Search This Blog

Wednesday, July 6, 2011

TARATIBU NA SHERIA ZA KUPIGA PENATI

PENALTY SHOOT-OUT

"Penalty shoot out" ni mipigo ya mpira kutoka kwenye alama maalum iliyowekwa katika "Penalty Box" ya uwanja wa mpira wa miguu.

Hii ni njia inayotumika katika sheria za mchezo wa soka zinazotumika kuamua ni timu gani isonge mbele kwenda hatua inayofuata katika michuano au kushinda michuano.

Mipigo hii ya penati inasimamiwa na sheria na kanuni ambazo zimewekwa na FIFA.




  • TARATIBU ZA KUPIGA PENATI

    *Timu ya kwanza kupiga mkwaju wa kwanza kuamuliwa kwa kurushwa shilingi na rafa ataamua ni goli lipi litumike kwa kupigia penati.

    *Mikwaju yote ya penati itapigwa katika goli moja ili kuhakikisha wapigaji wa penati na magolikipa wote wanakutana na hali yoyote isiyokuwa ya kawaida (kama ikiwepo).

    *Wachezaji wote isipokuwa mpigaji na magolikipa wanapaswa kubakia katikati ya uwanja.

    *Mipigo yote inatakiwa kupigwa kutokea katika alama ya kupigia penati, huku golini kukiwa na golikipa wa timu tofauti na mpigaji.Kipa anatakiwa kubaki katikati ya milingoti miwili huku akiwa amesimama katika mstari wa goli mpaka pale mpira utakapokuwa umepigwa, ingawa anaweza kurukaruka, kunyoosha mikono, kwenda upande mmoja mpaka mwingine akiwa ndani ya mstari wa goli.

    *Kila mpigaji anaweza kupiga mpira mara moja tu, ikiwa mpira aliopiga utazuiwa na golikipa, ukigonga mwamba mpigaji haruhusiwi kuupiga tena (lakini hii ni tofauti ni penati za ndani dk 90).

    *Hakuna mchezaji wa timu ya mpigaji anaruhusiwa kuugusa mpira.

    *Mpira unaweza kumgusa golikipa, milingoti ya pembeni na wa juu kwa idadi yoyote.

    Hali kama hii iliwahi kutokea katika mechi ya fainali za kombe la dunia mwaka 1986-Mexico katika mechi ya Brazil vs France, mechi ambayo iliamuliwa kwa mikwaju ya penati.Wakati wa kupiga penati mchezaji wa Ufaransa Bruno Bellone alipiga mkwaju ambao uligonga mwamba na kurudi uwanjani kisha ukarudi na kuingia golini.Mwamuzi Loan Igna akaamuru kuwa ni goli na nahodha wa Brazil Edinho alipopinga kuwa mpira ulipogonga mwamba na kurudi uwanjani ilitakiwa iamuriwe kuwa tayari France wamekosa akapewa kadi, lakini mwaka 1987 International Football Association Board walithibitisha kuwa kupitia sheria namba 14 inayohusu upigaji wa penalty kuwa maamuzi ya refa yalikuwa sahihi.

    *Ikiwa baada ya mipigo mitano kukamilika na timu zote zikalingana kwa idadi ya magoli, basi zitaanzwa kupigwa penati moja moja kwa kila timu mpaka timu moja itakapofunga na nyingine ikakosa.

    • *Wachezaji 22 pekee waliokuwepo ndani ya mchezo mpaka ulipomalizika ndio wanaruhusiwa kushiriki katika kupiga penati.
    • *Timu inaweza kumbadilisha golikipa ambaye atakuwa ameumia kipindi cha upigaji wa penati, ikiwa timu husika itakuwa haijamaliza idadi ya wachezaji wanaopaswa kubadilishwa.
    • *Ikiwa golikipa atapewa kadi nyekundu, mchezaji mwingine aliyekuwepo ndani uwanja kabla ya mpira kumalizika atachukua jukumu la kukaa golini.
    • *Ikiwa mchezaji mwingine isipokuwa golikipa akiumia au kupewa kadi nyekundu, mikwaju ya penati itaendelea bila kuwepo na mabadiliko yoyote.
    • *Mchezaji yoyote anaweza kuchukua majukumu ya golikipa aliyetolewa kwa kuumia au kwa kadi, na sio lazima mchezaji yuleyule adake mipigo yote anaweza akabadilishwa.
    • *Hakuna mchezaji anayeruhusiwa kupiga penati mara mbili kupigia mpaka pale mzungumko wa wachezaji wote wa timu husika watakapokuwa wamemaliza kupiga mpigo wa kwanza, akiwemo golikipa.
    • *Ikiwa itatokea hali ya ulazima kwa wachezaji kupiga penati kwa mara ya pili (kwa sababu kumekuwa na usawa wa matokeo mara ambapo wachezaji wote halali watakapokuwa wamemaliza mipigo yao ya kwanza) timu hazina ulazima wa kurudia wachezaji wale wale waliowatumia katika penati za 5 za kwanza.
    • *Ikiwa katika mwanzo wa upigaji penati timu moja itakuwa na wachezaji wengi uwanjani tofauti na nyingine, basi timu ambayo imebakiwa na wachezaji wengi uwanjani itabidi ichague mchezaji au wachezaji ambao watakuwa na idadi sawa na wapinzani wao.Mfano, ikiwa timu Team A itakuwa na wachezaji 11 lakini Team B ina wachezaji 10, basi Team A itabidi imchague mchezaji mmoja ambaye hatahusika kabisa na zoezi la upigaji penati hivyo golikipa hawezi kuchaguliwa kuondolewa katika listi ya wachezaji kumi wataohusika na kupiga penati huku akiendelea kudaka.Hatua inahusika ikiwa tu wachezaji/mchezaji alitolewa nje kwa kuumia au kwa kadi ndani ya dakika za kawaida za mchezo na sio ndani ya kipindi cha upigaji penati.

No comments:

Post a Comment