Search This Blog

Saturday, February 8, 2014

LIVE SCORE: YANGA SC 7-0 KOMOROZIE DE DEMONI - FULLTIME


Mpira umemalizika Yanga 7-0 Wacomoro

  Dakika ya 81, Didier Kavumbagu anaipatia Young Africans bao la saba

Dakika ya 75, Young Africans 6 - 0 Komorozine de Domoni

Dakika ya 68, Mrisho Ngasa anaipatia Young Africans bao la tano

Dakika ya 65, Mrisho Ngasa anaipatia Young Africans bao la tano

59' Hamisi Kiiza anapigilia bao la nne...pasi nzuri ya Kavumbagu.

57' Didier Kavumbagu anaipa Yanga bao la tatu.

54' Komorozine wanapata mkwaju wa adhabu, Simba wanashangilia, Yanga wanazomea...bado mpira umesinzia.

Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans inafanya mabadiliko anaingia Didier Kavumbagu kuchukua nafasi ya David Luhende

HT: Yanga 2-0 Komorozine ( Ngassa, Nadir Haroub ) #CAFChampionsleague

42' Yanga 2-0 Komorozine

39' Hamisi Kiiza ana uchu mno wa kufunga, mpaka sasa offside mara nne,

32' Komorozine wanapata kona ya kwanza. Kwa mara ya kwanza Simba wanapiga makofi.

Dakika ya 30, Young Africans 2 - 0 Komorozine de Domoni

23' Timu nzima ya Komorozine imegeuka kwa mabeki. Hawavuki mstari wao.

20' Nadir Haroub anamalizia kwa kichwa adhabu ndogo iliyopigwa na Msuva na kuaindikia Yanga bao la pili.

 13' Bao! Ngassa anachupa vizuri na kuiandikia Yanga bao la kwanza.

7' Kisigino cha Hamisi Kiiza kinatua mikononi mwa kipa wa Komorozine.

2'  Kona tasa. Shuti la Ngassa lililokuwa likielekea nyavuni limepanguliwa na beki na kuwa kona. Krosi ya Msuva.

1' Mpira umeanza...Yanga ndani ya jezi za kijani ilhali Komorozine wamevaa jezi za njano na bukta nyeusi.

No comments:

Post a Comment