Search This Blog

Saturday, March 2, 2013

TENGA: TFF HAITAKIWI KUINGILIWA - WAZIRI AMESHAURIWA VIBAYA



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesema ipo haja kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kufikiria upya uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya TFF ya mwaka 2012 na kutaka itumike ya mwaka 2006, kwani hautekelezeki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana, mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema ni muhimu jambo hilo likaangaliwa upya kwa sababu athari zake ni mbaya, na pengine Dk. Mukangara hakushauriwa vizuri kabla ya kufanya uamuzi huo.

“Kamati ya Utendaji ya TFF haitaki kubishana na Mheshimiwa Waziri hata kidogo, ila tunaamini wakati anatamka haya hakufahamu madhara yake, athari zake na ugumu wa utekelezaji wake. Kwa waliomshauri hili, wamemshauri vibaya,” amesema Rais Tenga.

Amesema rai ya TFF kwa Waziri ni kuwaita ili wamweleze ni kitu gani wafanye kunusuru mpira wa miguu wa Tanzania, kwani wanaamini jambo hili litakwisha baada ya kumwelimisha hasa kutokana na ukweli kuwa kabla ya kufanya uamuzi huo hakuwasikiliza.

Katika mkutano huo, Rais Tenga alianza kwa kusema kuwa TFF inaiheshimu sana Serikali, hivyo inaheshimu maagizo yaliyotolewa na Waziri, lakini akaongeza kuwa TFF ina wajibu wa kutoa ufafanuzi juu ya maagizo hayo.

Amesema lengo la kuelezea historia ya TFF ilikotoka ni kubaini migongano ya maagizo hayo na taratibu za TFF ambazo kwa bahati mbaya zinasigana na maagizo hayo.

Rais Tenga amesema TFF ni chombo cha wanachama, ambapo wanachama wake ni vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu, na ina taratibu za kufanya uamuzi kwa mujibu wa Katiba yake na za wanachama wake ambazo zimeidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema si TFF pekee, bali vyama vya nchi zote ambavyo vimeunganishwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), zinaheshimu na kufuata maagizo na miongozi ya shirikisho hilo la kimataifa la mpira wa miguu.

Rais Tenga amesema TFF haitakiwi kuingiliwa katika uongozi na uendeshaji wake, kwani jambo hilo likitokea rungu la FIFA litaiangukia TFF, na madhara yake ni makubwa. Miongozo ya FIFA inasisitiza uhuru wa wanachama wake katika uendeshaji shughuli za mpira wa miguu, na iko kwenye Katiba ya TFF.

“Sheria za nchi ndizo zilizozaa Katiba ya TFF. TFF ni chama kamili kinatakiwa kufanya uamuzi wake ili mradi uzingatie madhumuni ya kuanzishwa kwake. Leo TFF ikiacha mpira wa miguu na kuanza kujishughulisha na gofu, hapo Msajili ana haki ya kuingilia,” amesema Rais Tenga.

Kuhusu maagizo ya Waziri, Rais Tenga amesema kifungu cha 11 cha Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kinazungumzia usajili wa chama, na si marekebisho ya katiba, ingawa kanuni zinahusu marekebisho ambapo ameongeza kuwa uamuzi wa marekebisho ni wa Mkutano Mkuu na si Msajili.

“Ukienda kuomba viza, fomu unapewa na yule anayekupa viza. TFF tulipowasilisha marekebisho ya Katiba hatukupewa fomu. Msajili akasema sawa. Jambo la kujaza fomu si la TFF, ndiyo maana tunasema ipo haja ya jambo hili kufikiriwa upya.

“Usajili tayari umepita, kwamba Msajili hakutoa fomu, mwathirika anakuwaje TFF? Tunaona ni muhimu jambo hili likaangaliwa upya,” amesema Rais Tenga na kuongeza kuwa utaratibu wa kusajili Katiba ya 2006 ambayo ndiyo Waziri ameagiza itumike ulikuwa huo huo uliosajili Katiba ya 2012.

Akizungumzia historia ya TFF kutoka mikononi mwa BMT, Rais Tenga amesema ni zao za Katiba ya 2004 ambayo ilifanyiwa marekebisho ukumbini na kugongwa mhuri na Msajili hapo hapo na kuingia kwenye uchaguzi. Katiba hiyo ndiyo iliyoiondoa BMT kuisimamia TFF.

“Huko ndiko tulikotoka, si kwa kulazimishwa, bali kwa kupewa Katiba ya 2004. Katiba ina utaratibu mzima wa kufanya uamuzi. Maelekezo ya Waziri yamesahau huko tulikotoka siku nyingi. Uhalali wa marekebisho unatokana na ridhaa ya Mkutano Mkuu. Hiyo ni kwa mujibu wa Katiba yenyewe, hakuna nafasi ya BMT,” amesema.

Amesema katika maagizo ya Waziri, ameitaka TFF kufuata Katiba ya 2006 na kanuni za BMT, lakini Katiba hiyo hiyo ya 2006 haina nafasi ya BMT, na hata kama TFF ingetaka kutekeleza hilo haliwezekani.

“Kwa maagizo haya inaonekana Waziri kashauriwa vibaya. Tunajua hakuwepo katika nafasi hiyo (2004) wakati wa makubaliano kati ya Serikali na FIFA kuacha mpira wa miguu ujiendeshe wenyewe,” amesema Rais Tenga.

Pia amezungumzia umuhimu wa Katiba toleo la 2012, kwani kuna marekebisho mengi yalifanyika mwaka 2007, 2008, 2009 na 2011 ambapo ukiyafuta maana yake unakiweka pembeni Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Bodi ya Wadhamini, wanachama wapya (mikoa), Bodi ya Ligi, Kamati ya Rufani ya Uchaguzi, Leseni za Klabu na Kanuni za Fedha.

“Kwa uamuzi huu yote yaliyofanyika hayana maana. Waziri sidhani kama alikuwa anafahamu athari za maagizo yake. Kama angelijua asingefanya uamuzi huo. Si rahisi kurudi katika Katiba ya 2006. Hao wajumbe wa Katiba ya 2006 unawapata wapi? Maana yake hata vyama wanachama ni batili kwa vile vimerekebisha Katiba zao 2009 na 2010,” amesema Rais Tenga.

Amesema kwa Serikali kufuta, maana yake ni kutengua uamuzi wa TFF ambapo madhara yake ni nchi kufungiwa, ambapo timu za Taifa hazitacheza mpira, klabu hazitashiriki michuano ya kimataifa na wadhamini nao watakaa pembeni kwa vile hawawezi kudhamini timu ambazo hazishindani kimataifa.

“Dhana kwamba tukae tu tusicheze nje, ni dhana ya watu walio nje ya mpira wa miguu. Dhamira yetu ni kuhakikisha hatufungiwi. Waziri ametuagiza tupeleke barua FIFA kuwa ametengua marekebisho ya katiba. Hatupeleki hivyo, kwani hiyo ni Government interference, watatufungia.

“Nia yetu bado ni Waziri kutupa nafasi ya kutusikiliza,” amesema Rais Tenga na kuongeza kuwa kuhusu uchaguzi kwa vile FIFA wanakuja ombi la TFF kwa Waziri ni kuacha kwanza mchakato uendelee hadi ufike mwisho.

“FIFA wanakuja, tuwasubiri. Nilidhani utaratibu huo utaheshimika. Kama mtu wa mpira haitaki FIFA anataka nini? Ahadi yetu ni kuhakikisha watu wanapewa haki. Hiyo ndiyo ahadi yetu na tumeisimamia, na ndiyo maana FIFA wanakuja,” amesema.

Akijibu swali kuhusu waraka, Rais Tenga amesema marekebisho ya Katiba hayakufanywa kwa siri, ridhaa ya wajumbe wa Mkutano Mkuu kufanya marekebisho hayo kwa njia ya waraka ilipatikana ambapo 70 waliunga mkono na 33 walikataa.

KAMPUNI YA TANZANIA MWANDI YAANZISHA MICHUANO YA AFRICAN YOUTH FOOTBALL TOURNAMENT


Kampuni ya Tanzania Mwandi kwa kutambua kuwa Tanzania na Afrika nzima kuna vijana wengi ambao wana vipaji vya mpira wa miguu na hivyo wanachohitaji ni kuonyeshwa tu jinsi ya kuufikia ‘Ulimwengu Halisi’ wa Mpira duniani Tanzania Mwandi imeamua kuanzisha michuano ya African Youth Football Tournament ambayo itawashirikisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 21.

Michuano hiyo itaambatana na mafunzo kwa siku tano ambapo vijana hao watapata mafunzo ya mpira wa Miguu (elimu, ujuzi na hata mbinu za uwanjani) kutoka kwa makocha wawili wa hapa nchini na watatu wa kimataifa kutoka nje ya nchi, kuanzia tarehe 10/06/2013 hadi tarehe 14/06/2013 katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Aidha, mafunzo yatafanyika nyakati za asubuhi na jioni wachezaji hao watashiriki Mashindano ya kucheza wao kwa wao ili kupata vijana 11 bora miongoni mwa wachezaji watakaoshiriki.

