Search This Blog

Saturday, June 16, 2012

ALI AFIF: MWINYI KAZIMOTO AKA 'FAILASOUF' UNAPOTEZA MUDA TANZANIA NA KUUKALIA UTAJIRI WA KIPAJI CHAKO

Kama nilivyotoa taarifa jana kuhusu mazungumzo yangu niliyoyafanya na mchezaji wa klabu bingwa ya bara la Asia, Al Sadd, Ally Hassan Afif, mtoto wa mchezaji wa zamani wa Simba, leo hii naanza kuwaletea baadhi ya mazungumzo tuliyoyafanya, mojawapo lilikuwa ni nafasi ya wachezaji wa kitanzania kucheza soka la kulipwa nchini Qatar ambapo sasa kumekuwa kimbilio la wachezaji wengi wakubwa wa umri waliotamba barani ulaya na Amerika.

Akiongelea kuhusu kiwango cha wachezaji wa kitanzania ambao kwa siku za hivi karibuni alipata bahati ya kuwashuhudia wakicheza soka, Ally anasema wachezaji wengi wa kibongo wanaujua sana mpira na wanaweza kucheza nchini Qatar na kujivunia fedha nyingi sana ambazo zitawajengea misingi imara ya maisha yao mbele baada ya soka.


"Kiukweli Tanzania imebarikiwa vipaji vya wachezaji wengi sana, wanacheza mpira vizuri tena kwa kutumia vipaji vyao bila kuwekewa msingi mzuri walipokuwa wadogo. Kwa kipindi ambacho nilichokuwa Tanzania nimepata bahati ya kuwaona wachezaji wengi wazuri hasa kwenye timu ya taifa lakini yule anayevaa jezi namba 15, anaitwa Mwinyi Kazimoto ni hatari sana yule. Jamaa anaujua sana mpira, nakuhakikishia yule kama anakuja Qatar hata mie simuwezi na kipindi kifupi tu atakachocheza kule atakuwa akipokea fedha nyingi huku timu zikigombea saini yake. Mwinyi mie tangu nimuone nimekuwa namfuatilia sana mechi anazocheza, ana kila kitu ambacho kiungo wa timu anapaswa kuwa nacho, anajua sana ndio maana nimempa jina la 'Failasufu" nikiwa na maana ya Mwanafalsafa wa soka. Kwa hakika Mwinyi Kazimoto anapoteza muda wake nchini  Tanzania, namshauri aongee vizuri na timu yake ya Simba imruhusu aje ajiunge na timu kubwa huku Qatar ambazo zinaweza kumlipa sio chini dola 40,000 au zaidi kutokana na uwezo wake wa kisoka. Kiukweli amebarikiwa kipaji kikubwa ambacho ni haba kukipata kwa wachezaji wa kawaida."



"Pia nimewaona wachezaji wengine kama Kaseja na Ngassa kwa kweli wale nao wanatakiwa kucheza timu kubwa zaidi wanazozichezea sasa kwa kuwa ni wachezaji wa level ya juu, lakini ama kwa hakika mimi kama mimi Failasufu Mwinyi Kazimoto ni hatari zaidi na nitajaribu kwa njia zote kumleta Qatar."

R.I.P JAY LUGANO, RAFIKI YANGU WA FACEBOOK!

Nimepokea kwa majonzi makubwa kifo cha mmoja wa marafiki zangu kwenye mtandao wa kijamii wa FACEBOOK bwana Jay Lugano,alikua pia mmoja wa wafuatiliaji wa karibu sana wa www.shaffihdauda.com. Hatukuwahi kukutana uso kwa uso ila tulibadilishana sana mawazo juu ya mambo mbali mbali ya soka.
sina mengi ya kusema zaidi ya kumtakia mapumziko mema huko aendako! MUNGU AILAZE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU JAY LUGANO .AMEN!
 JAY LUGANO SHOTO AKIWA NA SHABANI KADO.
   HAPA AKIWA UWANJA WA TAIFA ENZI ZA UHAI WAKE.
Mungu ailaze mahala pema roho ya Jay Lugano ! AMEN.

KINDA LA YANGA LAJIUNGA NA COASTAL UNION!

