Search This Blog

Friday, July 8, 2011

WANYAMA AKARIBIA KUTUA CELTICS


Mdogo wake kiungo wa kimataifa wa Kenya anayecheza soka lake huko Italia kwneye klabu ya Inter Milan McDonald Mariga anayekwenda kwa jina Victor Wanyama Mugabe yuko mbioni kujiunga na klabu kubwa nchini Scotland ya Glasgow Celtics . Wanyama ambaye ambaye ameichezea timu yake ya taifa ya Harambee Stars mara kadhaa na anakaribia kusaini kuichezea Celtics baada ya kushinda rufaa yake ya kibali cha kazi nchini Scotland. Wanyama ambaye ana umri wa miaka 20 alikuwa anaichezea Germinal Beerschot na anaongeza idadi ya Waafrika mashariki wanaocheza soka huko Scotland baada ya Mganda David Obua ambaye anaichezea Hearts baada ya kusajili toka Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment