Search This Blog

Friday, March 29, 2013

REKODI ZA WAFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA TIMU KUBWA ZA TAIFA DUNIANI: RONALDO, KLOSE, VAN PERSIE WAKARIBIA KUANDIKA HISTORIA MPYA


Wanasema si sahihi kufananisha vizazi tofauti kwenye soka, kila staa anadumu kwa wakati wake na uzito wake. Lakini kwenye soka hili limekuwa halikwepi, kila siku tunawafananisha Messi au Maradona? Pele au Ronaldo? Ni mjadala unaozidi kuwa mkubwa kila siku iendayo kwa mungu.

Wakati tuliopo kwenye kizazi cha soka, linapokuja suala la wafungaji bora wa muda wote wa timu za taifa, kuna namba kubwa ya timu kubwa ambazo aidha tayari zina wachezaji wapya ambao ndio wafungaji bora wa muda wote au zinakaribia kufanya hivyo hivi karibuni. Inavyoonekana kipindi cha miaka 10 kutoka 2007 mpaka 2017 kinaweza kukumbukwa kama ndio kipindi ambacho historia ziliandikwa upya. Tayari historia zimeanza kuandikwa kuanzia Uruguay, France, Cote d'Ivoire, Spain na United States na pia Germany, Portugal na Holland zipo karibuni kupata wafalme wapya waliofumania nyavu mara nyingi wakiwa na jezi ya timu ya taifa husika, pia England, Sweden, Mexico and Argentina zinaweza zikafuatia.

Miroslav Klose kwa sasa ni majeruhi lakini amebakiza goli moja tu kuweza kuifikia rekodi ya gwiji Gerd Muller ambaye aliifungia Ujerumani mabao 68, wakati Kloseana mabao 67. Inavyoonekana hawezi kustaafu bila kuifikia rekodi hiyo.

Akiwa hajafunga mechi kadhaa ndani ya klabu ya Manchester United, Robin Van Persie amekuwa na hali tofauti ndani ya timu ya taifa ya Uholanzi, katika mechi za hivi karibuni amefunga mabao 3 katika mechi 2 dhidi ya Romani na Estonia, hivyo kufanikiwa kumpita Johan Cruyff kwenye listi ya wafungaji bora wa uholanzi , huku akifanikiwa kumfikia Klaas-Jan Huntelaar wote wakiwa na mabao 34. Van Persie na Huntelaar wote wanatimiza miaka 30 kipindi kijacho cha kiangazi na wote wanapigania namba ndani ya kikosi cha Van Gaal, wote wana nafasi ya kuifikia rekodi ya mabao 40 iliyowekwa na Patrick Kluivert.

Kijana mwingine ambaye anakaribia kuifikia rekodi iliyopo kwenye timu yake ya taifa ni Cristiano Ronaldo. Anashika nafasi ya tatu kwenye listi ya wafungaji bora wa muda wote wa Ureno, akiwa na mabao 38, nyuma ya Eusebio aliyemzidi matatu na Pauleta aliyemzidi tisa - lakini Ronaldo ndio kwanza ana miaka 28 aliyotimiza mwezi uliopita.

Kwa upande wa mabingwa wa dunia na ulaya Spain, David Villa tayari ameweza kuwa mfungaji bora wa muda wote wa La Furia Roja akiwa na mabao 53, akimpita Raul miaka miwili iliyopita. Ana miaka 31, hivyo tutegemee kuona idadi hiyo ikiongezeka mpaka siku atakapostaafu. 



Mwezi October 2011, Diego Forlan alimpita mkongwe Hector Scarone -- shujaa wa Copa America 1920s na kombe la dunia mwaka 1930 -- na kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Uruguay. Lakini mazingira yaliyopo yanayoonyesha kwamba Forlan, ambaye ana mabao 33, atapitwa siku chache zijazo na mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez mwenye mabao 31, na akiwa na miaka 7 pungufu kuliko aliyonayo Forlan.

Rekodi ya Michel Platini ya ufungaji bora wa muda wote kwa Ufaransa ilivunjwa mwaka 2007 wakati Thierry Henry, wakati huo akiwa na miaka 30, alimpita Platini aliyekuwa na mabao 41. Henry amestaafu kuichezea Les Bleus ingawa rekodi yake ya mabao ya 51 itaendelea kudumu kwa muda fulani. Mfungaji bora wa muda wote wa Cote d'Ivoire ni Dider Drogba ambaye ana mabao 60.


Penginepo? Wayne Rooney ana mabao 35 ndani ya jezi ya England. Ana miaka 27 na rekodi ya England inashikiliwa na Sir Bobby Charlton mwenye mabao 49, hivyo Rooney anahitajika kufunga mabao 15 ili aweze kuivunja rekodi hiyo. Zlatan Ibrahimovic ana mabao 31 na anahitaji mabao mengine 10 kuifikia rekodi ya Sven Rydell, jambo hilo linawezekana kwa kiwango alichonacho Zlatan hivi sasa.

 

Halafu kuna Lionel Messi: Gabriel Batistuta, ndio mfungaji bora wa muda wote wa Argentina akiwa na mabao 56. Lakini mwenye umri wa miaka 25 tayari ana mabao 32, anahitaji mengine 24 kuifikia rekodi ya Batgoal

 

Mexico pia wanakaribia kumpata mfungaji bora mpya: Javier Hernandez ana mabao 30 -- anayeshikilia rekodi Jared Borgetti ana mabao 46 -- lakini Chicharito bado mdogo sana akiwa na miaka 24.

