Search This Blog

Saturday, July 27, 2013

LIVE SCORE: UGANDA 3 - 1 TANZANIA (TAIFA STARS) FULL TIME




Mpira umemalizika Uganda 3-1 Tanzania. Jumala 4-1

David Luhende ametoka .. Vicent Barnbas

Ivan Ntege ndio mfungaji bao la tatu la The Cranes.

Uganda wanaongeza bao la tatu.

Uganda wanazidi kutawala mchezo jambo ambalo linaweza likawa tatizo kwa Tanzania.

Brian Majwega ndio mfungaji wa bao la Uganda.
Uganda wanapata bao la pili. Dakika ya 3 kipindi cha pili.

Uganda wanapata penati baada ya mchezaji wa Stars kushika mpira ndani ya boksi

Kipindi cha pili kimeanza.

Mpira mapumziko - Uganda 1-1 Tanzania

Frank Domayo anaumia anaingia Simon Msuva.

Zimeongezwa dakika mbili za nyongeza. 

Dakika ya 45 kipindi cha kwanza matokeo bado yanasoma 1-1.

Wafungaji wa mabao ni Kalanda Frank upande wa Uganda na Amri Kiemba upande wa Tanzania.

THOMAS MASHALI AWAFANANISHA MADA MAUGO NA KALAMA NYILAWILA KAMA MIDOLI WAKE

Bondia Thomas Mashali akionesha midoli yake anayoifananisha na mabondia wenzake, Kalama Nyilawila (kushoto) na Mada Maugo, wakati wa mazoezi yake yanayoendelea katika gym yake iliyopo Manzese, Dar es Salaam 
 
Bondia Thomas Mashal


BONDIA Thomas Mashali amewafananisha mabondia wenzake, Mada Maugo na Kalama Nyilawila kama midoli kwa kuwakebehi kuwa hawana lolote.

Hatua hiyo ya Mashali inatokana na awali kupondwa na Maugo kuwa hana uwezo na ni heri akageukia biashara ya kuuza chapati, wakati Kalama akimkebehi kuwa ni kibonde wake.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili katika gym yake, Manzese, Dar es Salaam jana, Mashali alisema mabondia hao hawana uwezo wa kupambana naye kwa sasa na ni kama midoli kwake.

Mashali, ambaye atapanda ulingoni Oktoba 30 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee kuzichapa na Maugo, yuko katika mazoezi makali kwa ajili ya pambano hilo kabla ya baadaye kupigana na Nyilawila.

"Unajua hawa ni kama midoli kwangu (huku akionesha midoli aliyoshika), na kwa kudhihirisha hilo nitaanza na maugo Oktoba 30 kumuonesha kuwa hatakiwi kuzungumza asichokijua," alisema Mashali.

Alisema anaamini uwezo wake wa sasa utakuwa wa juu zaidi ya Maugo na Nyilawila, ambapo alipata sare alipopigana na Nyilawila.

Katika pambano hilo la Mashali na Maugo la Oktoba 30, kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi, ambapo Ibrahim Class 'King Class Mawe' atapanda ulingoni kupambana na Halid Manje katika mchezo wa raundi sita.

Siku hiyo kutakuwa na uhuzwaji wa DVD mpya kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa masumbwi zitakazokuwa zikisabazwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'


DVD hizo mpya ni kati ya

mike tyson vs evander holyfield na felix trinidad vs roy jones jr
Felix 'Tito' Trinidad vs Pernell Whitaker

Dvd hizo zilizo rekodiwa kwa ubora wa hali ya juu kwa ajili ya kutoa mafunzo ya mchezo wa masumbwi nchini



Bondia Thomas Mashali akionesha midoli yake anayoifananisha na mabondia wenzake, Kalama Nyilawila (kushoto) na Mada Maugo, wakati wa mazoezi yake yanayoendelea katika gym yake iliyopo Manzese, Dar es Salaam picha na BLOG YA SUPA D

HARUNA CHANONGO - SINA AKAUNTI FACEBOOK - ANAYETUMIA JINA LANGU KWENYE MTANDAO HUO NI FEKI

Winga wa timu ya taifa ya Tanzania anayekipiga klabu ya Simba Haruna Chanongo amasema amesikitshwa mno na kitendo cha mtu asiyefahamika kutumia jina lake na picha kwenye mtandao wa Facebook.

Akizungumza na mtandao huu kutoka Kampala alipo na timu ya taifa ya Tanzania inayojiandaa kucheza mechi ya pili kuwania nafasi ya kucheza kombe la CHAN, amesema yeye binafsi hana akaunti kwenye mtandao wa kijamii wa FACEBOOK lakini anashangaa amekuwa akipokea malalamiko kutoka kwa watu wa karibu kuhusu suala la akaunti hiyo.

