Search This Blog

Saturday, July 2, 2011

TOP 10 YA MAKINDA GHALI ZAIDI KATIKA USAJILI WA EPL

Wakati dirisha la usajili barani ulaya, tumekuwa tukishuhudia ligi kuu ya England ikiendelea kufanya kufuru katika uhamisho wa wachezaji kutoka klabu moja hadi nyingine.

Recently tumeshuhudia Sunderland wakitumia Paundi million 8 kwa ajili ya mchezaji mwenye umri wa miaka 18, Cannor Wickham, huku Manchester United wakilipa mara mbili ya pesa hiyo kwa Phil Jones kutoka Blackburn.


Sasa tuangalie historia ya uhamisho ghali wa wachezaji makinda chini ya miaka 20 katika ligi kuu ya England.


10 - ROBBIE KEAN: WOLVES KWENDA COVENTRY (£6m)

Wolves wahitaji kunona kwa bank account yao ili kuweza kumwachia kijana wao wa ki-Irish na Coventry wakawajaza manoti.£6m ilikuwa ni rekodi ya usajili wa mchezaji kinda Robbie Kean mwaka 1999 akiwa na miaka 19 ambapo Coventry a.k.a Sky Blue walipomchukua kutoka Wolves.Hata hivyo ilikuja kuwa biashara nzuri kwa upande wa Coventry baada ya kocha wa Marcelo Lippi wa vigogo wa jiji la milan, Inter kulipa £13m kwa ajili Kean mwaka 2000.


9 - GLEN JOHNSON: WEST HAM KWENDA CHELSEA (£6m)

Akiwa na miaka 18, beki wa kulia alikuwa tayari ameshaichezea mechi 15 klabu yake ya West Ham kabla ya Chelsea kumchukua mwaka 2003 na kumfanya kuwa ndio mchezaji wa kwanza kusajiliwa chini ya utawala wa Roman Abramovich.Johnson ndiye mchezaji kinda ghali zaidi kuwahi kusajiliwa na Chelsea, lakini Jose Mourinho alipoingia Stamford Bridge alimuuza kwa Portsmouth.


8 - FABIAN DELPH: LEEDS KWENDA ASTON VILLA (£6m)


Ilikuwa ni kama nusu ya timu zote za EPL zilikuwa zinataka saini ya Delph katika kipindi kama hiki mwaka 2009.Kijana huyu aliyezaliwa Bradford alikuwa lulu katika kipindi cha usajili lakini hatimaye Aston Villa ilifanikiwa kupata saini ya kiungo huyu ambaye kipindi hicho alikuwa na umri wa miaka


7 . GARETH BALE: SOUTHMPTON KWENDA TOTTENHAM(£5m mpaka £10m)


Mwaka 2006, akiwa na miaka 17, Welsh-full back alikuwa katika kiwango kizuri ndani ya kikosi cha Southmpton, akiwa mtalaam wa mipira iliyokufa.

Man United walimtaka lakini Bale aliamua kwenda London na akasaini Tottenham kwa £5m katika hatua za mwanzo lakini baadae Spurs walilipa £10m kutokana na mafanikio atakayoyapata mchezaji husika.Usajili wa Bale kwa Spurs umekuwa na faida nyingi akiisaidia timu yake kucheza robo fainali ya klabu bingwa ya ulaya msimu uliopita, pia amekuwa mchezaji bora wa ligi kuu kwa chama ya wachezaji soka nchini England.


6- CONNOR WICKHAM: IPSWICH KWENDA SUNDERLAND(£8m mpaka £12M)

Japokuwa alikuwa akifuatilia na timu nyingi za ligi kuu tangu alipopata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Ipswich misimu miwili iliyopita.Wickham mwenye umri wa miaka 18, alikuwa moja ya washambuliaji waliounda safu ya mashambulizi ya kikosi cha England under 21 kilichoshiriki katika michuano ya EURO UNDER 21 iliyofanyika Denmark wiki kadhaa zilizopita.



5 - THEO WALCOTT: SOUTHMPTON KWENDA ARSENAL (£9m)


Alikuwa ni roomate na Gareth Bale wakiwa katika Academy ya Southmpton, lakini yeye aliamua kutofautiana na rafiki yake Bale baada ya kuamu a kwenda upande mwingine wa jiji la London.Walcott alijiunga na Arsenal mwaka 2006 kwa usajili uliowagharimu pesa nyingi Gunners, akiwa na miaka 16 alikuwa akizivutiaa na timu za Man United, Tottenham, Chelsea na Liverpool.Walcott alitawala katika vyombo vya habari pindi Sven Goran Eriksson alipomuita katika kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa kilichoshiriki World Cup mwaka 2006-German ingawa hakucheza hata mechi moja.


4 - CRISTIANO RONALDO: SPORTING LISBON > MAN UNITED (£12M)

Liverpool na Arsenal zote zilikuwa zikimtaka lakini Manchester United hatimaye walimnyakua mwaka 2003 baada ya kucheza dhidi ya Red Devils katika mechi za pre season.Walikuwa ni wachezaji wa United waliomshawishi bosi wao amsajili Ronaldo, na hatimaye United walilipa paundi millioni 12 kumchukua Ronnie ambaye kipindi hicho alikuwa na umri wa miaka 18.United wamepata faida ya zaidi ya £68m baada ya Real Madrid kulipa £80m mwaka 2009 kupata saini ya mreno huyo.


3 - PHIL JONES: BLACKBURN > MAN UNITED (16.5M)

Mechi 35 alizocheza akiwa na kikosi cha Blackburn zilitosha kumshawishi kuvunja benki na kutoa £16.5m kupata saini ya beki wa kati mwenye umri wa miaka 19, Phil Jones.

Usajili wa Jones ambaye Liverpool na Arsenal walikuwa tayari kulipa pesa ili kupata saini muingereza huyu ulipata baraka kubwa kutoka kwa Wayne Rooney aliyesema "Jones ni moja ya mabeki wagumu kukabiliana nao".



2 - ANDERSON: PORTO > MANCHESTER UTD(£18M)

Inaweza kushangaza kujua kwamba alinunuliwa kwa gharama ya paundi million 18, £6m zaidi ya Cristiano Ronaldo, lakini ndio ukweli wenyewe.Kiungo huyu mbrazili kutoka Porto aligharimu zaidi United zaidi mchezaji bora wa dunia wa 2008, akiwa na miaka 19, Anderson alimvutia Sir Alex Ferguson na kumfanya mscotish kufungua pochi kwa ajili yake.Amekuwa sio mchezaji wa kikosi cha kwanza mara kwa mara, na mara kadhaa amehusishwa na kuondoka O.T lakini ni vigumu sana kuamini kama United watarudisha fedha waliyomnunulia ikiwa wataamua kumuuza.


1 - WAYNE ROONEY: EVERTON > MAN UNITED - £27M


Moja ya usajili mwingine ambao Sir Alex Ferguson hatokaa kamwe kujilaumu kuufanya ni usajili wa nguzo ya klabu ya United na timu ya taifa ya England, Wayne Mark Rooney.

Alisajiliwa na United katika siku ya mwisho wa usajili mwaka mwaka 2004 baada ya kuwa kiwango kizuri katika timu ya taifa ndani ya EURO 2004.Akiwa na miaka 18 alishacheza misimu miwili ya EPL katika klabu ya Everton.Ameisadia United kushinda makombe manne ya EPL PLUS UEFA Champions League.








