Search This Blog

Friday, January 17, 2014

ANDERSON AKWEA PIPA KUELEKEA ITALIA KUJIUNGA NA FIORENTINA

Kiungo wa Manchester United Anderson amesafiri kwenda jijini  Florence kwa ajili ya kwenda kufanya vipimo vy afya kwa ajili ya kujiunga kwa mkopo na klabu ya Serie A ya Fiorentina.

Mbrazil huyo amewaambia rafiki zake kwamba anataka uhamisho wa moja kwa moja ili kujihakikishia muda wa kucheza lakini United kwa sasa wapo tayari kutoa ruhusa ya biashara ya mkopo tu.

Anderson alitokea jijini Manchester kupitia Frankfurt leo alhamisi na anategemewa kukamilisha kila kitu kesho mchana.  


Anderson amecheza mechi 4 tu katika premier league msimu huu, na nane kwa ujumla.

Alijiunga na United mwaka 2007 akitokea Porto kwa ada ya  £20million, ameichezea timu hiyo mechi 179 na kuifungia mabao 9.  

No comments:

Post a Comment