana kiasi cha kwamba wanacheza mpira mzuri sana tena wa  ushindani.
 
Swali: Wewe ni kocha mzalendo na timu yako ni moja ya zilizoonyesha ushindani hata kuzizidi zile zinazofundishwa na wazungu kutoka nje, nini siri ya mafanikio yako?
Jibu: Mafanikio yangu ni wachezaji wenyewe kusikiliza ninachowaagiza kwa kucheza kwa mujibu wa mbinu zetu. Tunafanikiwa kwa sababu ni timu ambayo niko nao kwa kipindi kirefu sasa ni mwaka wa nne tuko pamoja na kadri siku zinavyozidi kwenda kunakuwa na mabadiliko kimaendeleo. Ujuzi wa kocha ni kuaminiwa tu atakapoaminiwa atafanya kazi nzuri, tatizo la klabu
hizo zinazochukua makocha kutoka nje ya nchi tatizo lao hawawaamini wazalendo wakati si sawa, waamini tu kocha mzalendo anaweza kufanya mambo makubwa zaidi wageni.
Kosa lingine wageni hawawajulii wachezaji wetu vitu wanavyohitaji.
 
Swali: Fomesheni gani unapenda kutumia?
Jibu: Napenda kutumia 4-4-2 na mara nyingine ni 4-3-3.

MECKY MEXIME KOCHA MKUU MPYA WA MTIBWA SUGAR

Baada ya kuiwezesha timu ya mkoa wa Mororgoro kubeba taji lake la kwanza la mashindano ya Copa Coca Cola, leo hii mchezaji wa zamani Mtibwa Sugar na nahodha wa Taifa Stars aliyepita kabla ya Nsajigwa - Mecky Mexime ameteuliwa rasmi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Manungu Turiani - Mtibwa Sugar.


Mecky Mexime ambaye mara baada ya kustaafu soka miaka kadhaa iliyopita alipata kibarua kwenye benchi la ufundi la Mtibwa kama kocha msaidizi - mapema mwezi huu aliiongoza timu ya mkaoa wa Moro kuwa mbabe wa mikoa yote ya Tanzania kwa kuchukua ubingwa Copa Coca Cola na matokeo yake uongozi wa mabingwa wa zamani wa Tanzania bara umeamua kumpa ajir kamili ya ukocha mkuu wa timu yao ambayo kwa misimu ya hivi karibuni imeonekana kutofanya vizuri kwenye michuano mbalimbali inayoshiriki.

MPINZANI WA SEPP BLATTER FIFA - BIN HAMMAM ASHINDA RUFAA YA KUFUNGIWA MAISHA

Mgombea wa zamani wa nafasi ya uraisi wa FIFA Mohamed bin Hammam ameshinda kesi yake iliyomfanya aadhibiwe kufungiwa kujihusisha na soka maisha kutokana kutuhumiwa kutoa rushwa kwa wapiga kura wakati akikabiliana na Sepp Blatter.

Uamuzi huu utakuwa sio mzuri kwa Blatter, ambaye kwa sasa anakabiliana na vita kubwa ya rushwa kwenye soka huku akitaka kulimaliza tatioz hilo na kujipa sura safi mbele ya wapenda soka ulimwenguni.

Kwa bahati nzuri sasa kwa raisi huyo wa FIFA, Bin Hammam sasa amesimamishwa na shirikisho la soka barani A    sia - hivyo uwezekano wa kupishana na Blatter kwenye korido za FIFA itabidi kusubiri.

Habari nzuri kwa FIFA ni kwamba wakati wa usikilizwaji wa kesi ya Bin Hamman huko CAS - hakuonekana kutokuwa na makosa ju ya tuhuma za kutoa kiasi cha $40,000, ambazo zilichukuliwa na mjumbe wa kamati kuu ya FIFA Jack Warner ili kupeleka kwa wajumbe wa Caribbean Football Union.

Kwenye kesi ya CAS wajumbe watatu walipiga kura na zikipatikana 2-1, huku 2 zikiwa upande wa utetezi wa Bin Hammam kwa madai kwamba hakuna uthibitish kwamba zile fedha zilitoka kwa Hammam, hivyo kwa maana hiyo raia huyo wa Qatar anaweza asiwe amekiuka sheria za maadili ya kuweza kuongoza chombo cha kuongoza soka.