Afisa habari wa Coasta Union, Edo kumwembe akimkabidhi jezi mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Atupele Green ambaye ni mshambuliaji namba moja wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 21. Guys get ready...the young boy is real deal...ana mwili mkubwa, nguvu, kasi, stamina...mtambo wa mabao. Coastal Union, here we go!!!

DEIDRE LORENZ KUSHIRIKI MBIO ZA MOUNT KILIMANJARO JUNI 24

 Mcheza sinema maarufu duniani kutoka nchini Marekani Deidre Lorenz atakimbia mbio za kila mwaka za Mount Kilimanjaro Marathon zinazoanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 24 Juni mwaka huu kutoka Moshi Club mjini Moshi.
Mbio hizi zilizoanzishwa na mama Marie France kutoka katika mji wa Bethesda, Maryland nchini Marekani mwaka 1991 ni mbio zinazojulikana kama 7 continental Races na zimeshawahi kupata tuzo mbalimbali za kimataifa.
Ujio wa mcheza sinema huyu aliyecheza sinema nyingi kama vile Santorini Blue, Perfect Strangers, The Great Fight,  na nyingine nyingi unaiweka Tanzania katika macho ya dunia na kuwavutia watalii wengi kutoka taifa hili tajiri duniani. Deidre Lorenz alizaliwa katika jiji la Oregon nchini Marekani lakini akahamia katika jiji la New York City linalijulikana kama "The Big Apple" nchini Marekani akiwa na kampuni yake ya kutengeneza sinema inayoitwa Thira Films LLS.
eidre Lorenz ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kugombe tuzo za wacheza sinema maarufu duniani zinazojulikana kama Grammy Awards. Mcheza sinema huyu  ataambatana na Wamarekani wengine kuja nchini tarehe 21 Juni kukimbia mbio hizi ambazo zimetokea kuutangaza sana mji wa Moshi tangu mwaka 1991. Lorenz alipatikana katika bahati nasibu iliyochezwa wakati wa mbio za New York Marathon mwaka jana.
Naye mwanzilishi wa mbio hizi mama Marie Frances ana historia ya kuanzisha mbio na matamasha mbalimbali duniani. Alikuwa pia mwanzilishi wa mbio za Pyramid Marathon nchini Misri pamoja na Miss Universe Egypt matamasha yaliyojizolea sifa kemkem.Aliombwa kuja kuanzisha mbio za Marathon nchini Tanzania na balozi wa Tanzania wa wakati ule nchini Misri.Mbio za Mt. Kilimahjaro Marathon ni moja kati ya mbio tafauti za marathon zinazifanyika katika mji wa Moshi.
Mount Kilimanjaro Marathon zitaanzia Moshi Club mpaka Rau madukani na kurudi mara tatu ambazo zitakuwa kilimeta 42. Kutakuwa pia na mbio z akilometa 21, kilimeta 10 na kilometa 5 kwa watoto. Wakimbiaji hawahitaji kuwa na ujuzi wa kukimbia watu wote wanaweza kukimbia.

EDDA MISS KIGAMBONI CITY 2012



Redds Miss Kigamboni City  2012 , Edda Sylvester (21) akipunga mono kwa furaha mara baada ya kutangazwa mshindi na kuvikwa taji la Kigamboni City katika shindano lililofanyika katika Ukumbi wa Navy Kigamboni jijini Dar es Salaam jana. (Picha zote na Mroki Mroki) 

Warembo walioingia hatua ya tano bora ya Miss Kigamboni 2012, kutoka kulia Elizabeth Boniface, Ester Albert, Edna Sylvester, Hadija Kombo na Agnes Goodluck wakipozi kwa picha jukwaani baada ya kutajwa kuvuka nafasi hiyo na kupata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 baadea mwaka huu.

Warembo waliokuwa wakiwania taji la Miss Kigamboni City 2012 wakicheza show ya ufunguzi jukwaani.

