Search This Blog

Friday, August 19, 2011

MILLION 72 ZAMPELEKA JOSEPH OWINO CHAMAZI


Beki wa kimataifa wa Uganda Cranes Joseph Owino amejiunga rasmi na Azam Fc kwa ada ya uhamisho wa dola za kimarekani 30,000.

Owino ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia Simba Sports Club kabla ya kupata majeraha ya goti yaliyomweka nje ya uwanja kwa msimu wote uliopita na mwishowe aliachwa na Simba katika usajili wa msimu huu.

Beki huyo ambaye kwa sasa anaendelea vizuri na majeraha yake ya goti baada ya kuachwa na Simba, matajiri wa Vodacom Premier League Azam FC waliamua kumchukua na kumpeleka nchini India kwa ajili ya matibabu yaliyogharimu kiasi cha pesa kinachofikia dola 15,000 na baadae wakamsainisha mkataba wa miaka 3 wenye thamani ya $30,000.

Owino anatarajiwa kujiunga rasmi na Azam na kuanza kuitumikia klabu hiyo mwezi January mwakani wakati wa dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa.

No comments:

Post a Comment