Search This Blog

Saturday, August 13, 2011

MATOKEO YA MICHEZO MBALI MBALI

England: Premier League
Finished Blackburn 1 - 2 Wolverhampton
Finished Fulham 0 - 0 Aston Villa
Finished Liverpool 1 - 1 Sunderland
Finished Queens Park Rangers 0 - 4 Bolton
Postponed Tottenham - Everton
Finished Wigan 1 - 1 Norwich

Germany: 1. Bundesliga


Finished Freiburg 1 - 2 Mainz 05
Finished Hamburger SV 2 - 2 Hertha Berlin
Finished Hoffenheim 1 - 0 Borussia Dortmund
Finished Nurnberg 1 - 2 Hannover 96
Finished Wolfsburg 0 - 1 Bayern Munich
Finished Schalke 04 5 - 1 FC Cologne

Scotland: Premier League


Finished Inverness 0 - 2 Rangers
Finished Celtic 5 - 1 Dundee U.
Finished Hearts 3 - 0 Aberdeen
Finished St. Mirren 0 - 1 Motherwell
Finished St.Johnstone 0 - 1 Dunfermline

International: CAF Champions League grp. B


Finished Al Ahly 2 - 0 MC Alger

International: Club Friendlies


Finished Huelva 1 - 2 Atletico Madrid
Finished Valencia 3 - 0 Roma

Preview ya England Premier League: Newcastle vs Arsenal

Ligi ya England hatimaye imeanza na leo mechi kubwa itakuwa baina ya Newcastle United watakaokuwa wenyeji wa Arsenal kwenye uwanja wa St James Park .

Mara ya mwisho mechi hii ilimalizika kwa mabao nane kwenye sare ya 4-4 huku Newcastle wakishinda mchezo wa awali 1-0 . Kama kuna chochote kitakachojirudia kwenye mchezo wa leo basi hakika mchezo huu utakuwa mkali na wa kutegemewa kwa mengi.

Arsenal wamekuwa na bahati mbaya ya kuwa na majeruhi kwenye timu yao, hasa kwenye michezo ya pre-season ambapo Jack Wilshere,Theo Walcott, na Kieran Gibbs waliumia vibaya japo si vibaya sana lakini watakosa mchezo dhidi ya Newcastle ila Thomas Vermalen na Robin Van Persie watakuwa fiti kuanza .

Kitu ambacho kinakuja kama habari mbaya kwa Arsenal ni kukosekana kwa Samir Nasri na Cesc Fabregas ambao wako mbioni kuihama Arsenal .

Unaweza kushangazwa na jinsi kukosekana kwa watu hawa kunavyochukuliwa kuwa habari mbaya . Fabregas alitarajiwa kuondoka hilo halina ubishi ,

tatizo linakuja kwa kukosekana kwa wale waliokuwa wanatazamwa kama watu wanaokuja kuziba pengo lake , Samir Nasri na Jack Wilshere na hapo ndio unapoweza kuona shimo ambalo linaweza kuwagharimu Arsenal kwenye eneo la katikati ya kiwanja .

Ukiacha hayo kuna sababu ya furaha kwa wanaarsenal kwani nyota wao mpya Gervais Yao Kone atakuwepo na kila mmoja anajua uwezo wake . Akiwa sambamba na Robin Van persie ni dhahiri wataipa makali yanayohitajika safu ya ushambuliaji ya Arsenal .

Upande wa midfield Arsenal watalazimika kumtumia Aron Ramsay kama mbadala wa Jack Wilshere huku akisaidiwa na yoyote kati ya Abou Diaby na Alex Song huku Tomas Rosicky naye akiwemo kwenye orodha ya viungo walioko fiti kucheza . Wapo pia kina Andriy Arshavin , Riyo Miyachi na Alex Oxlade Chamberlain .

Golini atakuwepo Wojciech Szczesny huku akilindwa na Armand traore upande wa kushoto ambaye anakuja kuziba pengo la Kieran Gibbs aliyeumia , huku Bacary Sagna akiwa kwenye nafasi yake ya kawaida kwenye eneo la kulia kwenye safu ya ulinzi.

Mmojawapo kati ya Laureant Koscielny au Johan Djorou atakuwa pamoja na Thomas Vermalean kwenye moyo wa defence . Uwepo wa Thomas Vermalaen utaisaidia sana Arsenal ambayo imekuwa kwenye wakati mgumu kwenye eneo hilo hasa ukizingatia kuwa Newcastle itakuwa na watu wenye vimo virefu kwenye safu yao ya ushambuliaji Shola Ameobi na Demba Ba .

Swali gumu litakuwa nani atayecheza kama msaidizi wa Vermalen. Djorou alijitahidi sana msimu uliopita lakini Koscielny amecheza vizuri kwenye michezo ya Pre-seaon akionyesha uwezo mkubwa wa kuusoma mchezo na kukatiza pasi hatari za maadui na imani kubwa ya Arsene Wenger itakuwa kwake .

Kwa upande wa Newcastle , mchezo huu utakuwa mgumu kwao ukizingatia kuwa wameondokewa na wachezaji wengi muhimu waliokuwepo msimu uliopita . Newcastle ya sasa inawakosa kina Kevin Nolan , Andy Caroll na Jose Enrique ambaye hivi majuzi tu amemfuata Caroll Merseyside. Kuna utata juu ya uwepo wa Joey Barton ambaye pamoja na kuwa fiti na uwezo mkubwa aliounyesha msimu uliopita atakosekana kutokana na uhusiano mbovu alio nao na viongozi wa timu hususan mmiliki Mike Ashley na kocha Allan Pardew.

Bado Hatem Ben Arfa hajawa fiti kwa asilimia 100 na haya yote yanapunguza makali yalikuwepo Newcastle msimu uliopita kwa kiasi kikubwa sana . Ukiaachana na hayo bado Newcastle ni timu yenye uwezo wa kuiletea Arsenal matatizo . Demba Ba akishirikiana na Shola Ameobi ni watu wenye uwezo wa kufunga .

Kiungo kitakuwa chini ya Ismael Cheikh Tiote ambaye alifanya vizuri mno msimu uliopita . Atakuwepo pia kijana mpya toka Ufaransa Yoan Cabaye sambamba na wachezaji waliokuwepo msimu uliopita kama Jonas Guttierez na nahodha mpya Fabricio Coloccini.

Newcastle pia wana matatizo kwenye majeruhi ambapo watamkosa kipa Steven Harper na beki Noel Perch huku Dan Guthrie naye akikosekana.
Kama ilivyokuwa kwa michezo ya msimu uliopita , mchezo huu utakuwa mkali kwa kuwa timu zote zitautazama kama mchezo ambao matokeo yake yatakuwa mwelekeo wa msimu mzima .

