Search This Blog

Saturday, September 10, 2011

ROONEY NA CHICHARITO WAPELEKA MSIBA BOLTON



Manchester United imeendelea kutoa dozi nzito katika ligi kuu ya England baada ya kuwakandamiza Bolton kwa mabao matano kwa bila.

Shukrani ziwaendee Javier Hernandez aliyefunga mabao mawili na Wayne Rooney aliyefunga matatu, na kumfanya kufikisha hat tricks ya saba tangu aanze kucheza soka la ushindani kwa ngazi ya klabu.

JULIO AITA JESHI LA WACHEZAJI 24 WA KWENDA BRAZIL


KOCHA msaidizi wa timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Jamhuri Kihwelo, ameita wachezaji 24 ambao wataingia kambini jumapili kujiandaa na
mashindano ya Copa cocacola yatakayo fanyika nchini Brazil hapo baadae.

Julio kabla ya kuwataja wachezaji hao 24 alisema safari ya kwenda Brazil ipo lakini itakuja kuthibitishwa na Cocacola ambao ni wadhamini wa safari hiyo ya mafunzo na mashindano nchini Brazil. Msafara huo utakuwa na watu 18 huku wachezaji wakiwa 16 na viongozi wawili.

Kikosi hicho kinatarajiwa kuanza mazoezi Jumatatu na hapo baadae watachujwa na kubakia 16 watakao safiri. Wachezaji hao ni pamoja na Paulo John (Morogoro), Hamad Hamad (kinondoni), Mohamed H. Mohamed (kinondoni), Peter Manyika (Temeke), Ismail Gambo (Kigoma), Miraji Adam (Morogoro).

Wengine ni Basil
Seif (Morogoro), Huseni Twaha (Tanga), James Ambros (Morogoro), Aishi Salum (Morogoro), Hashim Mwalo (kigoma), Mohamed Salum (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Dar es salaam), Mbwana Hasani (kinondoni), Salvatory Rafael (kigoma), Paulo James (Shinyanga), Huseni Ibrahim (Morogoro), Gabson Nyamtema (kigoma), Mohamed kapeta (temeke), Joseph Kimwaga (kinondoni).

MATOKEO YA ENGLISH PREMIER LEAGUE


FULL-TIME: Arsenal 1-0 Swansea

Goal: Arshavin


FULL-TIME: Stoke 1-0 Liverpool

Goal: Jonathan Walters (p) 21'


FULL-TIME: Everton 2-2 Aston Villa

Goals:Leon Osman,19 – Stilian Petrov 63

Leighton Baines(p) 68 – Gabriel Agbonlahor 83’


FULL-TIME: Manchester City 3-0 Wigan

Goals:Sergio Aguero, dk 13, 63, 69.


FULL-TIME: Wolves 0-2 Tottenham

Goals: Adebayor 67’, Defoe 80


FULL-TIME: Sunderland 1 - 2 Chelsea

Goals: Ji Dong-Won 90' - John Terry 18’

Daniel Sturridge

YANGA WATOKA SULUHU NA RUVU SHOOTING

MABINGWA WATETEZI WA VODACOM PREMIER LEAGUE DAR YOUNG AFRICANS WAMEENDELEA KUJIWEKA KWENYE HALI MBAYA KATIKA HALI NGUMU YA KUTETEA UBINGWA WAO BAADA YA KUTOKA SARE YA BAO MOJA KWA MOJA DHIDI YA RUVU SHOOTING, KATIKA MECHI ILIYOCHEZWA LEO KWENYE UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR-ES SALAAM.

Katika mchezo wa leo wa ligi kuu ya vodacom Yanga walimaliza mchezo wakiwa pungufu baada ya Mnywarandwa Haruna Niyonzima kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika 64 ya mchezo.

Timu hizo zilikwenda mapumziko wakiwa suluhu pacha, huku mchezo ukiwa na kasi ya kawaida na kosa kosa ndogo.

Katika kipindi cha pili kipa wa Yanga Yew Berko alifanya kazi ya ziada ya kuokoa michomo mitatu ya Ruvu Shooting kabla ya kuandika goli maridadi la kuongoza katika dakika 74.

Dakika 6 baada ya goli hilo Kenneth Asamoah aliisawazishia Yanga goli na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare 1-1.

Kwa matokeo hayo Yanga wanabaki mkiani mwa ligi huku wakiwa wametimiza siku 65 kucheza bila kushinda mchezo wowote na ukiwa mchezo wa 8 kucheza bila ya kutoka na ushindi.

Friday, September 9, 2011

msimu uliopita Sunderland ni moja ya timu zilizoitesa Chelsea..

Chelsea chini ya Andre Villas Boas wamecheza michezo mitatu ambayo hadi sasa wamejikusanyia pointi 7. Kama unakumbuka Vizuri , msimu uliopita Sunderland ni moja ya timu zilizoitesa Chelsea msimu uliopita wakiwafunga The Blues bao 3-0 darajani Stamford Bridge.

Sunderland iliyoifunga Chelsea si sunderland hii iliyopo Leo kwani kipindi kile alikuwepo Danny Welbeck ambaye amerejea nyumbani United , alikuwepo Darren Bent ambaye ameuzwa Aston Villa , alikuwepo Nedum Onuoha ambaye naye kama Welbeck amerejea nyumbani Man City.

Kuondoka kwa wachezaji hao kumefagia njia ya kuingia kwa wachezaji kadhaa wakiwemo John O’shea na Wes Brown toka Man United , Nicklas Bendtner naye amekuja toka Arsenal na Sebastian Larson toka Birmingham City.
Kwa mchezo dhidi ya Chelsea Sunderland watamkosa John O’shea na hii inamaanisha kuwa beki Phil Bardsley atahama toka kushoto alikozoea na kuja kwenye nafasi ya beki wa kulia huku Kieran Richrdson akijaza nafasi yake kama beki wa kushoto na huenda atasaidiwa na Jack Colback huku Wes Brown akicheza katikati na Titus Bramble ambaye anakuja kuziba pengo la Anton Ferdinand aliyeuzwa QPR.
Kwa upande wa ushambuliaji Bruce huenda akamuanzisha Asamoah Gyan huku Stephane Sessegnon akisimama nyuma yake na Bendtner atakuwa benchi pamoja na kucheza vizuri katikati ya wiki akiwa na timu yake ya taifa na Anton Gadner na Seb Larson watacheza pembeni.
Kwa upande wa Chelsea bado Didier Drogba ataendelea kukosekana baada ya ajali aliyopata kwenye mchezo uliopita . Taarifa njema kwa mashabiki wa Chelsea ni kurejea kwa kipa Petr Cech ambaye amekosa takribani wiki tatu baada ya kuuumia goti .Boas pia atakuwa na David Luis ambaye atakuwa benchi baada ya kurudi baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Raul Meireles pia atakuwa benchi na inatarajiwa kuwa kuwa Juan Matta ataanza baada ya kucheza vizuri mara ya mwisho dhidi ya Norwich City .
Upande wa beki watakuwepo Nahodha John Terry ambaye atacheza pembeni ya Branislav Ivanovic huku Jose Bosingwa ambaye anaonekana kuzaliwa upya msimu huu akicheza upande wa beki ya kuli akisaidia kupandisha mashambulizi kwa upande huo huku Ashley Cole naye akifanya hivyo hivyo upande wa kushoto.
Safu ya kiungo itakuwa chini ya Ramires , Frank Lampard, na John Obi Mikel wakigawana majukumu ya kucheza kwenye injini ya chini kwa Ramires na Obi na injini ya juu ikiwa chini ya Lampard.
Andre Villas Boas atawatumia Florent Malouda , Juan Mata na Fernando Torres kweney safu ya ushambuliaji ambayo kwa vyovyote itafanya jitihada za hali na mali kumsaidia Fernando Torres afunge baada ya kufunga bao moja katika michezo 27 ya Chelsea .
Hadi sasa Sunderland wamefunga bao moja tu lililowekwa wavuni wakati msimu unaanza kwenye mechi dhidi ya Liverpool katika mchezo ulioisha kwa sare pale Anfield .
Sunderland wamekuwa wakicheza vibaya kwenye uwanja wao wa nyumbani tangu mwaka huu uanze ambapo wamevuna pointi 7 pale Stadium Of Light huku wakiwafunga Wigan 4-2 mara ya mwisho mwezi Aprili.
Hadi sasa Sunderland wameweza kuvuna kadi nane za njano huku Phil Bardsley akiwa mchezaji pekee aliyeonyeshwa kadi nyekundu na Chelsea wamepata kadi za njano 6 hadi sasa.
Sunderland waliifunga Chelsea 3-0 mara ya mwisho msimu uliopita huko Stamford Bridge lakini Chelsea nao walishinda huko Stadium Of Light kwa matokeo ya 4-2.
Mara ya mwisho kwa Chelsea kupata ushindi ugenini ilikuwa mwezi Aprili ambapo waliwafgunga West Brom 3-0 kwenye uwanja wa The Hawthorns.
Katika mara sita za mwisho walizocheza huko Stadium Of Light Chelsea wameweza kushinda mara zote huku mara pekee ambayo walishindwa kupata pointi zote tatu ikiwa mwaka 2001 wakati timu hizi zilipotoka sare ya bila kufungana .

