Search This Blog

Friday, April 4, 2014

CHAMPIONS LEAGUE ROBO FAINALI KWENYE NAMBA: MAN UNITED, BAYERN, RONALDO WAWEKA REKODI MPYA KATIKA MICHUANO HIYO



• Wachezaji Cristiano Ronaldo na Frank Lampard walitimiza mechi zao 100 za UEFA Champions League appearances katika mechi za kwanza za robo fainali na hivyo kuwa mchezaji wa 20 na 21 kufikia namba ya mechi hizo. Wachezaji pia walianza kucheza katika michuano ya ulaya siku moja,  16 September 2003.


• Lampard amekuwa mchezaji wa 12 kufanikiwa kutimiza mechi 100 akiwa na klabu moja na ndio mchezaji wa kwanza wa Chelsea kutimiza idadi ya mechi hizo.

• Idadi ya mechi 100 za Ronaldo imegawanyika katika sehemu mbili - ameitumikia Manchester United FC (mechi 52 ) na Madrid (48). Yupo karibuni kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza duniani kucheza 50 katika klabu mbili tofauti. 

• Hakuna mchezaji mwingine atakayeweza kufikisha idadi ya mechi 100 msimu huu katika wachezaji waliobakia kwenye mashindano - zimebakia mechi 4 - Mchezaji Andres Iniesta, John Tery wote wamecheza jumla ya mechi 95. Rio Ferdinand na Xabi Alonso wamecheza mechi 93 na 91. 
• Frank Ribery alitimiza mechi 50 za UEFA Champions League - zote amecheza akiwa na FC Bayern München.
• Mechi ya sare ya Manchester United dhidi ya Bayern imewafanya watimize jumla ya mechi 199 za  UEFA Champions League; mechi ijayo itawafanya watimize mechi 200 katika michuano hiyo. Wao ndio wanaongoza kwa kucheza mechi za UCL - ikiwa Real Madrid watafanikiwa kucheza mpaka fainali basi wataungana na United katika listi ya vilabu vilivyotimiza mechi 200.
• Mechi hiyo iliyofanyika Old Trafford ilikuwa mechi ya 99 ya michuano hiyo kufanyika katika dimba hilo - ni uwanja mmoja tu unaoizidi OT kwa kuchezewa mechi nyingi za UCL - San Siro, ambao unatumiwa na vilabu vya AC milan na  FC Internazionale Milano, uwanja huo umetumika kufanyika mechi zaidi ya (131).
• United na Bayern zote mbili zilitimiza jumla ya mechi 25 za hatua ya robo fainali ya UCL - hii ni rekodi ya mashindano. Barcelona na Real Madrid wote wamecheza mechi 17 za hatua hiyo.

No comments:

Post a Comment