Timu zinatarajiwa kuwa kama ifuatavyo.
NEWCASTLE UNITED

Krul
Simpson, Coloccini, S Taylor, R Taylor
Gutierrez, Barton, Cabaye, Tiote
Ameobi, Ba


ARSENAL

Szczesny
Sagna, Djourou, Vermaelen, Traore
Song, Ramsey, Rosicky
Gervinho, Walcott
Van Persie


Mrisho Ngassa Suits Up for Seattle Sounders FC versus Manchester United


August 13, 2011
Press Release from SEATTLE SOUNDERS FC

SEATTLE, Wash. -

In the 76th minute of the Sounders FC’s friendly with Manchester United last week, three players subbed into the match for Seattle.

Miguel Montano came on late in the match, a great opportunity for the 20-year-old Colombian to play against one of the top clubs in the world. O’Brian White made his first appearance since a blood clot was removed from his leg in April.

However, the third player may have been just as intriguing. Mrisho Ngassa came on and played the right wing, though his appearance was largely lost in the shuffle of a 7-0 loss taken by the Sounders.

Ngassa came to the Sounders on trial from Azam FC in his native Tanzania as the Sounders looked to expand the breadth of their scouting into the often unscoured countries in East Africa.. Kurt Schmid traveled to Tanzania last year to scout the National Team and watch them train. With his eye and the recommendation of National Team head coach Jan Poulsen, Ngassa was selected to trial with the Sounders.

“When you go to a place like Tanzania and see someone who stands out head and shoulders above the rest, you try and figure out why,” Schmid said.

That answer for Ngassa was quickness.

While he stands just 5-foot-5, he is able to use his speed and stealth to get in behind defenses and create opportunities. Even against Manchester United he was able to get a shot away in his limited action, missing high late in the match with Rio Ferdinand in close proximity.

“Ngassa is not the biggest guy, but we have experience with small guys doing good things in Seattle, so that didn’t really deter us. He’s incredibly quick. I think his quickness over small distances is phenomenal,” Schmid said. “Technically, he’s actually pretty good. He can dribble and shoot well. He reads the game well too. I think he needs to improve his defense a little bit, but he’s an attacking player and his awareness and technical ability in those arenas is very good.”

While the link to Tanzania could bear fruit for the Sounders at some point, the benefit won’t only come for the Seattle club. According to African Lyon owner and general manager Rahim Zamunda Kangezi, who accompanied Ngassa on the trip, opportunities with Seattle and other MLS clubs will only raise the profile of soccer in Tanzania and other East African countries the way France did for countries in West Africa.
“The talent is the same as West Africa, but in West Africa they have a connection with France. Adrian Hanauer is giving players in East Africa the opportunity to connect East Africa with the Sounders the same way,” Kangezi said. “When you talk about football in Africa, that is the dream of every young player. To see young players in the US would be great for the region.”

The Sounders agree that strengthening the bond between the club and representatives from Tanzania will only help the club build more relationships and could eventually bring the club some great talent from a region that the MLS hasn’t made much use of yet.

“It’s very untapped. There are guys coming out of the region in Belgium and Norway that have made their forays into different parts of the world,” Schmid said. “I think the region has potential and there are definitely players there, it just needs to be developed. With this relationship hopefully we can help develop those players.”

Ngassa already returned to Tanzania with the potential that he could rejoin the Sounders in training camp for the 2012 season.

The Seattle Sounders are also excited to be able to promote Tanzanian Tourism through the voice of soccer in the United States. Evidence of this was on full display throughout the game on the field boards and highlighted by a special half-time video of President Kikwete of Tanzania inviting all of Seattle to visit and invest in Tanzania.

Vice President of Seattle sounders Lance Lopez has said that he is impressed with President Jakaya Kikwete’s dedication to the sports sector in Tanzania. He said that he is looking forward to start up an academy here and assist in developing the local sports talent as well as providing quality education to deserving youth. Also opportunity for a minimum of two (2) players from Tanzania each year to receive an all expense paid trip to the Sounders training camp to compete for a roster spot on the Sounders team. And One (1) U-17 to have a two weeks trail with the Seattle Sounder Academy.
Picture taken during half time when the special clip was played.


President Jakaya Kikwete with Vice president of Seattle sounders Lance Lopez


Minister of tourism Ezekiel Maige with Vice president of Seattle sounders Lance Lopez




CEO of African Lyon FC Rahim Kangezi Zamunda with Vice president of Seattle sounders Lance Lopez during the Match




Special half-time video of President Kikwete

ARSENAL: TEVEZ KWA NASRI

Arsenal jana usiku wameiambia Manchester City:Tupeni Carlos Tevez na nyie mchukueni Samir Nasri.

Carlos Tevez amekuwa akijaribu kwa muda sasa kutaka kuondoka Manchester ndani ya kipindi hiki chote cha usajili, na kocha wa Arsenal akiwa kwenye pressure ya kununua top players, sasa ameamua ghafla kuja proposal hiyo ya kushtua.

Kiungo Samir Nasrialikuwa na matumainiya kusainiwa na Man City jana mchana baada ya kuhadiwa dili la mshahara wa £180,000 per week, lakini Arsene Wenger akiwa katika hatua za mwisho za kuondokea na nahodha wake Cesc Fabregas aliuzuia uhamisho wa Nasri huku akipeleka proposal ya kubadilishana na Tevez.

Gunners wanaamini wakimtoa Nasri itawagharimu kiasi cha kuongezea cha £10m ili kumpata Muargentina Tevez ambaye timu yake ya City amemuekea gharama ya usajili kuwa £50m.

Friday, August 12, 2011

BENNY McCATHY AWASHA MOTO ORLANDO PIRATES


Benny McCarthy aanza kazi Orlando Pirates.

Mshambuliaji mpya wa mabingwa wa soka nchini Afrika Kusini Orlando Pirates Benny McCarthy ameanza vyema maisha yake ya soka kwenye klabu yake mpya baada ya kufunga kwenye mchezo wake wa kwanza wa ligi ya PSL dhidi ya Black Leopards .

McCarthy alifunga bao hilo akiwa ameingia kwenye kipindi cha pili ambapo ilimchukua dakika nane tu kufungua akaunti yake ya mabao kwa klabu yake mpya .

Orlando ilishinda kwa mabao 2-0 huku bao lingine likiwekwa wavuni na mshambuliaji mwingine wa Pirates Bongani Ndulula aliyefunga mapema kwenye dakika ya 10 ya mchezo

VODACOM YATOA VIFAA LIGI KUU KWA TIMU SHIRIKI

MKUU WA UDHAMINI WA KAMPUNI YA VODACOM AKIONGEA WAKATI WA HAFLA HIYO ILIYOFANYIKA KATIKA HOTEL YA KILIMANJARO KEMPINSKI.

MAKAMU WA PILI WA RAISI WA TFF ATHUMAN NYAMLANI AKIZUNGUMZA KATIKA HAFLA YA MAKABIDHIANO YA VIFAA VITAKAVYOTUMIKA KATIKA LIGI KUU YA MSIMU UJAO.