Redds Miss Kigamboni City  2012 , Edda Sylvester (katikati) akiwa na mshindi wa pili Agnes Goodluck (kushoto) na mshindi wa tatu Elizabeth Boniphace mara baada ya kutangwazwa washindi. Edda aliwashinda warembo wengine 9 katika shindano hilo. (Picha zote na Mroki Mroki) 


Na Mwandishi Wetu
MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Mlimani jijini Dar es Salaam, Edda Silyvester, 21, usiku wa kuamkia juzi alifanikiwa kutangazwa kuwa mshindi wa taji la kitongoji cha Kigamboni 'Redd's Miss Kigamboni 2012' katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Navy Beach.
Kutokana na ushindi huo Edda alizawadiwa kitita cha Sh. 500,000 taslimu na mgeni rasmi katika shindano hilo, diwani wa Kata ya Kigamboni, Dotto Msawa.
Nafasi ya pili katika shindano hilo lililopambwa na burudani safi kutoka katika bendi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma ilichukuliwa na Agnes Goodluck ambaye naye alipata zawadi ya Sh. 350,000.
Elizabeth Boniface alichaguliwa kuwa mshindi wa tatu na kupata zawadi ya Sh. 300,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Esther Albert na mshindi watano akiwa ni Khadija Kombo. Elizabeth na Khadija kila mmoja alipata zawadi ya Sh. 200,000.
Jaji Mkuu wa shindano hilo, Benny Kisaka, alitangaza kuwa badala ya warembo watatu atachukua warembo wote watano kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ya Temeke baadaye mwaka huu.
Warembo wengine walioshiriki shindano hilo walikuwa ni Sophia Martin, Rosemary Peter, Doreen Kweka na Linnah David waliambulia kitita cha Sh. 150,000 kila mmoja.
Waratibu wa shindano hilo, kampuni ya K& L Media Solutions wanawashukuru wadau wote waliosaidia kufanikisha shindano hilo
Kwa kufanikisha onyesho hilo ambalo lilikuwa ni la mwisho kwenye kanda ya Temeke

YANGA KUANZA KUUTETEA UBINGWA WAO KAGAME JULAI 14 LIVE ON SUPERSPORT - CHAMAZI KUTUMIKA

Mashindano ya Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) yanayoandaliwa na Baraza la Vyama ya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) yatafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 14-29 mwaka huu ambapo timu zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kabla ya Juni 25 mwaka huu.
 
Yanga itashiriki mashindano hayo ikiwa bingwa mtetezi, wakati Tanzania Bara itawakilishwa na mabingwa wake Simba na Makamu bingwa Azam. Mashindano hayo yatafanyika jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Chamazi pekee kwa sababu ya kupunguza gharama za uendeshaji.
 
Ratiba ya mashindano hayo yanayoshirikisha mabingwa kutoka nchi kumi na moja ambao ni wanachama wa CECAFA itapangwa Juni 29 mwaka huu.
 
Mashindano haya ni muhimu kwa CECAFA na Tanzania Bara ambayo ndiyo mwenyeji kwa maendeleo ya mpira wa miguu na pia kukuza kiwango cha mchezo huo kwa ukanda huu ambao kwa Afrika unaoongoza kwa kufanya mashindano mengi ya timu za Taifa pamoja na klabu.
 
Mwenyekiti wa CECAFA ambaye pia ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewaomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo ambayo itaoneshwa na kituo cha televisheni cha SuperSport. Pia amewataka washabiki kujitokeza kwa wingi viwanjani kuunga mkono michuano hiyo.
 
CECAFA inawashukuru wadau wote kwa kuwezesha michuano hiyo kufanikiwa akiwemo Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa kutoa zawadi za fedha kwa washindi, Serikali ya Tanzania kwa kutoa Uwanja wa Taifa na Kamati ya Utendaji ya TFF kwa kukubali kuwa mwenyeji wa mashindano hayo.
 

TAIFA STARS WAWASILI SALAMA MSUMBIJI NA MAZOEZI MAKALI YANAENDELEA.




Shomari Kapombe na Kim Poulsen wakiingia kwenye basi baada ya kuwasili Msumbiji

Kim Poulsen akiwa na maongezi na balozi wa Tanzania nchini msumbiji.
Tom Ulimwengu akiwa dimbani na wenzake huku Kim Poulsen akisimamia.
John Bocco, Nurdin Bakary na Shabaan Nditi
                                      

MPO WAPI VIONGOZI MLIOKUWA MKIITAKA KAMPUNI YA LIGI KUU YA VODACOM?

Zile mbio za vilabu nchini kushinikiza kudai TFF ibadili mfumo mzima wa uendeshaji wa ligi kuu Tanzania bara ambayo imekua ikilalamikiwa na wadau wengi wa soka nchini ziliota mbawa baada ya shirikisho la soka kuteua kamati ya ligi ambayo kwa baadhi ya wajumbe wake ni viongozi wa vilabu waliokua kwa pamoja wakipinga suala la mfumo mzima wa Kamati hiyo.