"Kiukweli mie sina akaunti Facebook, sasa nashangaa muda mwingine napata malalamiko kutoka kwa watu wangu wa karibu na hata mashabiki kuhusu mambo ya ajabu huyo aliyofungua hiyo akaunti anayafanya. Ninachotaka kuweka wazi mie sina akaunti Facebook hivyo watu wote wafahamu kuhusu hilo," alimaliza Chanango amepa kwamba leo akipata nafasi atajitahidi kwa hali na mali kuiwezesha Tanzania kufuzu.


FAKE ACCOUNT

MAKALA: WAYNE ROONEY HANA WA KUMLAUMU KWA YANAYOMTOKEA - ANAONJA UTAMU WA DAWA ZAKE MWENYEWE

Wayne Rooney's testy relationship with now-retired manager Sir Alex Ferguson contributed to Rooney wanting to leave Manchester United in 2010.

Umetaarisha kitanda chako, sasa inabidi ukilalie. Kinachoenda huwa kina tabia ya kurudi. Unaishi kwa upanga utakufa kwa upanga. Unavuna ulichopanda. Vyovyote unavyoweza kuyasema maneno haya, hili suala la Wayne Rooney 'kuwa na hasira na kuachnganyikiwa' kuhusu nafasi yake ndani ya Manchester United -- ni jambo ambalo amejitakia mwenyewe.

Baadhi ya wachambuzi wa soka wamekuwa wakisema kwamba lilianza katika wiki za mwisho za utawala wa Sir Alex Ferguson kama kocha wa United, alipomuacha Rooney nje kwenye mechi za Champions League dhidi ya Real Madrid, na baada ya wiki kadhaa mchezaji akaomba kuuzwa kwa mujibu wa Fergie. Lakini hatua hii ni mojawapo baada ya sakata la Rooney kuomba kuondoka mwaka 2010 akitishia kwenda Manchester City ---jambo lilopelekea matusi mengi kuelekezwa kwake wakati akiwa bado ameomba kuondoka -- lakini hatimaye akaamua kubaki baada ya kupewa mkataba mpya mnono wa miaka mitano. '

Tangazo la Rooney mwishoni mwa mwaka 2010 halikutokea ghafla tu: yeye na Ferguson walianza kuzozana kuhusu majeruhi ya enka. Baada ya muda kidogo kabla ya mzozo huo wa majeruhi ya Rooney, ikatoka taarifa kwamba mshambuliaji huyo ameomba kuhama, alitoa taarifa rasmi akisema kwamba alikutana na klabu kuhusu mkataba wake mpya, na alitaka uhakika kuhusu uwezo wa klabu kuvutia wachezaji wakubwa duniani - jambo ambalo aliliona ni gumu kwa klabu kulifanikisha. 
'UNITED HAINA UWEZO WA KUFIKIA MATAMANIO YANGU',  vichwa vya habari vya magazeti na mitandao ya viliandika siku iliyofuata. City walisema walikuwa wanafuatilia kwa ukaribu sakata hilo la Rooney na United; kundi la mashabiki wenye hasira lilikusanyika nje ya nyumba ya Rooney kumtolea vitisho vya kumuua endapo angahamia upande wa pili wa mji wa Manchester.

Hiyo ilikuwa kati kati ya wiki. Ijumaa iliyofuatia Rooney akasaini mkataba mpya, akitoa sababu kwamba United walimhakikishia kwamba wana uwezo wa kuendelea kushindana kwenye hatua ya juu kabisa. "Siku zote wasiwasi wangu ulikuwa ni kuhusu siku za mbeleni. Katika siku kadhaa zilizopita, nimeongea na kocha na wamiliki ..... ninasaini mkataba mpya nikiwa naamini kabisa kwamba utawala, benchi la ufundi na bodi pamoja na wamiliki watahakikisha United inaendelea kuimarisha historia yao nzuri ya ushindi."

Pia wakawa wameongeza mara mbili mshahara wake. Toka wakati huo Ferguson hakuwa na mahusiano ya karibu mno na mchezaji husika; alikuwa kama mzee ambaye amelipwa mafao yake ya uzeeni, halafu akatokea kijana ambaye alimuonyesha paa lake limechakaa likiwa kwenye hali mbaya, lakini akamwambia angemsaidia kulitengeneza kwa kiasi cha fedha chote alicholipwa kwenye mafao yake.

