Search This Blog

Tuesday, October 29, 2013

TEGETE NI MFUNGAJI MZURI BADO ILA AMEKOSA UMAKINI TU


Na Baraka Mbolembole
" Ni kweli sisi wachezaji tunajua kuwa mashabiki wanazipenda timu zao, hasa kwa wale wa timu yetu ya Yanga tunajua wanaipenda sana timu yao, lakini nawashauri wabadilike sasa, wasiwazomee wachezaji wakati wanapokuwa wanafanya vibaya. Wawe na subira kama kweli wanaipenda timu yao. Kelee zao huwatoa mchezoni wachezaji na kujikuta wakifanya vibaya zaidi, na hili hupelekea hata kwa wale wachezaji wanaokuja kuingia katika uoga, nawasihi wawe na uvumilivu"
Ni maneno ya mshambuliaji aliye katika wakati mgumu hivi sasa katika klabu ya Yanga, Jerry Tegete, wakati nilipofanya nae mazungumzo hivi karibuni kuhusiana na mwenendo wake usiovutia hadi sasa katika klabu hiyo.

Jerry ambaye alianza vizuri msimu huu pale alipofunga maba mbili siku ya ufunguzi wa msimu dhidi ya Ashanti United, na akafunga tena katika mchezo uliofuata hila amekuwa akipoteza nafasi za wazi mara kwa mara na kupelekea ,kuwakera wengi.
Wakati ushindani wa kuwania nafasi ukiwa ni mkubwa katika safu ya mashambulizi ya Yanga, ambayo imekusanya washambuliaji sita wa kati na wengine wawili wakiwa kama viungo washambuliaji, Jerry amejikuta akipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza, na katika siku za karibuni amekuwa akikosa hata nafasi ya kuingia kama mchezaji wa akiba.

Didier Kavumbagu, ameoneka kuwa chaguo la kwanza mbele ya kocha, Ernie Brandts, na Mrundi huyo ameweza kuwa kiongozi wa safu yote ya mashambulizi, nguvu, akili na uwezo wa kumiliki mpira, unaambatana na umakini mkubwa wa kutumia nafasi anazotengenezewa, ' Kavu' amekuwa chaguo bora mbele ya Tegete katika vitu vingi, mwanzoni mwa msimu walipangwa walikuwa wakipangwa pamoja na wakaonekana kuwa wafungaji wazuri, walifunga kwa vichwa, na uwezo binafsi na matokeo yake wakawa chaguo la kwanza.
" Ushindani ni mkubwa sana, na nafasi imekuwa ni ngumu, kila mchezaji hutumia nafasi anayopata vizuri" anaongeza, Tegete. 'Kavu', Tegete, Said Bahanunzi, Hussein Javu, Kondo awali walikuwa washindani wa kwanza katika nafasi hii, ila kurejea kwa Hamis Kizza aliyekuwa kwenye majaribio nchi ya ng'ambo, na kumalizika kwa adhabu ya Mrisho Ngassa kumefanya hali ya mambo kuwa magumu zaidi.
Lakini inakuwaje kwa mchezaji kama Jerry kuzomewa mara kwa mara na mashabiki wa timu yake? Wakati fulani hali hii iliwahi kumtokea kiungo wa zamani wa timu hiyo, Nurdin Bakari, hasa pale alipokuwa akifanya vibaya uwanjani, kila mtu alikuwa anafahamu uwezo wake, lakini pasi mbili au tatu tu ' mbovu' uwanjani zilikuwa ni tatizo. Kitu kizuri huleta furaha ya siku zote katika maisha, ni shida sana kukishusha chini kitu kizuri, mafanikio hayahitaji kubweteka na kupelekea mtu kujisahau kule alipotoka na alipokuwa amepanga kufikia, umakini, nidhamu ya mchezo, huwa ni sehemu ya mipango mizuri ya wachezaji wote waliofanikiwa. Wapo ambao walipitia njia ya kupingwa na kuzomewa na mashabiki wa timu zao ila bado wakafanya kazi nzuri uwanjani na kujikuta wakifanikiwa.

Dr. Martin Luther King Jr aliwahi kusema; " Ukimya wa rafiki yako unaumiza sana kuliko kelele za adui yako" pengine, manaharakati huyu wa haki za binadamu, na aliyekuwa mtetezi wa watu weusi katika Marekani, alikuwa na maana nyingi lakini ni vyema wakati mwinmgine wachezaji kama Tegete wakachukulia kelele za zomea zomea za mashabiki wao ni sehemu za kuwakumbusha kuwa hawafanyi vizuri. Na mashabiki hawatakiwi kufanya hivyo mara kwa mara klwa kuwa mara moja au mbili inatosha kufikisha ujumbe kwa muhusika.

Katika miaka mitatu ya karibuni, Tegete amekuwa akikumbwa na majeraha ya mara kwa mara, na hajawahi kucheza michezo sita mfululizo ndani ya misimu mitatu sasa klabuni kwake.
" Namshukuru Mungu kwa kila jambo, nashukuru hivi sasa nimepona goti, hilo ndilo lilikuwa ni la muhimu sana kwangu. Unajua hata sisi wachezaji hatupendi kufanya vibaya, wakati wa mchezo na Simba niliumia na kusikitika sana kwa sababu hadi nusu ya kwanza tunaongoza 3-0, kipindi cha pili wakarudisha goli zote.

Niliumia sana goli kurudi na nilikuwa nina imani tungeweza kuongeza bao lingine muda wowote. Simba walijitahidi sana" . Hili ni kweli kuwa hakuna mchezaji anayependa kufanya vibaya na wakati mweingine matokeo yao mabaya uwanjani hutokana na uwezo mzuri wa timu nyingine. Ila mimi binafsi nahitaji mabao kutoa kwa Tegete, nimechoka kumuona akipoteza nafasi rahisi mara kwa mara mchezoni, ila ujumbe wangu kwa mashabiki wa Yanga ni kwamba, ' Muacheni, Jerry acheze mpira sasa, baaada ya kucheza walau michezo mitao hadi saba mfululizxo mnaweza kumuhukumu' . Tegete ni mfungaji mahiri bado, amekosa umakini tu kama aliona nao Kizza au Kavumbagu.
0714 08 43 08

1 comment:

  1. Hili limebaki galasa mjomba!! usilirembe. Sasa na umri huo na kiwango hicho hata haliuziki pia !!!!

    ReplyDelete