DAVID HAYE VS KLITSCHKO - MABONDIA WA ZAMANI NA SASA WANASEMAJE?


Yakiwa yamesalia masaa machache kabla ya mpambano kati ya David Haye na Vladmir Klitschko kila mtu amejaribu kutoa utabiri wake kuhusu nani atafanya nini kwenye pambano hilo lakini mabondia mbalimbali kwa upande wao wanasemaje ?

MIKE TYSON
BINGWA WA ZAMANI WA UZITO WA JUU.(Klitschko atashinda)
“Haye hataweza kudumu zaidi raundi mbili . Napenda jinsi Haye anavyopambana lakini nadhani Klityschko atakuwa amemzidi sana na hilo litaonekana , sidhani kama Haye atakuwa na mbinu za kutosha kumzuia Klitschko, ni wazi kuwa Klitschko atamchapa kisawasawa.


Bingwa wa WBA light-welterweight, Amir Khan: DAVID HAYE

“David Haye ni bondia mwenye staili ya kusisimua sana ya kupigana kwa sasa tangu enzi za Lenox Lewis . Najua kuwa Klitschko ana nguvu sana kumshinda Haye ila David ana ‘movement’ nzuri sana na kasi yake pia inaweza kumdhuru Klitschko , nadhani David atashinda kwenye raundi za mwisho.


Bingwa wa WBC super-middleweight Carl Froch: DAVID HAYE

"Nampa nafasi kubwa David Haye . Vladmir ni mrefu , ana nguvu na staili ya kupambana ya ajabu kidogo na kiukweli ni hatari kwa David . Ila jinsi anavyopigana David ndio sababu inayonifanya nimpe nafasi , nadhani anajiamini sana na atampa tabu Vladmir kwa sababu Haye si mtu wa kurudi nyuma , akija anakuja kweli na haangalii nyuma , nadhani ni kitu ambacho Vladmir hatarajii ila kinaweza tokea na ikiwa hivyo Vladmir atapata tabu sana"

Bingwa wa zamani wa uzito wa juu duniani . Lennox Lewis: DAVID HAYE

“On paper , Klitschko ni mtu ambaye wengi watampa nafasi kubwa kwa sababu anamzidi Haye kwa karibu kila kitu na ni bondia halisi wa uzito wa juu tofauti na Haye .Lakini kama Haye akiingia na mpango thabiti wa kumkabili Vladmir kama ambavyo amekuwa akifanya kwenye mapambano ya nyuma ana nafasi ya kufanya vizuri.



Bingwa wa zamani wa super-middleweight king na Ring magazine light-heavyweight
Joe Calzaghe: DAVID HAYE

“Vladmir ni mkubwa na ana mkono unaofika mbali na ana kila kitu ambacho Haye hana .David Haye ana kasi ya ajabu , na ana uwezo wa kuskuma makonde kwa Klitschko , na pia Klitschko si bonida sugu kwa sababu anadondoka kirahisi hata ukitazama kwenye mapambano ya nyuma amewahi kudondoshwa mara zisizopungua kumi . Kama akimuotea vizuri , David ana nafasi kubwa ya kushinda .


Promota wa ngumi za kulipwa Frank Warren: WLADIMIR KLITSCHKO
“Kwangu Klitschko ana nafasi kubwa ya kushinda. Kwanza ana umbo kubwa ambalo ni faida , najua wengi watasema kuwa hata Nikolay Valuev alikuwa mkubwa kwa Haye na akashinda lakini Vladmir ana uwezo halisi wa kupigana kuliko Nikolay , ngumi zake ni kali mno , sioni Haye akimzuia .

Mshindi wa medali ya dhahabu kwenye Olimpiki . James De Gale: WLADIMIR KLITSCHKO

“Unapopambana na yoyote kati ya wanandugu wa wawili wa Klitschko mjini Hamburg ujue huna nafasi ya kushinda hata kidogo , itakuwa ngumu sana kwa Haye kushinda , Naona kabisa jinsi Vladmir atakavyomuangusha Haye kwenye raundi za mwisho . Amemzidi kila kitu kuanzia umbo , uwezo na akili ya mchezo wa ndondi na kiukweli ni ngumu sana kwake kushindwa kumchapa Haye hapa. Ila huwezi jua kinachohitajika kushinda pambano la ngumi kama hili ni ngumi moja tu kali kama ilivyokuwa kwenye pambano la kwanza la Lewis na Rahman na Haye anao uwezo wa kufanya hivyo , ila sidhani kama tutaona maajabu hayo , namuona Klitschko akimuangusha Haye mara kama nne hivi kabla refa hajasimamisha pambano . Haye ana kasi ila ni bondia wa uzito wa juu mdogo na tunajua yanayowakuta mabondia kama hao .

Hayo ndio maneno ya mabondia mbalimbali juu ya pambano la leo , muda unazidi kwenda , tumgoje kuona kama itakuwa Haye au Vladmir .

UFUNGUZI WA COPA AMERICA ARGENTINA 1:1 BOLIVIA

Friday, July 1, 2011

kagame castle cup: match live center. SIMBA VS ETINCELLES

KICK OFF :KIKOSI CHA SIMBA LEO KIMEFANYIWA KIDOGO MABADILIKO AMBAPO SALUM KANONI AMECHUKUA NAFASI YA SAID NASSOR UPANDE WA BEKI YA KULIA,SHIJA MKINA AMECHUKUA NAFASI YA MUSA MGOSI,ATHUMANI IDD AMEANZA KWENYE KIUNGO AKIWA NA MOHAMED BANKA,JERRY SANTO, HARUNA MOSHI AKISAIDIANA NA SALUM MACHAKU KWENYE SAFU YA USHAMBULIAJI,KWENYE NGOME NI JUMA NYOSA NA DERECK WALUHYA,WAKATI AMIR MAFTAH AKIWA NYUMA KUSHOTO NA JUMA KASEJA GOLINI.

DAKIKA 11: MOHAMEDI BANKA ALMANUSURA AFUNGE LAKINI GOLIKIPA WA ETINCELLES AMEOKOA NA IMEKUA KONA.

DAKIKA 14: AMIR MAFTAH ALMANUSURA AFUNGE BAO KAMA ALILOFUNGA KWENYE MCHEZO DHIDI YA OCEAN VIEW.

DAKIKA 17: HARUNA MOSHI AMEPIGA BONGE LA SHUTI LIMETOKA PEMBENI KIDOGO,MATOKEO BADO 0:0

DAKIKA 19: SIMBA WAMEKOSA TENA BAO LA WAZI BAADA YA SALUM MACHAKU KUPIGA CROSS NZURI KUTOKA KUSHOTO MWA KIWANJA NA KUMKUTA BOBAN AMBAYE SHUTI LAKE LIMEMGONGA BEKI WA ETINCELLES

DAKIKA 22: SIMBA INAONGOZA 1:0

BAO ZURI LIMEFUNGWA NA HARUNA MOSHI KWA MGUU WA KUSHO BAADA YA KUMPIGA CHENGA BEKI WA ETINCELLES,
MPIRA ULIANZIA PEMBENI AMBAPO SALUM MACHAKU ALIPIGA KROSI ILIYUNGANISHWA KWA KICHWA NA MOHAMED BANKA NA MPIRA HUO KUGONGA MWAMBA KABLA YA KUMKUTA BOBAN.

DAKIKA 28: ETINCELLES WAMEPA KONA AMBAYO HAIKUZAA MATUNDA.

