Search This Blog

Friday, July 8, 2011

CHRIS SMALLING ASAINI MKATABA MPYA NA UTD


MANCHESTER UNITED wamempa Chris Smalling mkataba mpya wa miaka 5 baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mwaka wake wa kwanza ndani ya kikosi cha Red Devils. The 21-year old defender alihamia United akitokea Fulham last summer kwa deal la paundi million 7. Na akiwa ameonyesha uwezo mkubwa katika kuisadia United kushinda ubingwa wa 19 wa EPL , amezawadia mkataba huu mnono. Boss Sir Alex aliongea kuhusu mkataba huu mpya wa Smalling na kusema: "Nina furaha sana baada ya Chris kusaini mkataba mpya. Smalling amekuwa mchezaji muhimu tangu ajiunge nasi kutoka Fulham mwaka jana, ana umri mdogo lakini ana kipaji kikubwa, ana nguvu, akili na anajua kuusoma mchezo.Ni hazina kubwa kwa klabu hii." Smalling nae alisema: "Naangalia mbele kudumu na kupata mafanikio ndani ya klabu ya Manchester United".

No comments:

Post a Comment