Search This Blog

Saturday, April 14, 2012

JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI JANGWANI

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS



Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAMBIRAMBI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti  wa klabu ya mpira wa miguu ya Young Africans Sports Club (Yanga)  Bw. Lyod Nchunga kufuatia kifo cha Mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji, wakili Theonist Rutashoborwa, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kutokana na ugonjwa wa Shinikizo la Damu na Kisukari.

“Nimepokea kwa Masikitiko na huzuni sana taarifa za wakili Theonist Rutashoborwa kilichotokea usiku wa Kuamkia leo, hili ni pigo na pengo kubwa katika klabu ya Yanga katika kipindi hiki cha kushiriki ligi kuu” Rais amesema.

“Naomba unifikishie rambirambi zangu za dhati kwa familia, wachezaji na wana Yanga wote kwa kuondokewa na Mjumbe wao katika kipindi hiki” Rais ameongeza na kuwataka wana Yanga wawe wavumilivu wakati wa msiba huu na kumuombea Bw. Rutashoborwa mapumziko mema ya Milele.

……………Mwisho…………



Imetolewa na Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi.

Ikulu-Dar-Es-Salaam

12 April, 2012

RASMI SASA TBL WADHAMINI WAPYA TAIFA STARS

Meneja wa Kilimanjaro Beer, George kavishe kushoto
BIA ya Kilimanjaro Premeum Lager rasmi ndio mdhamini mpya wa timu ya taifa ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, bongostaz imeipata hiyo.
Bia hiyo inayozalishwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wiki hii itafanya hafa maalum ya kuutangaza rasmi udhamini huo.
Chanzo cha habari kutoka TBL, kimesema hafla hiyo itafanyikia katika hoteli ya Serena, iliyokuwa Royal Palm Movenpick, Dar es Salaam wiki hii.   
Tangu mwaka 2006, Taifa Stars imekuwa ikidhaminiwa na Serengeti Breweries Limited ambao wameshindwa kuingia mkataba mpya na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kwa sababu ya kupandishiwa dau.  
Baada ya mkataba wao (SBL) kufikia tamati Desemba, mwaka jana, TFF ikaipandishia dau la udhamini kutoka Sh. Bilioni 1.2 hadi Bilioni 3.6, ambayo ni zaidi ya asilimia 300.
TBL imekubali kuidhamini Stars kwa dau la Sh. Bilioni 3.6 kwa mwaka.
Kilimanjaro pia ni wadhamini wa watani wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga na mashindano ya Kombe la Taifa, Kili Taifa Cup.

Prisons, Mlale JKT zagawana pointi

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
Timu za Tanzania Prisons ya Mbeya na Mlale JKT ya Ruvuma zimetoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa fainali za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa leo (Aprili 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini hapa.
Kwa sare hiyo Tanzania Prisons imefikisha point inane wakati Mlale JKT inazo tano. Timu tatu za kwanza katika fainali hiyo ya 9 bora zitapanda kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao.
Mlale JKT ndiyo walioanza kufunga dakika ya 61 kwa mpira wa adhabu uliopigwa nje ya eneo la hatari na mshambuliaji Edward Malimi katika mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Shabani Shata kutoka Kigoma.
Dakika sita kabla ya filimbi ya mwisho beki Richard Mwakalinga aliisawazishia Tanzania Prisons inayofundishwa na Stephen Matata baada ya kufanya shambulizi kubwa langoni mwa Mlale JKT.
Hadi tuna kwenda mitamboni, mechi ya pili kati ya Rhino Rangers ya Tabora na Mbeya City ya Mbeya ilikuwa ikiendelea huku Rhino Rangers ikiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya 18 na kiungo Salum Tabayi.
Ligi hiyo inaendelea leo (Aprili 15 mwaka huu) kwa Mgambo Shooting ya Tanga inayoongoza ikiwa na pointi 11 kuivaa Polisi Tabora yenye pointi nne. Mechi ya pili itakuwa kati ya Polisi Morogoro yenye pointi kumi na Polisi Dar es Salaam yenye pointi sita.

SAMATA NA ULIMWENGU KUANZAMAZOEZI - UONGOZI WA MAZEMBE WAKANA SAFARI YA DAR KUCHEZA NA SIMBA.

Uongozi wa timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) umesema taarifa kuwa ina mpango wa kuja nchini kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Simba hazina ukweli na wameshangazwa na taarifa hizo.

Mdhamini wa zamani wa Simba, Azim Dewji alisema katikati ya wiki hii jijini Dar es Salaam, kwamba alikuwa akifanya mipango ya kuileta timu hiyo ya DRC kuja nchini kujipima nguvu na Wekundu hao wa Msimbazi.

Mbali ya uongozi wa Simba kutoa taarifa za kutoutambua ujio huo, Kocha Msaidizi wa TP Mazembe, David Mwakasu alisema hawana ratiba ya kuja Tanzania kwa ajili ya mechi hiyo na kuonyesha kushangazwa na taarifa hizo.

Mwakasu alisema kwa njia ya simu kuwa timu yao inakabiliwa na mechi ngumu wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya timu ya El Marreikh ya Sudan Kaskazini uliopangwa kuchezwa Uwanja wa Stade de la Kenya wa Jimbo la Katanga mjini Lubumbashi na wiki mbili badaye itacheza mechi ya marudiano mjini Khartoum.

Alisema kama msaidizi wa Kocha Mkuu, Lamine Ndiaye hawajapokea taarifa zozote kutoka kwa uongozi kuhusiana na mechi hiyo.
Sisi ndiyo tunaotoa taarifa kwa uongozi kuwa tunahitaji mechi za kirafiki kwa ajili ya kujua uwezo wa wachezaji wetu, hatujawahi kuzungumzia mechi dhidi ya Simba na wala uongozi haujatoa taarifa kwetu kama kuna maombi hayo, alisema Mwakasu.

Alisema wanafahamu wanakabiliwa na kibarua kigumu na lazima wawe makini katika mechi dhidi ya El Merreikh ambapo mshindi ataingia hatua ya makundi (robo fainali). Timu hiyo leo inacheza mchezo wake wa tano wa Ligi Kuu ya DRC dhidi ya timu ya AS Vita mjini Kinshasa. 