MKUU WA UDHAMINI WA KAMPUNI YA VODACOM AKIKABIDHI BAADHI YA VIFAA VITAKAVYOTUMIWA NA WAAMUZI KATIKA LIGI KUU YA TZ BARA MSIMU UJAO KWA MAKAMU WA PILI WA RAISI WA TFF


WAWAKILISHI WA UONGOZI WA AZAM FC NAO WAKIPIGA PICHA KUONYESHA JEZI ZAO WALIZOPEWA NA VODACOM

UKAWADIA WAKATI WA WEKUNDU WA MSIMBAZI NAO KUONYESHA UZI WAO WALIOPEWA NA MDHAMINI MKUU WA LIGI VODACOM.

KUTOKA BUKOBA MPAKA KEMPINSKI, KAGERA SUGAR NAO WAKING'ARA NA UZI WAO

VIONGOZI WA TIMU ILIYORUDI LIGI KUU KUU MSIMU HUU MORO UNITED NAO WALIKABIDHIWA JEZI ZAO.
WATOTO WA ZAMUNDA A.K.A AFRICAN LYON NAO WAKIONYESHA MFANO WA VIFAA WALIVYOKABIDHIWA NA VODACOM


VIONGOZI WA COAST UNION YA TANGA WAKIPIGA PICHA KUONYESHA JEZI ZITAKAZOTUMIWA NA TIMU KATIKA LIGI KUU YA MSIMU UJAO.


MECHI YA NGAO YA JAMII (COMMUNITY SHIELD) SASA KUPIGWA USIKU.

Mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kufungua msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya mabingwa watetezi Yanga na Makamu Bingwa Simba itachezwa usiku (Agosti 17 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Uamuzi wa mechi hiyo kuchezwa kuanzia saa 2.00 usiku umetokana na sababu kadhaa, kubwa zikiwa mbili; Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na pia Agosti 17 mwaka huu kuwa ni siku ya kazi.

Pambano hilo litatanguliwa na mechi ya vikosi vya pili (U20) vya timu hizo ambayo yenyewe itaanza saa 10.30 jioni. Mechi ya Ngao ya Jamii baada ya dakika 90 kama mshindi hatapatikana, zitaongezwa dakika 30. Katika muda huo nao kama mshindi atakuwa bado hajapatikana, itatumika mikwaju ya penalti.

Mechi hiyo imepata mwekezaji (Bigbon) na hivi sasa wadau wake wakuu- Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na klabu husika ziko katika mazungumzo ya mwisho mwekezaji huyo. Kwa redio ambazo zinataka kutangaza mechi hiyo moja kwa moja zinatakiwa kuwasiliana na Idara ya Habari na Mawasiliano ya TFF ili kupewa masharti ya kufanya hivyo.

Pia unafanyika utaratibu wa kuuzwa futari uwanjani mara baada ya mechi ya vikosi vya pili ili kuwawezesha washabiki waliofunga kutohangaika kutafuta sehemu ya kufuturu.

KAMATI TFF YAMREJESHA MCHAKI
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilikutana Agosti 10 na 11 mwaka huu kujadili rufani ya Frank Mchaki kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kumuengua kugombea nafasi ya Katibu Mkuu katika uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA).

Chini ya Mwenyekiti wake Deogratias Lyatto, Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilibaini kuwa pingamizi lililowekwa dhidi ya Mchaki na kujadiliwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, liliwasilishwa, kujadiliwa na kutolewa uamuzi kinyume na Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF Ibara ya 11(2) na (3) kwa kutotanguliwa na pingamizi mbele ya Kamati ya Uchaguzi ya KIFA, hivyo rufani hiyo haikuwa na sifa ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi na Kamati ya Uchaguzi ya TFF. Hata hivyo baada ya kupitia kiini cha pingamizi, Kamati imefikia uamuzi kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi ya mrufani zimekosa ithibati.

Kutokana na maelezo hayo, Kamati imekubaliana na rufani ya mrufani (Mchaki) dhidi ya uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, hivyo imemrejesha kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa KIFA.

Kwa kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF Ibara ya 8(3) Kamati ya Uchaguzi ya TFF inauahirisha uchaguzi wa KIFA uliokuwa ufanyike kesho (Agosti 13 mwaka huu) na sasa utafanyika Agosti 20 mwaka huu.

USAJILI LIGI DARAJA LA KWANZA
Usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Daraja la Kwanza kwa msimu huu utafanyika baada ya kumalizika Ligi ya Taifa hatua ya fainali inayoendelea hivi sasa kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.

Baada ya fainali hizo kumalizika Agosti 14 mwaka huu TFF itatoa mwelekeo wa usajili huo (roadmap) ikiwemo tarehe ya kuanza na kumalizika, pamoja na kipindi cha pingamizi. Timu tano kutoka kwenye fainali ya Ligi ya Taifa inayoshirikisha timu 12 zitapanda kuingia daraja la kwanza.

Ligi Daraja la Kwanza ambayo itaanza katika hatua ya makundi na baadaye kuchezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini itashirikisha jumla ya timu 18, na inatarajia kuanza Septemba 3 mwaka huu.

azam fc 0:0 Sc villa


Ikicheza kandanda safi lililowaacha na mshangao mkubwa watu wa Kampala. Azam FC leo imefanikiwa kutoka sare ya 0-0 na wenyeji SC Villa katika mchezo mkali wa kuvutia uliochezwa kwenye uwanja mkongwe wa Nakivubo.
Azam FC ambayo ipo kwenye mechi za majaribio leo ilijaribu mfumo wake mpya wa kucheza kwenye viwanja vibovu hasa ukizingatia kwenye ligi kuu ya Vodacom ambayo itaanza wiki ijayo kuna mechi zaidi ya sita ambazo tutapaswa kucheza kwenye viwanja vibovu. Viwanja hivyo ni Mkwakwani Tanga, Sheikh Amri Abeid Arusha, Jamhuri Dodoma, JKT Mlandizi na Kaitaba Bukoba huku viwanja vizuri vikiwa Taifa DSM, Azam Stadium Chamazi, Manungu Complex na CCM Kirumba Mwanza.
Said Morrad ambaye timu imemsajili toka Kagera Sugar, Abdul Halim Humud toka Simba na Waziri Salum toka Mafunzo ya Zanzibar leo walikuwa katika kiwango cha juu sana na walig’ara sana. Mwalimu Stewart Hall amesema amefurahishwa sana na kiwango cha timu yake leo hasa upande wa ulinzi na anachohitaji sasa ni kufanyia kazi eneo la ushambuliaji.
Azam FC iliwakilishwa na:

Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Said Morrad, Aggrey Morris, Abdulhalim Humud, Jabir Aziz, Ramadhan Chombo, John Bocco, Kipre Tchetche na Mrisho Ngasa

Wakati huo huo Azam FC kesho itashuka kwenye uwanja huo huo wa Nakivubo kukwaana na Kampala City Council katika muendelezo wa mechi zake za kujipima nguvu kambla ya kuanza ligi kuu ya Vodacom.
Kikosi kinachotarajia kuanza kesho ni:

Obren Cirkovic, Ibrahim Shikanda, Malika Philip Ndeule, Aggrey Morris, Nafiu Awudu, Himid Mao, Ibrahim mwaipopo, Salum Abubakar, Wahab Yahaya, Zahoro Pazi na Khamis Mcha Viali

