Search This Blog

Saturday, February 22, 2014

CARLO ANCELOTTI AKARIBIA KUVUNJA REKODI YA KUIWEZESHA REAL MADRID KUCHEZA MECHI NYINGI MFULULIZO BILA KUFUNGWA


Kocha wa kiitaliano Carlo Ancelotti anaweza kuandika historia mpya wikiendi hii endapo ataweza kuingoza Real Madrid kupata matokeo chanya katika mchezo wa wikiendi wa La Liga dhidi ya Elche.

Mpaka kufikia sasa Carlo Ancelotti ameshaiongoza Real kucheza jumla ya mechi 25 mfululizo bila kupoteza mechi hata moja.

Tangu walipofungwa na na Atletico Madrid 1-0 Santiago Bernabeu mwishoni mwa mwezi September, kisha
REAL MADRID: REKODI YA KUCHEZA MECHI NYINGI MFULULIZO BILA KUFUNGWA
 1988-89: 34 MECHI (25 USHINDI, 9 SARE)
Kikosi cha Leo Beenhakker kilicheza mechi 34 mfululizo bila kufungwa wakati waliposhinda La Liga na Copa del Rey msimu wa1988-89.
2013-14: 25 MECHI (21 USHINDI, 4 SARE)
Carlo Ancelotti ameiongoza Madrid kucheza mechi 25 mfululizo bila kufungwa katika msimu wake wa kwanza na anaweza kufikisha 26 endapo atapata matokeo chanya dhidi ya Elche wikiendi hii.
1996-97: 25 MECHI (17 USHINDI, 8 SARE)
Msimu wa kwanza wa Fabio Capello pale Bernabeu ulihusisha mechi 25 bila kufungwa wakati Madrid walipochukua ubingwa wa La Liga baada ya kumaliza nafasi ya 6 msimu wa 1995-96.
mwezi mmoja uliofuatia kufungwa na 1-0 na Barcelona pale Nou Camp, kikosi cha Ancelotti mpaka sasa kimeshacheza mechi 25 bila kupoteza tangu Oktoba 2013.

Wameshinda mechi 21, na wametoa sare mechi 4 na hawajafungwa. Wameshinda dhidi ya Sevilla, Rayo Vallecano, Real Sociedad, Almeria, Galatasaray, Valladolid, Olimpic Xativa, FC Copenhagen, Valencia, Osasuna (mechi 2 Copa del Rey), Celta Vigo, Espanyol ( La Liga na mara 2 kwenye Copa) Betis, Granada, Atletico (mechi 2 copa), Villarreal na Getafe, walitoka suluhu na Juventus, Osasuna na Athletic Bilbao.

Rekodi hii tayari ni nzuri kuliko ya kikosi cha Fabio Capello cha Madrid cha msimu wa 1996-97, ambacho kiliweza kucheza mechi 25 bila kufungwa, lakini walitoa sare mechi 8 - hii ilikuwa katika msimu wa kwanza wa mtaliano huyo.

No comments:

Post a Comment