Wachezaji Bora 11 watakaopatikana watakuwa mabalozi wa Mdhamini Mkuu wa Michuano ya African Youth Football Tournament na watapata fursa ya kutangazwa zaidi kimataifa na kutafutiwa vilabu vya kucheza soka Barani Ulaya katika nchi nane (Ufaransa, Ureno, Uswis, Ubelgiji, Uholanzi, Norway, Sweden na Denmark pamoja na barani Afrika na Asia.

Ili kupanua wigo wa kuwatangaza kimataifa wachezaji wengi zaidi, Michuano hii pia itaalika skauti na mawakala wa soka wa kimataifa ili kufuatilia uwezo wa wachezaji hao asubuhi katika mazoezi na jioni kwenye michuano, kuwapata vijana bora ambao watapendelea kuwatafutia timu nje ya nchi kukipiga huko kwa makubaliano ambayo pande hizo mbili (mchezaji na wakala) zitaafikiana.

Miongoni mwa Mawakala ambao watakuwepo ni wakala wa Kimataifa wa Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro, Phillip Mwakikosa (Sweden) na wengine wengi.

Hata hivyo kutokana na gharama kubwa za uandaaji wa Michuano hii, na ndio kwanza ikiwa inaanzishwa, Kampuni ya Tanzania Mwandi kwa kujali mahitaji ya Kitanzania tumeweka kiingilio kwa mchezaji wa Tanzania kuwa shilingi laki tatu (Tsh. 300, 000) na mchezaji wa nje ya Tanzania Dola 500 za Kimarekani (USD 500).

Fedha hizo zitagharamia malazi, chakula na mahitaji mengine yote kwa mchezaji pindi atakapokuwa kambini.
  
Hii ni fursa adimu kwa vijana wa Kitanzania kuonyesha uwezo wao ili kutimiza ndoto za kucheza soka barani Ulaya, Asia na barani Afrika katika vilabu vikubwa huku ikikumbukwa kuwa mnamo Mwaka 2012 ni wachezaji wachache sana wa Kitanzania waliopata fursa ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa kutokana na uchache wa mawakala na gharama hivyo kuletwa mawakala hao nyumbani Tanzania ni fursa pekee ya kufikia malengo.

Mpaka sasa tayari Kampuni ina majina takribani ya vijana 10 wa Nje ya nchi (Uganda, Nigeria na Ghana) ambao wameomba kushiriki hivyo tunatoa wito kwa Watanzania kutoipoteza fursa ya kuletewa njia ya kuelekea kusakata soka Barani Ulaya mlangoni mwao.

Lakini tunafahamu hali halisi ya maisha yetu kwahiyo nitoe wito kwa Wadhamini mbalimbali ambao tumewaomba kutusaidia kufanikisha Mashindano haya ambayo naamini yatalitangaza taifa letu na kulitangaza zaidi soka letu kimataifa. Pia udhamini wao utatuwezesha kupunguza hizi gharama kwa washiriki kutoka Tanzania na hivyo kuwachukua vijana wengi zaidi.

Kampuni ya Tanzania Mwandi ni Kampuni binafsi ambayo imejikita katika kuendeleza sekta za utalii, michezo na burudani ndani na nje ya nchi na hivyo kuiongezea kipato nchi moja kwa moja ama kupitia kuwawezesha wananchi kama vile kuwatengenezea fursa za ajira vijana kupitia michezo.

Fomu za ushiriki Michuano hii zinapatikana kupitia www.tanzaniamwandi.co.tz na www.blog.tanzaniamwandi.co.tz

“African Youth Football Tournament; Live your Dream.”

PHOTO OF THE DAY: SIMBA NDANI YA ANGOLA TAYARI KUPAMBANA NA LIBOLO

Baadhi ya wachezaji wa Simba wakiwa wamepozi nje ya Hotel Ritz na mchambuzi wa soka Edo Kumwembe huko Angola tayari kwa kupambana na Libolo siku ya kesho katika mechi ya pili ya Mabingwa wa Afrika.

WEST BROM VS CHELSEA: BENITEZ KUTIMULIWA LEO - AU ATAISHINDA HISTORIA?

Kocha wa Chelsea Rafa Benitez anapigana historia leo hii na anaweza kuishinda ikiwa atapata matokeo chanya dhidi ya timu yenye mkosi na makocha wa Chelsea - West Bromwich Albion.
 
West Brom, ambao wanaenda Stamford Bridge leo jumamosi, wamekuwa moja ya vyanzo vikuu vya kuondolewa kwenye benchi la ufundi la Chelsea kwa makocha wawili waliopita wa klabu hiyo. Mwaka mmoja uliopita goli la Gareth McAuley liliipa ushindi West Brom, na kumfukuzisha kazi Andre Villas Boas.

Miezi nane baadae, ushindi wa 2-1 kwenye uwanja wa Stamford Bridge dhidi ya Chelsea ukamaliza siku za kufundisha Chelsea kwa Robert Di Matteo.

Je leo Benitez atavunja mwiko na kuishinda historia dhidi ya West Brom? 

KOMBE LA DUNIA 2014: WATU WANENE WATENGENEZEWA SITI ZAO MAALUM

 

Wakati Brazil wakiwa bado wanapambana kukamilisha ujenzi wa viwanja vya soka kwa ajili ya kutumika kwenye 2014 World Cup na kombe la mabara, imegundulika kwamba zimetengenezwa siti maalum kwa ajili ya watu wanene(vibonge). 

Ripoti iliyotolewa na The Sun inasema kwamba siti hizo kwa ajili ya watu vingonge ni pana mara mbili kuliko zile za kawaida na zinaweza kuhimili uzito wa mtu 560 lbs. 

Hatua hii imekuja kutokana na uzoefu uliopatikana kwenye michuano kadhaa mikubwa iliyopita juu ya shida waliyokuwa wamepata watu maumbo makubwa.

FC KILIMANJARO YA SWEDEN YAOMBA MSAADA WA UDHAMINI



AZAM FC WATUA NA VYAKULA VYAO JUBA SUDAN

AZAM FC imenunua chakula chake binafsi kwa hofu ya hujuma wakati ikitarajiwa kuwasili leo Jumamosi kujiandaa na mechi dhidi ya Al Nasri kesho Jumapili.

Uongozi umenunua mchele mjini Nairobi, Kenya wakati mchele mwingine unatarajiwa kuletwa leo Jumamosi mjini Juba na viongozi wengine wa Azam.

Hata hivyo jumla ya kilo 30 za mchele zilinunuliwa Juba kwa ajili ya chakula cha wachezaji. Kwa mujibu wa Watanzania wanaoishi mjini Juba walisema, tatizo la kuwekeana sumu katika chakula mjini Juba ni suala la kawaida hivyo inabidi kuwa makini muda wote.

 Watu wa hapa Juba bado wana tatizo la kumalizana kwa kuwekeana sumu katika chakula, hata sisi wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa hatupikiwi chakula cha pamoja, sisi hununua chakula chetu na kila mtu hujipikia, alisema Kassim Matokeo ambaye ni Mtanzania anayefanya kazi katika ofisi za Umoja wa Mataifa hapa Sudan ya Kusini.

Tayari viongozi wa Azam waliotangulia kwa ajili ya kuandaa mazingira hapa Juba wameshaandaa utaratibu kwa ajili ya kupika wenyewe chakula hicho cha wachezaji ili kuepuka kuhujumiwa.

Azam itakabiliana na Al Nasri katika mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika. Katika mechi ya kwanza Azam ilishinda 3-1 Dar es Salaam.

Msafara wa Azam utakaokuwa na viongozi na wachezaji 20 utawasili saa 8:20 mchana ikitokea Dar es Salaam kupitia Nairobi.

Hali ya hewa hapa Jua ni jua na joto kali linalofikia nyuzi 40 ingawa wenyeji wanadai huongezeka zaidi ya hapo. Mji wa Juba unatumia umeme wa majenereta.

Uongozi wa Azam umeikataa Hoteli ya South Sudan ambayo ilikuwa imeandaliwa na wenyeji wao.

Mratibu wa Azam, Florian Kaijage akiwa na kocha msaidizi wa Azam, Kally Ongala waliikataa hoteli hiyo na kuchukua Hoteli ya Rainbow.

Gharama za hoteli hapa Juba zipo juu kwani hoteli zipo chache. Chumba kinaanzia dola 100(sh.160,000) kwenda juu.


