Search This Blog

Saturday, February 16, 2013

HIVI NDIVYO AZAM WALIVYOWATIA ADABU WASUDAN UWANJA WA TAIFA LEO

Kiungo wa timu ya Azam FC, Bolou Kipre (kushoto) akitafuta mbinu za kumtoka mshambuliaji wa El-Nasir FC ya Sudan ya Kusini, Abdallmelik Sebit katika mchezo wa Kombe la Shirikisho uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. (Picha na Dande JR)
 Wachezaji wa Azam FC wakishangilia bao la pili la timu yao lililofungwa na Kipre Tchetche (katikati) wakati ilipoibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya El Nasir ya Sudan ya Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
 Jabir Aziz akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa El Nasir FC ya Sudan ya Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji wa Azam FC, Brian Umomy akiwatoka walinzi wa timu ya El-Nasir FC ya Sudan ya Kusini, Jacob Osuru na Abdallmelik Sebit katika mchezo wa kombe la Shirikisho uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Kikosi cha el Nasir ya Sudan ya Kusini
 Kikosi cha Azam FC
Mashabiki wa Azam 

TENGA AWATAKA WALIOKATWA UCHAGUZI WA TFF KUFUATA TARATIBU ZA KUTAFUTA HAKI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewataka waombaji uongozi ambao hawaridhiki na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi kutafuta haki yao kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam leo (Februari 16 mwaka huu) mchana, Rais Tenga amesema  TFF ni moja ya taasisi ambazo zina utaratibu unaoeleweka kwa wadau wake.

“Wote tunafahamu taratibu ambazo tumejiwekea juu ya wagombea wetu wanachaguliwaje. TFF ni moja ya taasisi ambazo zina utaratibu unaoeleweka. Hii ni kuanzia wilayani. Kama kuna tatizo zipo njia za kufuata.

“Katika mchakato wa uchaguzi wengine wanafanikiwa, wengine wanaachwa. Wameachwa kwa sababu zilizotolewa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi. Ambaye haridhiki anafuata taratibu tulizojiwekea. Atafute haki yake kwa mujibu wa taratibu,” amesema.

Rais Tenga amesisitiza kuwa kikatiba hana uwezo wa kuingilia uamuzi unaofanywa na kamati ambazo ameziunda, kwani utawala bora ni kusimamia kanuni ambapo wanaofanya uamuzi lazima waweke wazi sababu za uamuzi waliofikia.

Amesema ambao hawakubaliani na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF dhidi yao wana njia tatu za kufuata. Njia hizo ni kuiomba Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ipitie uamuzi iliofanya (review), kuandika Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kuomba liingilie au kwenda Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo (CAS).

“Hata ukiweka ngazi nne, mtu akiathirika ataona ameonewa tu. Kwa Katiba yetu hapa (Kamati ya Rufani ya Uchaguzi) ndiyo mwisho. Hakuna chombo kingine. Ukiwaomba FIFA waingilie, watakuja na tutawaeleza mchakato wote ulivyokwenda. Tunapenda kuwahakikishia hawa (waathirika) kuwa kwa maslahi ya mpira wa miguu tutasaidia katika hilo wapate haki,” amesema Rais Tenga na kuongeza kuwa tayari waathirika wawili wa uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi wameomba marejeo (review) kwenye kamati hiyo hiyo.

Amesema TFF imelazimika kuzungumzia suala hilo kwa sababu limekuwa likizungumzwa kinazi zaidi wakati taratibu ziko wazi, hivyo kwa maslahi ya mpira wa miguu ni vizuri taratibu zikafuatwa.

“Nawaomba washabiki wa mpira wa miguu, tumejenga chombo hiki (TFF) kwa muda mrefu. Bado tunaomba watu watusaidie, kwa hiyo matusi hayawezi kubadili kitu. Tunachowahakikishia ni kuwa, mtu anapoomba msaada tutampa kutafuta haki yake.

“Hizi ni kamati huru, lazima ziheshimiwe. Ukianza kuziingilia utakuwa umeua mpira wa miguu. Uongozi ni utumishi, tusionekane tunagombana. Huu si ubunge, mbunge anachaguliwa anakwenda kulipwa mshahara. Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF halipwi mshahara. Tusirudi kwenye matusi, tulishaondoka huko,” amesema.

Kuhusu mabadiliko ya Katiba yaliyofanyika kwa njia ya waraka, Rais Tenga amesema yamefanyika kwa mujibu wa taratibu, na haikuwa siri. Maeneo yaliyofanyiwa marekebisho ilikuwa ni lazima, kwani mengi yalikuwa ni maagizo kutoka FIFA na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Amesisitiza kuwa mabadiliko hayo yamefuata taratibu na hakuna udanganyifu katika hilo, kwani ridhaa ya kutumia waraka iliombwa, na Mkutano ni watu ambao ndiyo wamepitisha mabadiliko hayo.

“Mkutano Mkuu ni watu, si kikao. Katika dunia ya leo mikutano inafanyika kwa tele conference, si lazima watu wakutane sehemu moja,” amesema na kuongeza kuwa mabadiliko hayo yalipitishwa kwa kura 70 dhidi ya 33 zilizokataa.

Kuhusu Kanuni kusainiwa kabla ya Katiba, Rais Tenga amesema tarehe ya kuanza kutumika Katiba ni siku ridhaa ilipopatikana, na si siku mhuri wa Msajili ulipopigwa. Mabadiliko ya Katiba yalipita Desemba 15 mwaka jana, Kanuni zilisainiwa Januari 7 mwaka huu.

LIVE MATCH CENTRE: AZAM FC 3-1 AL NASIR



Dk 90+4 Gooo....! Tchetche anaipatia Azam bao la tatu akimalizia pasi ya John Bocco. Azam 3-1 Al Nasir.

Dk 87 Azam imebadilika inacheza soka la kasi sana na wanafika langoni kwa Al Nasir mara kwa mara.

Dk 80 Gooo....! Kipre Tchetche anaipatia Azam bao la pili kwa kichwa akimalizia krosi ya Khamis Mcha. Azam 2-1 Al Nasir

Dk 79 Al Nasir inafanya mabadiliko, ametoka Abdallmelik Sebit ameingia Emmanuel Manasi.

Dk 77 Timu zinashambuliana kwa zamu mpira umechangamka.

Dk 62 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Abdi Kasim ameingia John Bocco.

>Dk 60 Al Nasir inafanya mabadiliko, ametoka Johnson James ameingia Adnan Nan.

Dk 57 Jabir Aziz wa Azam anakosa bao la wazi akiwa amebaki na lango la Al Nasir

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA!

Dk 45 HALF TIME!

Dk 44 Mpira umebadilika timu zinashambuliana kwa zamu sasa, Al Nasir wamezinduka.

Dk 38 Gooo....! Fobian Elias anaipatia Al Nasir bao la kusawazisha akimalizia pasi ya Kon James. Azam 1-1 Al Nasir

Dk 35 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Bolou Kipre ameingia Jabir Aziz.

Dk 26 Timu zinashambuliana kwa zamu, Al Nasir japokuwa hawajapata bao lakini wanaonekana wana malengo.

Dk 16 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Brian Umony ameingia Khamis Mcha.

Dk 14 Gooo...! Abdi Kasim anaipatia Azam bao la kwanza kwa kichwa akiunga krosi ya Kipre Tcheche. Azam 1-0 Al Nasir.

Dk 12 Timu zinashambuliana kwa zamu, Al Nasir wanacheza pasi nyingi.

Mpira umeanza hapa uwanja wa taifa

MSIMU WA VALENTINE NA BAILEYS WAFIKA TAMATI KWA MAFANIKIO

Miss Tanzania 2007 Richa Adhia aliyeshika chupa ya Baileys akiwa na
Gipson Godwin(kulia) na Scolastica Dotto ambaao ni mabalozi wa kinywaji
hicho kutoka Kampuni ya bia ya Serengeti.