Bolton vs Manchester Utd : Preview

Manchester United wanaingia kwenye mchezo huu utakaopigwa kwenye uwanja wa Reebok wakitafuta rekodi ya asilimia mia moja baada ya kushinda michezo yote mitatu huku wakiwa kileleni mwa ligi.
Kukweli United imeanza msimu huu ikiwa na sura na swagga mpya ambayo ni tofauti na kile kilichoonekana msimu uliopita.
Katika misimu ya Ligi kuu ya England imezoeleka kuwa United huaanza kwa staili ya marathon yaani wanaanza ligi kwa mwendo wa taratibu lakini wanakuja kushika kasi kuanzia miezi Fulani ya katikati ya ligi na hatimaye kumalizia vizuri. United ya sasa hivi imeanza ligi vyema huku ikiwa na kikosi kichanga.
Katika mchezo United inatarajiwa kuwakosa wachezaji ambao waliumia mwanzoni mwa msimu, mabeki Rio Ferdinand na Nemanja Vidic watakosa pambano hili sambamba na Rafael Da Silva.

Sidhani kama hili litakuwa tatizo sana kwa United kwa kuwa wana watu ambao watacheza kwenye nafsi za wachezaji hawa vizuri tu.
United pia itamkosa mshambuliaji Danny Welbeck ambaye aliumia kwenye mchezo dhidi ya Arsenal.
Bado siri ya ushindi wa United itaendelea kuwa ‘patnership’ ya Wayne rooney na Ashley Young ambayo imeonekana kufanya kazi vizuri sana huku viungo Anderson na kinda Tom Cleverly wakiunganisha mambo katikati mwa uwanja huku Darren Fletcher akitarajiwa kurejea pia baada ya kupona tatizo la kirusi lililokuwa linamsumbua ambapo amecheza vyema kwenye mechi mbili za timu yake ya taifa.

Kitu pekee kinachoweza kuwa tatizo kwa United ni kipa David De Gea ambaye hakika Owen Coyle lazima atawapa maagizo wachezaji wake hasa Martin Petrov na Ivan Klasnic ya kupiga mashuti ya mbali wakijua fika kuwa David De Gea ana tatizo kubwa la kucheza mipira ya mbali na hili linakuja kama changamoto kwa viungo na mabeki wa United kumpa De Gea ulinzi wa kutosha na kuepusha mianya ambayo wachezaji wa Bolton wanaweza kupiga mashuti.
Kwa upande wa Bolton kocha Owen Coyle atamkosa kiungo Marcos Alonso ambaye ana jeraha kubwa la mguu pamoja na lundo la wachezaji kama Tyrone Mears , Lee Chung-Yong , Stuart Holden, Sean Davis , Sam Ricketts , na Ricardo Gadner ambao wana majeraha ya muda mrefu.
Mshambuliaji aliyesjailiwa toka Liverpool David Ngo’g anaweza kuwa mtu muhimu ambapo huenda akatumika kama mbadala wa Kevin Davies na Ivan Klasnic watakaoanza kwenye safu ya ushambuliaji.
Kutakuwa na ‘batlle’ kubwa kati ya walinzi wa Bolton kina Gary Cahil , Paul robinson na Zat Knight ambao watakuwa na kazi kubwa ya kuwachunga Rooney na Young pamoja na Luis Nani.

Sir Alex Ferguson amekuwa akiwatumia Ashley Young na Luis Nani pembeni mwa uwanja huku Young akicheza kushoto na Nani akicheza kulia.
Young amekuwa hatari sana anapocheza kushoto ambako anaingia ndani na kujipasia kwenye mguu wa kulia anaoutumia kupiga mashuti kama alivyofanya kwenye mechi dhidi ya Arsenal na hata mechi dhidi ya West Brom ambapo alifunga mara mbili kwenye mechi ya Arsenal na alisababisha bao kwenye mechi ya West Brom.
Katikati Fabrice Muamba na Nigel Reo-Coker watapambana na Anderson na Cleverly au Fletcher au hata Michael Carrick , kumbuka United wanaweza kualzimika kupumzisha baadhi ya wachezaji wakiwa na wazo juu ya mchezo wao wa ligi ya mabingwa dhidi ya Benfica wiki ijayo.
Rooney anatarajiwa kuanza na Javier Hernandez upande wa juu wa United japo Dimitar Berbatov atakuwa benchi.
Bolton inaye mtu aliyewahi kuwa winga wa United Chris Eagles ambaye anaweza kutumia uwezo wake binafsi na jinsi anavyoijua United kiundani baada ya kuwa mchezaji wake kwa muda mrefu.
Bolton Wanderers wamewahi kushinda mara moja tu kati ya mara 17 za mwisho walizokutana na vija wa Sir Alex Fergusson.
Bolton wamekuwa wenyeji kwa Man United mara zisizopungua 58 kwenye mechi za ligi ambapo wameshinda mara 25 , wamefungwa mara 18 na wametoka sare mara 15.
Katika michuano yote waliyowahi kukutana Bolton wamefunga mabao 159 na United wamefunga mabao 187
Hadi sasa United imeshinda michezo yote mitatu ya ligi tangu mwanzo, wakifunga mabao 13 huku wakiongoza ligi.

Bolton wao wameshinda mchezo mmoja huku wakiwa wamefungwa miwili .
Wayne Rooney na Ashley Young wamefunga mabao saba kwa pamoja katika mnichezo mitatu ya United na ukihesabu na ile ya England wamefunga mabao 10.
Iwapo United itashinda utakuwa ushindi wake wa 200 wakiwa ugenini kwenye mechi ya ligi kuu ya

Arsenal mpya na Matarajio mapya...


Arsene Wenger amelazimika kukiongoza kikosi cha Arsenal kilichodhoofishwa na majeraha kwa wachezaji muhimu huku wengine wakifungiwa.
Bacary Sagna alikosa kipigo cha mabao manane dhidi ya Man United na baada ya hapo Thomas Vermaelen ambaye ndio kwanza alikuwa amerudi akiwa hajacheza hata mechi tano tangu akose msimu mzima uliopita naye ameumia tena safari hii akikosa miezi miwili kwa jeraha jipya la enka.

Vermalaen anaungana na Sebastien Squilaci ambaye ana jeraha kama lake,Kieran Gibbs ameumia misuli ya nyuma ya mguu na Jack Wilshere na Abou Diaby wote wana majeraha ya enka ambayo yanawafanya wakose miezi isiyopungua miwili kwa Wilshere na Abou Daiby amebakiza siku chache kabla ya kurudi uwanjani.

