Search This Blog

Saturday, July 9, 2011

COUNTDOWN TO KAGAME CASTLE CUP FINAL:VITUKO VYA MECHI ZA WATANI WAJADI


Timu mbili zenye upinzani wa enzi na enzi katika soka la Tanzania Yanga na Simba Jumapili hii july 10 zinakutana katika mchezo wa Fainali ya Kombe la Kagame Castle cup mwaka 2011, mchezo huo utakaofanyika kwenye uwanja Mkuu wa Taifa jijini Dar es Salaam. Blog yako inaaangalia baadhi ya vituko vya kusisimua vilivyowahi kutokea wakati wa matayarisho, wakati au baada ya michezo baina ya timu mbili hizo kumalizika.
- Mwaka 1968 katika matayarisho ya mechi ya Simba (wakati huo Sunderland) na Yanga mchezaji wa Simba Emmnuel Mbele ‘Dubu’ alikuwa amefungiwa kucheza mpira kwa kipindi cha miezi 6 kutokana na utovu wa nidhamu uliotokea katika moja ya michezo ya ligi (wakati huo ligi ya taifa). Mchezo huo ulikuwa umepangwa kufanyika uwanja wa Ilala (Sasa Uwanja wa Karume zilipo ofisi za TFF). Timu zote mbili zilifika uwanjani huku wachezaji wakiwa tayari wamevaa jezi lakini kumbe Suderland hawakuwa tayari kucheza mchezo huo kwa madai kwa sharti kuwa wasingecheza huku mchezaji wao tegemeo, Mbele akiwa amefungiwa. Kutokana na hali hiyo kikaitishwa kikao cha dharura kilichohusisha viongozi wa Chama cha mpira wa Miguu Tanganyika (Tanganyika Football Assocation - TFA) Sunderland na Yanga. Baada ya hoja ya Sunderland kuwekwa mezani huku ikiaminika kuwa Yanga walikuwa wakihofia uwezo wa Mbele, Kwa mshangao Yanga waliwaambia viongozi wa TFA kuwa kama kikwazo cha mchezo ilikuwa ni mchezji mmoja tu basi afuguliwe na mchezo uendelee. TFA ikamfugulia Mbele ili akipige. Mchezo ukachezwa Sunderland wakapata kipigo cha aina yake cha magoli 5-0 yaliyofungwa na Maulid Diluga (2), Salehe Zimbwe (2) na Kitwana Manara.

- Agosti 10, 1974 Uwanja wa Nyamagana Mwanza magwiji wawili Gibson Sembuli (Yanga) na Saad Ally (Simba) waligongana katika harakati za kuwania mpira katika mchezo huo unaoaminika kuwa moja ya michezo iliyokuwa ya kiwango cha juu kabisa katika historia ya timu hizo mbili. Inaaaminika kuwa mahali walipogongana magwiji hao kiliota kichuguu ambacho hadi leo kipo. Bado hakuna uthibitisho wa kisayansi kuwa kichuguu hicho kilitokana na kugongana huko.

- Agosti 10, 1985 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mlinzi wa kati wa Simba Twalib Hilal anaushika mbira uliokuwa ukilekea golini baada ya kupigwa kichwa na Abeid Mziba-aliyejipatia umaarufu mkubwa wa kufuga magoli kwa kichwa kuliko miguu. Inaamuliwa ipigwe adhabu kubwa (penati) kuelekea laqngo mwa mwa Simba. Mpira unawekwa na anakwenda kupiga Juma Mkambi ‘Jenerali’ Simba wanatoka katika eneo la mita kumi na nane ili penati ipigwe lakini ghafla mpigaji anabadilishwa na anakwenda kupiga Hussein Iddi. Kuona hivyo Zamoyoni Mogella (wa Simba) anakimbia na kuupiga nje ili penati isipigwe. Mpira unavunjika na baadaye Yanga wanapewa ushindi wa magoli 2-0 na kuibuka mabingwa mwaka huo.

- Agosti 31, 1991 Katika kile kilichoonesha imani za ushirikina zilizopindukia mipaka, ilinunuliwa mipira mipya ya kuchezea kwenye mchezo huo chini ya uwakilishi wa wazee wawili mmoja kutoka kila upande wa Simba na Yanga na kisha wazee hao wakaiweka mipira hiyo ndani ya mfuko mmoja na kwenda nayo uwanjani wakiilinda kwa zaidi ya saa nne hadi pambano lilipoanza. Simba ilipokea kipigo cha goli 1-0 lililofungwa na Said Sued ‘Scud’.