DAKIKA 43: SIMBA BADO INAONGOZA BAO 1:0
DAKIKA 45: MAPUMZIKO, SIMBA WANAONGOZA BAO 1:0

KIPINDI CHA PILI COMING SOON

KIPINDI CHA PILI KIMEANZA

ETINCELLES WANAFANYA MABADILIKO ANATOKA ALANI ANAINGI DIEL HARUKIZIMANA

DAKIKA 53: SIMBA WANAKOSA GOLI

DAKIKA54: ETINCELLES WANAPATA KONA LAKINI HAINA MAFANIKIO

DAKIKA58: SIMBA WANAPATA KONA

DAKIKA 59:SIMBA WANAKOSA GOLI

DAKIKA YA 61: SIMBA WANAKOSA GOLI

DAKIKA 64: SIMBA WANAPATA KONA AMBAYO INAKOSAKOSA GOLI

DAKIKA66: SIMBA WANA PATA KONA AMBAYO HAIJAZAA MATUNDA

DAKIKA 67:SIMBA WANAFANYA MMASHAMBULIZI YA HATARI KATIKA LANGO LA ETINCELLES

DAKIKA 69 :SIMBA WANAFANYA MABADILIKO

DAKIKA 75:SIMBA WANAPATA GOLI LA PILI KUPITIA ISSA MGOSI

DAKIKA 78: SIMBA WANA KOSA GOLI

DAKIKA 81:BADO HALI TETE KWA ETINCELLES

DAKIKA 87: SIMBA WANAKOSA GOLI

DAKIA 89: SIMBA WANAKOSA GOLI

DAKIKA92 :SIMBA WANAPATA KONA BILA MAFANIKIO
DAKIKA 93:SIMBA IMEMTOA ETINCELLES KWA MABAO 2-O
NA MPIRA UMEMALIZIKA

VILABU VINANVYOHANGAIKA KUTAFUTA MSHAMBULIAJI-MWANGALIENI HUYU Souleymane Coulibaly.







Kombe la dunia la vijana chini ya umri wa miaka 17 linaendelea huko Mexico.
mpaka sasa majina ya vijana hawa yametokea kuteka hisia za mashabiki wengi wa soka ulimwenguni nao ni Hallam Hope wa England,Ademilson wa Brazil,Samed Yesil wa Germany

Carlos Fierro wa Mexico, lakini kati yao mshambuliaji Souleymane Coulibaly wa Ivory Coast ameibuka shujaa mpaka sasa,akiwa ameshaweka kambani jumla ya mabao 8 huku likiwa limesalia goli moja ili kuifikia rekodi ya mashindano ya kufunga mabao mengi kwenye shindano moja,rekodi iliyowekwa mnamo mwaka 2001 na mshambuliaji Sinama Pongolle aliyekuwa mfungaji bora kwa kufunga jumla ya mabao 9.

COUNTDOWN: DAVID HAYE ANA NAFASI GANI DHIDI VLADMIR KLITSCHKO? WASIKILIZE WATU WATATU PEKEE WALIOWAHI KUMCHAPA VLADMIR





Dunia nzima inazizima kwa msisimko ikingojea kwa hamu pambano la masumbwi la uzito wa juu baina ya Wladmir Klitschko toka Ukraine na David Haye toka England.Ni vigumu sana kutabiri mshindi wa pambano hili kwa sababu kila mmoja anafaida ambazo zinaweza kumsaida kupata ushindi na kila mmoja ana mapungufu ambayo yanaweza kumpa mpinzani wake faida hivyo mpaka sasa kila mtu ana ‘chance’ ya kushinda 50-50.
Ila katika hali halisi ya mtazamo wa rekodi za mabondi hawa wawili ni dhahiri kuwa Wladmir Klitschko ana angalau faida ya silimia chache dhidi ya Haye , faida hiyo ni rekodi bora ya kushinda mapambano 55 na kupoteza mapambano matatu na ukweli kuwa yeye ndiye bondia wa uzito wa juu aliyeshikilia mkanda kwa muda mrefu kuliko wote kwenye historia ya mchezo . Faida hizi zinamaanisha kuwa Wladmir Klitschko ana uzoefu mkubwa sana katika ngazi hii kuliko Haye . Turudi nyuma kidogo , kwenye rekodi hiyo hiyo utona kuwa Wladmir amepoteza mapambano matatu na mara ya mwisho kupoteza pambano ilikuwa miaka 7 iliyopita .Wladmir ni bondia wa aina yake na ndio maana kwa muda mrefu amekuwa hana mpinzani , na katika mapambano haya matatu aliyopoteza aliyapoteza haswa kwani kwa umahiri alio nao Wladmir basi hao jamaa waliompiga kweli jasho liliwatoka .






Ross Puritty, raundi ya 11, 5 Desemba 1998, Kiev





Vladimir Klitschko alikutana na dhahama la kipigo kwamara ya kwanza toka kwa Ross Purity, Katika pambano lililopigwa tarehe 5 desemba mwaka 1998 huko Kiev Ukraine nyumbani kwao kina Klitschko Ross Purity alimsimamisha Wladmir kwenye raundi ya 11. Kwa maneno yake mwenyewe Ross anasema kuwa hakujiandaa kwa pambano hili kwani halikuwa kwenye ratiba na lilitokea tu kwa sababu bondia aliyekuwa apigane na Wladmir alimumia na kujitoa kwenye pambano hivyo kuokoa mamilioni ya fedha za udhamini Ross Purity aliletwa kujaza nafasi . Mazingira ya hali ya hewa ya baridi yalimpa tabu sana Ross kwa kuwa hajazoea mazingira hayo na ukizingatia ukweli kuwa hakupata hata wiki mbili za kujiandaa aliambiwa tu kuwa wiki ijayo utaenda kiev kupigana na wala hakupata hata muda wa kutazama mikanda ya mapambano ya nyuma ya Wladmir na wala hakujua anaenda kukutana na bondia wa aiana gani ili aandae mbinu za kumkabili . Katika mazingira kama haya ‘game plan’ ya Ross Purity ilikuwa si kujaribu kutafuta ushindi kwa kutupa makonde mfululizo bali kumzuia Wladmir asimwangushe kwa makonde yake . Alichofanbya Ross ni kuweka guard muda wote , kuzuia ngumi za Wladmir zisimdhuru , hi iliimaanisha kuwa Wladmir alikuwa anshinda kwenye kila raundi kwa kuwa Ross alikuwa hatupi makonde ambayo yangempa pointi , ila hayo yalienda hadi raundi ya 11 ambapo Wladmir alikuwa amechoka na kona yake ikaomba pambano lisimamishwe na Ross Purity akapewa ushindi wa TKO yaani technical knock-out . Kimsingi kilichompa ushindi Ross ni ukweli kwamba Wladmir alitupa makonde mpaka kufikia hatua ambapo hakuweza tena kutupa konde kwa sababu alikuwa amechoka vibaya na akashindwa kuendelea . Uzoefu wa Ross Purity kumsoma Wladmir na kujua kuwa anachotakiwa kufanya ni kumchosha ndio ilikuwa siri ya ushindi wake.