Labda Ferguson aliamua tu kujishusha na kuweka mambo sawa: Rooney alikuwa kwenye kiwango bora kabisa msimu wa 2009-10, akifunga mabao 34 na kutajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa wachezaji wa EPL.  Pamoja na tabia yake ya kuweka mbele klabu ya mtu yoyote, Ferguson amekuwa akiwapa nafasi kubwa wachezaji, pale anapohisi mchango wao uwanjani una faida kwa timu. Hali hiyo ilibidi iendelee baada ya Fergie kukubali ushauri wa Rooney kwamba inabidi kuhakikisha klabu inasajili wachezaji wakubwa wataohakikisha timu inaendelea kuwa juu.

Msimu mmoja baadae baada ya Manchester City kushinda ubingwa mbele ya United kwa tofauti ya mabao msimu wa 2011-12, Ferguson akampa Rooney alichokuwa anakitaka - uhakika wa kufanya vizuri kwa kumsaini Robin van Persie, mmiliki wa kiatu cha dhahabu cha EPL na mchezaji bora wa ligi msimu huo, akitokea Arsenal. Aina ya mshambuliaji ambaye Rooney alikuwa anamtaka ndani yake. Van Persiealifunga mabao manne katika mechi zake tatu za kwanza za United, na kutoa ishara kwamba makubwa zaidi yanakuja. Mabao yake, Ferguson alisema ndio yaliyorudisha kombe Old Trafford.

Usajili wa Shinji Kagawa nao ukaongeza uhakika anaoutaka Rooney. Mjapan huyu alipokuwa akicheza, alikuwa akichezeshwa alikuwa akionyesha kwamba anaweza kucheza namba 10 - jukumu ambalo Rooney alikuwa amepewa baada ya ujio wa Van Persie. 

Rooney huwa anaamika hakuwa amependa kucheza kwenye kiungo aliporudishwa; United wanaona wana watu au mtu wa kuziba nafasi yake katika namna ambayo hawakuwa na uwezo huo mwaka 2010 alipoomba kuondoka. Ikiwa United wataweza kumsajli  Cesc Fabregas kutoka Barcelona, hali ya ulazima wa kuwa na Rooney itazidi kupungua. 

Wakiwa tayari wameshakataa ofa ya $30.5 million kutoka kwa Chelsea, United wanasisitiza Rooney hauzwi. Huku Moyes akisema kwamba atamhitaji Rooney endapo Van Persie atakuwa majeruhi kwa maana ya nafasi ya ushambuliaji. Kwenye kiungo akiwa anataka kuongeza watu wengine wawili tena akitaka kwa kuwanunua kwa bei mbaya ina maana wanakuja kuingia moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza.

Sasa Je Rooney ana hasira na amechanganyikiwa kwa kugundua kwamba hana namba ya kdumu kama zamani au kauli za kocha wake mpya kwamba atamhitaji kama spea tairi kwa RobinVan Persie?
  
Je Rooney ana hasira na kuchanganyikiwa kwa sababu hizo? Au ameshikwa nayvu za mtego alioutengeneza mwenyewe?

Wayne Rooney hana wa kumlaumu kuhusu hili zaidi yake ya mwenyewe.



Friday, July 26, 2013

KALI YA LEO: ANGALIA WACHEZAJI WA MAN CITY WAKIJIFUNZA NAMNA YA KUJIRUSHA UWANJANI

RUSHWA: VIONGOZI WA SHIRIKISHO LA SOKA LA KENYA HATARINI KWENDA JELA KWA KUTAFUNA MAMILIONI YA FEDHA


Wakuu wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Kenya FKF, wanachunguzwa na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi kuhusiana na madai ya kutoweka kwa mamia ya maelfu ya dola pesa za shirikisha hilo.

Kwa mujibu wa maafisa hao, fedha zilizo zilitolewa na shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA na mashirika mengine.

Afisa mkuu wa uhusiano mwema wa tume hiyo, Yasin Ayila, amesema, tume hiyo imepokea malalamishi kuwa maafisa hao wametumia vibaya zaidi ya dola laki nne, mali ya FKF.

''Tumepata habari zote kuhusiana na akaunti na kila kitu kitachunguzwa, ili ni pamoja na stakabathi zote za benki, akaunti zote za FKF'' amesema afisa huyo.

Kiongozi wa FKF kutoka mkoa wa Pwani, Hussein Terry, amewasilisha stakabadhi za benki ambazo aliziwasilisha kwa tume hiyo, waziri wa michezo Hassan Wario, shirikisha la mchezo wa soka duniani FIFA na shirikisho la mchezo huo barani Afrika Caf.

Terry aliambatana na afisa mwingine wa FKF kutoka mkoa wa Nyanza Tom Alila, na naibu mwenyekiti wa FKF Sammy Sholei.

