Search This Blog

Wednesday, March 27, 2013

EXCLUSIVE: HAYA NDIO MAZINGIRA YA UWANJA WA LAKE TANGANYIKA KIGOMA - FREMU ZA MADUKA

Wakati kwenye viwanja vingine vyote duniani fremu za nje zinazonguka uwanja zimekuwa zikitumika kama vitega uchumi kwa wamiliki wa uwanja husika, hali ni tofauti mkoani Kigoma kwenye dimba la Lake Tanganyika. Uwanja huo mkongwe ambao unaingiza mashabiki takribani 20,000, upo kwenye hali mbaya kuanzia ndani mpaka nje.
 Sasa hivi fremu zilizozunguka uwanja huo zimegeuka makazi ya watu, haijaweza kufahamika kama wamekodi au wanaishi tu bure. Hata kama wanalipa lakini fremu hizo hazikuwa za matumizi ya watu kuishi kwenye eneo hilo.

Matokeo yake uwanja huo mkubwa wa mkoa umezidi kuwa kwenye mazingira mabovu, na inawezekana ukosefu wa mapato ya milangoni kutokana na kutokuwepo kwa mashindano ya maana ya kuvuta washabiki kuingia uwanjani hivyo kuzidi kusababisha ukosefu wa fedha za kuweza kuboresha mazingira ya uwanja huo.


8 comments:

  1. Asante mdau kwa kutuletea vituko hivyo! Jambo la kujiuliza je kuna viongozi wa michezo kweli ngazi ya mkoa?kama wapo ndio kusema hawalioni hilo? Au wanaona sawa tu bora watoto hawakosi kwenda maliwato.Mapinduzi ya michezo yanahitaji watu wenye miono ya mbali.kuweni makini mnapofanya chaguzi !!!!

    ReplyDelete
  2. jitihada zifanyike ccm irudishe viwanja serikalini sababu wakati wa ujenzi wa viwanja hvyo nchi ilikua na chama kimoja

    ReplyDelete
  3. Mimi sijui uwanja huu unamilikiwa na Serikali Chama au Mtu Binafsi, Insikitisha kuona Mkoa Kama wa Kigoma wenye heshima ya kutoa wachezaji Bora hapa nchini unakua katika mazingira ya hovyo kiasi hiki, lawama ziende wapi chama serikali au chama cha mpira. Ttanzania ni nchi ndogo sana lakini tumeona Brazil Ivory cost an nchi zingine zikija kucheza Taifa kwa nini??. kwa sababu Tanzania tuna uwanja wenye kiwango. Sasa hata kama Kigoma hatuna timu ligi kuu lakini kama kuna uwanja wenye ubora ni rahisi kualika timu kubwa kama samba yanga azam na zingine na zikakubali kuja Kigoma kama brazil walivyokubali kuja Bongo. Viongozi wa Mkoa serikali chama tawala na Chama cha mpira achenu blah blah na Fitna anagalieni hilo.

    Junior Mwamba

    ReplyDelete
  4. sasa fika pale kigoma kwenye chama cha soka jaribu kuwauliza kuhusu michakato mbalimbali ya TFF, watu watazungumza mpaka povu mdomoni jinsi mambo yanavyoendeshwa ndivyo sivyo, hlf tutegemee mjumbe kutoka huko nae anakuja dar kutuchagulia viongozi wa TFF!!.

    ReplyDelete
  5. Ndio maana tunataka mabadiliko katika uongozi wa mpira kuanzia Taifa yaani TFF hadi mikoani hii ni Aibu ya karne.Wao kazi ya kusingizia FIFA na serikali kuingilia ulaji wao.Makato kibao hela haijulikani inakopelekwa huku kocha na timu ya Taifa wanashindwa hata kuwalipa posho.DAWA YAO NI KUWAPIGA CHINI TU WOTE

    ReplyDelete
  6. Hv lake tanganyika unachukua wa2 20000 au 60000

    ReplyDelete
  7. KIGOOMA LEKA WATIGITE!!!!!!!!

    ReplyDelete