Search This Blog

Saturday, June 18, 2011

MORRATI ATAKA KUMRUDISHA ITALY CAPELLO


Raisi wa klabu Inter Milan Massimo Moratti amekiri kuwa atakuwa na furaha kama kocha wa England Fabio Capello atarudi Italy kuja kuongoza Inter.

Inter ambayo msimu uliopita walishika nafasi ya pili katika Seria A wamempoteza kocha wao Leonardo ambaye amejiunga na Paris Saint German hivyo kupelekea timu hiyo kukosa mwalimu, na sasa Moratti ameanza mchakato wa kutafuta kocha mpya huku majina yakitajwa kuhusishwa na kibarua vha kuinoa timu hiyo yenye maskani yake Giuseppe Meazza.

Alipoulizwa kuhusu Capello na vyombo vya habari Italia Moratti amesema: "Nani asiyempenda Fabio? ni kocha mzuri na ningependa kufanya nae kazi."

Capello ambaye kwa sasa bado ana mkataba na Three Lions mpaka baada ya kuisha kwa michuano ya EURO 2012 itayofanyika nchini Poland na Ukraine.

Makocha wengine wanaotajwa kuja kumrithi Leonardo ni pamoja mchezaji wa zamani wa Inter Sinisa Mihajlovic anayefundisha Fiorentina, kocha wa Palermo Delio Rossi, kocha wa zamani wa Geneo Giampiero Gasperini, Louis Van Gaal na makocha wa zamani wa Brazil Dunga na Zico.


VILLARREAL YAKATAA OFA YA BARCA KWA ROSSI


Villarreal wamekataa ofa ya kutoka Barcelona kwa ajili ya kumsajili Giusseppe Rossi.

Wakala wa Rossi Federico Pastorello amesema kuwa ofa ya Barca ilikuwa ndogo ukilinganisha na bei ya mwanzo iliyotajwa na Villarreal.

"Nafahamu juu ya Barca kupeleka ofa kwa ajili ya Giusseppe, lakini tumeambia ofa yao ilikuwa haijitoshelezi. Hatujaongea na timu yoyote ndani ya wiki hii.Pia nafahamu kuwa Catalunya bado wanajadiliana na Villarreal, hivyo kikubwa tunachofanya sasa ni kusubiri matokeo ya majadiliano hayo." alisema wakala wa Rossi.

LIVE MATCH CENTRE: TZ VS NIGERA

MATCH UPDATE: BREAKING NEWS - MECHI IMEHAIRISHWA HADI KESHO KUTOKANA UWANJA KUJAA MAJI NA MVUA KUBWA KUENDELEA KUNYESHA.CAF WANASEMA KAMA KESHO HALI YA HEWA IKIENDELEA MECHI ITACHEZWA JUMATATU KATIKA MJI TOFAUTI.

MATCH UPDATE: Uwanja wa Samuel Ogbemudia umejaa maji, timu zimeingia
uwajani tangu saa 9 za hapa Nigeria na bado mvua kubwa inanyesha.Match Delayed





TANZANIA FIRST ELEVEN
1: Abdul Juma, 2: Juma Abdul, 3: Zuberi Ubwa, 4: Obadia Mangusa, 5: Shomari Kapombe, 6: Jabir Aziz, 7: Jamal Mnyate, 8: Mohamed Soud, 9: Thomas Ulimwengu, 10: Mbwana Samatta

NIGERIA FIRST ELEVEN
1: Ajiboye Muniru, 2: Edet Ibok, 3:Orelesi Nurudeen, 4: Nwankwo Obiora, 5:Haruna Lukman, 6: Ekigho Ehiosub, 7: Aluko Omatsone, 8: Suswam Terna, 9: Oseni Bolaji, 10: Udoh Kingsley 11: Ahmed Musa.

Mechi inaanza saa 12 za Tanzania na Saa 10 kamili za Nigeria.

SIMBA WAPEWA BASI NA CHAKULA KIBOVU LAKINI BASSENA ASEMA TUTASHINDA




KOCHA Mkuu ya Simba Mganda Moses Bassena amesema licha ya kupata ushindi kiduchu katika mchezo uliopita ana imani kikosi chake kitajituma na kupata ushindi katika mchezo wao wa leo dhidi ya Motema Pembe utakafanyika kwenye Uwanja wa Stade de Martyrs kiswaili ni Uwanja wa mashujaa.

Akizungumza Bassena alisema ana imani kubwa na kikosi chake katika mchezo leo ambapo Simba ikishinda itakuwa imeingia hatua ya makundi .

Bassena alisema kwa muda uliobaki atautumia kurekebisha machache ambayo yalijitokeza katika mchezo ule .

"Nina Imani kubwa na kikosi changu kitaisambaratisha Motema Pembe kesho kwa kuifunga nyumbani kwao"- Bassena.

Naye Nahodha wa Simba nico Nyagawa, amewataka watanzania kuiombea dua timu yao iweze kufanya vizuri katika mchezo huo.



Aidha uongozi wa Simba jana ulibadilisha gari na kuamua kukodi basi lao wenyewe baada ya viongozi wa matoma Pembe kuwapa basi chakavu .

Licha kudibalisha gari uongozi wa Simba umeamua kuitafutia hoteli maalum kwa ajili ya kupata chakula kizuri cha wachezaji baada hoteli wanayokaa kuwapa chakula kkibovu .

SIMBA WAKIWA KINSHASA


JUMA JABU, BANKA NA WACHEZAJI WENGINE WAKIPASHA KWENYE UWANJA WA SHARK KINSHASA - CONGO
GOLIKIPA JUMA KASEJA AKIWA MAZOEZINI

KOCHA MOSES BASENA AKIWAONGOZA WACHEZAJI KATIKA MAZOEZI

VIONGOZI WA SIMBA WAKIPATA CHAKULA KATIKA HOTEL WALIYPFIKIA HAPA KINSHASA
EMMANUEL OKWI, KELVIN YONDAN NA JUMA NYOSSO WAKIPASHA



WACHEZAJI WA SIMBA WAKIPATA CHAI BAADA YA MAZOEZI YA LEO ASUBUHI

JUMA NYOSSO, SALUM KANONI NA JERRY SANTO WAKIPIGA TIZI

WADAU WA KLABU YA SIMBA WAKIWA KINSHASA

ON THIS DAY: WOZA 10

Hakuna siku ambayo kocha wa England Fabio Capello hataisahau kwenye maisha yake kama siku ya leo.

