Search This Blog

Saturday, September 3, 2011

GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE KUZINDULIWA DAR KESHO.


Meneja wa kinywaji cha GUINNESS, Maurice Njowoka akitoa ufafanuzi wa namna ya shindano la Guinness Football Challenge litakavyofanyika mapema leo mbele ya wanahabari,kwenye ofisi za makao makuu ya kampuni ya bia ya Serengeti,Oysterbay,jijini Dar.

Mashindano ya Guinness Football Challenge yanatarajiwa kufanyika hapo kesho kwenye viwanja vya Leaders,Kinondoni. kwa mujibu wa Meneja wa kinywaji cha Guinness bwana Maurice Njowopa,shindano hilo litashirikisha watanzania wote wenye jinsia zote kuanzia umri wa miaka 18. shindano hilo litagawanyika katika sehemu kuu mbili

i) uwezo wa kuuchezea mpira
ii ) uwezo wa kujibu maswali




kutokana na mgawanyo huo hapo juu kila timu inatakiwa kuwa na watu wawili mmoja katika kila kipengele, na timu nane zitakazokusanya pointi nyingi zitapata nafsi ya kwenda nchini afrika ya kusini kushindania kiasi cha dolla za kimarekani 50,000 zitakazotolewa kwa mshindi wa kila wiki katika shindano hilo litakalochukua majuma manane.




Pichani kulia ni muwakilishi wa kampuni ya Endemol ya nchini Afrika Kusini,Warren na mwisho kushoto ni Muwakilishi wa kampuni ya Carberry Commonication,Tom akiwa pamoja na Meneja masoko wa kinywaji cha GUINNESSS,Moses Kebba walipokuwa wakizungunza na Wanahabari jijini Dar leo.

Friday, September 2, 2011

CHAMA CHA TPBC KIMEKUFA !!

BW. KAIKE SIRAJU,
PROMOTA WA PAMBANO LA MADA MAUGO vs FRANCIS CHEKA.
ULIOMBA KIBALI NA KUPEWA NA PST ILI KUANDAA PAMBANO HILO.
PST HAITARUHUSU UTUMIE WAAMUZI WA TPBC KWA KUTUMIA KIBALI ILICHOTOA.
TPBC TAYARI IMEFUTWA NA SERIKALI SOMA BARUA TPBC.
UNAWEZA KUOMBA KIBALI CHA TPBO MAANA NDIO CHOMBO KINGINE HALALI.

ASANTE,
EMMANUEL MLUNDWA
RAIS WA PST






FRANCIS CHEKA AMTANDIKA TENA MADA MAUGO KWA POINTI.




Bondia Francis Cheka amefanikiwa kumshinda bondia Mada Maugo kwa pointi.



Pambano hilo lilichezeshwa na waamuzi toka chama cha TPBC lisilokuwa la ubingwa, walimpa ushindi cheka kama ifuatavyo



mwamuzi wa kwanza alitoa matokeo ya sare kwa mabondia wote 98-98



Jaji wa pili alimpa Cheka ushindi wa pointi 99-98



na jajin wa tatu alimpa Cheka ushindi wa 100-98


Thursday, September 1, 2011

DIRISHA LA USAJILI LIMEFUNGWA NA HAWA NDO WALIOBAKI NA KUONDOKA.

Arteta has signed a four-year deal. No news on squad number but I'd tip him to wear Nasri's old No8....

Meireles is a Chelsea player. £12m fee - four-year deal

Yossi so happy at Gunners move

LUKA MODRIC staying at Tottenham

WESLEY SNEIJDER IS NOT LEAVING INTER MILAN

DONE DEAL - SHauen Wright-Phillips has signed for QPR.

JAN VERTONGHEN staying at Ajax.

Fulham have confirmed the free transfer signing of defender Zdenek Grygera on a one-year deal with an option for a further year.

CAHILL NOT GOING TO SPURS - CONFIRMED





Wednesday, August 31, 2011

COUNTDOWN YA KUFUNGWA KWA DIRISHA LA USAJILI NANI ANAENDA WAPI FUATILIA


ELIA AJIUNGA JUVENTUS

Mkataba wa miaka 4 kwa winga wa kiholanzi, na kibibi kizee cha Turin watawalipa Hamburg €9m kama ada ya uhamisho uliotangazwa rasmi leo.

Juventus wameendelea kukimairisha kikosi chao chini Antonio Conte baada ya kufanikiwa kumsajili Eljero Elia kutoka Hamburg kwa gharama €9m ambayo inaweza kuifikia €10m.

Elia, 24, ameshawasili Turin tangu jana jioni na leo atafanyiwa vipimo kabla ya kurejea kwenye kambi ya timu ya taifa ya Uholanzi.


PAVLYUCHENKO AOMBA KUONDOKA SPURS

Yakiwa yamebaki masaa mahache kabla ya dirisha usajili kufungwa Roman Pavlyuchenko amewashangaza Tottenham baada ya kuondoka klabuni hapo.

Mrussia huyo ambaye alikuwa anategemewa kusaini mkataba mpya msimu, lakini sasa ameamua kubadili mawazo baada ya kusajiliwa kwa Emmanuel Adebayor White Hart Lane.

“Wakala wangu yupo London, amekutana na mwenyekiti Daniel Levy kujaribu kutafuta namna ya kuondoka, lakini mpaka sasa bado hakuna makubaliano.Tulitoa wazo la kuniruhusu kuondoka kwa mkopo kwa miezi 6 lakini Levy amekataa.

“Nafahamu Sunderland wamekuwa wakinihitaji, nasubiri kuona itakuwaje.Nchini England maajabu yanatokeaga kwenye siku ya mwisho ya usajili hivyo kuna tumaini japo sio kubwa.” Roman Pavlyuchenko.



REDKNAPP: MODRIC ANABAKI, NAMTAKA CAHIL AND PARKER

Asubuhi ya mwisho kabla ya dirisha la usajili kufungwa saa 6 usiku leo, Harry Redknapp amesisitiza kwamba Luka Modric anabaki White Hart Lane.

Chelsea ambayo bado walibaki japo namatumaini kidogo ya kiungo huyo wa Croatia, lakini Redknapp leo asubuhi amemwaga sumu kabisa katika dili hilo: “Nina uhakika asilimia million Modric atabaki.” Aliiambia Sky Sports News.

Pia taarifa kutoka upande wa Tottenham zinasema kuwa timu hiyo imeweka mezani ofa ambayo inajumuisha pesa pamoja na kuwatoa wachezaji David Bentley na Sebastian Bassong kwa Bolton ili kuweza kumsainisha Gary Cahil mwenye thamani ya £17m.





Ingawa zimeendelea kutoka kauli za kukatisha tamaa ya usajili wa Wesley Sneijder kutoka kwa pande zote za Inter Milan na Man United, lakini sasa tukiwa na tumebakiwa na masaa machache kufikia kufungwa kwa dirisha la usajili barani ulaya, gazeti la Daily Star la nchini Uingereza linaripoti kuwa kiungo huyo wa kiholanzi anaweza kuwa mchezaji wa United muda wowote kabla ya saa sita kesho.

Taarifa zinasema mazungumzo kati ya timu ya wawalikishi wa Sneijder na United wamefanya mazungumzo na kuafikiana mshahara wa £190,000 kwa wiki ili mchezaji huyo atue @ Old Trafford.

Pia Daily Star imethibitisha kuwa Inter Milan wamewaambia United wapo tayari kushusha ada ya uhamisho kwa ajili ya Sneijder baada ya kufanikiwa kumsaini Diego Forlan huku wakiwa katika hatua za mwisho za kumsaini kiungo wa kiargentina kutoka Lazio Mauro Zarate.

Jana Kocha msaidizi wa United alikiri kuwepo kwa uwezekano wa Sneijder kutua Theatre of Dreams, alisema: “Penye nia siku zote kuna njia.Kama klabu tunamhitaji na mchezaji pia anataka kuja, hivyo lolote linawezekana.Mchezaji mwenye kariba ya Sneijder atatufaa vizuri sana.”



CHELSEA WATUMA OFA YA £30M KWA RIBERY

Chelsea wametuma ofa ya £30m kwa ajili wa star wa kifaransa anayeichezea Bayern Munich Frank Ribery.

The Blues boss Andre Villas-Boas ameamua kumgeukia Ribery katika kumsaka kwake world class playmaker baada ya kushindwa kumsaini Luka Modric kutoka Spurs, lakini Bayern Munich wameshaweka wazi hawatoijadili ofa isiyozidi £36m.Chelsea wapo tayari kumpa mkataba wenye thamni ya £10m kwa mwaka Ribery.

Sasa AVB lazima aamue ama kukubali kulipa pesa waitakayo Bayern auamkose mchezaji huyo.

Ribery ambaye alisajiliwa na Bayern akitokea Mersaille kwa ada ya £22m mwaka 2007 kwa sasa ndio mchezaji anayevuta kisu kirefu kuliko wachezaji in Bundesliga akipata mshahara wa £180,000 kwa wiki.


SCOT PARKER KWENDA WHITE HART LANE BAADA YA KUOMBA UHAMISHO

Scot Parker yupo njiani kujiunga na Spurs muda wowote kutoka sasa baada ya kuomba uhamisho kutoka West Ham United.

Kiungo huyo wa kimataifa wa England aliamua kuingilia kati uhamisho wake baada ya hatihati ya kuvunjika kwa mazungumzo kati Hammers na Spurs kwa kuandika transfer request.

Parker alisema: “Nimekuwa kwa miaka 4 na sitosahau sapoti niliyopewa.Kocha na bodi ya wakurengenzi wajaribu kunishawishi lakini katika stage hii ya career yangu nahitaji kucheza katika premier especially sasa ambapo nina nafasi kwenye timu ya taifa.

Spurs wanategemewa kulipa ada ya uhamisho isiyozidi £6m kumsaini Scot Parker.


PORTO NA CHELSEA WAKUBALIANA ADA YA UHAMISHO WA ALVARO PEREIRA

Star wa Porto Alvaro Pereira yupo njiani kukamilisha ndoto yake kwa kuhamia Stamford Bridge leo.

The Blues jana usiku walikubali kulipa ada ya £20m kwa ajili winga huyo anayecheza kwa pamoja na Luis Suarez kawenye timu ya taifa ya Uruguay.

Raisi wa Porto Pinto Da Costa ameweka wazi kuwa winga huyo aliwekwa nje kwenye mchezo dhidi ya Barcelona ili kumuhepusha na majeraha ambayo yangeweza kuharibu dili la uhamisho kwenda Chelsea.

Tuesday, August 30, 2011

UHAMISHO WA MKOPO WA LUKAKU KWENDA STOKE CITY WASHINDIKANA

Stoke City wamekataliwa kumsajili kwa mkopo mshambuliaji mpya wa Chelsea Romelu Lukaku.

Straika huyu wa kibelgiji ambaye amejiunga na The Blues kwa ada ya uhamisho ya £20m kutoka Anderlecht mapema mwezi huu lakini ana mpambano mkali wa kugombea namba kwenye kikosi cha kwanza Stamford Bridge.

Boss Andre Villas Boas alikuwa tayari kumpeleka kinda huyo Britannia Stadium kwa miezi 6 ili aweze kumrudisha mshambuliaji katika mzunguko wa pili wa msimu, lakini sheria za premier league zinasema mchezaji aliyenunuliwa na timu moja haruhusiwi kuuzwa kwa mkopo kwenda klabu nyingine katika wakati mmoja wa usajili (transfer window).


Huku Didier Drogba akitegemewa kuondoka mwezi January kwa ajili ya African Cup of Nations, Lukaku ndio anatajwa kuchukua nafasi yake na ndio maana AVB alikuwa tayari kumtoa kwa mkopo wa miezi 6 tu.

VALDES AVUNJA REKODI BARCELONA


Victor Valdes sasa ndio golikipa aliyechezea Barcelona mechi nyingi katika historia ya klabu hiyo baada ya kucheza kwenye mechi dhidi ya Villareal na kufanikiwa kufikia rekodi ya kipa wa zamani wa timu hiyo Andoni Zubizarreta ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa michezo wa Barca.

Valdes ambaye alianza kuichezea Barcelona mwaka 2002 na tangu msimu wa 2003/2004 amekuwa hana mpinzani katika milingoti mitatu ya Barca.

Mpaka sasa Valdes ameshalinda lango la Barca katika mechi 410 na amefungwa mabao 323.

Amecheza mechi 296 za La Liga, Champions league 82, 12 spanish cup, 4 Kombe la dunia la klabu, 5 Uefa Cup, 8 Spanish super cup, 3 European Super Cup.

Ameshinda makombe 17, yakiwemo matano ya La Liga, na matatu ya Champions League.

Barcelona 5-0 Villarreal: Guardiola abadili mfumo dhidi ya Villareal.


MFUMO WA BARCELONA KIUNDANI.
Barcelona waliifunga Villareal bila hururma kwa mabao 5-1 na kuwajibu wapinzani wao Madrid ambao waliwafunga Zaragoza mabao 6-0.
Pep Guardiola aliwakosa Dani Alves , Carles Puyol na Gerard Pique hivyo akamchezesha Eric Abidal na akawatumia Sergio Busquets na Javier Mascherano kwenye ulinzi.

Xavi Hernandez na David Villa waliwekwa benchi huku Thiago Alcantara, Cesc Fabregas na Alexis Sanchez wote wakianza .
Juan Carlos Garido alipanga timu ile ile ya Villareal iliyotegemewa na wengi ambapo Bruno Soriano alirudi kwenye sehemu yake ya kiungo baada ya kuwa amecheza kaka beki katikati ya wiki na Gonzalo Rodriguez alirudi kucheza beki.

Mchezo huu ulikuwa si wa ushindani kama ule uliozikutanisha timu hizi mwaka jana . Villareal walikuwa hawana mashambulizi kabisa na walifia mikononi mwa Barca kwa urahisi ambao hakuna aliyeutegemea.

MFUMO WA BARCA UKIWA UMETENGWA.
Kwanza, kulikuwa na mfumo usioeleweka uliotumiwa na Barcelona na ulionekana kufanya kazi uwanjani kwa kiwango kikubwa sana .

