Search This Blog

Friday, July 8, 2011

KUTOKA EASTLANDS MPAKA ETIHAD STADIUM NA £100M


MANCHESTER CITY wametangaza dili lilivunja rekodi kupitia udhamini wa Etihad Airways.
Matajiri wa Premier League wameuza haki za jina la uwanja wao wa Eastlands, ambao sasa utajulikana kama Etihad Stadium. The Abu Dhabi Airline wamekubali kutoa udhamini wa miaka 10 wenye thamani paundi millioni 100, hivyo kuushinda mkataba kati ya Arsenal na Emirates Airline ambao nao una thamani ya £ 100m lakini ukiwa ni kwa kipindi cha miaka 10 kwa ajili ya kuupa jina la "Emirates " uwanja wa Gunners. Manchester City's CEO Garry Cook ameusifu mkataba huo kuwa ndio bora na muhimu katika historia ya soka.
"Tuna furaha kutangaza kuongeza mkataba wetu na Etihad Airways.Partnership yetu haitakuwa kwa jezi pekee lakini pia utahusu uwanja wetu- Etihad Stadium.Sehemu pana inayozunguka uwanja itajulikana kama "Etihad Campus".Kuna vitu vingine kama vile media, biashara na ushirikiano wa jamii na vitu vingine vingi. "Pengine huu unaweza kuwa mkataba mzuri zaidi katika historia ya Soka." Etihad tayari wameshakuwa wadhamini wa jezi za City kwa mkataba wa £ 2.8m per year. Huu ni mfano mwingine wa uwekezaji mkubwa kutoka Abu Dhabi ndani ya klabu hii, baada ya mwaka 2008 Sheikh Mansour kuinunua klabu hii na kutumia zaidi ya £ 1 billioni katika kuijenga upya timu kwa kununua wachezaji, mishahara, kukarabati uwanja na vifaa vya mazoezi. Mpaka sasa Sheikh Mansour ameshatumia pesa nyingi sana katika kununua wachezaji na mpaka mwisho wa msimu huu wa usajili anakadiriwa kutumia kwa jumla zaidi ya £ 400m.

No comments:

Post a Comment