SOURCE: GAZETI LA MWANASPOTI

HATIMAYE DORTMUND WATHIBITISHA LEWANDOSKI ATAONDOKA KWENYE TIMU YAO

Robert Lewandowski ataondoka Borussia Dortmund katika kipindi cha miezi 18 ijayo baada ya kukataa mkataba mpya, kwa mujibu wa mkurugenzi wa michezo wa Dortmund Michael Zorc.

Lewandowski, ambaye amekuwa akihusishwa sans na kujiunga na na Bayern Munich na Manchester United, yupo kwenye mkataba na mabingwa wa Bundesliga mpaka mwaka 2014 lakini Zorc  ameiambia SKY TV ya Ujerumani kwamba mchezaji huyo hatosaini mkataba mpya.

Wakala wa mchezaji huyo amemtaarifu Zorc kwamba mteja wake hana mpango wa kuendelea kubaki Dortmund, akimaanisha kwamba mpoland huyo ataondoka kwenye klabu hiyo.

"Anaweza kuondoka mwishoni maw msimu au akabaki kwa mwaka mwingine," alisema Zorc.

Huko nyuma, gazeti la mini Munchner Merkur liliripoti kwamba dili limeshakamilika kati ya Lewandoski na Bayern, na angetangazwa kujiunga na Bayern kwenye mechi ya jana usiku kati ya Dortmund na Bayern. Japokuwa hakukuwa na tangazo lolote kuhusu usajili na huku Bayern wakikanusha kupitia mkurugenzi wao wa michezo Mathias Sammer kwamba hawatozungumzia tena suala la tetesi zisizo za ukweli za usajili wa Lewandoski.


Friday, March 1, 2013

JERRY SANTO NJE WIKI SITA - AUMIA MGUU AFUNGWA BANDAJI NGUMU

Mchezaji tegemeo wa Coastal Union ya Tanga Jerry Santo akiwa nauguza majeraha ya mguu aliyoyapata hivi karibuni ambayo yatamuweka nje ya uwanja kwa wiki sita kama ilivyoripotiwa na klabu yake.

RAGE AMESOMA NA KUELEWA KITABU CHA KROENKE NA HILLWOO





Miaka 12 iliyopita nilikua na umri wa takribani miaka 8, Katika umri huo nilikua na akili ya utambuzi wa mema na mabaya. Darasa langu la tatu lilitosha kujua nini Wazazi wanapenda nifanye na nini hawataki kusikia nafanya. Japo ilikua ngumu kutimiza matakwa yote ya wazazi ila nilijaribu kuwaridhisha. Kati ya mambo ambayo wazazi wangu walichukia ni mchezo wa mpira wa miguu,hapo ndo kulikua na kazi,nilipopenda sana wao ndipo walipochukia sana. Nikakubali kuitwa mtoto msumbufu,mjeuri,mkaidi na majina mengine mengi mabaya kwa ajili ya huu mchezo. Wazazi hawakuishia hapo kila waliposikia nimeenda kucheza mpira jioni yake sebule hujaa fimbo nyingi, ungefikiri sungusungu wanafanya maandalizi kwa ajili ya kwenda kukamata na kupiga waarifu usiku huo, La hasha fimbo zote zilikua zinasubiri mwili wangu mdogo mfano wa fidodido. Nakumbuka nilikua Napata kipigo mithili ya mbwa mwizi. Lakini fimbo hizo hazikunizuia kesho yake kuibuka kwenye kiwanja changu cha koloni kilichopo mpakani mwa Vingunguti na Tabata na kuendelea kula ladha za sembo, nyuzi banana au kipere pasi na kukumbuka kipigo cha jana nillichopewa na bi mkubwa. Kabumbu litasakatwa mpaka mishale ya saa 12 na nusu jioni. Kila mmoja na njia yake kuelekea nyumbani kwake, hapo ndipo mafua ya ghafla yanaponianza sambamba na moyo kudunda mara 180 kwa dakika, huku nikihisi kibofu cha mkojo kinataka kupasuka. Hiyo ilikua ni hofu ya bakora kutoka kwa mama au baba. Nisipowakuta wazee nyumbani hua nafanya kazi nyingi za nyumbani hata zile zisizonihusu ili nifunike kombe mwanaharamu apite. Lakini sikuweza kuwashawishi mahakimu wangu kuwa huru na adhabu ya bakora. Ikafika kipindi ikawa ratiba niliyoizoea, asubuhi naenda shule nikitoka shule naelekea viwanja vya soka nikirudi nyumbani nachezea fimbo kabla ya kwenda kulala.

Nikaendelea kukua kiumri pia kiakili, siku moja nikamuweka mama kitako na kumuuliza “Mama kwanini hutaki na hupendi nicheze mpira?” Mama akanijibu “nakupenda sana mwanangu, sitaki uharibikiwe kama watoto wengine (huku akitoa mifano ya watoto hao kwa majina), wamepoteza muda wao mwingi kwenye michezo, shule imewashinda ona walivyo sasa hawana mbele wala nyuma(mama aliendelea)” Akaniuliza na wewe unataka kuja kua kama wao? Nikajibu kwa haraka “hapana mama” “basi mwanangu soma sana ili uje kua daktari, engeneer, au mwalimu achana na habari za mpira hakuna mtu aliyefanikiwa kwa mpira mpira wa miguu”. Maneno ya mama yaliniingia na kugusa moyo wangu, hasa pale nilipogeuza shingo yangu na kuangalia maisha ya wachezaji soka mashuhuri mtaani kwangu, niliangalia maisha ya Athumani Machepe aliyekua akiichezea Simba, sikuona tofauti yake na kijana asiye na ajira kwa kipindi hicho. Si machepe peke yake bali kuna wachezaji wengi wa miaka ya nyuma walipata kuwa maarufu sana huku mifuko yao ya suruali ikiwa imetoboka. Hao ndo wasakata kabumbu wa zamani, walikua na uzalendo na mapenzi thabiti na soka.

Achana na Habari za mwanzoni mwa karne ya21, siku hizi kuna MAONO MAPYA YA DUNIA. Ndani ya maono hayo kuna bosi na kiongozi mmoja tu. Bosi huyo ana majina mengi kwa kila nchi na kwa kila kabila,wengine watamuita maela, faranga,kwacha, yen, dollar, shilingi na kwa majina ya jumla anaitwa money au Pesa. Majina ya bosi huyu ni mengi lakini yana maana, lengo na kazi zinazofanana. Miaka ya nyuma ili uheshimike kwenye jamii ilikua lazima uwe na elimu, hapo utashinda dhidi ya umma. Lakini Maono mapya ya Dunia Hayatambui Elimu juu ya heshima, Maono mapya ya Dunia yanaamini Mtu mwenye busara, Hekima na kustahili kuheshimiwa ni yule mwenye pesa. 


Uingeneer, Udaktari, ualimu wako bila shekeli hakuna atakayetambua, kuthamini wala kuheshimu taaluma yako. Kwenye Dunia yetu mpya kila kitu pesa. Kinachonifurahisha zaidi hata kwenye ulimwengu wetu wa soka pesa ndiyo inacheza mpira, Wazungu wanasema “Money plays Football” Siku hizi Wazazi Wanaupenda na kuheshimu mchezo huu sababu ya pesa. Ni wazazi wachache sana wanawazuia watoto wao kucheza soka. Mbwana Samatta, Mrisho Ngassa na Juma kaseja wamefanya wazazi kuwahamasisha watoto wao kucheza mpira, miaka hii ya mpira pesa ukiomba hela kwa ajili ya njumu itawahi kuliko pesa ya daftari na peni, Sammata na gari lake anatafuta wapi pesa zake atawekeza huku injinia mwenye degree yake kila siku kwenye daladala na vyeti akitafuta ajira. Hiyo ndo Heshima ya soka bwana.

Katika miaka ya karibu tumeona mabilionea kama Moize Katumbi chapwe kutoka kongo, Patrice Thopane Motsepe wa South Afika, Said Salim Bakhresa wa Tanzania na wengine wengi wamewekeza zaidi kwenye soka na kufanya soka letu Afrika liwe la ushindani. Leo hii Teko Modise anaheshimika kuliko viongozi na watu wengi maaarufu wa mjini kwao SOWETO, Tresor Mabi Mputu ndiye mfalme wa KINSHASA, John Boko amekua maarufu kuliko vibopa wa Sinza na Kijitonyama, hiyo ndo heshima ya pesa za Motsepe, Bakhresa na Katumbi.