Mbali ya hayo, Mwakasu alisema mchezaji wao, Mbwana Samatta ameanza mazoezi madogo kwa ajili ya kuumia kwenye mechi dhidi ya Dynamo ya Zambia iliyochezwa mjini Lusaka.
Alisema kuwa wanamfuatilia kwa umakini mchezaji huyo ili aweze kurejea uwanjani kwani wanathamini mchango wake unaotokana na uwezo wake mkubwa uwanjani na hasa katika kufunga.
Kuhusiana na Thomas Ulimwengu, kocha huyo alisema alikuwa majeruhi muda mrefu na alitarajia kuanza mazoezi madogo madogo.
Wote ni majeruhi, lakini tulitarajia waanze mazoezi madogo madogo, alisema. Hata  hivyo Ulimwengu alitarajiwa kuwasili nchini jana kujiunga na kambi ya timu ya taifa ya chini ya umri wa miaka 20 kwa ajili ya mechi ya kufuzu dhidi ya Sudan Kaskazini.

source: mwananchi.co.tz

PELE: MTU NAMBA MOJA ANAYECHUKIZWA NA MAFANIKIO YA LIONEL MESSI



Pindi unapokaa na kufikiri - labda mchezaji bora wa muda wote - asingeweza kusema kitu chochote tena cha kumkosea heshima au kumdharaulisha Lionel Messi, lakini ameongea ujinga tena kumuhusu Messiah wa soka wa zama hizi.

Je hii itaisha?

Hivi karibuni katika press conference ya kusherehekea mafanikio ya soka ya Santos , mchawi wa soka maarufu kama Pele amesema tena maneno ya kumshusha Messi kwa kusema hivi:

"Sasa kila mtu anaongea kuhusu Messi, yule ni maarufu. Lakini kwa Messi kuwa ndio mchezaji bora wa muda wote, inabidi lazima kwanza ampite au awe bora kuliko Neymar."

OK, mtu aniambie ni lini Neymar alimpita au kufikia uwezo wa Messi kama mchezaji bora katika dunia? Labda mie sipo katika ulimwengu wa Pele, inawezekana nilipitiwa na usingizi kwa takribani miaka kadhaa nikakosa kushuhudia Neymar akimpita kwanza Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo na hatimaye Lionel Messi na kuwa mchezaji bora wa dunia.

Pele pia alisema kwamba hana kinyongo chochote dhidi ya mtu mwingine anayesemwa na watu wengine kama mchezaji bora wa muda , Diego Maradona.

"Nyie waandishi wa habari siku zote mnasema kwamba mmi ni hasimu wa Maradona, lakini sio kweli. Sijawahi kuwa hasimu wake, na yeye alikuwa kiungo mzuri dimbani."

Sijui hata nianzie wapi?

Sitaki kuamini wala kusema kitu ambacho kipo wazi kabisa, lakini hata chizi ambaye anafuatiliwa soka atakuambia Lionel Messi ndio mchezaji bora katika dunia kwa sasa. Huku wengine wakidiriki tayari ni mchezaji bora wa muda wote .

Naelewa Pele anataka kumsifu na kujiletea sifa kwa Neymar. Pele anataka mbrazili awe mchezaji bora duniani, lakini hii sasa inafikia katika pointi ambapo Pele anaanza kupoteza heshima ya mashabiki na maoni yake ya kipambavu na yenye majivuno.

Pele siku zote ataendelea kuheshimika kwa mchezaji wa soka aliyekuwa, lakini anapoteza heshima kwa kutomuheshimu na kumdidimiza Lionel Messi.

Huu uhasama wa Brazil vs Argentina umekuwepo kwa miaka mingi sasa na utaendelea. Kwa hakika mie mwenyewe sitaki uhasama huo upotee. Nani hapendi upinzani wa jadi wa soka la kimataifa - kama vile England vs Germany, Italy vs France au Nertherlands vs Germany?

Lakini kitu ambacho kinaniudhi mimi na mashabiki wengi wa soka, pamoja na kuwa ushabiki tofauti au utaifa , kama mchezaji wa mchezo wowote anastahili kuitwa mchezaji bora, inabidi apewe heshima yake kama mchezaji bora wa mchezo huo. Hakuna kitu chochote kibaya kwenye hilo.

Sasa kwanini Pele asiweke utaifa pembeni na kumtambua pamoja na kumpa heshima yake Messi kama mchezaji bora katika soka hivi sasa?

Pengine wachache kati yenu mnaweza kusema Neymar ni bora kuliko Messi ndio kitu kweli anachoamini. Stop it! Pele anaujua ukweli. Labda Pele ni kipofu - kitu ambacho nina uhakika sio ukweli kwa sababu alisema Messi ni maarufu, hivyo amemuona akicheza soka - sasa ni vipi anaweza kuamini Messi siop mzuri kuliko Neymar?

Sina kinyongo wala tatizo lolote na Neymar; ni mchezaji mwenye kipaji kizuri. Lakini katika kila kitu Leo anachofanya uwanjani - rekodi zote anazozivunja, makombe yote ambayo ameisadia Barcelona kushinda; yote akiyafanya akiwa na miaka 24 tu - ama kwa hakika Messi ndio mchezaji bora wa dunia kwa sasa. Je ni vipi Pele hayaoni haya?

Kinyongo cha Pele kwa Messi kimeanza muda mrefu uliopita. Kumekuwepo na muda ambapo Pele alizungumza maneno ya kumkejeli Messi, pia alipoulizwa anadhani kwamba Messi atakuja kuwa mchezaji bora wa muda wote Pele alijibu, " Kipindi Messi atakapofunga magoli 1,283 kama mimi, pindi atakaposhinda makombe matatu ya dunia, hapo ndipo tutakapoongea."

Muda mwingine, tena Pele alisema kwamba Argentina inahitaji kuamua nani ndio mchezaji bora kutoka nchini kwao - Maradona au Messi kabla ya kuwepo kwa mjadala nani ndio mchezaji bora wa muda wote. Inawezekana alisema hivyo ili kuonyesha dharau kwa Argentina, lakini mimi naona hapa alikuwa anatoa sifa, Arentina imetengeneza wachezaji azuri ambao lazima waingie katika listi ya wachezaji bora wa muda wote.

Kigezo kingine Pele anachokitumia kumkandamiza Pele ni mafanikio katika timu ya taifa.

Messi hahitaji kushinda makombe matatu ya dunia, lakini anahitaji kuiongoza nchini yake kushinda katika mechi kubwa, zaidi labda katika World Cup.

Hivi itakuwaje ikiwa Messi ataweza kuiongoza Argentina kushinda kombe la dunia mwaka 2014? Kushinda kombe ndani ardhi ya Brazil - wenyeji wa mashindano, Nyumbani kwa akina Pele na nchi hasimu mkubwa wa soka wa Argentina - fikiri Pele atauweka wapi uso wake. Hapo ndipo vita yake ya maneo kumdidimiza na kumkosea heshima Messi itakapoisha pia pamoja na kumaliza ubishi nani ndio mchezaji bora wa muda wote.

Lionel Messi hajawahi au hatowahi kumjibu Pele na maoni yake. Hayupo hivyo, lakini kitu muhimu kabisa, Messi ameacha uwezo wake wa uwanjani kujibu mashabulizi yake yote.

Diego Maradona anamtetea Messi na pia amekuwa akimjibu Pele. Diego nae kama huwa anajibu "Mchezaji wa nchi yangu ni mkali kuliko wa nchi yenu."
Lakini tofauti na Pele, Maradona ana pointi anaposema mchezaji bora wa dunia anatokea nchini kwao.

Labda Pele amuulize Neymar nani ndio mchezaji bora wa dunia.

"Siku zote nimekuwa nikisema Lionel Messi ndio mchezaji bora wa dunia." - Neymar

Pamoja na haya yote lakini bado Pele ameendelea kumkosea Messi, na inasikitisha kwa jinsi anavyojishushia heshima kwa maoni yake ya kijinga juuu ya Lionel Messi.  Ikiwa bado anaendelea kuamini kwamba Neymar ni bora kuliko Messi labda ni kweli Pele haangalii La Liga, UEFA Champions League au vipindi vya michezo ulimwenguni- au inawezekana vyombo vya Brazil haviaandiki wala kuonyesha habari zinazomhusu Messi kama ambavyo wanafanya kwa Neymar.

Lakini tuache utani pembeni, Pele anaujua ukweli chini ya uvungu wa moyo wake kwamba Lionel Andres Messi ndio mchezaji bora wa duniana anaweza kuja kuwa bora wa muda wote. Hilo linamuumiza zaidi na tena sana kwamba mtu fulani atakuja na kuuteka ulimwengu wa michezo - sio tu soka, na kuheshimika, kusifiwa na kupendwa na wengi.

Inawezekana Maradona hakuwa anapendwa na wachache na kutoheshimwa na wengi, kwa goli lake la mkono wa mungu, tabia chafu, matumizi ya madawa ya kulevya na mdomo mchafu uwanjani.

Messi anaweza akawa hapendwi na baadhi, lakini tofauti na Maradona, Messi anaheshimika dunia nzima.

Baadhi ya watu wamesema kwamba Pele ana wivu dhidi ya Messi. Mimi nafikiri Pele ana wivu na umaarufu wa Messi ambao umefikia hatua mpaka watoto wa baadhi ya wachezaji wa timu pinzani mfano watoto wa John Terry wenye miaka mitano wanampenda kiosoka kuliko wanavyompenda baba yao - Messi amekuwa akipendwa mno na habari zake zimekuwa zikikumbatiwa mno na media na mashabiki duniani kote kuliko ambavyo ilikuwa kwa Pele.

Messi amekuwa globally known tena na hii teknolojia inavyorahisha mambo kutoka pande zote za dunia, amekuwa lulu kwa kampuni za matangazo kiasi kwamba ndio amekuwa mchezaji anayeingiza mkwanja mrefu kuliko wote duniani. Hili kosa la Pele, ni utandawazi wa dunia ya sasa, media na teknolojia ambayo ipo sasa, na haikuwepo wakati wa enzi za Pele kama mchezaji, hivyo Pele hapaswi kuwa na wivu na umaarufu namafanikio ya Messi.

Kama Pele ana wasiwasi kwamba watu watamsahau jina lake/ ikiwa Lionel Messi atakuwa mchezaji bora wa muda wote, anahitaji kutokuwa na wasiwasi. Pele ni moja ya wachezaji bora wa muda wote, aliuteka ulimwengu wa soka na inawezekana ndio aliyeshinda sana katika historia ya mchezo. Hakuna atakayeshinda makombe matatu ya Dunia.

Pele jina lako halitosahaulika ikiwa Messi atakuwa mchezaji bora wa muda wote. Tafadhali uache kumdidimiza kipaji alichopewa na mungu Lione Messi, badala ashangalie namna mtoto huyu wa kiargentina anayolipenezesha soka kwa aina ya mchezo wake.

Friday, April 13, 2012

SABABU 5 KWANINI BARCELONA ITAENDELEA KUTAWALA ULIMWENGU WA SOKA KWA MIAKA 10 MBELE.

Kikosi cha sasa cha Barcelona bila shaka wala kelele ndio timu yenye  ubora kuliko zote kuwahi kutokea katika soka.

Hii ni imani ambayo imejengeka kwa waandishi na wachambuzi wa habari za michezo,  wacheza soka, makocha na mashabiki wa mchezo huu kwa wingi wakiamini hii ndio timu bora kabisa kuwahi kutokea kwenye soka - labda uwe unaishi jijini Madrid.

Pep Guardiola na kikosi chake wanacheza mpira ambao timu nyingine zinaweza tu kuota kucheza vile.

Miaka 3 iliyopita pale Nou Camp kumekuwepo na mataji 11, yakiwemo back to back la liga, 2 champions league, 2 Uefa Super Cup na 2 FIFA World Club Cup.
Listi itaendelea na kwa hakika inaweza ikaongezeka msimu huu, kwa kuwa bado wapo katika nusu fainali ya Champions league dhidi ya Chelsea huku wakiwafukuza kwa Karibu Madrid katika La Liga.

Lakini je ni lini utawala huu wa Barcelona utaisha? Wengi wamediriki kujiuliza hilo swali huku wengine wakidiriki kusema mwsiho wa Barcelona haupo mbali.

Lakini ukweli ni kwamba hakuna sababu inayoweza kukufanya usiamini kama timu itaendelea kupata nguvu na kutawala soka tena sio kwa mwaka mmoja au miwili - bali ni kwa takribani muongo mmoja.

Hizi ni sababu tano kwanini...........................


 
5 . PEP GUARDIOLA
Timu bora duniani ina kocha bora bora ulimwenguni na hiyo ndio kombinesheni ya kutisha kwa mtu yeyote kuivunja.

Guardiola amekuwa akihusishwa na klabu nyingine especially nchini England, lakini ishara zote zinaonyesha kwamba kocha huyo mwenye miaka 41 atakuwa Catalunya kwa muda mrefu na hiyo ni habari nyingine nzuri kwa mashabiki wa Barca na mbaya kwa wapinzani.

Mhispania huyo anaamini mafanikio yanakuja katika miaka 4 au 5 ya ukocha, akiacha maswali mengi kwamba anaweza kuondoka Catalunya na kuangalia changamoto nyingine sehemu tofauti.

Lakini Bodi ya Bacelona inajua ni mtu wa namna gani wanamhitaji na yupo incharge kwa sasa. Ikiwa Guardiola atakubali kusaini mkatanba mpya , hilo linamaanisha atakaa kwa miaka mingine 6 au 7.

Ikiwa Guardiola ataondoka, hawatokuwa na upungufu wa makocha dizaini ya yake ambao watambadili , akiwemo kocha wa Roma Luis Enrique  na kocha wa Athletic Bilbao Marcelo Biesla ndio watakaoongoza mbio hizo.

4. WACHEZAJI VIJANA WA BARCA
Ushindi wa 4-0 dhdi ya Bate Borisov katika champions league mwishoni mwa December last year ungeweza kuwafanya watu waishtuke, lakini wangepatwa na mshangao mkubwa asubuhi yake watakaposoma kikosi kilichocheza

Guardiola aliwapanga watoto wa Academy katika kikosi cha kwanza, waliokuwa na wastani wa umri wa miaka 20.

Kijana mwenye miaka 19 kiungo mwenye uwezo Sergio Roberto alifungua ukurasa wa magoli, akafuatiwa na Martin Mantoya.

Pia katika kikosi hicho walikuwemo Thiago Alcantara na 18-year old Rafinha.

Lionel Messi na wenzie wengi walikuwa nje wakiangalia namna vijana wakilitandaza soka la kutisha na kupata matokeo mazuri.

 
3. UTAWALA KATIKA SOKO LA UHAMISHO
Hakuna draft katika soka; wachovu hawapati wachezaji wazuri. Wachezaji wazuri wanataka kucheza katika timu bora.

Barcelona wana jina, mafanikio  na fedha za kununua wachezaji wazuri na kwalea wenye umri mdogo katika kuwasaidia kuwa masupastaa wa ukweli na kuifanya timu hiyo kuwa na mlolongo wa wachezaji wazuri, kila anayeingia na anayetoka dimbani wana viwango sawa ndivyo Barca ilivyo.

Mfano, mshambuliaji wa kibrazili Neymar ndio gumzo kwa sasa katika soko la uhamisho duniani na inaonekana magiants wa Catalunya wanaelekea kushinda vita dhidi ya Juventus, Madrid,Juventus na Chelsea katika kumuwania kinda hilo.

Angalia wachezaji wengine kama Jordi Alba na Thiago Silva ambao watakuja kuimarisha zaidi ukuta wa Barca.

Lakini kuongezwa kwa Neymar katika kikopsi cha Barcelona ndio balaa zaidi. Ikiwa atasajiliwa ina maana Fabregas atarudi chini zaidi kuungana na Iniesta na kumpisha dogo mbele na Mchawi Messi.

Kiukweli ukiachana na Ronaldo, jakuna mchezaji mwingine anayetajwa kufananinshwa kiuwezo na Messi kama Neymar- fikiria sasa wakiwa wanacheza timu moja kutakuwa na balaa kiasi gani.


2. BRAND YA BARCELONA
Ingawa kumekuwepo na malalamiko kuhusu dili lao la udhamini na Qatar Foundation, Barcelona bado hawajaitupa UNICEF logo.

Kunaonekana kuna kuongezeka kwa ubora na thamani ya klabu na kuwa timu kubwa na inayotengeneza faida zaidi katika soka duniani.

Pia hivi karibuni wamesaini dili la ushirikiano na Boca Juniors, dili ambalo kwa hakika litawapa faida kubwa ya kuweza kukusanya vipaji kutoka nchini Argentina, huku dili lao la udhamini wa jezi likiwapa uhakika kuwa na fedha za kutumia na kutanua mabavu katika soko la usajili kwa miaka kadhaa ijayo.

Pia wana Academy ambayo ina nguvu, inatengeneza wachezaji bora kabisa duniani, LA masia ni sehemu bora na inatajwa kuwa academy bora duniani kwa sasa kutokana na wachezaji inawotengeneza na waliopo tayari ambao ni masupastaa katika dunia ya soka.

Kwa vitu hivi vyote ni dhahiri future ya Barcelona ipo salama, na vitaongeza na kusaidia utawala mwingine wa Barca katika soka kwa miaka mingi ijayo.


 
1. LIONEL MESSI
Ni jina gani jingine ambalo tunaweza kulitumia kumzungumzia huyu kiumbe ambaye bila shaka ndio mchezaji bora wa soka la kisasa na inawezkana mchezaji bora kabisa kuwahi kutokea ulimwengu.

Maradona na Pele wanaweza wakabishana juu ya hili, lakini kuna watu wengi wanaamini muargentina huyu ni hatari na hajawahi kutokea kama yeye katika historia ya soka duniani.

Tuzo tatu za mfululizo za dunia zinakamilisha tuzo nyingi ambazo amezifungia nyumbani kwake, ambazo wachezaji wengi duniani wanaota tu kuzipata.

Lakini jambo la kutisha zaidi mchezaji huyu bora wa soka la kisasa ndio kwanza ana miaka 24 tu.

Hilo tu litakufanya uanze kufikiria mara mbili mbili huku likiwaumizavichwa mabeki katika ulimwengu wa soka, kwa sababu  katika zama hizi wapo wengi dizaini yake lakini Messi ni habari nyingine - simply unplayable.

Bado unajiuliza kwanini Barcelona itaendelea kutawala kwa miaka mingine 10 ? Jibu ni kwa sababu mchawi huyu ataendelea kuwepo katika klabu hiyo.

Fabrice Muamba awapatia keki wafanyakazi wa hospital.

  hii ndo keki waliopatiwa wafanyakazi wa hospital waliomtibu Fabrice Muamba.

Kiungo wa Bolton Wonderers Fabrice Muamba muda wowote kutoka hivi sasa sasa anaweza kutoka Hospitalini baada ya afya yake kutengamaa.

TAARIFA KUTOKA TFF!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Aprili 13, 2012

ULIMWENGU ATUA NGORONGORO HEROES
Mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye ndiye mchezaji pekee kutoka nje aliyeitwa na Kocha Kim Poulsen kwenye U20 (Ngorongoro Heroes) anatarajia kujiunga na kikosi hicho ambacho kiko kambini kesho (Aprili 14 mwaka huu).

Ulimwengu ambaye anachezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) atawasili saa 1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways akitokea jijini Lubumbashi.

Ngorongoro Heroes ambayo iliingia kambini Aprili 20 mwaka huu inajiandaa kwa mechi ya mashindano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 dhidi ya Sudan. Mechi hiyo itachezwa Aprili 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Kwa mujibu wa Kocha Poulsen, kikosi chake kesho (Aprili 14 mwaka huu) kitakuwa na awamu (sessions) mbili za mazoezi kwenye Uwanja wa Karume. Awali ya kwanza itakuwa asubuhi nay a pili itafanyika jioni.

