Search This Blog

Saturday, February 22, 2014

HATIMAYE WAYNE ROONEY AWA MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI - TAZAMA MCHANGANUO WA MALIPO YAKE


Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Wayne Rooney jana usiku hatimaye alimaliza tetesi za kuhusu hatma yake ndani ya klabu hiyo baada ya kusaini mkataba mpya utakaomuweka kwenye klabu hiyo mpaka mwaka 2019.

Rooney ambaye alisajiliwa na United akitokea Everton mwaka 2004, amesaini mkataba mpya wa miaka minne wenye thamani ya £300,000 kwa wiki.

Rooney sasa analipwa jumla ya £15.6m kwa mwaka - kwa maana 

MCHANGANUO WA MSHAHARA MPYA WA ROONEY

£15,600,000 kwa mwaka
£300,000 wiki
£43,000 kwa siku
£1,800 kwa saa
£30 kwa dakika
50p kwa sekunde
 hiyo Rooney sasa amemfunika Cristiano Ronaldo aliyekuwa akishika nafasi ya kwanza kwa kulipwa fedha nyingi za mshahara - Ronaldo mkataba wake mpya na Real Madrid analipwa kiasi cha £288,000 kwa wiki. Pia amemfunika Leo Messi ambaye analipwa kiasi cha £12.08m kwa mwaka, hii ni kwa mujibu wa 2013 Forbes rich list.

No comments:

Post a Comment