Search This Blog

Friday, January 17, 2014

VOGTS, WOLFGANG WAIBUKIA KAMBI YA YANGA


Wachezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Ujerumani  ambao kwa sasa ni makocha wa timu ya Taifa ya Azerbeijan Berti Vogts na msaidizi wake Wolfgang leo jioni kabla ya mazoezi waliibuka katika viwanja vya hotel ya Sueno Beach na kuongea kidogo na makocha wa Young Africans Hans na Mkwasa masuala ya kiufundi kisha kuagana nao na kuwaacha waendelee na progam yao ya mazoezi.
Vogts amabaye alikuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa Ujerumani kwa miaka nane (1990-1998) na kufanikiwa kushinda kombe la Ulaya mwaka 1996, na kufika hatua ya robo fainali ya kombe la Dunia mwaka 1998 alikuwa ameambatana na kocha wake msaidizi Wolfagang .
Kocha mpya wa Young Africans mholanzi Hans Van Der Plyum leo ameanza rasmi kazi ya kukinoa kikosi cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara katika viwanja vya hoteli ya Sueno Beach Side baada ya jana kuiongoza katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya Altay SK.


                                                        Mkwasa na Wolfagang

Hans ambaye amejiunga na Young Africans wiki hii akichukua nafasi ya kocha mholanzi aliyeondoka Ernie Brandts amesema atajitahid kadri ya uwezo wake pamoja na wachezaji na benchi la ufundi kuona wanaisaidia timu kufika hatua nyingine mbele zaidi.
"Amesema hawezi kufanya jambo lolote peke yake bali kwa kushirikiana kwa pamoja atafanikiwa kwani katika mchezo wa jana timu yake iliweza kucheza soka la kujituma na kushirikiana mwanzo mwisho kitu ambacho ndio falsafa yake katika ufundishaji" alisema Hans.
Timu ilifanya mazoezi ya asubuhi leo saa 5 kamili kwa saa za Uturuki mpaka saa 6:30 kabla ya kupumzika na kurejea tena mazoezini jioni saa 11 kamili jioni mpaka saa 12:30 ambapo alikuwa akiwaelekeza wachezaji jinsi gani anapendelea wacheze kwa kufuata mfumo wake.



 Kocha Msaidizi wa Young Africans Charles Mkwasa akiwa na Kocha Berti Vogts


Akiongea na www.youngafricans.co.tz mara baada ya mazoezi ya leo kocha Hans amesema timu ya Young Africans ina wachezaji wazuri ambao wana uwezo binafsi na bado wana nafasi ya kucheza soka kwa kipindi kirefu hivyo kikubwa wanapaswa kuwa fit muda wote ili waweze kutimiza majukumu yao.
Young Africnas itaendela na mazoezi kesho na asubuhi katika viwanja vya hotel ya Sueno kujiweka sawa kwa mchezo utakaofuata wa kirafiki kabla ya kurejea nchini wik ijayo tayari kwa mikikiki ya Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa. 

Kocha mkuu wa Young Africans Hans Van der Plyum akiwa na msaidizi wake Charles Mkwasa kabla ya kuanza mazoezi ya kuanza kwa mazoezi ya jioni katika viwanja vya hoteli ya Sueno Beach

No comments:

Post a Comment