Search This Blog

Friday, July 8, 2011

SHAY GIVEN KUHAMIA VILLA WIKI IJAYO


Aston Villa wana matumaini kuwa Shay Given atakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Alex McLeish wiki ijayo kwa dili la paundi 3.5 million kutoka Manchester City.
Villa wanataka huduma za kipa huyo kutoka Ireland ambaye amekosa nafasi ndani ya kikosi cha Eastlands ili kumbadili golikipa Brad Friedel aliyehamia Tottenham.
Klabu hizo mbili kwa muda sasa wamekuwa kwenye mazungumzo na chanzo cha habari kutoka Villa zinasema dili hilo kumsajili kipa huyo litakamilika wiki ijayo.
Given alikuwa namba 1 akiwa Newcastle kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 kabla hajaamia City miaka miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment