Search This Blog

Saturday, August 11, 2012

MBWANA SAMATTA NA GARI LA MILLIONI 50 -MCHEZA SOKA WA KIBONGO ANAYELIPWA FEDHA NDEFU ZAIDI


Akiwa ndio mchezaji aliyesajiliwa kwa fedha ndefu kutoka nchini Tanzania, Mbwana Ally Samatta anaishi ambayo mcheza soka wa kimataifa anastahili kuishi.

Akiwa ameuzwa kwa dola za kimarekani zaidi ya 100,000, kwenda TP Mazembe kutoka Simba, Mbwana Samatta analipwa kiasi cha dola 5000 kwa mwezi ambayo ni sawa na shilingi millioni 7.5 huku akichukua marupurupu ya kutosha.

Mbwana Samatta amekuwa akicheza na kuperfom kwa kiwango kikubwa katika kila nafasi anayopata anapoichezea klabu yake na kwa kiwango alichoonyesha kuna uwezekano mkubwa mkataba wake utaboreshwa zaidi na kuendelea kuvuna mkwanja mrefu zaidi.


Kwa sasa hivi Samatta amenunua gari la kisasa zaidi Chrysler Crossfire la mwaka 2006 ambalo limemgharimu takribani millioni 50 za kibongo.

Ikiwa Samatta ataendelea kucheza kiwango alichonacho sasa, basi ni dhahiri tutaendelea kuona akiishi kwenye majumba ya kifahari huku akipush magari ya gharama.

SIMBA NA YANGA ZAENDELEZA KUFANYIANA USAJILI KIHUNI - TETESI MBUYI TWITE ARUDISHA FEDHA ZA SIMBA, ASAINI YANGA



YANGA imeifanyia umafia mkubwa Simba baada ya kumteka na kumsainisha beki Mnyarwanda mzaliwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mbuyu Twite ambaye Mwenyekiti wa Wekundu hao, Ismail Aden Rage alimsainisha pia mjini Kigali wiki iliyopita ili atue Msimbazi.

Mbuyu ni miongoni mwa wachezaji wapya wa Simba waliotajwa kwenye tamasha la Simba Day, Jumatano iliyopita ingawa hakuwepo nchini.


Mashabiki wa Simba waliofurika kwenye Uwanja wa Taifa walionyeshwa jezi namba 4 ambayo Mbuyu atakuwa akivaa akiwa Simba.


Wapenzi wa Simba walishangilia wakijua kwamba tatizo limekwisha kwenye safu ya ulinzi kwani Mbuyu atasimama na Juma Nyosso, lakini sasa hali imebadilika.


Simba ilimpa mchezaji huyo dola 30,000 (Sh 45 milioni) na kumalizana naye kwa vita iliyodumu zaidi ya saa nane jijini Kigali, Rwanda ambayo ilipewa jina la Eight Hours in Kigali, ingawa sasa filamu hiyo imeingia katika sehemu ya pili ukipenda unaweza kusema Eight Hours in Kigali-2.


Baada ya Yanga kuchakazwa katika sehemu ya kwanza ya filamu hiyo, waliendelea kupambana vita ya msituni kupitia kwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallaa Binkleb na kufanikiwa kumshawishi mchezaji huyo ili arudishe fedha Simba na apewe kitita kikubwa zaidi.


Mbuyu aliwapigia simu viongozi wa Simba jana Ijumaa asubuhi akiwaambia kuwa amemtuma mtu arudishe fedha zao kwani anataka kurudi kuichezea timu yake ya zamani ya Lupopo ya Congo.


Hata hivyo ilivyofika mchana ilikwishafahamika kuwa ameshaini Yanga kwa kitita kikubwa zaidi.


Inadaiwa kuwa amesaini Yanga kwa kitita cha dola 50,000 (Sh 75 milioni)


Kisasi


Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Yanga na kigogo wa kamati ya usajili Abdallah Binkleb aliiambia Mwanaspoti wiki hii kwamba lazima alipize kisasi kutokana na nyodo za Simba iliyotangaza kumsainisha Mbuyu Twite kwa kumgaragaza yeye katika vita ya saa nane mjini Kigali.


Binkleb alitamka kuwa; "Simba wanasema mimi ni bwana mdogo siwawezi kwa fitna na ujuzi wa mambo ya mpira, wanasema sina uzoefu wowote kwenye mambo ya mpira, sasa ninachosema ni kwamba huyo Rage nimemsoma na lazima nilipize kisasi, siwezi kuvumilia maneno yao.