Katika vikao vyote ambavyo vilabu vilikaa, kwa pamoja walikubaliana kwamba uendeshaji mzima wa ligi uwe katika mfumo wa kampuni na kama haitoshi Agenda namba moja (No.1) ilikuwa ni kupinga kuendeshwa ligi kwa kamati. Viongozi wa vilabu kumi na nne (14) yani AZAM, AFRICAN LYON, KAGERA SUGAR, RUVU, COASTAL UNION, SHOOTING, VILLA SQUAD, SIMBA, YANGA, POLISI DODOMA, MTIBWA, TOTO, OLJORO, MORO, JKT RUVU waliteua viongozi wa kusimamia mchakato wakiongozwa na Mwenyekiti Geofrey Nyange Kaburu (Simba) Katibu Mkuu wa Yanga, Mwesiga Celestine (Makamu Mwenyekiti), wakati Katibu Mkuu wa kamati hiyo ni Meja Ruta      ( Ruvu Shooting) na wajumbe ni Iddi Godigodi (Villa Squad), Evodius Mtawala (Simba), Said Mohamed na Shani kutoka Azam FC.
Kwa nia ya kuliendeleza soka letu na pia ni mwanzo wa vilabu kuwa na sauti moja inapofika suala la maendeleo katika medani nzima ya soka.

Vilabu pia vilionyesha jinsi gani vina uchungu kwani ilfikia kipindi hata vilabu kutishia kugoma kucheza mzunguko wa pili wa ligi ya VODACOM 2011/2012 kama ile ajenda yao namba moja(No.1) haitofanyiwa kazi.

Umoja wa vilabu ulikuwa dissolved naweza kusema mara tu baada ya Rais wa shirikisho Leodgar Tenga kuteua kamati ya ligi kama ifuatavyo :- Wallace Karia ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF( Mwenyekiti), Said Mohamed kutoka Azam (Makamu Mwenyekiti), huku wajumbe ni Mwanasheria Damas Ndumbaro, Yahya Ahmed (Kagera Sugar), Meja Charles Mbuge (JKT Ruvu Stars), Steven Mnguto (Coastal Union), Kaburu (Simba), Seif Ahmed (Yanga), ACP Ahmed Msangi (Polisi Dar) na Henry Kabera (Majimaji). Hapa nampongeza sana Tenga kwani alijua udhaifu wa viongozi wetu wa soka na ilifikia kipindi alithubutu kuwaita wengine wadogo zangu huku akijisifu kuwa yeye ni MBA holder na kwa kweli alifanikiwa kwani viongozi ambao walikua wakipinga kamati katika agenda yao No.1 waliingia kwa moyo mmoja katika kamati ile yani (Nguruwe sili maini yake nakula)

Viongozi hao walikwenda kufanya kazi za kamati ambazo ni kuongeza vurugu katika soka kwani tumeshuhudia jinsi kamati hii ilivyokuwa ikitunishiana misuli na ile ya mzee wangu kamanda Alfred Tibaigana kwa maana sio tena kamati ya ligi na kuishia kufanya kazi za kamati ya sheria na kuleta vurugu kubwa sana mwishoni mwa msimu wa ligi.

Ni aibu kubwa kwani katika mambo ambayo tuliyapa kipaumbele yalikuwa ni Ligi daraja la kwanza suala zima la udhamini sasa angalia leo Fainali za ligi daraja la kwanza mkoa una invest fedha ili kupata fursa ya kuandaa fainali husika na hatimaye timu kutoka kituo mwenyeji kupanda kucheza kigi kuu Tanzania bara na hili tumelishuhudia miaka 4 mfululizo.

Ligi imekwisha viongozi wanahaha mara Zambia, Kenya, Uganda, Malawi, Rwanda na wamesahau kwamba mkataba wa Vodacom inabidi uangaliwe upya kwa vilabu kushirikishwa au kama wamekubali timu ndogo ziendelee kuambulia 5700/= gate collections Chamazi watuambie.