 
Timu kubwa ambazo inaonekana itakuwa taabu sana kwa rekodi za wafungaji bora wa muda wote kubadilika hivi karibuni ni Brazil na Italia. Pele aliweka nyavuni mipira 77, anayemfuatia Ronaldo ameshaastafu, huku kwa upande wa Italy rekodi ya mabao 35 ya  Gigi Riva itakaa sana mpaka Mario Baloteli aje kuifikia.
 

HAZARD, DEMBELE, FELLAINI, KOMPANY, NA MASTAA WENGINE WATAISHANGAZA DUNIA WAKIFUZU KWENDA BRAZIL 2014


Kuna miezi 14 imebaki mpaka kuanza kwa kombe la dunia nchini Brazil na kutoka kwenye matokeo ya michezo ya kufuzu mpaka sasa, tunaweza kutabiri timu mbili za juu kutoka kwenye kila kundi la brani ulaya. 
Katika kila msimu wa kombe la dunia, kumekuwa kukiwepo na timu ambazo hazipewi nafasi kabla ya mashindano ambazo huja kufanya vizuri. Uruguay ilisafiri kwenda South Africa wakiwa kama underdog mwaka 2010 lakini uwezo walionyesha uliwashangaza wengi. Wakiwa kwenye kiwango bora kabisa katika hatua za mwanzo, na hatimaye wakaishi mikononi wa Uholanzi kwenye nusu fainali.

Swali la kawaida ambalo lnaulizwa ni timugani isiyopewa nafasi itakayowasumbua vigogo katika kombe la dunia lijalo. Kuna timu nyingi kama vile Colombia, mabingwa wa AFCON Nigeria, labda Japan, lakini timu ambayo inaaminika italeta usumbufu mkubwa bila shaka ni Ubelgiji. 

Mapinduzi ya kizazi cha dhahabu cha soka la Ubelgiji:
Kizazi cha soka cha sasa cha Ubelgiji kinatajwa kutokea kwenye kipindi hiki wakiwa na lundo la wachezaji wenye vipaji vikubwa kwenye nafasi zote dimbani. Ukiacha wachezaji wanaoanza kwenye kikosi cha kwanza cha timu ya taifa, walio benchi karibia wote wanatajwa kuwa na thamani ya zaidi ya £10M. Rekodi yao kwenye cha hivi karibuni ni nzuri na kuvutia mno. Uimara wa timu yao upo kwenye maeneo yote muhimu. 



Kwenye ulinzi:
Wanaonza: Jan Vertonghen, Daniel Van Buyten, Vincent Kompany/ Thomas Vermaelen, Guillaume Gillet.

Tangu ahame kutoka Ajax kwenda Spurs kipindi cha kiangazi kilichopita, nafasi ya Jan Vertonghen katika kikosi cha kwanza imekuwa sio swali. Akiwa na uwezo wa kucheza kama beki wa kati pamoja na nafasi ya kushoto, Vertonghen amecheza part kubwa sana katika ukuta wa Spurs msimu huu. Uwezo halisi wa  Vertonghen uliwekewa kizuizi kwa majukumu ya ulinzi tu lakini ana uwezo mkubwa wa kushambulia na kufunga pamoja na kutengeneza nafasi kwa wenzie, angalia uwezo alionesha kwenye mechi dhidi ya Liverpool na Manchester United akifunga mabao muhimu.

Ukuta wa UBelgiji pia unaundwa na mchezaji mwengine kiraka aitwaye Guillaume Gillet. Mchezaji mwenye umri wa miaka 28 ambaye ana uwezo wa kucheza kama kiungo wa kati pia beki wa kulia, akicheza kwa kiwango kikubwa kwenye sehemu zote hizo. Goli lake dhidi ya Croatia katika mechi za kufuzu kombe la dunia, mwezi wa tisa mwaka jana, mchezo ulioisha kwa matokeo ya 1-1 lilionyesha ana msaada gani kwa timu yake. 


Nafasi ya ulinzi ya kati ya Ubelgiji inaonekana kuwa imara anapocheza Van Buyten na Kompany katikati. Van Buyten amekuwa na wakati mzuri na Bayern Munich msimu huu, akicheza karibia kila mchezo kwa timu hiyo ya Ujerumani. Ameweza kuuleta ushirikiano wake na Dante kwa Kompany. Uelewano uliopo baina ya wawili hawa ni mzuri sana. Komapny, ambaye alishinda taji na City msimu uliopita ana uwezo wa kucheza kwa kiwango cha juu sana, uelewano wao na Buyten unafananishwa na Maldini-Nesta Partnership.

 
Nafasi ya kiungo:
Waanzaji: Mousa Dembele, Kevin Mirallas, Eden Hazard, Marouane Fellaini, Axel Witsel.

