Search This Blog

Saturday, November 2, 2013

MAKALA: SIMBA NA YANGA, HAZITAKUFA ILA ZIKUBALI CHANGAMOTO MPYA


Na Baraka Mbolembole

Msimu wa kwanza kabisa wa soka la Tanzania ni ule wa mwaka 1965, mwaka ambao timu ya Simba ikifahamika kama Sunderland wakati huo ilitwaa ubingwa wa kwanza wa Tanzania Bara, wakati huo michuano ikifahamika kama klabu bingwa ya Tanzania Bara, ambayo ilikuwa ikianzia katika ngazi ya wilaya, mkoa na baadae kitaifa ambapo bingwa alipatikana.

Simba ilitwaa tena ubingwa huo mwaka uliofuata, kabla ya kuutema mwaka 1967 mbele ya timu ya Cosmopolitans, ambayo kwa sasa ipo, kama haipo.Wakati, Simba ikitwaa ubingwa huo wa nchini mara mbili mfululizo, Tanzania haikuwa mwanachama wa fifa, na hilo lilipelekea kushindwa kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa.

Yanga walitwaa ubingwa wao wa kwanza wa Tanzania , mwaka 1968 na kufanikiwa kuwa timu ya kwanza kutoka katika ligi ya Tanzania Bara kuwakilisha nchi katika michuano ya klabu bingwa Afrika, kwani tayari Tanzania ilikuwa imepata uanachama wa shirikisho la soka ulimenguni, Yanga wakawa timu ya kwanza kucheza michuano ya kimataifa mwaka 1969. Mabingwa hao mara 24 wa kihistoria, waliushikilia ubingwa huo kwa miaka mitano mfululizo hadi mwaka 1971 walipokuja kuutema kwa mahasimu wao Simba, ambao nao walitwaa mara mbili mfululizo, kuanzia 1972, na 1973 kabla ya Yanga kuurejesha tena, mwaka 1974.

Baada ya kupita miaka kumi huku timu za Dar es Salaam zikipokeza taji hili na kutawala soka la Tanzania, timu ya Mseto kutoka mkoani, Morogoro ilitwaa ubingwa huo, mwaka 1975 na kwa mara ya kwanza ubingwa ukatoka Dar es Salaam. Siimba ilifanikiwa kuurudisha tena ubingwa huo na kuushikilia kwa miaka mitano mfululizo, kuanzia mwaka 1976- 1980, kabla ya Yanga kuuchukua kwa mara ya kwanza baada ya kusubiri kwa miaka sita. Pan Africans ikaa timu ya nne kutwaa ubingwa huo, mwaka 1982 na kwa kipindi chote cha miaka kumi ya muongo wa pili, Simba ilitwaa mara sita, Yanga mara tatu na Pan Africans mara moja.

Muongo wa tatu, ulianza kwa ' nuksi' kwa timu za Dar es Salaam, wakati Mseto ilipotwaa ubingwa mwaka , 1975, miaka kumi baadae timu ya Tukuyu Stars, ikiwa imetoka kucheza ligi ya daraja la chini na kupanda ligi kuu, Tukuyu ilitwaa huo na kuwa timu ya sita katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanza kwa igi hiyo. Hiyo ilikuwa ni mwaka 1986, miaka miwili baadae timu ya Coastal ikiwa timu ya saba, ilipotwaa ubingwa wa mwaka 1988, ila bado Simba na Yanga zilifanikiwa kutwaa ubingwa huo mara 11 katika kipindi cha miaka 14 ya mwisho kuelekea karne ya 21. Mtibwa ilitwaa ubingwa mwaka 1999 na kuutetea mwaka 2000 na kuwa timu ya nane na ya mwisho kutwaa ubingwa huo hadi sasa.

kuanzia, mwaka 2001 hadi sasa ni Simba na Yanga tu ndiyo zimekuwa zikitawala ligi hiyo hadi sasa. Yanga imetwaa mara saba, na Simba imetwaa mara sita katika misimu 13 ya mwisho. Misimu sita ya karibuni imekuwa ni migumu sana kwao, na pengine mataji waliyotwaa miaka kumi ya m,wisho yapo ambayo yalikuwa na mitahani mikubwa na yalinogesha ligi kuu kwa ushindani mdogo uliokuwepo, mwaka Mwaka, 2002, ubingwa ulikuwa ni wa Tanzania Prisons ila ' waliuzwa' na kupoteza nafasi hiyo kwa mabao 4-1 katika dimba la Sokoine, mbele ya Yanga.

2003 ubingwa ulikuwa mikononi mwa Mtibwa, lakini Simba waliokuwa nafasi ya nne wakatwaa taji siku ya mwisho ya msimu. Mtibwa ilitakiwa kuifunga Twiga Sports ili kuwa mabingwa pasipo kujali matokeo ya timu nyingine, kama Mtibwa ingefungwa kama ilivyotokea, nafasi ilikuwa kwa mshindi wa mchezo wa Mbeya, kati ya Tanzania Prisons na Yanga, nako matokeo yakawa sare na kutoa nafasi kwa Simba iliyoifunga AFC Arusha, mjini Morogoro kutwaa ubingwa.


Mwaka, 2005, kilichoikuta Moro United kilimuondoa kabisa kwenye soka aliyekuwa mmiliki wa timu hiyo. Moro ilishindwa kupata pointi 15 katika michezo 15 ya raundiu ya pili mwaka 2005, ila waliweza kushinda michezo yote 15 ya raundi ya kwanza na kukusanya pointi 45. Sijui nini kiliwakuta, Ivo Mapunda, Shadrack Nnsajigwa, Salum Sued, Lulanga Mapunda na Waziri Mahadhi wanajua vizuri. Timu ' iliuzwa', ilikuwa washambuliaji wanafunga, walinzi wanafungisha. Yote sababu ya Simba na Yanga.


Msimu wa 2007/ 08 nafasi ilikuwa ya Prisons ila Yanga wakatoka chini na kufuta ' gepu' la pointi 11 kuanzia mwezi, januari hadi april na kutwaa taji. Simba ikatwaa ubingwa pasipo kufungwa mchezo wowote msimu wa 2009/ 10 ila walionekana ' nyanya' katika michuano ya Cecafa na Caf. Wakati wanachama wa klabu hizo wakiamua kuanzia au kumiliki klabu zao binafsi, ligi ilifikiliriwa kuwa ingekuwa imepata unafuu na kuwa bora zaidi, ila wakati Simba au Yanga, zikiwa katika hali mbaya, viongozi wa klabu kubwa huanza kuwatumia wachezaji wa timu pinzani huku ahadi yao kubwa ilikuwa ni kusajiliwa katika timu hizo. Upenzi uliotukuka kwa baadhi ya watu ndani ya timu nyingine ndiyo uliwanyima ubingwa baadhi ya timu huku zikionekana kuwa na uwezo wa kufanya hivyo. Rejea wakati ule, kwa Prisons, Mmtibwa, Twiga Sports, 82 Rangers, Moro United na kwa sasa Azam FC.


UDHAIFU WA KIUCHUMI ULIKUWA UKIWABEBA SIMBA NA YANGA

Simba na Yanga, wala si timu tajiri, hazina vitega uchumi vya kueleweka ila timu hizo zina watu wa pesa, zina wapenzi wenye pesa na pengine jambo hilo ndilo limekuwa likiwafanya kuwa na nguvu ya kutwaa ubingwa hata kwa njia za nje ya uwanja.. Udhaifu wa kiuchumi wa timu kama Bandari Mtwara, Polisi Dodoma, Polisi Morogoro, AFC Arusha, Majimaji, Villa Squad, Manyema Rangers, Coastal Union, Moro United, Toto Africans, na nyinginezo ambazo hazikuwa na uwezo au uhakika wa kuwalipa posho wachezaji wao achilia mbali mishahara yao ya mweizi, uwezo mdogo wa kumudu gharama za kiwango cha kawaida cha kuwasafirisha na kuwahudumia wachezaji wao, mambo hayo pia yamekuwa yakichangia ubora wa Simba na Yanga.


Azam walikuja na nmguvu na kufikiri kuwa wangeweza kushindana na kuzishinda Simba na Yanga kwa pamoja na kutwaa ubingwa. Ni kazi sana, ndiyo maana nao wameongeza udhamini katika ligi ili kujifanya timu nyingine pia kuwa na uwezo wa kucheza pasipo kuwa na chakula, viatu vya kucheza, na usafiri wa uhakika, kwa sasa kila timu inaingiza zaidi ya millioni 160 kwa mwaka kutoka kwa wadhamini wa ligi kuu pekee, Azam tv na kampuni ya simu ya mkononi ya Vodacom, ni dalili kuwa yale malalamiko madogo madogo kama posho, mishahara, usafiri na gharama ya malazi hayatakuwepo na kama yapo basi ni udhaifu wa viongozi wa klabu.


Ukitazama kwa sasa hali ya mambo jinsi ilivyo katika ligi kuu utaona ukweli kuwa udhamini umeongeza nguvu na hali mpya kwa wachezaji wa kila timu. Hata kama duru la pili ndiyo ' fainali ezeeni' ila hadi sasa tumeweza kujifunza kitu, kuwa ya kwamba soka linachezwa pasipo malalamiko ya kipuuzi kama ilivyokuwa misimu ya nyum,a, hatusikii timu kushindwa kusafiri, atusikii malalamiko ya wachezaji kugomea timu zao kwa kuwa hawalipwi mishahara, hatusikii malalamiko ya malazi yasiyovutia, tumekuwa tukisikia matatizo ya uchezashaji na vurugu za mashabiki.


Majuzi, mashabiki wa Simba walivunja viti wakati walipolazimishwa sare na Kagera Sugar, iliumiza sana kwa kuwa Simba ilikuwa ikicheza mchezo wake wa tano mfululizo pasipo kushinda, na wakati wakikaribia kufanya hivyo wakajikuta wakinyang'anywa tonge mdomoni. Unafikiri ilikuwa si penati? hapana hata kama macho yetu yanatuonesha kitu tofaoti mwamuzi hakudhamilia kuimaliza Simba, labda wanaona wao ndiyo wenye haki ya kushinda kila mchezo, na siyo Mbeya City ambayo imeshinda michezo mitano mfululizo. Sishangazwi sana na kinachotokea sasa ila nitapenda kuona Simba na Yanga wakiziheshimu timu nyingine na kufanya jitihada kubwa ili wapate ushindi vinginevyo, vurugu hazitakoma. Msimu huu, Yanga ndiyo walianza pale walipocheza na Ccoastal Union, kisha wakafuata mashabiki wa City, na sasa Simba.


Simba, na Yanga hazitakufa ila zinatakiwa kukubali changamoto mpya. Hivi sasa timu zimejiandaa, timu zina uwezo wa kuwagharamikia wachezaji wao mahitaji muhimu. Ila naamini kiufundi na mbinu bado zitakuwa juu, zikubali tu mabadiliko na changamoto zinazotokea sasa katika ligi kuu, waongeze uwezo wao wa mbinu, maarifa, ufundi na zaidi watambue kadri miaka inavyosonga, rushwa inazidi kupoteza nguvu katika soka. Wafikirie kutwaa ubingwa bila......


Msomaji, kiu gani umekipenda hadi sasa katika ligi kuu? Au kipi ambacho kimekukera hadi sasa? Tupe maoni yako pia na yatafanyiwa kazi
0714 08 53 08

MALINZI AKABIDHIWA OFISI TFF, TENGA AMKABIDHI SH. Mil 35, NYAMLANI AINGIA MITINI


RAIS mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi mchana huu amekabidhiwa rasmi ofisi za shirikisho sambamba na viongozi wenzake walioingia madarakani wikiendi iliyopita tayari kwa kuanza kazi.
Malinzi alikabidhiwa ofisi na nyaraka mbalimbali na rais aliyemaliza muda wake, Leodegar Chilla Tenga huku viongozi kadhaa wa serikali wakishuhudia.
Miongoni mwa viongozi waliokuwepo katika ofisi hizo ni Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Dioniz Malinzi na Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo.
Kabla ya kufanyika kwa makabidhiano hayo, Tenga alipata muda wa kuhutubia ambapo aliuomba uongozi mpya ulioingia madarakani kuhakikisha unaendeleza dhana ya utawala bora ambayo ilienziwa na uongozi wake ulioingia madarakani kwa mara ya kwanza Desemba 2004.
Tenga pia aliutaka uongozi mpya chini ya Malinzi kuhakikisha inatekeleza mradi wa utengenezaji wa makao makuu ya TFF pamoja na miradi iliyobuniwa kuzunguka ofisi hizo kwa kuzingatia eneo la makao makuu hayo.
“Nakutakia uongozi mwema ndugu yangu Malinzi na timu yako, jambo la muhimu ni kuhakikisha ile dhana ya utawala bora ambayo sisi tuliianza nyie hakikisheni inaendelea na mnakuwa makini na wawazi katika mambo yenu hasa fedha maana huko ndiko kwenye maneno mengi.
“Pia hakikisheni huu mradi wa kuboresha ofisi za TFF unafanyika haraka ili uweze kuendana na hadhi ya taasisi hii nyeti katika michezo nchini, nadhani kwa kufanya hivyo mtakuwa mmeweka mtaji mzuri wa kiungozi na hata umma utawaona ninyi mnafaa kuendelea kusukuma gurudumu ili la maendeleo ya soka nchini.
“Mimi namfahamu ndugu yangu Malinzi kama mfanyabiashara tena mwenye mafanikio makubwa, sasa kwa kuongoza TFF nadhani atafanya vitu vingi kuhakikisha TFF inafaidika na weredi wake katika biashara,” alisema Tenga.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi alisema ana uhakika uongozi mpya wa TFF utafanya kazi kwa kushirikiana katika kuinua soka nchini na kuweza kupiga hatua kubwa za kimaendeleo.
“Sitoi sifa hizi eti kwa kuwa huyu (Jamal) ni mdogo wangu, lakini imani yangu ipo kwa watu wote waliochaguliwa naye katika kuongoza soka nchini, nadhani hawa wataweza kutufikisha mahala tunapokutaka,” alisema Dioniz Malinzi.
Kwa upande wake, Thadeo aliupongeza uongozi ulioondoka marakani huku akiutakia uongozi mwema uongozi ulioingia madarakani chini ya Malinzi.
“Tenga na wenzake wamefanya kazi nzuri na ninyi mnaoanza kazi leo mna kila sababu ya kuendeleza mazuri yaliyoanzishwa na Tenga na wenzake, mkifanya hivyo itaonekana wazi wajumbe hawakukosea kuwachagua,” alisema Thadeo.
Naye Silaa aliwasifu TFF kwa kuendesha uchaguzi huru na wa haki na aliwatakiwa uongozi mwema Malinzi na wenzake.