Kufuatia maamuzi ya CAS, FIFA wametoa taarifa haraka kutoa ahadi kwamba watafungua uchunguzi mpya dhidi ya Bin Hammam. Wakisisitiza "Mohamed Bin Hammam bado hajasafishwa - hajaonekana hana kosa." FIFA wamehaidi kutoa vielelezo vyote na mafaili ya kesi ya Bin Hammam kwa kamati mpya inayosimamia maadili, kuamua kama kuna hatua yoyote kinahitajika kuchukuliwa dhidi ya Bin Hammam.

Thursday, July 19, 2012

HII KALI: EMMANUEL OKWI ANATOKA KIMAPENZI NA SINTAH?????

Baada ya kufanikiwa kuiwezesha Simba SC kunyakua ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania, striker mwenye kutupia jersey namba 25 yaonekana  sasa yuko in love with Sintah who used to be Juma Nature's girlfriend.

 Kwa taarifa yako ni kuwa penzi la Emanuel Okwi na Christine John "Sinta" who proclamed herself as JLO wa Bongo liko wazi wazi hakuna cha kuficha even followers wa twosome hawa kwenye Twitter knows bout this.


 "OMG!  nani kawaambieni uwa mie na-date na Sintah? she use to be my close friend toka akisoma nchini kwetu UG, but is there any problem kama nikiwa na mahusiano ya kimapenzi nae?" aliuliza Okwi ambaye kwa sasa yupo Austria baada ya kutwangiwa phone na Mwandishi wa Baabkubwa.


 Lakini side B kwa Sintah ambaye kwa sasa ni co-host wa show iitwayo "Hatua Tatu" alongside Steve Nyerere at Times FM  ilikuwa hivi, "Jamani Okwi ni mshakaji wangu wa karibu, nilikuwa karibu nae toka na-xul Uganda but tukapotezana baada ya yeye kwenda kucheza Rwanda ambapo hivi majuzi  mwenyewe ndio kanitafuta akitaka kunijulia hali"- alitok Sintah.
 Haikupita dakika kadhaa, Sintah called back asking about alichokisema Okwi, "Jamani simniambie amesemaje nifurahi jamani, niambieni kama kasema ananipenda au kama kanikana jamani?"
 Okwi uko tayari kutunga nyimbo kama alivyofanya Nature?


Source:www.baabkubwamagazine.com

 

MKOSI KWA SIMBA: AMIR MAFTAH KUIKOSA KAGAME - AVUNJIKA


BEKI wa pembeni wa Simba, Amir Maftar ameondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo kinachoshiriki michuano ya kombe la Kagame inayoendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Maftar ameondolewa kwenye kikosi hicho baada ya kidole chake cha mkono wake wa kulia kuvunjika, kwenye mechi dhidi ya Ports iliyochezwa jana saa 10: 00 jioni iliyomalizika kwa Simba kushinda mabao 3-0.

Kwa mujibu wa Daktari Mkuu wa timu hiyo, Cosmas Kapinga amesema kufuatia majeraha hayo aliyopata amevishwa P.OP kutokana na maumivu aliyoyapata katika kipindi cha pili cha mchezo huo.

Daktari huyo amesema, huenda akizikosa mechi zote zinazofuata za michuano hiyo inayoendelea, timu ikifuzu hatua ya robo ya fainali kwa ushindi huo walioupata .

“Maftar tumemuondoa kwenye kikosini, baada ya kupata majeraha ya kidole chake cha mkono wake wa kulia kuvunjika na kusababisha avishwe P.O.P, aliumia katika mechi na Ports tuliyocheza jana,” alisema Kapinga

JAIRZINHO WA SASA NA UBUNIFU WA CRISTIANO RONALDO? NI KITU GANI LUCAS MOURA ATALETA KWENYE KIKOSI CHA MANCHESTER UNITED

Jumanne jioni klabu ya Sao Paulo ilitangaza imekataa ofa mpya ya tatu kutoka kwa Manchester United kwa ajili ya kumsaini kiungo mshambuliaji Lucas Moura.

Ofa hizo tatu zimekuja kwenye kipindi cha wiki na kuona namna ambavyo United wamekuwa wakimhitaji kinda hilo la kibrazili kwa kutoka kutoa ofa ya €25 mpaka €38 million.

Inaaminika Sao Paulo wanaweza kukubali ada ya uhamisho ambayo itawapatia wao kiasi cha €35 million, watakayopipata katika malipo ya jumla ya mchezaji ambaye wanamiliki asilimia 80% ya haki zakeza kibiashara, kwa maana hiyo ili mchezaji apate asilimia 20 zake kutokana na malipo ya kusajiliwa kwake itabidi United walipe kiasi cha €44 million.

