Search This Blog

Friday, June 17, 2011

BOLTON: ARSENAL NA CITY LETENI OFA KWA AJILI YA CAHIL


OWEN COYLE ameziambia Arsenal na Manchester City kupeleka ofa kwa ajili ya Gary Cahil.

The Gunners na City kwa muda mrefu wamekuwa wakipigana vikumbo ili kuweza kupata saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye anacheza katika nafasi ya beki wa kati ndani ya Bolton.

Wanderers kwa muda mrefu wamekuwa wagumu kumuachia beki huyo wa timu ya taifa ya England lakini sasa manager Owen Coyle amewaalika Arsenal Wenger na Roberto Mancini kupeleka ofa rasmi.

Coyle amesema
:
"Naamini anaweza kucheza katika klabu yoyote.Kumekuwa na timu nyingi zilizoonyesha kumtaka zikiwemo timu kubwa ndani ya ligi kuu ya England.

"Inawezakana ili kumpata Cahil inabidi timu ilipe fedha nyingi, hivyo klabu zinazo mtaka zipeleke ofa kwa mwenyekiti.Gary sio mchezaji ambaye ningependa kumpoteza, suala lake linaniumiza kichwa lakini hatuna budi kukubali kumuachia kama zitakuja ofa nzuri zitazohusisha pesa nyingi ambazo tutatumia kujenga upya klabu yetu.
Kiukweli ningependa sana abaki hapa.Ni mchezaji mzuri kwa timu hii na sisemi nataka aondoke, lakini kama akiondoka basi naamini itakuwa ni biashara nzuri kwa klabu."

No comments:

Post a Comment