TENGA AKABIDHI SH. 37 MILIONI KWA MALINZI
Uongozi ulioamliza muda wake umekabidhi kiasi cha fedha Sh. 35 Milioni tu kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato kutoka ndani ya taasisi hiyo.
Tenga alisema mchanganuo wa fedha hizo ni kwamba fedha taslimu ni Sh. 33,518,000 na dola za kimarekani 1,390 zipo katika akaunti hivi sasa. Hii ni baada ya TFF kufanya malipo ya Shilingi 158,000,000 kwa ajili ya Mkutano Mkuu (uliofanyika wiki iliyopita) na malipo ya Shilingi 56,240,000 yaliyofanyika kwa ajili matayarisho ya timu ya Taifa ya Wanawake U-20 na gharama za mchezo baina ya timu ya Taifa na ile ya Msumbiji uliofanyika wiki iliyopita. 
Hata hivyo, Tenga alisema leo hii kiasi cha Sh. 664,000,000 kimehamishwa kutoka kwenye Akaunti za TBL kwenda kwenye Akaunti za TFF. Fedha hizo zitakuwa tayari kwenye Akaunti ya TFF ifikapo Jumanne wiki ijayo.  Malipo haya yalikuwa yafanyike karibu miezi miwili iliyopita lakini yalicheleweshwa ili kutoa nafasi kwa zoezi la ukaguzi wa fedha za udhamini wa TBL kufanyika.
Tenga alisema zoezi limefanyika vyema na kufikia ukingoni, ndiyo maana malipo yamefanyika. Malipo mengine yanayofanana na hayo, ya Sh. 672,000,000 yanatarajiwa kufanyika wiki mbili kutoka sasa.
MALINZI APIGA MKWARA VURUGU, UONGOZI WA KISASI
Muda mfupi bada ya kukabidhiwa ofisi, Rais mpya wa TFF, Jamal Malinzi alisema kamwe hatovumilia kuona watu wanafanya au kuhusika na vurugu, kabla, wakati na baada ya mchezo wowote wa soka nchini kwani kwa kufanya hivyo ni kukandamiza soka la Tanzania.
“Haingii akilini kwa shabiki aliyeacha familia yake anakwenda uwanjani na kuanzisha vurugu zisizo na maana, kama unahisi timu yako imeonewa zipo taratibu za kufuata ili kila mtu aweze kupata haki yake, narudia tena vurugu si suluhisho la kupata haki na sisi tutawashughulikia watu wa namna hii,” alisema Malinzi.
Malinzi alisema chini ya utawala wake atahakikisha kila kitu kinashughulikiwa na uongozi husika kwani haiwezekani mwamuzi kuadhibiwa na kamati isiyohusiana na uamuzi.
“Kila mwenye makosa sasa ataadhibiwa na kamati inayohusika na mkosaji moja kwa moja, kama ni mwamuzi basi kamati ya uamuzi ndiyo itakayoshughulika naye an si vinginevyo,” alisema Malinzi.
NYAMLANI AINGIA MITINI
Aliyekuwa mgombea urais wa TFF, Athuman Nyamlani ambaye katika uongozi uliopita alikuwa makamu wa rais, hakuweza kuonekana katika makabidhiano hayo na haikufahamika mara moja sababu ya yeye kufanya hivyo huku akiwa ni mmoja wa viongozi wa juu waliomaliza muda wao.

Friday, November 1, 2013

MSIMAMO WA LIGI KUU: YANGA YAWASHUSHA AZAM, YAKAMATA KILELE, SIMBA WASHIKA NAFASI YA NNE



YANGA YAENDELEZA WIMBI LA USHINDI, YAICHAPA JKT RUVU 4 - 0


Kikosi cha Young Africans kilichoanza leo dhidi ya JKT Ruvu






















Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Young Africans leo imekamata kiti cha uongozi baada ya kuendeleza wimbi la ushindi mfululizo kwa kuichapa timu ya Maafande wa jeshi la Kujenga Taifa nchini JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani kwa mabao 4- 0 mchezo uliofanyika katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kikosi cha mholanzi Ernie Brandts kiliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha kinapata pointi 3 muhimu , jambo ambalo vijana wake walilitekeleza na kuwapa furaha washabiki, wapenzi na wanachama wa klabu ya Yanga waliokwepo uwanjani kushuhudia mchezo huo.
 
Mshambuliaji Mrisho Ngassa aliipatia Young Africans bao la kwanza dakika ya 3 ya mchezo kwa shuti kali baada ya kuwatoka walinzi wa JKT Ruvu na kumtazama amekaa vipi mlinda mlango wa JKT Ruvu na kuukwamisha mpira wavuni.
 
Dakika ya 12 ya mchezo, Mrisho Ngassa tena aliwainua vitini mashabiki wa timu ya Young Africans baada ya kumalizia mpira ulipogwa na Saimon Msuva kabla ya kuwababatiza walinzi wa JKT Ruvu na kumkuta mfungaji ambaye aliukwamisha mpira wavuni kwa kichwa.
 
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, JKT Ruvu 0 - 2 Young Africans .
 