Mfumo huu ni wa 3-4-3 huku wachezaji wanne wa katikatiya uwanja wakicheza kwa mfumo wa ‘diamond’, ni wachezaji wawili tu ndio waliobaki kwenye sehemu zao muda wote nao walikuwa beki wa mwisho Sergio Busquets na kiungo mkabaji Seydou keita.
Eric Abidal na Javier Mascherano walikuwa wanaingia ndani kidogo wakati mwingine huku wakijaribu kuwarudisha nyuma Giuseppe Rossi na Nilmar. Viungo waliocheza nje Andres Iniseta na Thiago Alcantara walijaribu kucheza ndani wakati mwingine wakijaribu kubadilishana nafasi na Cesc Fabregas.


Kwa viungo wepesi kama hao na mkabaji mmoja ambaye ni Seydou Keita mfumo ulionekana kama 3-1-3-3 kwa muda mrefu wa mchezo.

Huku Barcelona wakiwa hawana kabisa mabeki wa pembeni au mawinga, wachezaji watatu wa mbele walizunguka zaidi na kuelekeza mipira pembeni mwa uwanja huku Sanchez na Pedro wakibaki sana pembeni kuliko kuingia ndani ghafla au bila kushtukiza. Kwa yote Mfumo huu ulionekana kuendana kidogo na mifumo ya kocha wa zamani wa Chile Marcelo Bielsa

Mfumo sahihi wa kucheza dhidi ya Villareal.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza ya Barcelona kwa msimu huuna kuna imani kubwa kuwa hii inaweza kuwa timu yao ya kwanza kwa msimu huu. Kuna tahadhari ya ziada inahitajika hapakwa kuwa Guardiola ana historia ya kucheza kwa kutuma mifumo isiyo kawaida kwa timu yake kwenye baadhi ya mechi ili kukabili kitu husika toka wapinznai wake.

Alichezesha mfumo wa 3-4-3 kwenye mchezo dhidi ya Atletico Madrid msimu uliopita kwa lengo la kuwasukuma mawinga wa timu pinzani kwenye eneo lao , pia aliwahi kumtumia Dani Alvez kama winga kwenye mechi dhihi ya Sevilla . Mara nyingi pia huwa anajaribu kitu tofauti kwenye michezo dhidi ya timu zenye washambuliaji wawili .
Mfumo huu hivyo ulikuwa sahihi kwa Villareal. Kwa kawaida wanachezesha mfumo wa 4-2-2-2 huku kukiwa na viungo wawili wanaocheza pembeni na wakati mwingine wanaingia ndani , na mara nyingine wanacheza 4-3-1-2, vyovyote ni mfumo ambao unabana uwanja .
Kwa kuanzia nyuma , Barca walikuwa na mtu wa ziada . Mascherano alikuwa anamkaba Rossi na Abidal alimkaba Nilmar kwani washambuliaji hao huwa wanacheza kila mmoja akienda upande wake pembeni mwa uwanja huku Busquets akiwa kama mtu wa mwisho asiye na jukumu maalum.


Hatari moja ya kucheza dhidi ya mfumo wa Villareal wa 4-2-2-2 ni kwamba wakati mwingine wanakuwa na viungo wa kati wanne ila kwa kuchezesha mfumo wa ‘diamond’ , Guardiola alikuwa anawakabili kwa kuhakikisha muda wote inakuwa vita ya 4v4 . Mbele zaidi mabeki wa pembeni wa Villareal ambao kwa kawaida huwa wanapanda kupunguza uwanja walibanwa na Pedro na Alexis Sanchez na hakuna mfumo bora zaidi ya huu wa kuutumia dhidi ya Villareal.



Timu zilivyoanza .
Ulikuwa mchezo wenye vita ya mifumo ndani yake.Kwa Barcelona mfumo wao ulikuwa na chembechembe nyingi za kufanana na ule wa Liverpool wakati Kenny Dalglish alipoiongoza timu yake kuifunga Chelsea mapema mwaka huu.

Carlo Ancelotti akiwa ndo kwanza amesajili Ferando Torres alichezesha mfumo wa 4-3-1-2 huku akiweka mtu wa ziada nyuma kusaidia ulinzi, Dalglish aliamua kuwapanga mabeki wa kati watatu huku akipanga viungo wanne ambao wanacheza kwenye shape ya’diamond’.
Tofauti ilikuwa mfumo wa Dalglish ulikuwa wa kasi zaidi ya ule wa Barca nah ii ni kwa sababu Liverpool kiasili hupendelea soka la mwendo wa kasi kama ilivyo kwaingereza wengi , Dalglish pia alitumia mawinga ambao ni mabeki na walifanya kazi ile ile ya mabeki wa pembeni.

Jinsi Barca walivyoshinda.
Bao la kwanza lilionekana kuwa la kiufundi haswa kwa kuwa lilikkuja toka kwa mchezaji wa Barcelona mwenye uhuru wa kufanya atakacho uwanjani.


Mfumo wa Villareal ulikuwa unatumia viungo wawili wakabaji, wakiwatumia Valero kama mharibifu wa mashambulizi ya wapinzani na mwenzie Cani akiwa mbali naye kkidogo pembeni uliwafanya Barca wamiliki mpira kirahisi.
Hili lilionekana kufanya kazi kwa kiasi Fulani mwanzoni pake ambapo Cani alionekana kama anaipenya ngome ya Barca, anaweza kuona kama anafanya jamba la msingi lakini katika hilo alikuwa anampa mwanya Thiago Alcantarra .

Hiyo ndio sababu kuu ya kwanini Alcantarra alipewa uhuru aliopewa katikati mwa uwanja, na madhara yake ni pale alipofunga bao rahisi ambapoa li-drible toka mbali hadi nje ya 18
Bao la pili lilionyesha mchango wa Cesc Fabregas kwenye timu hii.

Kitu ambacho wengi wanaweza kubisha ni ukweli kuwa Fabregas alikuwa anahitajika kwenye timu hii na ndio maana amekuja , msimu uliopita Barca walikosa mchezaji kama huyu. Alichokuwa anafanya Cesc ni kukimbia toka eneo la katikati mwa uwanja huku akifaidika na Movement za Lionel Messi.
Wakati mwingine Iniesta alionekana kufanya kazi hii japo anapenda kuingia ndani sana . Fabregas ni mtu sahihi wa kuiongezea Barcelona ‘movement’ za ziada katika ya uwanja-sio namba 10 wa asili lakini ni mchezaji anayependa kupandisha timu akiwapa presha mabeki . Uhusiano wake uwanjani na Messi unaonekana kufanya kazi vyema hadi sasa na ni rahisi kuona hivyo kwa kuwa amekuwa akifanya hivyo tangu akiwa Arsenal na Van Persie.
Fabregas anaweza kucheza kama ‘namba 9 wa uongo’ na wengine wameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa huenda akawa ‘namba 10 wauongo pia’.
Mabao matatu ya Barca ya kipindi cha pili yalikuja kwa kuwa Villareal waliweka mstari wa ulinzi eneo la juu sana na kwa hivyo wakajikuta wakinaswa kwa mtego wao wenyewe.

