Search This Blog

Friday, April 4, 2014

SIMBA WATUA SALAMA BUKOBA, WAFANYA MAZOEZI YAO YA MWISHO KAITABA LEO BILA KOCHA WAO LOGA!!, KESHO NI PATASHIKA KAGERA SUGAR v SIMBA SC

Baadhi ya Viongozi wa Simba wakiteta jambo kwenye Uwanja wa Kaitaba leo hii jioni, Bila shaka ni swala zima la mtanange wao kesho na Kagera Sugar huku wakijiuliza maswali kadhaa na kuucheki uwanja wa Kaitaba jinsi ulivyo katika kipindi hiki. Kocha wa Simba Zdravko Logarusic hakuwepo kabisa kwenye Mazoezi Hapa Kaitaba na inaoneka hakuja na Wachezaji wake. Taarifa zaidi inasemekana atakuja kesho jumamosi siku ya Mtanange.
Wachezaji wa Simba wakishuka kwenye basi lao kuingia kwenye uwanja wa Kaitaba, Tayari kufanya mazoezi kujiweka fiti na mtanange wa kesho na Wenyeji Kagera Sugar.
Baadhi ya Wachezaji wa Simba wakiingia tayari kwenye nyasi za Kaitaba hapa Bukoba
Safi sana...siku nyingi!!!
Tayari kwa mazoezi....
Wachezaji wa Simba wakiomba dakika chache kabla ya mazoezi yao kwenye Uwanja wa Kaitaba jioniWachezaji wa Simba wakiteta jambo kabla ya mazoezi, Kipa Ivo Mapunda (katikati) akiwacheki kwa karibu.Viongozi wa Simba wakiwacheki vijana wao wakijifua!Kesho tucheka na nyavu tuu....
Simba sc wanaingia katika mchezo wa kesho wakiwa hawana cha kupoteza, kwasababu hawahitaji ubingwa wala nafasi ya pili.

Hata hivyo ushindi ni muhimu kwao ili kulinda heshima yao inayozidi kupotea siku za karibuni.
Wataingia uwanjani wakiwa wamepoteza mechi mbili zilizopita dhidi ya Coastal Union na Azam fc, hivyo kupoteza mechi ya kesho ni kuwatonesha zaidi kidonda mashabiki wao. 
Simba mpaka sasa wapo nafasi ya 4 katika msimamo baada ya kucheza mechi 23 na kujikusanyia pointi 36.
Kagera Sugar wao wanahitaji nafasi ya tatu au nne msimu huu, hivyo kesho wataingia kutafuta pointin tatu muhimu.
Kagera kwasasa wapo nafasi ya 5 wakiwa na pointi 33 baada ya kucheza mechi 22.
Ligi hiyo itandelea tena jumapili (aprili 6) ambapo mechi kali ni baina ya mabingwa watetezi, Yanga dhidi ya JKT Ruvu uwanja wa Taifa.
Umuhimu wa ushindi kwa timu zote mbili ndio sababu ya mchezo huo kuwa na mvuto kwa mashabiki wa soka.Moja ya Kipa wa Simba, Ivo Mapunda mlinda mlango wa zamani wa Yanga na Klabu ya Gor Mahia ya Kenya akiwa kwenye nyasi za Uwanja wa Kaitaba hii leoMakipa wote wa Tatu wa Simba wakijifua!Ivo MapundaIvo Mpunda ajikiuliza kama kesho wanatoka au la!!Nani kesho ataanza langoni mwa Simba?Kipa ni Mchezaji muhimu sana kwenye Klabu yoyote ile, na Hapa Ivo Mapunda na mwenzake wanataka ushindi kwani wao ni wazoefu kwenye swala zima la kulinda milango.Baadhi ya Viongozi wa wekundu wa Msimbazi ya Jijini Dar es SalaamKesho tunataka timu yetu iibuke na pointi tatu muhimu!Kipa mwingine wa Simba
 
 Picha zote na Na Faustine Ruta wa www.bukobasports.com

No comments:

Post a Comment