Search This Blog

Thursday, June 16, 2011

UDINESE YAMWACHIA UAMUZI WA MWISHO SANCHEZ



Udinese wamethibitisha kuwa klabu tano za Juventus, Inter, Man City, Man United, na Barcelona wametoa ofa ambazo wanakubaliana nazo na sasa uamuzi kumuuza timu gani kati hizo wamemuachia Alexis Sanchez mwenyewe.

Mabingwa Europa Barcelona jana usiku kupitia makamu wa raisi alithibitisha kufanya mazungumzo na Udinese lakini kutokana kuwa na fungu dogo la usajili nafasi ya Sanchez kwenda Nou Camp itategemea na mchezaji mwenyewe.

City ambao wamekuwa wakiongoza mbio za kuwania saini ya mchile huyo kwa kipindi kirefu pamoja na kutoa ofa nzuri sana kwa Udinese lakini Sanchez mwenyewe haonekani kuwa na matamanio ya kujiunga nayo.

United ambao nao juzi walimtuma mkurugenzi mtendaji wao David Gill hadi Spain kwenda kumalizana na raisi wa klabu ya Udinese anayeishi Spain wanaonekana kuwa moja ya timu zinazopewa nafasi kubwa ya kumnyakua winga huyo, huku kocha Sir Alex Ferguson akionekana hayupo kufanya kosa alilolifanya kwa Ronaldinho kwa kumuacha Alexis Sanchez mchezaji ambayeamekuwa akimtamani kwa zaidi ya miaka 3 aende kwa mahasimu wa ulaya Barcelona.

Inter na Juve nao wamejitutumua kwa kutoa ofa zinazoeleweka lakini mchezaji mwenyewe anasema kama akihama Udinese angependa kwenda kucheza nje ya nchi ya Italy


Udinese's transfer consultant Stefano Antonelli, ambaye ndio anayedili na madili makubwa amethibitisha kuwa kwa sasa wanaaangalia chaguo bora la kumuuza Sanchez huku akisema Alexis mwenyewe atahusishwa na kuchagua wapi pa kwenda.

No comments:

Post a Comment