Jukumu alilopewa Mousa Dembele ndani ya Spurs ni tofauti na alilokuwa nalo Fulham. Martin Jol alimchezesha Dembele kama mchezeshaji wakati akiwa Fulham, wakati Villas boas amempa majukumu ya kiungo wa ulinzi. Kiwango cha Dembele kama kiungo mchezeshaji kilikuwa kizuri sana lakini majukumu mapya ya kiungo mkabaji yamezidi kumkamilisha Dembele, na ushirikiano wake aliounda na Scot Parker umekuwa na mafanikio sana kwenye kikosi cha Spurs. Namna anavyoutumia mwili wake na uwezo anakuwa kiungo mzuri sana wa ukabaji. 

Wakati tunajadili kuhusu kiungo wa aina ya When we discuss about box-to-box kwenye soka la kisasa, tunaweza tukamuweka mtu kama Artuto Vidal, Yaya Toure na listi haitokamilika kama tutashindwa kumuweka,  Marouane Fellaini. Kiungo mwenye miaka  25 anayeichezea, amekuwa tishio kubwa sana kwenye ligi kuu ya England, anaweza akasababisha hatari kwenye eneo lolote dimbani. Stamina alionayo, kasi, uwezo wa kupiga mipira mirefu imemfanya thamaniyake ipande mpaka kuwa £25M.
Kevin Mirallas ni tunda jingine linalopikwa pale Merseyside, kiungo ambaye ana uwezo wa kuchachafya ngome za wapinzani akitokea pembeni. Akicheza upande wa kushoto, Mirallas amekuwa na uelewano mkubwa na Fellaini, wakicheza wote kwenye klabu moja, uelewano wao unaleta taabu sana kwa wapinzani wao.

Manchester City, Manchester United na Chelsea walikuwa ladhi kulipa zaidi ya £30M kwa kiungo wa Lille, Eden Hazard mwaka jana. Baada ya tetesi za muda mrefu Hazard akaamua kujiunga na Chelsea kwa ada ya uhamisho wa £32.5M. Alipowasili  Stamford Bridge, Hazard alionyesha kiwango kizuri na kuleta mabadiliko ndani ya timu chini ya kocha aliyetimuliwa Roberto Di Matteo. Jukumu la Hazard kwenye kikosi cha sasa cha Chelsea ni muhimu sana, hasa kwenye siku za hivi karibuni ameonyesha kiwango kizuri, akiisadiai timu yake kuendelea kuwa ndani ya FA Cup akifunga goli la kusawazisha dhidi ya Man United wiki mbili zilizopita pale Old Trafford.
Bado wana kiungo mwingine mwenye thamani ya £32.5M, anayeichezea klabu ya Russia Zenit, Axel Witsel. Zenit walilipa fedha nyingi sana kwa Benfica ili kumsajili Witsel, ingawa bado hajaonekana kuwa muhimu sana nchini Russia, bado anahesabika kama mmoja ya viungo bora barani ulaya wenye uwezo wa kubadilisha matokeo muda wowote dimbani. Timu kubwa barani ulaya zimeonyesha zipo tayari kulipa kiasi kisichopungua £25M kumtoa mbelgiji huyo kutoka Russia.


Ushambuliaji:
Muanzaji: Christian Benteke.
Ukiachana na Christian Benteke, Romelu Lukaku ni mshambuliaji mwingine ambaye anaweza akaanza kwenye kikosi cha kwanza, lakini kutokana uwezo mkubwa umaliziaji Benteke anaaza mbele ya kinda la Chelsea, kocha Wilmots amekuwa anapenda kumuanzisha mshambuliaji wa Aston Villa siku za hivi karibuni.

World Cup 2014:
Belgium kwa sasa ndio wanashika nafasi ya pili katika kundi A kuwania kufuzu kwenda Brazili, wakiwa na pointi 13 kwenye mechi tano walizocheza, wakiwa nyuma ya Croatia waliowazidi kwa tofauti ya mabao.
 Ukiangalia ubora wa kikosi chao cha sasa, inategemewa kwamba  Belgium wanaweza kufuzu kwenda Brazil. Ikiwa watafuzu, wakaenda na kufanya vizuri hata kufikia hatua ya nusu fainali haitowashangaza wengi kama ilivyotokea kwa Uruguay, South Korea au Turkey miaka nyuma, kutokana na ubora wa wachezaji waliojazana kwenye kikosi chao.

Thursday, March 28, 2013

MSIMAMO WA LIGI KUU YA TANZANIA BARA NA RATIBA YA MECHI ZA WIKIENDI HII - RUVU YATAMBA KUICHINJA AZAM

Maafande wa jeshi la kujenga taifa, Ruvu Shooting ya mkoani Pwani wametamba kuwamaliza Azam Fc, Lambalamba katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara unaotarajiwa kupigwa uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani jumamosi ya wiki hii.

Ruvu Shooting wenye pointi 29 ,nafasi ya saba ya msimamo watashuka katika dimba lao la nyumbani kusaka ushindi ili kumaliza msimu huu wa ligi wakiwa nafasi nne za juu.