Mwisho

‘Perfomance’ nzuri toka kwa mabingwa watetezi wa ligi ya Hispania , ufundi hasa kwa Barcelona ulkikuwa wa hali ya juu. Angeweza kuwachezesha wachezaji wanne kwenye eneo la ulinzi labda angemrudisha Keita nyuma kidogo na kumuingiza kiungo kinda Anderu Fontas ila uamuzi wake wa kutumia 3-4-3 ulimlipa na ukawapa ushindi mzuri dhidi ya timu iliyowapa tabu msimu uliopita.
Je utakuwa mfumo mkuu wa Barcelona msimu huu? Labda . Ni muhimu kukumbuka kuwa walicheza na timu inayotumia mfumo huo huo Villareal.
Inaonekana kuwa kama Bracelona watatumia mfumo huu watajaribu kuchanganya na 4-3-3. Kama Pique na Puyol wakirudi kwenye ulinzi na kuwaruhusu Mascherano na Busquets kusogea juu kidogo , wanaweza kutumia mchanganyiko wa mifumo ya 3-4-3 au 4-3-3 huku wakiwa na bei wa kati anayecheza kwa kupandisha timu. Huu ni mfumo unaoweza kuzimudud timu zinazotumia ‘namba tisa’ wa uongo.

ARSENAL IMETANGAZA KUMSAJILI PARK



Arsenal have announced thaey have agreed to sign striker Chu Young Park from AS Monaco and Vladimir Weiss has left Manchester City and joined Spanish side Espanyol on a year long loan deal. The Slovakian winger has had previous spells away from City, at Bolton and Rangers.

OWEN HARGREAVES AKARIBIA AJIUNGA NA MANCHESTER CITY.


Owen Hargreaves akitoka kwenye Hospitali ya Bridgewater ambapo alifanyiwa vipimo vya afya kwa masaa matatu kabla ya kujiunga na Manchester City










Hiii ilikuwa mechi yake ya mwisho kuichezea Man utd.






hapa ilikuwa ni kipindi akifanya mazoezi makali.








































Wenger Anakaribia kumsajili kwa ada ya £8m beki Mjerumani Mertesacker baada ya kukamilisha usajili wa Andre Santos kwa ada ya £6.2m

Per Mertesacker



Andre Santos

Arsene Wenger anakaribia kumsajili beki wa kati Per Mertesacker kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 8,
Mapema leo Arsenal imekamilisha uhamisho wa beki wa kushoto Andres dos Santos toka Fenabahce ya Uturuk
Mertesacker anataraji kwenda jijini London kufanyiwa vipimo vya afya.

VIINGILIO STARS v ALGERIA,KIM AITA 30 TIMU YA VIJANA NA TWIGA STARS KUAGWA LEO,

VIINGILIO STARS v ALGERIA
Viingilio kwa ajili ya mechi ya mchujo kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Taifa Stars na Algeria vitakuwa kama ifuatavyo;

Viti vya kijani ni sh. 3,000, viti vya bluu sh. 5,000, viti vya rangi ya chungwa sh. 7,000, VIP C sh.10,000, VIP B sh. 20,000 na VIP A sh. 30,000. Tiketi zitaanza kuuzwa Septemba Mosi mwaka huu.

Taifa Stars tayari iko kambini tangu jana (Agosti 28 mwaka huu) na inaendelea na mazoezi Uwanja wa Karume ambapo wachezaji wote wa ndani waliripoti jana mchana na kuanza mazoezi jioni.

Wachezaji wan je waliofika jana usiku ni Abdi Kassim na Dan Mrwanda kutoka Vietnam na Mbwana Samata kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Athuman Machupa (Sweden), Henry Joseph (Norway) na Idrisa Rajab (Kenya) wanaingia leo jioni.

Nizar Khalfan wa Vancouver Whitecaps ya Canada ndiye atakayekuwa mchezaji wa mwisho kuripoti kambini. Khalfan atatua nchini kesho saa 5.15 usiku kwa ndege ya PrescisionAir akitokea Nairobi.

TWIGA STARS KUAGWA KESHO
Timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twigs Stars) inayoondoka Agosti 31 mwaka huu kwenda Maputo, Msumbiji kwenye michezo ya All Africa Games itakayofanyika nchini humo kuanzia Septemba 3-18 mwaka huu itaagwa kesho (Agosti 30 mwaka huu).

Twiga Stars wataagwa saa 6 mchana kambini kwao hoteli ya Itumbi iliyopo Magomeni Mwembechai, Dar es Salaam. Wakati huo huo Kocha Mkuu wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa leo ametangaza majina ya wachezaji 16 watakaokwenda Maputo.

Wachezaji hao ni Sophia Mwasikili, Fatuma Omary, Mwanaidi Tamba, Fatuma Bashiri, Mwajuma Abdallah, Asha Rashid, Mwanahamisi Omari, Pulkeria Charaji, Ester Chabruma, Zena Khamis, Fridian John, Fatuma Mustafa, Ettoe Mlenzi, Ftuma Khatib, Maimuna Said na Mwapewa Mtumwa.

Viongozi watakaofuatana na timu hiyo ni Mkwasa, kocha msaidizi Nasra Mohamed, daktari wa timu Dk. Gania Seif wakati Meneja wa timu hiyo ni Furaha Francis.

Mechi ya kwanza ya Twiga Stars itakuwa Septembe 5 mwaka huu dhidi ya Ghana wakati ya pili dhidi ya Afrika Kusini itachezwa Septemba 8 mwaka huu. Twiga Stars itacheza mechi yake ya mwisho katika hatua ya makundi Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe.

KIM AITA 30 TIMU YA VIJANA
Kocha wa timu za vijana Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 30 wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya mazoezi mwezi ujao.

Wachezaji walioitwa ni Saleh Ally (TSA), Jackson Wandwi (Azam), Hassan Kessy (Mtibwa Sugar), Khamis Mroki (Mtibwa Sugar), Yassin Mustapha (Polisi Dodoma), Andrew Kasembe (Moro United), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Ally Teru (Simba), Said Ruhava (Kagera Sugar), Samuel Mkomola (Azam), Frank Damayo (JKT Ruvu), Omega Seme (Yanga), Atupele Green (Yanga), Thomas Ulimwengu (ABC Sweden) na Jerome Lambele (Moro United).

Wengine ni Simon Msuvan (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Alex Joseph (Majimaji), Ibrahim Rajab (Azam), Renatus Patrick (Polisi Dodoma), Abdallah Kilala (AFC), Rajab Zahir (Moro United), Amani Kyata (TSA), Edward Shija (Simba), Alfred Amede (Russia), Khelf Hassan (Kenya), Emily Mgeta (TSC Mwanza), Ramadhan Salum (Simba), Frank Sekule (Simba) na Hassan Dilunga (Ruvu Shooting).