Wanaongea sana mpaka vitu vingine ambavyo havipo kabisa,"alisisitiza Binkleb na kudai kuwa yupo Kampala lakini Mwanaspoti liligundua baadaye kwamba alikuwa amejificha Kigali akipanga mikakati mpaka jana Ijumaa alipomaliza mambo.


Kabange Twite


Mwanaspoti lilimtafuta pacha wa Mbuyu, Kabange baada ya kumkosa Mbuyu na akasema:

"Nipo Kinshasa nafanya mambo yangu lakini nimeongea na Mbuyu aliniambia anakuja kucheza Tanzania, sijajua kama ni Simba au Yanga, nikiongea naye baadaye ndio atanihakikishia.

"Lakini mimi sina tatizo popote atakapoamua kucheza iwe Simba au Yanga ni sawa, hizo timu zote ni kubwa na zina mafaranga (fedha) nyingi, yeye anaenda kutafuta na mimi nitaenda kutafuta, si lazima tucheze timu moja kama siku zote,"alisema Kabange ambaye amenusurika kwenye rungu la APR lililopanga kuondoa wachezaji wote ambao si wazaliwa wa Rwanda.


APR imewatema Logbo Landry Didier (Ivory Coast), Alex De Avila Peixoto, Oliviero Alves na Douglas Lopes Carneirn (Brazil).


Ferwafa

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka la Rwanda(Ferwafa), Michel Gasingwa ameiambia Mwanaspoti kuwa; "Hatuna taarifa yoyote mpya kuhusiana na huyo mchezaji kujiunga na Simba au Yanga au kuondoka APR."


Kaburu alaani


Akizungumzia hilo, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' alisema walichokifanya Yanga ni uhuni ambao haukubaliki katika soka.


Kaburu alisema tayari beki huyo alishaini

Simba mjini Kigali mbele ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, viongozi wa Chama cha Soka Rwanda (Ferwafa) na maofisa wa APR.

"Tulifanya makubaliano na Mbuyu wakati wa michuano ya Kombe la Kagame. Tulikubaliana kila kitu.


Akaomba arudi Rwanda kumalizia mkataba wake na ndipo wiki iliyopita mwenyekiti wangu Rage alipokwenda kumsainisha mkataba wa miaka miwili mjini Kigali mbele ya maofisa wa APR na Ferwafa," alisema Kaburu.


"Baada ya kusaini aliomba kurudi kwenda kubadilisha pasipoti yake kwao Congo kabla ya kuja Dar es Salaam kuungana na wachezaji wa Simba, lakini tunashangazwa na mambo yanavyoendelea.


Tunadhani ametekwa na watu wa Yanga kwa sababu hata simu yake ameibadilisha.


Kaburu alisema kuwa walimpa kitita cha dola 30,000 (Sh 45 milioni), lakini Yanga wamempa fedha zaidi.


Kaburu alisema kuwa katika jambo la kushangaza Yanga wameomba ITC kupitia Congo, ambako mchezaji huyo amewahi kuchezea klabu ya Lupopo tofauti na kanuni zinavyosema kuwa leseni ya uhamisho wa kimataifa huombwa katika nchi ambako mchezaji amecheza kwa mara ya mwisho yaani Rwanda.


Kaburu alisema Simba nao haijakaa kimya kwani imeomba ITC kwa Ferwafa na kwamba hawatakuwa tayari kukubali kushindwa katika hilo.


Lupopo Congo

Kiongozi mmoja wa Lupopo ya Congo, ambaye hakutaka jina lake litajwa gazetini kwa sababu si msemaji alisema kuwa Mbuyu ni mchezaji wao na alikuwa amekwenda APR kwa mkopo tu.

"Ni kweli Yanga wamekuja hapa Congo, tumewapatia barua ya kuwaruhusu kumsajili Mbuyu na tumeipeleka nakala kwa Chama cha Soka Congo. Hivyo Yanga wanaweza kuomba ITC kupitia chama chetu hapa Congo," alisema kiongozi huyo.


Habari ambazo zilipatikana baadaye Mwanaspoti ikienda mtamboni zinasema kuwa tayari Yanga walikuwa wamepata uhamisho huo wa kimataifa kutoka Congo.


Source: Mwanaspoti.co.tz

NGORONGORO WAFIKA SALAMA NIGERIA - TAYARI KULIPA KISASI KWA FLYING EAGLES

Ngorongoro Heroes, timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 imewasili asubuhi hii (Agosti 10 mwaka huu) kwa ndege ya Overland Airways kwenye mji wa Ilorin, Jimbo la Kwara lililo Kusini mwa Nigeria tayari kwa mechi ya marudiano dhidi ya wenyeji Flying Eagles itakayochezwa Jumapili.

Mechi hiyo ya raundi ya pili ya michuano ya U20 ya Afrika itachezwa kwenye Uwanja wa Township kuanzia saa 10 kamili jioni kwa saa hapa ambapo Tanzania itakuwa ni saa 12 kamili jioni. Ngorongoro Heroes ilitua jana (Agosti 9 mwaka huu) jijini Lagos ambapo ililala kabla ya kuja hapa.

Msafara wa Ngorongoro Heroes wenye watu 27 ukiongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mtwara (MTWAREFA) ulipokea na Ofisa Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, Jones Mndeme na viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFF) umefikia hoteli ya Kingstone Grand Suites.

Kwa mujibu wa Kocha wa Ngorongoro Heroes, Jakob Michelsen, timu itafanya mazoezi leo jioni (Agosti 10 mwaka huu) wakati mazoezi ya mwisho yatakuwa kesho jioni (Agosti 11 mwaka huu) kwenye uwanja ambao utatumika kwa mechi ya Jumapili.

Wachezaji wote wako katika hali nzuri isipokuwa Issa Rashid na Aishi Manula ambao walikuwa wakisumbuliwa na tumbo baada ya timu kufika jana (Agosti 9 mwaka huu) jijini Nairobi, Kenya ambapo ilibadili ndege kuja Nigeria. Hata hivyo, hali zao zinaendelea vizuri na huenda wakawa sehemu ya kikosi cha kwanza kitakachoivaa Flying Eagles.

Mbali ya Rashid na Manula, wachezaji wengine walioko hapa kwenye kikosi cha Ngorongoro Heroes ni Barwany Khomeiny, Samir Ruhava, Dizana Yarouk, Leonard Muyinga, Hassan Ramadhan, Jamal Mroki, Omari Kheri, Frank Domayo, nahodha Omega Seme, Abdallah Kilala, Hassan Dilunga, Ramadhan Singano, Simon Msuva, Said Zege, Atupele Gren na Ramadhan Salum.

Mbali ya Michelsen, Benchi la Ufundi linaundwa na Mohamed Rishad 'Adolf' (Kocha Msaidizi), Peter Manyika (Kocha wa makipa), Nassoro Matuzya (Daktari), Joakim Mshanga (Physio), Juma Kizwezwe (Mtunza vifaa) na Meneja wa timu John Lyimo.

Flying Eagles ambayo ilishinda mechi ya kwanza mabao 2-1 nayo tayari imeshaingia hapa Ilorin ikitokea Lagos kwa mechi hiyo ambayo matokeo yake yataamua timu ipi itaingia raundi ya tatu ambayo ni ya mwisho kabla ya fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 zitakazofanyika mwakani nchini Algeria. Timu itakayovuka itacheza raundi hiyo na mshindi kati ya Congo Brazzavile na Afrika Kusini.

USAIN BOLT: BINADAMU MWENYE KASI ZAIDI DUNIANI - NA MWANARIADHA ANAYETENGENEZA FEDHA NYINGI ZAIDI KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA

Wakati zawadi ya fedha ni kidogo, fedha anayopokea Usain Bolt kwa siku ni kubwa shukrani kwa kwa malipo anayoyapata kwa kila anapocheza. Gharama zake kwa kila anapocheza zinaanzia £200,000 na zinaweza kufikia £350,000 kutokana na mchuano wenyewe. Bolt ana demand malipo makubwa kwa sababu uwepo wake kwenye mchuano unatoa guarantee ya uuzwaji wa tiketi zote.


"Bolt ndio mchezaji anayelipwa vizuri kuliko wote katika historia ya mchezo huu wa riadhaa, lakini pia inawezekana ndio anayelipwa kiasi kidogo sana kwenye historia ya mchezo, anasema Paul Doyle, wakala wa muda mrefu wa mchezo wa riadha, katika story ya Bolt iliyotolewa katika Sport Illustrated.

Uwepo wake katika mashindano ya Penn Relays mwaka 2010 ulipelekea idadi kubwa zaidi ya mashabiki kuhudhuria uwanjani walikuwepo watu 54,310 ikiwa ni historia kwa Penn Relays inayofanyika tangu miaka 118 iliyopita.

Bolt anastahili kulipwa vizuri zaidi kwa sababu amebadilisha upepo wa mchezo, kama Tiger Woods alivyofanya kwenye gofu na Micheal Jordan alivyofanya kwenye kikapu.