Corrie Sanders, raundi TKO, 8 Machi 2003, Hanover

Mara nyingine ambayo Wladmir alikutana na kipondo ilikuwa tarehe 8 machi mwaka 2003 ambapo aligongwa na Corrie Sanders kwenye raundi ya pili ya pambano lililofanyika huko Hannover Ujerumani . Corrie Sanders alikuwa hajapata fight yoyote kwa muda wa takribani miaka miwili na hivyo katika hali ya kawaida hakuwa kwenye condition ya kimchezo . Ila kwenye mazoezi yake , Corrie alipigana na mabondia wenye maumbo makubwa na hilo lilimsaidia sana kwa sababu alipata mbinu za ziada za kumkabili mpinzani wake(Wladmir) ambaye naye ana umbo kubwa .Alichoona Corrie na kukitumia na footwork na movement mbovu za Wladmir ambazo ni kwa sababu ya umbo lake kubwa na pia wakati ambapo pambano linakuwa gumu kwake Wladmir hupandwa na hasira na anashindwa kufocus kwenye pambano jambalo ambalo linampunguza makali kwa kiwango kikubwa sana na kwa hilo Corrie aliongeza presha na kasi ambayo ilimshinda kabisa Wladmir na kumfanya apoteza pambano katika staili mbaya kuliko mapambano yote aliyopoteza . Corrie anasema kuwa “unapopigana na Wladmir unapaswa kutumia akili nyingi sana, ongeza presha kwa kutupa makonde , kwepa sana kwa kutumia movement ya miguu ambayo yeye mwenyewe hana na wakati mwignine unapaswa kumngoja aje kwa sababu pambano linapokuwa gumu anakuwa anapoteza focus na anakuja kwa hasira jambo ambalo linamfanya asiweke guard na hapo ndio unapopaswa kuchukua ushindi wako ”Anachosema Corrie Sanders ndio kitu alichokifanya kwenye pambano lao na hakika yote hayo yalitokea kwani Wladmir alipigwa ndani ya Raundi tatu. Aliangushwa mara ya kwanza na akasimama kwa hasira na pambano lilipoendelea akaja kwa nguvu zote akijaribu kudhihirisha kuwa Corrie hakumuumiza alipomuangusha na hilo lilimgharimu mno kwani kama hakuumizwa mara ya kwanza basi hakika aliumizwa mara ya pili na mwamuzi akasimamisha pambano .


Lamon Brewster, raundi TKO, 10 April 2004, Las Vegas

Mara ya mwisho Wladmir kushindwa mchezo ilikuwa mwezi aprili tarehe 10 mwaka 2004 huko Las Vegas dhidi ya Lamon Brewster . Lamon aliingia kwenye pambano hili dhidi ya Wladmir akiwa na mpango madhubuti na akiwa amejiandaa vya kutosha. Brewster alijua wazi kuwa hawezi kushinda kutupa makonde na Wladmir kwa sababu Wladmir ana akili na nguvu nyingi na anavitumia vitu hivyo kwa utaalamu mkubwa . Lamon alitazama mapambano karibu yote ya nyuma ya Wladmir na kujaribu kucheza na mapungufu yake . Nilitazama pambano lake dhidi ya Ray Mercer lililochezwa juni 2002 ambapo Wladmir alishinda kwenye raundi ya sita . Katika pambano hili Ray Mercer alikuwa anamshambulia sana Wladmir na japo alishinda lakini alishinda huku akiwa amechoka sana , hivyo alichofanya Lamon ni kufanya kama Ray kwa kuwa yeye ni mdogo kuliko Ray Mercer kwa tofauti ya miaka 12 na alikuwa na mbinu bora zaidi ya Ray na uwezo wa kuzitumia mbinu hiozo kwa sababu ya umri na u-fit wa mwili hivyo aliamini kuwa kama Ray Mercer alimchosha kiasi kile basi Lamon angekuwa na nafasi zaidi ya kumpiga Wladmir . Kama ilivyokuwa kwenye pambano la kwanza alilopoteza Wladmir alipigwa na Lamon kwa kuwa alilazimika kutupa makonde mengi ambayo yalimchosha sana kwa sababu Lamon alikuwa akimfuata sana karibu kila raundi na kumfanya aamini kuwa angeweza kumshinda na hivyo ili kumshinda Lamon Wladmir alitupa makonde mengi sana hali ambayo ilimchosha vibaya . Baada ya pambano hilo timu ya Klitschko ilitoa kisingizio kuwa alipewa sumu kwenye chakula (food poisoning) lakini ukweli ni kuwa Wladmir alijichosha mwenyewe kwenye raundi nne ambazo alitupa makonde mengi kupita uwezo wake mwenyewe na kwenye raundi ya tano Lamon alimmaliza .
Ni dhahiri kwamba Wladmir Klitschko ni mtihani mgumu kuliko yote aliyowahi kukutana nayo na atakayowahi kukutana nayo kijana wa Kiingereza David Haye . Wengi wanaamini kuwa bondia mrefu kuliko wote Nikolay Valuev alikuwa mtihani mgumu kwa haye lakini si hivyo kwa sababu Valuev ni mvivu sana , hana movement nzuri, yuko slow tofauti na Haye ambaye ni kinyume cha hapo kwani yeye ni mwepesi zaidi na ana kasi ya ajabu hivyo alimmudu vyema Valuev . Wladmir Klitschko ni mtu mwenye uzoefu mkubwa sana , na amejifunza kutokana na mapambano ambayo amepoteza na ndio maana kwa miaka saba sasa hajapoteza mchezo wowote , amejijenga na kuyadhibiti mapungufu yake ambayo yalimfanya apoteze michezo hiyo mitatu pekee aliyopoteza hadi leo hii na ndio maana ili kushinda David ana kazi kubwa ya kufanya .
Upande wa pili kambi ya Klitschko imekiri kuwa kijana wao hajawahi kukutana na mtu ambaye anajiamini kama Haye , hii inamaanisha kuwa maneno ambayo Haye amekuwa akiyatoa kumkejeli Wladmir yamemuingia kichwani na yanamsumbua jambo ambalo huenda likampa Haye faida kisaikolojia kwani anampotezea Wladmir focus ya mchezo . Gwiji wa ngumi wa England Lenox Lewis amesema kuwa kama Haye anataka kushinda basi lazima ahakikishe anamchapa Wladmir kwa knock out kwa sababu ni njia hiyo pekee ambayo itampa ushindi kwa sababu akisema awategemee majaji na mwamuzi hali itakuwa ngumu kwake kwani anaenda Ujerumani kama mgeni na Wladmir yuko nyumbani hivyo kuna uwezekano mkubwa kuwa maamuzi makubwa yatakuwa ya faida kwa bondia wa nyumbani . Gwiji mwingine Mike Tyson yeye amesema kuwa haoni ni jinsi gani Haye anaweza kumshinda Bondia kwenye mchanganyiko wa nguvu na akili kaka Wladmir Klitschko . Sababu yake kuu ni uzoefu alio nao kijana toka Ukraine .
Ukweli kuwa hatutashuhudia pambano jingine kama hili kwa muda mrefu sana kama ambavyo imetuchukua miaka trakribani 10 kupata pambano hili ni kitu kitakacholifanya liwe la kipekee , na kwenye boxing tuna msemo mmoja unaosema kuwa “the punches will be the only talk when tha rounds begin” yaani makonde ndio pekee yatakayotoa sauti wakati raundi zikianza na hapo ndio maneno na tambo zote zitakapofikia ukomo .

Malota Soma:Mpachikaji mabao wa zamani wa Simba aliyekuwa na chenga za maudhi.

