Search This Blog

Wednesday, July 6, 2011

MAN CITY YAKAMILISHA USAJILI WA SAVIC




Manchester City wamekamilisha usajili wa beki Stefan Savic kutoka Partizan Belgrade kwa mkataba wa miaka wa miaka 4.

Beki huyo raia wa Montenegro mwenye umri wa miaka 20 alifanikiwa kupata kibali cha kufanya kazi nchini England na kuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na City ndani ya siku 3, baada ya Gael Clichy aliyetokea Arsenal.

Savic ambaye miezi 12 iliyopita alikuwa akifanya majaribio na Arsenal lakini hakufanikiwa kupata mkataba @ Emirates ameuambia mtandao wa Manchester City kuwa: "Nimekuwa nikiitizama Premier League muda wote na najua ni sehemu nzuri ya kuendeleza kipaji changu katika kuisaidia klabu hii kushinda vitu vikubwa.Tuna uwanja mzuri na nimeona ni jinsi gani mashabiki wa City walivyo na mapenzi na klabu hii."

Montenegro watacheza na England baadae mwaka huu hivyo nategemea kuwa na uchezaji wa kirafiki na waingereza, Nina furaha sana kuwa mchezaji wa Manchester City." - Amelonga Savic.

No comments:

Post a Comment