1) leo ni siku yake ya kuzaliwa ametimiza miaka 64- HAPPY BIRTHDAY CAPELLO
2) Mwaka jana siku kama ya leo alikua anasherehekea miaka 63 ya kuzaliwa kwake lakini pia alikua anakiongoza kikosi cha England kwenye mchezo dhidi ya Algeria kwenye WOZA 2010.
ENGLAND ilishindwa kuifunga ALGERIA na mchezo huo ukamalizika kwa timu hizo kushindwa kufungana.






MAADUI DIMBANI MARAFIKI BATANI

Man United straiker Wayne Rooney akiwa na Joe Hart golikipa wa Man City wakicheza na kufurahi pamoja katika visiwa vya Barbados, kwenye mapumziko.

Kumbe Uadui uwanjani urafiki batani.aaaaaaaaaaaaaaaaaaaah
ROONEY AKIWA AMEBEBWA NA JOE HART

WAKATI WAINGEREZA WAKIENDELEA KULA BATA, DIDIER DROGBA AVUTA JIKO

Didier Drogba amefunga ndoa ya kiasili na mama wa watoto wake wa 3 Lalla Diakite jijini Monaco-Ufaransa.

Drogba na Lalla wamekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka 12, na ndoa yao ilihudhuriwa na wageni zaidi 500 wakiwemo wachezaji wenzie Solomon Kalou, Florent Malouda na Micheal Essien.

Goli la Ulimwengu Ugenini dhidi ya Cameroon

Thomas Ulimwengu alifunga bao ugenini kwenye mchezo dhidi ya Cameroon ambao uliisha kwa Cameroon kushinda mabao 2-1, hata leo goli la ugenini ni muhimu mno..
GOOOO Goooo Tom Ulimwengu pamoja Mbwana Samatta.
Mbwana Samatta pia alifunga goli ugenini kwenye mchezo wake wa mwisho akiwa na kikosi cha timu kubwa ya Taifa dhidi ya Africa ya Kati, Stars pia ilifungwa 2-1
sasa unapata picha gani kwenye mchezo wa hapo baadae?





Timu ya U23 imewasili salama nchini Nigeria

THOMAS ULIMWENGU ATAONGOZA SAFU YA USHAMBULIAJI.

Boniface Wambura, Lagos

Timu ya U23 imewasili salama hapa saa 6.30 mchana kwa ndege ya Kenya Airways
kabla ya kuunganisha ndege ya Concord Airlines kwenda Benin City ambapo mechi
dhidi ya Nigeria itachezwa kesho kuanzia saa 10 kamili saa za hapa ambapo
nyumbani Tanzania itakuwa saa 12 kamili jioni.

Awali U23 ilikuwa ifike hapa saa 4 kamili asubuhi, lakini ikachelewa kutoka
Nairobi ambapo ilitoka saa 3.30 badala ya saa 1.30 baada ya ndege ya Kenya
Airways kuchelewa kuondoka.

Kocha Jamhuri Kihwelo amesema vijana wake katika hali nzuri ya kupeperusha
bendera ya Tanzania katika mechi hiyo ambapo mshindi baada ya matokeo ya
nyumbani ambapo U23 ilipata ushindi wa bao moja ataingia katika hatua ya makundi
kutafuta tiketi ya kuiwakilisha Afrika katika michezo ya Olimpiki itakayofanyika
mwakani jijini London, Uingereza.

Amesema timu yake itacheza mchezo wa kushambulia kwa kushtukiza huku akijaza
viungo wengi kwa lengo la kumiliki mpira kwa muda mrefu, hivyo kuzuia
mashambulizi ya timu pinzani kwa staili.

Kihwelo amesema mbele atatumia washambuliaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata.
Wachezaji wengine aliokuja nao hapa ni Jamal Mnyate, Jackson Wandwi, Hussein
Javu, Mohamed Soud, Obadia Mungusa, Abuu Ubwa, Juma Abdul, Abdul Juma, Himid
Mao, Issa Rashid, Khamis Mcha, Salum Abubakar, Shomari Kapombe, Jabir Aziz,
Godfrey Wambura na Awadh Juma.

NATAKA KUONDOKA - MODRIC


Luka Modric amewashangaza mashabiki wa Tottenham baada ya kukiri anataka kuondoka White Hart Lane.

Modric mwenyewe amevunja kuhusu suala la usajili wake baada kusema nataka kuondoka Spurs.

Akiongea na gazeti la Daily Mail, alisema: "Nataka kuondoka Tottenham nikiwa na uhusiano mzuri na klabu, nilifurahia sana uwepo wangu pale lakini huu ni muda sahihi kwangu kuangalia klabu nyingine."

Nimekuwa na makubaliano na mwenyekiti.Nilipokuwa nasaini mkataba alianiambia, ikitokea klabu itakayonitaka wataifikiria ofa.

Modric ambaye Chelsea juzi walipeleka ofa rasmi kwa Spurs na amekuwa akiuhusishwa pia na kujiunga na United lakini inaonekana Chelsea wana nafasi kubwa zaidi.

"Chelsea ni klabu kubwa na ina mmiliki mwenye ndoto za kufanikiwa.Wana wachezaji wazuri na wenye hamu ya mafanikio kwa kupigana kushinda EPL na Champions League.

"Nataka kubaki London.Nina furaha ndani jiji hili na pia familia yangu wanapapenda hapa."


TOP 20 YA WANAMICHEZO MATAJIRI WA KIMAREKANI MWAKA 2011


Pamoja na kuandamwa na skendo, nafasi yake ya kwanza kuchukuliwa lakini hakuna kinachomzuia mchezaji wa golf maarufu zaidi ulimwenguni Tiger Woods kuendelea kushikilia nafasi ya kwanza kama mwanamichezo wa kimarekani anayeingiza mkwanja mrefu kuliko wote.





