Search This Blog

Thursday, June 16, 2011

NYAMLANI ATEULIWA KUWA MJUMBE WA CAF



Makamu wa Kwanza wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani ameteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Rufani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa CAF, Hicham El Amrani iliyotumwa kwa Nyamlani jana, kikao kinachofuata cha Kamati hiyo kitafanyika Septemba 25 mwaka huu makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri. Nyamlani ambaye kitaaluma ni mwanasheria anakuwa Mtanzania wa kwanza kuingia katika kamati hiyo. Pia ni kiongozi wa mpira wa miguu kwa muda mrefu akianzia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Temeke (TEFA), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kilichokuwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) sasa TFF.

No comments:

Post a Comment