Lakini kwenye Ulimwengu huu huu wa mpira pesa kuna watu wajanja wajanja, wenye pesa kiasi wanaojua kuwatumia wachezaji kuchota pesa za kina Motsepe, Bakhresa na Katumbi.Wengi wao huwa wenyeviti au viongozi wa ngazi za juu kwenye timu husika. Kule Uingereza utamkuta mwenyekiti wa Arsenal, Bwana Peter Hillwood hakuna Arsenal bila Hillwood, babu yake mzee Samwel Hillwood alikuwa mwenyekiti wa Arsernal mnamo mwaka 1926-1936 na 1946-1949, pia baba yake mzee Dennis Hillwood alipata kuwa mwenyekiti wa Arsenal mnamo mwaka 1962-1982 kabla ya kufariki na mtoto wake Peter Hillwood kushika hatamu mpaka hivi leo. Peter Hillwood, Ivan Gazids na Mjasiliamali wa kimarekani Stan Kroenke hawa ndo wanaounda CC(central comitee) ya Arsenal. Watu hawa wamejaa siasa na roho ya ujasiliamali zaidi, akili yao yote ipo kwenye kutengeneza pesa kuliko kuimarisha na kujenga timu ya upinzani. Mungu awape nini watu hawa? Wamepata na kocha Mchumi anayejua kucheza na akili ya mashabiki. Profesa Wenger miaka 8 bila kombe ameingiza zaidi ya paund 50 million kama mshahara, Huku akina Piers Morgan na washabiki wenzake wa Arsenal wakiumia juu ya mwenendo wa timu wa kutoka kapa kila msimu, sambamba na kuuza wachezaji nguli bila kutafuta mbadala sahihi, CC ya Arsenal na Wenger wao hutazama kwenye zizi na kutafuta kondoo aliyenona kwa ajili ya kuuza na mwisho wa mwaka kugawana marupurupu kutokana na faida ya kondoo huyo. Hawa kwa kiasi wameifanya Man City iitwe Man city,wamejua jinsi ya kufyonza pesa za Sheikh Mansor, huku wakiumiza mioyo ya mashabiki wa arsenal

Hapa kwetu Bongo yupo fundi aliyepata mafunzo kama ya CC ya Arsenal japo kwenye vyuo tofauti. Si mwingine yeye anaitwa Mh. Aden Rage, mtu huyu amejaaliwa fitina ya soka, siasa pamoja na ujasiriamali. Mashabiki wa msimbazi nikiwauliza mbadala wa Samatta ni nani hawatanipa jibu, ila Rage kawapa kibuli cha kujisifu kwa kumuuza Samatta kwa mamilioni ya pesa. Hayo mamilioni ya Samatta yameenda wapi? au yameifanyia nini Simba hilo ndo swali la kujiuliza kama mshabiki wa Simba,vipi kuhusu  Okwi? Kama mmeshindwa kuhoji pesa zilipoenda hojini hata mbadala wa wachezaji hao. Simba ya sasa ina baadhi wachezaji wa kawaida na wasio na hadhi ya kuchezea Simba si kwenye mashindano ya kimataifa pekee bali hata ligi ya ndani. Sina uhakika kama Rage alikua anamtaka Yondani au pesa za usajili za Yondani? Si vibaya Simba kuuza wachezaji nje ya nchi, ni vizuri sana hasa kwa maendeleo ya soka letu kwa ujumla, tatizo lipo kwenye mbadala wa wachezajiwaliouzwa. Leo hii Haruna Chanogo, Singano na Chris Edward wanapewa majukumu makubwa kuzidi umri wao.

Si lazima uwe mshabiki maarufu wa Simba kama Mzee Magoma moto au Mshabiki Nguli wa Arsenal kama Piers Morgan ili uwe na machungu juu ya kupotea kwa ladha kutoka kwenye timu hizi zinazoongozwa na wajasiliamali waliojaa siasa za soka

By kaijage jr

middle ya juu

MCHEZAJI WA GHANA JOHN PAINTSIL HURU: KESI YA KUMJERUHI MKEWE NA KISU JICHONI YAFUTWA


Mke na jirani wa mchezaji wa kimataifa wa Ghana John Paintsil wote kwa pamoja wameamua kutoendelea na kesi walizofungua dhidi ya mchezaji huyo, polisi nchini Ghana imesema.

Afisa upelelezi Freeman Tetteh alisema Paintsil alituhumiwa kumsababishia majeraha mkewe, Richlove, na pia alimjeruhi jirani yake mmoja huko jijini Accra siku ya ijumaa iliyopita. Lakini afisa hugo wa polisi alikataa kuzungumzia chochote kuhusu ripoti kwamba Paintsil alimtoboa jichoni mkewe na kisu.

Hata hivyo mashtaka note dhidi ya mchezaji hyo yameondolewa dhidi ya mchezaji hugo wa zamani wa  West Ham na Fulham, Tetteh alisema, ingawa polisi imechukua maelezo kutoka mke wa Paintsil na jirani, ambaye ndiye aliyetoa taarifa polisi. Tetteh alisema kwamba 'hakuna anayekataa kwamba kulikuwa na vurugu ndani ya nyumba ya mchezaji huyo. Msemaji hugo wa polisi alikataa kuendelea kutoa taarifa nyingine zozote kuhusu kesi hiyo.



BAADA YA KUTUKANWA SANA - HATIMAYE BENITEZ ABWATUKA ASEMA ATAONDOKA CHELSEA MWISHONI MWA MSIMU


Rafael Benitez, amesema kuwa atakihama klabu ya Chelsea mwezi Mei mwaka huu na kutaja uamuzi wa kuumpa wadhifa wa kaimu kocha wa klabu hiyo kama kosa kubwa.

Akiongea baada ya kuongoza Chelsea kushinda klabu ya Middlesbrough kwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya raundi ya tan ya kuwania kombe la FA, kocha huyo kutoka Uhispania, vile vile aliwashutu mashabiki wa klabu hiyo.

Katika mahojiano na BBC, Benitez amesema uamuzi wa Chelsea wa kuumpa cheo cha kaimu kocha wa klabu hiyo ilikuwa kosa kwa sababu yeye ndiye kocha mkuu kwa sasa.

Amesema mashabiki wao hawajawapa msaada wanaohitaji na hivyo ameamua kuondoka mwisho wa msimu huu.

'' Mashabiki sasa hawana sababu ya kunung'unika kunihusu'' Alisema kocha huyo.


Hatua hiyo ya kocha huyo wa zamani wa Liverpool imekuja baada ya baadhi ya mashabiki wa klabu huyo kumdhihaki baada ya mechi yao na Middlesborough.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 52, hajapata uungwaji mkono kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo tangu alipoteuliwa kuchukua mahala pa Roberto Di Matteo mwezi Novemba mwaka uliopita.

Katika mechi nyingi zilizopita za Chelsea, mashabiki wa klabu hiyo hawakuficha hisia zao za kutaka kocha huyo kufutwa kazi.

TATHIMINI YA LIGI KUU: VINARA WA MABAO, NGOME DHAIFU, WALIONG'ARA NA KUBORONGA



Ligi Kuu Tanzania Bara ipo mbioni kumalizika. Timu zote 14 zikiwa zimebakisha takribani michezo saba hadi minane kuhitimisha msimu wa 2012/13.
Kila mtu alitabiri mambo yake aliyoyajua mwenyewe na kutoa sababu zake binafsi kwa mtazamo wake kulingana na alivyoziona timu hizo zikishiriki ligi hiyo.
Lakini sasa huenda ukawa wakati muafaka kuangalia mwelekeo wa vikosi hivyo. Tayari timu zinazoweza kupata ubingwa mwishoni mwa msimu huu zimeanza kujiengua taratibu.
Ni wengi ambao wanaweza kuishangaa Yanga kushika usukani wa ligi.
Pia, huenda ni watu wachache sana wanaoweza kushtuka kikosi hicho kikitwaa ubingwa msimu huu.
Awali, Simba ilionyesha kiwango na kukalia kiti cha uongozi wa ligi kwa muda mrefu, sasa ipo nafasi ya tatu, nyuma kwa pointi 11 na vinara Yanga yenye pointi 42 kibindoni.

Mbio za ubingwa
MBIO za kusaka taji la ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2012/13 zimeanza kuonekana wazi wakati pointi sita zikiwatofautisha Yanga na Azam FC ambazo zina nafasi pana ya kubeba taji hilo msimu huu.
Azam imetulia nafasi ya pili na pointi zake 36 na kuweka 'gap' la pointi sita na vinara Yanga yenye pointi 42 kibindoni.
Bingwa mtetezi, Simba imeketi nafasi ya tatu na pointi zake 31, tofauti ya pointi 11 na mtani, Yanga. Hiyo inaonyesha kuwa wateule wameanza kujitenga taratibu.