Miss Tanzania 2007 Richa Adhia  amewataka watanzania kujenga utamaduni wa kuwakupenda  na kuwajali watu wengine wakiwemo wenye mahitaji maalum kama watoto na wazee  kwa kuwa wanahitaji faraja toka kwa jamii nzima nyakati zote badala ya kusubiri  maadhimisho ya sikukuu mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kilele cha msimu wa  siku ya wapenda nao ulioandalia na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji cha Baileys katika viwanja vya shoppers jijini Dar es Salaam,  Richa alisema “siku ya wapendanao ikitumika  kuongeza ari ya kuwasaidia watu wenye mahitaji inakuwa na maana zaidi kuliko kuitumia siku  hiyo kwa mapenzi zaidi na sio vibaya kutumia siku ya wapendanao  kuanzisha mapenzi mapya au kuboresha mapenzi yaliyokuwepo lakini pia itumike kuwakumbuka wahitaji ambao ni wazee na watoto”.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa vinywaji vikali kutoka Kampuni ya bia ya Serengeti Emilian Rwejuna amesema “ tumeamua kufanya kampeni hii ili kuamsha ari ya kuwajali na kuwapenda wengine ikiwemo kujenga utamaduni wa kuwanunulia zawadi kama tulivyofanya kwa wapenzi wa kinywaji cha Baileys na kwa kuwa zawadi zina mchango mkubwa katika maisha ya mahusiano hivyo mtoto anayempa zawadi mzazi wake hujiweka katika mazingira mazuri kimahusiano kuliko asiyefanya hivyo”.Pia alielezea kuwa Kampuni ya bia ya Serengeti imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuhamasisha na kutoa chachu na kuahidi itaendelea kuhamasisha mahusiano mema  miongoni mwa jamii.

Kampeni ya msimu wa valentine  iliyoandaliwa na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Baileys ilinza tarehe mosi mwenzi wa Februari kwa kupita katika maeneo mbalimbali ya manunuzi ili kuwahamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kuwanunulia wenzi wao zawadi na kukamalika siku ya wapendanao Februari 14. Ambapo zawadi mbali mbali zilitolewa katika kampeni hiyo ikiwemo chupa ya Baileys, fulana, glasi, maua na kubwa zaidi pea nane zilipata bahati ya kupata chakula jioni katika mgahawa wa Akemi uliopo jijini Dar es Salaam.

Friday, February 15, 2013

MARADONA APATA MTOTO MWINGINE AKIWA NA UMRI WA MIAKA 52

Diego Maradona amekuwa baba tena baada ya mkewe Veronica Ojeda kujifungua mtoto wa kiume ambaye amepewa jina la Diego Fernando Maradona Ojeda. 
 
Jorge Auruccio, mwanasheria wa Ojeda, alisema kwamba mtoto alizaliwa na uzito wa 3.2 kilograms (7 pounds) na alizaliwa jumatano saaa 11:57 p.m. kwa muda wa Argentina katika hospitali ya Buenos Aires. Alisema na mtoto na mama yake wapo kwenye hali znuri ya kiafya. 

Maradona mwenye miaka 52 tayari ana watoto wawili wa kike kutoka kwenye ndoa yake na Claudia Vallafane - watoto hao ni Dalma and Giannina. Pia mkongwe huyo wa soka ana watoto wengine wawili ambao amekataa kuwatambua - japokuwa vipimo vya DNA vilivonyesha ni baba wa watoto hao.

Auruccio alisema kwamba Maradona alikuwa Dubai lakini alikuwa anajua kila kitu kilichokuwa kinaendelea kuwa kujifungua kwa mwenza wake. 

Maradona pia ana mtoto mwingine wa kiume aitwaye Diego Armando Maradona Sinagra, ambaye alimzaa wakati akiwa nchini Italy akiichezea Napoli. 

"Jaji ameniamuru nimlee mtoto, lakini hilo halinifanyi nijihisi kumpenda huyo mtoto," alisema Maradona mwaka 2005. 

BAADA YA KUTEMWA SIMBA - DANNY MRWANDA APATA TIMU TENA VETNAM

Miezi kadhaa baada ya kutemwa na klabu bingwa ya Tanzania bara, Simba Sports Club, mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Danny Mrwanda sasa amepata timu ya kuichezea huko nchini Vetnam.

Mrwanda ambaye miaka kadhaa iliyopita alikuwa mchezaji tegemeo wa Simba kabla hajauzwa kwenda nchini Vetnam kucheza soka la kulipwa katika vilabu vya Dong Tam Long An na Hoang Anh Gia Lai na baada ya kumaliza mkataba wake akarudi bongo kujiunga na Simba, lakini muda mfupi baada ya kujiunga na timu akatemwa kwa madai kwamba kiwango chake kimeshuka

Akizungumza na mtandao huu Mrwanda amesema kwamba baada ya kuondoka Bongo, alirudi nchini Vetnam ambapo sasa ameweza kujiunga na mabingwa wa ligi kuu ya Vetnam klabu ya DA NANG FC kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu.

"Nimepata timu huku ya DA NANG FC, hii timu ndio bingwa wa ligi kuu ya Vetnam. Sasa tutashiriki ligi ya mabingwa wa bara la Asia." - Alisema Mrwanda.









BOCCO ARUDI DIMBANI, ANAWEZA KUANZA KESHO DHIDI YA WASUDANI - HUKU KOCHA STEWART HALL AKITAMBA KUSHINDA

AZAM FC inashuka dimbani kesho kuumana na Al Nasir ya Sudan Kusini katika pambano la raundi ya kwanza ya Michuano ya Kombe la

Shirikisho litakalopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Azam inayoshiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu ilipotinga ligi kuu mwaka 2007, inalazimika kushinda mchezo huu na kujiweka katika nafasi nzuri yakusonga mbele.

Kocha wa Azam, Stewart Hall ametamba kuwa kikosi chake kipo tayari kwa mpambano huo kuhakikisha kinazindua kampeni yake kwa ushindi.

"Tumefanya maandalizi ya kutosha, tumecheza mechi nyingi za kujipima nguvu katika ziara yetu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Kenya sasa ni wakati wa kuwapa raha Watanzania kwa kuibuka na ushindi,".alisema Hall.

Katika pambano hilo,Hall huenda akampa nafasi japo kwa dakika chache  mshambuliaji John Bocco ambaye  afya yake imethibitishwa na daktari wa timu hiyo Mwanandi Mwankemwa kuwa imeimarika.

Bocco ambaye kwa muda mrefu amekuwa mpachikaji mabao tegemeo wa muda wote wa kikosi cha Azam alikuwa nje ya dimba kwa takribani mwezi mmoja baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.

Mwingereza huyo pia atamtegemea mshambuliaji mwingine tegemeo wa timu hiyo Kipre Tchetche kusaka mabao lakini ambaye atakuwa akilishwa mipira na Humprey Mieno, huku beki Jockins Atudo akisubiri kuzamisha mipira wavuni kwa mipira ya kona.

Pambano la marudiano kati ya Azam na Al Nasir litapigwa kati ya Machi 1,2 na 3 katika mji wa Juba,Sudan Kusini.

BAHANUZI - "NIMERUDI KWENYE FOMU ILA KOCHA ANASHINDWA KUNIAMINI KUNIPA NAFASI"

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Said Bahanuzi amesema anafikiri kwa sasa amerudi kwenye fomu isipokuwa tu kocha ndiye anashindwa kumwamini kuanza kikosi cha kwanza.
 

Kocha wa Yanga, Mholanzi Ernie Brandts amekuwa akimtumia Bahanuzi kama mchezaji wa akiba tangu aliporejea uwanjani.

Bahanuzi aliyejiunga na Yanga msimu huu akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro alikuwa anasumbuliwa na maamivu ya nyama za paja aliyoyapata akiwa na timu ya Taifa Stars mwaka jana.
 

Katika mechi mbili za ligi ambazo nyota huyo ametokea benchi zikiwa zimebaki dakika 15 kabla ya mchezo kumalizika amefanikiwa kutoa pasi ya bao kila mechi.

Mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Bahanuzi ndiye aliyetoa pasi kwa Hamis Kiiza kufunga bao la kusawazisha. Timu zote mbili zilifungana bao 1-1.


Pia, mchezo wa African Lyon uliochezwa Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Bahanuzi akitokea benchi alitoa pasi kwa Nizar Khalfan aliyefunga bao la tatu wakati Yanga ikishinda 4-0.


Mara zote anapoingia mshambuliaji huyo mwenye nguvu za miguu na uwezo wakufyatua mashuti makali, amekuwa akiichangamsha safu ya ushambuliaji ya Yanga tofauti alivyokuwa benchi.


"Kwa sasa nafikiri nimerejea kwenye fomu. Nafikiri kocha tu ndiye anashindwa kuniamini." alisema Bahanuzi mwenye bao moja kwenye ligi alilofunga kwa penalti dhidi ya Simba Oktoba 3, mwaka jana.


"Nilikuwa nasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja. Kwa sasa nafikiri hali yangu imeimarika kama awali." alisisitiza.