Sagna kwa upande wake anaweza kurudi ndani ya muda na kucheza mechu dhidi ya Swansea City na Gervinho, Alex Song na Carl Jenkinson wote wamefungiwa kucheza michezo kadhaa kwa kadi nyekundu walizopata kwenye michezo ya nyuma.
Kukosekana kwa Kieran Gibbs kunamaanisha kuwa njia ni nyeupe kwa Andre Santos kucheza mechi yake ya kwanza tangu asajiliwe toka Fernabance huku mchezaji mwingine mpya Per Mertersecker naye akitarajiwa kuonekana kwa mara ya kwanza tangu asajiliwe toka Werder Bremen akisaidiana na Johan Djorou katikati kwenye safu ya ulinzi.

Sambamba na hao Mikael Arteta naye atavaa uzi wa washika bunduki kwa mara ya kwanza tangu aondoke Everton .
Mchezaji mwingine mpya toka Korea ya Kusini Park Chung Young atakuwepo benchi kwa kuwa bado ana uchovu wa safari ndefu na mechi ngumu aliyocheza mwishoni mwa wiki iliyopita akiwa amerejea majuzi tu toka kwao Korea alikokuwa na timu yake ya taifa .
Kwa upamde wa Swansea Kocha Brendan Rogers hana wasiwasi wa kuwakosa wachezaji kutokana na majeraha mbalimbali kama ilivyo kwa Arsenal japoa atakosa huduma ya mchezaji Ferry Bodde ambaye anasumbuliwa na goti na Alan Tate ambaye anatarajiwa kukosa sehemu kubwa ya msimu kutokana na mguu wake kuvunjika.

Swanse wana habari njema za kurejea kwa Gary Monk ambaye hivi karibuni alifanya mazoezi na timu ya vijana baada ya kuwa majeruhi wa muda mrefu.

Wengi wataipa Arsenal nafasi kubwa ya kuondoka na pointi tatu kwa mara ya kwanza msimu huubaada ya kutoka sare na kufungwa michezo miwili huku kipigo cha bao nane toka kwa Man United bado kikipiga kengele masikioni mwa mashabiki wengi.
Kikosi cha Swansea kinashika nafasi ya sita kutoka mwisho wakiwa wametoka sare mara mbili na kufungwa mchezo mmoja na hadi sasa hawajaweza kufunga bao lolote tangu waje kwenye ligi kuu ya England.
Robin Van Persie akicheza na Theo Walcott pembeni yake huku Mikael Arteta akiwa nyuma yao kama mpishi mkuu wa mipira ya mwisho, Arteta atakuwa akisaidwa na Emanuel Frimpong ambaye atarejea toka kwneye adhabu ya kadi mbili za njano alizopata kwenye mchezo dhidi ya Liverpool.
Ni dhahiri Arsenal watakuwa na nafsi kubwa ya kushinda japo kila mmoja anangoja kuona kama homa yao imepona au la na kwa upande wao bado hawajashinda hadi leo wakitoka sare mara mbili na kufungwa mechi mbili.


Timu hizi mara ya mwisho zilicheza kwenye msimu wa mwaka 1982-83 ambapo Arsenal walishinda nyumbani na ugenini kwa matokeo ya 2-1.
Msimu wa kabla ya hapo Swansea wao ndio walioshinda mara mbili wakiwafunga Arsenal 2-0 mara zote.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa timu hizi kukutana tangu mfumo mpya wa ligi kuu ya England kuanzishwa.
Arsenal ndio timu ya kwanza kwenye historia ya Ligi kuu kuwa na wachezaji watatu waliotolewa kwa kadi nyekundu kwenye mechi tatu za kwanza za msimu na hadi sasa ukuta wao umeonekana kuvuja sana kwa kufungwa mabao 10 katika michezo miwili tu .

Liverpool wanatafuta ushindi wa kwanza kwenye uwanja wa Brittania .


Moja ya timu ambazo zimekuwa zikiipa Liverpool tabu ni Stoke City, tangu mwaka 2008 , Liverpool wametoka sare na Stoke mara mbili na wamefungwa na vijana hao wa Tony Pulis mara moja.
Wenyeji wa mchezo huu Stoke City wanatarajiwa kumpa mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Peter Crouch mechi yake ya kwanza tangu asajiliwe toka Tottenham siku ya mwisho ya usajili na kama bahati ikiwa kwake huenda akawadhuru mabosi wake wa zamani.
Crouch anakuja kwenye nafasi ya mmojawapo kati ya Kenwyne Jones na Jonathan Walters huku Wilson Palacios naye akitarajiwa kuonekana kwa mara yake ya kwanza kwenye timu yake mpya ya Stoke City, Palcios anaweza kucheza katikati na Rory Delap kama mrusha mipra huyu toka Ireland atakuwa amepona jeraha lake la misuli ya mguu.
Ujio wa Crouch , Cameron Jerome na Palcios kwa vyovyote utainufaisha Stoke kwa kuwa mitindo ya uchezaji wa watu hawa watau inaendana sana na falsafa ya soka linalochezwa kwenye klabu hii.

Mara nyingi vijana wa Tony Pulis huwa hawana vitu vingi kwenye mchezo wao, mfumo wao ni rahisi , mipira mirefu kwa mshambuliaji mmoja mwenye umbo kubwa na si vinginevyo huku viungo wa kati na mabeki wakicheza soka la shoka ambalo nguvu ndio hazina kubwa na ndio maana Liverpool wanateseka dhidi ya hawa jamaa hasa wanapolazimika kusafiri hadi Brittania ambako takwimu zinaonyesha kuwa kuna mashabiki wanaopiga kelele kuliko uwanja wowote kwenye ligi kuu ya England.
Kocha wa Stoke anaweza kuamua kumtumia beki Robert Huth kama beki wa pembeni ili kumpa nafasi Jonathan Woodgate kucheza katikati na Ryan Shawcross kama ilivyokuwa kwenye mchezo dhidi ya Chelsea ulioisha kwa sare ya bila kufungana siku ya kwanza ya msimu.

Kwa upande wa Mfalme wa Anfield, Charlie Adam ataanza baada ya kurejea haraka toka kwenye jeraha alilopata akiwa na timu yake ya taifa Scotland wiki iliyopita, beki wa pembeni Martin Kelly hataonekana na kwenye nafasi yake atarejea John Flanagan japo Glen Johnson ameanza mazoezi baada ya kurudi toka kwenye jeraha lililomuweka nje.

Bado Liverpool itaendelea kumkosa Captain Fantastic Steven Gerard ambaye anaendelea kupoba taratibu kutoka kwenye maumivu ya sehemu ya juu ya mguu wake yanayomsumbua kwa muda mrefu . Liverpool wanaweza kumtumia Craig Bellamy pamoja na beki mpya Sebastian Coates huku ‘cha ulevi’ Andy Carroll akiwa benchi ambapo Dalglish anatarajiwa kuchezesha ‘maforward’ wale wale Kuyt na Suarez walioiua Bolton mara ya mwisho Liverpool ilipocheza kwenye ligi kuu ya England.
Dalglish anapaswa kuhakikisha kuwa anaipa ‘balance’ ya kutosha timu yake na hapa pengine ingeweza kuwa busara kumuacha Charlie Adam kwenye benchi na kumpa nafasi ya Lucas Leiva ambaye kwenye mchezo wa msimu uliopita alipata kadi nyekundu.


Mechi kama hizi za Stoke ndio haswa zinazomfaa kwa kuwa anapenda soka la vurugu ambalo Stoke ndio nyumbani kwake na Luis Suarez atakuwa chaguo bora kwa ushambuliaji kwa kuwa ujanja wake hakika utawapa tabu mabeki wa Stoke kina Huth,Shawcross na wengineo ambao uchezaji wao wa nguvu na ujanja wa Suarez vinaweza kusababisha hatari kwa Stoke, hasa ukizingatia tabia ya Suarez ya kupenda kuwaibia waamuzi kwa kujiangusha na kutafuta penati.

