Search This Blog

Friday, June 17, 2011

BARBETOV KUTUMIKA KATIKA DEAL LA KUMSAINI MODRIC


Manchester United wapo tayari kumtoa Dimitar Berbatov kwa Tottenham kama sehemu ya deal la kuwawezesha kuwapiku Chelsea na kumsajili Luka Modric.

The Daily Star linaripoti kuwa Sir Alex Ferguson ni mtu ambaye anamtamani sana Modric na ameweka wazi kuwa kuwa kiungo wa Croatia ni moja ya wachezaji anawataka katika kipindi hiki cha usajili.

Spurs nao ambao juzi walikataa ofa ya paundi millioni 22 kutoka Chelsea kwa ajili ya Modric kupitia kocha wao wamekuwa wakiweka wazi kuwa Luka Modric hauzwi kwa bei yoyote na watafanya kila linalowezekana kumbakisha White Hart Lane.

Lakini kauli ya Spurs haionekani kumsumbua Ferguson ambaye kwa sasa anajipanga kuwapa Tottrnham ofa ya paundi millioni 18 cash + Dimitar Berbatov katika kuhakikisha anamsaini Modric ambaye wengi wanasema ndiye mrithi sahihi wa Paul Scholes.


No comments:

Post a Comment