Nii Lamptey, Pele aliyepotezwa na kupotea



. Aliteswa na baba yake kila kukicha
. Alitapeliwa mamilioni na wakala wake
. Kila siku anajifungia chumbani akilia

ILIKUWA ni katika mji wa Motherwell Juni 1989 wakati kwa mara ya kwanza dunia ilipomtambua Nii Ordety Lamptey. Ilikuwa ni katika pambano la ufunguzi la michuano ya kombe la dunia kwa vijana chini ya umri wa miaka 16.
Akiwa na miaka 14, Lamptey alionyesha kiwango cha kuishangaza dunia wakati huo katika pambano la ufunguzi kati ya Ghana na Scotland lililokwisha kwa suluhu ya bila kufungana.
Wakati mfalme wa soka Ulimwenguni Pele akimkabidhi kikombe kidogo Lamptey mara baada ya kumalizika kwa pambano hilo ikiwa ni ishara ya kuchaguliwa mchezaji bora wa mechi hiyo, alijikuta akimsifu kuliko kiasi huku akisema huyo alikuwa kinda pekee duniani ambaye alifanana kwa kila kitu nayeye mwenyewe enzi za usakataji wa soka lake.
Lamptey alionekana kujiandaa na safari ya kufanya mambo makubwa duniani. Lakini katika historia ya kusikitisha kupindukia, leo miaka 20 baadaye, maisha yake ya soka yamemalizika kimya kimya.
Akiwa amecheza chini ya mechi 200 tu, Lamptey amekumbana na mikasa mizito na nuksi zilizopindukia katika namna ambayo mwenyewe amefikia hatua ya kuamini kuwa alitolewa mhanga au kurogwa na baadhi ya watu.
Hata hivyo, moyo wa Lamptey bado haujavunjika moja kwa moja. Ingawa bado analia kwa matukio mabaya yaliyomtokea, lakini sasa anaendesha shule jijini Accra akiwa amepania kuwafundisha wengine kutodanganywa kama ilivyotokea kwake.
Maisha yake kwa sasa yamebaki kuwa Shule tu. Ukiwa unatembea katika madarasa unaweza kuona yote ameyapachika majina ya nchi alizochezea soka ambazo ni Uholanzi, Ubelgiji, Uingereza, Italia, Argentina, Uturuki, Ureno, Ujerumani, China, Dubai, Afrika Kusini na mwishowe nyumbani Ghana.
Lakini mji wa Motherwell unasimama kama nguzo imara kwa sababu uliibua kipaji chake na kumuondoa katika historia ya kusikitisha iliyomgubika siku za utoto wake.
>Kipaji cha Lamptey kilikuwa wazi tangu angali akiwa mdogo. Tangu akiwa na umri wa miaka minane tayari klabu mbalimbali zilikuwa zinasaka saini yake. Akiwa na umri wa miaka 13 tu tayari alikuwa anacheza katika michuano ya vijana chini ya miaka 20.
Alikuwa mwepesi, mwenye nguvu, akili na kipaji kikubwa cha kuusoma mchezo. Alikuwa mfupi na mwenye uwezo wa ajabu. Lakini maisha yake ya Accra , mji mkuu wa Ghana hayakuwa rahisi. Yalikuwa magumu sana .
“Sikuwa na uhusiano mzuri wa kifamilia” anasema Lamptey. “Nilikuwa kila sehemu. Wakati mwingine nisingerudi nyumbani. Ningekwenda kucheza soka lakini kurudi nyumbani ingekuwa matatizo. Lazima ningepigwa na Baba, au kutumwa kwenda kuchota maji kabla ya kunipatia chakula. Wakati mwingine usiku ningelala chini ya gari au Kioski fulani na kesho yake maisha yangeanza upya tena. Maisha yalikuwa magumu kwangu hata katika hatua za mwanzo za maisha. Sijawahi kujua habari ya uhusiano wa baba na Mama”
Wazazi wa Lamptey waliachana wakati akiwa na miaka nane, na mwenyewe aliamua kumfuata baba yake aliyekuwa anaishi mji wa Kumasi .
“Kulikuwa na ndoa nyingine kwa baba na kitendo cha mimi kuwa pale kilikuwa tatizo. Mke wake hakunipenda. Baba yangu alizoea kunipiga lakini na mimi nikaanza kuzoea pia kupigwa na wala sikuwa nalia. Wakati mwingine angeweza kuvuita Sigara na kunichoma nayo.” Anasema Lamptey.
Mambo yalizidi kuwa magumu mpaka akaamua kuondoka zake nyumbani na kwenda sehemu ambayo alitafutiwa na klabu yake aliyokuwa akichezea wakati huo, Kaloum Stars. Hata hivyo, hilo lilizidi kumuweka pabaya kwa baba ambaye wakati huo alikuwa anatawaliwa na tabia ya ulevi.
“Walikuwa waislamu. Na kwa sababu hiyo ilibidi niwe muislamu. Ningeweza kwenda Msikitini kusali lakini baba angekuja na kuanza kunipiga”
Hata hivyo, nchi ya Scotland ndiyo iliyompa fursa ya kwanza ya maisha Lamptey kwa sababu kwa mara ya kwanza alipewa kiasi fulani kikubwa cha fedha, lakini pia alikutana na Steven Keshi, mwanasoka wa kimataifa wa Nigeria na klabu ya Anderletch ya Ubelgiji.
Keshi alimpa Lamptey kadi iliyokuwa ya maelezo ya wakala mmoja wa jiji la Lagos na kisha akamwambia kwamba kama angewasiliana vema na mtu huyo basi angeweza kumuandalia safari ya kwenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.
Huku klabu za Rangers, Vasco da Gama na Anderletch zikiwa zimevutiwa na kile walichokiona kutoka kwa Lamptey katika michuano hiyo, Chama cha soka cha Ghana kilikuwa bado kinataka kukiweka pamoja kikosi hicho mahiri wakati timu iliporudi Ghana .
Matokeo yake FA ya Ghana iliwanyang’anya wachezaji wote hati zao za kusafiria. Hata hivyo, Lamptey akiwa amepania kuondoka zake, alitumia nafasi yake vema wakati wachezaji walipovunja kambi ya mazoezi.
“Sikumwambia mtu yoyote, hata wazazi wangu. Nilichukua kiasi kidogo cha fedha nilichokuwa nacho na na kwenda kituo cha basi ambako nilikutana na dereva aliyekuwa anakwenda Nigeria ” anasema Lamptey.
“Nilimwambia yule dereva hivi ‘ebwana hali iko hivi, mimi sina hati ya kusafiria lakini nataka kwenda Lagos ’, akasema kuwa kama ningemlipa vizuri basi angesema kuwa mimi nilikuwa mwanae”
Kuanzia hapo, Lamptey alifanikiwa kukaa nyuma ya siti ya dereva akijisingia kuwa amelala kila walipopita katika mipaka ya nchi, kutoka Ghana , kupitia Togo na kwenda Nigeria .
“Kulizuka kasheshe kubwa nchini Ghana ” anasema Lamptey. Watu wa GFA na Kaloumu Stars walikuwa wamekasirika kwa sababu walikuwa wamempoteza mchezaji wao kipenzi.
“Ilibakia kidogo wamtie mbaroni baba yangu kwa sababu walihisi kuwa alijua sehemu niliyokuwepo. Nilipowasili Ubelgiji nilimpigia simu mama yangu na nadhani alikuwa katika wodi ya wazazi. Hakujua nipo wapi. Niliwasili Lagos na kumpa kadi dereva wa Taksi ambaye alinipeleka moja kwa moja mpaka katika nyumba ya wakala. Alimpigia simu Keshi ambaye wakati huo alikuwa Ubelgiji kumwambia kwamba nilikuwa nimewasili na nilimsikia Keshi akipiga makelele ya furaha”