RATIBA YA MICHEZO YA JUMAMOSI

Blackburn - Wolverhampton
Fulham - Aston Villa
Liverpool - Sunderland
Queens Park Rangers - Bolton
Postponed Tottenham 0 - 0 Everton
Wigan - Norwich
Newcastle - Arsenal

PAZIA LA LIGI KUU YA ENGLAND LAFUNGULIWA RASMI

Msimu mpya wa ligi kuu ya England umebakiza masaa pungufu ya 89 kabla ya kurudi tena baada ya kumalizika kwa msimu uliopita . Mashabiki kwa muda wamekuwa wakipata burudani ya soka kwa kufuatilia mechi za “pre-season” ambazo kwa baadhi ya mashabiki zimewapa sababu ya kutabasamu na kuna baadhi zimewapa wasiwasi kwa kile walichoshuhudia .
Kwa kurejesha kumbukumbu mara ya mwisho Manchester United ndio waliomaliza kama mabingwa wakiweka historia ya kutwaa ubingwa wa 19 ambao hatimaye uliwazidi mahasimu wao wa muda mrefu Liverpool .



Kwa bahati mbaya kwa mashabiki wa Manchester United huwezi kuzungumzia taji la 19 la ligi bila kurejea “dhahma” ya Wembley. Huku wengi wakiamini kuwa United watafuta makosa ya mwaka 2009 na kuwafunga mabingwa wa Hispania ambao wengi wanawatazama kama timu inayocheza soka bora kuliko timu zote kwenye historia ya mchezo huu , Manchester United walikumbana na kipigo cha mabao 3-1 na kumaliza msimu wao kwa machungu yasiyosahaulika.


Kwa wale wanaotazama mchezo wa soka kwa jicho la tatu , la nne mpaka la tano walitambua moja kwa moja kuwa kipigo ilichokipata United pale Wembley lazima kingekuwa na athari Fulani kwenye kikosi cha United kwa msimu uliofuata( yaani huu unaoanza kesho ).
Na ndiyo kilichotokea Sir Alex Fergusson hakupoteza muda kwenye shughuli ya usajili huku akili yake ikiwa kwenye kulipa kisasi kwa Barcelona kwa jinsi “walivyomtetemesha” pale Wembley .United walianza kwa kumsajili kipa ambaye ndiye atakayekuwa mrithi wa Edwin Van Der Sar ,


walimnasa Mhispania David De Gea toka Atletico Madrid , baada ya hapo United walikamilisha Usajili wa beki chipukizi Phil Jones halafu wakamaliza na Ashley Young . Baada ya hapo United wakaanza kupunguza idadi ya wachezaji ambapo John O’shea , Wesley Brown na Gabriel Obertan waliuzwa kwa Sunderland na Newcastle United .


United bado wanaonekana kuwa kwenye soko la usajili baada ya kauli ya mkurugenzi mtendaji David Gill kusema kuwa bado kuna nafasi moja ya kujaza . Nafasi hii ni nafasi ambayo imekuwa gumzo kwa karibu wakati wote wa mapumziko ya kabla ya msimu kuanza .


Kama utakuwa umetazama kwa makini De Gea , Ashley Young na Phil Jones wamekuja kuziba mapengo ya kina Van Der Saar, Gary Neville na Ryan Giggs atakayestaafu mwishoni kwa msimu ujao .


Lakini bado kuna nafasi ya Paul Scholes ambayo bado iko wazi . Hapo linakuja jina la Wesley Sneijder mtu ambaye amekuwa akihusishwa na kurithi nafasi ya Scholes hasa baada ya tetesi za kuwasajili kina Luka Modric na Samir Nasri kuisha kimya kimya.Msimu huu utakuwa wa maadiliko makubwa kwa United ambayo inakuja na sura mpya ikiwa na vijana wengi huku wakongwe wakiwa wameendelea kupungua taratibu .


Kwa upande mwingine Chelsea timu iliyomaliza msimu ikiwa nafasi ya pili ilimaliza kwa kumfukuza kocha wake Carlo Ancelotti na wakati timu zingine zikifanya usajili Chelsea “walisajili” kocha Andre Villas Boas”, kocha ambaye ametokea kuliteka soka la ulaya akiwa na kikosi chake cha Fc Porto .

Andre Villas Boas alianza wakati wake akiwa na Chelsea kwa habari mbaya za kumkosa kiungo muhimu wa Chelsea Michael Essien ambaye alipata jeraha baya la goti ambalo litamuweka nje ya dimba kwa zaidi ya miezi sita . Villas Boas alijibu pigo hilo kwa kumsajili kinda wa Barcelona Ariel Romeu .

Baada ya hapo Chelsea imemsajili Romelu Lukaku , mshambuliaji mwenye umri wa miaka 18 toka Anderletch ya Ubelgiji . Lukaku anatajwa kama Didier Drogba mpya . Inavyoonekana kuna kila dalili kuwa Chelsea bado hawajamaliza usajili kwani kuna jina la Luka Modric ambalo limekuwa likihusishwa na jezi za bluu za London kwa muda mrefu .

Andre Villas Boas ana kazi kubwa sana ya kufanya kwenye kikosi chake ch Chelsea . Hakuna nayejua kwanini amemsajili Romelu Lukaku ilhali anao watu kama Drogba , Anelka, Torres na Daniel Sturidge .

Sawa unaweza kusema kuwa kwa umri wa miaka 33 alio nao Drogba na mwenzie Anelka Villas Boas anatazama mbali zaidi ya walipo washmabuliaji hawa wawili lakini vipi kuhusu Sturidge mtu ambaye alidhihirisha uwezo wake kwa mabao aliyofunga akiwa na Bolton alikokuwa kwa mkopo msimu uliopita .

Una maana gani kwa kijana huyu unaposajili mshambuliaji mwenye umri sawa na wake (sturidge) yaani Lukaku tena kwa fedha nyingi namna hii . Suala linguine muhimu ambalo litakuwa tatizo kwa sasa kwa Boas ni mbinu ya kuwachezesha Drogba na Torres kwenye uwanja mmoja .

Tatizo kubwa la Chelsea halijawahi kuwa kocha , bali mmiliki wa timu Roman Abramovich ambaye hajawahi kuwapa makocha muda wanaohitaji kujenga timu na kama hataiacha tabia ya kuwaajiri na kuwafukuza basi ni dhahiri mafanikio atakuwa akiyasikia kwa timu zingine .




Washindi wa tatu kwenye msimu uliopita walikuwa Manchester City . Kuna vitu ambavyo timu hii inayomilikiwa na mabilionea wa kiarabu inacho kama Baraka na wakati huo kama laana .


Vitu hivyo ni mshambuliaji toka Argentina Carlos Tevez na mwenzie toka Italia Mario Balotelli. Baloteli na Tevez kwa vipaji walivyo navyo ni kama baraka kwa timu yoyote itakayokuwa nao lakini ni laana pia kwani kwa nyakati tofauti wamekivuruga mno kichwa cha kocha wao Roberto Mancini .