Auheni kwa Stoke inakuja kutokana na uwepo wa Jonathan Woodgate mtu ambaye ni kaka mkuu kwa mabeki wenzie na pia ana ‘dimensio’ tofauti kwenye mchezo wake ambapo yeye si kama wenzie ambao hutumia nguvu sana yeye hutumia zaidi akili na ni mtulivu kuliko wenzie.

Stoke hawajawahi kufungwa na Liverpool kwenye uwanja wa Brittania tangu wapande daraja, Mara ya kwanza Liverpool kusafiri kuelekea huko walitoka sare ya bila kufungana wakati huo wababe wa Anfield wakiwa chini ya Rafa Benitez , na kwenye mchezo wa marudiano msimu huo huo Robert Huth alifunga bao la kusawazisha na kwenye msimu uliofuata wakati Liverpool wakiwa chini ya Roy Hodgson waliondoka mikono mitupu baada ya kufungwa mabao mawili bila .
Hadi hivi tunavyozungumza Stoke haijapoteza mchezo wowote kati ya michezo 7 ya kiushindani waliyocheza na wamefungwa bao moja tu ugenini kwenye mchezo dhidi ya Norwich, mechi nyingine walizocheza ni dhidi ya Chelsea na West brom kwenye ligi na dhidi ya Hadjuk Split na Fc Thun kwenye michezo ya kufuzu Ligi ya Europa .
Msimu uliopita Stoke walishinda mchezo huu kwa matokeo ya 2-0 kupitia kwa mabao ya Ricardo Fuller na Kenywyne Jones.
Kocha wa Stoke Tony Pulis amelitumia vizuri dirisha la usajili baada ya kuwanunua wachezaji watano na cha kushangaza kwa kocha wa Stoke ni ukweli hakutumia fedha yoyote hadi siku ya mwisho ya dirisha la usajili ,Matthew Upson na Jonathan Woodgate walisajiliwa bure huku Peter Crouch , Cameron Jerome na Wilson Palacios wakijumuisha matumizi ya paundi milioni 20 zilizotumika dakika za mwisho kabisa za dirisha la usajili.
Kwa upande wake Kenny Dalglish ametumia takribani Paundi milioni 50 kwa wachezaji sita wa kikosi cha kwanza walionunuliwa msimu huu, Jordan Henderson, Stewart Downing, Charlie Adam, Alexander Doni, Jose Enrique na Craig Bellamywote wamejumuisha paundi milioni 50 kuja Anfield msimu huu.
Mara ya mwisho kwa Liverpool kupata ushindi wa aina yoyote ile kwenye uwanja wa Brittania ilikuwa mwezi Novemba mwaka 2000 ambapo Liverpool walishinda 8-0 kwenye kombe la ligi.Stoke wamewahi kuifunga Liverpool mara 27 huku Liverpool wao wakishinda mara 55 katika michezo 112 ambayo timu hizi zimekutana ambapo mara ya mwisho ilikuwa msimu uliopita huko Anfield ambapo Luis Suarez alifunga kwenye mchezo wake wa kwanza .

Thursday, September 8, 2011

mzungu balaa,


VPL KUCHEZWA UWANJA WA TAIFA,TWIGA STARS, BANYANA BANYANA 2-2

Serikali imeruhusu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zinazohusu timu za Simba na Yanga. Hata hivyo ruhusa hiyo ni ya mechi mbili kwa wiki.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na klabu za VPL zenye maskani yake Dar es Salaam waliwasilisha tena maombi Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ili kutumia uwanja huo kwa mechi za ligi.

Kutokana na uamuzi huo wa Serikali mechi ambazo sasa zitachezwa kwenye uwanja huo ni Ruvu Shooting vs Yanga (Septemba 10), Azam vs Simba (Septemba 11), Simba vs Polisi Dodoma (Septemba 14), African Lyon v Yanga (Septemba 15), Azam vs Yanga (Septemba 18), Yanga vs Villa Squad (Septemba 21).

Nyingine ni Yanga vs Coastal Union (Septemba 24), Simba vs Mtibwa Sugar (Septemba 25), Yanga vs Kagera Sugar (Oktoba 14), Simba vs African Lyon (Oktoba 16), Simba vs Ruvu Shooting (Oktoba 19), Yanga vs Toto Africans (Oktoba 20), Simba vs JKT Ruvu (Oktoba 22), Yanga vs Oljoro (Oktoba 23), Yanga vs Simba (Oktoba 29) na Moro United vs Simba (Novemba 5).

TWIGA STARS, BANYANA BANYANA 2-2
Timu ya Taifa ya wanawake ya Tanzania (Twiga Stars) imetoka sare ya mabao 2-2 na Afrika Kusini (Banyana Banyana) katika mechi ya michezo ya All Africa Games (AAG) iliyochezwa leo Uwanja wa Machava jijini Maputo, Msumbiji.

Banyana Banyana ndiyo iliyoanza kupata bao kabla ya Twiga Stars kusawazisha dakika ya 25 kupitia kwa Mwanahamisi Shuruwa. Banyana Banyana ilianza kipindi cha pili kwa nguvu na kupata bao la pili. Zena Khamis aliisawazishia Twiga Stars dakika 60.

Twiga Stars itacheza mechi yake ya mwisho hatua ya makundi Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe kwenye uwanja huo huo. Katika mechi yake ya kwanza Zimbabwe ilifungwa na Banyana Banyana mabao 4-1.

TOKA KWENYE KIPIGO CHA BELFAST HADI KUITEKA ULAYA NA DUNIA NZIMA

Mwezi Septemba tarehe 6 mwaka 2006 Soka la Hispania lilifikia kiwango cha chini kuliko siku zote katika histoaria yake. Kipigo cha mabao 3-2 toka kwa Ireland ya Kaskazini huko Belfast kilikuwa kipigo kibaya zaidi kwa timu ambayo inatazamwa na watu kama timu inayotisha lakini haikuwahi kudhihirisha uwezo wake kwenye michuano mikubwa.
Ni wachache ambao wangeweza kutabiri kilichotokea baada ya hapo.
Miaka mitano baadae Timu ya taifa ya Hispania imekuwa bingwa wa ulaya na bingwa wa dunia na ni nani wa kusimama njiani wakielekea kutwaa ubingwa mwingine wa Ulaya, hakika hakuna.
Ushindi dhidi ya Lichteinstein umewahakikishia kufuzu kwa kombe ambalo wanaenda kulitetea na umewafanya watimize miaka mitano tangu walipofungwa na mabao matatu ya David Healy.
Usiku ule kwenye uwanja wa Windsor Park ambapo David Healy alifunga ‘Hat-trick’ ulikuwa usiku wa mapinduzi makubwa kwa aliyekuwa kocha Luis Aragones .Huku kazi yake ikiwa hatarini , mabadiliko yalilazimika kufanyika kwenye timu ya Hispania.
Akiwa ndio kwanza ametoka kwenye kashfa ya ubaguzi wa rangi baada ya kumtolea maneno ya kibaguzi Thierry Henry , kocha huyu wa Hispania alikuwa na maamuzi magumu ya kufanya.
Na katika maamuzi hayo gumu kuliko lote ilikuwa kumuacha mshambuliaji mkongwe na nahodha Raul Gonzalez. Usiku ule jijini Belfast ulikuwa wa mwisho kumuona Raul akiichezea timu ya taifa . Kama shuti lake alilopiga mwishoni mwa mchezo lisingegonga mwamba basi pengine tungeendelea kumuona Raul akiwa mchezaji wa timu ya taifa, lakini mambo yalienda kombo kwake.
Kuwekwa kando kwa Raul kulizua maswali mengi. Raul alikuwa kipenzi cha wengi na katika miaka yake yote ya kuichezea timu ya taifa hakuwahi kutwaa ubingwa wowote akiwa na timu hiyo.
Mwaka baadae kocha Aragones alilipuka kwa hasira alipouliza kuhusu Raul .’unajua Raul amecheza kwenye kombe la dunia mara ngapi?? Aragones aliuliza , Akajibiwa mara tatu, Akauliza tena ,amewahi kutwaa kombe hilo mara ngapi?? Akajibiwa kuwa hajawahi Akauliza tena na Kombe la Ulaya je?? Akajibiwa mara mbili , na amewahi kushinda mara ngapi?? Hajawahi.
Si lawama zote zinamwendea Raul , lakini mshambuliaji huyu wa Real Madrid amekuwa akicheza chini ya kiwango kwa muda mrefu kwenye timu ya taifa na mpaka kufikia kipindi hicho ilionekana kuwa muda umefika kwa Hispania kusonga mbele na kumuacha Raul. Inasemekana kuwa Raul alikuwa sababu ya mgogoro kwenye kambi ya kombe la dunia huko ujerumani mwaka 2006 ambako Hispania ilitolewa kwenye hatua ya raundi ya pili na Ufaransa
Mchezo huo ulichezwa huko Hannover mwezi juni lakini Hispania wlaibaki na Hangover mpaka mwezi septemba . Kufuatia kipigo dhidi ya Ireland ya kaskazini , na vipigo vingine dhidi ya Sweden na Romania Hispania waling’aa wakicheza mechi 35 bila kufungwa ambapo Hispania walitwaa ubingwa ulaya chini ya Aragones na wakaendelea kutwaa ubingwa wa dunia chini ya Vicente Del Bosque.
Wakati Aragones aliondoka alisema kuwa ili Hispania itwae ubingwa wa dunia ni lazima icheze kwa kutawala sehemu ya kiungo huku ikitumia mchezo wake wa kupiga pasi nyingi . Kiungo mwenye nguuv nyingi Marcos Sennna aliitwa kwenye timu kuongezea kwenye akili za viungo Xavi na Iniesta na mbele akaletwa David Villa kwenye nafasi iliyoachwa na Raul Gonzalez ambapo Villa aliunda safu ya ushambuliaji sambamba na Fernando Torres huku Villa akifunga mabao manne na Torres akifunga moja kwenye fainali ya EURO 2008 dhidi ya ujerumani .

Aragones aliachia ngazi baada ya euro 2008 ila Hispania walikuwa wazuri zaidi chini ya Del Bosque wakicheza soka la kuvutia machoni huku wakiiga mfumi unaotumika Barcelona na kutawala dunia kwa kutwaa kombe la Dunia afrika kusini .
Mpaka kufikia wakati huo Sergio Busquets na Pedro walikuwa wameongezwa na beki mwingine Gerard Pique ambaye alirudi Hispania toka Man United . Hispania ikawa timu iliyokamilika kuliko zote ulimwenguni ambayo mpaka hii leo wameendelea kutawala soka la dunia hii .

YANGA YAISHINDA TFF,YAENDELEA KUBURUZA MKIA

Yanga jana kwa mara ya kwanza walivaa jezi za mdhamini wa Ligi Kuu Vodacom, lakini zikiwa na alama nyeusi badala ya alama nyekundu


Hapo jana Yanga ililazimishwa sare ya bila kufungana na Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom.

Wakati huo huo bao la Gervais Kago liliipa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Villa Squard kwenye uwanja wa Mkwakwani Mkoani Tanga.






TENGA: SAHAUNI WAZO LA KAMPUNI KUENDESHA LIGI KUU YA TZ BARA.

Raisi wa TFF Leodegar Tenga amezitaka klabu za Ligi Kuu kusahau habari ya ligi kusimamiwa na kampuni na sasa yupo mbioni kuunda chombo kitakachoendesha ligi hiyo.
Tenga anadai migogoro inayoendelea katika nchi za Kenya na Uganda ni kwasababu ya ligi ya nchi hizo kuendeshwa na kampuni.
Akasisitiza kamati ya utendaji ya TFF ndio itakayoteua majina ya viongozi watakaounda chombo maalum cha kusimamia Ligi Kuu na Ligi daraja la kwanza ili kuwe na uwiano sawa.

Wednesday, September 7, 2011

Mbinu mbovu za mazoezi za timu za England ndio zinazoua wachezaji kwa majeraha .Kwa mujibu wa mtaalamu wa Kidachi Raymond Verheijen.

Wachezaji wengi wa kileo wanaweza kuwa wametimiza ndoto zao kwa vitu vingi , kama vile kazi ya kufanya ambayo ni ndoto ya maisha yake , akaunti ya benki inayosoma vizuri na vitu vingine vingi vinavyomfanya awe kwenye mazingira mazuri ya kufanyia kazi kuliko ilivyokuwa zamani.
Lakini tatizo kuu linalomkabili ni mbinu za mazoezi ambazo zimeegemea sana kwenye sayansi na teknolojia ya kisasa . Huu ni mtazamo wa mtaalamu wa masuala ya viungo wa Kidachi Raymond Verheijen.
Verheijen amewahi kufanya kazi kwenye timu za taifa za Uholanzi,Korea ya Kusini na Urusi pamoja na Vilabu kama Barcelona,Manchester City na Chelsea pamoja na chama cha soka cha Uholanzi.
Kwa mtazamo wake mazoezi ya kisasa hayapaswi kuzingatia sana ugumu wa mazoezi ya viungo na muda mrefu wa kuyafanya.
Yeye anasema kuwa mazoezi yanapaswa kuwa machache kwenye upande wa viungo ili kuwaweka wachezaji Fit kuchezea mpira kwa muda mrefu.
Raymond anasema siku hizi Kuna tofauti kubwa kwenye mbinu za kufundisha mpira ukilinganisha na zamani , tatizo ni kwamba watu wengi wanadhani kufanya mazoezi mengi na kwa muda mrefu ni kitu bora.
Kiasili anasema watu wanaamini kuwa kabla ya mechi unapaswa kuuandaa na kuujenga mwili.
Wanawasukuma wachezaji kufanya mazoezi wakati mwingine zaidi ya kiwango chao cha kawaida cha kufanya mazoezi ili mradi tu wawe fit kwa kuwa wanaiga mbinu za mazoezi toka kwenye michezo mingine.
Kiukweli kwenye michezo mingine kama Riadha, Mbio za baiskeli na kuogele kufanya mazoezi mengi ni vizuri lakini siyo kwenye soka.
Watu wanaufanya mchezo kuonekana mgumu pasipo na faida yoyote. Kwa sababu ya mapinduzi haya ya kisayansi watu wanaacha kufikiri kama wanadamu wa kawaida na wanaacha kufanya mambo kwa kufuata misingi.


Neno soka limeingiliwa na hili suala la Fitness na ndiyo maana mimi huwa nasema ni vyema kurudi kwenye mambo ya msingi.
Inawezekana vipi timu 10 tofauti zina makocha kumi tofauti wa masuala ya fitness na wanatumia mbinu 10 tofauti? Haiwezekani, wachezaji wanakuwa wahanga wa fitness. Mbinu za kufanya mazoezi hazipaswi kuegemea kwenye mawazo ya mtu mmoja au uzoefu wake .

Mazoezi ya soka yanapaswa kuwa ya soka na si kuongeza vitu toka mazoezi ya michezo mingine kama Hockey na Riadha.
Verheijen ambaye maisha yake ya soka yalikatishwa na jeraha la paja alilopata akiwa na umri wa miaka 17, amesomea masuala ya physiology na saikolojia ya michezo kwenye chuo cha Free Huko Amsterdam na mawazo yake yametumika kwenye kozi za kufundishia ukocha na ualimu wa michezo kwa jumla nchini kwao uholanzi.

Mtaalamu huyu mwenye umri wa miaka 39 ambaye ana Leseni ya ukocha daraja la A inayotambulika na UEFA anasema kuwa makocha wengi wa masuala ya fitness hawana histoaria ya mchezo wa soka na ametoa mifano mingi sana ya timu ambazo zina historia ya kuwa na wachezaji walioko fiti sana na wasioumia umia kila leo . Anatolea mfano timu ya Korea ya kusini ambayo amefanya nayo kazi kwenye michuano ya kombe la dunia mara 3 .
Nilipoanza kufanya kazi na Guus , nilimuuliza kwanini aliniita kufanya kazi na timu ile .Hawa watu tayari wako fit alisema , ila ngoja uone mechi yao ya kwanza ya kirafiki alisema Guus. Kwenye mchezo wao wa kwanza waliweza kucheza vyema kwenye dakika 60 za kwanza lakini baada ya hapo walichoka sana.