Wachezaji wengine walioko kwenye kikosi hicho cha Ngorongoro Heroes ni Saleh Malande, Aishi Manula, Hassan Kessy, Said Ruhava, Carlos Kilenge, Dizzana Issa, Amani Kyata, Issa Rashid, Emily Mgeta na Khamis Mroki.

Wengine ni Ramadhan Singano, Frank Sekule, Frank Domayo, Omega Seme, Abdallah Hussein, Ibrahim Rajab, Hassan Dilunga, Alhaje Zege, Jerome Lambele, Atupele Green na Simon Msuvan.

Mechi ya marudiano dhidi ya Sudan itachezwa jijini Khartoum kati ya Mei 4, 5 na 6 mwaka huu.

Fainali za Afrika kwa vijana zitafanyika Machi mwakani nchini Algeria. Timu nne za juu kwenye fainali hizo zitacheza Fainali za Dunia zitakazofanyika nchini Uturuki kuanzia Juni hadi Julai mwakani.

LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA 23
Raundi ya 23 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia raundi ya 23 kesho (Aprili 14 mwaka huu) kwa mechi nne. Polisi Dodoma wataikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma wakati JKT Ruvu watakuwa wageni wa Mtibwa Sugar mjini Turiani.

Mechi nyingine za raundi hiyo zitakuwa kati ya Kagera Sugar na African Lyon zitakazooneshana kazi kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Nayo Moro United inaikaribisha Oljoro JKT katika mechi itakayofanyika Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Raundi ya 23 itakamilika Jumapili (Aprili 15 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu Shooting na Simba itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Yanga itakuwa mgeni wa Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Villa Squad itapambana na Coastal Union kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Ligi hiyo itaendelea tena Aprili 18 mwaka huu kwa mechi tano. Kagera Sugar vs Yanga mjini Bukoba, Toto Africans vs African Lyon jijini Mwanza, JKT Ruvu vs Simba- Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Ruvu Shooting vs Moro United mjini Mlandizi na Polisi Dodoma vs Coastal Union mjini Dodoma.

BONGO MOVIE KUICHANGIA TWIGA STARS
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Twiga Stars) itacheza mechi ya kirafiki na timu ya wasanii wa filamu ya Bongo Movie itakayofanyika Jumamosi (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Lengo la mechi hiyo ya maonesho (exhibition) ni kuichangia Twiga Stars ambayo hivi sasa iko kwenye mashindano ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.

Pia asilimia mbili ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Twiga Stars na Bongo Movie yatakwenda kwenye familia ya mwigizaji nguli wa filamu Tanzania, Stephen Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7 mwaka huu.

Kiingilio katika mechi hiyo kitakuwa sh. 10,000 kwa VIP A, sh. 5,000 kwa VIP C na B na sh. 2,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Mechi itaanza saa 10 kamili jioni.

Machi 10 mwaka huu, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara alizindua akaunti ya Twiga Stars kupitia Tigo Pesa kuichangia timu hiyo ambayo inashiriki michuano ya AWC. Wachangiaji wanatakiwa kutuma mchango wao kwenda namba 13389.

RUFANI YA YANGA KWA TIBAIGANA
Kikao cha Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kilichokuwa kifanyike kesho (Aprili 14 mwaka huu) kujadili rufani ya Yanga kupinga kunyang’anywa pointi tatu kwa kumchezesha Nadir Haroub katika mechi dhidi ya Coastal Union kimeahirishwa.

Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Kamishna mstaafu wa Polisi, Alfred Tibaigana sasa kitafanyika Jumanne (Aprili 17 mwaka huu) saa 9 alasiri kwenye ofisi za TFF.

MIKOA 13 YAWASILISHA MABINGWA WAKE
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 17 ya Tanzania Bara vimewasilisha majina ya mabingwa wake kwa ajili ya Ligi ya Taifa iliyopangwa kuanza Aprili 22 mwaka huu katika vituo vitatu.

Mikoa hiyo na mabingwa wake katika mabano ni Kigoma (Kanembwa FC ya Kibondo), Kilimanjaro (Forest FC ya Siha), Ruvuma (Mighty Elephant ya Songea), Dodoma (CDA), Rukwa, (Mpanda Star ya Mpanda), Iringa (Kurugenzi FC ya Mufindi) na Lindi (Lindi SC).

Mingine ni Mtwara (Ndanda FC), Shinyanga (Mwadui FC), Mara (Polisi Mara), Singida (Aston Villa), Arusha (Flamingo SC) na Tabora (Majimaji FC). Mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wake ni Manyara, Dar es Salaam, Mwanza, Tanga, Morogoro, Pwani na Kagera.

Powered by Sorecson : Creation de site internet
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MAMBO MATANO YATAKAYOTOKEA IKIWA YAYA TOURE ATASTAAFU KUICHEZEA IVORY COAST

Mchezaji bora wa bara la Afrika mwaka 2011, Yaya Toure, , amepata mafanikio makubwa katika miaka 11 ya career yake, ambayo inajumuisha ubingwa wa Uefa Champions League akiwa na Barcelona na kombe la FA akiwa na Manchester City.
Japokuwa, kujiuzulu ama kustaafu katika soka la kimataifa na timu yake ya Taifa ya Cote d'Ivoire akiwa tu miaka 28, bila kupata tatizo lolote litakalopelekea kuchukua uamuzi huo, uamuzi huu unaonekana hauna mashiko kwa mchezaji ambaye anaonekana kuwa katika kilele cha kiwango chake cha soka.

Nini tatizo lilopelekea uamuzi wake. Whatever the reason nyuma ya uamuzi huu ambao ameupanga kuuchukua hivi karibuni kujiengua kutoka kwa Tembo wa Afrika, utapelekea kutokea kwa vitu kadhaa ambavyo havitaepukika kutokea kutokana na uamuzi wa Yaya kustaafu kucheza soka la kimataifa.

5. KUCHUKIWA NA MASHABIKI
Yaya Toure kwa sasa ni mchezaji maarufu na anayependwa kuliko na mashabiki wengi nchini kwao nyuma ya Didier Drogba. Mchezaji huy wa zamani wa Barcelona ni role model na anaangaliwa kama mfano wa kuigwa na vijana wengi wanaocheza soka na wenye ndoto za kuwa kama yeye.

Ni mtu anayesaidia sana katika mapambano dhidi ya HIV-aIDS,  amefanya matangazo mengi ya TV. Kuondoka kwake katika timu ya taifa kutaanza kuonekana katika mashindano makubwa ya timu ya taifa kama vile AFCON, au World Cup.

Kwa hakika mashabiki watakuwa wakiombeleza kutokuwepo kwake na wanaweza hata kumbadilikia na kumchukia kwa kutoonyesha mapenzi kwa timu yake ya taifa, kutokana na kujiuzulu bila sababu za msingi.