Shole pamoja na Alila wamesimamishwa kazi na FKF kwa madai ya kushutumu uongozi wa FKF madai ambayo wameyakanusha.

Watatu hao wanadai kuwa FKF ilipokea dola elfu mia nne na kumi kupitia akaunti yake na kwa sasa hayajumuishwa kwenye hesabu rasmi ya shirikisho hilo.

Mwenyekiti wa FKF, Sam Nyamweya amekanusha madai hayo akisema kuwa stakabadhi hizo ni bandia na kusema kuwa maafisa wa FKF ambao wanaidhini ya kushughulika na masuala ya fedha ndio watakaopewa stakabadhi kuhusu fedha zake.

Nyamweya amesema akaunti waliowasilisha kwa tume hiyo sio yao na kuwa tayari wamewasiliana na benki yao kuhusiana na suala hilo.

AZAM TV YALIPA BILLIONI 6.5 ILI KUONYESHA MECHI ZA LIGI KUU YA TANZANIA BARA


Badhi ya viongozi wa TFF wakisaini mikataba na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam, Said Mohammed (wa kwanza kulia) leo kwenye Ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam.
Televisheni ya Azam inayojulikana kama Azam TV imeingia mkataba wa miaka mitatu wa kuonesha michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambapo mkataba huo umetajwa kuwa na thamani ya Tsh bilioni 6.5
Aidha Televisheni hiyo itakuwa na majukumu ya kuonesha mechi za moja kwa moja (LIVE) zisizopungua 60 za Ligi hiyo huku nyingine 180 zikiwa zimerekodiwa.

SOURCE: GLOBAL PUBLISHER

KOCHA MPYA WA BARCELONA AWAAMBIA MAN UNITED - 'NITAIKATAA OFA MPYA YA UNITED KUMNUNUA FABREGAS"

Gerardo Martino amemwambia David Moyes kwamba Cesc Fabregas hauzwi baada ya kutambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa klabu ya FC Barcelona kwa mkataba wa miaka miwili.

Kocha huyo wa zamani wa Newell's Old Boys amerithi mikoba ya Tito Vilanova, ambaye alilazimika kujiuzulu kutokana matatizo yake ya kiafya.

Akiongea kwenye mkutano wa waandishi wa habari leo Ijumaa, Martino alisema: 'Man United inamtaka Cesc? Kama klabu ilikataa ofa mbili za kwanza, mie nitaikataa ya tatu. Cesc atabaki hapa.'

Makamu wa Raisi wa Barca Josep Maria Bartomeu amethibitisha maneno ya Martino, akiongeza: 'Ni kawaida United kuvutiwa na mchezaji, lakini tunamtegemea Cesc na hatutomuuza, haijalishi watatoa ofa ya kiasi gani.'


HIKI NDIO KINYWAJI RASMI CHA FC BARCELONA NDANI YA BARA LA AFRIKA - WAMPA RAISI KIKWETE JEZI YA NEYMAR

Kushilla Thomas, Mkurugenzi wa Masoko wa Tanzania Breweries Limited (TBL) nje ya ofisi za FC Barcelona huko Catalonia Hispania leo hii baada ya kutangazwa kwa udhamini wa Castle Lager kwa Barcelona.
Bia ya Castle Lager imeingia makubaliano ya kuidhamini moja ya klabu maarufu zaidi duniani ya FC Barcelona ya Hispania kwa kipindi cha miaka mitatu udhamini utakaokifanya kinywaji hicho kuwa bia rasmi ya FC Barcelona barani Afrika. 
Klabu ya FC Barcelona pia imempa zawadi ya Raisi Jakaya Kikwete kwa kutambua mchango wake kwenye maendeleo ya soka nchini
Ushirikiano huu, uliyosainiwa kwenye uwanja wa klabu Camp Nou, unaifanya CASTLE Lager kuwa bia rasmi itakayotumika kwa shughuli yoyote ambayo Barcelona itashiriki kwenye bara la Afrika na pia itafungua milango kwa mashabiki wa Barcelona Afrika kuwa karibu na wachezaji wa Barcelona, vifaa, na kumbukumbu. Pia kupata nafasi ya kusafiri kwenda Hispania kushuhudia kwa karibu timu ya Barcelona. 