Tevez ameonyesha dhamira yake kuwa hataki kuendelea kucheza soka kwenye klabu hii na Mario Balotelli mara kwa mara amekuwa akiudhihirishia ulimwengu kuwa yeye ni mwendawazimu kwa matendo yake anyoyafanya ndani na nje ya uwanja . Kwa tatizo la Tevez kocha Roberto Mancini ameonyesha kulipatia ufumbuzi kwa kumsajili mwenzie na Tevez kwenye timu ya taifa ya Argentina Sergio Aguerro . Kabla ya hapo Mancini alimsajili mchezaji Stefan Savic aje kusaidiana na mabeki wengine na pia amemsajili Gael Clichy toka Arsenal na kuna kila ishara kuwa anaweza kurejea Emirates kumnyakua mchezaji mwingine Samir Nasri.


Manchester City wanauanza msimu huu kama walivyouanza ule uliopita kwa kuonyesha kuwa wanakuja kuleta mapinduzi na tayari wameyaleta kwani leo hii haizungumzi kama top 4 bali top 5 au top 6 ukiwajumuisha na Tottenham , lakini bado safari ndefu ya kutwaa mataji ipo kwa kuwa Kocha Roberto Mancini bado hajapata “chemistry” muhimu ambayo itampa mataji .


Alicho nacho kwa sasa ni kundi kubwa la wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu lakini wachezaji hawa wanabaki na vipaji vyao na kwa pamoja hawana uhusiano muhimu ambao unaunda umoja unaoleta timu inayoweza kucheza kwa mafanikio uwanjani .




Arsenal ambao kwa miaka ya hivi karibuni wametokea kuwa Academy ya Manchester City wana matatizo makubwa . Imepita misimu sita tangu washika bunduki watwae kombe lao la mwisho . Sababu zinazoinyima Arsenal makombe ni zile zile , kipa , beki na kiungo .


Hakuna anayejua kinachoendelea kichwani mwa Arsene wenger zaidi yake yeye mwenyewe . Hadi sasa hajafanya usajili wa kuzingatia matatizo yanayoinyima Arsenal mafanikio na badala yake amemsajili kiungo mshambuliaji Gervinho toka Lille ya Ufaransa .


Labda amekuwa mzito kusajili beki kwa kuwa anajua kuna beki mmoja ambaye kurejea kwake ni kama mchezaji mpya aliyesajiliwa naye ni Thomas Vermalen . Zaidi ya hapo Arsene Wenger ametumia msimu wa usajili akijibu na kuondosha tetesi za kuondoka kwa Cesc Fabfergas na Samir Nasri .


Fabregas ni mtu ambaye ulimwengu mzima unatambua kuwa ana ndoto ya kurudi kwao Bracelona ambako anatazamwa kama mrithi wa Xavi Hernandez . Nasri ameshasema kuwa anataka kwenda kwingine ambako atapata mataji .


Tetesi za hivi karibuni zimekuwa zikimhusisha Arsene Wenger na majina ya watu kama Gary Cahill na Christopher Samba watu ambao kiukweli Arsenal inawahitaji ili kutibu ugonjwa wa muda mrefu lakini hadi sasa dalili zinaonyesha kuwa wameshawakosa na Arsene wenger amegeukia kwa Scott Dann wa Birmingham ambaye inasemekna mazungumzo yanaendela .


Hadi hapo ambapo Arsene Wenger atakapogundua kuwa kina Johan Djorou , Abou Diaby na vijana wengine wepesi wepesi ambao hawaiwezi mikikimikiki ya soka la England basi Arsenal wataendela kuwaumiza mashabiki wao kwa muda mrefu.




Mabingwa wa zamani Liverpool wameonekana kumaanisha biashara safari hii . Ukirudi nyuma wakati dirisha dogo la usajili lilipofunguliwa msimu uliopita King Kenny Dalglish alifanya usajili wa kumuuza Fernando Torres na kuwanunua Luis Suarez na Andy Caroll .


Kennya hajaishia hapo na wakati huu amenza kazi kwa kuwasajili Jordan Henderson , Charlie Adam, Stewart Downing , Alexander Doni , na pia wako mbioni kumnasa beki wa kushoto wa kihispania toka Newcastle United Jose Enrique . Kimsingi Liverpool wamekuja kurejesha zama zao za ufalme wa England ambao umepotea kwa muda mrefu na chini ya King Keny Daliglish kuna kila sababu na uwezo wa kutimiza azma hiyo .

FRIEND MATCH: SC VILLA 0-0 AZAM





Klabu ya Azam FC leo imeendelea na ziara yao ya kujifua kwa ajili ya ligi msimu ujao nchini baada ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi Sports Club Villa ya nchini ya Uganda katika uwanja wa Nakivubo jijini Kampala.

MSIMU MUHIMU KWA WACHEZAJI HAWA

Wakati mashabiki wa soka wakijiandaa kuukaribisha msimu mpya wa soka kwenye ligi kuu nchini England ni vyema tukawatazama baadhi ya wachezaji ambao wana madeni ya kulipa kwa mashabiki wa timu wanazochezea.




Aaron Ramsey (Arsenal)




Arsenal wamekumbwa na balaa la majeruhi ya wachezaji wake katika nyakati tofauti, majeraha haya yamewatia baadhi ya wachezaji vilema vya maisha kiasi kwamba japo wanacheza lakini hawachezi katika kiwango kile kile walichokuwa wanacheza kabla ya kuumia ,


Aaron Ramsey februari mwaka 2010 alivunjika mifupa miwili ya tibia na fibula kwenye mguu wake baada ya kugongana na Ryan Shawcross. Ramsey alivunjika vibaya kiasi kwamba hata Ryan Shawcros mwenyewe ambaye alipewa kadi nyekundu japo ni dhahiri hakukusudia alitoka uwanjani huku machozi yakimtiririka.


Mungu si Athumani Ramsey alirejea uwanjani mwezi Novemba mwaka huo huo akiwa kwenye klabu ya Nottingham Forest kwa mkopo. Ramsay aliporudi uwanjani mwanzoni alionekana kuwa tofauti na hakuwa Ramsey Yule wa siku zote. Japo uwezo wake wa asili ulikuwepo, alikuwa anaonekana dhahiri kuathirika kisaikolojia kutokana na jeraha alilopata miezi tisa nyuma.


Ila wazungu wana msemo usemao “time is a healer” yaani muda ni tiba tosha na ndio kilichotokea kwa Aron kwani aliutumia vyema muda wake akiwa na Nottingham Forest na alirejea Arsenal mwezi machi , Ramsey alionyesha kile walichokikosa mashabiki wa Arsenal muda aliokosekana kwa bao safi alilofunga kwenye mchezo dhidi ya Manchester United mwezi mei na bao lingine kwenye kombe la Emirates limewapa wana Arsenal matumaini zaidi .