KLABU ya SC ya Dar es Salaam ni miongoni mwa timu za hapa nchini ambayo kwa miaka mingi imebahatika kuwa na washambuliaji mahiri ambao kwa kipindi kirefu wameiletea mafanikio makubwa klabu hiyo yenye maskani yake Mtaa wa Msimbazi.

Mmoja wa washambuliaji ambaye alivuma sana kwa kipindi kirefu akiwa na klabu hiyo kati ya mwaka 1981 mpaka 1991 na kuiletea mafanikio makubwa ni mshambuliaji machachari na mwenye chenga za maudhi Malota Soma.

Umahiri wa mchezaji huyu ulitokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao wa kupiga chenga za maudhi, kufunga mabao na kusababisha kupatikana kwa mabao kwa timu yake na kutokana na sababu hiyo wapenzi wa soka nchini walimbatiza jina la ‘Ball Juggler’ wakimaanisha kuwa alikuwa na uwezo wa kuchezea mpira atakavyo.

Malota kwa hivi sasa hasikiki na wala haonekani viwanjani kama zamani, kwa sababu amestaafu kucheza soka ya ushindani mwaka 1999 akiwa na timu ya Tanzania Stars ambayo inashirikisha wachezaji wa zamani waliostaafu kucheza soka ya ushindani.

Ukilinganisha uwezo wa mshambuliaji huyu Malota Soma na wachezaji wa sasa wa klabu ya Simba ni tofauti kabisa, kwani licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kupiga chenga za maudhi, pia alikuwa na uwezo mkubwa wa kupachika mabao.

Umahiri wa Malota katika soka ulikuwa mkubwa mno, kwani alikuwa na uwezo wa kucheza nafasi zote za ushambuliaji, kuanzia winga zote mbili saba na kumi na moja na katikati tisa na kumi.

Licha ya uwezo mkubwa aliokuwa nao Malota wa kupachika mabao, pia washambuliaji wenzake wa Simba aliokuwa akicheza nao pia nao walikuwa na uwezo mkubwa wa kupachika mabao ulinganisha na safu ya ushambuliaji ya Simba ya hivi sasa.

Katika kipindi hicho wakati Malota Soma anacheza soka katikati kulikuwa na washambuliaji wawili ambao pia walikuwa na uwezo mkubwa wa kupachika mabao ambao ni Zamoyoni Mogela ‘Golden Boy’ na Edward Chumila (marehemu) wakati winga ya kushoto kulikuwa na winga machachari na mwenye kasi Sunday Juma.

Washambuliaji wote hawa walikuwa na uwezo wa kupachika mabao kama alivyokuwa Malota Soma ‘Ball Juggler’ na mwiba mkali kwa mabeki wa timu pinzani waliokuwa wakikabiliana nao na hasa Zamoyoni Mogela ambaye wapenzi wa soka nchini walimbatiza jina la ‘Golden Boy’.

Akizungumzia mechi anayoikumbuka zaidi wakati anacheza soka ya ushindani, Malota Soma anaitaja mechi iliyokutanisha timu yake ya Simba dhidi ya National Al- Ahly FC ya Misri, mchezo uliochezwa katika uwanja wa CCM Kirumba Mjini Mwanza mwaka 1985.

Mchezo huo ulikuwa ni wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika na matokeo ni kwamba Simba waliibuka washindi kwa kuwafunga National Al-Ahly ya Misri mabao 2-1.

Mechi hiyo Malota Soma anaikumbuka vizuri mno mpaka leo hii kwa sababu, licha ya yeye kutofunga goli siku hiyo, lakini alicheza vizuri mno na yeye ndiye aliyetoa pasi kwa mfungaji wa bao la kwanza Zamoyoni Mogela ‘Golden Boy’. Bao la pili na la ushindi siku hiyo lilifungwa katika dakika 15 hivi kabla ya mchezo kumalizika na kiungo mahiri Mtemi Ramadhani.

Kwa ushindi huo, Simba waliondoa ile dhana iliyokuwa imejengeka miongoni mwa wapenzi wa soka nchini kuwa timu za Tanzania haziwezi kuzifunga timu za Misri.

Kihistoria Malota Soma alianza kujulikana katika ulimwengu wa soka mwaka 1977 alipomaliza elimu ya Msingi aliposajiliwa na klabu ya daraja la pili iliyojulikana kwa jina la Jogoo FC ya Mjini Morogoro.

Mwaka 1978 Malota Soma alihama timu ya Jogoo FC na kujiunga na Reli FC pia ya Morogoro iliyokuwa inashiriki ligi daraja pili wakati huo. Baadhi ya wachezaji maarufu aliokuwa nao Reli ni kama Zamoyoni Mogela ‘Golden Boy’, Ali Jangalu, Stephen Mdachi, Sospeter Mwaluko na Ayoub Kahewanga.

Mwaka 1979 Malota Soma alihama klabu ya Reli na kujiunga na Tumbaku FC pia ya Morogoro iliyokuwa ikishiriki ligi darala la pili wakati huo. Baadhi ya wachezaji maarufu aliokuwa nao Tumbaku ni John Simkoko, Zamoyoni Mogela, Thobias Nkoma (marehemu), Shabani Mussa, Bona Bruno na Hussein Ngulungu.

Malota akiwa Tumbaku mwaka huo huo wa 1979 alichaguliwa kwa mara ya kwanza timu ya Taifa ya vijana iliyokuwa ikinolewa na kocha mzoefu Mohamed Msomali.

Baadhi ya wachezaji aliokuwa nao timu ya Taifa ya vijana ni Abdul Amasha, Hussein Iddi, Thobias Nkoma (marehemu), Zamoyoni Mogela ‘Golden Boy’, Ayoub Mzee, Sospeter Mwaluko na Juma Kiruzeruze.

Malota Soma alikaa na timu ya Tumbaku miaka miwili ambapo mwaka 1981 alihama timu hiyo na kujiunga na Simba SC ya Dar es Salaam maarufu kama ‘Wekundu wa Msimbazi’.

Baadhi ya wachezaji aliowakuta Simba na kucheza nao ni Mohamed Kajole ‘Machela’ (marehemu), Daudi Salum ‘Bruce Lee’, George Kulagwa, Sunday Juma, Mohamed Bakari ‘Tall’, Rahim Lumelezi, Abbas Kuka, Nico Njohole, Mussa Kiwhelo (marehemu), Thobias Nkoma (marehemu) na wengine wengi.

Mwaka huo huo wa 1981 Malota akiwa na klabu ya Simba alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuchezea timu ya Mkoa wa Dar es Salaam maarufu kama Mzizima United na katika michuano ya Taifa Cup ya mwaka huo Mzizima United ilitwaa taji la hilo.

Malota Soma alikaa na klabu ya Simba miaka 10 mfululizo , kabla ya mwaka 1991 kutimkia nchini Oman kucheza soka la kulipwa katika klabu ya daraja la kwanza Sohari FC.

Alirudi nchini mwaka 1993 na kujiunga na klabu yake ya zamani ambayo safari hii alikaa nayo misimu mitatu ambapo mwaka 1997 alijiunga na timu ya Tanzania Stars ambayo inashirikisha wachezaji wa zamani.

Malota Soma alistaafu kucheza soka ya ushindani mwaka 1999 na klabu yake ya mwisho kuichezea ilikuwa ni Tanzania Stars. Anasema kuma aliamua kustaafu kucheza soka ya ushindani ili kuwaachia vijana chipukizi waonyeshe vipaji vyao.