Mkataba huu utakuwa maalum kwa ajili ya CASTLE Lager kwenye nchi nyingi za Afrika isipokuwa kwa baadhi ya nchi chache zilizochaguliwa ambapo itatumika Castle Milk Stout.
Hii ni mara ya kwanza kwa timu ya FC Barcelona kusaini mkataba wa udhamini na kampuni ya bara la Afrika. Kushirikiana na bia bingwa Afrika litaongeza kwa haraka umaarufu wa timu ya FC Barcelona ndani ya bara la Afrika na kufungua milango kwa mashabiki wa klabu hii kupata bidhaa mbalimbali za Barcelona na nafasi za kushinda safari ya kwenda Barcelona kuitembelea klabu hiyo. 
Wawakilishi wa SABMiller kutoka nchi mbalimbali barani Afrika wakiwa nje ya ofisi ya FC Barcelona uko Catalonia Hispania leo hii

“Tumefurahi sana kuingia katika ushirikiano na Castle Lager na Castle Milk Stout, chapa zinayofahamika dunia nzima . Tunafanana na Castle kwa kuwa sote tuna historia ya zaidi ya miaka 100 na utamaduni uliotukuka. Na sote tuna mapenzi na mpira wa miguu pamoja na mashabiki wake katika soko muhimu kama Afrika,” alisema Javier Faus, Makamu wa Rais wa FC Barcelona anayeshughulikia masuala ya uchumi.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, Kushilla Thomas akimkabidhi zawadi ya asili kutoka Tanzania Bw. Javier Faus, Makamu wa Rais wa FC Barcelona anayeshughulikia uchumi huko Catalonia Hispania leo hii baada ya kutangazwa kwa udhamini wa Castle Lager kwa Barcelona.

 “Uamuzi wa Barcelona kuingia ushirika na na bia inayoongoza barani Afrika kutaongeza umaarufu wa bia hiyo kwenye bara hili na kuwawezesha wachezaji wa timu hiyo kufika maeneo amabyo hawajawahi kufika barani Afrika,” alisema David  Carruthers Mkurugenzi wa Masoko wa SabMiller Afrika (kampuni mama ya TBL).
CASTLE Lager si bidhaa mpya kwenye udhamini wa mpira wa miguu na vyama, ina miaka mingi ya kujihusisha katika soka barani Afrika kwa kipindi cha miaka 85 kupitia ligi mbalimbali za nchi tofauti kama vile Zimbabwe, Swaziland, Botswana, Lesotho na pia mashindano ya kanda kama COSAFA Kusini mwa Afrika na CECAFA Afrika Mashariki.
Kutokana na soka la Ulaya kupata umaarufu mkubwa na mashabiki wengi barani Afrika, Castle Lager imekuwa ikidhamini urushaji wa matangazo ya ligi hizo kwenye televisheni barani Afrikana kuwapa mashabiki fursa ya kufatilia kila kinachoendelea kwenye ligi hizo maarufu duniani ambazo ni Ligi Kuu ya Ulaya, Ligi Kuu ya Uingereza na La Liga ya Kihispania.

Kufuatia udhamini huu, wanywaji wa Castle Lager na Castle Milk Stout pamoja na mashabiki wa Barcelona barani Afrika sasa watarajie mambo mengi ya kusisimua katika ulimwengu wa soka.

PHOTOS: TAIFA STARS WAKIWA MAZOEZINI MANDELA NATIONAL STADIUM (NAMBOOLE) TAYARI KUIKABILI UGANDA

















KIUNGO WA AZAM HUMPHREY MIENO ATAJWA KWENDA KUZIBA NAFASI YA WANYAMA CELTIC


Victor Wanyama ameondoka Celtic Football Club na kujiunga na klabu inayoshiriki kwenye ligi kuu ya England - Southampto baada ya kukamilisha uhamisho wa wa £12.5million. Sasa ikiwa ni wiki kadhaa tangu kiungo huyo wa Kenya kuondoka, kocha wa Celtic Neil Lennon, amesema Wanyama alikuwa ndio kiungo wake bora wa ushambuliaji kwenye timu yake na sasa wanahitaji mbadala wake.
Kutokana na hilo sasa zimeibuka taarifa kwamba kocha huyo ambaye ni nahodha wa zamani wa Celtic anamuwania kiungo mwingine kutoka Kenya Humphrey Mieno. Mieno ambaye kwa sasa ni mchezaji wa Azam FC  inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Tanzania.
Celtic, itabidi ifanye haraka kumsaini mchezaji huyo wa Azam FC kwa kuwa kuna vilabu vingi barani Afrika kama miamba ya soka ya Tunisia Esperance na Club Africain zinamuwania kwa nguvu mchezaji huyo ambaye alihamia Azam akitokea Sofapaka ya Kenya.
Mpaka sasa sio Celtic wala Azam FC ambazo zimethibitisha kuhusu taarifa hizi.