IDDI GODIGODI

CABAYE NA MENEZ WAIPELEKA UFARANSA KILELENI MWA KUNDI D EURO - SHEVA AWASUBIRI ENGLAND MECHI YA MWISHO


Ukraine 0-2 France (Euro 2012 - Group D) by fasthighlights-2012vvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvvv

ANDY CARROLL, WALCOTT, NA WELBECK WAMLIZA IBRAHIMOVIC - ENGLAND IKIWATOA SWEDEN EURO 2012


Sweden 2-3 England (Euro 2012 - Group D) All Goals by fasthighlights-2012

Friday, June 15, 2012

EXCLUSIVE INTERVIEW NA MTOTO WA HASSAN AFIF ANAYECHEZA TIMU MOJA NA RAUL GONZALEZ


Mchana wa leo nilibahatika kufanya mazungumzo na mtoto wa mchezaji wa zamani wa Simba, Hassan Afif, Ally Afif ambaye ni mchezaji wa klabu bingwa ya bara la Asia Al Sadd ya nchini Qatar. Ally ambaye alizaliwa nchini Qatar na kuishi kidogo nchini Tanzania kabla ya yeye na baba yake Mzee Afif kurudi tena Doha ambapo ndio hasa alianza kukuza kipaji chake mpaka alipo sasa.


Nimepata kuongea mengi na Ally endelea kufuatilia shaffihdauda.com



                     

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB (YANGA)

Kamati ya Uchaguzi ya TFF inawataarifu wadau na wapenzi wa soka kuwa mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa YANGA kujaza nafasi zilizowazi za Kamati ya Utendaji unaendelea vizuri chini ya Kamati ya Uchaguzi ya YANGA.

Kamati ya Uchaguzi ya TFF imepokea kutoka Kamati ya Uchaguzi ya YANGA nakala za fomu za maombi ya uongozi wa YANGA pamoja na nakala za vyeti vya elimu vya waombaji uongozi kama sehemu ya taarifa ya awali ya mchakato wa uchaguzi huo wa YANGA. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imebaini kuwa baadhi ya waombaji uongozi wamewasilisha nakala za vyeti vya kuhudhuria masomo ya sekondari (Secondary School Leaving Certificate) badala ya nakala za vyeti vya kuhitimu masomo ya elimu ya sekondari (Certificate of Secondary Education).

Kamati ya Uchaguzi ya TFF imekwisha ielekeza Kamati ya Uchaguzi ya YANGA kuwataka wagombea wote kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF Ibara ya 10(4) na (5) inayowataka wagombea wote kujaza Fomu Na.1 ya maombi ya uongozi na  kuambatanisha nakala ya cheti cha Elimu ya Sekondari (Certificate of Secondary Education) kama ilivyoainishwa kwenye Fomu Na.1 kipengere Na.9. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya YANGA iwashauri wagombea ambao vyeti vyao vimepotea wawasiliane na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kwa maandishi ili kupata ‘Statement of Examination Results’ itakayotumwa kwa Kamati ya Uchaguzi ya YANGA kupitia TFF kuthibitisha kuwa wamehitimu elimu ya kidato cha nne.

Uhakiki  wa vyeti vya elimu ya sekondari vya waombaji uongozi hufanywa na NECTA na vyuo husika kwa elimu ya juu kwa chaguzi za wanachama wa TFF. Wanachama wote wa TFF wanatakiwa kuzingatia kikamilifu matakwa ya Kanuni za Uchaguzi.


Imetolewa na:

IDARA YA HABARI
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


SHOMARY KAPOMBE MWANAMICHEZO BORA WA MWAKA 2011


TUZO ZA TASWA ZILIVYOFANA USIKU HUU DIAMOND JUBILEE

Rais wa TFF, Leodegar Tenga wa pili kulia akiwa na Jellah Mtagwa kushoto kwake


Familia ya ndondi


Wadau wa ndondi
Tedi Mapunda kulia na bosi wake 


Eiphraim Mafuru kulia


Maswahiba wa siku nyingi, Shaaban Mkongwe kulia akiwa Waziri Mahadhi


Beki wa Mtibwa Salum Swedi 'Kussi'