Akizungumza na mtandao huu, Afisa habari wa Ruvu shooting, Masau Bwire, amesema kuwa maandalizi ya mchezo huo yanakwenda barabara huku kocha mkuu wa klabu hiyo Charles Boniface Mkwasa “Master” akirekebisha makosa yaliyojitokeza mechi iliyopita ambayo walifungwa 1-0 na vinara wa ligi hiyo, klabu ya Yanga.
Masau alisema Azam fc jana walishinda 3-0 dhidi ya wapiga kwata wenzao wa Tanzania Prisons hali ambayo imewapa nguvu kubwa ya kuwania ubingwa, lakini mchezo wao wa Jumamosi wasitarajie urahisi hata kidogo.
“Wapinzani wetu wamefanya vizuri kombe la shirikisho kwa kuwafunga Barrack Young Controller II mabo 2-1 ugenini, jana wamepata matokeo mazuri mbele ya Prisons na wanazidi kuamsha mizimu ya kuusaka ubingwa, sisi tunahitaji nafasi ya kushiriki hata Tusker cup mwaka huu, hatukubali kufungwa”. Masau alitamba.
Afisa habari huyo ameongeza kuwa mchezo uliopita dhidi ya Yanga ambao walipoteza, walistahili kushinda kutokana na kiwango cha vijana wao, lakini walikosa nafasi nzuri za kufunga na wapinzani wao walipata nafasi moja waliyoitumia kupata ushindi.
Masau alisema Mkwasa anaendelea kunoa makali ya washambuliaji wake wakiwemo Hassan Dilunga, Said Dilunga, Ernest Ernest, Ayubu kitala ili kuibuka wababe katika mchezo huo wa kukata na shoka.
“Watanzania wanawajua vizuri Ruvu shooting, moto tunaowasha si mchezo, tutawapiga Azam fc na baada ya hapo tutaanza hesabu za kuwavaa Polisi Morogoro wiki ijayo”. Masu aliongeza.
Akizungumzia malengo yao kwa sasa, msemaje huyo amesema wapo nafasi ya saba na ponti 27 huku wakiwa na michezo saba kibindoni, hali hii inawapa matumaini ya kufanya vizuri na kushika hata nafasi ya nne ili kucheza kwa mara ya kwanza michuano ya kimataifa yaani kombe la Tusker linaloshirikisha klabu za afrika mashariki.
Kwa upande wa Azam fc kupitia kwa afisa habari wao Jaffar Idd Maganga wamesema kuwa mchezo  huo utakuwa mgumu sana kwao na wanauchukulia kwa umakini mkubwa sana ili kupata pointi tatu na kuendeleza harakati zao za kuwania ubingwa.
Pia alisema mchezo huo wataumia kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa marudiano wa kombe la shirikisho dhidi ya Waliberia, Barrack Fc machi 9 mwaka huu dimba la taifa jijini Dar es salaam.
“Sisi kila mchezo kwetu ni fainali, katu hatudharau timu yoyote ya ligi kuu, tuna safari ndefu na tunakabiliwa na michuano ya kimataifa, lakini tunafanya jitihada kubwa kujiandaa kwa ajili ya mashindano yote, na jumamosi tutashinda kama jana”. Idd alisema.
Azam fc wapo nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu wakiwa na pointi 40 huku Yanga wakiwa kileleni na pointi 48. Mabingwa watetezi simba wanabakia nafasi ya tatu na pointi 34 baada ya kupoteza 1-0  mchezo wa jana dhidi ya Kagera sugar.
Ligi kuu kwa sasa imejigawa katika makundi matatu, kundi la kwanza ni timu zinazowania ubingwa wa ligi kuu kwa maana ya Yanga, Simba na Azam fc, kundi la pili ni zle zinazowania nafasi mojawapo za juu, Mtibwa Sugar, Coastal union, kagera sugar, JKT Oljoro, Ruvu shooting na kundi la mwisho ni zile zinazowania kukwepa mkasi wa kushuka daraja, JKT Ruvu, Tanzania Prisons, Toto Africans, African Lyon.

RATIBA: Jumamosi Machi 30
JKT OLJORO v JKT RUVU [SH. AMRI ABEID, ARUSHA]
RUVU SHOOTINGS v AZAM FC [MABATINI, PWANI]
AFRICAN LYON FC v COASTAL UNION [AZAM COMPLEX, KAGERA]
POLISI MOROGORO v YOUNG AFRICANS [JAMHURI, MOROGORO]
KAGERA SUGAR v MTIBWA SUGAR FC [KAITABA, KAGERA]
TOTO AFRICANS v SIMBA SC [CCM KIRUMBA, MWANZA]

MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
YANGA
20
15
3
2
25
48
2
AZAM FC
20
12
4
4
19
40
3
SIMBA
20
9
7
4
11
34
4
KAGERA
21
9
7
5
5
34
5
COASTAL
21
8
8
5
4
32
6
MTIBWA
21
8
8
5
4
32
7
RUVU SHOOTING
19
8
5
6
3
29
8
JKT OLJORO
21
6
7
8
-3
25
9
MGAMBO
21
7
3
11
-6
24
10
PRISONS
21
4
8
9
-9
20
11
JKT RUVU
18
5
4
9
-12
19
12
POLISI
21
3
8
10
-10
17
13
TOTO
21
3
8
10
-12
17
14
LYON
21
4
4
13
-18
16

BONANZA LA WAANDISHI LAHAMIA TCC KWASABABU YA MECHI YA AZAM VS BARRACK YOUNG CONTROLLERS

BONANZA la vyombo mbalimbali vya habari lililopangwa kufanyika Aprili 6 mwaka huu viwanja vya Leaders Klabu likiandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), sasa litafanyika viwanja vya Sigara (TCC), Chang’ombe pia Dar es Salaam.