VIDEO: BARCELONA WAMKOSA MRITHI WA LIONEL MESSI KWA KUKATAA KULIPA GHARAMA ZA KUWAHAMISHA WAZAZI WA MCHEZAJI SPAIN


Kupewa nafasi ya kwenda kujiunga na chuo cha soka kinachoongoza duniani kwa kutoa wachezaji bora La Masia cha Barcelona, ni jambo kubwa sana kwa mcheza soka. 
Huku watoto wengi wacheza soka wakiwa na ndoto za kujiunga na chuo hicho kilichozalisha vipaji kama cha Lionel Messi na Andres Iniesta, mtoto wa miaka 12 Cassiano Bouzon amekataa nafasi hiyo adimu ya kujiunga na kituo hicho cha soka na kuamua kujiunga  Flamengo ya nchini kwake Brazil.

Cassiano amepata kufahamika kimataifa akiitwa jina la  the "Next Lionel Messi"  baada ya vipande vya video zake kupata umaarufu mkubwa kwenye mtandao wa Youtube huku kukiwa na taarifa kwamba alipewa nafasi ya kufanya majaribio La Masia kwa wiki tatu
Lakini kwa mujibu wa wa Globoesporte, Barcelona hawakumpa ofa ya kulipia gharama za yeye kuhamia jijini Barcelona kwa pamoja na wazazi wake, hivyo Cassiano, kwa msaada wa baba yake wakaamua kuhamia kwenye klabu ya Flamengo.


KOCHA WA TAIFA STARS ASEMA WATASHAMBULIA MWANZO MWISHO DHIDI YA UGANDA


Moja ya mikakati ya Taifa Stars kwenye mechi ya kesho (Julai 27 mwaka huu) dhidi ya Uganda kuwania kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Tatu za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini ni kushambulia kwa muda mwingi wa mchezo.

Kocha Kim Poulsen amesema maandalizi ya Taifa Stars jijini Mwanza kwa ajili ya mechi hiyo ambayo Uganda inaongoza kwa bao 1-0 yalikuwa mazuri, lakini mabao ni muhimu hivyo watashambulia bila kusahau kulinda lango lao.

“Unapocheza mechi za aina hii za nyumbani na ugenini, huku mwenyeji akiwa anaongoza mabao yana maana kubwa katika mechi. Mabao yanabadili mchezo na pia wachezaji kifikra,” amesema Kim akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Mt. Zion ambayo Stars imefikia.

Amesema katika mechi ya kwanza walitengeneza nafasi nyingi lakini hawakuzitumia, hivyo wamekuwa wakifanya mazoezi ya kushambulia, jinsi ya kutengeneza nafasi, na jinsi ya kumalizia.

“Hivyo tuko hapa (Kampala) kwa ajili ya kufunga, ni lazima tufunge ili tuweze kuendelea na mashindano. Lakini ngome yetu nayo ni lazima iwe makini ili kutoruhusu bao,” amesema Kim na kuongeza kuwa kikosi chake cha kwanza ni lazima kitakuwa mabadiliko kutoka na Mwinyi Kazimoto kuingia mitini na Shomari Kapombe kwenda kwenye majaribio Uholanzi.

Amesema angalau kutakuwa na mabadiliko kwa kuingiza sura mbili mpya katika kikosi cha kwanza, na kuongeza kuwa wachezaji wanafahamu umuhimu wa mechi hiyo kwani timu ikienda kwenye Fainali za CHAN itakuwa manufaa kwao binafsi.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefanya mazoezi ya mwisho leo jioni Uwanja wa Mandela ulioko Namboole ambao utatumika kwa ajili ya mechi hiyo kesho.

Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki na itachezeshwa na waamuzi kutoka Madagascar wakiongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official). Kamishna wa mechi hiyo namba 38 ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende, Aggrey Morris, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Salum Abubakar, Frank Domayo, John Bocco, Amri Kiemba na Mrisho Ngasa.




EXCLUSIVE INTERVIEW NA SHEDRACK NSAJIGWA: AELEZEA SABABU ZA KUWA KOCHA NA KILICHOMUONDOA YANGA

HATIMAYE THIAGO ALCANTARA AFUNGUKA: 'MAN UNITED HAIKUWAHI KUNITAKA NI UONGO TU ULIOTUNGWA NA VYOMBO VYA HABARI " - ATAJA SABABU ZA KUONDOKA BARCA


Kiungo wa Bayern Munich Thiago Alcantara amesema kwamba ssio kweli kwamba alikataa kujiunga na Manchester United kama ilivyokuwa ikiripotiwa bali klabu hiyo ya England haikuwahi kumtaka hata siku moja.

Thiago alihusishwa sana kutakiwa na United kwenye dirisha hili la usajili kabla ya kuamua kujiunga na mabingwa wa ulaya mapema mwezi huu. 