Kwa upande wake Ernie Brandts alisema; "Siwezi kumchezesha dakika 90. Nadhani Bahanuzi ametoka kwenye majeruhi. Kwa hiyo nimekuwa nikimpa dakika 15 za mwisho kutizama maendeleo yake.


"Nafikiri ameimarika kwa mechi mechi ambazo nimemuona akicheza."

Zawadi nono kutolewa kwa wanariadha Kilimanjaro Marathon



Waandaaji wa Kilimanjaro Marathon 2013 wametangaza kutoa zawadi nono kwa wanariadha watakaoshiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.

George Kavishe, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager alisema katika taarifa kwa vyombo vyua habari jana kuwa“Kilimanjaro Premium Lager inaendelea kutambua mchango wa wanariadha kwa kuwazawadia kwa mara nyingine na mara hii ikiwa ni zawadi nono pamoja na motisha nyingine’’.

Alisema fedha kwa ajili ya zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu pande zote mbili wanaume na wanawake kwenye Kilimanjaro Marathon kilometa 42 ni zaidi ya shilingi milioni ishirini.

Washindi wa kwanza wa Kilimanjaro Marathon kilometa 42 upande wa wanaume na wanawake watajishindia Tsh Milioni 3 kila mmoja, lengo likiwa kuvutia wanariadha wa hadhi ya juu duniani, kuhamasisha uwekaji wa rekodi mpya na pia kusheherekea miaka kumi na moja ya Kilimanjaro Marathon. 
                     
Aliongeza kuwa ‘‘Kipaumbele cha Kilimanjaro Premium lager ni kuwapa motisha wanariadha wa Tanzania zaidi, na kwa sababu hiyo Kilimanjaro Premium Lager wametenga kiasi cha pembeni cha Tsh milioni 6 kwa wanariadha watanzania ambao watamaliza wa kwanza katika pande zote mbili wanaume na wanawake katika mbio ya Kilimanjaro Marathon kilometa 42 kila mmoja akijipatia milioni 3.
Kiasi hicho cha fedha kitakabidhiwa kwa wanariadha Watanzania kama nyongeza ya kile watakachopata kwenye ushindi wa mbio walizoshiriki na kushinda. “Tunaamini kuwa hii itawahamasisha wanariadha watanzania kuongeza juhudi na kumaliza mbio kwa muda mzuri”.
Washindi wa pili watajipatia shilingi milioni 1.5 kila mmoja na wa washindi wa tatu watajipatia shilingi 850,000 kila mmoja kwa wanawake na wanaume.

John Addison, Mkurugenzi Mtendaji wa Wild Frontiers ambao ni waandaaji wa tukio hilo alisema Mshindi wa nusu Marathon kwa wanaume na wanawake atajishindia Tsh 1,500,000 kila mmoja, mshindi wa pili Tsh 750,000 na mshindi wa tatu Tsh 375,000.

Washindi wa  mbio za GAPCO Nusu Marathon kwa walemavu watajipatia zawadi nono pia, ambapo mbio hizi zinajumuisha sehemu tatu yaani kiti cha matairi, hand cycle na walemavu wengine na kila mshindi kwenye kipengele chake atapata zawadi kama ifuatavyo;

Mshindi wa kwanza Tsh 300,000, mshindi wa pili kwa wanaume na wanawake Tsh 200,000, na mwisho mshindi wa tatu atajinyakulia Tsh 50,000.

Kwa upande wa mbio za kujifurahisha za Vodacom 5km Fun Run washiriki wote watakaomaliza mbio hawataondoka mikono mitupu bali watajipatia t-shirts na zawadi nyingine nono kama simu na muda wa maongezi pia zitatolewa kupitia bahati nasibu. Mbio hizi ndio zinazotoa fursa kwa watu wa rika zote kuwa sehemu ya Kilimanjaro Marathon.
Mbio hizo zinaratibiwa na Executive Solutions na kudhaminiwa na Kilimanjaro PremiumLager, huku wadhamini wengine wa tukio hilo ni pamoja na Vodacom Tanzania (5km Fun Run), GAPCO (Nusu Marathon Walemavu), Tanga Cement, CFAO Motors, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, TanzaniteOne, New Arusha Hoteli, Kilimanjaro Water, FastJet na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu

HUU NDIO MKWANJA ULIOINGIA KWENYE MECHI YANGA NA AFRICAN LYON

Mechi namba 119 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa juzi (Februari 13 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Yanga kuibuka ushindi wa mabao 4-0 imeingiza sh. 68,438,000.

Watazamaji 12,147 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 16,170,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,439,694.92.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo 10,982 walikata tiketi hizo na kuingiza sh. 54,910,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 8,222,162.26, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,933,297.36, Kamati ya Ligi sh. 4,933,297.36, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,466,648.68 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,918,504.53.

KATIBA ILIYOTUMIKA KUITISHA UCHAGUZI WA TFF NI BATILI-WAMBURA



Hivi karibuni kumetokea hali ya Sintofahamu kuhusiana na Uchaguzi kuu wa TFF uliopangwa kufanyika Tarehe 24/2/2013, mimi nilikuwa mmoja kati ya watanzania wengi waliojitokeza kuomba nafasi mbali mbali nikiwa nawania nafasi ya makamu wa Rais, matarajio yangu ya kuwania nafasi hiyo yalianza kuingia dosari kwa mara ya Nne(4) tangu 2008 katika chaguzi mbalimbali ambazo TFF ina maslahi nazo.
Kamati ya Uchaguzi ililiondoa jina langu kwa sababu mbili.
  1. Kamati inaheshimu maamuzi ya Kamati ya Jaji Mkwawa ya 2008 yaliyoniondoa katika kinyang’anyiro hicho.
  2.  Sababu ya pili ni  kuwa niliipeleka Simba mahakamani.
Katika kujaribu kutekeleza na kulinda maslahi yao kwa kuitumia  kamati ya Rufaa za  Uchaguzi, kwa ulafi wa kamati hiyo imejikuta ina kula mpaka vidole vyake, huku ikisema kuwa kuhusu wambura wanaheshimu maamuzi ya kamati  ya Jaji mkwawa, ni kwa nini hawakuheshimu maamuzi ya Kamati ya Rufaa ya prof FIMBO yaliyonisafisha wakati wa uchaguzi wa MARA? hivi tujiulize Kamati ile ilinifungia maisha nisigombee tena uongozi wa Mpira wa Miguu.
Kama kwenda mahakamani ni Kosa ni vipi leo Sunday Kayuni anakuwa mkurugenzi wa Ufundi wa TFF wakati aliwahi kuishitaki TFF katika mahakama ya Hakimu mkazi ya KISUTU kesi na 21 ya 2004. Kamati ya Uchaguzi ya  Lyatto pia Imempitisha Stanley lugenge kugombea ujumbe wa kamati ya Utendaji kanda ya Njombe na Songea huku kamati ikijua wazi alishirikiana na Sunday Kayuni kuishitaki TFF mahakamani inachoonekana kwenda mahakamani ni dhambi kwa Wambura tu.
Kamati ya Jaji mkwawa iliyotengua maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF 2008 baada ya kuliondoa Jina la Jamal Malinzi kwenye orodha ya wagombea Uraisi wa TFF, ni kwanini Kamati ya Mtinginjola haikuliona hilo katika mazingira hayo ninaamini TFF na Raisi wake kwa njia moja au nyingine wana  mkono kwenye hili la kuondoa jina la MALINZI Kwa sabau zifuatazo,
  1.  2008 Jamali malinzi aligombea Urais wa TFF  wakichuana na Tenga, katika hatua za awali za Mchakato Jina la Malinzi liliondolewa(kukatwa) kwenye orodha ya wagombea na kamati ya Uchaguzi iliyokuwa chini ya Tandau kwa sababu hizi hizi zilizo tolewa sasa na mtu wa kufikirika anayeitwa AGAPE  FUE.  Malinzi alikata rufaa kwenye kamati ya Rufaa chini ya Jaji  Mkwakwa, kwa mbinde jina lake likarudishwa kugombea, Katika Uchaguzi ule Kura hazikutosha kwa Malinzi, Tenga akachaguliwa kwa mara ya Pili.
Mara baada ya Uchaguzi, TFF alitoa shukurani na kuipongeza iliyokuwa  Kamati ya Uchaguzi kwa kazi nzuri kwa na  kwateua katika  kamati mbali mbali za TFF na wengine kuingia katika Kamati ya Utendaji.
Kamati ya Rufaa ya Jaji Mkwawa iliondolewa kwani wajumbe waliokuwa wameonekana walikuwa na nguvu na ushawishi kwenye kamati ile waliondolewa bila hata kushukuriwa wala kuteuliwa katika kamati pamoja na  kwa nzuri mbalimbali  walizokuwa wameifanyia TFF kwa kuwa tu walishiriki kulirudisha jina la Jamal Malinzi agombee Urais wa TFF kumpambana na  TENGA wajumbe wa kamati ile walikuwemo DR Dau-Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Mwanasheria William Urio- mkurugenzi Mkuu PPF, Marehemu Gratian Matovo wote hao hawakuteuliwa tena kwenye kamati ndogo ndogo za TFF.
  1. Mwaka 2012 TFF akijua wazi FIFA haikuiagiza TFF kuunda kamati ya rufaa ya uchaguzi ila ilishauri kuwa sio vyema kamati ya uchaguzi ikwa ndio ya mwisho  kwenye maamuzi ya Uchaguzi kwani yenyewe pia ndio inasimamia chaguzi hizo  ili haki itendeke kutokana  na ukweli wa Suala langu,TFF iliamua kuunda kamati nyingine kusikiliza rufaa za uchaguzi.
TFF  ilikuwa inafahamu fika Kanuni za uchaguzi mkuu wa TFF zilikuwa zinaelekeza masuala ya rufaa za Uchaguzi wa TFF yatashughulikiwa na Kamati ya Rufaa ya TFF, lakini kwa jinsi Kamati ya Rufaa  ya TFF inayoongozwa na Prof Fimbo ilivyo shughulikia suala langu katika Rufaa ya FAM(Mara)  na kunipa Ushindi, TFF Hakufurahishwa na ilihisi katika uchaguzi huu isingeweza kuishawishi kamati Prof Fimbo iwakate au kuwapitisha watu inaoataka wao.
Ili kutimiza matakwa yake Tff ikaamua kuvunja na kuisigina Katiba ya TFF kwa kutoa waraka wa kubadili katiba  kinyume na katiba ya TFF Ibara 22(1), 24(1)(l),27(1) ili aweze kuunda kamati zenye hila ambazo zitatekeleza amri zao, ambazo kwa kiwango kikubwa amefanikiwa kwa muda tu. TFF hakumtaka malinzi mwaka 2008 na haimtaki 2012 hainiingii akilini kuamini TFF haina mkono katika hili la kukatwa malinzi.
Nina hakika Jamal Kupitishwa na Kugombea  Kagera  ilikuwa ni kwa mbinde, kila njia na mbinu za kuondoa jina lake kupitia kamati ya Uchaguzi Kagera zilifanyika zikashindikana, nina hakika kama TFF hii ingeendelea kuwa madarakani au wakaingia vibaraka waao  basi Malinzi na watu wengine wenye uwezo na nia njema na mpira wa miguu wa Tanzania wangeondolewa kwa kutumia Kamati zenye Hila na Majungu za TFF.
Mpango wa Kuondolewa kwa Jina la Malinzi kwenye uchaguzi zilianza mapema na zilifanywa na watu wa kambi ya Mgombea Urais mmoja ambaye kwa kiasi kikubwa alishirikiana na Tenga kusigina katiba na Kuunda kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ambayo sehemu kubwa imejaa marafaiki wa mgombea huyo, baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo wenye heshima zao katika jamii Kama Prof Madundo Mtambo, Kamanda Mpinga  wamejikuta katikati ya watu waliokuwa tayari wana hila na maamuzi yao kabla ya kikao.Pamoja ya kuwa na Mjumbe kutoka mahakama kuu (FRANCIS KEBWE) tulipata imani ya kuwa atasaidia kamati kuelewa kuwa kwa kuwa Kamati ya Juu yaani Rufaani ya Jaji Mkwawa 2008  iliisha toa uamuzi wa Uzoefu wa Malinzi  na kwa kuwa hakuna chombo chochote kilicho wahi kuutengua basi walipaswa kuuheshimu na kuutumia kwenye maamuzi ya Kesi zinazo fanana za aina hiyo (PRECEDENCE) isipokuwa alikumbuka principle hiyo wakati anajadili rufaa ya wambura akasahau wakati wa rufani dhidi ya MALINZI, inawezekana ilikuwa ni bahati mbaya au ilipangwa na yeye alishiriki kujisahaulisha? Hiyo tunaiachia jammi ihukumu pamoja na kwamba kuna tetesi za ukaribu wake na mgombea mmoja wa Uraisi wa TFF na  ameahidi kuwa atatumia kofia yake mahakamani kuhakikisha  kama kuna mtu atataka kufungua shauri Mahakamani basi yeye atadhibiti kwa uwezo wake, ninapenda kumtahadharisha kutochanganya kazi na mambo ya jamii.
Mwenyekitiki wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi Ng Mtinginjola ni mwanasheria ninamfahamu , aliwahi kuwa kwenye kamati moja za DRFA wakati Nd Athmani  Nyamlani akiwa katibu wa DRFA, na baadaye  alihamishwa TFF kwenye kamati ya Nidhamu na Usuluhishi, hakuna ubishi anafahamiana vizuri na mgombea Nyamlani, Kisheria Mtinginjola alipaswa kujiondoa wakati wa rufaa ya Malinzi kwa kuwa asingeweza kuwa na mikono misafi  ya kutekelaza haki ya msingi ya Natural Justice kwani sheria inataka “ Si tu haki itendeke lakini ionekane kutendeka” kuna wanao sema Mtinginjola na Nyamlani waliwahi kufanya Kazi pamoja Katika Mahakama Temeke mmoja akiwa hakimu mwingine Karani wake, hivyo ni wazi Kulikuwa na mgongano wa kimaslahi kwenye Uamuzi juu ya rufani ya  Malinzi, Katiba ya TFF (2006)ibara ya 36(3) inamtaka “mjumbe wa kamati ya Utendaji kutoa tamko kama ana   maslahi na mjadala wowote na kujiondoa kwenye mjadala  kama kushirki kwake kuteleta mgongano wa kimaslahi”hivi ni kweli Mtinginjole na wenzake  hawakulijua hili au uwepo wao katika kamati hii ulikuwa wa kimkakati zaidi huku wakisimamiwa na TFF ili majina ya MALINZI na WAMBURA yaondolewe? Kanuni za Uchaguzi Ibara 2(1) inazungumzia democrasia ya Mgawanyo wa madaraka katika Uwazi bila kuacha kitu katika mchakato wa Uchaguzi wa TFF, swali je Urafiki, Hila, Ghilba ndio uwazi huo.

