Search This Blog

Friday, July 8, 2011

LIVERPOOL KUWAFUATA ARSENAL NA MAN CITY


Baada ya Manchester City na Arsenal kuuza haki za jina uwanja wao, sasa klabu ya Liverpool nayo iko mbioni kuuhama uwanja wake wa kihistoria wa Anfield . Klabu hiyo kwa sasa iko mbioni kuanza mradi wa kujenga uwanja mwingine lakini ili kufanikisha mradi huo klabu hiyo inatakiwa kutengeneza fedha za ziada ambazo kwa taarifa toka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa italazimika kuuza haki za kuupa jina uwanja wa Anfield YAANI “Naming Rights ” kwa kampuni itakayofika bei na kutoa fedha ambazo zitatumika kujenga uwanja mwingine kama ilivyokuwa kwa uwanja wa Arsenal The Emirates ambao kampuni ya usafiri wa Anga inayomiliki ndege za Emirates ambayo inadhamini uwanja huo kwa kuwa imelipia haki za kutumia jina la Brand yao kama jina la uwanja . Sasa unapoingia kwenye uwanja wa Anfield kaka inavyoonekana hapo kwenye picha inayomuonyesha Fernando Torres na Rafa Benitez kuna bango limeandikwa “THIS IS ANFIELD”, je Bango hili litabailishwa na kuandikwa “THIS ISN’T ANFIELD”??

No comments:

Post a Comment