Jana jumatano, baba yake Thiago, Mazinho aliiambia La Xarxa kwamba mtoto wake alikuwa anakaribia kwenda Old Trafford, lakini Thiago mwenyewe leo amekanusha taarifa hizo.

"Ukweli ni kwamba hakuna muda wowote ambao Manchester United walikuja kuongea na sisi. Mambo yote yalikuwa yakiandikwa na vyombo vya habari, ulikuwa niuongo dhahiri," aliiambia radio RAC1.

Akizungumzia uamuzi wake wa kuondoka Barcelona, alisema: "Sio sahihi kusema kwamba sikuwa mvumilivu. Klabu ilielewa hali yangu. Niliwasubiria wao, lakini hawakuwa wanawasiliana nami. Sikuhisi kwamba nina thamani kwao. 

"Nilitaka kushindana. Klabu ilitambua kwamba nataka kuondoka na hawakufanya lolote kubadilisha hilo.
"Kila mtu anaangalia maslahi yake, nilitaka kuona nathaminiwa na nilitaka kushindana hivyo niliamua kuondoka na kujiunga na Bayern.
"Niliwasubiri sana kipindi chote cha kiangazi na mwishowe nikaamua kufanya uamuzi mgumu.
"Anachokitaka kila mwanasoka ni kucheza soka na nilitaka kucheza, wao [Barcelona] hawakufanya chochote kunihakikishia hilo, hivyo ndio maana sasa nipo hapa."

MAKALA: MAMBO MUHIMU TULIYOJIFUNZA KUPITIA MECHI YA FC BAYERN MUNICH DHIDI YA FC BARCELONA


Hi-res-143681575_crop_650x440

Bayern Munich walishinda kombe la Uli Hoeness Cup jana jumatano kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Barcelona.
Ilikuwa ndio mara ya kwanza wanakutana tangu walipocheza kwenye nusu fainali ya ligi ya mbingwa ya ulaya, ambapo Bayern waliidhalilisha FC Barcelona kwa kuifunga 7-0.
Na kama ilikuwa haitoshi hamu ya mchezo huo ilizidi kuongezeka kwa sababu ilikuwa ndio mechi ya kwanza ambayo Pep Guardiola amekutana na timu yake ya zamani. Kocha huyo alidumu Camp Nou kwa miaka minne na kushinda makombe 14.
Thiago Alcantara pia alicheza kwenye mchezo huo dhidi ya timu yake ya zamani kwa mara ya kwanza, siku chache baada ya kununuliwa kwa ada ya uhamisho wa 21.6 million switch to Bayern earlier this month.
Barca, ambao wiki hii walimtangaza Gerardo Martino kuwa kocha wao mpya, walicheza bila kocha mpya na jahazi na kocha msaidizi Jordi Roura na Rubi.
Mchezo ndio ulikuwa wa kwanza kwa Barca kucheza kwenye pre season na kwa Bayern ulikuwa wa saba - hii ni katika kuweka sawa miili ya wachezaji tayari kwa mapambano msimu unaofuatia.
Japokuwa mchezo huo ulikuwa wa kirafiki - lakini kuna vitu muhimu ambavyo tumejifunza kupitia mechi hiyo.

MBINU ZA PEP GUARDIOLA
Hi-res-169506728_crop_650

Pep Guardiola tayari anaonekana kuanza kiurahisi maisha yake ndani ya Allianz Arena.
Jupp Heynckes alishinda makombe matatu msimu uliopita na kuacha vitu vikubwa kuvivaa, lakini Guardiola, anajiamini kwa uwezo alionao, na amekuwa sio muoga wa staili mpya ya kuiongoza klabu yake. 
Akiwa tayari ameshajaribu mifumo ya 4-1-4-1 na 4-3-3 katika pre season, Guardiola anaongeza kitu cha ziada katika kikosi cha Bayern.
Tayari ameshamhamisha nafasi Philipp Lahm, ambaye huko mwanzoni alikuwa anacheza beki wa kulia. 
Guardiola amemhamisha nahodha huyo na kumsogeza mbele kidogo, akicheza upande wa kulia mwa Thiago Alcantara katika kiungo, huku Rafinha akicheza kwenye nafasi ya beki wa kulia.
Lahm anaonekana kucheza vizuri kwenye nafasi yake mpya. Alifunga bao la kuongoza kwenye dakika ya 14 na pia alifunga katika ushindi wa mabao 5-1 kwenye michuano ya Telekom Cup dhidi ya Borussia Monchengladbach jumapili iliyopita.
Kwanini amlete Lahm katika kiungo ambacho tayari kina wachezaji wengi wazuri ambao wanaleta ugumu katika kuwapanga? Guardiola anapenda kufanya majaribio.
Anaweza akawa anatengeneza safu ya kiungo ambayo inaweza kufanya kila kitu - kuzuia, kushambulia, kupiga pasi. 
Bayern walicheza mechi sita kabla ya kucheza na Barca na walifunga mabao 35. Kama ni ishara ya kuonyesha namna mambo yatakvyokuwa huko mbele basi majaribio ya mbinu mpya za Guardiola yatakuwa mazuri sana....