1. Tiger Woods $62,294,116 - Golf


2. Phil Mickelson $61,185,933 - Golf


3. LeBron James $44,500,000 - Miami Heat (NBA)


4. Peyton Manning $38,070,000 - Indianapolis Colts (NFL)


5. Alex Rodriguez $36,000,000 - New York Yankees (MLB)


6. Kobe Bryant $34,806,250 - Los Angeles Lakers (NBA)


7. Kevin Garnett $32,832,044 - Boston Celtics (NBA)


8. Matt Ryan $32,700,000 - Atlanta Falcons (NFL)


9. Tom Brady $30,007,280 - New England Patriots (NFL)


10. Dwight Howard $28,647,180 - Orlando Magic (NBA)


11. Dwyane Wade $28,200,000 - Miami Heat (NBA)


12. Sam Bradford $27,250,000 - St. Louis Rams (NFL)


13. Dale Earnhardt Jr. $26,572,930 - Auto racing


14. Darrelle Revis $25,750,000 - New York Jets (NFL)


16. Amar'e Stoudemire $24,486,611 - New York Knicks (NBA)

15. Jim Furyk $25,334,622 - Golf


17. CC Sabathia $23,800,000 - New York Yankees (MLB)


18. Joe Mauer $23,750,000 - Minnesota Twins (MLB)


19. Jeff Gordon $23,703,710 - Auto racing


20. Vernon Wells $23,250,000 - Los Angeles Angels (MLB)



Friday, June 17, 2011

ON THIS DAY: WOZA 2010

SIKU KAMA YA LEO MSHAMBULIAJI YAKUBU ALIKOSA BAO AMBALO NAAMINI HATA WEWE UNGEWEZA KUFUNGA.
ILIKUA NI MECHI KATI YA NIGERIA NA KOREA REPUBLIC.




BOLTON: ARSENAL NA CITY LETENI OFA KWA AJILI YA CAHIL


OWEN COYLE ameziambia Arsenal na Manchester City kupeleka ofa kwa ajili ya Gary Cahil.

The Gunners na City kwa muda mrefu wamekuwa wakipigana vikumbo ili kuweza kupata saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye anacheza katika nafasi ya beki wa kati ndani ya Bolton.

Wanderers kwa muda mrefu wamekuwa wagumu kumuachia beki huyo wa timu ya taifa ya England lakini sasa manager Owen Coyle amewaalika Arsenal Wenger na Roberto Mancini kupeleka ofa rasmi.

Coyle amesema
:
"Naamini anaweza kucheza katika klabu yoyote.Kumekuwa na timu nyingi zilizoonyesha kumtaka zikiwemo timu kubwa ndani ya ligi kuu ya England.

"Inawezakana ili kumpata Cahil inabidi timu ilipe fedha nyingi, hivyo klabu zinazo mtaka zipeleke ofa kwa mwenyekiti.Gary sio mchezaji ambaye ningependa kumpoteza, suala lake linaniumiza kichwa lakini hatuna budi kukubali kumuachia kama zitakuja ofa nzuri zitazohusisha pesa nyingi ambazo tutatumia kujenga upya klabu yetu.
Kiukweli ningependa sana abaki hapa.Ni mchezaji mzuri kwa timu hii na sisemi nataka aondoke, lakini kama akiondoka basi naamini itakuwa ni biashara nzuri kwa klabu."

OFFICIAL: CHELSEA KWENYE MAZUNGUMZO YA KUMSAINI LUKAKU



Anderlecht wamethibitisha kwa mara ya kwanza kwamba wapo kwenye mazungumzo na Chelsea ya kufanya uhamisho wa mshambuliaji Romelu Lukaku kuelekea Stamford Bridge.

Lukaku, 18, amekuwa akihusishwa kujiunga na Chelsea timu ambayo amewahi kukiri kuwa na mapenzi nayo.

Tetesi zilikuwa zinasema kuwa Anderlecht general manager Herman van Holsbeeck alienda London kukutana na kumalizana na Chelsea, na sasa tetesi hizo sasa zimekuwa kweli baada ya timu hiyo ya Ubelgiji kuthibitisha kufanya mazungumzo na Roman Abramovich's team.

Van Holsbeeck aliiambia Sky Sports: "Bado kuna muda kidogo katika kufanya majadiliano.Tupo kwenye mazungumzo na Chelsea lakini pia kuna timu nyingine tumeongea nazo.

OFFICIAL: DEMBA BA AJIUNGA NA NEWCASTLE


DEMBA BA amekamilisha uhamisho wa kujiunga na Newcastle kwa mkataba wa miaka 3.

The Senegal international ambaye amekuwa kwa miezi sita ndani ya klabu ya West Ham anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Newcastle ndani kipindi hiki cha usajili baada ya Yohan Cabaye.

Ba akiwa na Wagonga Nyundo wa London alifanikiwa kufunga mabao 7 ndani ya mechi 12 baada ya kujiunga na West Ham kutoka Hoffenheim katika kipindi cha usajili mwezi January.

Newcastle boss Alan Pardew amesema:
"Demba alifanya mambo makubwa sana akiwa na West Ham msimu uliopita hivyo ni moja kati ya usajili mzuri kwa klabu hii.Ana kasi, ana uwezo mkubwa wa ufundi uwanjani, ni mzuri kwa mipira ya juu na pia ana uwezo wa kufunga mara kwa mara, lakini kikubwa zaidi ya yote ana mapenzi ya kucheza Newcastle."

Ba atapewa jezi 19 msimu ujao.

BARBETOV KUTUMIKA KATIKA DEAL LA KUMSAINI MODRIC


Manchester United wapo tayari kumtoa Dimitar Berbatov kwa Tottenham kama sehemu ya deal la kuwawezesha kuwapiku Chelsea na kumsajili Luka Modric.

The Daily Star linaripoti kuwa Sir Alex Ferguson ni mtu ambaye anamtamani sana Modric na ameweka wazi kuwa kuwa kiungo wa Croatia ni moja ya wachezaji anawataka katika kipindi hiki cha usajili.

Spurs nao ambao juzi walikataa ofa ya paundi millioni 22 kutoka Chelsea kwa ajili ya Modric kupitia kocha wao wamekuwa wakiweka wazi kuwa Luka Modric hauzwi kwa bei yoyote na watafanya kila linalowezekana kumbakisha White Hart Lane.