UVUNJIFU WA KATIBA YA TFF
Mpango huu wa kuondoa majina ya wagombea ulirasimiwa rasmi kwa nguvu ya kubadili katiba kwa njia ya waraka ukilenga kuunda chombo dhalili chenye mlengo wa kusaidia wagombea Fulani washinde uchaguzi.
Hivi sasa kuna njama zinafanyika ili uchaguzi usifanyike /Uharibike ili walioko madarakani waeendelee kuwapo nina kila sababu ya kuamini hiyo kwa sababu zifiatazo;
  1. Katiba iliyotumika kuitisha uchaguzi huu ni batili kwa kuwa mabadiliko ya katiba hayakufuata utaratibu wa Kikatiba Kwani hakuna mkutano Mkuu wowote wa TFF uliokaa kupitisha mabadiliko hayo. TFF imempotosha  Msajili wa vyama kupitia Ibara ya 76 ya katiba ya TFF  ya kuwa Mkutano Mkuu wa TFF ulikutana Tarehe 15th December 2012 kufanya mabadiliko hayo huku ikijua sio kweli, nina penda kuitahadhalisha TFF hili sio swala michezo ni swala la Kisheria, hivyo kwa mujibu wa sheria za nchi mwenye mamlaka ya kutafsiri sheria(Katiba) ni mahakama  hivo ni Ushauri wangu kwa TFF ili kuondoa uwezekano wa mkono wa sheria kuingia yafanyike yafuatayo,
i)             kusimamisha Matumizi ya Katiba hiyo mara moja kwani sio halali ili kuondoa uwezekano wa kutafutwa haki kwenye Mahakama za Kiraia.
ii)           Kuyafuta maamuzi yote na kuivunja   Kamati ya Rufani ya Uchaguzi inayoongozwa na Nd Mtinginjola, na ili matakwa ya kikatiba ya Uchaguzi yatimie rufani zote zirudishwe kwenye Kamati ya Rufaa kama katiba halali inavyotaka ili kukamilisha Mchakato  wa uchaguzi.
iii)          Maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya Uchaguzi chini ya Lyatto yaheshimiwe na kama kuna wasio ridhika wakate rufaa kwa Kamati ya Rufaa ya TFF.pamoja na kuwa maamuzi wa Lyatto hyana faida ya moja kwa moja na mimi lakini utaweka misingi bora ya kikatiba.
  1. Kwa mujibu wa katiba mpya ambayo mie naaita sio halali ibara ya 76 katiba hiyo imeeanza kutumika tarehe 15/12/2012  na Kanuni za Uchaguzi zimeanza kutumika tarehe 7/jan/2013 kanuni hizi na katiba yake ndio zilizotumika kuitisha uchaguzi huu.
Baada ya kupitisha katiba na kuanza kutumika TFF ilipaswa kuunda Kamati Mpya ya uchaguzi, Kwa mujibu wa Katiba ya TFF ibara 49(4) Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi anapashwa kuwa na taaluma ya Sheria(mwanasheria) sifa ambayo mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Bw Deogratius Lyatto hana sifa hiyo na hivyo ushiriki wake kuwa kinyume cha katiba ya TFF, kwa maana hiyo kuufanya mchakato wote wa uchaguzi kuwa batili na unapaswa kufutwa na kuteua kamati mpya ili mchakato uanze upya hivyo kuchelewesha kupatikana kwa viongozi wapya wa TFF.
  1. Kanuni hutengenezwa ili kuwezesha utekelezaji wa Katiba husika. Hivyo katiba hupitishwa na kusajiliwa kwanza na baadae hutungwa kanuni, cha kushangaza Kanuni za uchaguzi za  tff zilipitishwa na kusainiwa Tarehe 7/jan/2013 wakati katiba TFF  ilisajiliwa na kugongwa mhuri wa msajili Tarehe 10/jan/2013 siku tatu (3) baada ya kanuni kusainiwa. Swali linakuja kanuni hizi zilitungwa kwa mujibu wa katiba gani? Kwa maana hiyo kanuni za uchaguzi ni batili na katiba ni batili kisheria. Ninaishauri TFF ili kuondoa uwezekano wa kuingiza tff kwenye mgogoro wa kisheria uamuzi wa busara wa kuachana na Katiba batili  ni muhimu kwa maendeleo ya soka la Tanzania kwa kusimamisha matumizi ya katiba mpya batili ya TFF na matokeo ya maamuzi yote yanayotokana na katiba hiyo.

………………………………….
MICHAEL RICHARD WAMBURA
February 14, 2013

TOA MAONI YAKO JUU YA HIZI PICHA MBILI TOFAUTI!


Thursday, February 14, 2013

KOCHA WA COASTAL UNION: TUKIFUNGWA NA OLJORO A RUVU NAACHA KAZI


KOCHA wa Coastal Union, Hemed Morocco ameweka wazi kuwa endapo anafungwa mechi mbili zijazo dhidi ya Oljoro JKT na Ruvu Shootiga atabwaga manyanga.
Morocco alisema hayo baada ya timu hiyo kupata pointi moja Kanda ya Ziwa, kwa kutoka suluhu na vibonge Toto African na kufungwa bao 1-0 na Kagera Sugar.
Alisema yeye pamoja na kocha msaidizi Ally Kidi wamejitahidi kadri ya uwezo wao kuhakikisha timu inafanya vizuri lakini baadhi ya wachezaji hawana nia njema na klabu hiyo.
"Inavyoonekana kuna wachezaji hawana nia nzuri na timu yao. Kwa sababu hawataki kubadilika."
"Kwa hiyo siwezi kufanya kazi kwenye mazingira hayo hata siku moja. Kama tatizo ni mimi waniambie."
Kocha huyo alisema; "Kama timu itashindwa kufanya vizuri mechi mbili zijazo nafikiri sitatangaza kujiuzulu."
Coastal Union imecheza mechi nne za mzunguko wa pili wa ligi na kutoka sare mbili dhidi ya Prisons na Toto African. Imeshinda dhidi ya Mgambo JKT na kupoteza na Kagera Sugar. 

"SIDHANI KAMA TUTABAKI LIGI KUU" - KOCHA WA AFRICAN LYON


ALIYEKUWA kocha wa Zanzibar Heroes Salum Bausi ameweka wazi kuwa itakuwa miujiza kwake kuibakisha African Lyon  Ligi Kuu msimu ujao.
Kocha huyo aliyeiwezesha Heroes kushinda nafasi ya tatu kwenye michuano ya Chalenji iliyofanyika jijini Kampala Uganda mwaka jana na kujinyakulia kitika cha dola 10,000.
Alisema kwa jinsi alivyoiona Lyon ikicheza mechi mbili za ligi dhidi ya Prisons na Yanga ni kazi pevu kwake kuibakisha.
"Timu haieleweki. Haina misingi ya kiuchezaji. Kila mtu anacheza anavyojisikia." alisema Bausi
Bausi alisema alitua kukinoa kikosi hicho siku tisa zilizopita na kuambiwa timu hiyo ilikuwa ikifundishwa na kocha Pablo Veles wa Argentina.
"Nafikiri ndiye anayestahili kubeba lawama hizi. Timu haina stamina wala pumzi. Wachezaji wanaanguka hovyo."
Kocha huyo alisema kwa sasa ni vigumu kuanza kuijenga timu wakati ligi ndiyo inaishia ukingoni.
"Hakuna timu inayokubali kufungwa kwa sasa. Nafikiri kama itakuwa haitafuti nafasi yakukimbia kushuka daraja basi kutwaa ubingwa."
Alisisitiza kuwa kazi ambayo ipo mbele yake ni mzito na kuomba ushirikiano kutoka kwa viongozi, wachezaji na mashabiki.

"SIMON MSUVA NI HATARI - NDIO NGASSA MPYA WA YANGA"

BEKI wa Prisons ya Mbeya, Henri Mwalugala amekiri kuwa winga Simon Msuva ni msumbufu na kukiri alimweka kwenye wakati mgumu wakati timu yake ilipocheza na Yanga.

Mwalugala anayemudu nafasi ya beki wa kushoto alisema "Nafikiri Msuva kwa sasa amekaa vizuri."
"Nafikiri ukiwatizama Yanga kwa sasa wanamtumia sana winga huyo kujenga mashambulizi yao kupitia pembeni.
"Naamini Yanga imemrejesha Mrisho Ngassa mwingine."
Beki huyo alisema kwa mtazamo wake haoni kama Yanga ina sababu yakumsajili Mrisho Ngassa wa Simba wakati Msuva yupo.
Mwalugala akielezea jinsi timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam amekiri kuwa alishindwa kumzui.
"Kocha alivyoona dogo ananisumbua alinibadilisha kucheza kulia badala ya kushoto."
Alisema badiliko hilo lilikuwa na lengo la  Aziz Sibo aliyekuwa anacheza kulia kwenda kushoto kumkaba Msuva asiGlete madhara. Yanga ilishinda mabao 3-1.

TAIFA STARS WANUNULIWA BASI LA MILLIONI 200 NA KILIMANJARO

Hatimaye basi la Timu ya Taifa, Taifa Stars lililokuwa likisubiriwa kwa hamu sasa limewasili na liko tayari kukabidhiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager kwa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) ili Taifa Stars iweze kulitumia.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, inayodhamini Taifa Stars, George Kavishe alisema hii ni katika malengo yao ya kuinua hadhi ya timu ya Taifa ambayo kwa sasa imeonesha kiwango cha hali ya juu.

“Wakati tukichukua udhamini wa timu ya Taifa moja ya malengo yetu ilikuwa ni kuinua hadhi ya timu hii na mojawapo ya vitu tulivyoahidi ni kuinunulia basi la hadhi,” alisema Bw Kavishe.

Alisema basi hilo aina ya Yutong lenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 200, ni kubwa na la kisasa kabisa lenye uwezo wa kubeba abiria 50 pamoja na dereva na kuwa lina nafasi kubwa kutoka kiti kimoja hadi kingine hivi kuwafanya wachezaji wakae kwa raha zaidi wanaposafiri.

“Basi hili ni athletic coach na ni jipya kabisa, limetengenezwa mahususi kwa wanamichezo kwani lina nafasi kubwa chini ya kubeba vifaa vya michezo na mizigo mingine yeye uzito wa hadi tani tatu,” alisema Bw. Kavishe.

Aliendelea kusema kuwa basi hilo ni imara kwani chasis yake ni 4x2, injini yake ni aina ya  300 HP Cummins, ina retarder ya umeme na breki aina ya ABS, TV mbili za kisasa, muziki wa nguvu wenye spika nane, milango na mabuti ya kisasa, friji mbili na kiyoyozi cha nguvu.

