Search This Blog

Saturday, September 10, 2011

JULIO AITA JESHI LA WACHEZAJI 24 WA KWENDA BRAZIL


KOCHA msaidizi wa timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Jamhuri Kihwelo, ameita wachezaji 24 ambao wataingia kambini jumapili kujiandaa na
mashindano ya Copa cocacola yatakayo fanyika nchini Brazil hapo baadae.

Julio kabla ya kuwataja wachezaji hao 24 alisema safari ya kwenda Brazil ipo lakini itakuja kuthibitishwa na Cocacola ambao ni wadhamini wa safari hiyo ya mafunzo na mashindano nchini Brazil. Msafara huo utakuwa na watu 18 huku wachezaji wakiwa 16 na viongozi wawili.

Kikosi hicho kinatarajiwa kuanza mazoezi Jumatatu na hapo baadae watachujwa na kubakia 16 watakao safiri. Wachezaji hao ni pamoja na Paulo John (Morogoro), Hamad Hamad (kinondoni), Mohamed H. Mohamed (kinondoni), Peter Manyika (Temeke), Ismail Gambo (Kigoma), Miraji Adam (Morogoro).

Wengine ni Basil
Seif (Morogoro), Huseni Twaha (Tanga), James Ambros (Morogoro), Aishi Salum (Morogoro), Hashim Mwalo (kigoma), Mohamed Salum (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Dar es salaam), Mbwana Hasani (kinondoni), Salvatory Rafael (kigoma), Paulo James (Shinyanga), Huseni Ibrahim (Morogoro), Gabson Nyamtema (kigoma), Mohamed kapeta (temeke), Joseph Kimwaga (kinondoni).

No comments:

Post a Comment