Search This Blog

Tuesday, September 6, 2011

MIKAEL ARTETA NA NJIA 5 ZA KUWA IMARA KIAKILI MCHEZONI



Kiungo mpya wa Arsenal Mikael Arteta anajaribu kutoa mafunzo ni jinsi gani ya kuwa imara kiakili kipindi cha michezo migumu.


1: FIKIRIA KUSHINDA

“Kitu muhimu zaidi kabla ya mechi ni kwenda uwanjani ukiwa mentality ya ushindi.Huwezi ku-control pressuere ya mchezo hivyo ni vizuri kuji-control mwenyewe na kitakachoenda kutokea mchezoni.Kama unajiamini, then kipaji chako kitaonekana tu na uta-perform vizuri.”


2: USIOGOPE WALA USIWE NA JAZBA BAADA YA KUCHEZEWA RAFU KWA MARA KWA MARA.

“Mpinzani wako anapokuchezea vibaya hakikisha anaadhibiwa mapema ili ajiadhari kupata red card.Kufanya hivyo, kutampeleka sehemu ambayo wewe unataka akufanyie madhambi, ndani au pembeni ya penati boksi.”


3: JINSI YA KUPIGA PENATI

“Kwa kawaida mpigaji penati uwa na advantage kubwa zaidi.Acha mambo yote ya nje uwanja pembeni, na akili yako yote iwe kwenye na mpira-jinsi ya kuupiga, wapi utaupiga na namna ya kufunga goli.”


4: KAMA MCHEZESHAJI, CHEZA KWA UTULIVU UKIWA UNATAFUTA GOLI.

“Usi-panic, cheza kwa utulivu ndani ya aina ya mchezo wa asili.Usijipe pressure kutoa pasi ya mwisho, wachezaji wengine uwanjani wanaweza kufanya hivyo pia.”


5: USIJARI MANENO YA MPINZANI WAKO

“Ukiwa unajari mno maneno anayoyatoa mpinzani wako kiwanjani, utakosa concentration uwanjani, na hilo ndilo lengo lake.Jibu maneno yake kwa kucheza vizuri.”

No comments:

Post a Comment