Vibonde wajulikana
KAMA ambavyo huwezi kushtuka Yanga ikichukua ubingwa. Pia, huwezi kushangaa kuona Polisi Moro, Toto African na
African Lyon zikishuka daraja.
Kuna 'gap' la tofauti ya pointi kama 29 kati ya vinara Yanga na timu ya African Lyon inayoburuza mkia. Lyon ina pointi 13 wakati Yanga inayoongoza ligi ina pointi 42.
Pia, Toto inayoshika nafasi ya pili kutoka mkiani ina pointi 14.
Klabu hizo tatu zinatakiwa kupigana kufa na kupona kuhakikisha zinashinda mechi zote zilizobaki kujinasua kwenye eneo hilo hatari. La! sivyo zitakwenda na maji.
Hata hivyo, timu tatu zinazomilikiwa na majeshi, JKT Ruvu, Tanzania Prisons na JKT Oljoro zinatakiwa kujiweka sawa kulingana nafasi zilizopo.

Timu zilizotisha kuna timu ambazo zimekuwa tishio la
vigogo msimu huu. Mtibwa Sugar na Kagera Sugar zimeweza kuzifunga Yanga na Simba kwa wakati tofauti.
Kwa hali inavyoonyesha zinaweza kufanya vizuri katika mechi zilizobaki na kushika nafasi tatu za juu.
Pia, Coastal Union imeonyesha kuja kivingine na kuwa kizingiti kikubwa kwa vigogo hasa ikiwa kwenye viwanja wake wa nyumbani Mkwakwani, Tanga.
Nayo Ruvu Shooting inatakiwa kupigiwa 'saluti' kwa kiwango ilichokionyesha kwa mzunguko wa pili wa ligi.
Ndiyo maana ipo nafasi ya saba na pointi 26 huku ikiwa imesaliwa na mechi tisa mkononi.

Ufungaji bora
NYOTA wawili, Kipre Tchetche wa Azam FC na Didier Kavumbagu wa Yanga wanawania ufungaji bora.
'Mapro' hao wanatofautiana kwa bao moja tu la kufunga.
Tchetche raia wa Ivory Coast amefunga mabao 10 wakati Mrundi Kavumbagu amepachika tisa na kuzifanya timu hizo  kushika nafasi mbili za juu kwenye msimamo wa ligi.
Ingawa washambuliaji, Jerry Tegete wa Yanga, Paulo Nonga wa Oljoro JKT na kiungo Amri Kiemba wa Simba wana kila  sababu kuendelea kufunga hata kuwapiku endapo watalewa sifa na kushindwa kuendeleza kasi yao kuzitikisa nyavu za  timu pinzani.
Kuna kila hali mfungaji bora msimu huu akamaliza akiwa na mabao 20 na kuvunja rekodi ya straika John Bocco wa Azam FC aliyepachika mabao 19 msimu uliopita.


Timu vinara ufungaji
YANGA inaongoza kwa kila kitu. Ikiwa kwa pointi na pia mabao yakufunga.
Shukrani ziwafikie Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na mabeki Mbuyu Twite na Nadir Haroub 'Cannavaro'
Yanga imejikusanyia mabao 35 yakufunga ikiwa ni wastani wa mabao mawili katika kila mechi. Pia, ni timu ambayo imefungwa mabao machache. Imeruhusu mabao 12 tu  kugusa nyavu zake katika mechi 18.

Lakini African Lyon ndiyo timu iliyoonyesha udhaifu kwenye ngome yake. Lyon imefungwa mabao 31 katika mechi 19
iliyocheza kwenye ligi.

Mabao yakufungwa
TIMU mbili, African Lyon na JKT Ruvu ndizo zimeonyesha udhaifu kwenye safu ya ulinzi.
JKT Ruvu imeruhusu kufungwa mabao 27 katika mechi 18 iliyocheza. Ingawa ipo nafasi ya nne kutoka mkiani mwa msimamo wa ligi hiyo.
Lyon ipo nafasi ya 13, imefungwa mabao 31 huku yenyewe ikizamisha 13 tu katika mechi 19.

Hat trick
HAKUNA mchezaji aliyebahatika kufunga mabao matatu mchezoni, kwa lugha ya kimichezo 'hat trick'.
Mshambuliaji Juma Semsue wa Polisi Dodoma ndiye aliyefunga hat trick msimu uliopita.
Lakini mpaka ligi inaelekea kufika tamati msimu huu hakuna mchezaji aliyeweza kuvunja rekodi hiyo.
Askari huyo alifunga mabao hayo kwenye pambano dhidi ya Moro United mwaka jana wakati timu hizo zikishiriki Ligi Kuu
kabla yakwenda na maji.
Mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi, ulimalizika kwa Polisi Dodoma kuibuka na ushindi wa mabao 5-2.

Walioboronga
TIMU tatu za Polisi Moro, Toto African na African Lyon ni timu ambazo zimeshinda michezo mitatu tangu kuanza
kwa ligi.
Polisi inayonolewa na kocha mpya Adolf Rishard ilimaliza mzunguko wa kwanza pasipo kupata ushindi wowote wakati huo ikinolewa na kocha John Simkoko aliyetupiwa virago.  

Thursday, February 28, 2013

SAKATA LA KATIBA YA TFF: MWAKALEBELA ASHINDILIA MSUMARI WA MOTO, ASEMA SERIKALI IPO SAHIHI KUIFUTA KATIBA YA SASA


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF FREDERICK MWAKALEBELA amezidi kuushindilia msumari wa motomchakato wa uchaguzi Mkuu wa TFF ambao umesitishwa na serikali na kudai kwamba haukufuata taratibu husika kama katiba ya chama hicho inavyotaka.

MWAKALEBELA ambaye amewahi kukiongoza kwa mafanikio chama hicho amesema, kufuatia kukiukwa kwa taratibu husika wakati wa upitishwaji na usajili wa marekebisho yaliyofanywa na TFF kwa njia ya waraka hivi karibuni ndio maana Serikali imeingilia kati na kutaka katiba ya mwaka 2006 itumike ili kutenda haki kwa wagombea wote.

Kwa maana hiyo MWAKALEBELA anapingana na taarifa zilizotolewa na Katibu Mkuu wa TFF ANGETILE OSIAH na baadhi yak viongozi wa Shirikisho hilo kwa kwa kuusimamisha uchaguzi huo Serikali inaingia maamuzi ya TFF jambo ambalo linapingwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA.

Akizungumza na Sports Extra ya CLODS FM MWAKALEBELA ameelezea kuwa Serikali haijaingilia maamuzi yak TFF katika mchakato wa uchaguzi na ilichofanya kuangalia sheria na kanuni za serikali ambazo zilikiukwa jambo ambalo lilikuwa likiiindolea TFF sifa za kuendesha shughuli zake nchini.

“Unaposema kuingia ni pale ambapo TFF imetoa maamuzi yake kwa mfano Mtibwa Sugar imepewa point baada ya kukata rufaa dhidi ya Yanga, hapa ikiwa Serikali itaingia na kutaka ushindi huo ubaki kwa Yanga itakuwa imeingia maamuzi ya chama cha soka na hilo ndilo jambo linakatazwa,” alisema MWAKALEBELA.

Mbali na hayo amesema kama chama cha mpira wa soka katika nchi yoyote ile hakijasajiliwa kwa kufuata sheria za nchi husika FIFA haiwezi kutoa kibali kwa chama hicho kushiriki na kuendesha mashindani yoyote jambo ambalo hapa nchini linafanywa na Baraza la Michezo la Taifa BMT na Msajili ya Michezo nchini.

Akizungumzia juu ya utaratibu uliotumiwa na Msajili wa Michezo nchini kupitisha waraka bila kufuatwa kwa taratibu MWAKALEBELA amesema, tayari Serikali imeyaona mapungufu hayo na kuchukua hatua stahiki huku akiikingia kifua TFF kwamba iliamua kuendesha uchaguzi baada ya msajili kuusajili waraka wao.

Kwa upande wake Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF kutoka Mkoa wa Dodoma MULAMU NGHAMBI amesema mgogoro wote ulioikumba mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF umetokana na Shirikisho hilo kukiuka katiba yake iliyojiwekea.

Akifafanua amesema licha ya baadhi ya Wajumbe kutoka mikoa mbalimbali kupinga utaratibu wa kupitisha katiba ya shirikisho hilo kwa njia ya waraka, TFF haikuchukua hatua hali ambayo imepelekea kuzuka kwa mgogoro huo.

MULAMU amesema katiba ya TFF inaeleza kinagaubaga kila jambo namna linavyotakiwa kuendeshwa ikiwemo jinsi ya kufanya marekebisho ya katiba lakini kilichofanyika hivi karibuni ni wazi TFF ilikiuka katiba yake mwenyewe.

Akifafanua Mjumbe huyo amewataka wadau wa Soka nchini kuachana na upotoshaji unaoendelea kwamba Serikali imeyakataa mabadiliko yote ya Katiba yaliyofanywa tangu mwaka 2006 na kwamba kilichofanyika ni kupingwa kwa mabadiliko ya sheria yaliyopitishwa mwaka 2012 kwa njia ya waraka.