Tatizo kubwa lilikuwa namna ya kumtoa Lamptey nje ya Nigeria . Baada ya siku chache Keshi aliwasili Lagos kwa ajili ya kucheza pambano la kimataifa la kirafiki. Huku akisingizia kuwa Lamptey alikuwa mwanae, Keshi alifanikiwa kupata hati ya kusafiria kwa ajili ya Lamptey na wakaenda zao Ubelgiji pamoja.
“Kila mtu alimjua” anasema Lamptey akimzungumzia Keshi “Kwa hiyo ilikuwa rahisi kupita uhamiaji. Tulipofika Ubelgiji kitu cha kwanza kufanya ilikuwa ni kutupa hati yangu ya kusafiria. Mimi ni Mghana kwa hiyo tuliwapigia simu maofisa na rais wa Anderlecht . Wao ni timu kubwa kwa hiyo wana nguvu sana . Nilikwenda katika ubalozi wa Ghana na wakanipa makaratasi”
Hata hivyo, bado alikuwa na kazi ngumu ya kuthibitisha kwa klabu yake kwamba alikuwa anastahili juhudi walizomfanyia.
“Mwanzoni Anderlecht hawakuwa na uhakika kama mimi nilikuwa Lamptey ambaye walikuwa wanamtafuta. Katika Luninga walikuwa wananiona mkubwa zaidi. Walibishana sana na Keshi na wakamwambia ‘Si yeye’ lakini Keshi akawaambia ‘Ndiye yeye’. Baada ya siku mbili tatu za kupumzika nikiwa nyumbani kwa Keshi, hatimaye nikaanza mazoezi na wachezaji wengine wa umri wangu.kila mtu alikuwa pale, maofisa wa bodi na Rais. Baada ya kuugusa mpira mara mbili waligundua kuwa nilikuwa Lamptey halisi”
Alisaini mkataba wa miaka mitano na Anderlecht na kwa wakati huo kila kitu kilikwenda sawa. Lamptey alicheza mechi 14 katika msimu wa 1990-91 na alifunga mabao saba kitu ambacho kilikuwa kinadhihirisha kipaji chake.
Wakati Ghana ikitwaa michuano ya kombe la dunia chini ya miaka 17, Lamptey alitajwa kuwa mchezaji bora wa michuano akiwashinda Juan Sebastian Veron wa Argentina na Alessandro del Piero wa Italia.
Alicheza mechi yake ya kwanza kwa timu ya taifa ya wakubwa mwaka huo huo na kuanzia hapo ndipo mambo yalipoanza kwenda kombo.
“Nilikuwa natapika damu uwanjani.” Anasema Lamptey huku lawama zake akizielekeza kwa wachawi wa klabu yake ya Ghana , Kaloumu Stars ambao aliamini kuwa walikuwa wamemroga ikiwa ni adhabu yake kwa kuitoroka timu hiyo. Lakini pia kulikuwa na matatizo mengine katika timu yao .
“Hakukuwa na umoja katika kikosi cha mwaka 1992. kingeweza kushinda kombe la dunia lakini kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yanaendelea. Niliwekwa matatizoni lakini niliamua kukaa kimya”.
Kuumwa, majeruhi na kushuka kwa kiwango chake kulipelekea Lamptey acheze mechi moja tu msimu wa 1992-93, lakini klabu ya PSV Eindhoven ikiwa inatafuta mchezaji wa kuziba pengo la Romario aliyeoondoka kwenda Barcelona ilikuwa imejiandaa kumchukua kwa mkopo msimu mmoja baadaye.
Msimu huo, kwa mujibu wa Lamptey mwenyewe anauelezea kama ni msimu bora katika maisha yake ya soka. Ingawa kilikuwa kipindi cha mpito wa PSV alifanikiwa kuwa mfungaji bora wa klabu akifunga mabao nane katika mechi 22 katika Ligi.
Kumbukumbu kubwa ilikuja katika pambano dhidi ya wapinzani wao Ajax ambapo alifunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1. Hata hivyo, pamoja na kuonyesha matumaini ya kuwa staa wa baadaye, PSV iligoma kulipa kiasi cha paundi milioni nane kumnunua Lamptey kama Anderlecht walivyotaka.
Mawakala walikuwa katika mazungumzo mazito, lakini mwishowe akajikuta akiangukia katika kikosi cha Aston Villa kilichokuwa kinafundishwa na kocha Ron Atkinson mwaka 1994. mwenyewe anasema ilikuwa ni kwa mkopo ingawa mpaka leo bado haieleweki vizuri.
Katika siku yake ya kwanza Aston Villa, Atkinson alimuita chemba na kumuuliza namna anavyotaka alipwe kiasi chake cha fedha za uhamisho. Lamptey alishangaa sana . Kamwe hakuwahi kusikia chochote kuhusu kiasi cha fedha za uhamisho hapo awali. Ndipo alipofahamu kuwa kumbe wakala wake alikuwa amemdhulumu kiasi cha fedha wakati alipozichezea Anderlecht na PSV.
“Niliwapa akaunti yangu na wakaniwekea fedha moja kwa moja. Wiki mbili baadaye wakala wangu alikuja kutaka kuchukua fedha hizo. Walimwambia kuwa fedha hizo nilikuwa nimepewa mimi moja kwa moja na alionekana kuudhika sana . Alisema watu wengi walikuwa wamo ndani ya dili hilo ”
Mpaka leo, Lamptey anamshukuru sana Atkinson na alimpigia simu ya kumtia moyo wakati kocha huyo alipokumbwa na kashfa ya kutoa maneno ya kibaguzi kwa mlinzi wa zamani wa Ufaransa, Marcel Desailly katika kituo cha televisheni cha ITV.
“Big Ron alikuwa mtu mzuri sana katika maisha yangu. Amenisaidia sana na namuheshimu mno. Namjua Big Ron, angeweza kufanya kitu kama hicho lakini asimaanishe. Wakati nilipokuwa Villa kulikuwa na wachezaji weusi kama John Fashanu, Dalian Atkinson, Ugo Ehiogu, Dwight Yorke na mimi mwenyewe. Vipi kuhusu ubaguzi? Ron ni mtu mchekeshaji, anapenda utani. Labda alisema hivyo lakini hakumaanisha”
Katika kipindi chake akiwa Villa, Lamptey alihitaji msaada wa Atkinson, wakati akijaribu kujenga upya uhusiano wake na baba yake mzazi.
“Baada ya kusafiri kiasi alijua nilichotaka kwa hiyo alitulia kidogo. Baba yake alipenda kunywa pombe na hilo lilikuwa tatizo. Siku moja nilirudi nyumbani likizo nikamkuta amelewa chakari huku akiwa amezimia. Nilimchukua katika hospitali ya kulipia na wakamtibu vizuri. Madaktari walimwambia aweke ahadi kuwa hatakunywa tena. Walimwambia ‘bila ya mwanao ungekufa kwa sababu ini lako lilishapoteza nguvu”
Lamptey alikuja kufunga ndoa, lakini hilo lilileta matatizo zaidi. “Kitendo cha kukutana na mke wangu Gloria kilikuwa ni tatizo jingine. Wengi walipinga. Wazazi wangu walipinga, sijui kwa nini?”. Marafiki zake pia kutoka Kumasi walipinga suala hilo .
“Watu wote hawa walitaka nioe mtu kutoka katika familia zao. Walisema nisimuoe angeniibia fedha zangu tu. Baadaye wakaniuliza kwa nini nina haraka. Waliniambia ningeweza kumuoa mtoto wa Rais kama ningetaka”
Katika soka mambo yalianza kumuendea kombo. Lamptey alijikuta akipata wakati mgumu kuzoea soka la Kiingereza huku pia akishindwa kumudu majukumu ya timu ya taifa.
“Ron ilibidi agombane na FA ya Ghana . Nilikuwa nachezea timu ya taifa chini ya miaka 20, na pia nilikuwa nachezea timu ya chini miaka 23. unaweza kufikiria mzigo niliokuwa naubeba? Ilikuwa hatari sana .”