Kama Guus angekuwa amemleta mtu ambaye ni mtaalamu wa mazoezi angemwambia kuwa wachezaji wa Korea ya kusini wanakosa pumzi na hivyo angewakimbiza kuzunguka uwanja raundi kadhaa au angewakimbiza msituni au mlimani ili kuwapa pumzi. Ila mimi sikutafsiri tatizo la wakorea kama hivyo, kwangu niliona kuwa wakorea hawawezi kucheza kwa mtindo mmoja kwa muda wa dakika 90. Hii inamaanisha kuwa unapaswa kutumia lugha ya mchezo wa Soka kufafanua tatizo na si vinginevyo .
Tulilitatua tatizo hili kwa kucheza kwa kugawanya muda wa dakika kumi kumi, huku tukiongeza idadi ya makundi ya muda huo wa dakika kumi kumi taratibu kuanzia mara nne , tano , sita kabla ya kucheza kwa mtindo huu kwa muda wa dakika 90.


Unapaswa kuwalazimisha wachezaji kufanya masuala Fulani hata kama mwili unasema hapana , unapaswa kuwazoesha hivyo. Kama unataka kucheza mtindo Fulani kwa muda mrefu unapaswa kufanya mazoezi ya kuucheza mtindo huo uwanjani kwa muda mrefu.
Mbinu hii ya kugawanywa muda ilibuniwa na Mwalimu wa kirusi ili kuzuia kufanya mazoezi zaidi na kumfanya mchezaji aperform kwa kiwango cha juu.

Kama unataka kupiga hatua kama mchezaji kitu muhimu cha kufanyia kazi ni spidi ya vitu unavyofanya kama mchezaji. Na hili linaonyesha kuwa soka ni mchezo wa kiwango cha matukio na sio mchezo wa kuvumilia mateso ya mazoezi. Kwenye mchezo wa kuvumilia mazoezi magumu unapaswa kufanya mazoezi kwa muda mrefu lakini kwenye mchezo wa kiwango unapaswa kuzingatia kiwango cha mazoezi unayoyafanya.
Kama unataka kuongeza kasi ya matendo yako uwanjani uchovu ni adui yako namba moja . kwa kila kipindi cha mazoezi unapaswa kuwa fresh na kama unataka kuongeza kiwango kama mchezaji unahitaji pia kuwa fresh.


Kwa maneno mengine ‘chache ni zaidi’ . Njia pekee ambayo mchezaji atapiga hatua kwenye kiwango chake ni kwa kufanya mazoezi yaliyo bora na si kufanya mazoezi zaidi .
Mwangalie Arjen Robben ambaye ametumia muda mwingi akiwasumbua madkatari pale Stamford Bridge kuliko alivyokuwa anawasumbua mabeki kwa miaka yake mitatu aliyokuwa Stamford Bridge.

Akiwa Chelsea walimuita ‘the man of glass’ , mwaka jana alicheza Bayern Munich . Walichofanya pale ni kupunguza mazoezi aliyokuwa anayafanya . Alicheza kwenye kiwango cha juu sana na walitwaa mataji kwa sababu yake .
Ghafla Robben hakuwa majeruhi tena.


Swali ni kwamba Robben alikuwa ‘mchezaji wa glassi au makocha waliomfundisha ndio walikuwa makocha wa glassi? Wachezaji kama Robben na Va Persie hutumia nguvu kwenye matendo yao kuliko wachezaji wengine .
Wanapofanya mazoezi kama wachezaji wengine matumizi yao ya nguvu yanakuwa mara mbili zaidi hivyo ni lazima uwapunguzie mazoezi wafanye angalau asilimia 50 na ni kitu ambacho Bayern walifanya kwa Robben .

Unapokuwa umechoka ishara toka kwenye ubongo wako kwenda kwenye mwili wako inakuwa inasafiri taratibu kuliko kawaida . Kama ishara inakwenda taratibu inahatarisha viungo vyako kwakuwa unatumia nguvu nyingi kuliko uwezo wako wa kawaida na hivi ndio unasikia vitu kama magoti,enka,nyonga, nyama za paja na vingine ving vinaumia .

Timu nyingi za ligi kuu nchini England zinatumia teknolojia ya kompyuta kupima kiwango cha ‘perfomance ‘ ya mchezaji na hata kiwango cha uchovu . Pamoja na vipimo hivyo vya sayansi na teknolojia mpya bado kulikuwa na wachezaji karibu 108 ambao rekodi zilisoma kuwa hawakuwepo kwenye viwango vyao vya kawaida kwenye wikiendi ya desemba , nah ii ni sawa na asilimia 5.4 ya wachezaji kwenye kila timu, mahesabu haya yanaonyesha kuwa kuna tatizo kubwa.

Aston Villa na Tottenham ndio walioathirika sana kuliko wengine huku wakiwa na karibu wachezaji 11 wenye majeraha na Arsenal walimpoteza beki wao Kieran Gibbs kwa jeraha la Enka . Kwa ujumla timu hizi tatu ukitazama kwa undani ndio zenye tatizo la kuwapa wachezaji mazoezi magumu kuliko inavyotakiwa.

Sawa kuna watu waliowahi kuvunjia mifupa vibaya kama Eduardo na Ramsay lakini vipi kuhusu Robin Van Persie ambaye amekaa nje kuliko hata hawa wachezaji waliowahi kuvunjika vibaya , na Van Persie majeraha yake si ya kuvunjika mifupa , amekuwa na matatizo ya misuli san asana .

Verheijen anamtumia mchezaji mwingine wa kidachi Rafael Van Der Vaart kama mfano . Verheijen anakataa katakata imani ya Tottenham kuwa mchezaji huyu hayuko ‘fit’ .
Hana uzito usio wa kawaida , namjua tangu utoto wake , nilifanya naye kazi mwaka 2001 wakati nikisaidia kwenye timu ya Uholanzi ya Under 20 kwenye kombe la dunia huko Argentina na jinsi alivyokuwa kimwili .

Van Der Vart amekuwa na msimu mrefu sana na hakupumzika kwa kuwa alilazimika kucheza kwenye kombe la dunia ambako timu yake ilicheza mpaka fainali. Fitness yake ilikuwa juu lakini hakuwa Fresh kwa kuwa hakupata muda wa kutosha kupumzisha mwili wake.

Wachezaji wanaocheza kombe la dunia mara zote wanakuwa fiut lakini uchovu ndio adui yao, na uchovu huufanya mwili upoteze mawasiliano baina yake na ubongo na hapo ndio majeraha hasa ya misuli na nyama yanapokuja na kuwamaliza wachezaji hawa.
Wanachohitaji ni muda wa kutosha wa kupumzika na mazoezi ambayo yanazingatia hilo.


Mazoezi kwa kipindi kimoja kwa siku na mazoezi haya hayapaswi kuwa na lundo la mazoezi magumu ya viunngo na kunatakiwa kuwa na muda mwingi katikati ya vipindi vya mazoezi wa kuuruhusu mwili kurejea kwenye hali yake ya kawaida baada ya mazoezi.Verheijen anasema kuwa alitumia mfumo huu akiwa na Barcelona ya Frank Rijkaard mwaka 2004 baada ya michuano ya Euro.

Verheijen amewahi kufanya kazi kwenye ligi kuu ya England ambako alikuwa kwenye timu ya Man City chini ya Mark Hughes kwenye mzunguko wa pili wa msimu wa mwaka 2009.
Katika kipindi cha Julai na Novemba mwaka jana Man City walikuwa na rekodi bora kwenye ligi kuu ya wachezaji kutoumia.