Kufuatia hatua hiyo MULAMU ameiomba TFF na wadau wengine wa soka kufuata taratibu za soka walizojiwekea na kupitishwa kwenye Katiba ya TFF inayokubalika na Serikali ili hatimaye shirikisho hilo liweze kupata viongozi bora watakaoinua kiwango cha soka nchini.

MILOVAN AONDOKA BONGO - RAGE AKIMWAGIA LAWAMA KUHUSU USAJILI - CIRKOVIC AJIBU MAPIGO


ALIYEKUWA kocha wa Simba Milovan Cirkovic ameondoka nchini jana alfajili na shirika la ndege ya Uturuki baada ya kufanikiwa kulipwa fedha zake dola 32 alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kocha huyo ambaye alikuja nchini mapema mwezi huu kwa ajili ya kudai fedha zake baada ya kudanganywa na uongozi wa Simba kuwa wanamtamlipa fedha zake bila mafanikio yoyote ndipo aliamua kuja kudai mwenyewe.

Hata hivyo baada ya kusota muda mrefu huku viongozi wakiwa wanampa ahadi kila siku hatimaye jana alfajiri alifanikiwa kuondoka baada ya kulipwa deni lake la Dola 32 kutoka kwa Malkia wa nyuki Rahma Al Kharoos ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na mfadhili wa klabu hiyo.

Kocha huyo ameondoka na rekodi ya ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0 dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
 

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema kuwa uongozi wake haupaswi kulaumiwa kwa kusajili wachezaji wasio kuwa na uwezo bali anayetakiwa kulaumiwa ni aliyekuwa kocha wao Mserbia Milovan Cirkovic.

Rage alisema kuwa wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni pendekezo la kocha huyo ambaye alitimuliwa raundi ya kwanza baada ya timu kutofanya vizuri katika michezo yake ya mwisho.

Alisema awali waliwaleta wachezaji wawili kutoka Cameroon lakini kocha aliwakataa na kuwasajili wachezaji wake ambao aliwataka yeye.

Aliongeza kuwa haoni sababu ya wao kulaumiwa kwa sababu wao ni uongozi na sio wachezaji na kuongeza kuwa kama watu wanawalaumu wao wanacheza namba ngapi uwanjani.

Rage akiwa anatoa kauli hiyo tayari kocha Milovan kwa upande wake alikwisha sema kuwa katika wachezaji ambao alitaka wasajiliwe aliyesajiliwa ni Mrisho Ngassa pekee na wengine uongozi ulishindwa.

Msimu huu simba iliweza kusajili beki Lino Musombo, Kanu Mbiyavanga (Congo), Patrick Ochierg (Kenya) na Komabil Keita (Mali).

Lakini baadaye waliwaacha wachezaji watatu na kumbakiza mmoja Keita kwa madai ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri katika timu yao.

SKENDO BARCELONA: YATUHUMIWA KUPEPELEZA MAISHA BINAFSI YA WACHEZAJI WAKE - KUANZIA AKINA DINHO, ETO'O, DECO NA SASA PIQUE NA SHAKIRA


Parents imminently: Shakira and boyfriend Gerard Pique have teamed up with charity UNICEF to create a virtual baby shower in the lead up to the birth Klabu ya FC Barcelona imetuhumiwa na suala la kumpeleleza mchezaji Gerard Pique na maisha yake binafsi kwa sababu wana wasiwasi juu uhusiano wa beki huyo na mwanamuziki wa kikolombia Shakira. 

Mfanyakazi wa zamani wa kampuni ya upelelezi Metodo 3, amekaririwa akisema kwamba walikuwa wakimfuatilia mlinzi huyo wa kihispania ikiwa ni amri iliyotolewa na uongozi wa Barca ambao walikuwa wakihisi kwamba uhusiano wa Pique na Shakira unaharibu uwezo wa kucheza vizuri wa beki dimbani.

Taarifa zisizo rasmi ni kwamba Metodo 3 -  It is rumoured that Metodo 3 - ambayo kwa sasa imefungwa - pia ilifanya kazi ya kuwapeleleza mastaa wengine wa Barca kama vile Samuel Eto'o, Ronaldinho, na Deco huko nyuma. 

Taarifa hizi ambazo zimekuwa ni siri zinazofichwa na Metodo 3 zimekuwa zikisambaa kutoka kwa wafanyakazi wa zamani wa kampuni hiyo baada ya kampuni hiyo ya upelelezi kufunga shughuli zao. Gazeti la  El Confidencial limeripoti kwamba Barcelona iliwatuma wapelelezi kumfuatilia Pique mwaka 2010 kuangalia ni muda gani anaotumia kufanya starehe.

Mchezaji huyo Barcelona na Spain anaripotiwa kufuatiliwa baada ya kwenda kwenye show ya shakira mjini Barcelona, na wapelelezi walikuwa wanahesabu hata pombe alizokunywa na kuripoti kwa uongozi. 

El Confidencial limeandika kwamba hatimaye mchezaji husika aligundua kwamba anafuatiliwa, lakini klabu ikamwambia walikuwa ni waandishi wa habari za udaku. 

Msemaji wa FC Barcelona, ambayo ni moja ya klabu yenye mafanikio makubwa duniani, alitoa taarifa siku ya jumanne iliyosema kwamba klabu hiyo haitotoa maoni yoyote kuhusu madai hayo, kwa kuwa hakuna ushahidi wowote uliotolewa then wanapinga taarifa hizo.

Doting dad: Pique kisses his son Milan who was born in January this year

Mkuu wa idara ya ulinzi ya Barcelona aliyeacha kazi Xavier Martorell - ambaye kwa sasa ni mkuu wa gereza la Catalonia ameripotiwa kukiri kwamba aliwahi kuagizwa kuajiri kampuni ya upelelezi kufanya kazi kwa ajili ya chama cha siasa cha Hispania.

Toni Freixa, msemaji wa bodi ya wakurugenzi wa Barca, aliongea na gazeti la Marca kuhusu tuhuma za kupeleleza wachezaji na hivi ndivyo alivyosema: "Tulipoingia madarakani mwaka 2010 tuligundua €3 million zilikuwa zimetumika kwenye masuala ya ulinzi lakini hatukupewa mahesabu ya namna fedha hizo zilizivyotumika. Hivyo tunaweza tusikatae tuhuma hizi, lakini pia hatuwezi kusema ni kweli."

Wednesday, February 27, 2013

AZAM WAMUOMBEA KALI ONGALA KUKAA BENCHI



UONGOZI wa timu ya Azam umeliandikia barua Shirikisho la Soka  Tanzania (TFF) ya kuomba kocha wao msaidizi Kali Ongala aruhusiwe kukaa  benchi, baada ya kocha wao Mkuu Stewart Hall kufungiwa mechi tatu na kulipa faini ya Sh500,000 kwa kosa la kuvua bukta Uwanjani.Ongala amesimamishwa na TFF, kwa
kwa kuwa hana yeti vinavyo mtambulisha kama kocha msaidizi wa Azam.Kamati ya ligi kuu ilitangaza kumfungia kocha Stewart  mechi tatu na faini ya Sh500,000 kwa kosa la kuvua bukta uwanjani wakati wa mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar.
Katibu Mkuu wa Azam, Idrissa Nassor alisema kuwa baada kufungiwa kocha wao wameiandikia barua TFF,  kuomba wamruhusu Ongala kukaa benchi mpaka uchunguzi wa vyeti vyake utakapokamilika.''Ongala alifungiwa lakini tulishapeleka vyeti vyake muda mrefu lakini mpaka sasa wamekaa kimya hivyo tumewaandikia barua ya kumruhusu kocha huo msaidizi mpaka pale watakapojiridhisha na uchunguzi wao'' alisema Nassoro.
Katika hatua nyingine, Nassor alisema  kuwa timu yao inatarajia kuondoka nchini Jumamosi Asubuhi kwenda Sudan kusini kwa ajili ya kucheza mchezo wao wa marudioano dhidi ya El Nasri Juba.Alisema wanatarajia kupata upinzani  mkubwa ugenini kwa kuwa nia yao na ya kwao wote ni kuakikisha wanasonga mbele katika michuano hiyo.
Alisema timu itaondoka ikiwa na wachezaji 20 na viongozi saba tayari kwa  ajili ya mchezo wao wa Jumapili