Kipindi cha pili cha mchezo kilianza kwa kasi na Young Africans kupata bao la tatu la mchezo dakika ya 47 kupitia kwa Oscar Joshua ambaye alikutana na mpira uliokolewa walinzi wa JKT na kumkuta mfungaji ambaye alifunga bao lake la kwanza tangu ajiunge na klabu ya Yanga miaka mitatu iliyopita.
 
Mabadiliko yaliyofanya na kocha mholanzi Ernie Brandts kuwaingiza Reliants Lusajo, Ibrahim Job na Jerson Tegete yaliongeza kasi na uwezo wa kumiliki mchezo kwani waliweza kucheza vizuri na kulilinda lango lao lisipatwe na madhara yoyote.
 
Dakika ya 89 Jerson Tegete aliipatia Yanga bao la nne la mwisho katika mchezo huo kufuatia migongeo ya Saimon Msuva na Ngassa kabla ya kumkuta Tegete akiwa peke yake na kuukwamisha mpira wavuni.
 
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, JKT Ruvu 0 - 4 Young Africans

Young Africans: 1.Dida, 2.Twite/Job, 3.Oscar, 4.Cannavaro 5.Yondani/Lusajio, 6.Chuji 7.Msuva 8.Domayo, 9.Kavumbagu/Tegete, 10.Ngassa, 11.Kiiza

source: http://www.youngafricans.co.tz

Thursday, October 31, 2013

MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUMENYANA BONANZA LA NANI MTANI JEMBE SONGEA.

Na Mwandishi Wetu

Mashabiki wa Simba na Yanga mjini Songea watamenyana vikali katika michezo mbalimbali kupitia bonanza maalum la Nani Mtani Jembe lililoandaliwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager litakalofanyika uwanja wa Maji Maji mjini Songea Jumapili wikendi hii.

Mratibu wa bonanza hilo Amadeus Kalumuna, amesema kuwa michezo mbalimbali ikiwemo soka bonanza la wachezaji saba kila upande, kuvuta kamba, na pia mpira wa mezani maarufu kama fussball itapamba bonanza hilo. Burudani mbalimbali pia zitapamba bonanza hilo zikiwemo burudani ya muziki kutoka bendi ya Mastaa wa Kusini, kikundi cha sanaa cha Umoja Star au maarufu kama “Manyoka”, wacheza show wa Chicharito Group pamoja na wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya wa mkoani Ruvuma.

Kalumuna pia amesema kuwa vilevile kuwa michezo mbalimbali ya kujifurahisha kama vile kufukuza kuku wa kienyeji, kukimbia na gunia na kupiga penati ukiwa umefungwa kitambaa usoni itapamba bonanza hilo ambalo ni la kwanza kufanyika katika mkoa wa Ruvuma kupitia Nani Mtani Jembe. Kampeni hii ya aina yake inatoa fursa ya kipekee kwa mashabiki hao kujumuika pamoja na kuburudika na vile vile imeongeza chachu ya ushindani na utani wa jadi kati ya mashabiki hao huku ikiwapa fursa ya kipekee kuonyesha mapenzi kwa timu zao.

Bonanza hilo linalotarajiwa kuanza saa tatu asubuhi ni mwendelezo wa kampeni ya Nani Mtani Jembe ambayo ilizinduliwa Oktoba 2 na  inafanyika nchi nzima ikiwashirikisha mashabiki wa timu kongwe za Simba na Yanga. Kupitia kampeni hiyo, Kilimanjaro Premium Lager inayozidhamini timu za Simba ya Yanga imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 na kisha kuzigawanya kwa timu hizo ambapo kila timu inazo shilingi milioni 50 ambazo zinashindaniwa na mashabiki wao.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe alisema kuwa mashabikiwa Simba na Yanga wanatakiwa kushindana kwa kushiriki kwenye kampeni hiyo ili kuhakikisha kuwa timu mojawapo inapata fedha nyingi zaidi ya timu nyingine.
Akielezea namna ya kushiriki, Kavishe alisema kuwa mpaka kila timu imetengewa shilingi milioni 50 na kuwa mshiriki wa shindano hilo la Nani Mtani Jembe ambaye ni shabiki wa Simba au Yanga anachotakiwa kufanya ni kununua bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambayo kwenye kizibo chake kuna namba ya kushiriki.

Alisema baada ya shabiki kununua bia ya Kilimanjaro na kuona namba ya kwenye kizibo, anachotakiwa kufanya ni kuchukua simu yake ya kiganjani na kuandika ujumbe mfupi wa maneno akianza na jina la timu anayoshabikia kisha anaandika namba iliyo kwenye kizibo na kuituma kwenye namba 15440.

Alisema baada ya shabiki kutuma namba hiyo, atakuwa amepunguza shilingi 1,000 kutoka kwa timu pinzani yaani ikiwa shabiki aliyetuma ujumbe huo ni wa Simba atakuwa amefanikiwa kupunguza shilingi 1,000 kutoka kwenye fungu la Yanga na ikiwa shabiki ni wa Yanga pia atakuwa amepunguza shilingi 1,000 kutoka kwa Simba.

Kwa mujibu wa Kavishe matokeo ya uwiano wa fedha zinavyopungua kutoka Simba au Yanga yatangazwa kila siku hadi siku ya mwisho wa shindano hilo Desemba 14, mwaka huu.

MASHABIKI WAVUNJA VITI 100, ADHABU YAINYEMELEA SIMBA - ANGALIA PICHA MECHI NA VURUGU



SEKUNDE chache kabla ya mwamuzi Mohamed Theofile wa Morogoro hajamaliza pambano la Ligi Kuu ya Bara kati ya Simba na Kagera Sugar, mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Simba, wamevunja viti zaidi ya 100 na kuvirusha uwanjani imefahamika.
Mwandishi wa mtandao huu alishuhudia mashabiki hao wakivunja na kuvirusha uwanjani viti hivyo baada ya mwamuzi huyo kuwapa Kagera penalti iliyofungwa na Salum Kanoni.
Mashabiki hao ambao licha ya kuwa walikaa katika majukwaa tofauti, waliweza kufanya kitendo hicho kwa kile kilichoelezwa baadaye kwamba ni kupingana na maamuzi ya mwamuzi huyo.
Viti vilivyovunjwa vingi vina rangi ya chungwa na bluu ambavyo kwa haraka haraka idadi yake inaweza kuwa zaidi ya 100.
Kutokana na hali hiyo, askari wa Jeshi la Polisi walilazimika kulipua mabomu matatu ya machozi ili kuwatuliza mashabiki hao walioonekana kuwa na hasira.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura ameuambia mtandao huu kwamba, kwa kitendo hicho kamati ya mashindano na ile ya nidhamu zinaweza kukaa na kutathimini uhalibifu uliofanywa na mashabiki hao kisha timu husika kuwajibika kulipa.
“Kila mtu ameona kilichotokea na vurugu za kuvunja viti zilianza tangu wakati wa mapumziko hivyo uchunguzi utafanyika na klabu iliyohusika italipa faini kama utaratibu ulivyo,” alisema Wambura kwa kifupi.    


 Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, akimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.
  Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, na Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden, wakimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.
 Wachezaji wa akiba wa Simba wakisikitika baada ya kuamuliwa kupigwa penati hiyo.
 Askari wakiendelea kumdhibiti shabiki aliyekamatwa baada ya mashabiki hao kuvunja viti na kuanza kuruka uwanjani.
Askari wakiendelea kudhibiti vurugu..
 Sehemu ya viti vilivyoharibiwa....
 Wachezaji wa Simba, wakimpongeza beki wao Salum Kanon, baada ya kusawazisha bao hilo kwa mkwaju wa penati.
 Patashika langoni mwa Kagera Sugar.
 Kiungo wa Kagera Sugar, George Kavila (kulia) akimtoka mshambuliaji wa SImba, Amis Tambwe, wakati wa mchezo huo.
 Amis Tambwe, akidhibitiwa.
 Ramadhan Singano wa Simba (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Kagera Sugar, Malegesi Mwangwa.
 Hatari langoni mwa kagera.
 Tambwe akidhibitiwa. (PICHA ZOTE KWA HISANI YA SUFIANI MAFOTO WEBSITE)

SIMBA YAVUTWA NA KAGERA SUGAR TAIFA LEO, MABOMU YAPIGWA UWANJANI


PENALTI iliyopigwa dakika za nyongeza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Bara uliozikutanisha Simba na Kagera Sugar muda mfupi uliopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilibadili matokeo na kufanya mchezo huo kuisha kwa sare ya bao 1-1.
Huku mashabiki wengi wakidhani mechi hiyo ingemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0, mwamuzi Mohamed Theofile wa Morogoro aliipa penalti Kagera wakati mwamuzi wa akiba akiwa ameshaonyesha dakika nne za nyongeza na mashabiki kutoamini kilichotokea.
Beki Joseph Owino ndiye aliyesababisha penalti hiyo baada ya kumchezea vibaya Daudi Jumanne wa Kagera ndani ya eneo la hatari ambapo, beki Salum Kanoni wa Kagera alifunga penalti hiyo na sekunde chache baadaye mwamuzi alimaliza pambano hilo.
Awali Simba ilipata bao la kuongoza dakika ya 45 lililofungwa na Amisi Tambwe baada ya mabeki wa Kagera kujichanganya katika kuokoa. Bao hilo lilidumu hadi timu hizo zilipoenda kupumzika.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi lakini hadi dakika ya 85, hakuna timu iliyoweza kupata bao kutokana na safu zote za ushambuliaji kutokuwa makini.
Mshambuliaji wa Kagera, Themi Felix pamoja na winga Paul Ngwai leo hawakuweza kufurukuta mbele ya mabeki wa Simba waliokuwa wakiongozwa na nahodha wao Nassor Masoud ‘Chollo’.
Nao washambuliaji wa Simba, Tambwe na Betram Mombeki hawakuweza kufuruka kutokana na mabeki wa Kagera kucheza kwa nguvu zaidi wakiongozwa na Maregesi Mwangwa ambaye ni nahodha wao.
Muda mfupi baada ya Kanoni kufunga bao, alienda kushangilia akiwa sambamba na wenzake mahala ambapo mashabiki wa Simba wamekaa na kuzua tafrani ya kurushiwa chupa za maji na viti vilivyovunjwa na mashabiki hao.
Kutokana na hali hiyo, askari wa Jeshi la Polisi waliokuwepo uwanjani hapo walilazimika kulipua mabomu matatu ya machozi ili kutawanya mashabiki hao, hali iliyozua hali ya taharuki uwanjani hapo.
Matokeo haya yanaifanya Simba kufikisha pointi 21 na kubaki katika nafasi ya nne baada ya kucheza mechi 12.Nayo Kagera imepanda hadi nafasi ya tano ikiwa na pointi 17.

;LIVE SCORE: SIMBA SC 1 - 1 KAGERA SUGAR



Mashabiki wa Simba wanang'oa viti vya uwanja wa taifa na mashabiki wanapambana na Polisi ambao wanalipua mabomu ya machozi. 

Dk 90+5 FULL TIME! Simba 1-1 Kagera. 

Dk 90+4 GOOOOO....! Salum Kanoni anaipatia Kagera bao la kusawazisha kwa njia ya penalti. Simba 1-1 Kagera. 

Tunaomba radhi kwa uchelewaji wa updates ni kutokana na network mbovu uwanjani.

Dk 84 Tambwe anachezewa faulo na Martin Muganyizi. Simba 1-0 Kagera. 

Dk 73 Kagera wanapiga faulo na kukosa. 

Dk 73 Kipa wa Simba anachelewesha mpira na mwamuzi anaamuru faulo ipigwe kuelekea lango la Simba. Simba 1-0 Kagera. 

DK 60 Simba 1 - 0 Kagera 

Dk 57 Timu zinashambuliana kwa zamu na Kagera wanaonekana wameamka. 
Kipindi cha pili kinaanza
Dk 45 HALF TIME...! Simba 1-0 Kagera. 

Dk 45 GOOOOO...!  Simba imepata bao la kwanza kupitia kwa Amisi Tambwe ambae aliwatoka mabeki wa Kagera, Salum Kanoni na Ernest Mwalupani. 

DK 40 Simba wanalisakama lango la Kagera wakisaka goli. Ila milango bado ni migumu.

DK 30' Simba 0-0 Kagera Sugar 

Dk 21 Kagera wamefanya mabadiliko ya kipa, katoka agaton anthony ambaye ameumia bada ya kugongana na Tambwe kaingia hannington kalyesubula. 

DK 10 - Simba 0-0 Kagera Sugar

DK 5 Timu zinacheza soka taratibu kwa kusomana

Dk 00 MPIRA UMEANZA! 