Kwa mujibu wa Bw. Kavishe basi hili linatarajiwa kukabidhiwa kwa Taifa Stars Februari 21 katika hafla itakayofanyika katika makao makuu ya TBL Ilala Jijini Dar es Salaam na itahudhuriwa na wadau mbalimbali wa soka nchini na wageni wengine.

Baada ya kukabidhiwa kwa Taifa Stars basi hilo linatarajiwa kuzunguka katika mitaa mbalimbali ya JIji la Dar es Salaam ili wananchi walione na wapige nalo picha za kumbukumbu.

“Hii ni zawadi ya watanzania kwa timu ya Taifa kwani ndio wanatuwezesha kufanya mambo yote haya…kadri wanavyozidi kutuunga mkono kwa kunywa bia yetu ya Kilimanjaro Premium Lager ndivyo na sisi tunapata fedha za kuidhamini timu yetu ya Taifa,” alisema.

Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ilianza kuidhamini Timu ya Taifa tangu  mwezi Mei mwaka jana kwa kuwekeza zaidi ya bilioni mbili kwa mwaka kwenye timu hii kwa muda wa miaka mitano.

Moja ya masuala ambayo yamo kwenye mkataba kati ya TBL na TFF ni ununuzi wa basi mpya ya Taifa Stars jambo ambalo TBL imefanikisha ndani ya mwaka mmoja wa udhamini wake.

Mpaka sasa TFF imeonyesha kuridhishwa na udhamini mnono wa Kilimanjaro Premium Lager kwani shirikisho hilo lina uwezo wa kufanya mipango ya muda mrefu zaidi kwa uhakika.

Udhamini wa Kilimanajro Premium Lager ndio mkubwa kabisa ambao TFF imewahi kupokea kutoka kwa kampuni au shirika lolote nchini kudhamini mpira.

Wednesday, February 13, 2013

JERRY TEGETE IS ON FIRE APIGA 2 - YANGA IKIZIDI KUJIKITA KILELENI - YAIPIGA AFRICAN LYON 4-0, COAST YARAMBISHWA SUKARI NA KAGERA SUGAR

KLABU ya soka ya Yanga imeendeleza mauaji katika Ligi Kuu ya Bara baada ya leo kuitandika African Lyon mabao 4-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Kwa ushindi huo, Yanga imefikisha pointi 36 na kuzidi kujikita kileleni mwa ligi hiyo, wakati Lyon nayo imezidi kudidimia mkiani mwa ligi hiyo.
 
Straika Jerry Tegete ndiye aliyekuwa kinara wa mchezo huo baada ya kufunga mabao mawili katika mchezo huo licha ya kukosa kadhaa katika kipindi cha kwanza.
 
Tegete alifunga bao la kwanza dakika ya 21 kwa kichwa akiunganisha krosi safi ya beki wa kushoto David Luhende aliyepanda kuongeza nguvu ya mashambulizi.
 
Baada ya bao hilo, Lyon walizinduka na kulishambulia kwa kasi lango la Yanga lakini washambuliaji wake wakiongozwa na Ike Bright hawakuweza kuleta madhara Zaidi katika lango la Yanga.
 
Dakika ya 42, Tegete aliifungia Yanga bao la pili kwa kisigino mpira aliopigiwa na winga Simon Msuva ambaye aliisumbua vilivyo ngome ya Lyon iliyokuwa ikiongozwa na Obinna Salamusasa. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.
 
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikijaribu kushambulia lango la mwenzake lakini walikuwa ni Yanga waliofanikiwa kupata penalti dakika ya 46 baada ya beki wa Lyon kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari. Hamis Kiiza alipiga penalti hiyo lakini kipa wa Lyon, Abdul Seif aliidaka.
 
Baada ya penalty hiyo, Yanga ilizidisha mashambulizi huku ikiwa imetawala kiungo na kufanikiwa kupata penalti nyingine dakika ya 69. Penalti hiyo ilikuja baada ya beki Salamusasa kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari. Straika Didier Kavumbagu alipiga penalti hiyo kuiandikia Yanga bao la tatu dakika ya 69.
 
Kocha wa Yanga, Ernie Brandts alifanya mabadiliko kwa kumtoa Kiiza na kumuingiza kiungo Nizar Khalfan ambaye dakika ya 80 aliifungia Yanga bao la nne kwa shuti kali.
 
Nizar alifunga bao hilo akiunganisha krosi safi ya Said Bahanuzi kutoka wingi ya kushoto.
 
Dakika ya 90, mwamuzi Martin Saanya alimuonyesha kadi nyekundu beki Yusuf Mlipili wa Lyon baada ya kumchezea vibaya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima.
Hadi mwisho wa mchezo, Yanga 4-0 Lyon.
 
Katika michezo mingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, JKT Mgambo imeifunga Oljoro JKT mabao 2-0, Kagera Sugar imeifunga Coastal Union bao 1-0, Toto African imetoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Polisi Moro na Mtibwa Sugar imetoka suluhu na Ruvu Shooting.

LIVE MATCH CENTRE: YANGA 4 - 0 AFRICAN LYON


Dk 90+3 FULL TIME! Yanga 4-0 Lyon

Dk 90 RED CARD..! Yusuf Mlipili wa Lyon anaonyeshwa kadi ya njano kisha nyekundu baada ya kumchezea rafu Haruna Niyonzima. Yanga 4-0 Lyon

DK ya 89 Yanga wanazidi kuliandama lango la Lyon.


Dakika ya 80, Nizar Khalfani anaipatia Young Africans bao la nne - African Lyon 0 - 4 Young Africans

Dk 78 Yanga inafanya mabadiliko, anatoka Hamis Kiiza anaingia Said Bahanuz.

Dk 75 Lyon wanaonekana wamepoteana katikati, Yanga imetawala kiungo.

Dk 69 Yanga inafanya mabadiliko, anatoka Simon Msuva anaingia Nizar Khalfan.

Dk 69 Goooo...! Kavumbagu anaipatia Yanga bao la tatu kwa penalti. Yanga 3-0 Lyon

Dk 67 Penaltii...! Yanga inapata penalti baada ya beki wa Lyon kuunawa mpira.

Dk 47 Hamis Kiiza wa Yanga anapiga penalti lakini anakosa.

Dk 46 Penaltii...! Yanga inapata penalti baada ya beki wa Lyon kuunawa mpira.

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA

Dk 42 Goooo...! Tegete anaipatia Yanga bao la pili kwa kisigino akimalizia pasi ya Simon Msuva. Yanga 2-0 Lyon

Dk 21 Goooo...! Jerry Tegete anaipatia Yanga bao la kwanza kwa kichwa akiunga krosi ya David Luhende. Yanga 1-0 Lyon

Dk 12 African Lyon inafanya mabadiliko, anatoka Idd Mbaga anaingia Yussuf Mgwao.

Mpira umeanza hapa uwanja wa Taifa kati ya African Lyon Vs Young Africans


Young Africans line-up to face African Lyon today:
1.Ally Mustafa
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nadir Haroub
5.Kelvin Yondani
6.Athuman Idd
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Jerson Tegete
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Said Mohamed
2.Shadrack Nsajigwa
3.Stephano Mwasika
4.Nurdin Bakari
5.Nizar Khalfani
6.Said Bahanuzi
7.Didier Kavumbagu

SAMUEL ETO'O: SIKUJA TANZANIA NILIOGOPA KUPOTEZA MAISHA YANGU



MASHABIKI wa soka nchini walitoka mikoani kuja Dar es Salaam ili kumwona nyota wa Cameroon, Samuel Eto'o timu yake ilipocheza mechi ya kirafiki na Taifa Stars Uwanja wa Taifa, Jumatano iliyopita.

Lakini hakuja na timu yake ikalala bao 1-0. Benchi la ufundi la Cameroon likadanganya Watanzania kwamba straika huyo alikuwa majeruhi. Kumbe ni uongo.


Sasa yeye mwenyewe ameibuka na kutamka kuwa aligoma kuja nchini kutokana na kuhofia kuuawa.


Nahodha huyo ameibua mjadala mzito baada ya kuwatuhumu maofisa wa Shirikisho la Soka la Cameroon (FECAFOOT) kwa kutaka kumuua.


Sambamba na kauli hiyo, Eto'o, amesema kwamba yuko tayari kwa mjadala wa suala hilo ambao utarushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa.


 Wanataka kuniua, katika timu ya taifa naishi na mashushushu, si kwamba siko makini katika hilo kwani hata jezi ya timu ya taifa navaa yangu binafsi niliyotengenezewa na Puma, alisema mchezaji huyo kupitia Jarida la Je Wanda.