Wakati wa olympic mwaka huu, siku ilipofanyika fainali ya riadha mita 100, waandaji wa London Olympic 2012 walipata maombi zaidi ya watu millioni 1 kwa ajili ya tiketi kwa gharama ya $1,130, tiketi ya ghali zaidi kuliko mchezo wowote kwenye michezo hiyo inayoendelea huko London.  Bolt alikuwa na ushindani mkali na mjamaica mwenzie Yohan Blake, ambaye ni bingwa wa dunia wa mbio za mita 100, baada ya Bolt kuondolewa kwenye mbio za mwaka uliopita kwa kucheza ndivyo sivyo. Blake pia alimshinda Bolt kwenye mashindano ya majaribio ya mbio huko Jamaica.

Bolt alimshinda Blake kwenye mbio za mita za Olympic jumapili iliyopita akiweka rekodi mpya ya kukimbia kwa muda mfupi zaidi ikiwa ni 9.63 seconds. Anaungana na Carl Lewis kuwa binadamu pekee kushinda mfululizo medali za dhahabu katika mbio za wanaume za mita 100.

Akiendelea kushikilia ubingwa jina lake la utani kama binadamu mwenye kasi zaidi duniani, atakuwa na uwezo wa kuendelea kutaka kulipwa fedha nyingi kupitia ada yake ya kushiriki mashindano pamoja na mikataba ya matangazo.

MCHEZAJI HUYU ANASAKWA NA VILABU MAARUFU BARANI ULAYA

Friday, August 10, 2012

African Lyon yatambulisha kocha mpya kutoka Argentina

Kocha mpya wa timu ya African Lyon inayoshiriki  Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Pablo Ignacio Velez  kutoka Argentina wa kwanza kulia, akizungumzia nini atafanya akiwa  na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao uliopangwa kuanza Septemba Mosi mwaka huu. Kocha huyo amesaini mkataba wa miaka mitatu na timu hiyo. Wengine katika picha ni Charles Otieno ambaye ni mkurugenzi wa ufundi na Biashara wa timu hiyo na Meneja Mkuu na Mmiliki wa timu hiyo, Rahim Kangezi.

 
KOCHA mpya wa timu ya soka ya African Lyon, Pablo Ignacio Velez, amewasili nchini tayari kuanza kuinoa timu hiyo na kuomba apewe muda wa kukisuka upya kikosi hicho huku akiahidi mabadiliko zaidi ya soka kwenye timu hiyo.
Pablo raia wa Argentina aliyasema hayo jana baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia timu hiyo na kusisitiza lengo lake kubwa ni kuhakikisha vijana wanapewa nafasi ya kuonyesha vipaji vyao na ndivyo itakavyokuwa Afrika Lyon.
"Sikuja Tanzania kutafuta pesa, ndoto yangu kubwa ilikuwa kufundisha soka barani Afrika hivyo wakati ni sasa," alisisitiza kocha anayezungumza lugha ya 'kiispanyola'.
Pablo alisema "kazi ya aina yoyote lazima ipewe muda na mchezaji lazima atengenezwe hivyo watanzania wawe na subira kwa ajili ya kupata matunda mazuri ya vijana hapo baadae kutoka African Lyon.
Kocha huyo aliyewai kuzichezea timu za taifa za vijana chini ya miaka 17 na 20 za Argentina hakusita kusisitiza suala la nidhamu kwa wachezaji wa timu hiyo ya ndani na nje ya uwanja.
"Nidhamu ni muhimu kwa wachezaji wangu cha msingi tushirikiane katika kufanikisha hili kwa vijana kwani mchezaji anatakiwa kati ya miaka 18 na 19 awe ametengeneza jina kupitia soka ,"  alisema Pablo.
Naye Mmiliki wa African Lyon, Rahmu Kangezi alisema lengo la kumleta kocha huyo ni kuhakikisha timu hiyo inajongea mbele zaidi.
Kangezi alisema licha ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja lakini wanaweza kumtumia Pablo kwa kipindi kirefu kulingana na mfumo wa kuhakikisha wanaendeleza vijana katika timu yao.
"Pablo ni zaidi ya kocha, ana uwezo pia amecheza mpira pia ni kocha wa kwanza kutoka Argentina kuja Tanzania hivyo tunaimani timu yetu ya African Lyon itafika mbali zaidi kisoka," alisitiza Kangezi.
Pablo mwenye miaka 38 aliyechukua mikoba iliyoachwa na Jumanne Chale amewai kuifundisha  klabu ya Atletico Colo Colo De Chile (1998).
Klabu nyingine alizowai kufundisha ni Atletico Calchin (2000), Atletico Belgrano De Cordoba (1997), Atletico River Plate (1993-1995).
Klabu nyingine ni Banco De Cordoba (1991 na 1997), Deportivo Lasallano (1992) Atletico Argentino Penarol kwa miaka minne na klabu nyingine nyingi za Hispania na Argentina.