Atkinson alifukuzwa Villa mwaka 1994, lakini haraka haraka akachaguliwa kuwa kocha wa Coventry City . Ingawa Lamptey alikuwa ameichezea Villa mechi 10 tu, lakini Atkinson alikuwa na imani naye na akamsajili Coventry . Hata hivyo, Lamptey alikuwa karibu sana na baba yake.
“Tulikuwa karibu tena katika mwaka ambao nilichezea Coventry . Halafu akafariki dunia. Nilikuwa nimemnunulia nyumba na alikuja kuishi na mimi. Kitu kimoja alichoniambia ni kwamba alitamani niache imani ya Kiislamu na ndiyo maana niliacha. Kwa sasa mimi ni Mkristo kamili”
Kifo cha baba yake kilisababisha Lamptey ajikute katika wakati mgumu katika mahusiano na wanafamilia wenzake.
“Nilikuwa England wakati niliposikia kuwa amefariki, kwa hiyo nilirudi na ilibidi nimzike peke yangu. Sisi kina kaka hatuko pamoja. Sidhani kama ni wivu lakini huwa hatuwi pamoja. Nilikuwa na kitu mfukoni kwa hiyo kaka zangu na mama walikuwa wananitazama mimi. Unajua barani Afrika, watu wakijua una fedha wanakuachia kila kitu. Hata mama yangu nilimzika peke yangu. Nimepitia katika matatizo makubwa”
Kulikuwa na matatizo pia katika mahusiano ya Lamptey na timu ya taifa ya Ghana sana sana baada ya kutolewa nje katika pambano la nusu fainali za kombe la mataifa ya Afrika mwaka 1996.
“Katika kombe la mataifa ya Afrika kuna kitu cha kusikitisha kilitokea.” Anasema Lamptey.
Ingawa katika maongezi haya alionekana kuwa muwazi, lakini kusita kwake kuelezea kitu kilichotokea kunadhihirisha kwamba tukio hilo lilikuwa kubwa sana huku pia likimuhusisha nyota wa zamani wa Ghana na timu ya Marseille ya Ufaransa, Abeid Pele.
“Mimi na yeye si marafiki kabisa. Anajua kwa nini”
Lamptey aliichezea Coventry mechi sita tu kitu ambacho kilisababisha kibali chake cha kazi kisiongezwe muda. Aliondoka na kwenda zake Venezia. Kiwango chake kilikuwa cha hali ya chini sana . Akiwa amevunjika moyo huku akiwa anajaribu kuishi katika nchi ya nne ndani ya kipindi cha miaka minne alihamia Boca Junior huku bado akijua kwamba ulikuwa ni mkopo tu kutoka Anderlecht .
Wakati huo alikuwa anaonekana kama mchezaji wa kigeni wa tano wakati ni wachezaji wanne tu waliokuwa wanaruhusiwa. Hatimaye alipelekwa Union de Santa Fe . Ilikuwa ni wakati yupo hapo ndipo mtoto wake wa tatu alipozaliwa na kumpa jina la Diego ikiwa ni heshima yake kwa Maradona.
“Alizaliwa mwezi mmoja kabla. Madaktari walisema kuwa alikuwa hana tatizo, lakini baada ya wiki mbili tukiwa nyumbani matatizo yalianza. Kama angelia ungeweza kuona machozi tu yakitoka, lakini usingesikia kilio.” Madaktari walishangaa sana na walimwambia aende katika hospitali kubwa jijini Buenos Aries
“Ilibidi nisimame kucheza mpira na mimi na mke wangu pamoja na watoto wetu wawili ilibidi tumwangalie mtoto kwa karibu. Tulipanga katika hoteli iliyokuwa karibu na hospitali. Madaktari walifanya kila walichoweza, walichukua vipimo vyote, lakini hakuweza kupumua. Alikuwa pale kwa miezi miwili na nusu kwa hiyo alikuwa na miezi minne wakati alipofariki huku akiwa katika usimamizi wa hali ya juu” katika tukio hili, Lamptey anaamini kulikuwa na ushirikina ndani yake.
Akiwa amevunja mkataba wake, Lamptey alirudi kwanza Ghana kabla ya kwenda tena Ulaya ambako aligundua kuwa hakuwa na mkataba tena na Anderlecht . Mpaka sasa hajui kilichotokea lakini inaonekana kuwa wakala wake alikuwa amemnunua na kummiliki bila ya yeye mwenyewe kujijua.
Alifanikiwa kuvunja mikataba yote na kubaki mwenyewe ingawa mpaka sasa hajui kabisa kilichotokea wakati akihamishwa kutoka timu moja kwenda nyingine miaka ya 1990. bado hajielewi mpaka leo na ingawa ana uwezo wa kuongea lugha tisa, anajichukulia kama mtu asiyeweza kuandika walau barua tu.
Klabu ya Ankaragacu ya Uturuki ilimchukua, lakini kiwango chake bado kilikuwa chini sana . Baadaye alikwenda Uniao Leiera ya Ureno na kisha Greuther Furth ya Ujerumani. Aliichezea timu hii mechi nyingi zaidi (36) kuliko timu nyingine yoyote. Lakini janga jingine lilitokea.
Mkewe Gloria alimzaa mtoto mwingine wa kike, Lisa. “Ilikuwa ni kama mwanzo. Mtoto huyu pia alikuwa na miezi minne wakati alipofariki.” Hakutaka kujihatarisha kutafuta mtoto mwingine, lakini Gloria alimshawishi na sasa ana mtoto mwingine wa kike ambaye atatimiza miaka minne mwaka huu.
Lamptey alikwenda Dubai na China akijaribu kuendelea kutafuta maajabu yake ya soka la utotoni bila ya mafanikio. Mwishowe alirudi nyumbani kuichezea timu ya Asante Kotoko ya Kumasi .
“Niliamua kurudi nyumbani na kusajili katika timu moja ambako nilicheza kwa miezi sita kwa ajili ya kutengeneza CV yangu tu. Nilitaka kufanya hivyo. Nilikuwa niko sawa pale, lakini kama unavyowajua Waghana, siku zote matazamio yao yako juu. Mengi yalisemwa. Walisema nilikuwa nafanya hivyo kwa sababu nilikuwa nataka kurudi katika timu ya taifa.”
Kotoko ilichukua ubingwa wa Ligi na Lamptey akaamua kujiunga na klabu ya Jomo Cosmos ya Afrika Kusini. Mwishowe aliamua kuachana na soka baada ya kusmbuliwa na goti lake.
Alikuwa na miaka 31 na kama angeweza kufanya vitu vyake basi ingekuwa rahisi tu kwake kuichezea timu ya taifa ya Ghana katika kombe la dunia.
“Majuto?, najua kama watu wangeachana na mimi, kama Mungu alivyoniumba, sasa hivi ningekuwa nachezea Real Madrid. Lakini watu walitaka nianguke. Mambo mengi…..”
Mapema mwaka huu, Lamptey alirudi katika soka kama kocha msaidizi wa Eleven wise Men . Maumivu ya mchezo wa soka bado anayo na fikra za angekuwa nani kama angefanikiwa bado ziko katika kichwa chake.
“Wakati mwingine nitakuwa katika chumba changu na nitalia. Unajiona kwamba kuna kitu unaweza kufanya lakini kitu hicho kimechukuliwa kutoka kwako. Inauma sana . Lakini utafanya nini? Kuna uchawi katika soka.
“Nakumbuka nilikuwa Kumasi wakati nilipokutana na mke wangu, watu fulani, Waislamu ambao nilikuwa nasali nao walikuwa wanawaambia watu ‘Tutaona kama ataichezea timu ya taifa tena’. Na imekuwa kweli. Tangu mwaka 1996 sijaichezea Ghana na labda, labda, labda haikuwa sehemu yangu”.
Badala yake anaamini kuwa labda sehemu yake ilikuwa kuendesha shule yake na kuwapa elimu vijana wa Ghana ambayo yeye alinyimwa