YANGA YAENDELEA KUJIKITA KILELENI,YAIFUNGA KAGERA SUGAR BAO 1:0

 
YANGA imeendelea kujikita kileleni   na kuicha Azam kwa pointi 6 baada ya  kuichapa Kagera Sugar kwa bao 1-0  katika mchezo wa jana kwenye Uwanja  wa Taifa, Dar es Salaam.  Kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima aliwainua mashabiki  wa Yanga baada ya kufunga bao hilo kwa shuti la umbali wa mita 20, lililomshinda kipa wa Kagera Sugar, Hannington Kalyesubula.
Kwa matokeo hayo Yanga sasa imefikisha pointi 42 ikifutiwa na Azam (36), huku mabingwa watetezi Simba  akiwa nafasi ya tatu na pointi zake 31.Kipa wa Kagera,  Kalyesubula alifanya  kazi nzuri kuinyima Yanga bao la  mapema baada ya kupangua kichwa  kilichopigwa na Didier Kavumbagu  aliyeunganisha kwa uzuri krosi ya Simon Msuva dakika ya kwanza.
Viungo wa Yanga, Frank Domayo, Athumain Idd na Haruna Niyonzima walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo na kuwafanya Kagera Sugar muda  wote kucheza kwa kujiami.Katika dakika 15, Yanga ilikuwa imefika langoni kwa Kagera mara tano wakati vijana wa Kaitaba wakijibu mapigo mara moja tu.
Kocha wa Yanga, Ernest Brandts alimweka benchi mshambuliaji wake Jerryson Tegete baada ya kuonyesha kiwango cha chini katika mchezo uliopita dhidi ya Azam na kumwazisha Kavumbagu.Mshambuliaji huyo wa Burundi, alinyima Yanga bao katika dakika 45 baada ya mkwaju wake wa penalti kupaa juu ya lango la Kagera Sugar.Yanga ilipata penalti hiyo baada ya kipa Kalyesubula kumwagusha Kavumbagu kwenye eneo la hatari na mwamuzi Simon Mberwa wa Pwani kupuliza filimbi.
Yanga walirudi kwa kasi kipindi cha pili katika dakika 48, shuti la Domayo  liligonga mwamba na kurudi uwanjani.Kagera Sugar iliwapumzisha Julius Mrope na Darlington Enyinna na kuwaingiza Temi Felix, Paul Ngwai, wakati Yanga iliwatoa Said Bahanuzi na Kavumbagu kuwaingiza Jerryson Tegete na Hamis Kiiza.Mabadiliko hayo yalikuwa na faida kwa Yanga katika dakika 65 walifanikiwa kupata bao lililofungwa na Niyonzima kwa shuti la umbali wa mita 20.
Katika michezo mingine Polisi Morogoro wakiwa kwenye uwanja wa nyumbani Jamhuri waliwatambia  Mgambo JKT kwa kuichapa bao 1-0.Shujaa wa Polisi alikuwa Nahoda Bakari aliyefunga bao akimalizia mpira uliotemwa na kipa wa Mgambo, Tonny Kavishe akipangua penalti Kondo Salum baada ya beki Musa Ngunda kushika mpira kwenye eneo la hatari. Mkwakwani, Coastal Union walishindwa kuhutumia vizuri uwanja  wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa kwenda suluhu na Ruvu Shooting, sawa na matokeo ya Mtibwa
Sugar na Prisons uliochezwa Manungu, Turiani.

PHOTOZ: YANGA ILIVYOZIDI KUJICHIMBIA KILELENI KWA KUINYOOSHA KAGERA 1-0



PICHA NA FRANCIS DANDE BLOG

LIVE MATCH CENTRE: YANGA 1 - 0 KAGERA SUGAR


Dk 90+5 FULL TIME. YANGA 1-0 KAGERA.

Dk 89 Mkina wa Kagera anakosa bao la wazi akiwa amebaki na kipa wa Yanga.

Dk 85 Ngwai wa Kagera anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Mbuyu Twite.

Dk 79 Mwamuzi Mberwa anawapa kadi za njano wachezaji wa akiba wa Yanga, Nizar Khalfan na David Luhende baada ya kuacha kufanya mazoezi na kusimama wakitazama mpira wakiwa jirani na benchi lao.

Dk 73 Cannavaro anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Paul Ngwai wa Kagera.

Dk 73 Chuji anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Shija Mkina wa Kagera.
Dk 71 Kagera imefanya mabadiliko, ametoka Enyinna, ameingia Themi Felix.

Young Africans inafanya mabadiliko wanaingia Jerson Tegete na Hamis Kiiza kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu na Said Bahanuzi

Dk 70 Goooooooal Haruna Niyonzima anaipatia Yanga bao la kwanza

Dk 63 Themi Felix wa Kagera anapasha misuli moto.

Dk 62 Kagera imefanya mabadiliko, ametoka Mrope, ameingia Paul Ngwai.

Dk 60 Said Bahanunzi wa Yanga anaonyeshwa kadi ya njano.

Dk 56 Wachezaji wa akiba wa Yanga, Jerry Tegete na Hamis Kiiza wanapasha misuli moto.

Dk 48 Frank Domayo wa Yanga anapiga shuti kali limalogonga mwamba wa lango la Kagera na kurudi uwanjani baada ya kupokea pasi ya Niyonzima.

Dk 46 Chuji anamchezea faulo Nade wa Kagera. Yanga 0-0 Kagera.

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA!

Dk 45+3 HALF TIME! YANGA 0-0 KAGERA.

Dk 45+3 Kavumbagu wa Yanga anapiga penalti lakini anakosa baada ya mpira alioupiga kupaa juu ya lango la Kagera. Yanga 0-0 Kagera.

Dk 45+2 Kagera wanakubali penalti ipigwe lakini kipa wao Kalyesubula anaonyeshwa kadi ya njano kwa kitendo cha kugomea penalti hiyo kwa kwenda katika benchi la timu yake.

Dk 45 PENAAALTY...! Yanga inapata penalti baada ya mshambuliaji wake Didier Kavumbagu kuangushwa katika eneo la hatari na kipa wa Kagera, Kalyesubula. Kagera wanagomea penalti.

Dk 44 Oscar Joshua wa Yanga anapiga shuti kali kuelekea lango la Kagera na mpira unatoka nje.

Dk 43 Safu ya kiungo ya Yanga inapwaya na kupoteza pasi nyingi huku Kagera wakionekana kuzinduka na kucheza soka safi.

Dk 41 Haruna Niyonzima wa Yanga anamvuta jezi Muganyizi Martin na mwamuzi anaamuru ipigwe faulo kuelekea lango la Yanga.

Dk 39 Julius Mrope wa Kagera anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Athuman Idd Chuji.

Dk 32 George Kavila wa Kagera anapiga faulo inayotoka juu ya lango la Yanga.

Dk 31 Beki Oscar Joshua wa Yanga anamchezea vibaya Juma Nade wa Kagera na mwamuzi anaamuru ipigwe faulo kuelekea lango la Yanga.

Dk 29 Benjamin Asukile wa Kagera anamwangusha Msuva nje kidogo ya eneo la hatari la Kagera na mwamuzi Simon Mberwa wa Pwani anaamuru ipigwe faulo kuelekea lango la Kagera.

Dk 27 Kagera wamebadilika sasa wanatawala kiungo na kulifikia lango la Yanga mara kadhaa.

Dk 27 Kagera wamebadilika sasa wanatawala kiungo na kulifikia lango la Yanga mara kadhaa.

Dk 23 Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' anaumia baada ya kugongana na mshambuliaji wa Kagera Darlington Enyinna. Yanga 0-0 Kagera.

Dk 20 Mpira unasimama kwa muda kipa wa Kagera, Kalyesubula anarekebisha viatu vyake.

Dk 15 Kagera wanacheza kwa kuinda zaidi lango lao.

Dk 13 Msuva wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa Kagera lakini kipa Hannington Kalyesubula anaudaka mpira.

Dk 10 Yanga inacheza zaidi katika eneo la Kagera.

Dk 5 Yanga inapata kona baada ya Maregesi Mwangwa wa Kagera kuutoa nje mpira. Yanga 0-0 Kagera.

Dk 2 Didier Kavumbagu wa Yanga anakosa baada ya mpira wa kichwa alioupiga kugonga mwamba wa lango la Kagera.

Dk 1 Muganyizi Martin wa Kagera Sugar anamchezea vibaya Simon Msuva wa Yanga.

Young Africans line-up to face Kagera Sugar today:
1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athumani Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo 'Chumvi'
9.Said Bahanuzi
10.Didier Kavumbagu
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Said Mohamed
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nurdin Bakari
5.Nizar Khalfani
6.Hamis Kiiza
7.Jerson Tegete


KAGERA SUGAR LINE UP: Hannington Kalyesubula, Benjamin Asukile, Muganyizi Martin, Malegesi Mwangwa, Amandus Nesta (C), George Kavila, Julius Mrope, Juma Nade, Darlington Enyinna, Shija Mkina, Daudi Jumanne.

MJADALA: AZAM Vs YANGA- GOLI AU SIYO GOLI!

REAL MADRID YAICHINJA BARCELONA 3:1,YAINGIA FAINALI YA KOMBE LA MFALME!

CLOUDS FM THE SUPER BRAND RADIO STATION IN BONGO!