JAMHURI KHWELU JULIO - SERIKALI HAINA MSAADA WA DHATI KWA WANASOKA WA TANZANIA

Baada ya serikali kupitia wizara ya Habari na michezo kukataa kuwapa uwanja wa taifa taasisi ya Njohole Foundation kwa ajili ya kucheza mechi ya uzinduzi wa taasisi hiyo, mmoja ya wachezaji wa zamani na kocha ambaye ameshazifundisha timu kadhaa ikiwemo timu ya taifa ya Tanzania under 17, Jamhuri Kihwelu Julio leo ametoa ya moyoni kuhusu wizara hiyo ya michezo na jinsi inavyofanya kazi zake katika kukuza na kuisadia michezo nchini.

Jamhuri Kihwelo anasema kwamba wizara ya michezo ya Tanzania haina msaada wowote na wanasoka wa sasa mpaka wa zamani waliowahi kulitumikia taifa hili.

"Wizara ya michezo haijali kwa dhati michezo ya Tanzania, wanafanya mambo kisiasa sana, na wanamuangusha Raissi Kikwete ambaye sio siri amejitahidi katika kusaidia michezo. Hawa watu wa Njohole wanataka kusaidia soka kwa kufundisha vijana na kupeleka makocha nje kusomea na kuja kufundisha kwenye shule lakini serikali inashindwa uwasapoti katika kuzindua shughuli zao, eti wanataka millioni 20 kwa ajili ya uwanja. Mbona TFF wanatumia uwanja huo na wanatumia mamilioni ya pesa lakini uwanja bado kila siku unaendelea kuwa na hali mbaya? Hizo millioni 20 zitwasaidia nini sasa. Hii ni kitu kufaidisha watanzania hivyo serikali ilibidi wasapoti kwa hali na mali.

"Hii tabia ya serikali kutaka fedha nyingi kwa ajili kutumia uwanja inaleta matatizo sana kwenye soka. Kwa mfano sasa hivi kuna hii michuano ya Super 8 ambayo imeshindikana kufanyika kwnye uwanja wa taifa kutokana na masuala hayo hayo serikali kutaka fedha nyingi kwa ajili ya mechi zinazochezwa hapo. Sasa hivi mivhuano hiyo inafanyika Chamzi, ambao ni uwanja mzuri lakini kwa wadhamini inakuwa tofauti kidogo, kwa kuwa wanakuwa hawapati nafasi nzuri ya kujitangaza, tofauti na mechi zinapofanyika kwenye eneo kubwa na zuri zaidi kama kwenye uwanja wa taifa. Hivyo pia kutokana na hivi hali hii itatukimbizia wadhamini ambao wamekuwa ni moja ya kilio cha muda mrefu kwenye michezo."

MSIKILIZE JULIO AKIWAPAKA WIZARA YA MICHEZO

SERIKALI YAINYIMA UWANJA NJOHOLE FOUNDATION

Renatus Njohole muasisi wa Njohole Foundation

Wakati sekta ya michezo Tanzania ikiendelea kuzorota, baadhi ya wadau wa michezo wamekuwa wakitajitahidi kufanya wawezalo kuweza kuisadia michezo ipige hatua hapa nchini, lakini cha ajabu wamekuwa hawapati sapoti ya kutosha kutoka kwa serikali - hasa kupitia wizara yake ya michezo.
Baadhi ya wachezaji washiriki wa mechi hiyo ya uzinduzi wa Njohole Foundatio - Mwenye fulana ya njano ni Bakary Malima Jembe Ulaya

Moja ya kitendo ambacho kimefanyika hivi karibuni, Taasisi ya Njohole Foundation ambayo ipo chini ya familia ya wacheza soka maarufu akina Renatus Njohole, Likembe Njohole na wengineo kwa ajili ya kuwasaidia wacheza soka wa zamani na wa sasa ili kuweza kuwa kuvitumia vizuri vipaji vyao katika kuiwezesha nchi kufanikiwa kimichezo na  wao kunufaika vizuri na kazi yao ya soka.
Baadhi ya wachezaji watakaoshiriki katika mchezo wa mchezo wa kesho kati ya Njohole XI na mastaa wengine wa soka.

Taasisi hiyo imeandaa mchezo maalum wa hisani ambao utawashirikisha wachezaji tofauti wa zamani na sasa katika kuizindua taasisi hiyo, na mapato yatakayopatikana yataingia katika mfuko wa foundation hiyo, ili kuweza kufanya vizuri shuguli hiyo taaisi hiyo ikapeleka maombi kwa Wizara ya Habari na Michezo kwa ajili ya kupewa ruhusa ya kutumia uwanja wa taifa kwa ajili ya kufanyika kwa mchezo huo, cha ajabu wakaambia ikiwa wanataka kuutumia uwanja huo itabidi walipe millioni 20.


"Tulikuwa tumetuma maombi ya kuweza kuutumia uwanja wa taifa kwa ajili ya mchezo huo, lakini serikali ikashindwa kuturuhusu mpaka tutoe millioni 20. Hili jambo limetushangaza sana kwanza wenyewe serikali ilibidi watusapoti kwa hali na mali katika kuweza kufanya mambo yetu, lakini badala yake wanataka tuwalipe millioni 20 ambazo zinaweza kusadia katika kuendesha shuguli za kila za foundation yetu, ikizingatiwa hatupati msaada wowote kutoka kwao."
Bakary Malima Jembe Ulaya akiwa mazoezini leaders Club

Taasisi ya Njohole Foundation wanasema pamoja na kutoa mafunzo ya soka kwa vijana wadogo, pia itakuwa inachukua wachezaji wa zamani na kuwapeleka nje kusoma then watakapohitimu masomo yao watarudi nchini na kufundisha soka kwenye shule mbalimbali. Pia watakuwa wanatoa elimu kwa wachezaji namna ya kuweza kuzitumia vizuri fedha wanazopata katika soka ili kujiwekea misingi mizuri ya kimaisha mara pale watakapoacha kucheza mpira baada ya umri uwa mkubwa au sababu nyingine kama vile kupata majeraha yatakamfanya ashindwe kuendelea kuingia dimbani. ANGALIA VIDEO HIZI UONE WANA FAMILIA YA NJOHOLE WAKIONGELEA TAASISI YAO.

CHEMSHA BONGO! HUYU NI NANI NA KWANINI ALINYOA HIKI KIDUKU.

Hint: ni Raisi wa klabu moja ya soka nchini Ufaransa.

LUCAS MOURA ALETA KIZAIZAI KWENYE SOKO LA USAJILI - AS ROMA WASEMA DE ROSSI ANAUZWA KWA ZAIDI YA €100 MILLION, SANTOS WASEMA NEYMAR NDIO HAGUSIKI KABISA



Siku moja baada ya mchezaji wa kimataifa wa Brazil anayeichezea Sao Paolo Lucas Moura kusajiliwa kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekdi kwenye soko la usajili nchini Brazil kwenda Paris Saint Germain, marais wa vilabu vingine duniani wameanza kutoa kauli ambazo zitaleta gumzosana kwenye soko la usajili duniani.

PSG wametumia kiasi cha £150 millioni katika kipindi cha mwezi mmoja kufanya manunuzi ya kuwasajili Lucas Moura, Zlatan Ibrahimovic  na Thiago Silva.

Matumizi ya namna hii yameanza kuwatia vichaa baadhi ya viongozi wa vilabu vingine, Kwa upande wa AS Roma ambao mchezaji wao Daniele de Rossi amekuwa akitakiwa na Manchester City nao wameingia tamaa.


Akiongea mkurugenzi wa Roma Walter Sabatini mara laipoulizwa juu ya thamani ya Rossi, akaanza kwanza kuzungumzia mchezaji wa Fiorentina Stevan Jovetic ambaye aliwekwa kwenye thamani ya €30 million na klabu yake, na Napoli nao ambao walisema mchezaji wao Edinson Cavani  alikuwa na thamani ya €100 million kwa timu ambazo zilikuwa zinamtolea macho.

"Gharama ya De Rossi ni juu zaidi ya majina yote uliyoyataja hapo juu, kwani maana hiyo Rossi ana gharama zaidi €100 miilion na zaidi." -Sabatini

Ikiwa na kiungo huyo mwenye miaka 29 atakuwa na gharama hiyo , unadhani mchezaji ambaye anatajwa kuja kuwa na kiwango kikubwa kuliko wote, Neymar atakuwa thamani ya fedha ngapi?

Kwa mujibu wa raisi wa Santos Luis Alvaro, amesema baada ya Lucas Moura kuuzwa kwa bei ya €45 million huku alilipwa mshahara wa £250,000 kwa wiki, basi bei ya Neymar haielezeki - yaani anaweza hata asiuzike.

Neymar kwenye mkataba wake ana kipengele kinachomruhsu kuuzwa endapo klabu inayomtaka itatoa £57 million.

Lakini baada ya Moura kuuzwa kwa bei chafu bei  hiyo ya Neymar inaweza ikapanda maradufu.

ANDIKA CHOCHOTE KUTOKANA NA HIZI PICHA ZA MBWANA SAMATTA.


HIKI NDICHO ALICHOKISEMA MSEMAJI WA SIMBA EZEKIEL KAMWAGA.


Salaam ! Kwa waliosoma gazeti la Super Star la leo, watakuwa wameona stori yenye kichwa cha habari; "Sinema Mpya Ngassa, Twite." Ndani yake kuna maelezo kwamba Ngassa na Mbuyi Twite wanakwenda Yanga. Kuwa eti Azam wameamua kumpeleka Yanga kwa vile wamekasirishwa na hatua ya Simba kumsajili Redondo. Chanzo cha habari, hakitajwi. Wamezungumza na mimi nimesema hakuna kitu kama hicho. Wamezungumza na Msemaji wa Azam kawaambia hakuna kitu kama hicho. Lakini wameandika hiyo stori kwa kutumia "VYANZO VYAO." Hivi mwandishi kama huyu nikigoma kumpa ushirikiano nitakuwa nimekosea? Chini yake kuna stori ya Okwi. Uongo mtupu. Sote tunajua Okwi amekwenda kuitumikia timu yake ya taifa na atarejea baada ya hapo. Lakini mwandishi, kwa sababu zake, ameamua kufanya hilo lionekane ni tatizo!!!!!! Kwamba sasa Okwi bye bye Simba...Inauma sana lakini waandishi hawa ni rafiki zangu, wanataaluma wenzangu nk.... Tutafanyaje kazi zetu katika mazingira haya ambapo mtu anatunga stori ili auze gazeti????? Naomba mfahamu kwamba kuna watu wanaumia sana kwa habari za namna hii. Hawali wakashiba na wanakaa na wahka siku nzima. Tuthamini hisia za wenzetu

MECHI YA WIKI: RONALDO APIGA BAO MBILI, REAL MADRID WAKIICHINJA 5-1 AC MILAN

GOLI LA SIKU: ANAYEJUA ANAJUA TU - JUNINHO AENDELEA KUDHIHIRISHA UTALAAM WAKE WA KUPIGA FREE KICKS

Thursday, August 9, 2012

HUYU NDIO SHABIKI NO.1 WA RAMADHAN CHOMBO REDONDO ANAHAMA NAE KILA TIMU ANAYOENDA - SASA AIKACHA AZAM BAADA YA REDONDO KURUDI MSIMBAZI

AFRICAN LYON KUMTAMBULISHA KOCHA MUARGENTINA KESHO

Mmiliki wa African Lyon akiwa na kocha mkuu wa Chelsea Roberto Di Matteo
Klabu ya African Lyon imeendelea na utaratibu wake wa kuchukua makocha kutoka nje ya nchi, baada ya kufundishwa na kocha Mreno Eduardo Almeida takribani misimu miwili iliyopita, timu hiyo yenye maskani yake jijini Dar es Salaam kesho inatarajia kumtambulisha rasmi kocha mpya atakayoiongoza timu hiyo kwenye msimu ujao wa ligi unaotarajia kuanza hivi karibuni. 

Kwa mujibu wa mmiliki wa klabu hiyo Rahim Zamunda, kocha mpya wa timu anatoka nchini Argentina na anaitwa Pablo Ignacio Velez, atatambulishwa kesho kwenye mkutano wa waandishi wa habari katika hoteli ya New Avon Hotel.

Huu ndio wasifu wa kocha huyo mpya kutoka Argentina

PERSONAL DATA.
GENERAL INFORMATION PROMPTS.



NAMES:     PABLO IGNACIO.

SURNAME:     VELEZ.

NATIONALITY:     ARGENTINEAN.

DNI:     23195057.

PLACE AND DATE OF BIRTH:     CÒRDOBA, ARGENTINA.  JANUARY 28, OF 1973.

AGE:     38 YEARS OLD.




ACADEMIC FORMATION.




ELEMENTERY SCHOOL:     INSTITUTO HOGAR LA INMACULADA.



HIGH SCHOOL:     INSTITUTO HOGAR LA INMACULADA.


COLLEGE EDUCATION:


1) BLAS PASCAL UNIVERSITY:

-      COMPUTER SYSTEMS ANALYST.
-      PROGRAMMER ANALYST.
-   PC OPERATOR.



2)  ASSOCIATION OF ARGENTINIAN SOCCER COACHES (A.T.F.A.) – NATIONAL SCHOOL OF TECHNICIAN Nº29 – CÒRDOBA BRANCH:

-      SOCCER COACH.