Lakini kauli ya Spurs haionekani kumsumbua Ferguson ambaye kwa sasa anajipanga kuwapa Tottrnham ofa ya paundi millioni 18 cash + Dimitar Berbatov katika kuhakikisha anamsaini Modric ambaye wengi wanasema ndiye mrithi sahihi wa Paul Scholes.


LAMPARD AMCHUMBIA DEMU WAKE, HUKU ASHLEY COLE, SHAUN WRIGHT PHILIPPS NA ASHLEY YOUNG NA DEMU WAKE WAKILA BATA IN U.S

HAKUNA ANAWAWEZA WAINGEREZA KWA KUTUMIA MISHAHARA YAO MIKUBWA WANAYOIPATA KUTOKA KWENYE TIMU ZAO - ANGALIA WANAVYOTUMIA.

ASHLEY COLE, SHAUN WRIGHT PHILIPPS PAMOJA NA ZAT KNIGHT WAKILA BATA HUKO BEVERLY HILLS-CALIFORNIA

ASHLEY YOUNG BAADA KUSITISHA NDOA NA MPENZI WAKE SASA WAPO VEGAS


FRANK LAMPARD NA CHRISTINE BLEAKLEY WAKIWA UWANJA WA NDEGE WA L.A KURUDI HOME BAADA YA KUCHUMBIANA WIKI HII
MALAVIDAVI MPAKA UWANJANI


NI MUDA WA FABREGAS KUONDOKA ARSENAL


Muda umefika kwa Arsenal Wenger kuwa na maamuzi sahihi kwa kuamua kufanya maamuzi ya kijasiri ya kumuuza Cesc Fabregas.
Naamini kila ambavyo Fabregas anapolilia kurudi Catulunya ndivyo ambavyo uwezo wa kuisadia Arsenal utakavyopungua, kama mchezaji na kiongozi uwanjani.
Ni wazi kabisa kuwa Fabregas anataka kujiunga na timu ambayo imemlea na kumkuza kama mchezaji, hata amejaribu kudhihirisha mapenzi yake kwa Barca kwa kuamua kuchora tattoo ya motto wa Barca 'Mes que un club'.
Fabregas amejaribu kutimiza ndoto yake kuwa kweli katika kipindi cha misimu 3 iliyopita na bado Wenger mara zote amekuwa akisisitiza mchezaji huyo hauzwi.
KWANINI TUWE TUNASIKIA HUU UJINGA KILA UNAPOFIKA WAKATI WA USAJILI

Cesc anazidi kuchanganyikiwa na kukosa umakini katika kuitumikia Arsenal.Wenger alimpa kitambaa cha unaodha Fabregas kuonyesha ni kiasi gani anamuhitaji mchezaji na anapenda aendelee kubaki Emirates na sio kwa sababu Cesc angeweza kuwa kiongozi mzuri.
Ikiwa unajua timu inaongozwa na mchezaji ambaye anapenda kwenda kucheza timu nyingine basi huyo sio kiongozi katika kuwahamasisha wenzie kuipigania timu kwa mapenzi yote.

Fabregas akiwa majeruhi hakujishughulisha hata kidogo kwenda kuiangalia na kuhamasisha wachezaji wa timu anayoiongoza ikicheza mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Fulha, mchezo ambayo kimsingi ilikuwa ni muhimu kwa timu katika kujihakikishia nafasi ya kucheza Champions League, badala yake bwana mkubwa Fabregas aliamua kwenda kuangalia mashindano ya mbio za magari "Spanish Grand Prix".Inaonekana Fabregas hakuwa anajali kama ambavyo nahodha wa Liverpool Steven Gerrard ambaye pamoja na kuwa timu yake alikuwa imeshakosa nafasi ya kucheza Champions League alienda kuangalia timu yake akicheza dhidi ya Aston Villa.
.
Fabregas aliulizwa wiki hii kuhusu sakata la Samir Nasri kama mfaransa huyo anapaswa kubaki au kuondoka Emirates alisema: "Samir ana furaha hapa lakini sijui ni kitu gani bora kwa ajili yake".Hii ina maana Fabregas anakosa uhalali wa kumwambia Nasri asiondoke wakati yeye mwenyewe(Fabregas) nataka kuihama klabu hiyo.
Hivi juzi Bacary Sagna amesema ni bora Fabregas aondoke: "Cesc anahitaji kurudi kwenye nchi yake, nyumbani kwake, kuungana na familia yake.Anahitaji kucheza katika moja ya vilabu bora duniani ambayo ni Barcelona."

Mashabiki wengi wa Arsenal wanatofautiana kuhusu Fabregas ambaye msimu uliopita hakuwa katika kiwango kizuri na hakuwa timamu kiafya.
Naamini mashabiki watakubaliana na kuuzwa kwa Fabregas akiwa Wenger atatumia pesa na kusajili wachezaji bora,ikizingatiwa ni ukweli kwamba Arsenal haijashinda kombe lolote tangu Fabregas aje ukiacha kombe la FA ambalo walichukua miaka 6 iliyopita.

Sir Alex Ferguson alijua muda sahihi wa kumuuza Cristiano Ronaldo, United hawakuwa na furaha kuwa na kikosi bila Ronaldo na Ferguson kama angeweza angemrudisha mvhezaji huyo hata leo lakini Boss huyo wa Man United anajua kuuzwa kwa Cristiano ulikuwa ni uamuzi chanya kwa kuwa mchezaji alishaonyesha nia ya kutaka kuondoka hivyo kuendelea kumn'ganinia kungeshusha hadhi ya timu.
Wenger anahitaji kuchukua falsafa ya Fergie kuwa hakuna mcheza mkubwa kuliko timu kwa kuamua kumuuza Fabregas na kutumia fedha kushindana kusajili wachezaji bora duniani.
Kuendelea kumng'aninia Fabregas sio uimara bali ni udhaifu na inaonyesha kuwa Wenger hajui ni jinsi gani ataenwesha timu bila mhispania huyo.