ATAPOTEZA HESHIMA YA KUDUMU
Ikiwa timu ya taifa ya Ivory Coast itafanya vizuri na kufanikiwa kucheza kwa mafanikio katika michuano ya AFCON 2013 au 2014 World Cup bila kuwepo kwa Yaya, mchezaji huyo atakuwa amefanya kosa kubwa sana katika maisha yake ya soka.

Ikitokea hivyo Yaya atapoteza heshima kubwa aliyokuwa amejiwekea, legacy itapotea kama upepo, na wachambuzi wa soka nchini kwao watakuwa wa kwanza kuwakumbusha mashabiki kwamba hakuwa na umuhimu mkubwa katika kuiletea mafanikio Ivory Coast.

Mashabiki siku zote huwa na mapenzi na waliopo na sio waliopita, au huwa wana tabia ya kusahau historia pale mambo yanapowaendea vizuri na timu zao wanazoshabikia, na haitowachukua muda mrefu kumsahau Yaya ikiwa nchi yao itaingia katika zama za ushindi bila yeye.

MADHARA KWA KWACHEZAJI WENZIE
Ni namna gani hali ya kuondoka kwa Yaya katika timu ya taifa kutawaathiri wachezaji wenzie ndani ya timu ya taifa? Wengine walisema wataachia jahazi kwa vijana ikiwa timu ya taifa itashindwa kuchukua ubingwa wa AFCON 2012. Timu ikafungwa kwenye fainali na Zambia na huku hakuna hata mchezaji mmoja aliyesema anajiuzulu baada ya mchuano kumalizika.

Je kujiuzulu kwa Toure kunaweza kuchochea kuondoka kwa wengine, katika njia moja kama ilivyokuwa kwa Zinedine Zidane alipojiuzulu kucheza timu ya taifa wachezaji wengine walimfuata kama vile Lizarazu, Marcel Desailly, Claude Makelele na Lilian Thuram. Je wachezaji wakubwa wa Ivory Coast hawatofuata mfano wa akina Lizarazu baada ya Toure kuondoka ikizingatiwa walishasema watawapisha vijana ikiwa watafeli kuchukua kombela afcon 2012.

IVORY COAST KUPOTEZA MCHEZAJI MUHIMU
Kuondoka kwa Toure kutaleta utofauti mkubwa katika kikosi cha The Elephants. Ni mchezaji muhimu katika timu kwenye nafasi ya ulinzi na mashambulizi, na kutokuwepo kwake kutaleta mianya ambayo iliwafanya wawe wagumu katika kushindana nao siku za nyuma.

Mchezaji huyu Manchester City anakamilisha namba ya wachezaji wa class ya dunia wanaoipa Coted'Ivoire uwezo mkubwa wa kiakili na kinguvu na uwezo wa soka.
Jukumu lake la kuvunja mashambulizi ya wapinzani, kugawa mipira, kupiga mashuti na ku-cover ukuta wake likumuangukia mtu mwingine katika kikiosi cha kwanza, hakuna guarentee kwamba mbadala wake atakuwa na uwezo kama wake au kupata mafanikio kama ya mdogo wake Kolo Toure.

KUMKOSA KIONGOZI
Timu ya Ivory Coast itammiss uwezo wa Yaya kuzuia na kugawa mipira katika midfield, ikizangatiwa kwamba mchezaji wa zamani wa Tottenham Didier Zakora, ambaye alikuwa ndio the best katika eneo hilo kwa sasa ndio anaishia, na mchezaji wa Newcastle Cheik Tiote bado hajaweza kujitengenezea nafasi wala jina katika timu ya taifa.

Na huku michuano ya AFCON 2013 ikikaribia, itakuwa taabu sana kupata mbadala halisi wa Yaya kama kiongozi wa asili pale  katikati ya dimba na mchezaji aina ya TIOTE, haswa pale presha ya kufanya vizuri inapoongezeaka ndani ya kikosi wachezaji wengi wenye uzoefu ndio wangeweza kuhimili mikikimikiki.

Kwa maana hiyo kumkosa Toure katika situation za namna ni pengo  la kiuongozi ndani ya kikosi .

TANGA CEMENT WAIPA BASI COASTAL UNION

Basi walilopewa Coastal Union

MABINGWA wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, 1988, Coastal Union ya Tanga, maarufu kama ‘Wagosi wa Kaya’, wamekabidhiwa basi lenye thamani ya Sh Milioni 45 na kampuni ya Tanga Cement.
Akikabidhi basi hilo kwa viongozi wa Coastal, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Cement, Erick Westerberg, alisema, basi hilo wamelitoa kutokana na juhudi zilionyeshwa na timu hiyo katika Ligi Kuu msimu, inayoelekea ukingoni.
Hata hivyo, Westerberg, alitoa rai kwa viongozi wa klabu hiyo watambue kuwa, basi hilo ni kwa matumizi ya timu tu na sio mengine binafsi, huku akiwataka kulitunza kwa maendeleo ya timu yao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Coastal Union, Ally Ahemed ‘Aurora’, alisema, msaada kampuni hiyo waliyoutoa, ni wa kwanza katika kipindi hiki na hiyo ni kutokana na kikosi hicho kufanya vizuri katika ligi.
Aurora, aliomba kampuni nyingine zenye moyo wa kizalendo, kuisaidia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri zaidi katika mechi za ligi ijayo, kwani hii ya sasa iko mwishoni.
Kwa upande wake, Nahodha wa timu hiyo, Said Sued, aliwahakikishia mashabiki wao kuwa, watahakikisha wanabaki nafasi ya nne mwishoni mwa ligi kuu, huku akisisitiza umoja na mshikamo kwa viongozi na wachezaji wenzie, kuwa ndio siri kubwa ya mafanikio.
Timu hiyo, kwa sasa inaendelea na mazoezi kwenye uwanja wa Mkwakwani kwa maandalizi ya mchezo wake unaofuata dhidi ya Villa Squad utakaochezwa jijini Dar es Salaam wiki hii.

KIONGOZI YANGA AFARIKI DUNIA


MJUMBE wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Wakili Theonist Rutashoborwa amefariki dunia usiku wa kuamkia leo, nyumbani kwake, Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu ameaimbia bongostaz asubuhi hii kwamba bado wanawasiliana na familia ya marehemu ili kujua zaidi na saa 5:00 asubuhi watafanya Mkutano na Waandishi wa Habari.
Rutta ni mwanachama ambaye alichangia kwa kiasi kikubwa klabu hiyo kupata ufadhili wa Yussuf Manji mwaka 2006, kutokana na harakati alizoanzisha za Harambee ya Yanga kufuatia hali mbaya ya kifedha ndani ya klabu hiyo chini ya uongozi wa Francis Mponjoli Kifukwe enzi hizo.