Pia timu hii ilikuwa na takwimu bora kwenye mbio wakati wa mechi na walifanya mazoezi mara moja kwa siku.Mazoezi yalikuwa na kiwango bora na hayakuwa ya kuchosha , kwa muda wote huo Man City walikuwa na mchezaji mmoja tu aliyeumia na alikuwa Benjani ambaye Verheijen anakiri kuwa jeraha alilopata lingeweza kuzuilika

Alipokuja Roberto Mancini aliongeza mazoezi ya nguvu wakati alipokuja , jambo ambalo lilipingwa na wachezaji kama Craig Bellamy na Carlos Tevez. Mancini aliongeza mazoezi kutoka kwenye kipindi kimoja kwenda kwenye vipindi viwili na pia aliongeza muda wa mazoezi hayo toka kwenye dakika 75 hadi masaa mawili. Katika siku zake 10 za kwanza kulikuwa na wachezaji takribani 10 walioumia , hakuna mwandishi wa habari anayechambua suala hili, huu ni upuuzi.
Wakati Mancini alipokuja bado nilikuwa City japo si kwenye nafasi yangu niliyokuwa nayo wakati wa Hughes anasema Verheijen,.


Lakini baada ya wiki mbili na majeraha kwa wachezaji yakiongezeka niliamua kuondoka kwa kuwa watu walinihusisha na majeraha yale kwa wachezaji, anaongeza Verheijen.
City walilaumu kipindi cha Krismasi kuwa ndio kilisababisha majeraha kwa wachezaji , kwa mujibu wao majeraha yale yasingeweza kuzuilika.
Kwa sasa majeraha haya yamepungua kwa sababu wana mechi nyingi katikati ya wiki na hivyo wamelazimika kupunguza muda wa mazoezi kuwa mara moja na si mara mbili
Anachojaribu kueleza mtaalamu huyu ni timu hasa za nchini England kuondokana na dhana potofu kuwa ‘fitness’ ya mchezaji inaongezeka kwa vipindi virefu vya mazoezi magumu , wachezaji wanaumia kwa sababu hii na si sababu nyingine , maisha yao ya uchezaji yanakuwa mafupi kwa sababu hii na si sababu nyingine .
Makocha wengi wanafanya hivi , hawazingatii umri wa mchezaji na vitu vingine muhimu , kila mtu anataka mbinu hizi za mazoezi ambazo hazisaidii.
Mtaalamu huyu anafanya kazi ya kumuweka fit Craig Bellamy kwa siku mbili za wiki kwa gharama za mchezaji huyu , na amekuwa mstari wa mbele kujaribu kuleta mabadiliko kwenye mazoezi .

Mtwa Kiwhelu Akitaja kikosi chake Bora cha Yanga.





Steven Nemes
Alikuwa kipa mahiri na aliyetisha langoni. Hakuwa mtu aliyetaka masikhara uwanjani.

Mtwa Kihwelo
Mimi mwenyewe nilikuwa sitaki mzaha katika upande wa kulia na nilicheza kama beki wa kupanda na kushuka.

Ken Mkapa
Beki mrefu aliyekuwa katika fomu enzi zake na ambaye alikuwa roho ya Yanga upande wa kushoto. Alicheza soka la uhakika la kupanda na kushuka.

Willy Mtendamema
Alikuwa mahiri katika safu ya ulinzi na muda wote alionekana kuwakumbusha wenzake majukumu yao vema.

Issa Athuman
Marehemu kwa sasa. Alikuwa mchezaji tegemeo katika safu ya ulinzi. Namkumbuka kwa kuwa mkali sana kama ukifanya makosa ya kijinga.

Method Mogella
Marehemu kwa sasa. Alikuwa kiungo mtaratibu uwanjani huku akicheza sana soka la akili. Atakumbukwa na wengi kutokana na kipaji chake murua.

Zamoyoni Mogella
Alikuwa hana mfano uwanjani na alikuwa roho ya timu. Vile vile alikuwa mshauri mzuri kwa wachezaji wengine.

Steven Mussa
Marehemu kwa sasa. Alikuwa mchezaji mtaratibu lakini mshindani uwanjani. Alikuwa kiungo maridadi sana na aliweza kuunganisha timu muda wote bila ya kuchoka.

Said Mwamba
Marehemu kwa sasa. Wengi wanakifahamu kipaji cha Said. Alikuwa bora sana uwanjani na asiye na mzaha kama utafanya makosa ya kijinga.

Mohamed Hussein
Alikuwa mfungaji hodari wakati huo. Asingeweza kupoteza nafasi mbili za wazi kama washambuliaji wa kileo.

Edibily Lunyamila
Wote tunafahamu sifa za Edibily. Ndiye aliyekuwa nyota wa michuano ile. Alikuwa fiti sana Eddy na alitubeba kwa kiasi kikubwa.

NIZAR AMKABIDHI JEZI RAISI Dr JAKAYA KIKWETE




























Tuesday, September 6, 2011

MIKAEL ARTETA NA NJIA 5 ZA KUWA IMARA KIAKILI MCHEZONI



Kiungo mpya wa Arsenal Mikael Arteta anajaribu kutoa mafunzo ni jinsi gani ya kuwa imara kiakili kipindi cha michezo migumu.


1: FIKIRIA KUSHINDA

“Kitu muhimu zaidi kabla ya mechi ni kwenda uwanjani ukiwa mentality ya ushindi.Huwezi ku-control pressuere ya mchezo hivyo ni vizuri kuji-control mwenyewe na kitakachoenda kutokea mchezoni.Kama unajiamini, then kipaji chako kitaonekana tu na uta-perform vizuri.”


2: USIOGOPE WALA USIWE NA JAZBA BAADA YA KUCHEZEWA RAFU KWA MARA KWA MARA.

“Mpinzani wako anapokuchezea vibaya hakikisha anaadhibiwa mapema ili ajiadhari kupata red card.Kufanya hivyo, kutampeleka sehemu ambayo wewe unataka akufanyie madhambi, ndani au pembeni ya penati boksi.”


3: JINSI YA KUPIGA PENATI

“Kwa kawaida mpigaji penati uwa na advantage kubwa zaidi.Acha mambo yote ya nje uwanja pembeni, na akili yako yote iwe kwenye na mpira-jinsi ya kuupiga, wapi utaupiga na namna ya kufunga goli.”


4: KAMA MCHEZESHAJI, CHEZA KWA UTULIVU UKIWA UNATAFUTA GOLI.

“Usi-panic, cheza kwa utulivu ndani ya aina ya mchezo wa asili.Usijipe pressure kutoa pasi ya mwisho, wachezaji wengine uwanjani wanaweza kufanya hivyo pia.”


5: USIJARI MANENO YA MPINZANI WAKO

“Ukiwa unajari mno maneno anayoyatoa mpinzani wako kiwanjani, utakosa concentration uwanjani, na hilo ndilo lengo lake.Jibu maneno yake kwa kucheza vizuri.”

JKT Ruvu 3 Coastal Union 0,Nyoso apata timu South Afrika.


Klabu ya Simba inatarajia kuvuna mamilioni mengine kutoka kwa beki wake ambaye pia huchezea 'Taifa Stars', Juma Nyosso baada ya kufikia muafaka na Klabu ya Platnum Stars inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini, ambayo imeonesha nia ya kumsajili.

Hapo jana JKT Ruvu ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Coastal union ushindi ambao uliwapeleka kileleni mwa msimamo wa ligi kuu y a VODACOM kwa kufikisha pointi 9.
mabao ya JKT Ruvu yalifungwa na Sostenes Manyasi,Rajabu Chau na Emmanuel Lucas.

MARSH AWAMWAGIA UPUPU MAKOCHA WA KIGENI




Kocha msaidizi wa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars Syllvester Marsh amesema moja ya sababu inayochangia timu ya taifa kufanya vibaya ni ubishi wa makocha wa kigeni.