Tuesday, February 26, 2013

REVEALED:KIKULACHO KINGUONI MWAKO, KINACHOITAFUNA SIMBA HIKI HAPA-PART 2


KOCHA wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic amesema klabu hiyo ilimsitishia mkataba kishenzi baada ya kukataa kufanya kazi kwa ‘remote’ alipokuwa anaifundisha klabu hiyo.

Akizungumza katika mahojiano exclusive na mtandao huu, Milovan raia wa Serbia alisema muda mfupi baada ya kwenda likizo kwao Serbia baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Bara kuisha, alianzishiwa vituko kutoka kwa uongozi.

“Nilipokuwa likizo Serbia mambo hayakuwa mazuri kama ilivyokuwa awali, wakati zamani naenda likizo Simba walikuwa wakinipigia simu na kuzungumza mambo mbalimbali kuhusu maendeleo ya timu. Mara hii hawakufanya lolote kwangu nami nikakaa kimya,” anasema Milovan.


SIMBA WAMNYIMA TIKETI BILA SABABU


Kila mara Milovan anapokuwa kwao Serbia kwa likizo, uongozi wa Simba ulikuwa ukimtumia tiketi ya kurudi Tanzania. Hata tiketi ya kwenda huwa anakatiwa na Simba. Lakini yalibadilika ghafla.

“Muda ulipofika wa mimi kutumiwa tiketi kama ilivyo kawaida, kila nikiwapigia simu viongozi wananiambia subiri, muda ukawa unaenda nami kila nikiuliza jibu linakuwa lile lile kwamba subiri subiri.

“Wakati nafanya nao mazungumzo ya tiketi, hata siku moja sikuwahi kuongea nao vibaya. Sasa kuna kitu nikawa najiuliza hawa jamaa wana nia gani na mimi, Je, maendeleo ya kikosi yakoje? Sikupata jibu lakini kuna kitu nikaanza kuhisi,” anasema Milovan.


MKATABA WAKE WASITISHWA ‘KIAINA’


Wakati bado yupo Serbia, Milovan anasema wakati mazungumzo yake ya kudai tiketi yalipokuwa yakiendelea alikuwa akizungumza vizuri na viongozi wa Simba na hata siku moja hawakuwahi kumwambia wanamsitishia mkataba wake.

“Hatukuwa na mazungumzo mabaya hata siku moja, kila siku Simba walikuwa wakiniambia subiri tiketi, hata mara moja hawakuonyesha kama wamechukizwa nami au kuna jambo lingine wanalotaka kufanya,” anasema Milovan.

Milovan anasema taarifa za kibarua chake kuota nyasi alizijua baada ya kusoma katika vyombo vya habari kisha akaamua kuwasiliana na Simba na bado majibu yakawa yaleyale yanayomtaka kusubiri.


FRIENDS OF SIMBA, MESSI WAMPONZA


Milovan moja kwa moja anahisi kitendo chake cha kukataa kupangiwa timu ndicho kilichouuzi uongozi wa Simba na kuamua ‘kumchinjia baharini’ kwa kuwa alikuwa akienda kinyume na matakwa ya mabosi wake, hilo likawa tatizo kwa uongozi.

Kwa mfano, uongozi ulikuwa unataka kocha kumtumia kila mara mchezaji Ramadhani Singano ‘Messi’ katika kila mechi, Milovan hakutaka hali hiyo japokuwa alikuwa akikubali uwezo wa mchezaji huyo na kumpanga kila mara.

“Messi alikuwa mchezaji mzuri na mimi nlikuwa namtumia katika mechi zangu nyingi, tazama hata Kigali (Rwanda, katika mechi dhidi ya Kiyovu) nilimtumia na alifanya vizuri. Tatizo wao wakawa wanataka kila mara nimchezeshe, hilo llikuwa tatizo kwangu kwani mimi nina mipango yangu maalum na siyo nimfuate mtu anavyotaka,” anasema Milovan.

Milovan anatolea mfano Kundi la Friends of Simba lilivyokuwa likimwingilia katika upangaji wa timu na kila mara alikuwa akitofautiana nao huku ikionekana wazi kwamba wao ndiyo walioshikilia ajira yake kwa kiasi kikubwa.

“Kama ilivyokuwa kwa uongozi, Friends of Simba nao walikuwa na mambo yao, walikuwa wanataka kunipangia wachezaji wa kuwachezesha namna wanavyotaka na si vinginevyo, hapo sikukubaliana nao.

“Mimi nilikuwa natekeleza wajibu wangu katika kupanga kikosi, yeyote aliyekuwa akitaka kuniingilia katika upangaji timu sikusita kumwambia kwamba sihitaji hali hiyo. Yawezkana msimamo wangu huo haukupendwa na kundi hilo lenye nguvu ndani ya Simba,” anasema Milovan.

HAKUHUSISHWA KUSIMAMISHWA BOBAN, NYOSSO

Milovan anasema wakati wachezaji Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Said ‘Nyosso’ wanasimamishwa kuichezea Simba, hakuhusishwa kama kocha kitendo ambacho kilienda kinyume na maadili.

Simba ikiwa katika mechi zake za mwisho za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Bara, ilimsimamisha Boban kutokana na utovu wa nidhamu na Nyosso alisimamishwa kupelekwa timu B kwa kile kilichoelezwa ameshuka kiwango.

Milovan anasema uongozi haukumshirikisha kuhusu wachezaji hao na ulichukua dhidi yao kabla ya kuwasiliana naye. Mbaya zaidi uongozi ulimuita katika kikao cha kuwajadili wachezaji hao wakiwa tayari wameshasimamishwa.

“Viongozi waliwasimamisha Nyosso na Boban bila kunitaarifu halafu baadaye wakaniita kuwajadili wachezaji hao, hii si taaluma. Anayejua kuhusu kushuka kiwango cha mchezaji ni kocha, sasa iweje viongozi waseme mchezaji kashuka kiwango? Hii haikuwa haki na niliueleza uongozi,” anasema Milovan.

SIMBA YAMLIPA MAMILIONI

Milovan anasema amekuja nchini kufuatilia malipo ya kusitishwa kwa mkataba wake ambao ulipaswa kuisha Julai mwaka huu. Japokuwa Milovan hakuwa tayari kuweka wazi mshahara wake, mtandao huu unaamini kocha huyo anaweza kulipwa zaidi ya Sh. 52 milioni ambazo ni sawa na dola 35,000 za kimarekani.

“Wanatakiwa wanilipe stahili zangu zote, mimi mkataba wangu unaisha Julai mwaka huu wao wameuvunja tena kienyeji, unategemea nini? Lazima wanilipe ili kila mtu aweze kuwa salama,” anasema Milovan.

Aliyelipa fedha kwa Milovan si uongozi wa Simba ambao ulimterekeza, bali ni mmoja wa wanakamati wake wa kamati ya fedha, Rahma Al Kharuus ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya RBP Oil.

ENDELEA KUSOMA MTANDAO HUU KWA SEHEMU YA 3 YA ALICHOSEMA MILOVAN KWA SIMBA

KUELEKEA EL CLASSICO USIKU HUU - HIZI NDIO TAKWIMU ZA BARCA NA MADRID MSIMU



YANGA NA AZAM WAZIFUNIKA SIMBA NA MTIBWA KIMAPATO

Katika mechi zilizochezwa wikiendi iliyopita zilizowahusisha watani wa jadi Simba na Yanga, zilizocheza mechi dhidi ya Mtibwa Sugar na Azam mapato yaliyopatikana kutokana na viingilio hizi yametolewa hadharani kama kawaida. Na kama ilivyokuwa huko nyuma Yanga imeendelea kuipeleka Simba kwa kuingiza fedha nyingi kutokana kwenye mechi zinazoihusisha klabu hiyo ya jangwani.

Wakati katika mechi kati ya Simba na Mtibwa ikiingia millioni 62, mechi ya Yanga na Azam imeingiza 240.
  
  MECHI YA SIMBA, MTIBWA YAINGIZA MIL 62/-
Mechi namba 121 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa juzi (Februari 24 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Mtibwa Sugar kuibuka ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba imeingiza sh. 239,686,000.

Watazamaji 10,669 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,577,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,467,694.92.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 9,491 na kuingiza sh. 47,455,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 105 na kuingiza sh. 2,100,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,412,162.26, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,447,297.36, Kamati ya Ligi sh. 4,447,297.36, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,223,648.68 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,729,504.53.

MECHI YA YANGA, AZAM YAINGIZA MIL 240/-
Mechi namba 120 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa jana (Februari 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Yanga kuibuka ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam imeingiza sh. 239,686,000.

Watazamaji 39,315 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 58,794,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 36,562,271.19.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 33,315 na kuingiza sh. 165,655,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 485 na kuingiza sh. 9,700,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 29,895,725.82, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 17,937,435.49, Kamati ya Ligi sh. 17,937,435.49, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 8,968,717.75 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 6,975,669.36.