Azam FC yatua Dodoma tayari kuikwaa Polisi.


Azam FC iliondoka DSM na wachezaji wote 24 isipokuwa Aishi Salum aliyekwenda kujiunga na kikosi cha timu ya taifa, Akizungumza na tovuti ya www.azamfc.co.tz Mapema kabla ya kuondoka kocha wa Azam Stewart Hall amesema timu inaenda Dodoma mapema ili kupata muda wa kufanya mazoezi katika uwanja huo unaotofautiana na uwanja wanaotumia wa Azam Chamazi.
Stewart alisema wanaenda Dodoma wakiwa wamejiandaa vya kutosha kuweza kupata pointi tatu muhimu zitakazowaweka vizuri katika harakati za kusaka nafasi mbili za juu.
“Safari yetu tunaomba iwe yenye heri, tunatarajia kupata pointi tatu kwa kuwa tupo vizuri na wachezaji wote wamejiandaa na wana ari ya kimchezo japo tutakuwa ugenini”
Alisema wameamua kuondoka na wachezaji wote kwakuwa kikosi cha timu ya vijana Academy kipo visiwani Zanzibar, hivyo wachezaji watakaobaki hawatakuwa wanafanya mazoezi, wanaondoka wakafanye mazoezi na wenzao.
Akielezea hali ya wachezaji wenye majeruhi Abdi Kassim ‘Babi’ na Joseph Owino, kocha alisema nao watakuwa katika msafara huo kwa kuwa wanafanya mazoezi ya taratibu.
Wakati huo huo, Azam Academy jana iliwasili salama visiwani Zanzibar kwenye kambi ya siku nne, na leo wamecheza mchezo wake wa kwanza na Kilimani City inayoshiriki ligi daraja la pili na kuifunga 2-1 kwenye uwanja wa Ngome. Magoli ya vijana yakifungwa na Mudhhatir Yahya na Joseph Kimwaga.
Kesho Kikosi cha Vivek Nagul kitakwaana na kikosi cha Zanzibar Under 17
Kikosi kilichopo Dodoma ni, Mwadini Ally, Agrey Moris, Erasto Nyoni, Said Morad, Wazir Salum, Haji Nuhu, Abdulhalim Humud, Abdi Kassim, Jabir Aziz, Salum Aboubakar na  Michael Bolou Kipre.
Wengine ni  Herman Tchetche Kipre, John Bocco, Gaudence Mwaikimba, Himid Mao, Ibrahim Shikanda, Luckson Kakolaki, Abdulghan Gulam, Ibrahim Mwaipopo, Khamis Mcha, Mrisho Ngassa na Zahor Pazi. Joseph Owino na Juckson Wandwi

LIGI KUU YA VODACOM KUENDELEA JUMA HILI !

 Ben and kyata at kaitaba stadium in preparation for the game on saturdary against kagera sugar

Mreno kukabidhiwa mikoba ya Papic Yanga







Vicky Kimaro na Imani Makongoro

MABINGWA wa Tanzania, Yanga wapo mbioni kumnasa kocha kutoka Ureno kuja kurithi mikoba ya Mserbia Kostadin Papic anayemaliza mkataba wake wiki ijayo Aprili 18.

Mmoja wa viongozi wa Yanga ambaye hakutaka kuweka hadharani jina lake alisema kuna makocha wawili ambao CV zao zipo mezani mmoja kutoka Ureno na mwingine kutoka Romania, huku wa Ureno akipewa nafasi kubwa ya kuongoza jahazi hilo la Yanga.

Chanzo hicho cha habari kilisema kuwa wameamua kuachana na Papic kwa kile walichodai kuwa hana jipya katika timu yao huku wakimtuhumu kuwasiliana na marafiki wa Simba 'Friends of Simba' kila mara.

"Hatuwezi kumvumilia kocha ambaye mara kwa mara anawasiliana na Friends of Simba, kwanza nidhamu ya wachezaji wetu imeshuka sana tofauti na mwanzo, tunasubiri mkataba wake uishe alipwe chake aondoke," kilidai chanzo hicho.

Alisema,"kwa kifupi ni kwamba tumeshapata CV za makocha wawili mmoja wa Ureno na mwingine wa Romania, tunasubiri mkataba wake uishe tumalizane naye aondoke zake, mechi yake ya mwisho ni mechi ya Kagera Sugar, hawezi kukaa tena benchi wakati mkataba wake utakuwa umeshamalizika."

Kufuatia hali hiyo, katika mechi ya marudiano na mahasimu wao Simba itakayochezwa Mei 5, Mserbia huyo hatakaa katika benchi la Yanga na huenda Mreno akaongoza jahazi.

Zipo taarifa kwamba Papic hajaongozana na timu yake kwenda Mwanza kwa ajili ya mechi yao ya marudiano dhidi ya Toto Afrika kwa kuwa anaumwa ila ni mgomo baridi baada ya kucheleweshewa mshahara wake wa miezi mitatu hata hivyo habari hizo zimepingwa vikali na Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesigwa.

"Papic hadai chochote, kila mwezi tunampa fedha zake, alidai mshahara wa mwezi mmoja tu hapa alipiga kelele,  iweje avumilie mshahara wa miezi mitatu? na hilo la mkataba wake muulizeni mwenyewe kama ataendelea au la, mimi siwezi kuuzungumzia mkataba wake wakati bado haujaisha,"alisema Mwesigwa

Hata hivyo, chanzo kingine cha habari kilisema kuwa Yanga ambayo inapokea Sh 26m kila mwezi kutoka kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kama wadhamini wao ipo kwenye matatizo makubwa ya mtikisiko wa uchumi baada ya kulipa fedha nyingi kwa aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo raia wa Uganda, Sam Timbe waliyemfungashia virago mapema mwaka jana huku akiwa na mkataba wa miaka miwili.

Yanga walilazimika kumlipa Timbe mamilioni ya fedha kitu ambacho kimesababisha mpaka leo klabu hiyo kuyumba kiuchumi na mapema mwaka huu wachezaji wa klabu hiyo walitishia kugoma hadi walipwe fedha zao za mishahara huku Papic akitangaza kubwaga manyanga iwapo uongozi hautamalizana na wachezaji na kwamba asilaumiwe kwa matokeo ya uwanjani.

Wakati huo huo; mabingwa hao wamesema mapambano ya kutetea ubingwa msimu huu bado yanaendelea licha ya kuachwa kwa pointi saba na Simba wanaoshikilia usukani wa ligi hiyo.