Siku ya Jumanne kuna taarifa zilitoka tena nchini Brazili, zikiripoti kwamba maofisa wa klabu ya Sao tayari wameshaikubali ofa ya United, lakini huku Inter Milan wakiwa nao wapo kwenye mchakato wa kumtaka, raisi wa klabu ya Sao Paulo anajaribu kucheza kamari kuona kama timu hizo mbili za ulaya zitaendelea kumpandia dau kinda lake.

Lakini muda unazidi kwenda.

Mwezi ujao, Sao Paulo watapoteza asilimia 10 kwenye haki za kibiashara za Lucas Moura, hivyo kubakiwa na 70% na kumi zikienda kwa mchezaji mwenyewe hivyo kufikisha 30% kwa mujibu wa mkataba wao.

Ikiwa dili linatakiwa kukamilika then inabidi limalizike mwanzoni mwa August.

Lucas, kwa upande wake ametulia na yupo comfortable pale Morumbi, ambapo anapata £10,000 kwa wiki kwa mazingira ya Brazil.

Kuhamia England au Italy kutamuongezea malipo makubwa bila shaka, lakini mpaka leo bado hajatoa tamko la kutaka kuhamia popote.

Fedha za udhamini na nyingine wanazopata kwenye matangazo ya Televison zinamaanisha Sao Paulo hawapo kwenye uharaka wa kumuuza Moura.

Kama Moura ataendelea kubaki Brazil, kwa hakika ataendelea vizuri na kuhakikisha anapata malipo mara tatu zaidi ya anachokipata sasa baada ya kusaini mkataba mpya na klabu yake.

Kinda la Santos Neymar, kwa mfano, analipwa £90,000 kwa wiki - mshara mkubwa sana kwa kinda la miaka 20 kwa viwango vya ligi yoyote.

Vijana makinda wa kibrazil kwa sasa hawana tena mshawasha wa kuhitaji kwenda kucheza ulaya wakiwa na umri mdogo kwa maana ya kutaka fedha zaidi.

Lucas, kwa bahati nzuri atacheza mechi moja pale Old Trafford pale Brazil itakapokutana na Belarus kwenye mchezo wa group C tarehe 29 mwezi huu kwenye Olympic.

Lakini ili kuweza kuwa na uhakika wa kuendelea kucheza kwenye uwanja huo Lucas itabidi aombe aidha United waongeze ofa kwa mara nyingine tena au Sao Paulo wapunguze bei yake.

Ikiwa United watafanikiwa kumnasa Lucas Moura watakuwa wamejipatia mshambuliaji ambaye anaweza kucheza popote kwenye eneo la ushambuliaji.

Mchezaji aliyekamilika akiwa na nguvu, ujuzi na kasi - ni mchezaji anayeweza kuitingisha ngome yoyote ya ulinzi kwa uwezo na kasi aliyonayo.

Huku akiwa amesememwa ya kuwa na tabia ya ubinfsi kipindi cha nyuma kwa kumiliki sana mpira mwenyewe na kushindwa kuwalisha wachezaji wenzie, lakini pia ana uwezo wa binafsi ambao United wamekuwa wakiukosa tangu kuondoka kwa Cristiano Ronaldo mwaka 2009.

Lucas anaweza kucheza kwa kwenye nafasi yoyote kati ya hizi tatu kwa mfumo wa 4-2-3-1 au kucheza upande wa pembeni kulia kwa mfumo wa 4-3-3.

Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakijaribu kumfananisha na Hulk au Pato, lakini wachambuzi wengi wa soka nchini Brazil wanasema mtu sahihi wa kumfananisha nae ni mbrazili mwenzie Gwiji Jairzinho.

Akiwa anafanana na mshindi wa kombe la dunia 1970 kwa mwili na staili ya kucheza, Lucas pia anavaa namba aliyokuwa akivaa Jairzinho (namba 7) kwenye timu ya taifa.

Sasa muangalie Lucas akiwa dimbani.

GOLI LA SIKU: THIERRY HENRY BADO NOMA - ATUMA SALAAM KWA WAPINZANI

PICS OF THE DAY: BAADA YA KUNYAKUA EURO 2012: SASA XABI ALONSO AFUATA MKUMBO WA AKINA RONALDO ALA BATA NA FAMILIA YAKE

Mchezaji wa Real Madrid Xabi Alonso akiwa na mkewe Nagore Aramburu huku mtoto wao wa kike akiwa anacheza wakati wakiwa kwenye matembezi huku Spain.

Xabi Alonso, mkewe na watoto wawo wawili.


Carry me home: the footballer held his daughter Ane in his armsCarry me home: the footballer held his daughter Ane in his arms