Uamuzi wa kuhamisha bonanza hilo umechukuliwa na sekretarieti ya TASWA kutokana na maombi ya waandishi wengi wa michezo kwa vile siku hiyo kuna mechi ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika kati ya timu ya soka ya Azam na Barrack Young Controllers ya Liberia  itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam siku hiyo.

Azam ni timu pekee ya Tanzania iliyobaki kwenye michuano ya Afrika kwa ngazi ya klabu baada ya Simba na Jamhuri ya Pemba kutolewa katika raundi ya awali.

Tunaamini kwa bonanza kufanyika Sigara itakuwa rahisi kwa wadau wetu kushiriki kwenye bonanza na wale wengine watakaohitaji kwenda uwanjani wafanye hivyo wakitokea Sigara kwa hakuna umbali mrefu na kisha warejee kujumuika na wenzao mpaka mwisho.

Tunawaomba radhi kwa mabadiliko hayo, lakini yakiwa na lengo la kujenga na kuwa pamoja na wenzetu wa Azam kuhakikisha tunashirikiana nao kwa namna mbalimbali siku hiyo.

Bonanza hili linadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) likiwa na lengo la kuwaweka pamoja waandishi wote wa habari bila kujali ni wa siasa, michezo, uchumi, afya na mambo mengine pamoja na wafanyakazi wa vyombo mbalimbali vya habari ili kubadilishana mawazo na kufurahi pamoja.

Bonanza hilo ambalo litahusisha wadau 1,500 kutoka vyombo mbalimbali vya habari litaambatana na michezo mbalimbali itakayohusisha vyombo vyote vitakavyoshiriki na pia kutakuwa na burudani ya muziki kutoka katika moja ya bendi kubwa za muziki wa dansi hapa nchini, ambayo itatangazwa siku zijazo.

Nawasilisha

Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA

WAKENYA WAFURUKUTA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE


Washindi wa kipindi cha pili cha Guinness Football Challenge,Kepha Kimani kutoka Thika Kenya(kushoto) na Francis Ngigi kutoka Nairobi Kenya(kulia) katika picha ya pamoja na watangazaji wa kipindi hicho Larry Asego and Flavia Tumsiime jana baada ya ushindi.

EXCLUSIVE INTERVIEW NA MAMADOU GAYE - AWAPONDA TENGA NA VIONGOZI WENGINE WA VYAMA VYA SOKA AFRIKA KWA KUWA VIBARAKA WA HAYATOU


Siku mbili zilizopita mshauri na mchambuzi wa masuala ya soka la kiafrika kutoka nchini Ivory Coast Mamadou Gaye alifanya mahojiano ya kipekee na mtandao kuhusu mambo mbalimbali yanayohusiana na soka la Afrika, kuanzia michuano ya kufuzu kombe la dunia ambapo nchi yake ya Ivory Coast ipo kundi moja na Tanzania, mpaka kuhusu uchaguzi wa uraisi wa shirikisho la soka la Afrika CAF.

Mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo:

Watu wa Ivory Coast wameupokeaje ushindi wa Tanzania dhidi ya Morocco ikizingatiwa kuna pengo la pointi moja inayowatenganisha na Taifa Stars kwenye msimamo wa kundi lao?

Mamadou: Ushindi wa Tanzania umetengeneza sana vichwa vya habari vya magazeti. Pia nadhani ushindi huu umeiletea heshima kubwa nchi yenu kwenye soka, ni mafanikio makubwa.

Ni lini ilikuwa mara ya mwisho kwa Ivory Coast kucheza mechi ya mashindano ya ukubwa kama wa mashindano haya bila uwepo wa nahodha aliyeachwa Didier Drogba? 

Mamadou: Hii sio mara ya kwanza kwa drogba kutokuwemo kwenye kikosi cha Ivory Coast, nakumbuka hata kwenye mechi za kuwania kufuzu kwenye AFCON 2012 Drogba hakucheza mechi nyingi, pia kwenye AFCON 2013 kuna baadhi ya mechi alianzia benchi. Timu yetu ya Taifa haina upungufu kwenye ushambuliaji, Drogba kwa sasa hana umuhimu mkubwa, na kwa upande wangu nadhani hakustahili hata kuwemo kwenye kikosi kilichoshiriki AFCON 2013.

Hatimaye uchaguzi wa CAF hivi karibuni umemrudisha tena Issa Hayatou madarakani kwa kipindi kingine. Je ni yapi maoni yako kuhusu ushindi wake? 

Kamati kuu ya CAF.

Mamadou: Nadhani hii ni aibu kubwa kwa soka la Afrika, kwa kitendo cha Issa Hayatou kuwarubuni maraisi wa vyama vya soka barani Afrika kufanya marekebisho ya sheria ya uchaguzi ili kuweza kumuondoa kwenye kugombea nafasi ya uraisi bwana Jacques Anouma.

Hii inanikumbusha miaka ile ya nchi za Afrika kufanya uchaguzi kwa kuchagua mtu mmoja kupitia mfumo wa sera ya chama kimoja. Hili suala linarudisha nyuma maendeleo ya mpira ndani ya bara letu. La kusikitisha zaidi kuhusu wafanya maamuzi wa CAF, ni kwamba Amadou Diakite wa Mali ambaye alifungiwa na FIFA kwa tuhuma za rushwa michezoni anaruhusiwa kuingia kwenye kamati ya utendaji ya CAF ambayo inatoa maamuzi ya kumpitisha Hayatou agombee pekee yake. 

