Search This Blog

Wednesday, February 5, 2014

TASWIRA YA MCHEZO KATI YA SIMBA NA MTIBWA SUGAR KATIKA UWANJA WA JAMUHURI MOROGORO,ZAFUNGANA 1-1.

Kikosi cha Timu ya Soka ya Simba Kilichoanza Dhidi ya Mtibwa leo
Nyuma Kuanzia Kushoto: Kocha Msaidizi Seleman Matola,Tambwe,Amri Kiemba,Joseph Owino,Jonas Mkude,Musoti.Mbele Kushoto:Singano,Awadhi,Haruna Chanongo,Ivo Mapunda,Rashid Baba Ubaya,Haruna Shamte.
 Kikosi cha Timu ya Soka ya Mtibwa Nyuma kuanzia Kushoto:JumaLuizio,Shaban Nditi, Hassan Ramadhan,Ally Shomary  Salim Mbonde.Mbele Kuanzia Kushoto : Jamal Mnyate,Said Mkopi,Shaban Kisiga, Husein Sharif,Salvatory Mtebe,Mussa Mgosi.
Waamuzi wa Mchezo wa Leo wakiwa na Manaodha wa Timu Zote Mbili.
 Wachezaji wa Timu ya Soka ya Mtibwa Sugar Wkishanilia Goli Lililofungwa na Musa Mgosi  Katika Dakika ya 18 ya Mchezo.
 Rashid Baba Ubaya Akitafuta Mbinu za Kumtoka Beki wa Mtibwa Sugar Said Mkopi.
 Kipa wa Mtibwa Hasani  Sharifu  
 Mashabiki waliojitokeza katika Mchezo huo wakishangilia muda wote wa Mchezo

 Golikipa wa Timu ya Mtibwa Sugar Hussein Sharif Akiwa Ameokoa Moja ya Purukushani katika Lango Lake.Akishihudiwa na Beki wake Salim Mbonde Pamoja na Mshambuliaji wa Simba Khamisi Tambwe.
 Simba wakishangilia Goli lao lilofungwa na Khamis Tambwe Bao lililofungwa dakika 50 ya mchezo.

Mpira Umemalizika Mtibwa 1 -1 Simba. Goli la Mtibwa Sugar Lilifungwa dakika ya 18 ya Mchezo bao Lililofungwa na Mussa Mgosi .Hadi Mapumziko Mtibwa walikuwa wanaongoza kwa Goli Hilo Moja.Kipindi cha Pili Mpira ulianza kwa kasi Simba walishambulia Lango la Mtibwa mara kwa mara Na kujipatia bao la Kusawazisha katika dakika ya 50 ya Mchezo.Katika Mchezo Mchezaji wa Mtibwa Shaban Nditi Alionyeshwa kadi Nyekundu Dakika ya 69 baada ya Kutoa maneno Machafu kwa Mwamuzi.Dakika ya 72 Said Ndemla anaingia Kuchukua nafasi ya  Haruna Shamte,Dakika ya 75, Juma Mpakala Aliingia Kuchukua nafasi ya  Jamal Mnyate. Dakika ya 87  wanafanya mabadiliko ya mwisho, aliingia Abdallah Salum Kuchukua nafasi  Mgosi..

1 comment:

  1. Wanasimba wenzangu tujifunze kutofautisha mechi za bonanza kama nani mtani jembe na mechi za ligi kuu.Katika mechi ya mtani jembe timu iliyoshinda ilipata kombe na timu iliyoshindwa nayo ilipata kombe,kama inavyokuwa kwenye mabonanza,na pia kwenye mabonanza mchezaji anaweza akacheza na kufunga goli hata kama amefanya mazoezi kwa siku moja tu(Okwi).Kuna faida gani kuweka kambi ya wiki moja Zanzibar kwa ajili ya mechi moja ya bonanza halafu tunashindwa kuweka timu kambini kwa ajili ya mechi 13 za ligi kuu?Matokeo yake sasa tutachekwa mwaka mzima sababu ya furaha ya siku moja tu.

    ReplyDelete