3)  UNIVERSIDAD NACIONAL DE CÒRDOBA (UNC), FACULTAD DE CIENCIAS MEDICAS / INSTITUTO DE FISIOLOGIA HUMANA:

-      PHYSICAL TRAINER.
-      PERSONAL TRAINER.
-      FITNESS INSTRUCTOR.
-      INSTRUCTOR of techniques of adaptation:  Column disorders,
    Metabolic disorders (Obesity/Diabetes Type 2),     
    Cardiovascular Rehabilitation.



4)  HECTOR GONZALES CEBALLOS KARATE SCHOOL:
 
     -  KARATE INSTRUCTOR / BLACK BELT/ 1st DAN.





SPORTS ANTECEDENTS.




CLUB:          ATLETICO ARGENTINO PEÑAROL.
DIVISION:       6TH, 5TH, 4TH, 3RD, AND 1ST.  
PERIOD:           YEARS 1987/88/90 AND 99.


CLUB:          ATLETICO ROSARIO CENTRAL.
DIVISION:       4TH.
PERIOD:           YEAR 1989.

CLUB:          HURACAN DE LAS VARILLAS.
DIVISION:       1ST.
PERIOD:           YEAR 1990.

CLUB:          DEPORTIVO LASALLANO.
DIVISION:       1ST.
PERIOD:           YEAR 1992.

CLUB:          CLUB BANCO DE CORDOBA.
DIVISION:       1ST.
PERIOD:           YEARS 1991 AND 1997.

CLUB:          CLUB ATLETICO RIVER PLATE.
DIVISION:       3RD AND 1ST.
PERIOD:            YEARS 1993 / 94 / 95.

CLUB:          CLUB ATLETICO BELGRANO DE CORDOBA.
DIVISION:       1ST
PERIOD:           YEAR 1997

CLUB:          ATLETICO COLO COLO DE CHILE.
DIVISION:       1ST.
PERIOD:           YEAR 1998.

CLUB:          ATLETICO CALCHIN.
DIVISION:       1ST.
PERIOD:          YEAR 2000.



 PROFESSIONAL WORK EXPERIENCE IN CLUBS.

CLUB:              BANCO DE CORDOBA.

POSITION:        SOCCER COACH OF 4TH, 5TH AND 6TH DIVISION.
                                       ASSISTANT COACH OF 1ST DIVISION.
                                       GOALKEEPERS COACH.

PERIOD:                YEAR 2006.




CLUB:                BANCO DE CORDOBA.

POSITION:          SPORTS COORDINATOR,
                                         SOCCER COACH OF 1ST DIVISION.
                                        GOALKEEPERS COACH.

PERIOD:                YEAR 2007.


CLUB:                 CLUB ATLETICO ARGENTINO PEÑAROL.

POSITION:          SPORTS COORDINATOR,
                                         PHYSICAL TRAINING COORDINATOR,
                                         PHYSICAL TRAINING OF 1ST DIVISION,
                                        ASSISTANT COACH OF 1ST DIVISION.
                                        GOALKEEPERS COACH.

PERIOD:               YEAR 2008 AND 2009.





CLUB:             CLUB ATLETICO ARGENTINO PEÑAROL.

POSITION:         PHYSICAL TRAINING OF 1ST DIVISION.
                                        ASSISTANT COACH OF 1ST DIVISION. ( OF COACH JOSE MARIA SUAREZ : EX SOCCER PLAYER OF CLUB ATLETICO BOCA JUNIORS, BELGRANO, SELECCIÓN ARGENTINA) .
(SPORTING ACHIEVEMENTS : CHAMPION WITH BOCA JUNIORS OF THE LOCAL TOURNAMENT , COPA LIBERTADORES TWICE, AND COPA INTERCONTINENTAL), 
                                        GOALKEEPERS COACH..

PERIOD:                YEAR 2009 AND 2010.






SPORTING ACHIEVEMENTS.


TORNEO PROVINCIAL DE FUTBOL 2009 (WITH ARGENTINO PEÑAROL):

-      3RD POSITION.

-      - SPECIAL MENTION OF THE FEDERACION CORDOBESA DE FÙTBOL AS BEST PHYSICAL TRAINING OF CÒRDOBA.




TORNEO PROVINCIAL DE FUTBOL 2010 (CON ARGENTINO PEÑAROL):

-      3RD POSITION.

-      - SPECIAL MENTION OF THE FEDERACION CORDOBESA DE FÙTBOL AS BEST PHYSICAL TRAINING OF CÒRDOBA.
-       








SPECIAL CONSIDERATIONS.





SPECIAL NOTE: My technical team is currently composed of  JoSÈ Marìa Suarez, who Serves as my ASSISTANT COACH now