Etoo ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi pia alisema kwamba hata anapokuwa mazoezini wakati wote yuko makini na maisha yake.


Etoo ni miongoni mwa wachezaji 11 wa Cameroon ambao hawakuitikia wito wa kuichezea timu hiyo mechi ya kirafiki dhidi ya Tanzania iliyopigwa Jumatano iliyopita na Cameroon kulala bao 1-0 lililofungwa na Mbwana Samatta.


Hawa wazee wametafuna fedha zetu kiasi cha kutosha, badala ya kusimamia soka kwa ajili ya umma wako katika mipango ya uongo, kusafiri daraja la kwanza kwenye ndege na kunufaisha akaunti zao za siri katika mabenki ya Ulaya, alisema.


Cameroon itaumana na Togo mwezi ujao katika mechi ya awali ya fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014 na Etoo anadhani timu hiyo haina uwezo wa kuifunga Togo.


FECAFOOT haijasema lolote kuhusu hoja hizo za Etoo ingawa mmoja wa maofisa wa shirikisho hilo anadaiwa kumwambia Etoo kuwa amekosa uzalendo na hoja zake ni kichekesho.


Kocha wa Cameroon, Jean Paul Akono, alisema jijini Dar es Salaam kwamba anataka kupunguza wachezaji wenye umri na majina makubwa kwenye kikosi hicho na kutengeneza kizazi kipya kitakachorejesha heshima ya Taifa hilo kisoka.


SOURCE: MWANASPOTI 

HIVI NDIVYO SIMBA INAVYOJIFUA ARUSHA TAYARI KUWAUMIZA WAANGOLA JUMAPILI



Julio akiongoza mazoezi

Mrisho Ngassa na Salim Kinje

SIMBA WAANZISHA MAHUSIANO NA SUNDERLAND YA ENGLAND

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya Simba, Rahma Al Kharusi akiwa na Mwenyekiti wa Sunderland ya England, Ellis Short baada ya kukutana jana kwenye hoteli ya Hayat jijini Dar es Salaam.

Baada ya kukutana, wawili hao walijadili kuhusiana na klabu hizo mbili kuanzisha uhusiano wa kibiashara pamoja na mafunzo na Simba imepata mwaliko.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Short alisema ushawishi wa Malkia wa Nyuki umechangia yeye kutoa mwaliko huo na anaamini timu zote zitafaidika.
"Mazungumzo yetu na Rahma yalikuwa mazuri sana, nimefarijika na ninaamini mwaliko niliotoa utakuwa mwanzo wa uhusiano mzuri kwa kuwa mwanamama huyu amenishawishi," alisema.
Malikia wa Nyuki ataiongoza Simba nchini England mwezi Machi ambako watatembelea viwanja vya Sunderland ikiwa ni pamoja na kujifunza uendeshaji wa klabu.
Awali Simba, ilijulikana kwa jina la Sunderland.

HATMA YA SOKA LA BONGO,BAADA YA MVURUGANO WA MAAMUZI YA KAMATI YA UCHAGUZI YA KUWAENGUA BAADHI YA WAGOMBEA.

-->

Huu ni mwaka 2013,ukirudi nyuma kwa miezi minne yaani mwezi wa 11 mwaka 2012,yalifanyika mashindano ya Soka kwa Timu za Taifa kutoka Ukanda wa Africa Mashariki na Kati,maarufu kama Challenge.
Mmoja wa washiriki wa michuano hiyo iliyomalizika kwa wenyeji Uganda kuitwaa,ni Timu ya Taifa ya Tanzania Bara,ambao walitolewa katika hatua ya nusu fainali na ndugu zao Tanzania Visiwani.
Kitendo cha Timu Zote mbili yaani Tanzania Bara na Visiwani kufika nusu fainali,kilikuwa furaha tosha kwa Watanzania wote kwa ujumla katika kipindi cha mashindano hayo.
Pia,Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars,hivi karibuni imecheza mechi tatu za kirafiki,ambapo mchezo wa kwanza imeshinda bao 1-0 dhidi Zambia,mechi ya pili ilipoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Ethiopia wakati wiki mbili zilizopita imeshinda goli moja kwa bila dhidi ya Mabingwa wazamani wa Africa Cameroon.
Matokeo ya mechi hizi ukijumuisha na hatua zilipofikia timu za Taifa za Tanzania Bara na Visiwani,yamekuwa tumaini jipya la kufufuka kwa soka la Tanzania na hatimaye kufanya vyema katika michezo tofauti ikiwemo ya kufuzu Mataifa ya Africa.
Wakati Watanzania wakiunganisha Sara zao kuliombea Soka la nyumbani,Kamati ya uchaguzi na kamati ya Rufani ya uchaguzi mkuu wa TFF na Bodi ya Ligi wameibuka na jambo jipya lakukatisha tamaa juu ya mafanikio ya Soka la Bongo.
Kamati hizo  zimetumia sababu dhaifu,kuwaengua baadhi ya wagombea wa nafasi tofauti katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Mwezi Feb 22 na 24,akiwemo mgombea wa nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo la Soka Nchini Jamal Malinzi,kwa kukataa kusaini katiba ya mabadiliko ya leseni ya Ligi na kutokuwa na uzoefu wa uongozi  kwa miaka 5
Maamuzi haya yanaonesha wazi nia ya kuwabeba baadhi ya wagombea kwa kuwatengenezea mazingira ya kushinda uchaguzi bila kupingwa,hii ni aibu kwa wadau husika hasa katika wakati huu ambapo kila mtu anafahamu kinachoendelea kutokana na kuwepo kwa uwazi na ukweli.
Aidha Maamuzi haya yanalenga kurudisha nyuma maendeleo ya Soka la Bongo,kwa kuwa baadhi ya wagombea walioenguliwa,pengine walikuwa na mipango thabiti ya kuliinua Soka hili na kulifikisha mbali zaidi ya hapa.
Katika kuonesha kuwa kitendo hiki si haki na sio cha kiungwana,Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Amos Makala,ametoa tamko kali la kuitaka kamati ya Uchaguzi ya TFF kusimamisha  shughuli za uchaguzi huo adi suala hilo litakapopatiwa ufumbuzi,ikiwa pamoja na kuwarudisha wagombea walioenguliwa kimakosa.
Kama ninafikiria vyema,basi ninaamini kuwa maamuzi ya kamati hii yaliyomshangaza kila mpenda Soka na kuwavunja moyo waliokuwa njiani kupenda Soka,ni msukumo kutoka kwa baadhi ya wagombea wanaotaka madaraka kwa hali na mali.
Hii ni hali ya hatari kwa hatma ya Soka la bongo ambalo lilianza kuchanua,kwa kuwa uzoefu unaonesha kuwa mtu anayetumia nguvu ya ziada kupata uongozi,huwa hayupo kwa maslahi ya Taifa isipokuwa maslahi yake binfasi kama ilivyo kwa baadhi ya Viongozi wa Siasa Nchini na nchi za jirani.
Mimi binafsi ninaamini wakati muafaka na sahihi kwa Watanzania kukemea mambo haya yaliyopitwa na wakati ni sasa,na sio baada ya maamuzi na mbinu za ya kurudisha nyuma Soka kufanikiwa.
Sote tunafahamu kuwa Mpira wa Miguu ni Mchezo unaoongoza kwa kupendwa Duniani kote,na pia ni mchezo unaotoa ajira nyingi kwa Vijana wenye kipaji cha Mchezo huo kiasi cha wachezaji wengine kuingia kwenye orodha ya watu matajiri.
Kutokana na hilo,Wadau wote wa Soka na Michezo kwa ujumla nchini,tuungane kuhakikisha jitahada za kukuza Soka la Bongo lenye vijana wenye ndoto za kufanikiwa kitaifa na kimataifa na hatimaye kuitangaza Nchi zinafanikiwa kwa kuwa na uzalendo.
========
========

JAMAL MALINZI AZUNGUMZIA KUONDOLEWA KWAKE KATIKA KUGOMBEA URAISI WA TFF



Ndugu zangu,kupitia vyombo vyenu vya habari ninaomba niueleze umma wa watanzania,hususani wadau wa mpira wa miguu,yafuatayo kuhusu kuenguliwa kwangu.
Awali ya yote nieleze kusikitishwa kwangu na maamuzi yaliyotolewa na kamati ya rufaa ya TFF ya kuniengua kugombea urais wa TFF.Sikubaliani na maamuzi haya .
Katika kuniengua kamati ya rufaa ya uchaguzi ya TFF imetoa sababu mbili (nanukuu magazeti ya jana tarehe 12/02/2013 maana hadi leo sijakabidhiwa barua ya kuenguliwa).