- Novemba 13, 1991, (Ligi ya Muungano), Mchezo wa marudiano wa ligi hiyo ulifikia mapumziko huku timu hizo zikiwa hazijafungama. Timu zilipoingia katika vyumba vya kubadilishia mavazi, Simba hawakurejea dimbani. Madai ambayo hadi leo hayajawahi kuthibitishwa na mtu au chombo chochote ni kuwa mwamuzi wa mchezo huo – Hafidh Ali alinukuliwa akiwaambia wachezaji wa Simba kuwa wangepokea kipigo cha magoli 3-0 iwapo wangethubutu kurejea uwanjani baada ya mapumziko.

- Septemba 26, 1992 Yanga iliyokuwa tayari imetawazwa mabingwa kwa mwaka wa pili mfululizo iligoma kupeleka timu uwanja wa Taifa kwa madai kuwa mchezo huo haukuwa na umuhimu wowote kwao, hivyo Simba ikapewa ushindi na chama cha mpira wa miguu FAT.




- Julai 2, 1994 Yanga inafungwa goli 4-1 kipigo ambacho kinabakia kuwa kikubwa zaidi cha karibuni katika michezo ya ligi. Magoli ya George Masatu, Atuman China, Madaraka Seleman na Dua Said yalitosha kuikandamiza Yanga huku goli la Yanga likifungwa na Costantine Kimanda. Baada ya mchezo ambao ulichangia kuipa Simba ubingwa baada ya kuukosa kwa miaka mitatu, timu ya Yanga ikisambaratika huku wachezaji waandamizi kama Stephene Nemes, Said Mwamba, Nico Bambaga na Edibily Lunyamila wakiiacha timu hiyo ikipepesuka na hatimaye kusajili wachezaji wengi vijana wakiwemo Willy Mtendamema, Nonda Shaban Maalim Saleh na Sylvatus Ibrahim ‘Polisi’

- Februari 25, 1996 Simba iligoma kupeleka timu uwanja wa Taifa ikiishinikiza FAT kuilipa kwanza fedha kutoka CAF kutokana na faini iliyolipwa na klabu ya Chapungu ya Zimbabwe. Chapungu ilitozwa faini hiyo baada ya kushindwa kusafiri nchini kucheza mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Afrika. Inasadikiwa kuwa Simba haikuwahi kulipwa deni hilo.

- 2002, mchezo ambao ulikuwa umepangwa miezi kadhaa uliahirishwa dakika za mwisho kwa amri ya Waziri wa Kazi Maendeleo ya Vijana na michezo Juma Kapuya kutokana kile ambacho Yanga walidai walikuwa wakinyanyaswa kisaiklojia baada ya kiungo wao wa pembeni kulia Said Maulid ‘SMG’ kutangazwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuwa si raia wa Tanzania. Mchezo huo ulichezwa baadaye na timu hizo kutoka sare ya magoli 2-2.

- Oktoba 24, 2007 Uwanja wa Jamhuri Morogogoro; Pambano linamalizika huku Simba wakiwa washindi goli 1-0 la Ulimboka Mwakingwe. Baada ya hapo mashabiki wa Yanga wanawashmbulia baadhi ya wachezaji na kuwapiga wakati wakielekea kupanda gari lao. Jioni hiyohiyo baadhi ya wchezaji waliopigwa kipa Ivo Mapunda na mlinzi Shadrack Nsajigwa wanaondoka kambini wakidai kuhofia usalama wao. Uongozi wa Yanga unakutana siku chache baadaye na kuamua kuwafungia kutocheza mpira kwa kipindi cha miezi 6.

- Julai 27, 2008 (Kombe la Kagame). Yanga inakataa kupeleka timu uwanjani kuikabili Simba katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu ya Kombe la Kagame ambao ungekuwa mchezo wa kwanza kuzikutanisha timu hizo katika Uwanja Mkuu wa Taifa. Yanga ilidai kuwa haikupeleka timu kwa vile haikutekelezewa ahadi ya kulipwa na TFF shilingi milioni 50 kabla ya mchezo huo kama yalivyokuwa makubaliano ya kuwalipa Yanga na Simba kila moja kiasi hicho cha fedha. Yanga inaadhibiwa na CECAFA kutocheza michezo yake kwa kipindi cha miaka 3 na pia kutozwa faini ya Dola za Marekani 35,000. TFF nayo inaifungia Yanga kutocheza michezo yote ya kimataifa ya kirafiki na mashindano kwa kipindi cha miaka miwili. Hata hivyo adhabu hiyo ilitenguliwa baadaye na Kamati ya Nidhamu ya TFF na badala yake Yanga ikatozwa faini ya Dola za Marekani 20,000 na kutakiwa kuiomba radhi TFF na wadau wa mpira wote nchini.

No comments:

Post a Comment