Yanga wamesema pamoja na kupokonywa pointi tatu bado wana uhakika wa kuutetea ubingwa huo kama ilivyokuwa mwaka jana, ambapo timu hiyo ilifanya mapinduzi katika hatua za mwisho za ligi na kufanikiwa kutwaa kombe hilo.

Katibu Mkuu wa timu ya Yanga, Celestin Mwesigwa alisema jana jijini Dar es Salaam kwamba bado mapambano yanaendelea ili kutetea kombe lao, ambapo mwaka huu watani wao wa Jadi Simba wameonyesha dalili na nia ya kulitwaa mapema.

"Hatuwezi kukata tamaa licha ya kuwa tumenyang'anywa pointi tatu, matumaini ya kutetea ubingwa wetu yapo na hilo linawezekana," alisema Mwesigwa.

Mwesigwa alihoji kama mwaka jana waliweza kutwaa ubingwa huokwanini mwaka huu washindwe?, huku akisisitiza kwamba mechi tano walizobakisha kabla ya kumaliza ligi hiyo ndiyo zitawafanya walitwae kombe hilo kwa mara nyingine tena.

"Ninachoweza kusema ni kwamba mashabiki wetu wasiwe na wasiwasi, tuliachwa kwa pointi nyingi mwaka jana na bado tukachukua kombe iweje tushindwe mwaka huu?," alihoji tena Mwesigwa na kuongeza kuwa bado ligi inaendelea hivyo mashabiki wao wajiandae kucheka na kushuhudia timu yao ikitwaa ubingwa.

Akizungumzia suala la rufaa yao kupinga maamuzi ya Kamati ya Nidhamu kuwapokonya pointi tatu za mechi dhidi ya Costal Union, Mwesigwa alisema suala hilo liko chini ya Kamati hivyo anaichia ili ifanye maamuzi.

"Nimesikia kwenye vyombo vya habari kwamba Kamati itakutana Jumamosi, lakini mimi sijaambiwa chochote juu ya kukutana huko hivyo nasubiri taarifa kutoka kwao, jambo la msingi ni kusubiri maamuzi ya Kamati,"alisema Mwesigwa.

Yanga inashika nafasi ya tatu nyuma ya Simba inayoongoza Ligi Kuu ikifuatiwa na Azam inayoshika nafasi ya pili hadi sasa

Gunnerz 4 life !!!!

Thursday, April 12, 2012

SABABU 5 KWANINI MARIO BALOTELLI SIO WA KULAUMIWA KWA MSIMU WA CITY KUANZA KWENDA VIBAYA


Ndio ni mkorofi, anapigana mazoezini na wenzie, anagombania kupiga free kicks na wenzie uwanjani na pia anapata red cards mara kwa mara. Japokuwa makosa yake ni makubwa lakini Mario Balotelli sio sababu kubwa ya msimu wa Manchester City kwenda vibaya mwishoni mwa msimu.
 Roberto Mancini amechukua jambo hili na kumtoa kafara mshambuliaji huyu kwa kumtupia lawama ili kujaribu kulinda kibarua chake, lakini hizi ni sababu tano zinaonyesha ukweli kuhusu mambo kwenda mlama pale City.


KIWANGO CHA DAVID SILVA
Katika nusu ya kwanza yote ya msimu David Silva alikuwa akitajwa kama mchezaji bora wa ligi kuu ya England. Mhispania huyo ndio alikuwa roho ya City  akifanya maajabu wiki baada ya wiki.
Lakini baadae kuna kitu kimetokea. Labda ni majeraha au uchovu, Silva si yule wa mwanzo wa msimu, amekuwa katika kiwango cha chini katika mechi za hivi karibuni.
Baada ya Silva kupoteza kiwango, na timu nayo ikawa hivyo hivyo. Na sio jambo la kushangaza kwa kuwa mchawi huyu wa kihispania ndio alikuwa mtu muhimu katika kuuinganisha timu hii ya Roberto Mancini.


SAMIR NASRI WA CITY SIO YULE WA ARSENAL
Baada ya kufunga magoli 16 katika mashindano yote akiwa na Arsenal msimu uliopita, mashabiki wa City wanaweza kusamehewa kwa kutegemea makubwa zaidi kutoka Nasri ambaye mapaka sasa amefunga magoli 5 msimu mzima.

Anaweza akawa anawatolea maneno ya kejeli mashabiki wa Arsenal kwenye Twitter  baada ya mchezo wa wikiendi iliyopita, lakini alishindwa kufanya lolote la maana kuweza kuisadia timu yake isiepukane na kipigo.
 Lakini sasa mashabiki wa City watakuwa wameshaanza kuuona uwezo wake wa kuongea ni mkubwa kuliko kucheza soka.


SERGIO AGUERO AMEPOTEA
Sergiuo Aguero ana magoli mawili kupita magoli ya kawaida katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Hakika, ndio amekosa michezo kadhaa kutokana na majeraha yake ya kijinga kama anavyoyaita Mancini, lakini hicho sio kisingizio kinachotosha kwa mshambuliaji wa kariba yake.
 Muargentina huyo alifunga magoli 9 katika miezi yake mitatu ya kwanza pale Etihad.



ROBERTO MANCINI
Uwezo mdogo wa  Mancinikuweza kuwatuliza na kuwa-manage wachezaji ni tatizo ambalo limepelekea city kuwa walipo.

Kwa ufupi, kama Mario Balotelli ndio tatizo pale City, Roberto Mancini anahitaji kutafuta suluhisho. Mfano bora upo karibu yake kwa jirani yake Sir Alex Ferguson jinsi alivyoweza ku-handle ukorofi wa Rooney ambaye kwa sasa msimu huu hana kadi hata moja.

Lakini amekosa namna ya kumshugulikia au kumrekebisha Balotelli na mwishowe ndio anamtupia lawama ambazo hazina mashiko, matokeo yake timu imekosa muelekeo wala mshikamano miongoni mwa wachezaji.




CARLOS TEVEZ
Carlos Tevez aliifanya City itishe msimu uliopita. Lakini kutokana na kitendo chake cha kukataa kucheza katika champions league mwezi september kiliharibu kila kitu.
Japokuwa baada ya Tevez kufungiwa na kugoma kucheza, City waliendelea kucheza na kushinda. Then Roberto Mancini akaanza kelele za kutaka kumrudisha Carlitos kwenye timu, na hapo ndipo City walipoanza kupoteza points  na kufanya mbio za ubingwa kwa United kuwa nyepesi.

Tangu ndege ya Tevez kutoaka alipokuwa ilipotua jijini Manchester just after Valentines Day, City wameshinda mechi nne tu kati ya nane na  kupitwa points 8 na United kabla ya jana watoto wa Fergie kuteleza na kupunguza pengo hilo.