Thursday, June 30, 2011

KAGAME CASTLE CUP: YANGA 2-0 ELMAN


yanga wakishangilia bao.





Mshambuliaji wa Yanga, Davies Mwape (kulia) akitafuta mbinu za kutoka beki wa
Elman FC, Mohamed Hassan Ali wakati wa mchezo wa Kombe la Kagame Castle kwenye
uwanja wa Taifa Dar es Salaam leo


Kiungo Mshambuliaji wa Yanga, Nurdin Bakari akimtoka mchezaji wa Elman FC ya
Somalia, Saad Salah Hassein wakati wa mchezo wa Kombe la Kagame uliofanyika
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo



kikosi cha Yanga.

kikosi cha Elman ya Somalia

ESTHER CHABRUMA: TFF ANZISHENI LIGI KUU YA WANAWAKE


Naibu Mkurugenzi Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Juliana Yassoda
akimkabidhi bendera ya taifa nahodha wa timu ya taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’
Sophia Mwasikili wakati wa kuiaga timu hiyo inayokwenda Zimbabwe kushiriki
michuano ya COSAFA



CHENGA za maudhi, kasi na uwezo wa kumiliki mpira uwanjani vilimwezesha kupata umaarufu mkubwa katika muda mfupi kupitia soka la wanawake.

Mwonekano wake, mfupi na mwenye mwili wa wastani, pia ulisaidiwa kubatizwa jina lililozoeleka kama utambulisho wake kwa mashabiki wengi ndani na nje ya uwanja.

Huyu si mwingine bali ni Ester Chabruma, kiungo mshambuliaji wa timu ya soka ya Sayari FC na ile ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’.

Wengi hupenda kumuita Lunyamila wakimfananisha na mshambuliaji wa zamani wa Yanga Edibily Lunyamila ambaye alijizolea sifa kubwa wakati akisakata kabumbu.

Kwa sasa Ester ndiye mchezaji pekee mkongwe wa kikosi cha sasa cha Twiga Stars inayojiandaa kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake Oktoba mwaka huu, ameweza kuwamo katika kikosi hicho kwa miaka nane mfululizo tangu mwaka 2002.

Ester alizaliwa Julai 21, mwaka 1987, na kuanza kucheza soka akiwa na umri wa miaka nane katika timu ya watoto ya Sayari kisha ya wakubwa na kuendelea na timu hiyo hadi sasa, akiwa hajawahi kucheza klabu nyingine yoyoye hapa nchini.

"Tangu nilipojiunga na Sayari mwaka 1995 baada ya kuletwa na kaka yangu, sijaihama timu hiyo na sitarajii kuihama labda niende nje ya nchi," anasema Ester.

Akielezea maisha yake ya soka, Ester anasema kuzaliwa akiwa wa katikati ya kaka zake wawili ndicho kitu kikubwa kilichomfanya hadi akawa anapenda kucheza mpira wa miguu kwani alikuwa akienda na kaka zake katika michezo yao, huku mchezo mkubwa ukiwa wa mpira wa miguu.

"Kutokuwa na dada wa kucheza nae, kulinifanya niwe kila mahali na kaka zangu wakienda sehemu nami nimo wakicheza mpira wa miguu nami nimo, tangu hapo nikawa nacheza nao sambamba hadi kaka aliponileta Sayari," anasema Ester.

Katika historia yake ya soka, Ester alipata timu ya kucheza soka la kulipwa nchini Sweden ambako alicheza kwa misimu mitatu, kabla ya kurejea nchini.

"Nilipokuwa Sweden nilicheza katika ligi daraja la tatu nikiwa na klabu ya soka ya wanawake inayoitwa Kotodara FC katika misimu mitatu tangu mwaka 2003-06, maisha katika klabu ile yalikuwa mazuri sana ukilinganisha na hapa nchini," anasema.

Anasema Sweden ina mfumo mzuri wa ligi ya wanawake, ina ligi kuanzia Daraja la Nane hadi kufikia ligi kuu, ina timu nzuri ya taifa ya wanawake yenye wachezaji ‘professional’ kutoka klabu mbalimbali za ligi hiyo.

Anaongeza kuwa Sweden hata klabu za wanawake zinakuwa na viwanja vyao vya mazoezi na kuchezea mechi za ligi, kuliko hapa kwetu timu hazina viwanja hata vya kufanyia mazoezi.

"Nimejifunza mengi kupitia timu ile ndiyo maana hadi sasa sijaacha mpira, nikiwa kule nilipata mafunzo ambayo yananisaidia katika maisha ya mpira hadi sasa, yameniongezea kujiamini zaidi katika kazi yangu," anasema Ester.

Akielezea ilikuwaje hadi akarudi nchini Ester, anasema mkataba wake wa kuendelea kucheza katika timu hiyo uliisha, hivyo akarejea nchini Septemba, 2006 na kurudi tena katika timu yake ya Sayari hadi sasa.

Ester mmoja wa wachezaji wa kikosi kilichoundwa kwa mara ya kwanza cha Twiga Stars mwaka 2002 kwa ajili ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanawake mwaka huo.

Ester alikuwa ni mmoja kati ya wachezaji walioiokoa Twiga Stars kufuzu kucheza hatua ya pili ya michuano hiyo kwa kufunga bao la ushindi katika dakika ya 89 ya mchezo dhidi ya Eritrea kwa kuwa na ushindi wa 3-2 huku mechi ya kwanza wakiwa wametoka sare ya mabao 2-2, hivyo Twiga ilifanikiwa kuingia hatua ya pili kwa jumla ya mabao 5-4 lakini walitolewa na Zimbabwe katika hatua hiyo.

"Ushindi ule ulikuwa muhimu kwetu, ikiwa ni mara ya kwanza kushiriki katika michuano mikubwa kama hiyo, najivunia mpaka sasa kwa kutumia nafasi ile vizuri," anasema Ester.

Akizungumzia tofauti iliyopo katika Twiga Stars ya mwaka 2002 na Twiga ya mwaka 2010, Ester anasema timu ya kipindi kile ilikuwa ikiundwa na wachezaji wengi wa klabu moja ya Sayari na wachezaji walikuwa na umri mkubwa lakini Twiga ya sasa inaundwa na wachezaji wadogo wanajua kucheza mpira pia wametoka katika klabu tofauti tofauti.

“Katika kikosi chetu mchezaji wa zamani ni mimi peke yangu niliyebaki hadi sasa, wengine hawapo katika timu ya taifa, wapo waliokufa, wengine wanacheza katika timu mbalimbali na wengine wamestaafu na kuachana na mpira kabisa,” Ester.

Ester ambaye ana matarajio ya kucheza kwa miaka mingine zaidi, anasema alipewa jina la mchezaji wa zamani wa Yanga, Edibily Lunyamila kutokana na uchezaji wake, anasimulia jinsi alivyolipokea jina hilo.

"Sikuwa na jinsi ya kulikataa jina hilo ambalo lilinipa changamoto zaidi kwa kufananishwa na mchezaji mzuri kama Lunyamila, watu walisema tunafanana uchezaji, nafasi za uwanjani (wote washambuliaji), tunatumia mguu wa kushoto hivyo sikuona sababu ya kulikataa jina hilo," anasema Ester.