 LA MASIA BADO IPO IMARA SANA
Hi-res-160202787_crop_650

Ni jambo ambalo linafahamika vyema kwamba La Masia ndio academy inayoongoza kwa kutoa vipaji vingi vya wachezaji wakubwa waliopo kwenye soka hivi sasa - ambao wana uwezo wa kuingia kwenye vikosi vya timu nyingi kubwa barani ulaya. 
Barca walicheza mechi ya jana bila wachezaji wengi wa kikosi cha kwanz, XaviAndres IniestaCesc Fabregas, Sergio Busquets, Gerard Pique, Dani Alves na Neymar wote wakiwa bado wapo mapumzikoni baada ya kutoka kushiriki michuano ya kombe la mabara huku Carles Puyol akiwa bado majeruhi, wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza walikuwa hawapo.  

La Blaugrana walianza mchezo huo golini akiwa Pinto, huku Martin Montoya, Marc Bartra, Javier Mascherano na Adriano Correia wakiunfa safu ya ulinzi. Alex Song alicheza kiungo cha kati, huku Jonathan dos Santos akicheza kulia na Sergi Roberto akicheza kushoto. Alexis Sanchez, Lionel Messi na Cristian Tello waliunda safu ya ushambuliaji. 
Kipindi cha kwanza chote kilitawalia na Bayern Munich na mpaka wanakwenda mapumziko walikuwa mbele kwa 1-0. Mascherano na Bartra walijipatia kadi za njano kwa kumchezea faulo  Franck Ribery.

Kipindi cha pili ndipo angalau Barcelona walionekana kutulia na kusogeza timu mbele na kufanya mabadiliko kadhaa kwenye kikosi. Aliingia kipa wa Barca B Oier Olazabal na hivyo kuongeza idadi ya wachezaji wachanga ndani ya kikosi hicho na bahati mbaya wakaongezwa bao la pili lakini kwa kuangalia kwa jicho la tatu inaonekana hatma ya FC Barcelona huko mbele ni nzuri sana kwa vipaji walivyonavyo wachezaji wake wachanga.

 THIAGO ALCANTARA



Thiago Alcantara ameanza kuzoea mfumo wa FC Bayern Munich bila tatizo tena kwa haraka.

Katika mchezo wake wa tatu wa pre season akiitumikia Bayern, alionekana kutulia na mwenye furaha. Kiungo huyo tayari ameshafunga bao la kwanza akiwa na timu yake mpya. 
Katika ushindi wa 5-1 dhidi ya Borussia Monchengladbach, alifunga bao lake akitumia kifua chake.
Katika safu ya kiungo ambayo tayari ina watu wenye vipaji kama Mario Gotze, Bastian Schweinsteiger, Toni Kroos, Arjen Robben, Franck Ribery na Javi Martinez, miongoni mwa hao, ilionekana wazi anaweza akapata shida kuingia moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza. .
Lakini kama kiwango alichoonyesha kwenye pre season kitaendelea kuimarika, then atakuwa amejihakikishia nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha Guardiola. 
FRANK RIBERRY NDIO MCHEZAJI BORA BARANI ULAYA?
Ribery—won the treble with Bayern Munich last season.
Ribery—won the treble with Bayern Munich last season.
Alex Grimm/Getty Images
Kiwango cha Franck Ribery dhidi ya Barcelona kilinikumbusha ubora wa mchezaji huyu.
Ingawa alikuwa anacheza na kikosi dhaifu cha Barca, lakini alicheza vizuri sana. 
Dhidi ya Barca, krosi yake ilipelekea goli la kwanza lilofungwa kwa kichwa na Lahm. Ribery alicheza vizuri sana na kuwasumbua sana mabeki wa Barca kiasi cha kuwafanya Mascherano na Bartra kupewa kadi za njano wakijaribu kumsimamisha mfaransa huyo. .
Baada ya kushinda makombe matatu msimu uliopita, huu ndio muda muafaka wa Ribery kuwaashinda Cristiano Ronaldo na Lionel Messi katika tuzo ya uchezaji bora wa ulaya.