Kaburu kulia akikabidhi tuzo


Daud Salum 'Bruce Lee' kulia akikabidhi tuzo


Athumani Hamisi akikabidhi tuzo


Asha Baraka akikabidhi tuzo


Mafuru akikabidhi tuzo


Ridhiwani Kikwete kulia akiwa na Benny Kisaka kushoto, cheko la maana


Dioniz Malinzi kushoto akikabidhi tuzo


Kapombe akipokea tuzo ya Mwanamichezo Bora Chipukizi kutoka kwa Salim Amir


Mzee Matumla akimkabidhi Kaburu tuzo ya Emmanuel Okwi


Mwenyekiti wa RT, akimkabidhi tuzo Mwanahamisi Gaucho


Aggrey Morris kushoto akipokea tuzo ya Mwanasoka Bora wa mwaka 


Ally Choky akikabidhi tuzo


Mafuru akipakia msosi


Kim Poulsen kulia akiwa na nani sijui


Jamal Rwambow kulia na Kaburu wakati wa maakuli


Serengeti Beer inapokolea, mambo huwa hivi...


Mzee El Maamry akimkabidhi tuzo George Tarimo


Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Adolph Rishard


Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Peter Tino


Mzee Mwinyi akikabidhi tuzo


Waziri Mahadhi akimpokelea tuzo marehemu baba yake, Omar Mahadhi


Kaburu akimsaidia Kapombe kupokea tuzo ya Mwanamichezo Bora wa mwaka 2011 


Juma Pinto akikabidhi tuzo


Zena Chande na swahiba zake


Shaffih Dauda kulia, Amour Hassan na Michael Maluwe


Tullo Chambo na bosi wake


Akina nani sijui hawa


BIN ZUBEIRY kulia na Shaffih Dauda


MAJINA YA WASHINDI

1: OLIMPIKI MAALUM-Zanzibar
Ahmada Bakar:

2:OLIMPIKI MAALUM-TANZANIA BARA
HERITH SULEIMAN

3: PARALIMPIKI: WANAUME
ZAHARANI MWENEMTI

4:PARALIMPIKI: WANAWAKE
FAUDHIA CHAFUMBWE

5: KIKAPU: WANAUME
GEORGE TARIMO:

6:  KIKAPU WANAWAKE
EVODIA  KAZINJA:-

7: NETIBOLI:
LILIAN SYLIDION

8:  GOFU WANAWAKE:
MADINA IDDI

9: GOFU WANAUME:
Frank Roman:

10: NGUMI ZA RIDHAA
SULEIMAN SALUM KIDUNDA

12:  WAOGELEAJI MWANAMKE
MAGDALENA MOSHI     

WAOGELEAJI MWANAUME
AMMAAR GHADIYALI  -  MEN

13:JUDO...
AZZAN HUSSEIN KHAMIS (ZANZIBAR)
14:JUDO BARA: . MBAROUK SELEMANI

14: WAVU WANAWAKE
THERESIA ABWAO  

15: WAVU WANAUME
MBWANA ALLY

16: NGUMI ZA KULIPWA
 Nasibu Ramadhan

17. TENISI:Wanaume
WAZIRI SALUMU

18. TENISI WANAWAKE: 
REHEMA ATHUMANI

20: BAISKELI (Wanawake)
Sophia Hussein
-
21: BAISKELI WANAUME
Richard Laizer

22: WACHEZAJI WA TANZANIA WANAOCHEZA NJE
Mbwana Samatta-

23: MCHEZAJI BORA CHIPUKIZI
SHOMARI KAPOMBE- (soka) SIMBA

24: MCHEZAJI WA NJE ANAYECHEZA TANZANIA
Emmanuel Okwi-Simba

25: SOKA (WANAWAKE)
MWANAHAMISI OMARI

26: SOKA WANAUME
Aggrey Morris-Azam:

27: RIADHA
WANAWAKE
Zakia Mrisho:

28: RIADHA WANAUME
Alphonce Felix:

29: MIKONO WANAUME
Kazad Monga-Magereza Kiwira
Faraji Shaibu  Khamis-Nyuki Zbar

30:  MIKONO WANAWAKE
Zakia Seif-Ngome Dar

31: Kriketi WANAWAKE
Miss. Monika Pascal

32; KRIKETI WANAUME
Mr. Kassimu Nassoro

33: TUZO YA HESHIMA:
KIKOSI KILICHOFUZU FAINALI ZA MATAIFA YA AFRIKA 1980

34:MWANAMICHEZO BORA WA TANZANIA MWAKA 2011-
SHOMARI KAPOMBE