Naamini Arsenal imewahi kuwa na wachezaji bora kuliko Fabregas, tuikumbe Gunners ya akina Tony Adams na kizazi bora kabisa ambacho kiliweka historia nzuri katika ulimwengu soka duniani, hakikuwa na Cesc lakini kilipata mafanikio makubwa.Hivyo kuondoka kwa Fabregas kunaweza kumaanisha kuzaliwa upya kwa Arsenal ambayo italeta furaha iliyopotea katika sura za mashabiki wa GUNNERS.

Naomba kuwasilisha.


MICHEAL BALLACK'S TRIBUTE



Saa 24 zilizopita ulimwengu wa soka ulishuhudia Micheal Ballack moja kati ya viungo bora wa soka kuwahi kutokea duniani kutangaza kustaafu soka katika ngazi ya kimataifa.
Ballack ambaye currently anaichezea klabu ya Bayern Leverkusen ni moja kati ya wachezaji waliofunga mabao mengi katika timu ya taifa katika historia ya soka la timu ya taifa ya Ujerumani.
Micheal Ballack ambaye alizaliwa mnamo mwaka 1976 alianza kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 1996 akianzia katika timu ya vijana na baadae mnamo mwaka 1999 aliitwa katika timu ya wakubwa.
Mpaka anaastafu Ballack tayari amefanikiwa kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mechi 98 na akifunga magoli 42.
Kitu kimoja kinachomtofautisha Ballack na wachezaji wengine wa kijerumani Micheal amefanikiwa kuvaa jezi namba 13 katika kila timu aliyowahi kuichezea isipokuwa Kaiserslautern.
Ballack alikuwa ni moja kati ya wachezaji bora 125 ambao wapo hai waliotajwa na mfalme wa soka ulimwenguni Pele

Micheal Ballack pia ni moja kati ya wachezaji wachache ambao hawana bahati na mechi za fainali akiwa na timu tofauti.

MIKOSI
Msimu wa 2001/02 na 2007/8 - akiwa na Bayern Leverkusen(2001) walifungwa na Real Madrid katika fainali ya UEFA Champions League, mwaka 2008 akiwa Chelsea walifungwa na Man United in uefa champions league.

Mwaka 2002 akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani walifungwa na Brazil katika fainali ya World Cup.

Mwaka 2008 akiwa na Ujerumani walifungwa na Spain katika fainali EURO.


HIZI NI BAADHI AWARDS ALIZOJISHINDIA BINAFSI

UEFA Club Midfielder of the Year in 2002.
German Footballer of the Year award three times – in 2002, 2003 and 2005.




Thursday, June 16, 2011

MAMBO AMBAYO SIMBA INAPASWA KUZINGATIA UGENINI DHIDI YA DC MOTEMA PEMBE.

Moses Basena-Kocha wa Simba

Kuelekea kwenye mchezo wa marudiano wa michuano ya kombe la shirikisho ambapo wawakilishi pekee waliosalia wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa Simba Sports Club watakuwa wanavaana na timu ya Dc Motema Pembe toka Congo ( Jamhuri ya Kidemokrasia) Blog yako maalum kwa masuala ya michezo imeandaa uchambuzi mfupi wa baadhi ya mambo ambayo Simba wanapaswa kuzingatia ili kuingia kwenye hatua ya makundi ya kombe la shirikisho .
1.Simba wanapaswa kuelewa kuwa huu ni mchezo wa ugenini.
DC Motema Pembe ina wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kucheza soka pengine hata kuliko wachezaji wengi wa Simba na ninaposema wana uwezo pengine kuwazidi wachezaji wa Simba simaanishi kuwa Simba haina wachezaji wenye uwezo ila kwa mchezo uliochezwa Jumapili iliyopita Dc Motema Pembe walicheza kwa mbinu na ufundi wa hali ya juu mno.

Kila mchezaji anatambua jukumu lake na analitekeleza kwa ufanisi wa asilimia mia moja hamsini. Kama Simba wakitambua kuwa wanacheza na timu yenye uwezo mkubwa wanapaswa kufanya kila liwezekanalo kucheza kama inavyopasa kucheza ukiwa ugenini . Ukirejea nyuma kwenye msimu wa mwaka 2007/2008 ambapo Manchester United walitwaa ubingwa wa ulaya walikutana na Inter Milan kwenye hatua ya Robo Fainali.

Kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa kule Milan Sir Alex Fergusson alipanga kikosi ambacho mtazamo wake ulikuwa ulinzi kwanza , kwa jinsi United ilivyokuwa kwenye fomu kipindi kile wangeweza kushinda mchezo ule lakini haikuwa kwenye mipango ya Fergie kujilipua na kushambulia mwanzo mwisho , alichezesha timu ambayo ilikuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa wavu hauguswi na hilo lilitimia.

Hivyo Simba wanapaswa kwenda wakiwa na jukumu la msingi ambalo ni kuhakikisha Juma Kaseja haokoti mpira ukiwa umeingia wavuni bali analindwa kiufundi .Kwa msimu huu pekee Simba imecheza mechi zisizopungua tatu za kimataifa nje ya mipaka ya Tanzania na ningependa kuamini kuwa wachezaji wa Simba wamejifunza kitu kwenye mechi hizo hivyo ni vyema wakacheza kama inavyopaswa kucheza unapokuwa ugenini .