Akizungumzia mechi ya Twiga Stars dhidi ya Eritrea itakayochezwa hivi karibuni baada ya kuiondosha Ethiopia katika michuano ya kuwania nafasi ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake baadaye huko Afrika Kusini ambapo Twiga ilishinda jumla ya mabao 4-2 katika mechi zote mbili, Ester anasema; "Tulikuwa na uhakika wa kufanya vizuri kwani Eritrea haikuwa timu ya kutisha sana.”

Ester ametoa wito kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Chama cha Soka cha Wanawake Tanzania (TWFA) kuanzisha ligi kubwa ya soka la wanawake, ili kutafuta vipaji vipya zaidi huku akiamini wapo wachezaji wa kike wenye uwezo zaidi yake, lakini hawajapata nafasi ya kuonyesha uwezo wao, hivyo kupitia ligi kubwa wataonekana wengi.

Mshambuliaji huyo wa pembeni amewataka wazazi wawape nafasi watoto wao wa kike waweze kucheza mpira wa miguu kwani siyo uhuni kama wanavyodhani pia amewaasa wachezaji wa kike wasiwe na aibu ya kujitokeza kucheza, wajiamini na kuongeza kuwa wakiwa na juhudi watafanikiwa.

makala ya timu ya taifa ya Tanzania ( twiga stars ).



Thomas Ulimwengu: Nampenda sana ALICIA KEYS.

Number 10: Umezaliwa mwaka gani na wapi?
Ulimwengu: Nimezaliwa tarehe 14/6/1993, Dodoma .

Number 10: Ulianza kucheza timu gani kabla ya kujiunga na Moro United?
Ulimwengu: Nilitokea katika michuano ya Copa Coca Cola 2008, nikitokea Dodoma baada ya michuano nikaitwa Tanzania Soccer Academy ndipo nilipoenda Moro United.

Number 10: Wakati unakua ni timu gani ulikuwa ukiipenda sana hadi sasa?
Ulimwengu: Manchester United ya England .

Number 10: Unapokuwa uwanjani kitu gani hutumia kama silaha kwako?
Ulimwengu: Kasi (speed) na kupia mashuti makali niwapo uwanjani

Number 10: Mapungufu gani umeyagundua pindi uwapo uwanjani?
Ulimwengu: Nasumbuliwa sana na mabeki wa timu pinzani japokuwa sipendi hali hiyo.

Number 10: Mchezaji gani unamchukulia kama shujaa kwako?
Ulimwengu: Didier Drogba wa Chelsea na Mussa Hassan Mgosi wa Simba.

Number 10: Nini matarajio yako katika mpira wa miguu?
Ulimwengu: Kuwa mchezaji wa kulipwa nje ya nchi.





Number 10: Katika kucheza mpira ni siku gani ulihuzunika sana ?
Ulimwengu: Siku nilipoumia nyonga, nilipata maumivu makali sana sitakuja kusahau.

Number 10: Kitu gani kilikushawishi hadi ukaamua kuwa mchezaji?
Ulimwengu: Mpira ulikuwa ni ndoto yangu hivyo nilitaka siku moja kuitimiza.

Number 10: Nani alikushawishi uendelee kucheza mpira?
Ulimwengu: Marafiki zangu mbalimbali walinishauri, nikaamua kuendelea.

Number 10: Ulijisikiaje ulipoanza mazoezi na Tanzania Soccer Academy ?
Ulimwengu: Nilijisikia furaha na kuamini kuwa ndoto zangu za kuwa mchezaji zinaanza kutimia.

Number 10: Kwanini uliamua kuvaa jezi namba 11?
Ulimwengu: Kutokana na washambuliaji wengi kuvaa namba 11 nami nikiwa mshambuliaji nikaona nastahili kuvaa namba hiyo.
Number 10: Mchezaji gani unamuona bora kwa sasa?
Ulimwengu: Didier Drogba wa Chelsea

Number 10: Mchezaji yupi unamuona mtukutu lakini anafurahisha na kuwa kiburudisho katika timu?
Ulimwengu: Ni Keiko Master, tupo naye TSA huyu ni mtundu kupita kiasi ila ni muhimu sana katika kikosi chetu.

Number 10: Unapenda aina gani ya muziki pindi unapokuwa umepumzika?



Brad Pitt


Ulimwengu: Muziki wa taratibu ‘blues’, napenda pia nyimbo za mwanamuziki Timberland wa Marekani.

Number 10? Ukifanikiwa kupata fedha ungependa kununua gari aina gani?
Ulimwengu: Napenda sana Range , ni gari zuri sana hasa kwa barabara zetu hapa Tanzania .

Number 10: Mwanadada gani unamhusudu sana ?
Ulimwengu: Nampenda sana mwanamuziki anayeitwa Alicia Keys, anaimba vizuri sana .

Number 10: Ni filamu ipi unaipenda na kwa nini?
Ulimwengu: Napenda filamu ya Mr and Mrs Smith ya Angelina Jolie na Brad Pitt inafundisha na kuburudisha hasa kwa vijana.

Number 10: Unaweza kutueleza jambo lolote tusilolifahamu kuhusu wewe:
Ulimwengu: Sipendi kuongea ongea kila mara, mimi ni mkimya sana ila marafiki zangu hawalijui hilo .

Number 10: Unaonekana bado kijana mdogo, unasoma?
Ulimwengu: Nimemaliza kidato cha nne mwaka jana 2009.
Number 10: Kama usingekuwa mwanamichezo ungependa ufanye kazi gani?
Ulimwengu: Nilipenda kuwa mchezaji hivyo sikupanga kufanya kazi nyingine

Number 10: Ukipata nafasi ya kuchagua mchezaji wa kucheza nae, ungependa ucheze na nani?
Ulimwengu: Ningependa kucheza na mchezaji Steven Gerrard kwa kuwa ana uwezo wa kutoa pasi vizuri.



Alicia Keys


Number 10: Kipindi gani cha runinga cha vijana unachokipenda?
Ulimwengu: Vipindi vyote vya michezo, pia taarifa za habari za michezo.

Number 10: Kipindi gani cha michezo cha redio unachopenda kukisikiliza?
Ulimwengu: Sports Extra cha Clouds FM watangazaji wanajua kuchambua michezo kwa ufasaha.



SOURCE: NUMBER10 FOOTBALL MAGAZINE.


Wednesday, June 29, 2011

UBAVU WA KUSHOTO WA KIPA MPYA WA MAN UNITED

Ulimwengu mzima una taarifa za Manchester United kumsajili kipa kinda David De Gea kama mrithi wa Edwin Van Der Saar . Kuna jambo moja ambalo limewapita nalo ni rafiki wa kike au mpenzi wa De Gea . Kama inavyotambulika kuwa marafiki wa kike , wapenzi na wake wa wacheza soka ni ‘hot cake’ nchini England na hakika mpenzi wa De Gea anaingia moja kwa moja kwenye mkumbo huo . Binti mwenye umri wa miaka 25 Edurne ndiye mpenzi wa De Gea na hajaupata umaarufu kwa ajili ya De Gea kwani na yeye ni maarufu kwa upande wake kutokana na kazi anayoifanya ambayo ni uimbaji . Tazama clip ya video yenye wimbo wake hapo chini na ndio utakapotambua kuwa De Gea anakuja Old Trafford si tu kuchukua namba iliyoachwa wazi na Edwin Van Der golini bali amekuja kuchukua ufalme uliochwa wazi na David Beckham na malkia wake posh spice .­
http://www.youtube.com/v/wD3FY2fOd7Q?version=3&hl=en_US">

EXCLUSIVE: COCKTAIL PARTY YA ANDY COLE.

juma katunda ( cameraman wa sports bar ya clouds tv) akiwa na nick humphrey



aidan seif mmoja wa 'ma-engineer' wa blog akiwa na mkurugenzi wamahusiano wa Man utd mr nick humphrey

duuuh kweli milima haikutani ila binadamu hukutana....'yorke' unafanya nini huku ?,inaelekea ndivyo andy cole anavyomshangaa mtangazi wa kipindi cha jahazi cha clouds fm mr kibonde kwa jinsi anavyoonekana kufanana kisura na mshambuliajiwa zamani wa man utd dwight yorke.

wafanyakazi wa kampuni ya AIRTEL wakipiga picha ya pamoja na gwiji wa soka Andy Cole.


HAPA NIKIWA NA MWENYEKITI WA KLABU YA SIMBA MHESHIMIWA ADEN RAGE.


'AISEE KIJANA KWA UMRI WAKO WA MIAKA 40 UNAWEZA KUTUSAIDIA SANA SIMBA KWENYE SAFU YA USHAMBULIAJI....MADARAKA SELEMAN ALICHEZA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 42 SEMBUSE WEWE TENA UMECHEZEA MANCHESTER UTD ? NJOO MSIMBAZI BWANA!!!'


MIMI,GEOFREY LEA NA KATIBU MKUU WA TFF ANGETILEH OSEAH TUKIWA NA ANDY COLE MARA BAADA YA MAHOJIANO.


MDAU FARAJA MASSAWE WA ACTIVE TOOURS KAMPUNI ILIYOKUA NA JUKUMU LA KUMTEMBEZA ANDY COLE.

WDAU WA BLOG HII WALIOSHINDA COMPLEMENTARY YA KUKUTANA NA ANDY COLE KUPITIA SPORTS XTRA YA CLOUDS FM WAKISAINIWA KWENYE OUTOGRAPH ZAO NA ANDY COLE.


GEOFREY LEA MMOJA WA 'MA-ENGINEER' WA HII BLOG AKIJINAFASI NA ANDY COLE.

ANDY COLE AKIHUTUBIA WAGENI WAALIKWA KWENYE SHEREHE YAKE YA VINYWAJI NA VITAFUNWA.

ANDY COLE AKITETA JAMBO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA AIRTEL TZ,SAM ELANGAALLOOR KWENYE CORKTAIL PARTY ILIYOFANYIKA HOTEL YA KEMPINSKI.

ANDY COLE AKIINGIA KWENYE UKUMBINI KUKUTANA NA WADAU WAKE.



NIKIWA NA WAFANYAKAZI WA AIRTEL TANZANIA.




KELVIN TWISSA ( KUSHOTO), OBINNA ANICHE ( KATI ) PAMOJA NA MDAU.






















AIRTEL NA MAN UNITED WAZINDUA PROGRAM YA “AIRTEL RISING STARS”




KAMPUNI YA SIMU YA AIRTEL TANZANIA KWA KUSHIRIKIANA NA KLABU YA MANCHESTER UNITED LEO IMEZINDUA PROGRAM YA KUIBUA VIPAJI VYA SOKA NCHINI TANZANIA KUANZIA NGAZI YA CHINI HADI TAIFA.


PROGRAM HIYO INAFAHAMIKA KAMA AIRTEL RISING STARS INAJUMUISHA BARA ZIMA LA AFRICA ILI KUWEZA KUTOA NAFASI KWA WANASOKA CHIPUKIZI CHINI YA UMRI WA MIAKA 17 KUONYESHA UWEZO WAO MBELE YA MAWAKALA WA SOKA NA MAKOCHA ILI KUWEZA KUPATA FURSA YA KUJIENDELEZA ZAIDI.MPANGO UNAWAHUSISHA WASICHANA NA WAVULANA.


PROGRAM HII HAPA TANZANIA ITAFANYIKA KATIKA MIKOA YA DAR, MOROGORO, MWANZA NA ARUSHA IKISHIRIKISHA VIJANA ZAIDI YA 500 AMBAPO WAWILI KATI YA HAO WATACHAGULIWA KUJIUNGA NA KLINIKI YA SOKA ITAKAYOFANYIKA NCHINI GABON NA TANZANIA CHINI YA USIMAMIZI WA JOPO LA MAKOCHA KUTOKA MANCHESTER UNITED.


PIA KAMPUNI YA AIRTEL AMBAYO INA MKATABA WA KUIDHAMINI MANCHESTER UNITED KWA MIAKA 4 IMESEMA ITAFANYA KAZI NA WIZARA YA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO PAMOJA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA(TFF) KATIKA KUTEKELEZA PROGRAM HII YA AIRTEL RISING STARS.




MKUU WA SHULE YA MAKONGO MAJOR SELESTINI MWANGASI AKIWA NA MANAGING DIRECTOR WA AIRTEL TZ SAM ELANGALOOR,ANDY COLE, NAIBU WAZIRI WA HABARI,VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO FENELLA MUKANGARA PAMOJA NA NICK HUMPHREY.













ANDY COLE AKISHIRIKIANA NA NAIBU WAZIRI WA MICHEZO FENELLA MUKANGARA AKIWA KMURUGENZI MTENDAJI WA KAMPUNI YA SIMU ZA MIKONONI YA AIRTEL TZ SAM ELANGALOOR WAKIZINDUA JEZI ZITAKAZOTUMIKA KATIKA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS


ANDY COLE AKIWA ANACHEZA MPIRA PAMOJA NA WACHEZAJI WA SHULE YA MAKONGO KATIKA KUASHIRIA UZINDUZI WA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS-LEO MCHANA KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA SEKONDARI YA MAKONGO-JIJINI DSM



MOJA YA VITU AMBAVYO ANDY COLE AMEVIGUNDUA HARAKA NI MAGOLIKIPA WA TIMU YA SHULE YA MAKONGO KUKOSA MISINGI YA UGOLIKIPA.HIVYO ALIMSHAURI MWALIMU WA MICHEZO WA SHULE HIYO AWEKE MKAZO KUTATUA TATIZO HILO. KWENYE PICHA NI NICK HUMPHREY AKIMPA MAZOEZI MMOJA WA MAKIPA WA MAKONGO.


ANDY COLE AKIWAPA MAELEKEZO WACHEZAJI WA SHULE YA MAKONGO


MANAGING DIRECTOR WA AIRTEL TZ MR SAM ELENGALLOR (KATIKATI ) AKIONGEA NA BAADHI YA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA AIRTELWALIOKUWA KATIKA MSAFARA WA ANDY COLE KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA MAKONGO.



ANDY COLE AKIWA NA WACHEZAJI WA SHULE YA MAKONGO KWENYE UZINDUZI WA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS.



MARKETING EXECUTIVE WA AIRTEL MARY KIMARIO (KUSHOTO ) AKIPATA PICHA NA ANDY COLE KATIKA OFISI ZA AIRTEL TZ


MWAKILISHI WA JOPO LA MAKOCHA WA MAN UNITED NICK HUMPHREY (KUSHOTO )PAMOJA NA ANDY COLE WAKIONGEA NA MKURUGENZI WA MAWASILIANO WA KAMPUNI YA SIMU ZA MIKONONI YA AIRTEL BI BEATRICE SINGANO WAKIWA MAKAO MAKUU YA KAMPUNI HIYO.