Search This Blog

Thursday, July 7, 2011

OKWI AENDA KUFANYIWA VIPIMO KAIZER CHIEFS


Mshambuliaji wa Uganda “Cranes” na Simba ya Tanzania Emmanuel Okwi anakaribia kukamilisha usajili wake kutoka Msimbazi kuelekea katika klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika ya Kusini.

Okwi ambaye bado ana mkataba wa kuichezea klabu yake ya Simba amekuwa kwenye rada za moja ya klabu kubwa kusini mwa afrika, anatarajiwa kufanyiwa vipimo leo na endapo atafaulu atasaini mkataba ambao utaoiingizia akaunti ya Simba donge nono kama ilivyokuwa kwa wachezaji Mbwana Samatta na Patrick Ochan waliouzwa fedha zaidi ya shilingi mil. 300.

No comments:

Post a Comment