Pia Anjorin Musharraf ambaye alifungwa nchini kwake kwa kugundulika kujihusisha na rushwa michezoni pamoja na kula fedha za udhamini, na baada ya kutoka kwa dhamana, Issa Hayatou akamruhusu kuingia kwenye kamati ya utendaji ya CAF. Hili linakupa picha kwamba CAF ni nyumba inayonuka rushwa chafu yenye sumu ambayo imeanza kusambaa kwenye vyama vya soka vya nchi wanachama, ambao baadhi yao wameonekana kuanza kuiga njia ya Hayatou kwa kubadili katiba au sheria za uchaguzi kwa manufaa yao.

Na pindi baadhi ya watu au serikali inapoingilia utaratibu huo mbovu, viongozi wa shirikisho wanakimbilia FIFA kusema vyama vinaingilia na mamalaka nyingine za nchi ili FIFA watishie kuifungia nchi na hatimaye serikali ziogope na viongozi wa mashirikisho waweze kutimiza azma zao.

Kamati kuu yote ya CAF imejaa wala rushwa na viongozi wabinafsi wenye kuangalia maslahi yao binafsi. Hayatou na wenzie wote ni wamoja. Raisi wa sasa wa shirikisho la soka la Tanzania ni mjumbe wa kamati kuu, yeye ni mmoja ya wafuasi wa Hayatou. Kama sio kama anaona upuuzi wote unaofanyika chini ya kamati yao ilibidi awajibike kujitoa kwa kujiudhuru kwenye kamati hiyo, lakini hakuna anayefanya hivyo. Wajumbe wote wa kamati kuu ni wamoja na wanasapoti vyote anavyofanya Issa Hayatou."

Wednesday, March 27, 2013

MNYAMA ACHINJWA BUKOBA - AZAM YAWALAMBISHA KONI PRISONS



Mabingwa watetezi wa VPL, Simba SC leo wameendelea kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wao baada ya kufungwa bao 1-0 na Kagera Sugar katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera. Kwa upande mwingine Azam FC leo hii wameishindilia Prisons 3-0 kwa dimba la Chamazi.
Kikosi cha Kagera Sukari (PICHA ZOTE KWA HISANI YA BUKOBASPORTS.COM)
Waamuzi wa leo hii waliochezasha mpambo

Waamuzi na makapteni wakiteta jambo
Benchi la Kagera Sukari
Benchi la Simba
Wadau wakifuatilia soka

Tangu Mechi ianze kocha huyu wa Simba alionekana kuwa na mawazo sana

Kocha wa Kagera Sugar King Kibadeni
Wachezaji wakisalimiana




Uwanja wa Kaitaba unavyofanana ambao unauwezo wa Kuingiza watu 3,000
Mtanange ukiendelea
Mchezaji wa Kagera Sukari akiangaliwa baada ya kuumia









Wadau mbalimbali wa Soka
Ubao huooooo...dakika 90
Mpira umeisha...Kagera Sugar 1 Simba 0.

EXCLUSIVE: KUONDOKA KWA THOMAS MLAMBO NA MAMADOU GAYE SUPER SPORT

Thomas Mlambo wa kwanza kushoto,Mamadou Gaye ni wa pili kutoka kushoto.


Katika siku za hivi karibuni wapenzi wa kipindi cha soccer Africa kinachorushwa kwenye Super Sport wamekuwa wakijiuliza ni wapi walipo wachambuzi mahiri waliokuwa wanaounda timu ya watangazaji wa kipindi hicho Thomas Mlambo na Mamadou Gaye.

Kwa taarifa za uhakika kutoka kwa Mamadou Gaye na Thomas Mlambo ni kwamba wawili hao kwa sasa sio wafanyakazi tena wa kituo hicho.

Thomas Mlambo ameacha kazi Super Sport na kujiunga na shirika la utangazaji la South Africa (SABC) baada ya kupewa mkataba mnono zaidi na shirika hilo ambalo lipo chini ya serikali ya Afrika Kusini.

Kwa upande wa Mamadou Gaye ambaye mara ya kwanza alisimamishwa baada ya kutoa shutuma nzito kwa baadhi ya vyama vya soka na viongozi wake ndani ya bara la Afrika, hasa kwa shirikisho la Zambia na Raisi wake Kalusha Bwalya.

Akizungumza na mtandao huu Mamadou amesema alisimamishwa na kituo hicho baada ya kutoa shutuma za ukweli kwa Shirikisho la soka la Zambia na Raisi wake Kalusha Bwayla kuhusu kuwa mmoja wa vibaraka wa Issa Hayatou, na kutokana na ushawishi alionao Bwalya kwa kufanya biashara na Super Sport kwa kuwapa dili la kuonyesha ligi kuu ya Zambia, hivyo akasimamishwa. Pindi walipomuita kurudi kazini Mamadou akagoma kwa sababu aliamini alisimamishwa kwa kuifanya vizuri kazi yake.

UJUMBE WA FIFA KUSIKILIZA WAGOMBEA WA UCHAGUZI MKUU TFF APRILI 16


SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo lilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokana na baadhi ya wagombea kulalamika kuenguliwa sasa litatuma ujumbe wake nchini katikati ya mwezi ujao.