1.  Kukosa uadilifu kwa kupinga waraka  uliotolewa na TFF wa kubadili Katiba ya TFF mwezi Desemba 2012.

2. Kukosa uzoefu wa miaka mitano ya uongozi.
Ndugu zangu,kiini cha maamuzi ya Kamati ya rufaa dhidi yangu ni pingamizi lililowekwa na mtu mmoja anayeitwa AGAPE FUE.Bwana Agape Fue aliniwekea pingamizi katika kamati ya uchaguzi  akidai mimi nilipinga waraka wa kubadili katiba ya TFF na pia sina uzoefu wa miaka mitano ya uongozi wa mpira.Kinyume na matakwa ya kamati ya uchaguzi kama yalivyotangazwa kuwa mtoa pingamizi aje mwenyewe kutetea pingamizi lake ,Bwana Agape Fue hakutokea mbele ya Kamati ya Bwana Lyatto.Matokeo yake tarehe  31/01/2012 kamati ya uchaguzi  ya TFF ilitoa maamuzi ya ya kutupilia mbali pingamizi hili.
Bwana  Agape Fue hakuishia hapo  kwa mara nyingine tarehe 06/02/2013 alikata rufaa kwenye kamati ya rufaa ya uchaguzi akidai kamati ya uchaguzi haikumtendea haki. Rufaa hii haikuwa na anwani wala namba ya simu  ya Bw.Agape Fue.Rufaa ilisikilizwa tarehe 10/02/2013 na maamuzi ya kukata jina langu yakatangazwa jioni ya tarehe 11/02/2013.
Mpaka leo najiuliza hivi huyu Bw. Agape Fue ni mwanaume au  ni mwanamke?(hakueleza kama ni Bwana au Bibi Agape Fue). Agape Fue ni nani hasa? Anaishi wapi?Je ni Mtanzania au sio Mtanzania maana kikanuni  wasio watanzania hawaruhusiwi kujihusisha na uchaguzi wa TFF (rejea kifungu cha 9 cha kanuni za uchaguzi),pingamizi lake halikuambatana na udhibitisha wa uraia. Kwa nini alichukua maamuzi haya? Sipati jibu.  Iweje  mtu achukue maamuzi mazito ya kumkatia mtu rufaa kisha uishie kusaini karatasi na kuwaachia wengine wakusemee na usije hata kushuhudia kinachoendelea kama kweli una maslahi na madai yako? Waandishi wa habari mnisaidie kupata majibu.

Ndugu zangu ,mtoa pingamizi alidai haikuwa sahihi kupinga azimio la kubadili katiba ya TFF kwa njia ya waraka.Naomba nisistize mambo matatu:

Wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF wanawakilisha matakwa ya vyama vilivyowatuma kwenda  kwenye  mkutano  mkuu wa TFF,na ndio maana chama cha mpira cha mkoa wa Kagera (KRFA) kiliitisha kikao cha kamati ya utendaji  ili kamati iweze kutoa mwongozo  kwa wajumbe wake kuhusu nini kifanyike kuhusu waraka ulioletwa na TFF,hivyo maamuzi yaliyotolewa ya kuukataa waraka huu yalikuwa ni maamuzi ya chama cha mpira mkoa wa Kagera na wala hayakuwa ni maamuzi ya Jamal Malinzi,iweje malinzi niadhibiwe kwa maamuzi haya,kwa nini usiadhibiwe mkoa mzima na mikoa yote iliyopinga waraka?hii ni haki kweli? Siamini kama kuna mjumbe wa mkutano mkuu aliyekiuka maamuzi ya kamati yake ya utendaji.

2.  Katika mchakato wa kubadili katiba kwa njia ya waraka kilichokuwa kinagomba sio maudhui (content) ya mabadiliko ya Katiba bali utaratibu uliotumika kubadili Katiba. Swali la msingi tulilojiuliza wajumbe wa kamati ya utendaji KRFA  ni kwamba je kwa mujibu wa Katiba ya TFF kifungu 22 na kifungu 30 wapi katiba inatamka kuwa inaweza kubadilishwa kwa njia ya waraka? Mpaka leo hilo jibu hakuna,labda aliyeniwekea pingamizi atusaidie kupata jibu la swali hili. Katiba ya TFF iko wazi kabisa inatamka  kuwa Katiba itabadilishwa kwa njia ya Mkutano Mkuu tu (General Assembly).

3. Ni kweli FIFA iliagiza yafanyike mabadiliko ya Katiba ya kuingiza kipendele cha ‘club licencing’ katika Katiba ,lakini je FIFA katika agizo hilo ilisema Katiba ya TFF ivunjwe ili kutimiza azma hiyo? Ikumbukwe kuwa mwaka 2004 FIFA iliagiza TFF iingize kwenye Katiba kipengele cha Katibu Mkuu awe wa kuajiriwa badala ya kuchaguliwa,agizo hili lilitekelezwa kwa kupitishwa na Mktano Mkuu wa TFF,iweje leo utaratibu huu ukiukwe? Hata majuzi CAF walipotaka kubadili katiba ili Rais wa CAF atokane na wajumbe wa Kamati ya Utendaji jambo hili lilitekelezwa kwa kuitisha mkutano mkuu wa dharura  uliofanyika Seychelles majuzi. Katiba ndio msingi mkuu wa uendeshajiwa TFF,nitaipigania siku zote.Huo ndio utaratibu,si CAF si FIFA si Vyama vya mpira vya nchi,hakuna anayebadili  Katiba kwa njia ya waraka,kama kuna mwenye ushahidi aulete.

Kuengua jina langu eti kwa kuwa nilipinga waraka wa kubadili Katiba sio uamuzi sahihi.

Kuhusu uzoefu wa miaka mitano katika Uongozi:
Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi mkuu wa TFF mwaka 2008 niligombea na jina langu lilikatwa na kamati  ya uchaguzi ya TFF.Nilikata rufaa katika Kamati ya Rufaa ya TFF na kushinda . Hukumu hii ni halali hadi leo.Iweje leo hii miaka minne baadae Kamati hiyo hiyo ya rufaa (kubadili majina ya wajumbe sio kubadili taasisi) inione sina uzoefu?.Si hilo tu ,hata katika kujaza fomu namba moja ya kugombea niliambatanisha vielelezo vyote vya uzoefu wangu ikiwa ni pamoja na kudhibitisha kuwa katika kipindi cha miaka mine iliyopita  nimekuwa:
-Mjumbe wa Baraza la michezo mkoa wa Dar es salaam.
-Mwenyekiti wa kamati ya mashindano chama cha mpira mkoa wa Pwani COREFA.
-Mjumbe wa mkutano mkuu wa mkoa wa Kagera
-Mwenyekiti wa chama cha mpira mkoa wa Kagera
Hii ni pamoja na kuongoza Yanga 2002-2005.
Hivi katika nafasi hizi za uongozi ipi ni ya kuongoza ‘bonanza’? Nimedhalilishwa sana.


HITIMISHO
Vyombo vya habari kupitia makala,tahariri na maoni ya wasikilizaji/wasomaji/watazamaji vimesifia sana awamu mbili za uongozi wa Bwana Leodeger Tenga.Bwana Tenga amesifiwa kwa umahiri wake wa kuleta utulivu katika sekta ya mpira wa miguu Tanzania.Amesifiwa kwa kujenga taasisi imara ambayo mhimili wake mkuu ni sekretarieti makini na kamati mbali mbali zilizo imara .Let him rise to the occasion,muda wa kuonyesha uongozi imara ni huu,historia itamhukumu kwa jinsi gani atasimamia suala hili,haki sio lazima itendeke lakini pia inatakiwa ionekane inatendeka.
Kamati ya utendaji ya TFF inayo mamlaka ya kubatilisha maamuzi haya kwa maslahi ya mpira wa Tanzania.Ninamshauri Rais wa TFF aitishe kikao cha dharura cha kamati ya utendaji ili kijadili hali hii na kunirudishia haki yangu ya kugombea urais wa TFF.
Nihitimishe kwa kuwaomba wadau wa mpira wa miguu Tanzania  wawe watulivu wakati tukisubiri kupata ufumbuzi wa suala hili.

Mungu ibariki Afrika,
Mungu ibariki Tanzania.
Ahsanteni sana,

Jamal Emil Malinzi
Dar es salaam
13/02/2013