Jeraha la Aaron lilikuwa kama la Eduardo lakini bahati nzuri kwa Aaron ni kuwa ameweza kurejea kwenye kiwango chake kile kile na wakati huu ambao huenda Arsenal ikawapoteza viungo wake wawili muhimu Samir Nasri na Cesc Fabregas inaweza kuwa nafasi muhimu kwa Ramsey kuingia na kuchukua mojawapo ya nafasi hizi mbili na kuwapa Arsenal malipo ya imani yao kwake .





Stephen Ireland (Aston Villa)

Japo kuna wiki kadhaa zimebakia kabla hajasherehekea kutimiza umri wa miaka 25 , Stephen Ireland anaonekana kama mtu aliyecheza ligi kuu ya England kwa muda mrefu sana kiasi cha kuwa mkongwe , hii ni kwa sababu katika kipindi kifupi ameweza kupanda na kushuka baada ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa msimu wa 2008/09 wa Manchester City.


Kitu ambacho kimemtatiza sana Ireland ni imani ndogo waliyo nayo makocha kwake. Mwezi Novemba mwaka 2008 alimtaja kocha Mark Hughes kama mmoja wa makocha bora aliowahi kucheza chini yao, lakini kufikia Februari mwaka 2010 Hughes huyo huyo alikuwa akilaumiwa kwa kushuka kiwango cha Ireland sababu kuu ikitajwa ni kumchezesha Ireland katika nafasi ambayo si yake .


Ireland alimtaja Roberto Mancini kuwa ndiye aliyemrejesha kwenye kiwango chake, lakini mwezi Agosti mwaka 2010 huyo huyo Ireland akamponda Mancini kwa kushindwa kujenga mahusiano mazuri na wachezaji wake.
Stephen Ireland aliondoka Man City na kujiunga na Aston Villa na ndani ya muda mfupi kocha aliyemnunua Martin O’neal aliondoka na aliyekuja kuchukua nafasi yake Gerard Houllier hakuwa na mpango naye .


Houllier alisema kuwa Ireland anahitaji kufanyia kazi soka lake ; Ireland alijibu mapigo kwa kusema kuwa katika mara chache alizocheza alicheza vizuri na mfano ni mechi ya Chelsea ambako alikuwa “Man of the match” ila Houllier hakuliona hilo.


Mwisho wa siku Stephen Ireland alipelekwa Newcastle United kwa mkopo “ Ireland alizungumzia uhamisho wake kwa mkopo kwa maneno haya ‘kwa mara ya kwanza niko chini ya kocha ambaye anihitaji kwenye timu yake’ lakini cha ajabu ni kuwa mpaka kufikia mwisho wa mkataba wake wa mkopo Alan Pardew aliamua kuwa hamhitaji Ireland Newcastle ambako alicheza mechi mbili tu huku muda mrefu akiwa majeruhi.
Kocha mpya wa Aston Villa Alex McLeish ameonekana kuwa tayari kumpa nafasi Ireland. McLeish amesema kuwa Ireland amekuwa na bahati mbaya sana kwa kuwa mambo hayajamuendea vyema ila uwezo aliounyesha kwenye mazoezi umempa imani kuwa anastahili kupewa nafasi na ana imani kuwa atarejesha fomu aliyokuwa nayo. Ni wakati wa Ireland kuwadhihirishia makocha wake wa siku za nyuma kuwa walikuwa na makosa kwa kutomuamini.




Fernando Torres (Chelsea)

Mshindi wa kombe la dunia akiwa na timu yake ya taifa ya Hispania na mchezaji ghali kuliko wote nchini England , sifa zote hizi Fernando Torres hakuzitendea haki na katika miezi yake sita akiwa na Chelsea iliyomnunua toka Liverpool alifunga bao moja tu.


Torres alikuwa na wakati mgumu sana mwaka 2010, pamoja na kwamba alivaa medali ya ushindi kwenye timu ya taifa lakini ukweli ni kwamba Torres alikuwa abiria tu kwenye ndege ya Hispania akiwasindikiza wenzake kwani hata kwenye fainali aliingia kama mchezaji wa akiba na baadaye alitolewa akiwa ameumia .


Dalili za Torres wa zamani kurejea zilionekana akiwa na Liverpool lakini lilipokuja dirisha dogo aliuzwa kwenda Chelsea ambako bundi alionekana kumuandama tena . Torres alionekana kama mpotevu kwenye kikosi cha Chelsea .


Jukumu la kucheza pamoja na Didier Drogba lilionekna gumu kwake huku kila mmoja kati yake na Drogba akifanya kila awezalo kuudhihirishia uongozi kuwa usajili wake haukuwa sahihi (kwa drogba) na kwa upande wake ulikuwa sahihi. Kwa ufupi Torres alipata wakati mgumu sana huku wengi wakifananisha usajili wake na ule wa Andriy Chevchenko mwaka 2006.


Torres ni mtu ambaye uwezo wake unafahamika na wachezaji wote wanaocheza ligi kuu ya England , akiwa amepata muda wa kutosha kwenye “pre-season” wa kujiandaa na kujiweka fit na pengine ujio wa kocha mpya Andre Villas Boas utampa nguvu mpya kwani mashabiki wa Chelsea wana hamu ya kumuona Fernando Torres wa zamani aliyewahi kuwatungua mara 8 kwenye mechi mbalimbali akiwa na Liverpool,


japo kuna kila dalili kuwa bado Villas Boas hajapata mfumo sahihi wa kumchezesha Torres na ishara zinaonyesha kuwa Torres ataanzia Benchi msimu utakapoanza hasa ukizingatia kuwa Chelsea imemsajili mshambuliaji mpya Romelu Lukaku.



Jack Rodwell (Everton)


Pamoja na umri wake mdogo wa miaka 20 tu , Rodwell ni mtu aliyeko kwenye hatua muhimu sana kwenye maisha yake kama mcheza soka . Kwa muda mrefu kijana huyu amehusishwa na uhamisho wa kwenda Manchester United lakini hivi karibuni Sir Alex Fergusson alichagua kumsajili Phil Jones baada ya Rodwell kuwa majeruhi kwa muda mrefu kwenye msimu uliopita.

Mwenyewe amekiri kuwa msimu wa mwaka 2011/12 utakuwa muhimu sana kwake . Rodwell alishindwa kupata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha Everton . Rodwell ana uwezo wa kucheza kwenye nafasi ya kiungo mkabaji japo anauwezo wa kupanda mbele pia au hata nafasi ya beki wa kati . Kama hatapata nafasi ambayo atatulia nayo kuna uwezekano mkubwa akajikuta akitumika kama mchezaji wa kujaza nafasi za wachezaji wengine wanapokosekana uwanjani .





Stewart Downing (Liverpool)



Ana kasi , ni mjanja , ana mguu wa kushoto wa hatari sana ,ana uwezo wa kufunga , kutengeneza mabao . Pengine timu nyingine hazitambui uwezo wake ila sisi tunaujua na ndio maana tumemsajili kwa kuwa ni mchezaji mwenye vitu vingi sana kiufundi na ndio tulichokuwa tunahitaji kwenye timu yetu”.

Hayo yalikuwa maneno ya mkurugenzi wa masuala ya soka kwenye klabu ya Liverpool Damiano Commoli ambaye hakusita kumsifia Stewart Downing baada ya kukamilisha usajili wake toka klabu ya Aston Villa. Maneno ya Commoli yanaweza kuonekana kuwa na chumvi iliyozidi kwa kuwa kila mtu anafahamu kuwa Downing hana uwezo na kasi inayohitajika kwa mawinga japo ana kipaji kisichopingika .

Unapokuwa na mtu kama Andy Carrol ni dhahiri kuwa unahitaji kuwa mawinga watakaomlisha krosi nyingi za ukweli, hiyo itakuwa kazi kubwa ya Stewart Downing kwenye timu ya Liverpool na kama akishindwa kuifanya basi watu hawatakuwa nyuma kuhoji paundi million 20 zilizotumika kumsajili.

Thamani yake kiukweli imeongezekan kutokana na ukweli kuwa ni raia wa England na mashabiki wengi ambao walikuwa wanahitaji kuona mchezaji kama Marko Mantin au Juan Mata watahitaji kudhihirishiwa thamani ya Stewart Downing .




Jonathan Woodgate (Stoke)



Jonathan Woodgate ni mtu ambaye ametumia muda wake mwingi akitibu majeraha mbalimbali , mara zote nne ambazo amewahi kuuzwa toka klabu moja kwenda nyingine amekuwa akiuzwa kwa thamni kubwa sana . Usajili wake wa mwisho unamshuhudia akisajiliwa na Stoke City kwa usajili wa bure .

Kwenye miaka yake miwili ya mwisho akiwa na Tottenham hotspurs Woodgate alicheza jumla ya mechi nne , na klabu ikaamua kutomuongeza mkataba . Akiwa na umri wa miaka 31 ni ajabu kuwa maisha yake katika soka la ngazi ya juu kama ligi kuu ya England bado hayajaisha , ila Tony Pulis ana imani kuwa maisha haya yanweza kurefushwa japo kidogo kwa kuzipa umuhimu siku za mechi kuliko mazoezi .

Tony Pulis amesema kuwa atajitahidi kumpa muda mfupi wa mazoezi na muda mrefu wa mechi ili kumuongeza muda wa kucheza kwa hali yake ya kiafya . Pullis anasema kuwa anaamini kuwa Stoke ina timu nzuri ya wataalamu wa afya. Inawezekana kuwa Tottenham timu yake ya zamani ina njia tofauti ya kufanya mambo ila kwetu ni tofauti na Woodgate atakuwa msaada kwetu .

Kama Tottenham walivyoweza kumchezesha Ledley King mchezaji mwingine mwenye majeraha sugu ya goti mechi 32 kwenye msimu uliopita basi hilo linawezekana pia kwa Stoke japo bado kuna wasiwasi mkubwa juu ya uwezo wa mwili wa Woodgate kuhimili mikikimikiki ya ligi kuu ya England . Kwa Tony Pulis , ana imani kuwa Woodgate anaweza kuwa moja ya usajili bora wa msimu .

Kama ilivyo kwa wengine kwenye orodha hii Woodgate naye anapaswa kutumia msimu huu kama nafasi yake ya mwisho ya kuwaonyesha watu kuwa miaka yote aliyopigana na majeraha mbalimbali ya goti haijaenda bure .

Jermain Defoe (Tottenham)



Umekuwa wakati mgumu sana kwa Jermaine Defoe . Akiwa amefunga mabao 18 kwenye ligi msimu wa mwaka 2009-10 , defoe alifunga mabao 4 tu msimu uliofuata . Majaliwa yake hayakusaidiwa na ukweli kuwa aliumia siku nne tu baada ya kufunga hat-trick kwenye mchezo baina ya England na Bulgaria mwezi septemba , lakini hata pale alipokuwa fiti Defoe hakufanya makubwa .

Mwezi mei Ddefoe alisema kuwa anaweza kulazimika kuondoka ikifikia hatua mbaya baada ya kuwa ameanza mechi 14 tu . Kocha wake Harry Redknapp alisema kuwa kama Defoe akicheza vyema atapangwa kama asipocheza vyema siwezi kumchagua kwenye timu .

Ukosefu wa mshambuliaji aliye kwenye fomu uliigharimu Spurs vibaya mno kwani wameshindwakurejea kwenye ligi ya mabingwa . Huku wakiwa na lengo la kurejea huko msimu ujao ni wakati wa Defoe kurudi kwenye kiwango chake au atajikuta anatafuta pa kwenda .




Mario Balotelli (Manchester City)



Baloteli ni mtu mwenye uwezo na kipaji kisichopingika . Cha ajabu ni kwamba badala ya kutengeneza vichwa vya habari kwa kutumia kipaji chake na kuiteka dunia kwa uwezo wake mkubwa Balotelli siku zote amekuwa akipamba vichwa vya habari kwa sababu mbaya .

Maisha yake ya soka yamejaa matatizo ya nje ya uwanja na wakati mwingine huwa analeta utata wake hata ndani ya uwanja .
Akiwa na Inter Milan , Balotelli aliwahi kutukanwa na kocha wake Jose Mourinho na wakati mwingine aliwahi kuchapwa makofi na mchezaji mwenzie Marco Materazzi kwa tabia yake chafu aliyoionyesha wakati wa mchezo dhidi ya Barcelona ;


Akiwa City Roberto Mancini alishindwa kuvumilia upuuzi wa Balotelli pale alipotolewa kwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi ya Europa dhidi ya Dynamo Kyiv . Mwezi Aprili mwaka huu Silvio Berlusconi alitangaza kuwa ndoto ya Balotelli ya kuichezea timu anayoipenda ya Ac Milan haitotimia , kwa maneno yake mwenyewe Berlusconi alisema hivi “ kuna tabia ambayo watu wanaohusishwa na Ac Milan wanapaswa kuwa nayo na sidhani kama Balotelli yuko karibu na kuwa na tabia hiyo “.

Hayo ni baadhi tu ya mambo ambayo mwehu Balotelli ameyafanya katika kipindi kifupi akiwa na Man city ila umefikia wakati way eye kujitambua kama mchezaji na kutambua kuwa Mancini amefikia hatua ya mwisho kwake na kama hatadhihirisha uwezo wake msimu huu basi huu unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wake .




Anderson (Manchester United)



Japo bado ana umri wa miaka 23 , Anderson anajiandaa kuanza msimu wake wa tano akiwa Old Trafford . Fc Porto walilipwa euro million 20 wakati walipomuuza Anderson kwa Man United mwaka 2007 , na katika kipindi hicho Anderson ameonyesha ishara za thamani ya fedha zilizolipwa kwa ajili yake lakini bado hajawa na mwendelezo wa uwezo na kipaji chake yaani ‘consistency’ndani ya kikosi cha kwanza cha Man United .

