Search This Blog

Thursday, February 14, 2013

TAIFA STARS WANUNULIWA BASI LA MILLIONI 200 NA KILIMANJARO

Hatimaye basi la Timu ya Taifa, Taifa Stars lililokuwa likisubiriwa kwa hamu sasa limewasili na liko tayari kukabidhiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager kwa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) ili Taifa Stars iweze kulitumia.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, inayodhamini Taifa Stars, George Kavishe alisema hii ni katika malengo yao ya kuinua hadhi ya timu ya Taifa ambayo kwa sasa imeonesha kiwango cha hali ya juu.

“Wakati tukichukua udhamini wa timu ya Taifa moja ya malengo yetu ilikuwa ni kuinua hadhi ya timu hii na mojawapo ya vitu tulivyoahidi ni kuinunulia basi la hadhi,” alisema Bw Kavishe.

Alisema basi hilo aina ya Yutong lenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 200, ni kubwa na la kisasa kabisa lenye uwezo wa kubeba abiria 50 pamoja na dereva na kuwa lina nafasi kubwa kutoka kiti kimoja hadi kingine hivi kuwafanya wachezaji wakae kwa raha zaidi wanaposafiri.

“Basi hili ni athletic coach na ni jipya kabisa, limetengenezwa mahususi kwa wanamichezo kwani lina nafasi kubwa chini ya kubeba vifaa vya michezo na mizigo mingine yeye uzito wa hadi tani tatu,” alisema Bw. Kavishe.

Aliendelea kusema kuwa basi hilo ni imara kwani chasis yake ni 4x2, injini yake ni aina ya  300 HP Cummins, ina retarder ya umeme na breki aina ya ABS, TV mbili za kisasa, muziki wa nguvu wenye spika nane, milango na mabuti ya kisasa, friji mbili na kiyoyozi cha nguvu.

Kwa mujibu wa Bw. Kavishe basi hili linatarajiwa kukabidhiwa kwa Taifa Stars Februari 21 katika hafla itakayofanyika katika makao makuu ya TBL Ilala Jijini Dar es Salaam na itahudhuriwa na wadau mbalimbali wa soka nchini na wageni wengine.

Baada ya kukabidhiwa kwa Taifa Stars basi hilo linatarajiwa kuzunguka katika mitaa mbalimbali ya JIji la Dar es Salaam ili wananchi walione na wapige nalo picha za kumbukumbu.

“Hii ni zawadi ya watanzania kwa timu ya Taifa kwani ndio wanatuwezesha kufanya mambo yote haya…kadri wanavyozidi kutuunga mkono kwa kunywa bia yetu ya Kilimanjaro Premium Lager ndivyo na sisi tunapata fedha za kuidhamini timu yetu ya Taifa,” alisema.

Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ilianza kuidhamini Timu ya Taifa tangu  mwezi Mei mwaka jana kwa kuwekeza zaidi ya bilioni mbili kwa mwaka kwenye timu hii kwa muda wa miaka mitano.

Moja ya masuala ambayo yamo kwenye mkataba kati ya TBL na TFF ni ununuzi wa basi mpya ya Taifa Stars jambo ambalo TBL imefanikisha ndani ya mwaka mmoja wa udhamini wake.

Mpaka sasa TFF imeonyesha kuridhishwa na udhamini mnono wa Kilimanjaro Premium Lager kwani shirikisho hilo lina uwezo wa kufanya mipango ya muda mrefu zaidi kwa uhakika.

Udhamini wa Kilimanajro Premium Lager ndio mkubwa kabisa ambao TFF imewahi kupokea kutoka kwa kampuni au shirika lolote nchini kudhamini mpira.

2 comments:

  1. TFF wanapata hela na udhamini mzuri lakini watendaji hawapo kiuzalendo zaidi bali wanajali maslahi yao, mfano mzuri ni katika sakata zima la uchaguzi unakuja unatuonyesha i jinsi gani wapo kibnafsi zaidi na maslahi yao. Naomba watanzania tuamke KUKEMEA vitendo visivyoendana na mfumo mzima wa maendeleo ya soka nchini. HONGERA SANA TBL. Mimi pia ni ndau mzuri wa bia yenu ya KILIMANJARO

    ReplyDelete
  2. KWANI SERIKALI AU TFF ILISHINDWA KUWANUNULIA TIMU YA TAIFA USAFIRI KAMA HUO?

    ReplyDelete