Ujumbe huo ambao moja ya shughuli zake kuwasikiliza wote walioenguliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na hawakuridhika na uamuzi huo, utakuwepo nchini Aprili 16 na 17 mwaka huu.

Kwa mujibu wa barua ya Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valcke kwenda kwa Rais wa TFF, Leodegar Tenga, kazi ya ujumbe huo ni kubaini tatizo lililopo na kutoa ripoti kwa mamlaka zinazohusika ndani ya FIFA kwa ajili ya kutoa mwongozo.

Ujumbe huo utakutana na pande mbalimbali zinazohusika wakiwemo wagombea, kamati za uchaguzi za TFF. Lakini pia ujumbe huo unatarajia kumtembelea Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara pamoja na watendaji wake wizarani.

Uchaguzi wa viongozi wa TFF ulikuwa ufanyike Februari 24 mwaka huu, lakini ukasimamishwa na FIFA baada ya baadhi ya wagombea walioenguliwa kulalamika kuwa hawakutendewa haki na wangependa shirikisho hilo liingilie kati.

EXCLUSIVE: HAYA NDIO MAZINGIRA YA UWANJA WA LAKE TANGANYIKA KIGOMA - FREMU ZA MADUKA

Wakati kwenye viwanja vingine vyote duniani fremu za nje zinazonguka uwanja zimekuwa zikitumika kama vitega uchumi kwa wamiliki wa uwanja husika, hali ni tofauti mkoani Kigoma kwenye dimba la Lake Tanganyika. Uwanja huo mkongwe ambao unaingiza mashabiki takribani 20,000, upo kwenye hali mbaya kuanzia ndani mpaka nje.
 Sasa hivi fremu zilizozunguka uwanja huo zimegeuka makazi ya watu, haijaweza kufahamika kama wamekodi au wanaishi tu bure. Hata kama wanalipa lakini fremu hizo hazikuwa za matumizi ya watu kuishi kwenye eneo hilo.

Matokeo yake uwanja huo mkubwa wa mkoa umezidi kuwa kwenye mazingira mabovu, na inawezekana ukosefu wa mapato ya milangoni kutokana na kutokuwepo kwa mashindano ya maana ya kuvuta washabiki kuingia uwanjani hivyo kuzidi kusababisha ukosefu wa fedha za kuweza kuboresha mazingira ya uwanja huo.


CHAGUA JIBU SAHII

MARIO BALOTELLI, NIANG NA STEPHAN El SHAARAWY - MWANGA MPYA WA MATUMAINI NDANI YA AC MILAN


 31st January 2013 Mario Balotelli alikamilisha uhamisho wa  €20m kutoka Manchester City kujiunga na klabu yake ya utotoni. Adriano Galliani, makamu mwenyekiti wa Milan, alisema "Balotelli ndani ya Rossoneri ni ndoto ambayo imekamilika. Ni uhamisho ambao kila mtu aliutaka; klabu, raisi na mashabiki." 
  Aidha uhamisho huu ndio uliosababisha kuondoka kwa Pato kurudi Brazil na Robinho kuendelea kufeli au vyovyote ilivyokuwa inasemwa, kama jaribio la kupata kura kwa viongozi lakini yote hayakuwa na maana, la msingi Balo alikuwa amerudi nyumbani.

 Kwa vyombo vya habari vya Uingereza ndoto ilikuwa imeisha, kijana ambaye alisababisha matukio mengi ya utata yaliyoleta burudani na kutengeneza vichwa vya habari vingi alikuwa ameondoka. Ingawa uhamisho huu ndio kitu ambacho Mario anahitaji, ingawa itamuumiza kutengana na baba yake wa soka Roberto Mancini, hapa ndio mahala ambapo anaweza kuthibitisha ubora na kuwa kwenye daraja la washambuliaji bora duniani. Hivyo Balo anaihitaji Milan, Milan wanamtaka Balo, lakini je Milan kama timu inamhitaji Balo? 


Kwa wale ambao wanaangalia soka kwa mbali wanaweza wakawa wanadhani kwamba Milan bado ni timu yenye nguvu kama ilivyokuwa zamani. Miongo na miongo ya mafanikio yaliyoifanya Milan kuwa moja klabu kubwa ulimwenguni lakini kwenye miaka ya hivi karibuni historia hii nzuri imeanza kudondoka. Kuondoka kwa  Pirlo,  Dida,  Ibrahimovic,  SilvaMaldiniNestaGattuso na wengineo. Magwiji wa kweli kama vile Maldini imeshindikana kuziba mapengo yao, au pale vipaji kama vile cha Thiago Silva ambavyo walikuwa ndani ya timu wameshindwa kuwashikilia. AC wana matatizo ya kifedha kama ambavyo Berlusconi alivyokiri kwamba anaweza akaiuza klabu, mastaa waliruhusiwa kuondoka huku wahudhuriaji na mauzo ya tiketi yakishuka. Ingawa, mwanga wa matumaini umeonekana: wachezaji watatu, mwenye umri mkubwa kati ya hawa ana umri wa miaka 22.  M’Baye Niang (18), Stephen El Shaarawy (20) and Mario Balotelli (22)... Je hawa wanaume watatu wanaweza wakawa waokozi wa Milan???