Anderson alifika Old Traford akiwa na lengo la kucheza kama beki wa kushoto lakini amejikuta akiwa kiungo mkabaji kwa muda mrefu akiwa England , ambapo ameonyesha kiasi fulani cha uwezo wake lakini bado hajaweza kujihakikishia nafasi ya kudumu huku akihangaika na matatizo ya majeruhi ya muda mrefu .

Alipokuwa Ureno Anderson alionyesha kila sababu ya kuitwa mrithi wa Paul Scholes na sasa ambapo ‘maestro’ huyu wa midfield ya Man United akiwa amestaafu pengine ni wakati sahihi kwa Anderson kuingia na kuonyesha kile alichokiona Ferguson nchini ureno .


Matt Jarvis (Wolves)
Jarvis alicheza vizuri sana akiwa na Wolves msimu uliopita , alitwaa tuzo za mchezaji bora wa mashabiki na mchezaji bora kwa wachezaji wenzie kwa timu yake ya Wolves , na mwezi machi alicheza mechi yake ya kwanza akiwa na timu ya taifa ya England alipocheza dakika 20 za mchezo wa kirafiki dhidi ya Ghana .

Pamoja na hayo kiwango chake kilishuka baada ya mchezo wake wa kwanza akiwa na England na alikaa benchi kwenye michezo miwili ya mwisho ya msimu kwa timu yake .Mick McCarthy alimzungumzia Matt Jarvis kuwa na tatizo la kukosa changamoto wakati msimu ukielekea mwisho ,

ameweza kuwapita mabeki wengi wa pembeni msimu huu na amewapa wakati mgumu sana lakini unapofika wakati kama huo unapaswa kupiga hatua kwa kuwa watu wanakuchukulia tofauti .

Ana mambo machache ya kudhihirisha kwa mashabiki wa Wolves lakini pia kama mchezaji wa timu ya taifa ya England na pia kama mtu aliyehisishwa na kuhamishwa na vilabu vikubwa , anao uhakika wa nafasi kwenye timu ya Wolves ila bado ana mengi ya kudhihirisha .

Thursday, August 11, 2011

MUTU AFUNGIWA SOKA MAISHA ROMANIA


Msahmbuliaji wa klabu ya Casena ya Italia Adrian Mutu amefungiwa kwa maisha kuichezea timu ya taifa ya Romania baada ya kugundulika kutumia pombe usiku wa kuamkia mechi ya kirafiki dhidi ya San Marino.

Adhabu hiyo pia imemkumba beki wa West Brom Albion Gabriel Tamas ambaye alikuwa na Mutu kipindi wakigonga kilaji.

Romania iliifunga San Marino 1-0 kwenye mechi yao kirafiki jana Jumatano, wachezaji wote wawili waliondolewa kwenye kikosi kabla ya kick off baada kutolewa kwenye vyombo vya habari zikisema walikwenda kulewa pombe usiku wa Jumatatu katika Pub ya Crawl.

Baada ya mchezo huo, Kocha wa Romania Victor Piturca alielezea sababu ya adhabu hiyo.

“Wachezaji hawa wawili wamefungiwa kwa maisha kwenye timu ya taifa, ni huruma lakini ni sheria inabidi tuzifuate, walitakiwa walitambue hilo.”

Mutu nae alijibu baada ya kuambiwa amefungiwa, “Tumeuelewa uamuzi wa Piturca.”

ENRIQUE AFANYIWA VIPIMO LIVERPOOL



Jose Enrique yupo katika hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wa kujiunga na Liverpool baada ya kufanyiwa vipimo.


Liverpool wamekubali kulipa ada ya £6m kwa Newcastle United kwa ajili mlinzi huyo mwenye miaka 25.




Taarifa ya Newcastle ilisema: “Newcastle United Football Club inathibitisha ada ya uhamisho wa Jose Enrique kwenda Liverpool imekubaliwa.Mchezaji ataenda Liverpool leo na kujadili maslahi yake binafsi pamoja na kufanyiwa vipimo vya afya.”


FABREGAS KUJILIPIA ADA YA UHAMISHO KWENDA BARCA



Cesc Fabregas yupo katika hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wa kwenda Barcelona.

Lakini kiungo huyo wa Kihispania itabidi alipe £4.5 kutoka kwenye mfuko .

Arsenal wapo tayri kukubali ofa ya £35.9 kutoka kwa Barcelona lakini watapata nyongeza ya peasa ikiwa Fabregas atashinda mataji makubwa 2@ Nou Camp.

Pia ofa hiyo itahusisha malipo ya £900,000 kwa mwaka ambayo Fabregas amekubali kuilipa Arsenal kutoka mshahara wake kutoka katika mkataba wake wa miaka 5 na Barca.

Kilichobakia kwa sasa ni kwa Fabregas kukubaliana matakwa binafsi ya Catalan club ili kukamilisha sakata la uhamisho huo uliodumu kwa zaidi ya miaka 3.


Wakati huo huo, Samir Nasri anategemewa nae kuondoka Arsenal kujiunga na Manchester City.

Kiungo wa kifaransa yupo katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Gunners, ingawa kocha wake Arsene Wenger alikuwa anataka kumbakisha lakini mabosi wa Emirates hawapo tayari kuona anaondoka bure msimu ujao.

City wanajitarisha kumlipa Nasri mshahara wa £180,000 kwa wiki huku wakiilipa Arsenal £25m.

Akizungumza na press striker wa Arsenal Marouane Chamakh alisema “Nafikiri wote wawili Cesc na Samir wataondoka ndani ya klabu hii.”

MATOKEO YA MICHEZO YA KIRAFIKI

Japan 3 - 0 South Korea

China 1 - 0 Jamaica

Kazakhstan 1 - 1 Syria

Azerbaijan 0 - 1 Macedonia

Russia 1 - 0 Serbia

Lithuania 3 - 0 Armenia

Latvia 0 - 2 Finland

Belarus 1 - 0 Bulgaria

Cyprus 3 - 2 Moldova

Senegal 0 - 2 Morocco

Ivory Coast 4 - 3 Israel

Hungary 4 - 0 Iceland

Albania 3 - 2 Montenegro

Norway 3 - 0 Czech Republic

Ukraine 0 - 1 Sweden

Liechtenstein 1 - 2 Switzerland

South Africa 3 - 0 Burkina Faso

Austria 1 - 2 Slovakia

Malta 2 - 1 Central African Rep.

Poland 1 - 0 Georgia

San Marino 0 - 1 Romania

Turkey 3 - 0 Estonia

Germany 3 - 2 Brazil

Ireland 0 - 0 Croatia

Italy 2 - 1 Spain

Scotland 2 - 1 Denmark

Slovenia 0 - 0 Belgium

Wales 1 - 2 Australia

Bosnia-Herzegovina 0 - 0 Greece

France 1 - 1 Chile

Portugal 5 - 0 Luxembourg

Tunisia 3 - 2 Mali

HILI NI ENEO LA OFISI ZA KLABU YA TP MAZEMBE.....SIMBA NA YANGA JIPANGENI !!!!!.

















































































HUYU HATA AKIAGA NYUMBANI ANAENDA KAZINI, KWELI INAINGIA AKILINI....