Monday, August 29, 2011

FORLAN ATHIBITISHA KUJIUNGA NA INTER MILAN


Diego Forlan amethibitisha kuwa atajiunga na Inter Milan baada ya muda wake wa kubaki Atletico Madrid kuisha.

Uruguay straiker mwenye umri wa miaka 32 amefanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza kwamba hatoendelea kuwepo ndani ya Uwanja wa Vincente Calderon kama mchezaji wa Atletico na sasa anaelekea jijini Milan kuitumikia klabu inayotumia uwanja wa Giuseppe De Maeaza.

Forlan sasa atasafiri kueleka Milan ambapo atafanyiwa vipimo vya afya na baadae kusaini mkataba wa kuitumikia Inter Milan.

“Naenda kujiunga na klabu kubwa na kuna changamoto kubwa mbele yangu.Nataka kumshukuru Massimo Moratti kwa nafasi hii.

“Nimeshaongea na Estaban Cambiasso na Diego Milito, wote ni marafiki zangu.Naifahamu Serie A kwa kuwa nimeshaangalia mechi nyingi kwenye TV na nina furaha kubwa kucheza nchini Italia baada ya Premier League na La Liga.” – Forlan

WIKI YA WAKALI WA HAT-TRICKS BARANI ULAYA



Michezo ya iliyochezwa weekend hii katika ligi mbalimbali barani ulaya.Kuanzia kwenye Bundesliga, La Liga, mpaka kwenye Barclays premier league tumeshuhudia nyota kama Wayne Rooney, Edin Dzeko, Cristiano Ronaldo, Roberto Soldado na Maria Gomez wakifunga zaidi ya mabao 15 ndani ya wikiendi hii.




CRISTIANO RONALDO – REAL MADRID (LA LIGA)



Akicheza mechi yake ya kwanza ya La Liga, winga wa kimataifa wa Ureno Cristiano Ronaldo alifanikiwa kufikisha idadi ya magoli 102 tangu ajiunge na Real Madrid miaka 2 iliyopita.


Cristiano Ronaldo alifunga hat-trick katika mchezo huo dhidi Zaragoza, na kufikisha jumla ya hat tricks 9 tangu atue Santiago Bernebeu.




EDIN DZEKO (MAN CITY – EPL)



Baada ya kuhangaika kutafuta fomu yake msimu uliopita, mshambuliaji kutoka Bosnia Edin Dzeko amezidi kuwakata mdomo wote waliokuwa wana mashaka na uwezo baada ya jana kufunga mabao manne katika ushindi wa mbao 5-1 dhidi ya Tottenham Hotspur.


Dzeko ambaye alianza msimu kwa kufunga moja ya mabao katika mechi ya ngao ya hisani dhdi ya Manchester, kwa sasa ndio anaongoza kwa ufungaji katika premier league akiwa na magoli 6.




ROBERTO SOLDADO – VALENCIA (LA LIGA)




Mshambuliaji wa zamani Real Madrid nae alifuata nyayo za Cristiano Ronaldo baada ya kuisaidia Valencia kuitandika Racing Santander kwa mabao 4-3 kwenye mchezo wa ufunguzi wa La Liga.


Soldado ambaye alilewa kwenye academy ya Real Madrid kabla kufanikiwa kuichezea Real Madrid B, baadae akafanikiwa kupanda mpaka kikosi cha wakubwa na alicheza kwa mechi takribani 11, na kufunga mabao mawili kwenye La Liga pekee, baadae akapitia kwenye timu kama Osasuna, Getafe na sasa yupo Valencia.


Mpaka sasa Soldado ameshafunga jumla ya mabao 63 katika michezo 141.




MARIO GOMEZ – BAYERN MUNICH (BUNDESLIGA)



Bayern Munich walienda kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Ujerumani baada ya ushindi wa 3-0 dhidi Kaiserslautern, shukrani kwa mtoto wa nyumbani Mario Gomez aliyefunga mabao yote.


Mshambuliaji huyo wa Ujerumani ambaye alifunga goli pekee katika mchezo dhidi ya FC Zurich alianza kwa kufunga kwa penati dk ya 37 na baadae akafunga mengine mawili kipindi cha pili.


Gomez ambaye ndiye mchezaji ghali zaidi kwenye Bundesliga, alikuwa mfungaji bora katika msimu uliopita wa ligi hiyo kwa kufunga mabao 28.




WAYNE ROONEY – MANCHESTER UNITED



Siku ya jana itakuwa ni siku ya kukumbukwa kwa Wayne Rooney baada ya kufunga mabao 3 katika ushindi wa 8-2 wa Man United dhidi ya Arsenal.


Hat-tricks ya jana ilikuwa ya 6 tangu ajiunge na United, akifikisha jumla ya mabao 152 akiwa Old Trafford na kumfanya aweze kuingia katika vitabu vya historia ndani ya United kwa kuwemo kwenye orodha ya wafungaji bora 10 wa muda wote wa klabu hiyo.



Pia jana Rooney aliendeleza historia yake ya kuifunga Arsenal, Rooney alifunga bao la kwanza kabisa akiwa na Everton dhidi ya Gunners in 2002, na pia Baba Kai alifunga bao la kwanza la EPL na goli 100 akiwa na United katika mechi dhidi ya Arsenal.