 Rossoneri wamekuwa na vipaji vingi vya ushambuliaji katika historia yao, hivi karibuni ShevchenkoInzaghi na Kaka ndio walikuwa watu watatu waliotingisha sana nyavu za wapinzani lakini kwenye miaka ya 1950s walikuwa na wasweden watatu waliojulikana kama Gre-No-LiGunnar GrenGunnar Nordahl na Nils Liedholm walikuwa washindi wa medali za dhahabu kutoka kwenye mashindano ya 1948 London Olympics na ndani ya misimu miwili wote watatu walijiunga na Milan. Kwenye msimu wa 1949/50 Milan walifunga mabao 118 kwenye mechi 38 huku  Gunnar Nordahl akifunga 35 na kufuatiwa na ubingwa wa scudetto mwaka uliofuata. Kila mchezaji alikuwa na mafanikio ya namna yake ndani ya Giuseppe Meazza.
     Gunnar Gren, Gunnar Nordahl & Nils Liedholm (Gre-No-Li)

Gunnar Gren walikuwa na muda mfupi ndani ya Rossoneri, alifunga mabao 38 kwenye mechi 133 za ligi. Il Professore (“The Professor”) alikuwa kocha kwa muda mfupi mwaka 1952 kabla ya kuondoka 1953 na kustaafu 1957. Liedholm alikuwa ndio kiungo mchezeshaji wa watatu hawa, aliendelea kucheza mpaka alipokuwa na miaka 38 akicheza mechi karibia 350 akifunga mabao 81. Liedholm alishinda  4 Scudettos ana aliiongoza kama nahodha Milan wakati wa mechi ya fainali ya UCL mwaka 1958 mbele ya  Real Madrid, moja ya kikosi bora cha muda wote. Inasemekana kwamba Liedholm alikuwa mpiga pasi mzuri sana na iliwachukua Milan miaka 2 kumpata mbadala wake. Wakati anacheza mechi yake ya mwisho pale San Siro washabiki walismama kwa dakika 5 wakimshangilia! Kutokea hapo Nils akaenda kuifundisha AC Milan na kufanikiwa kushinda taji la Scudetto baada ya miaka 10. 

Gunnar Nordahl alifunga mabao  210 kwenye michezo 257 na hivi karibuni ndo amkuja kupitwa na kushushwa mpaka nafasi ya tatu katika listi ya wafungaji bora wa muda wote wa Serie A nyuma ya Silvio Piola na Francesco Totti (ambao wote wawili wameshacheza mechi zaidi ya 500). Nordahl ndio mfungaji bora wa muda wote wa Milan, akishikilia rekodi ya kuwa mfungaji bora mara nyingi - mara 5 huku akiwa na uwiano mzuri wa  0.77 goals/match (225 in 291 total). Nordahl alishinda makombe 2 ya Serie A, 4 Italian Cups and 2 Coppa Latina akistaafu na jumala ya mabao 422 goals katika mechi 504. 
 Hivyo ni vipi Balotelli, Niang na El Shaarawy watapambana? Kiukweli itakuwa jambo gumu sana, ukizingatia uwezo wa kifedha wa Milan, bado wakiwa kwenye kuijenga upya timu lakini kama watatu hawa wataunda ushirikiano mzuri hata kufikia nusu ya ya ule wa akina Gre-No-Li mambo yatakuwa tofauti kwa Rossoneri. Tarehe 3rd February Mario alicheza mechi yake ya kwanza akiwa na Milan, huku Pazzini akijitoa kwenye mechi baada ya kuumia misuli wakati wakipasha hivyo akitoa nafasi kwa watatu hawa kucheza pamoja kwa mara ya kwanza. Stadio Meazza ilikuwa tofauti usiku huo kuanzia dakika ya kwanza ya mchezo watatu hawa wakicheza kwa kasi, nguvu na uelewano wa hali ya juu. 


Ndani ya sekunde 30 Balotelli akapata nafasi alkini akashindwa kuitumia vizuri, lakini hawakusubiri sana kwani dakika ya 24, kutokana na krosi safi ya El Shaarawy, Mario akafungua ukurasa wa mabao ndan ya jezi ya Milan. Baadae akaenda na kufunga bao la pili kwa mkwaju wa penati. Ushirikiano wa watatu hawa tangu wakati huo umezidi kukua na Niang nae amekuwa akimtengenezea Mario nafasi nyingi, mpaka sasa Balo ana mabao 7 kwenye mechi 6. Tarehe 21/3/13 Mario aliungana tena na wachezaji wenzie wa Italia kucheza dhidi ya Brazil na akafunga bao zuri, sasa hivi ana mabao 6 katika mechi 18 ndani ya uzi wa Azzurri, ni jambo zuri kuona namna gani anavyoijali Italy na ikiwa ataleta mapenzi haya kwenye timu yake ya utotoni then tutaona makubwa yakitokea. 
 Huku wachezaji wengine wazuri kama De Sciglio wakianza kuchipukia kuingia timu ya kwanza labda utatu wa Balo na wenzie nai mwanzo tu, nani anajua? Kitu kimoja cha uhakika watoto hawa wapya wa Rossoneri... wanaweza kufanya maajabu ya utatu wa Gre-No-LI.