Search This Blog

Friday, July 15, 2011

MBWANA SAMATTA AIFUNGIA TP MAZEMBE BAO LA USHINDI.

MBWANA SAMATTA JEZI NAMBA 29 AKIFUNGA BAO PEKEE KWA KICHWA.



Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta juzi aliikoa timu yake ya Tp Mazembe na kuipa ushindi wa bao moja bila katika mchezo wa ligi . Samatta aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Serge Lofo alifunga bao hilo katika dakika ya 89 ya mchezo huo ambao kwake ulikuwa wa kwanza tangu ajiunge toka Simba Sports Club .
Sammatta aliingia kwenye mchezo huo sambamba na mwenzie waliyejiunga naye toka Simba Patrick Ochan ambaye naye alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza ambapo alichukua nafasi ya Rainford Kalaba aliyeumia dakika 15 baada ya mchezo kuanza . Tp Mazembe pia ilimkaribisha kiungo wake Guy Lusadisu aliyecheza mchezo wake wa kwanza tangu atoke kwenye adhabu ya kifungo cha FIFA baada ya kufanya fujo kwenye michuano ya kombe la Kagame huko Rwanda mwaka jana.


Hii ni mara ya tata kwa Samatta kufunga bao kwenye mchezo wake wa kwanza rasmi ambapo aliifungia Simba mabao mawili dhidi ya African Lyon ambayo ni timu yake ya zamani katika mchezo wake wa kwanza akiwa na Simba kwenye ligi kuu ya Vodacom msimu uliopita , pia aliifungia timu ya taifa ya wakubwa katika mchezo wake wa kwanza akitokea benchi dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya kati na sasa ameifungia klabu yake mpya kwenye mchezo wake wa kwanza wa ligi.

No comments:

Post a Comment