Akihojiwa na Sports xtra ya Clouds fm, Marsh alisema kuwa kitendo makocha wa kigeni kudharau ushauri wa wazawa kinatokana na wao kuamini wazawa hawajui chochote kuhusu masuala ya soka.

Alisema kuwa alibaini kuwepo kwa fikra hizo zilizotawala miongoni mwa makocha wazungu wakati alipokuwa akifanya kazi na aliyewahi kuwa kocha wa timu za taifa za vijana, Marcus Tino baada ya kumwambia kwamba anashangaa kuona Tanzania ina makocha wazuri.

"Niseme ukweli kwamba, kuna tabia ya makocha wakigeni wanaokuja hapa kudharau ushauri wa wazawa, hii inatokana na wao kuamini pengine sisi hatujui chochote kuhusu soka.

"Ukweli makocha wakigeni wanaamini kwamba mpaka wao wanachukuliwa maana yake labda hapa hakuna kocha mzuri, kumbe si hivyo, Congo juzi tu wamemtimua kocha wao kwa sababu hizo hizo kwamba hashauriki.

"Kwa mfano wakati ule nafanya kazi na Tinoco aliwahi kuniambia kwamba kumbe Tanzania kuna makocha wazuri akionekana kushangaa, lakini sio suala la kulaumu kwasababu pengine mazingira ndiyo wanayakuta yanawafanya wafikiri hivyo,"alisema Marsh.

Marsh pia alizungumzia tabia ya makocha wa kigeni kutodumu muda mrefu kwa kusema kuwa, hilo linasababishwa hasa pale wanapokutana na mazingira tofauti na yale waliyoyategemea kuyakuta wakati wanatoka kwao.

"Mimi ni mzawa ninaweza kuvulimia kwasababu naijua vizuri hali halisi ya nchi yangu, lakini wao inakuwa vigumu kwasababu unakuta amezoea kupata kila kitu huko kwao sasa anapohitaji kitu fulani hasipotimiziwa hawezi kukaa,"alisema

Marsh amekuwa kocha msaidizi kwenye kikosi cha Taifa Stars kwa takribani miaka mitano tangu enzi za kocha Mbrazil Marcio Maximo, pia amewahi kuifundisha timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys akiwa kocha msaidizi wa Abdalah Kibadeni pamoja na kuzifundisha timu kadhaa za ligi kuu ikiwemo Kagera Sugar.



Monday, September 5, 2011

Washindi wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE




Washindi wa shindano la GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE waliopata nafasi ya kwenda nchini Afrika ya Kusini kuiwakilisha Tanzania:

014 - SULTAN MOHAMED SULTAN
- MANSOUR SEIF MANSOUR

003- HAFIDH MTORO MKAMBALA
- RAJAB SELEMAN RAJAB

011 - JUMA NASSOR JUMA
- MASUDI AMLANI MASUDI

002 - AMIRI ALLY AMIR
- IMAN JOSEPH MANDU

006 - NELSON ALLEN KESSY
- RAMADHANI RAMADHAN MTIBIRO

021 - LUKUBA GEORGE JOEL
- FREDY JORDAN NGULWA

007 - ALAWI OMAR RASHID
- ABDUL OMARI MADOHORA

009 - ALLY BIN ALLY MATUMBI
- RICK JOHN SANGA



















































MAPATO STARS v ALGERIA


Pambano la mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Algeria (Desert Warriors) limeingiza sh.148,220,000. Mechi hiyo ilichezwa Septemba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mashabiki waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo ni 29,892. Viti vya kijani ambavyo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 ndivyo vilivyovutia mashabiki wengi ambapo 17,650 ikiwa ni zaidi ya nusu ya mashabiki wote walinunua tiketi kwa ajili ya viti hivyo.

VIP A ambapo ndipo kulikokuwa na kiingilio cha juu cha sh. 30,000, jumla ya mashabiki 394 walinunua tiketi kwa ajili ya eneo hilo. Viti vya bluu ambapo kiingilio kilikuwa sh. 5,000, mashabiki walionunua tiketi walikuwa ni 8,166.

Viingilio vingine katika pambano hilo vilikuwa sh. 7,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 VIP C na sh. 20,000 VIP B.

TWIGA STARS YAPOTEZA MCHEZO WA KWANZA KWENYE ALL AFRICAN GAMES


Timu ya wanawake ya Taifa ya Tanzania (Twiga Stars) imepoteza mechi yake ya kwanza ya michezo ya All Africa Games (AAG) baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Ghana katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Machava, jijini Maputo.

Kwa mujibu wa Meneja wa Twiga Stars, Furaha Francis hadi mapumziko timu hiyo ilikuwa nyuma kwa bao 1-0. Mwanahamisi Shuruwa aliisawazishia Twiga Stars dakika ya 85, lakini Ghana ikapata bao la pili dakika tatu kabla ya filimbi ya mwisho.

Twiga Stars itacheza mechi yake ya pili Septemba 8 mwaka huu dhidi Afrika Kusini. Mechi ya mwisho katika hatua hiyo ya makundi itakuwa Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe
.

LUKAKU, FORLAN NA HARGREAVES KUWA WATAZAMAJI KWENYE CHAMPIONS LEAGUE



Wanasoka Diego Forlan wa Inter Milan na kiungo mpya wa Manchester City, Owen Hargreaves pamoja na mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku ni miongoni mwa wachezaji walionguliwa kwenye vikosi vya timu zao kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa.

Forlan aliyesajiliwa na Inter hivi karibuni aliichezea Atletico Madrid kwenye kusaka tiketi ya Europa Ligi kabla ya kuhamia Italia.Mshambuliaji huyo wa Uruguay alichezea Atletico dhidi ya timu ya Norway ya Stromsgodset katika hatua ya tatu ya kusaka kufuzu kwa michuano ya Europa.

Alijiengua kwenye mchezo dhidi ya Vitoria Guimaraes wakati huo akiwa na mazungumzo na klabu hiyo ya San Siro, lakini sheria ya UEFA inamzuia mchezaji huyo aliyecheza Europe kuichezea Inter sasa labda hadi mwakani.

Inter imepagwa Kundi B pamoja na CSKA Moscow, Lille na Trabzonspor, lakini bado safu yao ya ushambuliaji ipo imara kwa kuwepo kwa Giampaolo Pazzini, Diego Milito, Mauro Zarate na chipukizi kwenye miaka 18, kutoka Uholanzi, Luc Castaignos .

Hargreaves na Lukaku pia wameachwa kwenye vikosi vyao kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa.
Hargreaves, 30, aliyejiunga na City wiki iliyopita akiwa na tumaini na kurudi kwenye kiwango chake baada ya kuachwa na Manchester United.

Kiungo huyo wa zamani wa England bado anakazi kubwa ya kurudi kwenye kiwango chake baada ya kuwa majeruhi ya goti kwa muda mrefu na City wameamua kutomweka kwenye orodha 17 watakaocheza Ligi ya Mabingwa.

Wachezaji wengine nane kati ya 25 ni lazima wawe ni wale wa akiba wa nyumbani au chipukizi.

Kuondolewa huko kwa Hargreaves kunamfanya hakose mechi mbili za Kundi A dhidi ya timu yake ya zamani Bayern Munich, wakati City itapocheza kwa mara ya kwanza michuano hiyo.

Hata hivyo, kocha wa City, Roberto Mancini anayo nafasi ya kumtumia kwenye kikosi chake cha Januari kama atafanikiwa kufuzu kwa hatua ya makundi.

Wakati huohuo, mshambuliaji wa kimataifa wa Ubelgiji, Lukaku pia ameondolewa kwa kushangaza kwenye kikosi cha Chelsea kwa ajili ya mashindano hayo hatua ya makundi.

Lukaku aliyesajiliwa kwa pauni 18 milioni kutoka Anderlecht mwezi uliopita, ataweza kucheza kwenye 16 bora, lakini Chelsea imewajumuisha wachezaji waliosajili siku ya mwisho ya usajili Oriol Romeu, Juan Mata na Raul Meireles kwenye kikosi chao cha wachezaji 22.