Search This Blog

Saturday, September 10, 2011

YANGA WATOKA SULUHU NA RUVU SHOOTING

MABINGWA WATETEZI WA VODACOM PREMIER LEAGUE DAR YOUNG AFRICANS WAMEENDELEA KUJIWEKA KWENYE HALI MBAYA KATIKA HALI NGUMU YA KUTETEA UBINGWA WAO BAADA YA KUTOKA SARE YA BAO MOJA KWA MOJA DHIDI YA RUVU SHOOTING, KATIKA MECHI ILIYOCHEZWA LEO KWENYE UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR-ES SALAAM.

Katika mchezo wa leo wa ligi kuu ya vodacom Yanga walimaliza mchezo wakiwa pungufu baada ya Mnywarandwa Haruna Niyonzima kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika 64 ya mchezo.

Timu hizo zilikwenda mapumziko wakiwa suluhu pacha, huku mchezo ukiwa na kasi ya kawaida na kosa kosa ndogo.

Katika kipindi cha pili kipa wa Yanga Yew Berko alifanya kazi ya ziada ya kuokoa michomo mitatu ya Ruvu Shooting kabla ya kuandika goli maridadi la kuongoza katika dakika 74.

Dakika 6 baada ya goli hilo Kenneth Asamoah aliisawazishia Yanga goli na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare 1-1.

Kwa matokeo hayo Yanga wanabaki mkiani mwa ligi huku wakiwa wametimiza siku 65 kucheza bila kushinda mchezo wowote na ukiwa mchezo wa 8 kucheza bila ya kutoka na ushindi.

No comments:

Post a Comment