Simba: Abuu Hashimu, Nassoro Masoud 'Chollo', Issa Rashid, Joseph Owino, Hassan Khatib, Jonas Mkude, Ramadhani Singano, Said Ndemla, Betram Mwombeki, Amisi Tambwe na William Lucian

Kagera Sugar: Agaton Antony, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Ernest Mwalupani, Malegezi Mwangwa, Zuberi Dabi, Benjamin Asukule, George Kavilla, Themi Felix, Daudi Jumanne na Paul Ngwai

Wednesday, October 30, 2013

SIR ALEX FERGUSON AVUNJA REKODI NYINGINE - MAUZO YA KITABU CHAKE YAFUNIKA

Hot cakes: Fergie's book has been a quick seller
Hot cakes: Fergie's book has been a quick seller
REUTERS
Kitabu cha Sir Alex Ferguson kimeweka rekodi ya kuwa kitabu kilichooza kwa haraka zaidi ndani ya Uingereza kikiuza nakala 115,547 katika siku chache za mauzo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka The Bookseller, kitabu hicho cha mocha wa zamani wa Manchester United kimevunja rekodi ya  Delia Smith,  ambaye kitabu chake cha mwaka 1999 cha mapishi kiliuza kopi 112,000 katika wiki take ya kwanza.

Pia kitabu cha Fergie kimevunja rekodi ya mauzo ya kitabu cha rafiki yake waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair, ambacho kiliuza kopi 92,000 katika wiki ya kwanza.

VITABU VILIVYOUZA ZAIDI UK:
Sir Alex Ferguson - My Autobiography - 115,547
Delia Smith - How to Cook - book two - 112,000
Tony Blair - A Journey - 92,000
David Beckham - My Side - 86,000
Paul Burrell - A Royal Duty - 77,000

SIMBA KURUDISHA MAKALI YAKE KESHO DHIDI YA KAGERA SUGAR???


SIMBA, KAGERA SUGAR KUUMANA KESHO
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaanza raundi ya 12 kesho (Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Viingilio katika mechi hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kupitia TBC 1 vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A.

Nayo Yanga itashuka uwanjani Novemba Mosi mwaka huu katika mechi nyingine ya ligi hiyo dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.

Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

PAMBANO LA YANGA, MGAMBO SHOOTING LAINGIZA MIL 37/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Mgambo Shooting lililochezwa jana (Oktoba 29 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 37,915,000.

Washabiki waliohudhuria mechi hiyo namba 46 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 walikuwa 6,515 ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 5,783,644.07, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,145,790 wakati kila klabu ilipata sh. 8,550,741.95.

Wamiliki wa uwanja walipata sh. 4,347,834.89, gharama za mchezo sh. 2,608,700.93, Bodi ya Ligi sh. 2,608,700.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,304,350.47, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,014,494.81.

URAISI WA TFF - RAISI WA CAF ISSA HAYATOU AMPONGEZA JAMAL MALINZI


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Issa Hayatou amempongeza Jamal Malinzi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 27 mwaka huu.

Katika salamu zake kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF na familia ya mpira wa miguu Afrika, Rais Hayatou amesema uchaguzi huo unampa Rais Malinzi fursa ya kuupeleka mbele mpira wa miguu nchini Tanzania.

Amesema CAF ina imani uwezo wake katika uongozi, uzoefu na ujuzi katika mpira wa miguu havitausaidia mpira wa miguu Tanzania pekee bali Afrika kwa ujumla, na kuongeza kuwa ataendeleza ushirikiano uliopo ili kuwanufaisha zaidi vijana wa bara hili.

Rais Hayatou amemtakia Rais Malinzi kila la kheri katika kipindi chake cha uongozi na kumhakikishia kuwa CAF iko pamoja naye katika kusukuma mbele gurudumu la kuendeleza mpira wa miguu.


FIFA YATOA MAJINA YA WANASOKA WANAOWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA.



YANGA YAENDELEZA WIMBI LA USHINDI LIGI KUU - YAIPIGA MGAMBO 3-0


Kikosi cha Young Africans kilichoanza dhidi ya Mgambo Shooting


 Young Africans mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara leo wameendeleza wimbi la ushindi baada ya kuichapa timu ya Mgambo Shooting kutoka mkoani Tanga kwa mabao 3-0, mchezo uliofanyika katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Ikiwa na kumbukumbu ya ushindi katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Rhino Rangers kwa mabao 3-0, kikosi cha Young Africans kiliingia uwanjani kwa lengo la kuendeleza wimbi la ushindi na ndivyo hali ilivyokuwa

Hamis Kiiza, Saimon Msuva na Mrisho Ngasa walikosa mabao ya wazi dakika 15 za kipindi cha kwanza kufuatia kutokua makini katika umaliziaji na kujikuta mipira yao ikitoka pembeni mwa lango la Mgambo Shooting na mingine ikiokolewa na golikipa wa Mgambo Shooting Tonny Kavishe.

Mbuyu Twite aliipatia Young Africans bao la kwanza Young Africans dakika ya 31 ya mchezo kwa shuti kali la mita 25 kwa mpira wa adhabu alioupiga na kujaa moja kwa moja wavuni na kuamsha shangwe kwa washabiki wa Yanga.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 1 - 0 Mgambo Shooting.

Kipindi cha pili kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo aliingia nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' kuchukua nafasi ya Rajab Zahir mabadiliko ambayo yaliongeza uwezo wa kumiliki mchezo na kulinda vyema lango lao.

Dakika ya 50 ya mchezo, Hamis Kiiza 'Diego' aliipatia Young Africans bao la pili kwa mkwaju wa penati kufuatia mlinda mlango wa Mgambo Shooting Tony Kavishe kumuangusha Didier Kavumbagu ndani ya eneo la hatari na mwamuzi kuamuru ipigwe penati ambayo Kiiza hakufanya makosa.

Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao tatu la mchezo dakika ya 67 ya mchezo baada ya mpira uliorushwa na mlinzi Mbuyu Twite kumkuta Kavumbagu ambaye aliwazidi maarifa walinzi wa Mgambo Shooting na kuukwamisha mpira wavuni.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 0 Mgambo Shooting.

Msimu uliopita katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika kati ya timu hizi Young Africans pia iliibuka na ushindi wa mabao 3-0, mabao yaliyofungwa na Didier Kavumbagu, Jerson Tegete na Nadir Haroub 'Cannavaro'

Young Africans: 1.Dida, 2.Twite 3.Oscar, 4.Rajab/Cannavaro 5.Yondani, 6.Chuji, 7.Msuva/Lusajo 8.Domayo, 9.Kavumbagu, 10.Ngassa, 11.Kiiza

Tuesday, October 29, 2013

BAHATI MGUNGA- ''UMUHIMU WA KUWA NA VILABU IMARA,VIONGOZI WA MIKOA IMARA''.




TEGETE NI MFUNGAJI MZURI BADO ILA AMEKOSA UMAKINI TU


Na Baraka Mbolembole
" Ni kweli sisi wachezaji tunajua kuwa mashabiki wanazipenda timu zao, hasa kwa wale wa timu yetu ya Yanga tunajua wanaipenda sana timu yao, lakini nawashauri wabadilike sasa, wasiwazomee wachezaji wakati wanapokuwa wanafanya vibaya. Wawe na subira kama kweli wanaipenda timu yao. Kelee zao huwatoa mchezoni wachezaji na kujikuta wakifanya vibaya zaidi, na hili hupelekea hata kwa wale wachezaji wanaokuja kuingia katika uoga, nawasihi wawe na uvumilivu"
Ni maneno ya mshambuliaji aliye katika wakati mgumu hivi sasa katika klabu ya Yanga, Jerry Tegete, wakati nilipofanya nae mazungumzo hivi karibuni kuhusiana na mwenendo wake usiovutia hadi sasa katika klabu hiyo.

Jerry ambaye alianza vizuri msimu huu pale alipofunga maba mbili siku ya ufunguzi wa msimu dhidi ya Ashanti United, na akafunga tena katika mchezo uliofuata hila amekuwa akipoteza nafasi za wazi mara kwa mara na kupelekea ,kuwakera wengi.
Wakati ushindani wa kuwania nafasi ukiwa ni mkubwa katika safu ya mashambulizi ya Yanga, ambayo imekusanya washambuliaji sita wa kati na wengine wawili wakiwa kama viungo washambuliaji, Jerry amejikuta akipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza, na katika siku za karibuni amekuwa akikosa hata nafasi ya kuingia kama mchezaji wa akiba.

Didier Kavumbagu, ameoneka kuwa chaguo la kwanza mbele ya kocha, Ernie Brandts, na Mrundi huyo ameweza kuwa kiongozi wa safu yote ya mashambulizi, nguvu, akili na uwezo wa kumiliki mpira, unaambatana na umakini mkubwa wa kutumia nafasi anazotengenezewa, ' Kavu' amekuwa chaguo bora mbele ya Tegete katika vitu vingi, mwanzoni mwa msimu walipangwa walikuwa wakipangwa pamoja na wakaonekana kuwa wafungaji wazuri, walifunga kwa vichwa, na uwezo binafsi na matokeo yake wakawa chaguo la kwanza.
" Ushindani ni mkubwa sana, na nafasi imekuwa ni ngumu, kila mchezaji hutumia nafasi anayopata vizuri" anaongeza, Tegete. 'Kavu', Tegete, Said Bahanunzi, Hussein Javu, Kondo awali walikuwa washindani wa kwanza katika nafasi hii, ila kurejea kwa Hamis Kizza aliyekuwa kwenye majaribio nchi ya ng'ambo, na kumalizika kwa adhabu ya Mrisho Ngassa kumefanya hali ya mambo kuwa magumu zaidi.
Lakini inakuwaje kwa mchezaji kama Jerry kuzomewa mara kwa mara na mashabiki wa timu yake? Wakati fulani hali hii iliwahi kumtokea kiungo wa zamani wa timu hiyo, Nurdin Bakari, hasa pale alipokuwa akifanya vibaya uwanjani, kila mtu alikuwa anafahamu uwezo wake, lakini pasi mbili au tatu tu ' mbovu' uwanjani zilikuwa ni tatizo. Kitu kizuri huleta furaha ya siku zote katika maisha, ni shida sana kukishusha chini kitu kizuri, mafanikio hayahitaji kubweteka na kupelekea mtu kujisahau kule alipotoka na alipokuwa amepanga kufikia, umakini, nidhamu ya mchezo, huwa ni sehemu ya mipango mizuri ya wachezaji wote waliofanikiwa. Wapo ambao walipitia njia ya kupingwa na kuzomewa na mashabiki wa timu zao ila bado wakafanya kazi nzuri uwanjani na kujikuta wakifanikiwa.

Dr. Martin Luther King Jr aliwahi kusema; " Ukimya wa rafiki yako unaumiza sana kuliko kelele za adui yako" pengine, manaharakati huyu wa haki za binadamu, na aliyekuwa mtetezi wa watu weusi katika Marekani, alikuwa na maana nyingi lakini ni vyema wakati mwinmgine wachezaji kama Tegete wakachukulia kelele za zomea zomea za mashabiki wao ni sehemu za kuwakumbusha kuwa hawafanyi vizuri. Na mashabiki hawatakiwi kufanya hivyo mara kwa mara klwa kuwa mara moja au mbili inatosha kufikisha ujumbe kwa muhusika.

Katika miaka mitatu ya karibuni, Tegete amekuwa akikumbwa na majeraha ya mara kwa mara, na hajawahi kucheza michezo sita mfululizo ndani ya misimu mitatu sasa klabuni kwake.
" Namshukuru Mungu kwa kila jambo, nashukuru hivi sasa nimepona goti, hilo ndilo lilikuwa ni la muhimu sana kwangu. Unajua hata sisi wachezaji hatupendi kufanya vibaya, wakati wa mchezo na Simba niliumia na kusikitika sana kwa sababu hadi nusu ya kwanza tunaongoza 3-0, kipindi cha pili wakarudisha goli zote.

Niliumia sana goli kurudi na nilikuwa nina imani tungeweza kuongeza bao lingine muda wowote. Simba walijitahidi sana" . Hili ni kweli kuwa hakuna mchezaji anayependa kufanya vibaya na wakati mweingine matokeo yao mabaya uwanjani hutokana na uwezo mzuri wa timu nyingine. Ila mimi binafsi nahitaji mabao kutoa kwa Tegete, nimechoka kumuona akipoteza nafasi rahisi mara kwa mara mchezoni, ila ujumbe wangu kwa mashabiki wa Yanga ni kwamba, ' Muacheni, Jerry acheze mpira sasa, baaada ya kucheza walau michezo mitao hadi saba mfululizxo mnaweza kumuhukumu' . Tegete ni mfungaji mahiri bado, amekosa umakini tu kama aliona nao Kizza au Kavumbagu.
0714 08 43 08

YANGA, MGAMBO JKT KUVAANA TAIFA LEO

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Bara leo itashuka katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kupambana na Mgambo JKT katika mchezo wa raundi ya kumi na moja ya ligi hiyo.

Yanga inaingia uwanjani leo ikiwa na pointi 19 ilizopata katika mechi 10 ilizocheza huku ikiwa nafasi ya nne. Azam inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 23 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 20 huku zote zikiwa zimecheza mechi 10. Mbeya City ni ya tatu ikiwa na pointi 20 katika mechi 10.

Kwa upande wao, Mgambo wanaingai uwanjani wakiwa na pointi tano walizopata katika mechi 10. Timu hiyo inaburuza mkia katika ligi hiyo.
Kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo kutakuwa mchezo utakaozikutanisha timu mwenyeji za mkoa huo ambazo ni Mbeya City na Tanzania Prisons. Rhino Rangers na JKT Ruvu zitacheza katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Raundi ya 12 ya ligi hiyo itaanza Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Novemba Mosi mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Yanga na JKT Ruvu kwenye uwanja huo huo.
Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.

Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Monday, October 28, 2013

MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM BAADA YA AZAM KUISURUBU SIMBA



KIBADENI AKUBALI YAISHE, MALARIA YAIPONZA SIMBA


MUDA mfupi tu baada ya timu yake kufungwa mabao 2-1 na Azam FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni, amesema, “Nakubali tumefungwa kwa haki na ni moja ya sehemu ya mchezo.”
Kibadeni amesema kiukweli mabao yote ya Azam yalitokana na makosa waliyofanya lakini amewasifu vijana wake kuweza kucheza vizuri hasa kipindi cha kwanza japokuwa wamefungwa. Hii ni mara ya kwanza Simba kufungwa katika msimu huu wa ligi ikiwa chini ya Kibadeni.
“Nakubali matokeo haya, nadhani wote mmeona jinsi mpira ulivyochezwa, wenzetu wametumia makosa yetu na kupata ushindi. Katika soka ukipata nafasi ya kufunga unatakiwa kufanya hivyo kama walivyofanya Azam, sasa tunajiandaa na mchezo ujao,” alisema Kibadeni.
Naalipoulizwa kutokuwepo kwa baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza kama mabeki Gilbert Kaze na Nassor Masoud ‘Chollo’ ambao nafasi zao zilichezwa na William Lucian ‘Gallas’ na Hassan Khatib, Kibadeni alijibu; “Wachezaji hao ni wagonjwa, Kaze anaumwa malaria kama ilivyo kwa Chollo ndiyo maana leo hamjawaona uwanjani.
“Kiasi fulani kukosekana kwao kumeifanya mechi hii kuwa ngumu kidogo maana hawa vijana bado wadogo wanaohitaji muda kuweza kumudu michezo mikubwa kama hii.”
Kibadeni pia hakumchezesha mshambuliaji Amisi Tambwe ambaye hadi sasa anaongoza kwa ufungaji katika ligi hiyo akiwa amefunga mabao nane, akifuatiwa na Hamisi Kiiza wa Yanga, Juma Liuzio wa Mtibwa na Elius Maguri wa Ruvu Shooting ambao wote wana mabao saba.
Kocah huyo alisema, hakuweza kumpanga Tambwe kutokana na kuwa majeruhi wa goti lakini anaweza kucheza mechi ijayo endapo afya yake itaimarika ndani ya saa 72 zijazo.
Ushindi huo wa Azam unaifanya timu hiyo kuishusha Simba kileleni mwa ligi hiyo na kuketi yenyewe ikiongoza kwa pointi 23 ilizopata baada ya kucheza mechi 11 kama ilivyo kwa Simba ambayo inapoteza mechi yake ya kwanza tangu kuanza kwa ligi hii msimu huu.
Matokeo hayo yanaifanya Simba kushika nafasi ya pili ikiwa na pointi 20 ilizopata baada ya kucheza mechi 11, ambapo imeshinda mechi tano na kutoka sare tano. Simba imefunga mabao 21 na kufungwa mabao 10.
Katika mchezo wake ujao, Simba itacheza na Kagera Sugar Oktoba 31 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku Azam ikipambana na Ruvu Shooting Novemba 2 mwaka huu kwenye Uwanaj wa Azam Complex, Dar es Salaam.

AZAM YAIPIGA SIMBA 2-1, YATIBUA REKODI YA MNYAMA, KIPRE TCHETCHE AFUNGA BAO LA MWAKA



BAO lililofungwa dakika ya 73 na mshambuliaji Kipre Tchetche raia wa Ivory Coast limeiwezesha Azam FC kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Bara uliochezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tcheche alifunga bao hilo akiwa wingi ya kushoto ya uwanja huo na alipiga shuti kali la chinichini akiwa pembeni mwa uwanja (impossible angle) na mpira kutinga wavuni moja kwa moja. Kipa Abel Dhaira wa Simba pengine alidhani mfungaji alipiga mpira huo kama krosi kwenda kwa John Bocco, hivyo hakuwa makini kuzuia mpira huo wa kwanza.
Awali Tchetche alikuwa amepokea pasi kutoka kwa Salum Aboubakary ‘Sure Boy’ kutoka katikati ya uwanja. Sure Boy alipokea pasi baada ya mshambuliaji wa Simba, Betram Mombeki kupokonywa mpira jirani na katikati ya uwanja.
Ushindi huo wa Azam unaifanya timu hiyo kuishusha Simba kileleni mwa ligi hiyo na kuketi yenyewe ikiongoza kwa pointi 23 ilizopata baada ya kucheza mechi 11 kama ilivyo kwa Simba ambayo inapoteza mechi yake ya kwanza tangu kuanza kwa ligi hii msimu huu.
Matokeo hayo yanaifanya Simba kushika nafasi ya pili ikiwa na pointi 20 ilizopata baada ya kucheza mechi 11, ambapo imeshinda mechi tano na kutoka sare tano. Simba imefunga mabao 21 na kufungwa mabao 10.
Bao la kwanza la Simba lilifungwa na Ramadhan Singano ‘Messi’ dakika ya 22 akimalizia pasi safi ya Zahor Pazi na kuamsha furaha kwa mashabiki wa klabu hiyo yenye maskani yake mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Baada ya kuingia kwa bao hilo, Simba ilionekana kutawala mchezo lakini Azam walizinduka kuanzia dakika ya 35 na kulishambulia lango la Simba kama nyuki na kufanikiwa kupata bao dakika ya 43 mfungaji akiwa ni Tchetche aliyemalizia kazi nzuri ya beki Erasto Nyoni.
Hadi timu hizo zinakwenda mapumziko matokeo yalikuwa ni bao 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa Azam kufanya mabadiliko ambapo walimtoa beki Said Moradi na nafasi yake kuchukuliwa na David Mwantika ambaye aliweza kupunguza kasi ya mashambulizi ya Simba kwa kiasi fulani.
Dakika 10 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Simba ilifanya mabadiliko baada ya kuwatoa kwa mpigo Zahor Pazi na Amri Kiemba na nafasi zao kuchukuliwa na Sino Augustino na Edward Christopher.
Mabadiliko hayo hayakuweza kuisaidai Simba licha ya mara kadhaa kufika langoni kwa Azam lakini washambuliaji wake Sino Augustino na Mombeki hawakuwa makini kumalizia mipira mingi waliyokuwa wakipewa na viungo.
Tatizo la ukabaji wa nafasi ndilo lililoigharimu Simba na kumfanya Tchetche aifungie Azam bao la pili dakika ya 73.
Katika mchezo wake ujao, Simba itacheza na Kagera Sugar huku Azam ikipambana na Ruvu Shooting.