2. Akili ya ziada ya kucheza soka tofauti na lile walilozoea kwa kawaida.
Simba ni klabu ambayo ina falsafa ya kucheza soka la kuvutia , kushambulia kwa uvumilivu huku wakitumia viungo wenye uwezo mkubwa wa kumiliki mpira na kuuchezea kama watakavyo , lakini kwa mchezo wa ugenini hii haitakuwa jambo la busara sana kwani Dc wana uwezo wa kufanya lolote na kitibua sherehe ambayo Simba wako njiani kuiandaa.
Kwenye mchezo wa Jumapili Simba hawana budi kucheza kwa tahadhari ya hali ya juu sana wakitambua fika kuwa wanatafuta aina Fulani ya matokeo . Mara nyingi mbinu kuu ya ulinzi kwenye soka ni mashambulizi lakini Simba sasa haina Mbwana Samatta mmoja wa wachezaji wachache wenye uwezo wa kufunga pale anapotaka kufanya hivyo ,hivyo kutokana na hazina ya bao moja ambayo ipo ni vyema falsafa ya Simba ikabadilika japo kwa dakika tisini tu.
3. kuchezesha viungo watano.
Ukitazama safu ya kiungo ya Simba kwenye mchezo wa kwanza ilionekana kupwaya sana . Mohamed Banka na Nico Nyagawa walionekana kuelemewa mwishoni mwa mchezo.Sababu kuu ya hili ni ama kukosekana kwa Jerry Santo au umri wao mkubwa unaweza kuwa uliwagalimu viungo hawa.
Santo anacheza kama kiungo wa kukaba alikosa mchezo huo kutokana na kuwa na kadi mbili za manjano. Ni vyema kocha akatambua mchango wa Santo kwa Simba na kumpa nafasi yake kwenye kikosi kitakachocheza.
Lakini pia ili kuwanyima mwanya viungo DCMP wakiongozwa na (NDANDA KOSOVO na KANU) ambao walitumia vyema maumbo yao dhidi ya maumbo madogo ya kina Banka na Nyagawa,
Ili simba iweze kuwadhibiti inatakiwa kuwa na viungo watano Amir Maftah acheze kiungo cha kushoto,Shija Mkina kiungo cha kulia,katikati wacheze santo,nyoso na mbele yao acheze Amri Kiemba.
Santo ana umbo kubwa kama la KANU wa Motema Pembe hivyo kama akipewa jukumu la kucheza naye bluzi (kumkaba ng’ado kwa ng’ado yaani ‘zero distance ‘ kama wafanyavyo maharusi wakicheza blues) tatizo kubwa lililoikabili Simba kwenye mchezo wa kwanza litakuwa limesuluhishwa.

4. Kuepuka kutoa mipira na kucheza madhambi karibu na eneo la hatari.
Unaweza ukashangazwa na hili lakini linaweza kuidhuru Simba . Dc motema Pembe wana mtu ambaye anarusha mipira kwa staili ya aina yake .Jamaa anabinuka sarakasi anaporusha na mipira yake inaenda kwa spidi ya hatari kutokana na nguvu za ziada anazozitumia zinazoupa mpira spidi ya ajabu .
Mipira anayorusha huyu jamaa inaenda kama kona vile na kama ikitokea Simba wakawa wanatoa mipira karibu na eneo la hatari wanaweza kujikuta wakiwapa wapinzani faida kwa kuwa mipira inayoweza kusababisha kizaa zaa kwenye lango la Simba,Pia simba wanatakiwa kuwa makini sana na kufanya madhambi karibu na goli lao.
5. Ally Shiboli aanze badala ya Emanuel Okwi.
Hakuna uficho kuwa Emanuel Okwi alikuwa nyota wa mchezo wakati timu hizi mbili zilipokutana wiki iliyopita . Alikuwa akiifanya ngome ya Motema Pembe kama alivyokuwa anataka na kama Simba wangekuwa makini wangeondoka na ushindi mnono zaidi siku ile kutokana na nafasi nyingi alizokuwa anatengeneza okwi.pia Okwi alicheza vizuri dhidi ya TP Mazembe mchezo uliofanyika huko Lubumbashi,
Kwa hakika Motema Pembe lazima watakuwa wamemtazama kwa karibu mganda huyu na kumtengenezea mbinu za kumkabili wakijua kuwa ndiye anayeweza kuwa tishio hiyo Jumapili.
Kama ningekuwa kocha wa Simba ningecheza na akili zao kisaikolojia kama anavyofanya Jose Mourinho au Sir Alex Fergusson. Kwa vyovyote Simba watafanya mkutano na waandishi wa habari kabla ya mchezo hivyo nigeenda na okwi na kumpa nafasi ya kuwa mzungumzaji mkuu na ningemwambia awaeleze waandishi kuwa ataongoza mashambulizi siku ya mchezo . Kwa vyovyote Motema Pembe wataingia na akili ya kumkabili kwa kuwa watatumia muda mwingi kutazama jinsi ya kumkabili lakini siku ya mechi anaanzia benchi na nafasi yake nampa Shiboli ambaye ana kasi na nguvu.
Kwa kifupi Simba wanatakiwa kujua kuwa wanaingia kutupa karata ya mwisho na karata hii ndio yenye uhai wao linapokuja suala la michuano ya kimataifa , michuano ambayo kwa msimu huu ulioisha imewapa Simba faida ya kujipatia fedha nyingi kutokana na mauzo ya Mbwana Samata na Patrick Ochan waliouzwa baada ya kung’aa kwenye mchezo dhidi ya Tp Mazembe . Huwezi jua pengine kuna vilabu vingine vinavyoweza kuwaona kina Kaseja,okwi,Santo ,Amir Maftah na wengine wakiichezea Simba kwenye hatua ya makundi ya kombe la shirikisho , lakini nafasi hii itakuja kutokana na jinsi watakavyocheza siku ya jumapili ,
6.Seleman Matola kuwepo kwenye benchi la ufundi.
Kwenye mchezo wa kwanza moja kati ya matatizo niliyoyaona ni kukosekana mzawa kwenye benchi la ufundi la Simba ambaye anatakiwa kuwa anawasiliana na wachezaji mara kwa mara wakati mchezo ukiendelea.
Kwa mtizamo wangu Seleman Matola ndiye anayefaa kwenye jukumu hilo,akiwa kama nahodha mwenye mafanikio kuliko wote kwenye historia ya Simba,kitu ambacho kinamfanya kuwa na heshima kikosini.
Mungu Ibariki Simba, Mungu Ibariki Tanzania .

KALI YA LEO: GOLIKIPA AKISHANGILIA BAADA YA TIMU YAKE KUPANDA DARAJA SERIE A + MATUSI YA RONALDINHO



Golikipa wa timu ya Novara Jimmy Fontana akishangilia kwa staili ya aina baada ya kushinda mechi ambayo ilisaidia timu yake kupanda daraja na kufanikiwa kucheza ligi kuu ya Italia msimu ujao.

ANGALIA MATUSI YA DINHO

USAJILI WAZIDI KUPAMBA MOTO BARANI ULAYA.




Totenham imeikataa offer ya paundi milioni 25 kutoka chelsea kumsajili kiungo Luca Modric.




Arsenal imeongeza kasi kuwasajili Gary Cahill,Christopher Samba na Gervinho.
Mtendaji mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis amekutana na bosi wa Bolton Phil Gartside kuzungumzia uhamisho wa beki Gry Cahill pia wapo kwenye mazungumzo mazito na Blackburn kuzungumzia uhamisho wa beki Christopher Samba.


Wakti huo huo Arsenal wamekubaliana na mshambuliaji Gervinho na yupo tayari kumwaga wino kuichezea timu hiyo kwa ada ya uhamisho inayokadiliwa kufika euro milioni 12.





Siyabonga Nomvethe amesaini mkataba wa miaka miwil kuendela kuichezea Moroka Swallows

MUDA WA KUHAMIA ENGLAND UMEWADIA: SAMUEL ETO'O


Samuel Eto'o ametoa habari za kuwashtua wapenzi na mashabiki wa Inter Milan baada ya kusema anatamani kujiunga na ligi kuu ya England- Premier Lague.

Ujumbe huu wa Cameroon straiker umekuja masaa 24 baada ya Inter kuthibitisha kuwa kocha wao Leonardo yupo mbioni kujiunga na PSG.
Eto'o ameliambia gazeti la Corriere dello Sport:
"Nafikiria kuhusu kuhusu suala hili, nina mwezi mzima wa kuamua juu ya hili ama niondoke au nibaki.Nina umri wa miaka 30 sasa hivyo inabidi nifikirie vizuri kabla sijasaini mkataba mpya. Niliamua vizuri kucheza Italy na sasa akili yangu inaniambia muda wa kucheza England umewadia."


Kauli ya Eto'o inategemea kuzusha mapigano makubwa miongoni mwa vilabu vya England.

Manchester City, Chelsea and Arsenal wanaonekana ndio watakaokuwa wa kwanza kuanza mbio za kumuwania mcameroon huyo.
Hata hivyo Eto'o aliwahoi kukaririwa akisema angependa kufanya kazi na Gunner's coach Asenal Wenger.

WACHEZAJI WALIOACHWA NA VILABU VYAO KWENYE PREMIER LEAGUE



Arsenal
Thomas Cruise, Roarie Deacon, Mark Randall

Aston Villa
Durrell Berry, John Carew, Ellis Deeney, Calum Flanagan, Harry Forrester, Arsenio Halfhuid, Isaiah Osbourne, Robert Pires, Nigel Reo-Coker, Moustapha Salifou

Birmingham City
Marcus Bent, Lee Bowyer, Sebastian Larsson, James McFadden, Mitchell McPike, James O'Shea, Stuart Parnaby, Kevin Phillips, Daniel Preston, Luke Rowe, Robin Shroot, Maik Taylor

Blackburn Rovers
Jordan Bowen, Jason Brown, Zurab Khizanishvili, Benjani Mwaruwari, Michael Potts, Maceo Rigters

Blackpool
David Carney, Daniel Coid, Ishmel Demontagnac, Rob Edwards, Jason Euell, Marlon Harewood, Richard Kingson, Malaury Martin, Paul Rachubka, Andy Reid, Salaheddine Sbai

Bolton Wanderers
Tamir Cohen, Johan Elmander, Ricardo Gardner, Joey O'Brien, Jlloyd Samuel, Samuel Sheridan

Chelsea
Samuel Hutchinson, Carl Magnay, Danny Philliskirk, Jan Sebek, Michael Woods

Everton
Kieran Agard, Hope Akpan, Nathan Craig, Gerard Kinsella, Lee McArdle, Iain Turner

Fulham
Zoltan Gera, Edward Johnson, Diomansy Kamara, John Pantsil, Matthew Saunders

Liverpool
Jason Banton, Deale Chamberlain, Douglas Cooper, Sean Highdale Steven Irwin, Nikola Saric

Manchester City
Javier Garrido, Scott Kay, James Poole, Shaleum Logan, Andrew Tutte, Javan Vidal, Patrick Vieira, James Wood

Manchester United
Conor Devlin, Owen Hargreaves, Gary Neville, Paul Scholes, Edwin van der Sar

Newcastle United
Sol Campbell, Shefki Kuqi, Patrick McLaughlin

Stoke City
Abdoulaye Faye, Eidur Gudjohnsen, Ibrahima Sonko

Sunderland
Michael Kay, Nathan Luscombe, Daniel Madden, Robert Weir, Nathan Wilson, Mvoto Jean-Yves, Bolo Zenden

Tottenham Hotspur
Jonathan Woodgate

West Bromwich Albion
Giles Barnes, Marcus Haber, Dean Kiely, Abdoulaye MƩƮtƩ

West Ham United
Anthony Edgar, Holmar Eyjolfsson, Daniel Gabbidon, Lars Jacobsen, Filip Modelski, Jonathan Spector, Adam Street, Matthew Upson

Wigan Athletic
Steven Caldwell, Daniel De Ridder, Joseph Holt, Jason Koumas, Thomas Lambert, Thomas Oakes, Francis Pollitt, Abian Serrano Davila

Wolverhampton Wanderers
Adriano Basso, Jody Craddock, John Dunleavy, Marcus Hahnemann, David Jones, Nathan Rooney

ON THIS DAY:

SIKU KAMA YA LEO MWAKA JANA KWENYE WOZA 2010,HISPANIA ILIFUNGWA BAO 1-0 NA SWITZERLAND KWENYE UWANJA WA MOSES MABHIDA JIJINI DURBAN.NA NDIO ILIKUA MARA YA MWISHO TIMU YA TAIFA YA HISPANIA KUFUNGWA KWENYE MCHEZO WA MASHINDANO.

NYAMLANI ATEULIWA KUWA MJUMBE WA CAF



Makamu wa Kwanza wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Rufani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa CAF, Hicham El Amrani iliyotumwa kwa Nyamlani jana, kikao kinachofuata cha Kamati hiyo kitafanyika Septemba 25 mwaka huu makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri. Nyamlani ambaye kitaaluma ni mwanasheria anakuwa Mtanzania wa kwanza kuingia katika kamati hiyo. Pia ni kiongozi wa mpira wa miguu kwa muda mrefu akianzia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Temeke (TEFA), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kilichokuwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) sasa TFF.

