Search This Blog

Wednesday, February 5, 2014

MATCH LIVE CENTRE: MTIBWA SUGAR 1 - 1 SIMBA SC FULL TIME


Dakika ya 90, Mtibwa 1 -1 Simba. Kiujumla mechi haikuwa ya kuvutia sana kutokana na pitch mbovu ya uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro. Mtibwa wamepata kona dakika ya mwisho ila haikutoa matunda. Mechi imekwisha kwa sare ya bao 1-1

Dakika ya 87, Mtibwa 1-1 Simba. Mtibwa wanafanya mabadiliko ya mwisho, anaingia Abdallah Salum anatoka Mgosi

Dakika ya 84, Simba wanapata kona ila haina madhara

Dakika ya 78, Hassan Ramadhani anapewa kadi ya njano

Dakika ya 75, Juma Mpakala wa Mtibwa ameingia mahala kwa Jamal Mnyate

Dakika ya 72, Mtibwa 1-1 Simba- Said Ndemla anaingia mahala kwa Haruna Shamte

Dakika ya 69, naodha wa Mtibwa, Nditti anaoneshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa uwanjani

Dakika ya 67, Mtibwa wanafanya mabadiliko ya kwanza, Vicent Barnabas anaingia Juma Luizio anatoka. Timu zinashambuliana ila Simba wanashambulia zaidi

Dakika ya 65, Mtibwa hawajafanya mabadiliko hadi wakati huu, Simbaw ameshafanya mabadiliko ya wachezaji wawili. Makipa wote wapo likizo

Dakika ya 60, Mtibwa 1-1 Simba. Mtibwa wanaonekana kupunguzwa kasi

Dakika ya 58, Simba wanaonekana kubadili stahili ya mchezo na kucheza mipira mirefu ili kuendana na hali ya uwanja

Dakika ya 55, Mtibwa 1-1. Mpira umeanza kuwa na kasi

Dakika ya 52, Uhuru Suleiman anaingia kuchukua nafasi ya Chanongo kwa upande wa Simba

Dakika ya 50 , GOOOO, Tabwe , Mtibwa 1-1 Simba

Dakika ya 48, Mtibwa 1- 0 Simba

Dakika ya 46, Tambwe anapoteza nafasi. Simba tayari wamefika mara mbili katika lango la Mtibwa

Dakika 45 za kipindi cha pili zinaanza. Mtibwa ndiyo wanaanza mpira

Goli la Mtibwa Sugar limefungwa na mshambuliaji wa zamani wa Simba, Mussa Hasan Mgosi.

Dakika 45 , mpira ni mapumziko . Katika kipindi hiki Mtibwa wamecheza kwa kufuata maelekezo, huku Simba wakionekana kupoteza mawasiliano wao wenyewe, japo uwanja unaonekana kuwasumbua kwa kuwa mpira hautulii.

Dakika 44, Nditti anapata kadi ya njano

Dakika 43 mpira umesimama, Mkopi amepata maumivu tena

Dakika ya 40, Mtibwa 1-0 Simba

Dakika ya 39 Mtibwa wanapata faulo ila wanapoteza

Dakika ya 36, Awadh Juma anatoka anaingia Ally Badru upande wa Simba

Dakika ya 34, Simba wanapata kona Mkude anapiga fyongo

Dakika ya 28, Mtibwa bado wanawabana sana Simba, hawawapi nafasi ya kucheza

Dakika ya 28, Mtibwa bado wanawabana sana Simba, hawawapi nafasi ya kucheza

Dakika ya 26, Mtibwa 1-0 Simba. Uwanja wa Jamhuri sehemu ya kuchezea si nzuri.

Dakika ya 22, Shaaban Nditti na Kisiga wameonekana kumiliki eneo la kiungo.

Dakika ya 20, Mtibwa  1-0 Simba

Dakika 17, Amri Kiemba anaunganisha kwa kichwa mpira wa faulo uliopigwa na Issa Rashid ila unatoka nje

Dakika ya 15, Simba wamepata kona moja, ila haikuzaa matunda. Mtibwa wanacheza soka la nguvu kuliko Simba. Wachezaji, Jamal Simba, Shaaban Kisiga, Mgosi, na Luizio wanawasumbua sana walinzi wa Simba

Dakika ya kumi mpira bado unachezwa bila mipango. Tayari Simbawamecheza faulo tatu. Mtibwa wanapata bao la kuongoza lililofungwa na Mussa Hassan Mgosi. Ni makosa ya kipa Ivo Mapunda

Dakika ya sita, kipa Husein Shariff anadaka mpira wa kwanza uliopigwa na Amis Tambwe
Dakika ya pili, Mtibwa wanapata faulo, Said Mkopi anapiga ila wanapoteza

Dakika ya kwanza mpira umeanza hapa uwanja wa Jamhuri, Simba ndiyo wameanza mpira . Juma Luizio anafanya shambulizi la kwanza

No comments:

Post a Comment