Search This Blog

Friday, September 20, 2013

SHAFFIH DAUDA: MICHEZO INA FURSA KUBWA NA WAZI ZA MAENDELEO ….BUKOBA!


SHAFII DAUDA: MICHEZO INA FURSA KUBWA NA WAZI ZA MAENDELEO ….BUKOBA!


Mdau wa michezo na mwanamichezo wa sports extra wa Clouds Fm, anazungumzia jinsi gani ambavyo wadau wa soka wanavyoweza kuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya michezo nchini Tanzani,kupitia ununuaji wa bidhaa mpaka ulipiaji wa matangazo ya Moja kwa Moja hata ya kulipia ya Televisheni .
Lakini sasa anakazia katika kijana mmoja mmoja kati ya wale wenye kipaji ambavyo anavyoweza kujijenga mwenyewe na kufikia kuwa Brand, jina lenye kujiuza kama akina Cristiano Ronaldo,David Beckham….. Vijana Hawa wanapaswa kufanya nini kufikia huko.
Anatolea mfano ni kwa nini vijana wengi wenye kipaji Cha kucheza soka mkoani Kagera,wameshindwa hata kupata nafasi ya kucheza soka katika timu inayoshiriki ligi kuu ya mkoani humo Kagera Sugar.
Anasema jambo la kwanza ni kujitambua, jambo ambalo anasema limekuwa ni kikwazo kikubwa kwa wachezaji wa Tanzania,tofauti na wachezaji wengine wa Afrika mashariki na kati ambao sasa wanacheza soka ya kulipwa barani Ulaya.
Mfano mzuri akiutoa kwa mchezaji Shabani Nonda aliyetoka Congo kupitia Burundi, Tanzania, Afrika kusini, mpaka ulaya.
Huku akizungumzia jinsi wachezaji wetu kama akina Boban walivyokwama kucheza soka katika kiwango cha juu, kwa sababu ya kukosa kujitambua, kujituma,kujithamini na kuamini katika vipaji kuwa fursa kubwa ya kufanikiwa maishani.

TWENDZETUUU …….!

SOURCE: www.kibonde24.com 

No comments:

Post a Comment