OFFFICIAL: JEZI MPYA YA LIVERPOOL (AWAY)


UNITED YATHIBITISHA KUONDOKA KWA MKOPO


Manchester United wamethibitisha kuwa winga wao Bebe anakwenda kucheza kwa mkopo katika klabu ya Basiktas ya Uturuki msimu mzima wa 2011/2012
Bebe alisajiliwa na Sir Alex Ferguson kutoka Vitoria kwa ada ya paundi millioni 7.4 msimu uliopita ingawa na mchezaji huyo hakuwahi kuichezea timu hiyo ya Ureno mechi yoyote.

UDINESE YAMWACHIA UAMUZI WA MWISHO SANCHEZ



Udinese wamethibitisha kuwa klabu tano za Juventus, Inter, Man City, Man United, na Barcelona wametoa ofa ambazo wanakubaliana nazo na sasa uamuzi kumuuza timu gani kati hizo wamemuachia Alexis Sanchez mwenyewe.

Mabingwa Europa Barcelona jana usiku kupitia makamu wa raisi alithibitisha kufanya mazungumzo na Udinese lakini kutokana kuwa na fungu dogo la usajili nafasi ya Sanchez kwenda Nou Camp itategemea na mchezaji mwenyewe.

City ambao wamekuwa wakiongoza mbio za kuwania saini ya mchile huyo kwa kipindi kirefu pamoja na kutoa ofa nzuri sana kwa Udinese lakini Sanchez mwenyewe haonekani kuwa na matamanio ya kujiunga nayo.

United ambao nao juzi walimtuma mkurugenzi mtendaji wao David Gill hadi Spain kwenda kumalizana na raisi wa klabu ya Udinese anayeishi Spain wanaonekana kuwa moja ya timu zinazopewa nafasi kubwa ya kumnyakua winga huyo, huku kocha Sir Alex Ferguson akionekana hayupo kufanya kosa alilolifanya kwa Ronaldinho kwa kumuacha Alexis Sanchez mchezaji ambayeamekuwa akimtamani kwa zaidi ya miaka 3 aende kwa mahasimu wa ulaya Barcelona.

Inter na Juve nao wamejitutumua kwa kutoa ofa zinazoeleweka lakini mchezaji mwenyewe anasema kama akihama Udinese angependa kwenda kucheza nje ya nchi ya Italy


Udinese's transfer consultant Stefano Antonelli, ambaye ndio anayedili na madili makubwa amethibitisha kuwa kwa sasa wanaaangalia chaguo bora la kumuuza Sanchez huku akisema Alexis mwenyewe atahusishwa na kuchagua wapi pa kwenda.

BLOG HII INAITAKIA SIMBA SAFARI NJEMA!

Kikosi cha Simba Kilichoondoka asubuhi ya leo kwenda jijini Kinshasa kwenye mchezo wa marejeano dhidi ya DC Motema Pembe hapo siku ya Jumamosi.


Magolikipa:
Juma Kaseja,Ally Mustafa
Mabeki:
Salum Kanoni,Juma Jabu,Amir Maftaha,Kelvin Yondani,Juma Nyoso na Meshack Abel
Viungo
Nico Nyagawa ( Nahodha ),Mohamed Banka,Amri Kiemba,Jerry Santo,Abdulhalim Humud
Washambuliaji
Mussa Hassan Mgosi,Emanuel Okwi,Ally Ahmad Shiboli,Kelvin Charles na Shija Mkina.

HATUMUUZI NEYMAR - SANTOS WAIAMBIA CHELSEA


CHELSEA wameambiwa kuwa wanapoteza muda wao kwa kujaribu kumsajili Brazilian wonder kid Neymar.
Onyo hilo limetolewa na na raisi ywa klabu ya Santos Luis Avaro de Oliveira.
The Blues walimtuma na kumpa madaraka wakala maarufu wa wachezaji Pini Zahavi kwenda Brazil kufungua majadiliano ya kumsaini Neymar Chelsea, lakini Santos kupitia raisi wake wameweka wazi kuwa kinda wa hauzwi ingawa Chelsea wanaamini hiyo janja tu Santos kutaka kupandisha bei ya Neymar.
De Oliveira amesisitiza kuwa,:
" Kwa sasa tupo katika maongezi na wadhamini wetu wakubwa waweze kutufanikishia mpango wa kuhakikisha Neymay anaendelea kuwa mchezaji wetu kwa kumpa dili nzuri ya kueleweka.Kumekuwa hakuna ofa mpya iliyokuja ndani ya siku kadhaa zilizopita lakini zikija bado tutazikataa."
Neymar mwenyewe amezungumza na kusema kuwa "Ndoto ya wabrazili wengi ni kucheza ulaya na kwangu haipo tofauti."

Wednesday, June 15, 2011

EDMUNDO KWENDA JELA KWA KESI YA MAUAJI



Jaji wa mahakama ya jiji ya Rio De Jeneiro Eduardo Carvalho de Figueirdo ametoa amri ya kukamatwa kwa straiker wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil Edmundo kwa kusababisha ajali ya gari ambayo ilichukua maisha ya watu 3 mwaka 1995.
Edmundo ambaye aliwakutwa na hatia ya kufanya mauji bila kukusudia mwaka 1999., lakini akakata rufaa na akashindwa lakini hatua za kisheria dhidi yake hazikuchuliwa mpaka jana Jumanne Jaji Eduardo alipotoa amri ya kukamatwa kwake.
Mawakili wa Edmundo wamesema watakata rufaa tena.Kwa sasa bado Edmundo hajakamatwa.
Edmundo kwa sasa ana umri wa miaka 40 aliwahi kuzichezea klabu 13 tofauti akianzia Vasco Da Gama, Flamengo, Palmeiras, Corinthians, Napoli, Cruzeiro, Fluminense, Fiorentina, Santos, Tokyo Verdy, Urawa Red Diamonds, Nova IguaƧu, na Figueirense.
Katika kipindi cha hivi karibuni Edmundo amekuwa ni commentator wa television nchini Brazil.


JIKUMBUSHE KIDOGO UWEZO WA EDMUNDO THE ANIMAL