Search This Blog

Friday, June 17, 2011

MICHEAL BALLACK'S TRIBUTE



Saa 24 zilizopita ulimwengu wa soka ulishuhudia Micheal Ballack moja kati ya viungo bora wa soka kuwahi kutokea duniani kutangaza kustaafu soka katika ngazi ya kimataifa.
Ballack ambaye currently anaichezea klabu ya Bayern Leverkusen ni moja kati ya wachezaji waliofunga mabao mengi katika timu ya taifa katika historia ya soka la timu ya taifa ya Ujerumani.
Micheal Ballack ambaye alizaliwa mnamo mwaka 1976 alianza kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 1996 akianzia katika timu ya vijana na baadae mnamo mwaka 1999 aliitwa katika timu ya wakubwa.
Mpaka anaastafu Ballack tayari amefanikiwa kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani mechi 98 na akifunga magoli 42.
Kitu kimoja kinachomtofautisha Ballack na wachezaji wengine wa kijerumani Micheal amefanikiwa kuvaa jezi namba 13 katika kila timu aliyowahi kuichezea isipokuwa Kaiserslautern.
Ballack alikuwa ni moja kati ya wachezaji bora 125 ambao wapo hai waliotajwa na mfalme wa soka ulimwenguni Pele

Micheal Ballack pia ni moja kati ya wachezaji wachache ambao hawana bahati na mechi za fainali akiwa na timu tofauti.

MIKOSI
Msimu wa 2001/02 na 2007/8 - akiwa na Bayern Leverkusen(2001) walifungwa na Real Madrid katika fainali ya UEFA Champions League, mwaka 2008 akiwa Chelsea walifungwa na Man United in uefa champions league.

Mwaka 2002 akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani walifungwa na Brazil katika fainali ya World Cup.

Mwaka 2008 akiwa na Ujerumani walifungwa na Spain katika fainali EURO.


HIZI NI BAADHI AWARDS ALIZOJISHINDIA BINAFSI

UEFA Club Midfielder of the Year in 2002.
German Footballer of the Year award three times – in 2002, 2003 and 2005.




No comments:

Post a Comment